Yni najua huwezi kujibu yale maswali mna Elimu yko ni ndogo mnooo
sasa ww nani kakwambia kua swali hujibiwa kwa swali
Aliyeanza kujibu swali kwa swali ni mtume,je Mtume hajui kujibu kama mimi ?
Katika hadithi ambayo mayahudi walimtolea mtume salamu mbaya mtume akawajibu "waaleykum"
Mama aisha akaongeza maneno ya laana kwa wale wayahudi kwamba "na nyie Laana za Allah ziwe juu yenu"
Mtume akamkataza mama aisha kwamba usiwajibu hivyo hao.
Mama aisha akamuuliza mtume "huoni waliyokuambia ewe mtume ?
Mtume akajibu " nawewe huoni nilivyowajibu ewe aisha ?(kamjibu kwa swali)
Umeona hapo mtume kajibu swali kwa swali ndugu yangu ?
2.
Mtume aliwaambia masahaba zake kwamba "hata mtu akimuingilia mmoja wenu mkewe basi anapata thawabu.
Masahaba wakastaajabu wakamuuliza mtume "yaani mmoja wetu anapata matamanio anamuendea mkewe kisha katika starehe hiyo anapata ujira pia ?
Mtume akawajibu kwa SWALI "je munaonaje lau mtu huyo akiweka tupu yake katika haramu,atapata madhambi ?"
Hiyo ni baadhi ya mifano tu ambayo mtume wetu alijibu maswali kwa kutumia maswali,wewe nani mbele ya mtume ndugu yangu ?