Ujio wa CCJ: Yote unayotaka kujua

Ujio wa CCJ: Yote unayotaka kujua

Haya ni maoni yangu, ukiangalia hivi sasa mikoa ambayo ina wapinzani mfano Kilimanjaro, Arusha, Kigoma, Shinyanga na Pemba utaona kuwa wamechagua personality zaidi kuliko sera. Na hata hapa Dar wale wapinzani waliokuwepo kina Mrema walikuwa ni mashuhuri zaidi kuliko vyama vyao. Sina uhakika labda kama kuna analyst mzuri humu ndani atupe ushauri zaidi kuhusu hili.

Ila ni vizuri kuanisha yafuatayo;

Cheyo na UDP wana nguvu kule kwao Shinyanga, Chadema wamejikita kwa kina Slaa, Kabwe na Kilimanjaro, CUF wanapeta Unguja na Pemba. Sasa sijui kama hi ni sababu ya ukabila au watu wa huko wanakubaliana zaidi na sera za hivi vyama kuliko sehemu nyingine bongo.

Hujanielewa, wanaowachagua hao akina cheyo, marehemu kabuye, maremu chacha na mrithi wa chacha wa leo ,ni watu wa mjini?? yani watu wa dar, mwanza dodoma mjini ndo wanaenda kupiga kura kule???
 
Nani asiyeijua Clouds; ni vibaraka wa CCM. Kwao kujipendekeza kwa system ndo motto wao.
 
Kama wanakiona hiki Chama hakina nguvu kwanini wanakibania kukipa Usajili?Kwanini Tendwa anaogopa kukisajili ili kishiriki uchaguzi wa October?.Hata kama wanachama wanajaa kwenye handbag si wakipatie usajili?.
 
kweli pamoja ni mbunge watu walikua hawamjui.....sio rank za akina kingunge.
 
ikiwa kila utakalo sikia kwenye redio utalileta hapa basi itakuwa haina maana, hakuna haja ya kuwajadili wale ni wachekeshaji....kuwajadili ni kuwapa hadhi.....kama wanavyotaka
 
Huyu kijana namwangalia kwa mbali tu!!
anatumika vibaya!! ethics haziruhusu, yy jeuri ya kuwakashifu watu anaitoa wapi?
 
Nipo nimepumzika nasikiliza kipindi cha Jahazi Clouds FM ambapo kama kawaida Ephraem Kibonde akiwa na Partiner wake Gadna Habash wanasherehesha.

Katika Habari waliyoisoma wamekataa kata kata kuwa Mpendazoe kuwa ni kigogo wa CCM. Wamewataja vigogo kuwa ni Jakaya, Mkapa, Msekwa, Kingunge na wengine wenye rank zinazofanana na za hao.

Walichonishangaza na kunisononesha ni kuwa Mpendazoe ametajwa na Kibonde kuwa hana hadhi ya kuwa Kigogo ndani ya CCM badala yake ana hadhi ya TOOTH PICK na katu asijidanganye kuwa ni KIGOGO.
Pia amemponda kuwa asijifanye kigogo kwa kuhama chama kwakuwa hata yeye alihama kutoka CTN kwenda Clouds (kama concept ya kigogo ni kuhama kutoka point moja kwenda nyingine) basi na yeye ni KIGOGO.

Mwenyekiti wa CCJ ameibiwa nyaraka zake Kariakoo leo na katika nyaraka hizo yalikuwepo majina ya wanachama wao. Kibonde amemkejeli sana na pamoja na mambo mengine amekikejeli CCJ kuwa eti " chama gani wanachama wanajaa kwenye handbag(nadhani anamaanisha wanachama ni wachache) na akatoa mfano CCM ambacho kina wanachama kuanzia chipukizi, shule za sekondari hadi vyuo vikuu.

Great thinkers mnaonaje hili? Sio kama ni mpango umeandaliwa na wahuni fulani wa kisiasa kufifisha vuguvugu hili la mabadiliko linaloendelea sasa kwa kuwatumia wanahabari pamoja na vyombo vya habari?

Mzi
Clous FM=Original comedy, wameishiwa.
 
"God hates corruption. Join him! "-Mzittokabwela.
Dare not to forget kuwa Tanzania loves it.Change your citizenship!!
 
Wamzizima

Kitu kingine unatakiwa ukumbuke watanzania tunachagua mtu ktk ubunge.

Kwa hiyo sio kweli kabisa unayoongea kwamba jumla ya kura za upinzani zilikuwa nyingi kuliko za ccm. Nafikiri lazima utambue kuna option A B......

Hivyo kuna uwezekano mkubwa kwamba kama mgombea wa TLP asingekuwepo basi ningepigia wa CCM. Kumbe basi kuunganisha vyama hakuna maana kwamba wale wote ambao walipigia wapinzani wengi tofautitofauti ni hao wote wangempigia mpinzani mmoja.

Mfano Mrema asipogombea urais basi kura yake haitaenda kwa lipumba ,bali itaenda ccm.upo??

MkamaP
Hapa nilikuwa naongela suala la majimbo ya Dar wala si nchi nzima. Ni kweli kwa nchi nzima CCM ilishina kwa kishindo ila kwa Dar natoa mfano tu hapa kwamba e.g Temeke jumla ya kura zilizopigwa zilikuwa 300,000 CCM wakapata 100,000 CUF 60,000 Chadema 40,000 TLP 10,000

Na ni kweli kuwa hakuna ushahidi kuwa kwamba kama wapinzani wangesimamisha mtu mmoja basi wangepata hizo kura 110,000 kama inavoonyesha hapo juu ila kungekuwa na ushindani zaidi na ushawishi mkubwa zaidi kwa watu kuwapigia kura. Ni kweli kwamba labda mpenzi wa chadema akaona ni heri kuwapa CCM kura yake kuliko mgombea wa upinzani say wa CUF
LAKINI ni bora kuliko sasa ambako watu wengi wanaangalia CCM upande mmoja na upinzani upande mwingine ilhali huu upande wa pili yaani upinzani una utitiri wa vyama.
 
Wao wanatakiwa waendelee ku-ze comedyka kwenye mambo ya ki-ze comedy; mtu kama kahama chama wao watuelimishe tu sio kumponda mtu. Shame on them!!!
 
Kwa mtazamo wangu Kibonde amejishushia hadhi katika jamii licha hakuwa nayo
 
kweli pamoja ni mbunge watu walikua hawamjui.....sio rank za akina kingunge.

Mbona mwenyekiti wa upinzani akitoka na kujiunga na CCM mnasema kingunge wa upinzani ahama, sasa huyu kahama CCM pamoja na ubunge bado sio kingunge.
 
Ni wazo zuri ndugu but tunarudi pale pale katika umoja lazima watu wajulikane ni akina nani? chadema tunamjua mzee mtei na Mbowe, CUF yuko Lipumba na Seif, NCCR Mageuzi na wengineo wengi. Haya tuambie CCJ ni akina nani? Historia zao zikoje.

Hivi unadhani wewe utaungana na mtu ambae haumjui mtaaminiana? Kama ana nia kuwavuruga vuruga je?[/QUOTE]

Mkuu mdodoaji,

Niko na wewe katika hili. Kama vigogo walio nyuma ya CCJ bado wanafanywa siri kwa sababu za msingi, sawa hilo nalikubali lakini mbona historia ya huyu Kiyabo haitolewi watu tukamjua? Kuna mtu amedokeza hapa kwamba alikuwa ni mfanyakazi au bado ni mfanyakazi TISS. Sasa kwa ukweli huu mdogo tulionao tayari, mtu atatokaje TISS aazishe chama na TISS nasikia ukishakuwa huko ni kifo tu kinakufanya uache kuwa mfanyakazi huko halafu sisi tumuamini kwamba hii sio janja ya CCM?

Tunaomba muongozo hapa!!

Tiba
 
huyu mgeni hapa ... hajui hapa ni kamili...JAMII INTELLIGENCE UNIT ni kamili...na habari za JF ni 95% confidence interval...

...FM- mzee moto wa ememe..wa gesi lete issuez!!...nipo kimya lakini nakusoma sana ..kwa TAARIFA !!

- Ahsante ndugu yangu ninakusikia sana, moto huo unawaka magogoni hakukaliki jana kidogo watu wale vibao huko, mawasliano leo ni magumu sana lakini upepo ukikaa sawa kama kawa!

Respect.


FMEs!
 
Hawana lolote hao clouds wanapelekwa tu,kama mi ng'ombe,njaa zao zitawaumiza si unakumbuka jinsi walivyoendekeza njaa mpaka wakachukua ZINDUKA ile deal ya SUGU,wakiongozwa na Vasco Da Gama!!
 
yes kibonde ni problem lakini jee mpendazoe ni kigogo?
 
asante sana bro,kuanzia leo,will not take your topic serious yaani ntakua natupa kapuni km sina akili nzuri vile,good that kuna ignore list.
 
Ni wazo zuri ndugu but tunarudi pale pale katika umoja lazima watu wajulikane ni akina nani? chadema tunamjua mzee mtei na Mbowe, CUF yuko Lipumba na Seif, NCCR Mageuzi na wengineo wengi. Haya tuambie CCJ ni akina nani? Historia zao zikoje.

Hivi unadhani wewe utaungana na mtu ambae haumjui mtaaminiana? Kama ana nia kuwavuruga vuruga je?[/QUOTE]

Mkuu mdodoaji,

Niko na wewe katika hili. Kama vigogo walio nyuma ya CCJ bado wanafanywa siri kwa sababu za msingi, sawa hilo nalikubali lakini mbona historia ya huyu Kiyabo haitolewi watu tukamjua? Kuna mtu amedokeza hapa kwamba alikuwa ni mfanyakazi au bado ni mfanyakazi TISS. Sasa kwa ukweli huu mdogo tulionao tayari, mtu atatokaje TISS aazishe chama na TISS nasikia ukishakuwa huko ni kifo tu kinakufanya uache kuwa mfanyakazi huko halafu sisi tumuamini kwamba hii sio janja ya CCM?

Tunaomba muongozo hapa!!

Tiba

Unapoenda kupigana vita ,ngoja tuseme vita ya msituni mbona huwa wanaenda misituni? na wasiende jangwani kweupe upande ule na wa huku waonane vizuri wanapotwangana??
 
Back
Top Bottom