Ujenzi wa madarasa nchini na madhila wanayoyapata wakuu wa Shule

Victor Mlaki

JF-Expert Member
May 1, 2016
3,542
3,451
Habarini wanajamvi!..

Tunafahamu kinachoendelea juu ya ujenzi wa madarasa kote nchini chini ya ufadhili wa IMF lakini kinachofanyika kimenisukuma kuandika haya.

Mosi, wakuu wa shule wamejikuta katika wakati mgumu sana kutokana na kuwepo kwa wimbi kubwa la wakaguzi na wafuatiliaji ambao kila mmoja amekuwa akitoa mapendekezo yake juu ya ujenzi licha ya kuwepo kwa muongozo katika Bill of Quantity (BOQ)

Pili, kumeibuka wimbi la watu wa kati wanaovuruga biashara ya vifaa vya ujenzi, jambo linalosababisha vifaa hivyo kuuzwa kwa bei kubwa kuliko kawaida yake.

Tatu, muda uliopangwa ili kukamilisha ujenzi wa madarasa hayo ni mfupi kiasi cha kutia mashaka juu ya ubora, mathalani hakuna muda wa kutosha ili kumwagilia maji majengo hayo licha ya kutumia saruji nyingi.

Nne, Bill of Quantity haijaonesha gharama zote mfano gharama za maji, umwagiliaji na usafiri.

Tano, licha ya ukweli kuwa kazi hii inahitaji usimamaizi wa karibu katika muda wote wa kazi, hakuna kiasi kilichotengwa kwa ajili ya chakula au maji ya wasimamizi.
 
Anakuja Afisa Elimu anakupangia cha kufanya....

Unakuta anakwambia Halmashauri imeagiza mabati huko kiwandani....lipieni!😎
ah..ah.. hii kuna mahali wanafanya halafu wakaguzi wanawaliza wakuu wa shule juu ya bati. Majibu hawana wanaamua kunyamaza kuwalinda maafisa wao.
 
Walimu chapeni kazi nyie si ndio wamaccm na chama kinawaamini?

Mnasimamia uchaguzi sembuse ujenzi wa madarasa??

Tatizo kujipendekeza sana ili mpewe vyeo.
 
Ni vichekesho. Miradi ya ujenzi wasimamizi kibao! Mara Mkurugenzi(huyu ni sawa akifanya hivyo japo haiwezekani akawa kila shule kwa wakti mmoja), mara DEO, mara Wasaidizi wa DEO, mara sijui mkuu wa idara ya kilimo!

Jambo la ajabu ma kuchekesha wote hawa hawana ujuzi wala uwelewa wa ujenzi. Kila anayekuja anatia maelekezo yake! wakati mwingine wana challenge ushauri wa wahandisi na wasanifu majengo wa Halamashauri!
 
Mimi namuona mwalimu mmoja hapa sengerema kawa kama mwendawazimu. Anashindwa aanze na lipi amalize na lipi....! Kila leo maagizo
Mkuu, hawa walimu wakuu wanapata pressure kubwa sana kutoka kwa viongozi wa Halmashauri zao. Hii miradi inatekelezwa kisiasa zaidi. Na Mkuu wa Shule asipoangalia ang'oka!
 
Back
Top Bottom