Ujasusi - Umoja namba 97

Ujasusi - Umoja namba 97

Mkuu mie ni mmoja wa wafuatiliaji wa stori yako hii nzuri. Pendekezo langu ni kwamba, ili kuleta mtiririko mzuri kwa msomaji, zingatia swala la majina ya watu na miji nafkiri umepitiwa tuu, ila yanapaswa kuanza kwa herufi kubwa.
 
Mkuu mie ni mmoja wa wafuatiliaji wa stori yako hii nzuri. Pendekezo langu ni kwamba, ili kuleta mtiririko mzuri kwa msomaji, zingatia swala la majina ya watu na miji nafkiri umepitiwa tuu, ila yanapaswa kuanza kwa herufi kubwa.
shukrani mkuu .. nitazingatia zaidi katika hili
 
KAULI YA MWISHO YA RAISI
KABLA YA KIFO
UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
UNITY NIGHTY SEVEN (U-97).
MWANDISHI: SINGANOJR

SAFARI YA BENDERA KUELEKEA IKULU

SEHEMU YA 32
Mara baada ya mheshimiwa raisi kumaliza kazi zake siku hio alionekana akiwa kwenye mawazo kweli kwani hata sura yake haikuonesha kuwa sawa kabisa , alionekana kuna jambo alilokuwa akiliwazia muda wote , baada ya kazi alitoka ofisini na kuingia kwenye chumba chake cha mapumziko , hakutaka bughuza siku hio kwani hata mlinzi wake alimpa maaagizo ya kutotaka kuonana na mtu wa aina yoyote , muda huo ilikuwa ni saa kumi za jioni , aliingia kwenye chumba chake hicho na kisha alilala huku akiangalia juu ya ceiling board , alionekana kuwa mbali sana kimawazo .
“Hili swala la Damiani linaniumiza kichwa sana , ni nini Bendera aliacha pasipo ya mimi kujua “ aliongea raisi huku akiingia kwenye mawazo na kurudisha kumbukumbu zake nyuma miaka kadhaa ilio pita
****
Ni mwaka 2014 , kipindi hiki kilikuwa ni kipindi ambacho wanachama wa NLP tulikuwa bize sana hususani na swala la uchaguzi uliokuwa upo mbele yetu , moja ya vitu vilivyokuwa vikituumiza kichwa ni juu ya raisi wa awamu ya nane ajae , hakuna aliekuwa akielewa ni raisi gani ambae anakuja kuchaguliwa na chama na hatimae kuipeperusha bendera , nikiwa moja ya watu ambao nilitamani sana na sio kutamani tu nilikuwa na nia haswa ya kuwa mgombea kupitia chama changu ya kuwania kiti cha uraisi ,lakini japo nilikuwa nikikubalika katika halmashauri kuu ya chama , lakini swala hilo lilikuwa na ugumu wake.

Moja ya watu ambao walikuwa nyuma yangu alikuwa ni rafiki yangu Bendera , ndio nasema ni rafiki yangu kwani tulikuwa tukishirikiana mambo mengi ya kiuongozi , kwani bendera wakati huo alikuwa ni waziri wa ardhi na mimi ni kiwa waziri wa maliasili na utalii .
“ Henry unaonaje harakati za uchaguzi ujao ?” lilikuwa ni moja ya swali aliloniuliza bendera siku hio tukitoka kwenye kikao cha mawaziri , kikao kilichoongozwa na mheshimiwa mwenyewe raisi Athumani ndalu .
“ Mchakato unaonekana kuwa mgumu sana , japo nia yangu ya kupata nafasi ya kupeperisha bendera iko palepale “.
“Ni kweli hata mimi kwa sasa sijui mheshimiwa anampendekeza nani , lakini sio swala la kukata tamaa , lazima ujiimarishe ndani ya chama hususani kwa wajumbe ili uweze kupata nafasi ya kupeperusha bendera “ Aliongea Bendera maneno ambao kwa namna moja ama nyingine yalinitia nguvu sana .

Siku zikakatika huku vikao vingi ndani ya chama vikiendelea , viongozi mbali mbali wakubwa walikuwa wakitamani kuaminiwa na chama na kupewa bendera kwa ajili ya kuipeperusha katika kinyang`anyiro cha uchaguzi ujao , kila mtu alikuwa akionekana kujiimarisha vizuri ndani ya chama hususani halmashauri kuu , kwa upande wangu japo nilikuwa na wasiwasi lakini nilikuwa na uhakika wa kupata nafasi , kwani nilikuwa nimefanya kazi kubwa sana ya kuweka watu wangu ndani ya wajumbe ambao nilikuwa nikiamini kama ni swala la kura basi na mimi ningekuwa moja ya watu ambao ningekuwa na kura nyingi sana , pia swala hilo sikuwa nikilifanya mwenyewe kwani kulikuwa na watu wangu wa karibu ambao walikuwa wakinipa sapoti ,moja ya watu ambao walikuwa wakinipa sapoti ni Bendera alikuwa na yeye kwa namna yake akijaribu kushawishi watu wanichague , japo hata yeye siku za mwisho mwisho alichukua fomu ya kuwania uraisi lakini hakuacha kunipa sapoti , mpaka kuna muda niliwaza , Bendera alichukua fomu ya nini ,maana hakuwa mtu wa kujipigia kampeni Zaidi ya kuwahamasisha watu wanichague mimi , watu walio chukua fomu walikuwa ni wengi sana na mchujo ulikuwa ni mkali .

Basi baada ya miezi kupita hatimae ilikuwa ni kikao cha halmashauri kuu kwa ajili y a kumchagua mtu ambae ataipeperusha bendera ya chama katika uchaguzi utakao fanyika mwaka huo miezi michache ijayo , maraisi mbali mbali wastaafu na wabobezi wachama walikuwepo kuhakikisha kwamba hakuna kitu kinacho haribika , siku hio nilikuwa nipo nyumbani kwani sisi ambao tulikuwa tumechukua fomu hatukuruhusiwa kuhudhuria vikao hivyo .

Macho yote yalikuwa kwenye runinga kuangalia kile kinacho endelea , familia yangu mke wangu wema ambae nilikuwa nikimpenda sana hakuwa mbali namimi kiufupi alikuwa ni moja ya wanawake ambao walikuwa wakinipa faraja sana katika dunia hii , kwani tulipotoka mpaka kufikia wakati huu maisha hayakuwa rahisi hapo nyuma tumepitia changamoto nyingi sana za kimaisha kiasi kwamba kuna kipindi nilitaka kukata tamaa , lakini kwa msaada wa mke wangu niliweza kuyavumilia yote .

Kikao cha halmashauri kilichelewa sana kumalizika mpaka kuna muda tulikuwa tukishangaa ni jambo gani lilikuwa likiendelea ndani ya kikao hicho , kila kilichokuwa kikifanyika kilikuwa ni siri tena siri kubwa sana kiasi kwamba hakuna ambae alikuwa akijua ni nini kilikuwa kikiendelea ndani ya kikao hicho, sio mimi sio bendera na wengine waliokuwa wamechukua fomu walikuwa hawajui ni nini kilikuwa kikiendelea kwenye kikao hicho .

Saa moja kamilii ndio waandishi wa habari walionekana kuzonga zonga viongozi na ni muda ambao uliashiria kabisa kuwa sasa kikao kilikuwa kimeisha na ni wakati wa kutoa matokeo ya kile kilicholkuwa kikiendelea siku nzima kwenye kikao hicho .

Alikuwa ni katibu mkuu wa chama ndie alikuwa kwenye mahojiano na waandishi wa habari huku mkononni akionekana kushika karatasi ambao kwa hakika ilikuwa ni ya wale ambao walikuwa wamepita katika tano bora ambao moja kwa moja baada ya kutangazwa kungeitishwa kikao cha mwisho cha wajumbe ambao wangempigia kura mtu mmoja kati ya hao watanao na ambae angeweza kushinda kwa kura nyingi basi angekuwa ndio mtu atakae shindania nafasi ya uraisi kwa mwaka huo , roho yangu ilikuwa juu juu kusikiliza matokeo hayo .
“ Awali ya yote nimshikuru sana mungu kwa kutupigania mpaka muda huu , kwa kuendela kutupa uhai na kutuweka wazima na hata pia kulilinda taifa letu zuri la Tanzania , najua ndugu waandishi wa habari mnayo hamu ya kusikiliza kile ambacho kimeamuliwa katika kamati kuu ya chama na nipo mbele yenu hapa kwa ajili ya kutangaza tano bora ambayo imepita, wagombea ni mia moja ndani ya chama ambao wamechukua fomu , na bila kupoteza muda niende moja kwa moja katika kutangaza majina hayo , wagombea waliopita ni Damasi macha , Ridhiwani kileo , Albert jumbe , Nusra hassani na wa mwisho ni John Bendera Onyango “

Nilijikuta nikisimama huku siamini kabisa , sikuamini kama nilikuwa nimekosekana hata kuingia kwenye tano bora na kilicho nishangaza Zaidi ni juu ya rafiki yangu Bendera kuingia kwenye kumi bora kwani hakuwa hata na juhudi za kugombea nafasi hio na hata kwa fomu alichukua mwisho mwisho , sikuamini kabisa , lakini sikua mwenyewe ambae siamini kwa matokeo hayo, kwani watu wengi hawakutegemea kabisa , kwani walikuwepo watu wakubwa ambao walikuwa wakikubalika ndani ya chama na pia hata kwa wananchi ambao hawakupita katika nafasi hio lilikuwa ni jambo la kushangaza lakini pia liloacha maswali ni kipi kilikuwa kikiendelea katika kikao hicho .
Mke wangu aliishia kunifariji lakini kwa wakati huo ni kama moyo wangu ulisimama , kwani nikikumbuka hela nyingi ambazo nimetumia kwa ajili ya kupata nafasi ya kuipeperusha bendera moyo uliuma sikua na jinsi kabisa wala jambo ka kufanya kwa wakati huo jambo ambalo nilikuwa nikitaka kulifanya kwa wakati huo lilikuwa ni kupumzika na kutuliza akili yangu kwani niliamini nisipofanya hivyo naweza kupata mshituko wa moyo , simu kutoka kwa Bendera ndio ilionitoa kwenye dimbwi la mawazo , niliingalia jinsi inavyo ita huku nikijishauri niipokee ama nisipokee , mke wangu na yeye alikuwa akiangalia ni hatua ipi ambayo ningefanya kwa wakati huo , lakini alionekana ni mtu ambae alikuwa akionekana kunitaka nipokee simu hio , iliita mara ya kwanza ikakata na ikaanza kuita mara ya pili na hapo ndipo niliponyoosha mkono wangu na kuchukua simu hio na kisha niliipokea na kuweka sikioni..

“ Rafiki yangu nimeyaona matokeo ya tano bora , lakini hata mimi yamenishangaza sana , sijui ni nini kilichokuwa kikiendelea katika kikao hicho , kwani jambo la wewe kukosa limeniumiza sana lakini pia nimeshangaa mimi kupata kuingia kwenye tano bora “ Alingea Bendera na alinifanya moyo wangu uume Zaidi kwani niliona kwa wakati huo alikuwa akinikejeli , niliona kama ni mtu ambae amenizunguka kwani sikuamini kabisa kama Bendera angepita ilihali hakuwa mtu ambae aliweka juhudi ya aina yoyote katika kupita katika kinyang`anyiro hicho , sikua na cha kumjibu Zaidi ya kumwambia hongera na kuwa na kubaliana na matokeo.
“ Hongera sana Bendera rafiki yangu , hakuja haribika kitu nakubaliana na matokeo , ilihali wewe upo kwenye tano bora tuombe uingie kwenye top 3” niliongea japo moyo ulikuwa ukiniuma sana , niliona ndoto zangu za kuwa raisi zilikuwa zinakomea hapo.

Nilicho shukuru ni uwepo wa mke wangu , kwani alikuwa akijua vyema kunituliza na kurudi kwenye hali ya kawaida , basi baada ya kukubaliana na mtokeo huku watu wengi wakionekana kushangazwa na watu waliopita lakini kwa upande wangu sikuwa na lingine la kuzungumza kwani niliona kilichokuwa kimetendeka kilikuwa kimetendeka na matokeo yashatoka na hakukuwa na uwezekano wa kuyabadilisha , nilichokuwa nikisubiria kwa wakati huo ni kutaka kujua ni nani atapita katika tatu bora , japo kwa Bendera alikuwa amepita lakini kwangu niliona asingeweza kufanikiwa kuvuka kuingia tatu bora .
Basi siku mbili baadae kikao cha wakuu wa kamati kilikaa tena kwa jili ya kufanya mchujo wa tatu bora , siku hio na mimi nilikuwepo jijini Dodoma kuhudhuria kikao cha halmasharui kuu kama mjumbe na hata pia kwa mke wangu niliongozana nae siku hio .
Siku hio kikao hakikukawia sana kumalizika kwani baada ya masaa mawili tu ya kikao hiko kufanyika hatimae matokeo yalitolewa , lakini ajabu na jambo ambalo sikulitegemea kabisa ni rafiki yangu kupita katika tatu bora hio , japo moyo uliniuma kwani niliona labda kuna mchezo wa chini chini Bendera alikuwa akiufanya pasipo ya mimi kujua lakini pia nilikuwa nafuraha juu yake kupita katika hatua hio , mbaya Zaidi ni kwamba watu ambo alikuwa amepitishwa nao walikuwa hawana ushindani wa aina yoyoate jambo ambalo kwangu niliona Bendera alikuwa na nafasi kubwa ya kishinda ndani ya tatu bora hio , watu wengi hawakuamini kama bendera alikuwa kwenye tatu bora hio .
Basi hatua ya kupiga kura ikaandaliwa utaratibu wake huku watu wakiwa wameujaza ukumbi vilivyo wajumbe kutoka mikoa mbali mbali walikuwa katika eneo hilo kuhakikisha kwamba wanamchangua mtu ambae wlaikuwa wakimini anaweza kuiongoza Tanzania na kuifikisha katika maendeleo .
Baada ya wagombea kujinadi akiwemo rafiki yangu Bendera nilifarijika sana , kwani niliona japo nilipoteza pesa nyingi katika kutaka kupata na fasi ya kuwania kiti cha uraisi lakini niliona gharama zangu hazikwenda bure kwani rafiki yangu Bendera alikuwa kwenye nafasi nzuri ambayo niliamini kupitia yeye ningeweza kuzirudisha .

Baada ya kujinadi hatimae wajumbe walipewa nafasi ya kupiga kura , zoezi ambao halikuchukua muda mrefu sana maana lilikuwa kwenye mpangiliio mzuri wa kiutaratibu , baada ya zoezi hilo kuisha hatimae ilikuwa ni wakati wa kuhesabu kura , zoezi ambalo kulikuwa na watu maalumu ambao walikuwa wakihusika na kulifanya zoezi hilo basi sisi wajumbe wengine ambao kwangu mimi niliona ni ndoto kwani mwanzoni nilikuwa na uhaikika kwa kushinda , tulikuwa tukiburudishwa na nyimbo za wasanii mbali mbali huku tukisubiria matokeo .

Masaa machache tu matokeo yalikuwa tayari na katibu wa chama wa uenezi alitoa matokeo hayo na hapo kila mtu alionekana kuwa na furaha sio mimi tu niliokuwa na furaha lakini pia hata mke wangu aliekuwa pembeni yangu alionekana kuwa na furaha kiasi cha kutoa machozi na hio ni mara baada ya Bendera kupewa nafasi ya kuipeperusha bendera katika kuwania nafasi ya uraisi watu wengi walionekana kutoaamini kile kilicho tokea lakini matokeo yalikuwa ndio hivyo , nilimpa mkono wa hongera rafiki yangu Bendera , na sikua na kinyongo nae kwani urafiki wetu likuwa Zaidi ya mafanikio , hivyo hakukuwa nasababu ya kumchukia rafiki yangu kisa kapata nafasi ambayo na mimi ilikuwa ni ndoto yangu ya kuipata .

Baada ya bendera kupewa maiki na kuwashukuru watu wote kwa kumpigia kura kwa kumwamini hatimae alipewa nafasi ya kuchagua mtu ambae angeweza kuwa mgombea mweza yaani makamu , na hapo ndipo nilipopigwa na butwaa na hio ni mara baada ya Bendera kulitamka jina langu , ni kama nilikuwa mtu ambae siku sikia vizuri lakini furaha ya mke wangu ilinijulisha kwamba nilikuwa nimesikia vizuri , basi kwa shangwe nilikaribishwa na kupewa maiki na kuongea machache ambayo kiukweli nilikuwa sina cha kuongea Zaidi ya kutaka kumshukuru bendera lakini pia kuwaahidi wananchi kwamba endapo tutapata ridhaa ya kuingia ikulu basi tungejitahidi kwa uwezo wetu wote kuhakikisha tunawatendea yalio mazuri wa Tanzania kupitia kusimamia haki na maendeleo ya taifa kwa ujumla .

Hatimae baada ya kikao hicho kampeni ya kuzunguka nchi nzima ilianza , kwangu japo sikua katika nafasi ya kuwa raisi lakini swala la kumpa sapoti rafiki yangu bendera lilikuwa ni swala ambalo nililifurahia lakini pia nilifanya kwa moyo wote .
Ilikuwa ni swala ambalo tulikuwa tumegawana kwani kama Bendera ataenda mashariki kwenye kampeni basi na mimi ningeenda kaskazini au magharibi kwenye kampeni , kwa muda wa miezi miwili tulifanikiwa kufanya kazi nchi nzima na kilicho baki kilikuwa ni wananchi kutupigia kura na kuwachagua wale viongozi waiokuwa wakiwapenda .

Ushindani ulikuwa ni mkubwa sana kwani kuna waliokuwa wapo ndani ya chama na wakahamia kwenda kwenye vyama vingine na walikuwa na ushawishi wa hali ya juu , lakini jambo hilo halikuwa sabau ya sisi kukata tamaa ,uhakika wa kushinda ulikuwa upo pale pale na mimi nafasi ya kuwa makamu wa raisi na bendra kuwa raisi wa JMT ulikuwa pale pale .

Hatimae siku ya kupiga kura iliwadia wananchi katika kila jimbo walipewa utaratibu wa kupiga kura huku wakihamasishwa kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kuchagua viongozi wanao wapenda iikiwemo wabunge madiwani na raisi , tulikuwa tukipenda kuita mafiga matatu yaani , yaani kwamba ili sufuria ifiti jikoni basi ilikuwa ikihitahi mafiga matatu .

Basi zoezi la kupiga kura lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kila vituo , japo viongozi wengi walionekana kuwa na presha juu ya mshindi lakini pia changamoto za hapa na pale katika uchaguzi huo hazikukosekana , lakini la kumshukuru mungu ni kwamba zoezi lilienda kama lilivyopangwa na tume ilionekana kuwa mahiri katika kusimamia zoezi hilo , moja wapo waliopiga kura ni mimi na bendera , nilikuwa na wasiwasi na furaha , urafiki wangu mimi na bendera ulikuwa mkubwa sana kiasi ambacho ilikuwa kututenganisha ilikuwa ni ngumu sana kwani wapo wengi walijaribu kufanya hivyo lakini walishindwa , kwani urafiki wetu haukuwa kwenye siasa tu bali mpaka kwenye familia , siku hio nilikuwa nyumbani kwa Bendera mimi na na mke wangu katika kusubiria matokeo hayo kwa siku hio ya kwanza .

Matokeo yalitangazwa huku mchuano ukiwa mkali kweli , ilikuwa ni nusu kwa nusu kwani mwingine akishinda jimbo hili mwingine alikuwa akishinda jimbo lile , ilikuwa ni presha presha tu lakini pia tulikuwa wavumilivu kuona hadi mwisho .

Hatimae saa saba usiku siku ya pili ya kuhesabu kula bendera alitangazwa kuwa mshindi na kuwa raisi mteule wa JMT , hakika ilikuwa ni furaha kwa Bendera na pia kwa wafuasi wake na kwa familia kwa ujumla , nilifurahia pia kwa mafanikio hayo rafiki yangu alioyafikia, watu mbali mbali walitoa pongezi za dhati kwa raisi Bendera kwa kufanikiwa kuchukua ofisi ya raisi , kuna muda nilitamani ningekuwa mimi lakini sikuwa na jinsi kabisa kwani pia nilishukuru kuwa katika nafasi hio ya umakamu wa uraisi kwani nilimini pia ingenipa nafasi ya kuwatumikia wananchi katika kuwaletea maendeleo .

Hatimae baada ya siku mbili hafla ya kumwapisha raisi wa JMT mteule bwana bendera ilifanyika kikamilifu na kuwanzia siku hio na saa hio raisi Athumani ndalu akaachia madaraka rasmi na kumkabidhi mheshimiwa Bendera , ilikuwa ni swala la kujivunia sana kwa Tanzania kwani mambo mengi yalifanyika kiamani kabisa tofauti na nchi nyingine ambayo raisi kuachia madaraka lazima nguvu itumike lakini katiba ya Tanzania iliheshimiwa vilivyo


SEHEMU YA 33

MWANZO WA CHOKOCHOKO

Basi siku mbili mbele mheshimiwa Bendera alikuwa amekabidhiwa ofisi rasmi na mimi pia nilikuwa makamu wa raisi rasmi na nilikuwa na ofisi yangu , kusema ukweli nilikuwa nikimshukuru sana rafiki yangu Bendera kwa kuniweka katika nafasi hio kwani sikujua kama ningekuwa katika hali gani kwa wakati huo kwani nilikuwa nimewekeza kiasi kikubwa mno cha pesa katika uchaguzi huo ili kuja kuwa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania , lakini kuwa makamu wa raisi kidogo kulipunguza yale makali ya hasara ambayo nimepata , lakini niliona pia sio mbaya kwani ni moja ya hatua ambayo nilikuwa nimepiga katika maisha yangu , mke wangu na familia yangu walinipa hngera na kunitia moyo kwani na wao pia walikuwa ni watu waliokuwa wakijua kuwa nilikuwa nikiwa na ndoto ya kuwa raisi kwani niliwashirikisha kabisa , watoto wangu wa tatu , yaani Patrick na wadogo zake wawili wa wakike , watoto ambao nilibahatika au niseme Mungu alinijaalia kunipatia nikiwa na mke wangu kipenzi wema , labda nigusie tu nilikuwa nikimpenda sana mkwe wangu Wema , alikuwa ni moja ya wanawake ambao walikuwa wana akili ya kimaisha sana , kwani nakumbuka kipindi ambacho nilijuana nae alikuwa ni mwanamke moja mashuhuri sana kibiashara hapa nchini , na kipindi hicho alikuwa mrembo kweli na siku ya kwanza tu kumuona nilitokea kumpenda hapo hapo na kipindi hicho nikiwa waziri basi ndipo nilimfukuzia mpaka kuja kumpata nikiwa nimetumia nguvu nyingi kumuweka katika himaya yangu na hatimae kuoana nae , ni mwanamke ambae anatabia njema sana kwa kipindi nilichomjua hakuwa na skendo yoyote mbaya .

Basi hatimae baada ya kuwa na madaraka kamili ya kuwa makamu wa raisi na rafiki yangu Bendera kuwa raisi hatimae kazi rasmi ilianza , nilikuwa na munkari kweli wa kuhakikisha namshauri vyema rafiki yangu Bendera ili kufikia malengo na ilani ya chama kama ilivyokuwa ikitutaka , lakini Bendera mara baada ya kupewa madaraka alionekana kubadilika kwanzia kimtazamo na 'approach';zake katika uongozi m kwangu haikuwa na shida sana kwani niliamini kuwa raisi wa nchi sio jambo rahisi , ni swala ambalo kila mtu alikuwa akikuangalia utafanya nini, na mimi niliona sikua kwenye nafasi ya kumlaumu bendera , Zaidi ya yote kuhakikisha ninatimiza majukumu yangu kama makamu na kumshauri pale itakapo bidi , basi raisi bendera alianza na sakata la kukomesha madawa ya kulevya nchini swala ambalo hata mimi nilimuunga mkono kwa asilimia zote na swala hilo lilifanikiwa kwa asilimia kubwa japo kuna mambo mengi yalifanyika mpaka kuandikiana mikataba na wafanya biashara hao kutoa biashara zao hapa nchini na sababu hio ni kutokana na swala hilo lilikuwa likihusisha viongozi wakubwa wa nchi hii .

Ni baada ya miaka miwili ya uongozi wa rafiki yangu raisi Bendera sasa alikuwa moja ya watu wachapakazi kweli kweli na mimi nilimjua vyema tokea akiwa waziri , japo kuna madhaifu aliokuwa nayo lakini mimi nilikuwa nikimpenda kwa nafasi yake na nilikuwa nikimtetea kwa jambo lolote lile , japo mishale kwake ilikuwa mingi na watu wakimtuhumu kama raisi asiependa ushauri na mengineyo mengi lakini kwangu mimi nilikuwa nikimkubali sana na pia alikuwa ni rafiki yangu na nilikuawa nikimjua alikuwa na nia ya kulifikisha taifa hili katika sehemu ambayo wananchi wengi watakuwa na maendeleo na kumkumbuka kwa mazuri alio yafanya .

Kazi kubwa ambayo nilikuwa nikiifanya kama makamu wa raisi ilikuwa ni kumuwakilishwa raisi Bendera katika ziara nyingi za mataifa ya nje , kwani ni moja ya mtu ambae hakuwa kabisa akipenda kusafiri na wala hata mimi muda mwingine sikumwelewa na kuna muda najaribu kumshauri kusafiri lakini kwake ilikuwa ngumu kwani alisema alikuwa na kazi nyingi za kufanya na huku akinihakikishia kwamba nikienda mimi na yeye atakuwa ameenda kwani anaamini nitamuwakilisha vyema .

Ilikuwa ni siku ambayo nilisafiri kutoka nchini Tanzania kwa ajili ya kumuwakilisha raisi katika kikao cha wakuu wa nchi kikao cha jumuia ya Afrika maishariki yaani EAC (EAST AFRICA COMMUNITY ) , kwangu kusafiri na kumuwakilisha mheshimiwa halikuwa swala baya kwangu kwani ni swala ambalo lilinifanya kujuana na watu wengi na kufanya 'exposure' yangu kuwa kubwa na nilijenga 'connection' nyingi kweli za kibiashara , sasa ni muda wa saa kumi na mbili ndio muda ambao kikao cha wakuu wa nchi kilikamilika na mimi kwa upande wangu nilikuwa nimechoka haswa , na kwa wakati huo nilikuwa nikiwaza kuondoka na kurudi hotelini ili kujipumzisha , nilitoka nikiwa nimeongoza na baadhi ya wasaidizi wangu na ndani ya madakika kadhaa tu nilikuwa ndani ya hoteli hio ijulikanayo kwa jina la EKA , nilinyoosha moja kwa moja mpaka kwenye lift na kuelekea upande wa chumba changu , lakini ile natoka kwenye lift hapo ndipo nilipopokea ujumbe , ujumbe ambao ulinishangaza , ujumbe ambao ulikuwa ukinihitaji kuonana na raisi mstaafu wa wamu ya saba bwana Athumani ndalu , sikujua mheshimiwa alikuwa na shida gani na mimi lakini nilinuia kutii wito , kwani jambo la yeye kuwa katika hoteli hio tena nchini Kenya niliona huenda likawa jambo la muhimu , basi baada ya mimi kuingia kwenye chumba changu niliweza kubadili nguo na baada ya kuoga nilichukua simu na kuwasiliana na mke wangu kipenzi , kwani mwanamke huyu alikuwa akinitia nguvu kila ninapo isikia sauti yake hususani pale ninapokuwa nimechoka na majukumu ya kazi .

Basi masaa mawili baadae nilitoka kwenye chumba changu mara baada ya kujiandaa na kisha nilielekea kwenye miadi ya kuonana na raisi mstaafu , japo nilikuwa nimefanya nae kazi kama waziiri wake katika uongozi wake lakini sikuwa nimemzoea sana .

Basi baada ya kukaribishana na mheshimiwa huku akiyafanya mazungumzo yetu yawe ya kirafiki Zaidi na mimi sikuwa na waswasi kwani nilifika hapo kwa ajili ya kujua kile alicho niitia hivyo sikuona shaka kabisa , swali kubwa aliloniuliza lilikuwa ni juu ya maoni yangu juu ya uongozi wa Bendera swala ambalo niliamini kabisa lazima angetegemea jibu zuri kutoka kwangu kwani hakuna mtu ambae hakujua mahusano yangu na Bendera ukiachana kazini lakini pia katika familia ,kwa hio nilikuwa katika nafasi ambayo nisingeweza kutoa mawazo ambayo hayamuungi mkono mheshimiwa ..

“ Kwanza niseme kwamba , katika kipindi kile cha kumpitisha mgombea nilijitahidi kuliweka sana jina lako katika kipaumbele , kwani nilikuwa mmoja ya watu ambao waliokuwa wakiamini sana katika juhudi zako katika utawala bora , kwanzia ukiwa waziri wangu wa maliasili na utalii ulionesha uhodari mkubwa katika kuiongoza wizara na kuleta mandeleo chanya hususani katika kuiboresha sekta ya utalii na kuifanya kuongeza mapato kwenye serikali , licha zilikuwepo sababu nyingi sana za mimi kuweka jina lako , lakini nafasi hio ilishindikana , na naamini mpaka sasa hujaelewa ni kwanini Bendera alipita na si wewe ?”

“ Mheshimiwa hilo swala silijui kabisa na hata mimi nilishangazwa na matokeo , lakini nilikubali yote matokeo”.
“ Niliamini kabisa utakubaliana na matokeo kwani wewe ni moja ya watu majasiri na waliojaliwa na busara kubwa sana , na naamini kabisa taifa hili linakuhitaji na sio kama makamu wa raisi lakini kama raisi kamili “ Aliongea mheshimiwa na kunifanya nishituke , maana sikuwa nikijua anacho maanisha .
“ Unamaanisha nini mheshimiwa , maana naamini kwenye nafasi yangu kuwa raisi tena ni jambo ambalo haliwezekani na kwasasa nimeamua kwa nguvu zangu zote kuhakikisha namsapoti raisi bendera kuhakikisha taifa linapata maendeleo .”
“ Ni kweli uyazungumzayo , lakini swali ni moja je unamuamini mheshimiwa bendera atalifikisha taifa katika maono ya watanzania wengi , kile ambacho wanategemea ?”.
“ Mheshimiwa mstaafu swala hilo ni la muda kufanyika na linahitajika mipango katika kulitimiza , lakini mimi namjua raisi bendera kabla hata ya kuingia kwenye maswala ya siasa , hivyo kwa nia yake ya dhati kabisa naamini atalifikisha “.
“ Unamwamini rafiki yako ?”.
“ Ndio namwamini mheshimiwa kwanini unauliza hivyo ?”
“ Nnajua kwanini yeye ni raisi na sio wewe ?”
“ Hilo siwezi kulifahamu nyie si ndio mlioteuwa mpaka kuwa leo ni raisi “ Nilijibu huku akioneakana kabisa kufurahishwa na jibu hilo kwani aliinua glass yake ya wine na kisha alipiga pafu moja na kisha akaiweka mezani huku akikunja nne .
“Labda nikwambie jambo ambalo hulijui , ni kwamba rafiki yako kuchukua fomu kwake hakukuwa kwa bahati mbaya , ila kuna watu ambao walimshauri kuchukua fomu ya uraisi , je wewe unalifahamu hilo kama kweli ni rafiki yako “. Aliongea na swala hilo kidogo lilinifikirisha maana ni kweli siku ambayo bendera anachukua fomu aliniambia yeye anaongeza idadi tu ya wanao chukua fomu na wala hana nia ya kuwania uraisi , lakini leo nikunganisha na maneno ya mstaafu kuna picha inayojengeka kwenye kichwa changu , sababu alionipaga bendera leo ndio nilijua ilikuwa sio ya kimantiki .
“ Labda nikwambie tu kwamba aliemshauri kuchukua fomu sio mtu mmoja , ni wakongwe wa chama wakiwemo wastaafu wa uraisi namaanisha maraisi watatu wa awamu ya sita ,ya tano na ya nne , huku wakishirikiana kiukaribu na mstaafu wa TISS bwana Ngalu kuhakikisha wana 'mobilize' (kuwashawishi ) wajumbe kumpigia kura , lakini pia kupitishwa katika kamati kuu ya chama “ aliongea mheshimiwa Ndalu na jambo hilo lilionekana kuwa na ukweli kwani hizi tetesi nilikuwa nikizisikia sana , lakini sikutaka kuzifatilia lakini leo najua ukweli wake .
“ Nadhani walimuamini kama anaweza kutuongoza na ndio maana wakamshawishi kugombea nafasi ya uraisi , kwa hio kama hao walimuamini mimi sina kinyongo kabisa , japo kuna mambo ambayo hajaniambia lakini naamini kulikuwa kuna sababu na Bendera ni rafiki yangu tunaweza tukakaa na tukaongea na yakaisha sina kinyongo juu ya swala hilo “
Niliongea kwani hata hivyo siku taka mambo yaliopita yakanifanya nigombane na raisi wangu , niliona jambo jema na la busara nikusahau yaliopita .
“ Uyazungumzayo ni ya kweli , lakini taifa hili linahitaji watu ambao wanaaminiana , hapa nikimaanisha kama viongzi wakuu wa nchi , kwani kupitia ninyi ndio maendeleo ya nchi yataonekana , ila mkiwa na mitazamo tofauti , nchi haitaendelea kwahio siku ya leo kuja kukutana na wewe ni kukupa ushauri kwamba swala hili unatakiwa kulifanyia uchunguzi , lakini swala la mwisho nataka nikuambie: “ Aliongea huku akivuta pumzi na kuendelea ,
" Nadhani ushaona raisi Bendera alivyotokomeza biashara ya madawa ya kulevya , lakini naamini mpaka sasa unajua kuwa mimi ni mmoja ya wahusika wa sakata hilo , na kwanza ni kupe hongera kwa kumshauri vyema mheshimiwa lakini kuna jambo haulijui wewe na kama moja ya viongozi wa juu unapaswa ulifahamu “.
“ Swala gani mheshimiwa ?”
“Hili ni swala muhimu Zaidi kwako na pia kwa maisha yako kwa ujumla , nadhani unamjua Bruno Lamberk vizuri na habari zake , ukiachana na kusaidia watu lakini pia naamini kuna mengi ambayo unayajua ambayo wananchi wa Tanzania hawayajui , lakini nataka kukwambia kwamba kuna zaidi ya ambayo huyajui “
“ Mheshimiwa umeniacha kwenye njia panda ni jambo gani hilo ?”
“ Unafikiri kwa mtu kama Bruno ilikuwa kwake ni rahisi kuacha biashara yake inayo muingizia madolla na kujiunga na raisi kwa ajili ya kutokomeaza madawa ya kulevya , au unaamini ni swala jepesi kwa mtu kama bruno kusaliti umoja wenye nguvu duniani kote U-97 na kujiunga na raisi huku akijiingiza katika viita ambayo hawezi kushinda na umoja huo ? “.

“ Mheshimiwa swala hilo nalifahamu fika na japo sitoliweka wazi kwani ni moja ya kazi za siri za nchi lakini naomba nikwambie kwamba swala hilo nalijua na hata kama ni mimi ningekuwa kwenye nafasi ya bruno ningeweza kufanya aliofanya “
Niliongeea na alionekana hakuwa na waswasi kwani alionekana kutabasamu jambo ambalo lilinichanganya kwani niliamini kila ninacho kiiongea ni kama alitegemea kama nitaongea hivyo

“ Fuatilia historia ya Bruno kwa undani kuhusu maisha yake baada ya kufika Tanzania , na utaamini maneno yangu ninayo sema hapa yanamaanisha nini , na nikwambie tu kwamba kama ulivyo sema kwamba swala la Bruno alilolifanya lilikuwa ni sawa kwamba hata wewe ungelifanya , basi jaribu kufanya na hili na utaona na wewe ,swala hili linakuhusu kwa asilimia mia moja “ aliongea raisi na kunifanya nishituke , sikujua ni jambo gani analotaka kuongea .
“ Mheshimiwa kwanini usiniweke wazi “.
“ Kwangu msaada mkubwa nina kupatia ni kukusaidia kukufumbua macho na kuna mengi sana ambayo huyajui na yanayo igusa familia yako moja kwa moja , na mimi kwanzia sasa sina mengine ya kuongea , ndio jambo ambalo limenileta hapa , lakini pia nimefanya haya kwakuwa na kuamini sana na najua unaweza kuwa kiongozi bora sana watanzania wanaemhitaji kwa hio jaribu kufatilia swala hili “ Aliongea mheshimiwa na kisha alihitimisha maneno yake na mimi ilibidi nitoke huku nikiwa nimechanganyikiwa , sikujua mheshimiwa alikuwa akimaanisha nini .
Nilirudi kwenye chumba changu nikiwa na mawazo mengi , mambo mengi yalianza kupita katika kichwa changu , niliona swala hilo ni kama fumbo kubwa ambalo kwangu mimi ndie muhusika ambae nilikuwa nikihitaji ufumbuzi wake , sikujua ni kipi mheshimiwa ndalu alichokuwa akimaanisha , lakini maneno yake yalikuwa na ukweli , lakini sasa ni ukweli upi ambao mimi nilikuwa si ujui ambao Bendera alinificha , jambo lilopelekea mpaka mheshimiwa mstaafu kunifata nchini kenya , ni lipi dhumuni lake la kuniambia hayo yote , anataka kutimiza nini . yalikuwa moja ya maswali mengi ambayo yalikuwa yakitiririka katika kichwa changu .

Basi hatimae kikao cha wakuu wa nchi kilikamilika na kuisha siku iliofuta japo sikuwa sawa kabisa kimawazo mood yangu yote juu ya kikao hicho ilikuwa imepotea , swala nililokuwa nikiliwazia kwa muda huo lilikuwa ni kurudi nchini kwangu kwa ajili ya kukaa nchini na kuwazua jambo ambalo mheshimiwa ndalu alikuwa ameniambia .

Basi hatimae nilirudi nchini Tanzania na kuendelea na majukumu mengi ya kikazi , wakati narudi sikuweza kumkuta mheshimiwa raisi kwani kwa wakati huo alikuwa ziairani mikoani , hivyo niliwasilaiana nae kwa simu na kumjulisha kuwa nimerudi na kunipongeza na kunipa pole , baada ya siku kadhaa mheshimiwa alimaliza ziara yake , nilipanga kuonana nae kwa ajili ya maswali kadhaa kwani swala la mstaafu aliloniambia lilikuwa likiniumiza kichwa sana
“ Mheshimiwa mheshimiwa kuna mgeni wako “
Ilikuwa ni sauti ya bodyguard wa raisi ndio iliomshitua mheshimiwa henry aliekuwa kwenye dimbwi la mawazo , alijikuta akishituka na kuangalia saa na kuona alikuwa kwenye kumbukumbu ya kimawazo na wala sio kupumzika kwa muda mrefu sana .
“ Ni nani ? aliuliza
“Ni tajiri samueli saitoto “ aliongea bodyguard na kumfanya mheshimiwa ashangae kwani alikuwa akijua kuwa mtu huyo hakuwa nchini , lakini kidogo swala hilo lilimpa unafuu kwani ni mara nyingi alijaribu kumtafuta bwana huyo .bila mafanikio .
ITAENDELEA
NDIO MWANZO WA SEASON 2 ITAENDELRA KU APO MAJALIWA


UNAWEZA KUWASILIANA NAMI KWA NJIA YA WATSAP KUPITIA NAMBA 0687151346

AU UNAWEZA KUGUSA HIO LINK HAPO CHINI ITAKUPELEKA MOJA KWA MOJA KWENYE WATSAPP

 
SEHEMU YA 34
THE HEIR AND DEATH INVESTIATIONS
MRITHI NA UCHUNGUZI WA KIFO
Naam ni mara baada ya mheshimiwa raisi Henry raisi wa awamu ya tisa kushituliwa katika kumbukizi nzito ya miaka ya nyuma akiwa waziri mpaka kuja kuwa makamu wa raisi , ni kumbukumbu iliokuwa ikimkumbusha mambo mengi sana katika uongozi wake akiwa makamu huku raisi akiwa ni mheshimiwaJohn bendera onyango ambaye walikuwa ni marafiki sana .
Basi mheshimiwa raisi alitoka katika chumba chake cha mapumziko na kwenda mpaka ukumbi wa kukutania wageni kwani aliambiwa kuwa bwana Samueli saitoto alikuwa amefika ndani ya ikulu anataka kuonana na yeye .
Ndani ya ukumbi wa kukutania wageni ndani ya ikulu ya dar es salaam alikuwepo Samuel saitoto akiwa na mwanaume mmoja wa kizungu alievalia suti yake ya majivu na suruali nyeusi na shati jeupe , ni bwana wa makamo kati ya miaka therathini na tano kwenda juu .
“ Mheshimiwa za siku nyingi “ ilikuwa ni sauti ya sam mara baada tu ya raisi kuingia ndani ya ukumbi huo .
“ Salama kabisa Sam , karibuni sana “ aliongea mheshimiwa raisi huku waliketi wote .
“ Naona ulipotea kwenye miezi hii michache “ .
“ Ni kweli muheshimiwa , kuna mambo ambayo nilikuwa nikiyashughulikia , nilishindwa kutoa taarifa ya mahali nilipo kutokana na kazi yenyewe “.
“ Sawa , karibu tena Tanzania “
“ Asante muheshimiwa , kwanza huyu alieoko mbele yako ni bwana Reynold Epifani ni mwanasheria wa maswala ya kimikataba ya kimataifa , na nimeona nije nae leo kwani kuna mambo nataka tuyazungumze “
“ Karibu sana bwana Epifani “ Aliongea raisi akimkaribisha bwana Epifani.
“ Mheshimiwa mara baada ya kuwasiliana na kimbona aliniambia mambo ambayao yalikuwa yakiendelea hapa nchini juu ya mali za bwana bruno kuuzwa kwa kampuni ya INNOVA “
“ Ndio bwana sam na hilo ni swala ambalo lilikuwa likininyima usingizi sana na nilimuachia bwana kimbona alifatilie ili nijue undani wake “.
“ Sasa mimi baada ya kupata taarifa hio nilijaribu kufatilia ya kile kinacho endelea juu ya mali zake , na kama taarifa ilivyo tufikia ni kweli kwamba bruno aliuza mali zake kwenda kampuni ya INNOVA , na swala hilo ndio lilinifanya nimtafute mwanasheria wa maswala ya mikataba kimataifa kuhusiana na maswala ya mauzo ya makampuni , amenieleza mengi kuhusu mauzo hayo na nataka na yeye ajaribu kukufahamisha ili tuone tunafanya maamuzi gani “ Aliongea sam na kisha alimpa nafasi bwana epifanio na kuanza kuongea .
“ Mheshimiwa raisi labda niende moja kwa moja katika mkataba uliofanyika kati ya kampuni ya INNOVA na BRUNO ENTERPRISES , lakini kabla ya kwenda huko moja kwa moja niende kwenye kampuni ya HUAWEI , miaka michache nyuma kampuni ya HUAWEI iliingia katika migogoro na serikali ya Marekani nchini ya raisi Trump na kupelekea kukosa kibali cha kuendesha bishara zake ndani ya taifa hilo kwa kile kilichosemekana kwamba walikuwa wanahatarisha usalama wa nchi , mazunguzmo baina ya pande zote mbili , yaani HUAWEI na serikali yalifanyika lakini mwisho wa siku kulikosekana muafaka na hivyo kampuni hii kutangaza kusitisha shughuli zake zote katika taifa la Marekani , swala hili lilipelekea kampuni hii kupata hasara kubwa sana katika mauzo yake kwani moja ya masoko yake makubwa ilikuwa ni ndani ya taifa hilo , jambo hilo lilipelekea kampuni ya HUAWEI kukaa kikao na wakuu wake wa bodi ya wakurugenzi ili kujadiliana ni kwa namna gani wanaweza wakaendelea na biashara pasipo kupata hasara Zaidi , moja ya wakuu wa bodi ambao walikuwa wakimiliki hisa nyingi katika kampuni hio ni INNOVA hii ni kampuni ya kiteknlojia ambayo makazi yake yapo nchini Italy katika jiji la Rome , kampuni hii kupita uongozi wake walifikia hatamu ya kuuza hisa zake ndani ya kampuni ya HUAWEI kwani walikuwa na madhumuni ya muda mrefu ya kujitegemea katika maswala ya kiteknolojia , lakini pia hawakutaka kupata hasara Zaidi kwani walikuwa wakiulamu uongozi wa HUAWEI kwa kutofikia makubaliano na serikali ya kimarekani mpaka kutangaza kufunga shughuri zake “ alinyamaza na kisha alifungua kibegi chake na kutoa baadhi ya karatasi kisha akaendelea .
“ kabla ya kampuni ya INNOVA kufikia maamuzi hayo miaka ya nyuma walifika nchini Tanzania kwa lengo la kuwekeza katika maswala ya kiteknolijia huku wakiwa na mkataba uliokuwa unakipengele cha kutaka kuendeleza teknolojia nchini lakini kwa masharti ya makampuni yote ya kiteknolojia kufungwa na moja ya kampuni hizo ni kampuni ya BRUNO ENTERPRISES , swala hili raisi Bendera alishindwa kulifanyia maamuzi ya moja kwa moja na kushindwa kusaini mkataba ule , lakini mara baada ya kupewa taarifa na waziri wa mambo ya ndani ya china juu ya hisa za HUAWEI ndipo bwana Bendera alipoona hio ni nafasi ya kipekee ya kumshawishi Bruno lamberk kuingia dili na kampuni ya INNOVA kwa kufanya ‘legal stock exchange’ na ushawishi wake ulizaa matunda kwani bwana Bruno alikubali na kuuza kampuni yake kwenda kwa kampuni ya INNOVA huku malipo ni kupewa uhisani wa asilimia 25 ya hisa za HUAWEI “ alinyamza kisha akatoa karatasi nyingine na kumpatia raisi .
“ Hio ni moja ya nakala nilioipata kutoka kampuni ya sheria ya kichina ijulikanayo kwa jina la ‘DANTON LAW FIRM’ , kampuni hii ndio iliosimamia mauzo yote ya ‘stock exchange’ kutoka kwa bruno kwenda kwa INNOVA lakini pia kutambuliwa kwa bruno kama mwanahisa ndani ya kampuni ya HUAWEI , hilo ni moja , lakini mwisho ni kwamba baada ya mwaka mmoja kupita ya mauzo hayo Bruno aliandika wosia( final will and testament ) ambao wosia huu ulikuwa ukimtaja mmiliki halali wa mali zote za bwana Bruno lakini wosia huo haukuwa umebeba jina la muhusika Zaidi ya kuwa na nembo ambayo inamtambulisha mmiliki.” Alisimama kuongea na kisha alitoa karatasi nyingine .
“ Hio ni karatasi ambayo inamuhusisha mmiliki na mpaka sasa ninapo ongea ni kwamba karatasi hio imekwisha sainiwa na mmiliki halali wa mali zote za Bruno amekwisha kukabidhiwa kisheria , bwana huyo anafahamika kwa jina la Stephano lamberk ” aliongea na hapo ndipo alipomfanya raisi atoe jicho kusikia kuwa mali za bruno mmiliki wake ashakwisha kutokea
“Unamaanisha kwamba tayari mali za bruno mmiliki wake ashakwisha kufahamika ?”.
“ Ndio muheshimiwa lakini mpaka sasa mmiliki ashafahamika kisheria na amekwisha tambulishwa katika wakuu wa bodi ya HUAWEI na kutokana na ratiba zake anaweza kuingia nchini muda wowote kwa ajili ya kumalizia vipengele vya kisheria ili kumalizia umiliki wa mali zote za Bruno ambazo hazikuwa chini ya kampuni “ aliongea bwana Epifanio na kumfanya raisi kuchoka , na kazi ya mwanasheria iliishia hapo kwani aliondoka na kuwaacha Sam na mheshimiwa raisi .
“Bwana Sam haya mambo nilikua sijajua kabisa , nakili nilikuwa makamu wa raisi lakini mambo mengi ya nchi hii nilikuwa siyajui kwani Bendera alikuwa akiyafanya kimya kimya “ Aliongea mheshimiwa Henry.
‘ Ni kweli muheshimiwa na swala hilo hata mimi kidogo limenishangaza kwa ujumla wake , nadhani ni chenga ambayo Bruno ametupiga “.
“ Sasa kama ni hvyo tunafanyaje na huyu bwana Stephano lamberk ni nani ?”.
“Kuhusu taarifa za awali za bwana zinasema kwamba bwana huyo ni mtoto wa Bruno “.
“ Mtoto wa Bruno!: Bruno anamtoto ??”
“ Mheshimiwa hata mimi hilo swali limenifikirisha sana mpaka sasa , na nimejaribu kufatilia taarifa zake Bruno nimekuja kugundua ni kweli alikuwa na mtoto aliekuwa akifahamika kwa jina la Stephan , lakini mtoto huyu na mama yake waliuliwa kikatili miaka ya nyuma kabla hajaingia hapa nchini “
“ Sasa kama mtoto wake na mama yake wameuliwa , huyo Stephan ni nani ?”.
“ Mheshimiwa hilo swala majibu yake hakuna lakini nina jambo lingine la kukuambia “ aliongea sam na kumwngalia mheshimiwa .
“ Ongea bwana Sam “.
“ Miaka ya nyuma raisi Bendera wakati anaingia madarakani alianzisha vita juu ya madawa kulevya na kipindi kile sisi ndio tuliokuwa tukiendesha bishara hio hapa nchini huku kiongozi wetu mkubwa akiwa ni Bruno lamberk , lakini katika jambo la kushangaza ni kwamba Bruno kutusaliti , swala hili halikuwa jepesi sana kutokea kwa Bruno kutusaliti na kuingia kweney vita na U-97 , kwa akili za kawaida ni kwamba lazima Bendera alikuwa akiujua udhaifu wa bwana Bruno “ Aliongea Sam na kumfanya Henry na yeye aanze kutafakari na kuona maneno ya Sam yana maana yake .
“ Kwa hio unataka kumaanisha nini ?”
“Nataka kufahamu ni jambo gani ambalo Bendera aliweza kumshawishi Bruno mpaka kupelekea kusaliti kazi yake ambayo alikuwa ameifanya kwa miaka mingi , kwani wewe ni moja ya viongozi waliokuwa katika kikao hicho na waliokuwa wakimsaidia mheshimiwa katika kazi yake “
Aliongea Sam na kumfanya raisi Henry afikirie na kisha alitingisha kichwa kama anakubaliana na bwana Sam , kwani hata yeye juu ya maswala yanayomuhusu bwana Bruno alikuwa hayajui kabisa .
“ Inabidi swala hili nilifatilie mimi mwenyewe , moja ya watu wa karibu waliokuwa wakishughurikia swala hilo ni bwana Abdallah halifa , mkuu wa majeshi “ aliongea raisi.
“ Nadhani kwanzia sasa inabidi tujue maisha ya Bruno kwa ujumla wake , watu ambao alikuwa anauhusian nao , watoto wake na mengineyo yanayomuhusu , kuhusu huyu bwana Stephano akiingia tu hapa nchini inabidi tumfatilie tujue ni nani , je ni kweli anamahusiano na bwana Bruno “
“ Hakuna shida mheshimiwa , swala hilo nadhani nikuachie kwani linaonekana lipo kwenye uwezo wako “
Aliongea Sam na kisha waliagana na sam kuondoka muda huo ilikuwa yapata saa kumi na mbili za jioni , na mara baada ya kuondoka ikulu moja kwa moja alitoa simu yake na kupiga .
“ Uko wapi ?”
“ Colleseum hoteli “
“ Nakuja hapo sasa hivi “
“ Poa nakusubiri “
Gari iliendeshwa mpaka maeneo ya masaki na ndani ya hoteli ya COLLeseum hotel , na mara baada ya kufika ndani ya hoteli hii gari ilisimamishwa na bwana Sam alishuka huku simu ikiwa mkononi .
“ Nishafika uko upande wa wapi ?”
“ Niko fitness club nachukua mazoezi “
“ Sawa nakuja “
“Poa unakuja kuchukua mazoezi?”
“ Ndio “
Basi Sam alienda moja kwa moja mpaka ndani ya jengo hilo na kuingia ndani ya eneo la kuchukulia mazoeizi ndani ya hoteli hio , ilikkuwa ni sehemu moja ya ghali sana kuingia kwa ajili ya mazoezi , baada ya kuingia alielekea mpaka kwenye vyumba vya kubadilisha na kuchukua tracksuit.
Ndani ya eneo hilo alionekana kimbona akiwa bize anachukua mazoezi kwenye ‘treadmill’ ( mashine ya kutembea ama kukimbia ndani ya gym ) , huku jasho likuwa linamtoka kweli , na bado alionekana kuwa bize kwani alikuwa akiongeza spidi tu kila muda unavyosonga , wakati akiendelea pembeni yake aliikuja Sam na yeye kuwasha mashine na kuanza kukimbia , Kimbona alimwangalia Sam na kisha alitabasamu huku akichukua maji yake ya uhai na kunywa.
“ Vipi mheshimiwa anasemaje ?”
“ Anaonekana kuwa na waswasi tu , sijamwambia chochote kuhusu Damiani , mpaka nijue ni mtu gani anampa sapoti kijana yule , maana mpaka kufika Thailland ni jambo ambalo hawezi kulipanga mwenyewe “ Aliongea huku akiongeza spidi ya kukimbia.
“ Vipi kuhusu Stephano lamberk ni kweli ni mtoto wa Bruno ?”.
“ Hilo nalo pia linanipa utata , ila naamini muda si mrefu ataingia hapa nchini na nitafanya juu chini hata kumteka nijue ni nani , nina uhakika asilimia mia sio mtoto wa Bruno “
“ Ni Kweli tunapaswa kufanya hivyo , lakini unadhani ni kipi kilipelekea bruno kutusaliti miaka ile ya nyuma Bendera alipoingia madarakani ?”
“ Mheshimiwa kaniambia atalifartilia hilo kwani mpaka sasa hakuweza kulifatilia swala hilo “ aliongea Sam huku akionekana kuvuja jasho kweli kwani spidi ya ‘Treadmill’ yake ilikuwa juu .
“ Vipi biashara ?“
“ Biashara imerudi kwa kasi sana yaani pesa ni nyingi mno , na hapa ninapo ongea kuna mzigo wa tani nzima unaingia bandarini “
“ Safi mwaka wa kwetu huu wa kutajirika hakuna wa kutuzuia kwa sasa “ aliongea Sam huku akimwangalia Kimbona ambae alikuwa amechoka na amezima mashine akiwa ameikalia kwa chini .
Wakati wakiendelea kuongea , simu ya Kimbona ilitoa mlio kuashiria kuna ujumbe umeingia aliitoa huku akiweka chupa ya maji chini na kisha aliufungua na hapo ndipo alipo toa macho , alimwangalia Sam ambae alikuwa bize kwenye kukimbia .
“Sam mambo yamekiwisha haribika “ Aliongea Kimbona na kumfanya Sam asimamishe mashine na kushuka huku akichukua simu ya Kimbona mkononi .
BOSS MZIGO TULIOPEWA BANDARINI KWENYE KONTENA SIO WENYEWE , TUMERUDI KUFATILIA BANDARINI LAKINI HATUJAKUTA KONTENA ,”
Ulikuwa ni ujumbe pia uliomshangaza kimbona na Sam kwa wakati mmoja , hawakujua ni kipi kimetoka , kimbona alichukua simu na kupiga ile namba .
“ Ni uzembe gani mmefanya mpaka kuchukua kontena ambalo sio la kwetu “
“ Boss nyaraka ulizonipatia asubuhi zinaonesha kabisa kontena tliolichukua ndio lenyewe “
“ Hilo kontena liko wapi sasa? “.
“ Chimbo “
“ Nakuja “
“ Sam tutaonana ngoja nikafatilie hilo swala “ aliongea kimbona na kutoka ndani ya gym na kisha alielekea kweney chumba cha hoteli na kisha alionga na kuvaa suti na kutoka kwenye gari na kuondoka .
****
Kazi aliopewa ilikuwa na ugumu wake , lakini aliamini kwa utaalamu wake lazima agepata majibu ambayo yalikuwa yakihitajiwa na maboss wake , pesa aliokuwa ameahidiwa pia ilikuwa ni kubwa kiasi kwamba alipata msukumo wa kufanya kazi hio na kuikamilisha kwa muda mfupi , huyu si mwingine basi alikuwa ni agent z mwana mitindo maarufu Tanzania lakini pia akiwa jasusi wa kujitegemea , mpaka wakati huo aliona kuna mwanga flani wa kupata kile ambacho anakitafuta , siku hio alikuwa ndani ya mji wa Lushoto katika kijiji cha Mkuzi , hakujua kwanini yupo mhali hapo , lakini aliamini kabisa kuna jambo angelipata ambalo lingemuwezesha kujua ama kupata mwanga wa kazi yake aliopewa .
Japo hakuwa na uzoefu na kijiji hicho lakini aliamini lazima angepata taarifa aliokuwa akiitaka , baada tu ya kufikia watu akiwa na gari yake aina ya V8 alimwita kijana mmoja aliekuwa akiuza miwa barabarani na kununua mua kisha akamuomba amuelekeze mahali ambapo familia ya Damiani inapatikana , na kwakuwa Damiani kwa kipindi hicho alikuwa gumzo kutokana na matukio ya hivi karibuni ambayo yalikwisha kumtokea , basi kwake haikuwa shida kabisa kwani alielekezwa mpaka kijiji husika tena alipatiwa kijana mdogo kwa ajili ya kupelekwa ndani ya kijiji hicho .
Mara baada ya kufika alionyeshwa nyumba ya Damiani na akagonga mlango kwa madakika kadhaa , lakini hakukuwa na majibu , lakini wakati akiwa anasubiri akizungusha macho alionana na bwana mmoja wa makamo hivi akiingia ndani hapo huku akiwa amebeba majani ya mbuzi .
“ Karibu “
“ Asante sana “
“Karibu kiti ukae “ aliongea bwana yule wa makamo huku akionekana kuchafuka na alionekana ni muda ambao alikuwa akitoka shambani .
“ Naitwa Lazaro nganyasu nimetokea jiji la dar es salaam , mimi nimpelelezi na nipo hapa kwa ajili ya kukuuliza maswali kadhaa yanayohusu kifo cha mama wa nyumba hii “
“ Karibu sana mpelelez”
“ Siku ya tukio ulikuwepo hapa ??”
“ Hapana sikuwepo na nimerudi baada ya tukio kutokea kwani nilikuwa safarini “
“ nataka kujua ni watu gani walikuwepo wakati watukio “
“ walikuwepo ndani ya tukio kwa taarifa nilizopata alikuwa ni Damiani , na mzee mmoja ambae ni mganga wa asili anafahamika kwa jina la Kivinje na alikuja hapa kwa ajili ya kumpa msaada wa kimatibabu majeruhi na hapo ndipo alipokuta tayari mauaji yashafanyika “
“ unataarifa zozote kuhusu Damiani ?”
“ hapana kwa kweli tokea atoweke hapa sijawahi kupata taarifa yoyote kutoka kwake “
“ huyu mzee ambae ulisema ni mganga wa tiba za asili , nampataje ?”
“ ni upande wa pili tu hapo anapatikana kwa jina anaitwa mzee Kivinje , ukifika hapo ulizia “.
Agent z alielekezwa mpaka kwenye nyumba anayopatikana mganga huyo na kweli mara baada ya kuulizia alipata kuonana na mzee kivinje aliekuwa akijiandaa kwa ajili ya kuanza kuwatibia baadhi ya watu .
“ kwa hio mzee unamaanisha uliona watu wawili eneo hilo ?”
“ ndio walikuwa ni watu wawili mmoja alitoka na kukimbia , lakini mwingine alikuwa amejificha ndani , lakini mtu wa nje alikuwa akivuja damu kwani aliacha michirizi ya damu “.
“ asante sana mzee wangu kwa maelezo yako “ aliongea agent z na kisha alitoka hapo na hakutaka kubaki kabisa ndani ya Lushoto , kwani muda huo ilikuwa yapata saa tisa na kwa mahesabu yake aliona atawahi kufika ndani ya jiji la Dar mapema tu.
Lakini wakati wote huo alikuwa akiifkirisha akili yake , kwani kila akijaribu kuyafikiria maelezo ya mzee kivinje hayakuchukuana kabisa ndani ya ubongo wake , aliona kabisa kuna jambo ambalo halikuwa sawa .
“ kwanini kuwe na watu wawili kwa wakati mmoja , kama kweli mmoja alikuwa na jeraha la risasi na mwingine kajificha hawa watu wametumwa na mtu mmoja ama ni watu wawili tofauti , ila nitajua ukweli wote “ aliongea Agent Z muda huo alikuwa akipita sehemu moja ilikuwa ikiitwa Vuga road na safari ilikuwa imepamba moto kuelekea Dar .
JE UNAHISI STEPHANO LAMBERK NI NANI ??
NITAJITAHIDI KUWALETEA MUENDELEZO KILA SIKU LEO NITAISHIA HAPA
TUKUTANE KESHO .
ITAENDELEA
UNAWEZA KUWASILIANA NAMI KWA NJIA YA WATSAP KUPITIA NAMBA 0687151346

AU UNAWEZA KUGUSA HIO LINK HAPO CHINI ITAKUPELEKA MOJA KWA MOJA KWENYE WATSAPP
 
SEHEMU YA 34
THE HEIR AND DEATH INVESTIATIONS
MRITHI NA UCHUNGUZI WA KIFO
Naam ni mara baada ya mheshimiwa raisi Henry raisi wa awamu ya tisa kushituliwa katika kumbukizi nzito ya miaka ya nyuma akiwa waziri mpaka kuja kuwa makamu wa raisi , ni kumbukumbu iliokuwa ikimkumbusha mambo mengi sana katika uongozi wake akiwa makamu huku raisi akiwa ni mheshimiwaJohn bendera onyango ambaye walikuwa ni marafiki sana .
Basi mheshimiwa raisi alitoka katika chumba chake cha mapumziko na kwenda mpaka ukumbi wa kukutania wageni kwani aliambiwa kuwa bwana Samueli saitoto alikuwa amefika ndani ya ikulu anataka kuonana na yeye .
Ndani ya ukumbi wa kukutania wageni ndani ya ikulu ya dar es salaam alikuwepo Samuel saitoto akiwa na mwanaume mmoja wa kizungu alievalia suti yake ya majivu na suruali nyeusi na shati jeupe , ni bwana wa makamo kati ya miaka therathini na tano kwenda juu .
“ Mheshimiwa za siku nyingi “ ilikuwa ni sauti ya sam mara baada tu ya raisi kuingia ndani ya ukumbi huo .
“ Salama kabisa Sam , karibuni sana “ aliongea mheshimiwa raisi huku waliketi wote .
“ Naona ulipotea kwenye miezi hii michache “ .
“ Ni kweli muheshimiwa , kuna mambo ambayo nilikuwa nikiyashughulikia , nilishindwa kutoa taarifa ya mahali nilipo kutokana na kazi yenyewe “.
“ Sawa , karibu tena Tanzania “
“ Asante muheshimiwa , kwanza huyu alieoko mbele yako ni bwana Reynold Epifani ni mwanasheria wa maswala ya kimikataba ya kimataifa , na nimeona nije nae leo kwani kuna mambo nataka tuyazungumze “
“ Karibu sana bwana Epifani “ Aliongea raisi akimkaribisha bwana Epifani.
“ Mheshimiwa mara baada ya kuwasiliana na kimbona aliniambia mambo ambayao yalikuwa yakiendelea hapa nchini juu ya mali za bwana bruno kuuzwa kwa kampuni ya INNOVA “
“ Ndio bwana sam na hilo ni swala ambalo lilikuwa likininyima usingizi sana na nilimuachia bwana kimbona alifatilie ili nijue undani wake “.
“ Sasa mimi baada ya kupata taarifa hio nilijaribu kufatilia ya kile kinacho endelea juu ya mali zake , na kama taarifa ilivyo tufikia ni kweli kwamba bruno aliuza mali zake kwenda kampuni ya INNOVA , na swala hilo ndio lilinifanya nimtafute mwanasheria wa maswala ya mikataba kimataifa kuhusiana na maswala ya mauzo ya makampuni , amenieleza mengi kuhusu mauzo hayo na nataka na yeye ajaribu kukufahamisha ili tuone tunafanya maamuzi gani “ Aliongea sam na kisha alimpa nafasi bwana epifanio na kuanza kuongea .
“ Mheshimiwa raisi labda niende moja kwa moja katika mkataba uliofanyika kati ya kampuni ya INNOVA na BRUNO ENTERPRISES , lakini kabla ya kwenda huko moja kwa moja niende kwenye kampuni ya HUAWEI , miaka michache nyuma kampuni ya HUAWEI iliingia katika migogoro na serikali ya Marekani nchini ya raisi Trump na kupelekea kukosa kibali cha kuendesha bishara zake ndani ya taifa hilo kwa kile kilichosemekana kwamba walikuwa wanahatarisha usalama wa nchi , mazunguzmo baina ya pande zote mbili , yaani HUAWEI na serikali yalifanyika lakini mwisho wa siku kulikosekana muafaka na hivyo kampuni hii kutangaza kusitisha shughuli zake zote katika taifa la Marekani , swala hili lilipelekea kampuni hii kupata hasara kubwa sana katika mauzo yake kwani moja ya masoko yake makubwa ilikuwa ni ndani ya taifa hilo , jambo hilo lilipelekea kampuni ya HUAWEI kukaa kikao na wakuu wake wa bodi ya wakurugenzi ili kujadiliana ni kwa namna gani wanaweza wakaendelea na biashara pasipo kupata hasara Zaidi , moja ya wakuu wa bodi ambao walikuwa wakimiliki hisa nyingi katika kampuni hio ni INNOVA hii ni kampuni ya kiteknlojia ambayo makazi yake yapo nchini Italy katika jiji la Rome , kampuni hii kupita uongozi wake walifikia hatamu ya kuuza hisa zake ndani ya kampuni ya HUAWEI kwani walikuwa na madhumuni ya muda mrefu ya kujitegemea katika maswala ya kiteknolojia , lakini pia hawakutaka kupata hasara Zaidi kwani walikuwa wakiulamu uongozi wa HUAWEI kwa kutofikia makubaliano na serikali ya kimarekani mpaka kutangaza kufunga shughuri zake “ alinyamaza na kisha alifungua kibegi chake na kutoa baadhi ya karatasi kisha akaendelea .
“ kabla ya kampuni ya INNOVA kufikia maamuzi hayo miaka ya nyuma walifika nchini Tanzania kwa lengo la kuwekeza katika maswala ya kiteknolijia huku wakiwa na mkataba uliokuwa unakipengele cha kutaka kuendeleza teknolojia nchini lakini kwa masharti ya makampuni yote ya kiteknolojia kufungwa na moja ya kampuni hizo ni kampuni ya BRUNO ENTERPRISES , swala hili raisi Bendera alishindwa kulifanyia maamuzi ya moja kwa moja na kushindwa kusaini mkataba ule , lakini mara baada ya kupewa taarifa na waziri wa mambo ya ndani ya china juu ya hisa za HUAWEI ndipo bwana Bendera alipoona hio ni nafasi ya kipekee ya kumshawishi Bruno lamberk kuingia dili na kampuni ya INNOVA kwa kufanya ‘legal stock exchange’ na ushawishi wake ulizaa matunda kwani bwana Bruno alikubali na kuuza kampuni yake kwenda kwa kampuni ya INNOVA huku malipo ni kupewa uhisani wa asilimia 25 ya hisa za HUAWEI “ alinyamza kisha akatoa karatasi nyingine na kumpatia raisi .
“ Hio ni moja ya nakala nilioipata kutoka kampuni ya sheria ya kichina ijulikanayo kwa jina la ‘DANTON LAW FIRM’ , kampuni hii ndio iliosimamia mauzo yote ya ‘stock exchange’ kutoka kwa bruno kwenda kwa INNOVA lakini pia kutambuliwa kwa bruno kama mwanahisa ndani ya kampuni ya HUAWEI , hilo ni moja , lakini mwisho ni kwamba baada ya mwaka mmoja kupita ya mauzo hayo Bruno aliandika wosia( final will and testament ) ambao wosia huu ulikuwa ukimtaja mmiliki halali wa mali zote za bwana Bruno lakini wosia huo haukuwa umebeba jina la muhusika Zaidi ya kuwa na nembo ambayo inamtambulisha mmiliki.” Alisimama kuongea na kisha alitoa karatasi nyingine .
“ Hio ni karatasi ambayo inamuhusisha mmiliki na mpaka sasa ninapo ongea ni kwamba karatasi hio imekwisha sainiwa na mmiliki halali wa mali zote za Bruno amekwisha kukabidhiwa kisheria , bwana huyo anafahamika kwa jina la Stephano lamberk ” aliongea na hapo ndipo alipomfanya raisi atoe jicho kusikia kuwa mali za bruno mmiliki wake ashakwisha kutokea
“Unamaanisha kwamba tayari mali za bruno mmiliki wake ashakwisha kufahamika ?”.
“ Ndio muheshimiwa lakini mpaka sasa mmiliki ashafahamika kisheria na amekwisha tambulishwa katika wakuu wa bodi ya HUAWEI na kutokana na ratiba zake anaweza kuingia nchini muda wowote kwa ajili ya kumalizia vipengele vya kisheria ili kumalizia umiliki wa mali zote za Bruno ambazo hazikuwa chini ya kampuni “ aliongea bwana Epifanio na kumfanya raisi kuchoka , na kazi ya mwanasheria iliishia hapo kwani aliondoka na kuwaacha Sam na mheshimiwa raisi .
“Bwana Sam haya mambo nilikua sijajua kabisa , nakili nilikuwa makamu wa raisi lakini mambo mengi ya nchi hii nilikuwa siyajui kwani Bendera alikuwa akiyafanya kimya kimya “ Aliongea mheshimiwa Henry.
‘ Ni kweli muheshimiwa na swala hilo hata mimi kidogo limenishangaza kwa ujumla wake , nadhani ni chenga ambayo Bruno ametupiga “.
“ Sasa kama ni hvyo tunafanyaje na huyu bwana Stephano lamberk ni nani ?”.
“Kuhusu taarifa za awali za bwana zinasema kwamba bwana huyo ni mtoto wa Bruno “.
“ Mtoto wa Bruno!: Bruno anamtoto ??”
“ Mheshimiwa hata mimi hilo swali limenifikirisha sana mpaka sasa , na nimejaribu kufatilia taarifa zake Bruno nimekuja kugundua ni kweli alikuwa na mtoto aliekuwa akifahamika kwa jina la Stephan , lakini mtoto huyu na mama yake waliuliwa kikatili miaka ya nyuma kabla hajaingia hapa nchini “
“ Sasa kama mtoto wake na mama yake wameuliwa , huyo Stephan ni nani ?”.
“ Mheshimiwa hilo swala majibu yake hakuna lakini nina jambo lingine la kukuambia “ aliongea sam na kumwngalia mheshimiwa .
“ Ongea bwana Sam “.
“ Miaka ya nyuma raisi Bendera wakati anaingia madarakani alianzisha vita juu ya madawa kulevya na kipindi kile sisi ndio tuliokuwa tukiendesha bishara hio hapa nchini huku kiongozi wetu mkubwa akiwa ni Bruno lamberk , lakini katika jambo la kushangaza ni kwamba Bruno kutusaliti , swala hili halikuwa jepesi sana kutokea kwa Bruno kutusaliti na kuingia kweney vita na U-97 , kwa akili za kawaida ni kwamba lazima Bendera alikuwa akiujua udhaifu wa bwana Bruno “ Aliongea Sam na kumfanya Henry na yeye aanze kutafakari na kuona maneno ya Sam yana maana yake .
“ Kwa hio unataka kumaanisha nini ?”
“Nataka kufahamu ni jambo gani ambalo Bendera aliweza kumshawishi Bruno mpaka kupelekea kusaliti kazi yake ambayo alikuwa ameifanya kwa miaka mingi , kwani wewe ni moja ya viongozi waliokuwa katika kikao hicho na waliokuwa wakimsaidia mheshimiwa katika kazi yake “
Aliongea Sam na kumfanya raisi Henry afikirie na kisha alitingisha kichwa kama anakubaliana na bwana Sam , kwani hata yeye juu ya maswala yanayomuhusu bwana Bruno alikuwa hayajui kabisa .
“ Inabidi swala hili nilifatilie mimi mwenyewe , moja ya watu wa karibu waliokuwa wakishughurikia swala hilo ni bwana Abdallah halifa , mkuu wa majeshi “ aliongea raisi.
“ Nadhani kwanzia sasa inabidi tujue maisha ya Bruno kwa ujumla wake , watu ambao alikuwa anauhusian nao , watoto wake na mengineyo yanayomuhusu , kuhusu huyu bwana Stephano akiingia tu hapa nchini inabidi tumfatilie tujue ni nani , je ni kweli anamahusiano na bwana Bruno “
“ Hakuna shida mheshimiwa , swala hilo nadhani nikuachie kwani linaonekana lipo kwenye uwezo wako “
Aliongea Sam na kisha waliagana na sam kuondoka muda huo ilikuwa yapata saa kumi na mbili za jioni , na mara baada ya kuondoka ikulu moja kwa moja alitoa simu yake na kupiga .
“ Uko wapi ?”
“ Colleseum hoteli “
“ Nakuja hapo sasa hivi “
“ Poa nakusubiri “
Gari iliendeshwa mpaka maeneo ya masaki na ndani ya hoteli ya COLLeseum hotel , na mara baada ya kufika ndani ya hoteli hii gari ilisimamishwa na bwana Sam alishuka huku simu ikiwa mkononi .
“ Nishafika uko upande wa wapi ?”
“ Niko fitness club nachukua mazoezi “
“ Sawa nakuja “
“Poa unakuja kuchukua mazoezi?”
“ Ndio “
Basi Sam alienda moja kwa moja mpaka ndani ya jengo hilo na kuingia ndani ya eneo la kuchukulia mazoeizi ndani ya hoteli hio , ilikkuwa ni sehemu moja ya ghali sana kuingia kwa ajili ya mazoezi , baada ya kuingia alielekea mpaka kwenye vyumba vya kubadilisha na kuchukua tracksuit.
Ndani ya eneo hilo alionekana kimbona akiwa bize anachukua mazoezi kwenye ‘treadmill’ ( mashine ya kutembea ama kukimbia ndani ya gym ) , huku jasho likuwa linamtoka kweli , na bado alionekana kuwa bize kwani alikuwa akiongeza spidi tu kila muda unavyosonga , wakati akiendelea pembeni yake aliikuja Sam na yeye kuwasha mashine na kuanza kukimbia , Kimbona alimwangalia Sam na kisha alitabasamu huku akichukua maji yake ya uhai na kunywa.
“ Vipi mheshimiwa anasemaje ?”
“ Anaonekana kuwa na waswasi tu , sijamwambia chochote kuhusu Damiani , mpaka nijue ni mtu gani anampa sapoti kijana yule , maana mpaka kufika Thailland ni jambo ambalo hawezi kulipanga mwenyewe “ Aliongea huku akiongeza spidi ya kukimbia.
“ Vipi kuhusu Stephano lamberk ni kweli ni mtoto wa Bruno ?”.
“ Hilo nalo pia linanipa utata , ila naamini muda si mrefu ataingia hapa nchini na nitafanya juu chini hata kumteka nijue ni nani , nina uhakika asilimia mia sio mtoto wa Bruno “
“ Ni Kweli tunapaswa kufanya hivyo , lakini unadhani ni kipi kilipelekea bruno kutusaliti miaka ile ya nyuma Bendera alipoingia madarakani ?”
“ Mheshimiwa kaniambia atalifartilia hilo kwani mpaka sasa hakuweza kulifatilia swala hilo “ aliongea Sam huku akionekana kuvuja jasho kweli kwani spidi ya ‘Treadmill’ yake ilikuwa juu .
“ Vipi biashara ?“
“ Biashara imerudi kwa kasi sana yaani pesa ni nyingi mno , na hapa ninapo ongea kuna mzigo wa tani nzima unaingia bandarini “
“ Safi mwaka wa kwetu huu wa kutajirika hakuna wa kutuzuia kwa sasa “ aliongea Sam huku akimwangalia Kimbona ambae alikuwa amechoka na amezima mashine akiwa ameikalia kwa chini .
Wakati wakiendelea kuongea , simu ya Kimbona ilitoa mlio kuashiria kuna ujumbe umeingia aliitoa huku akiweka chupa ya maji chini na kisha aliufungua na hapo ndipo alipo toa macho , alimwangalia Sam ambae alikuwa bize kwenye kukimbia .
“Sam mambo yamekiwisha haribika “ Aliongea Kimbona na kumfanya Sam asimamishe mashine na kushuka huku akichukua simu ya Kimbona mkononi .
BOSS MZIGO TULIOPEWA BANDARINI KWENYE KONTENA SIO WENYEWE , TUMERUDI KUFATILIA BANDARINI LAKINI HATUJAKUTA KONTENA ,”
Ulikuwa ni ujumbe pia uliomshangaza kimbona na Sam kwa wakati mmoja , hawakujua ni kipi kimetoka , kimbona alichukua simu na kupiga ile namba .
“ Ni uzembe gani mmefanya mpaka kuchukua kontena ambalo sio la kwetu “
“ Boss nyaraka ulizonipatia asubuhi zinaonesha kabisa kontena tliolichukua ndio lenyewe “
“ Hilo kontena liko wapi sasa? “.
“ Chimbo “
“ Nakuja “
“ Sam tutaonana ngoja nikafatilie hilo swala “ aliongea kimbona na kutoka ndani ya gym na kisha alielekea kweney chumba cha hoteli na kisha alionga na kuvaa suti na kutoka kwenye gari na kuondoka .
****
Kazi aliopewa ilikuwa na ugumu wake , lakini aliamini kwa utaalamu wake lazima agepata majibu ambayo yalikuwa yakihitajiwa na maboss wake , pesa aliokuwa ameahidiwa pia ilikuwa ni kubwa kiasi kwamba alipata msukumo wa kufanya kazi hio na kuikamilisha kwa muda mfupi , huyu si mwingine basi alikuwa ni agent z mwana mitindo maarufu Tanzania lakini pia akiwa jasusi wa kujitegemea , mpaka wakati huo aliona kuna mwanga flani wa kupata kile ambacho anakitafuta , siku hio alikuwa ndani ya mji wa Lushoto katika kijiji cha Mkuzi , hakujua kwanini yupo mhali hapo , lakini aliamini kabisa kuna jambo angelipata ambalo lingemuwezesha kujua ama kupata mwanga wa kazi yake aliopewa .
Japo hakuwa na uzoefu na kijiji hicho lakini aliamini lazima angepata taarifa aliokuwa akiitaka , baada tu ya kufikia watu akiwa na gari yake aina ya V8 alimwita kijana mmoja aliekuwa akiuza miwa barabarani na kununua mua kisha akamuomba amuelekeze mahali ambapo familia ya Damiani inapatikana , na kwakuwa Damiani kwa kipindi hicho alikuwa gumzo kutokana na matukio ya hivi karibuni ambayo yalikwisha kumtokea , basi kwake haikuwa shida kabisa kwani alielekezwa mpaka kijiji husika tena alipatiwa kijana mdogo kwa ajili ya kupelekwa ndani ya kijiji hicho .
Mara baada ya kufika alionyeshwa nyumba ya Damiani na akagonga mlango kwa madakika kadhaa , lakini hakukuwa na majibu , lakini wakati akiwa anasubiri akizungusha macho alionana na bwana mmoja wa makamo hivi akiingia ndani hapo huku akiwa amebeba majani ya mbuzi .
“ Karibu “
“ Asante sana “
“Karibu kiti ukae “ aliongea bwana yule wa makamo huku akionekana kuchafuka na alionekana ni muda ambao alikuwa akitoka shambani .
“ Naitwa Lazaro nganyasu nimetokea jiji la dar es salaam , mimi nimpelelezi na nipo hapa kwa ajili ya kukuuliza maswali kadhaa yanayohusu kifo cha mama wa nyumba hii “
“ Karibu sana mpelelez”
“ Siku ya tukio ulikuwepo hapa ??”
“ Hapana sikuwepo na nimerudi baada ya tukio kutokea kwani nilikuwa safarini “
“ nataka kujua ni watu gani walikuwepo wakati watukio “
“ walikuwepo ndani ya tukio kwa taarifa nilizopata alikuwa ni Damiani , na mzee mmoja ambae ni mganga wa asili anafahamika kwa jina la Kivinje na alikuja hapa kwa ajili ya kumpa msaada wa kimatibabu majeruhi na hapo ndipo alipokuta tayari mauaji yashafanyika “
“ unataarifa zozote kuhusu Damiani ?”
“ hapana kwa kweli tokea atoweke hapa sijawahi kupata taarifa yoyote kutoka kwake “
“ huyu mzee ambae ulisema ni mganga wa tiba za asili , nampataje ?”
“ ni upande wa pili tu hapo anapatikana kwa jina anaitwa mzee Kivinje , ukifika hapo ulizia “.
Agent z alielekezwa mpaka kwenye nyumba anayopatikana mganga huyo na kweli mara baada ya kuulizia alipata kuonana na mzee kivinje aliekuwa akijiandaa kwa ajili ya kuanza kuwatibia baadhi ya watu .
“ kwa hio mzee unamaanisha uliona watu wawili eneo hilo ?”
“ ndio walikuwa ni watu wawili mmoja alitoka na kukimbia , lakini mwingine alikuwa amejificha ndani , lakini mtu wa nje alikuwa akivuja damu kwani aliacha michirizi ya damu “.
“ asante sana mzee wangu kwa maelezo yako “ aliongea agent z na kisha alitoka hapo na hakutaka kubaki kabisa ndani ya Lushoto , kwani muda huo ilikuwa yapata saa tisa na kwa mahesabu yake aliona atawahi kufika ndani ya jiji la Dar mapema tu.
Lakini wakati wote huo alikuwa akiifkirisha akili yake , kwani kila akijaribu kuyafikiria maelezo ya mzee kivinje hayakuchukuana kabisa ndani ya ubongo wake , aliona kabisa kuna jambo ambalo halikuwa sawa .
“ kwanini kuwe na watu wawili kwa wakati mmoja , kama kweli mmoja alikuwa na jeraha la risasi na mwingine kajificha hawa watu wametumwa na mtu mmoja ama ni watu wawili tofauti , ila nitajua ukweli wote “ aliongea Agent Z muda huo alikuwa akipita sehemu moja ilikuwa ikiitwa Vuga road na safari ilikuwa imepamba moto kuelekea Dar .
JE UNAHISI STEPHANO LAMBERK NI NANI ??
NITAJITAHIDI KUWALETEA MUENDELEZO KILA SIKU LEO NITAISHIA HAPA
TUKUTANE KESHO .
ITAENDELEA
UNAWEZA KUWASILIANA NAMI KWA NJIA YA WATSAP KUPITIA NAMBA 0687151346

AU UNAWEZA KUGUSA HIO LINK HAPO CHINI ITAKUPELEKA MOJA KWA MOJA KWENYE WATSAPP
Shukran sana kwa mwendelezo tunasubir yajayo kwa hamu
 
KUNA MAKOSA KIDOGO YA KIUANDISHI KWENYE SCRIPT NA MAJINA NADHANI TUTAVUMILIANA NIMEKOSA MUDA WA KU EDIT. BUT INASOMEKA VIZURI TU

SEHEMU YA 35
Ni ndani ya jumba moja la kifahari lililokuwa ndani ya ununio jijini dar es salaam , alionekana mwanamke mmoja mrembo sana akiwa ndani ya jumba hilo huku akiwa amevalia kijigauni kilichomuacha maungio yake kuwa nje kabisa na wala hakuwa akijali kabisa japo ya kwamba ndani hapo alikuwa amezungukwa na walinzi ( mabodigadi) waliokuwa wakimlinda , lakini yeye hakuwa akijali , muda huo mlimbwende huyu mwenye umbo lake matata sana linaloweza kumdatisha kila mwanaume aliekuwa akimwangalia , alikuwa ameshikilia glass iliokuwa na mvinyo huku akiangalia maji yaliokuwa kwenye swimming pool kama mtu aliekuwa akiyashangaa , huku akionekana alikuwa akiwaza jambo.
Wakati huo upande wa getini ilionekana gari aina ya Subaru ikiingia ndani hapo na kwenda moja kwa moja kupark .
“ janeth yuko wapi “ ni mwanaume mmoja mtanashati mwenye mwili wa kimazoezi ndie alietoka kwenye gari hio na kisha kumuulizia janeth .
“ yupo garden “ alijibiwa kisha moja kwa moja alitoka na kuelekea mpaka upande wa garden na kweli alimkuta mrembo huyo akiwa hana habari na uwepo wake alisimama kisha akatabasamu na kumsogelea .
“ boss” aliita mwanaume huyo na kumfanya mlimbwende huyo ageuze shingo yake kimadaha na kumwangalia mwanume huyo .
“Abasi karibu “ aliongea mlimbwende huyo akimuonesha abasi sehemu ya kukaa .
“ vipi kazi imefanikiwa ?”
“ imefanikiwa kwa asilimia mia na kama ulivyoagiza tumechukua kontena na kulipeleka chimbo ,vijana kwa sasa wanasubiria maagizo yako tu “.
“safi sana nadhani kimbona sasa anababaika huko “ aliongea mlimbwende huyo huku akikunja nne na kumfanya kijana abasi amwangalie kwa uchu wa kimatamanio .
“ tunafanyaje na hayo madawa “.
“ nataka niyachome moto , siwezi kuyaruhusu yaingie mtaani ilihali yanaharibu vijana wa taifa hili , nina mipango mikubwa na Tanzania , hivyo nataka uyachome moto “.
“ sawa bosi ngoja niwape vijana maagizo “.
“ hapana nitaenda mwenyewe kushuhudia yakiteketea kwa moto “ aliongea mlimbwende huyo na kisha alinyanyuka na kuingia ndani ya jumba hilo la kifahari huku akimuacha kijana abasi akiwa anamwangalia kwa uchu kwa nyuma jinsi makalio ya mwanadada huyo yalivyokuwa yakienda kushoto kulia .
Alikuwa ni mwanadada wa miaka kati ya ishirini na saba kwenda therathini , mrefu saizi ya kati mweye rangi nyeupe na uso wake ulioumbwa vizuri , alikuwa amejaaliwa moja ya shepu moja nzuri sana , shepu ambayo kwa mwanaume rijali angemuona angemmezea mate huyu ndio mlimbwende janeth .
Dakika kumi mbele mlimbwende huyo alitoka huku akiwa amevalia suti ya zambarau na kiatu cheusi cha high heels na kisha alilisogelea gari aina ya mercedez benz wagon , gari moja ya kifahari na kisha abasi na yeye alifatia kwenye gari hio na gari ikatolewa ndani ya jengo hilo .
Masaa kadhaa mbele walikuwa wakipita bagamoyo , na walikuwa wakielekea njia ya kwenda msata baada ya kufika eneo moja lililokuwa likifahamika kwa jina la kidomole relini walikunja kushoto na kuingia kwenye barabara ya vumbi iliokuwa ikielekea kanisa la katoliki na baada ya kufika hapo walikunja kulia na kwa mbele kulionekana karakana moja imejengwa , waliendesha mpaka eneo hilo na kisha walipaki gari , na kuingia ndani na hapo ndipo walipokutana na kontena likiwa ndani ya gari bado.
“ litoeni hapa tunaenda fukayose ‘ aliongea janeth na kisha gari lile lililobeba kontena lilitolewa na kwenda mpaka fukayose , baada ya kufika eneo hilo nyuma kidogo gari ile ilikunja kushoto na kuingia kwenye moja ya shamba kubwa .
“ hili shamba la nani ?” aliuliza abasi .
“ la kimbona “ aliongea mwanadada yule huku akionekana kwenye sura ya kazi , baada ya kufika ndani ya shamba hilo walifanya utaratibu wa kushusha lile kontena na walifanikiwa kisha janeth aliwaamrisha vijana walifungue , na kweli lilifunguliwa na madawa ya kulevya yaliokuwa kwenye mfumo wa unga unga yalitolewa na kisha kubwaga chini na kumwagiwa mafuta ya petroli na janeth alitoa kiberiti cha gesi na kisha alitupia kwenye madawa hayo yalioanza kuteketea .
“ nyie mnaweza kuondoka “ aliamrisha vijana wake na wakapanda kwenye gari na kuondoka , huku janeth akiangalia mpaka alipohakikisha kila kitu kimebaki majivu alipanda kwenye gari akiwa na abasi na kisha walisepa .
*****
Kimbona mara baada ya lutoka moja kwa moja alienda mpaka chimbo ambako vijana wake ndio walipokuwepo , alisimamisha gari yake na muda huo kigiza kilikuwa kishaanza kuingia , alisogea kwenye karakana hio na kuingia ndani na kukutana na vijana wake waliokuwa wakimsubiri .
” derick ni nini kimetokea ?”
“ boss tumefika bandarini na kuonesha nyaraka ya kuhitaji mzigo na tukapewa , lakini baada ya kufika hapa na kuufungua tumekutana na chumvi “ aliongea derick na kumfanya kimbona asogelee lle kontena na kuhakiki na kweli iilikuwa ni chumvi kutoka kenya .
“ *** ! kuna mchezo hapa tumefanyiwa ila nitajua .aliongea kimbona na wakati huo simu yake ilitoa mlio na aliitoa na kuangalia kwani ulikua ni ujumbe wa meseji “.
“ MZIGO WAKO UMEFIKA SALAMA , UPO SHAMBANI KWAKO FUKAYOSE , BY MZALENDO “ ilikuwa ni meseji ambayo ilimshangaza lakini hakutaka kupoteza muda alitaka kujaribu kupiga ile namba ila ilikuwa ni private namba .
“ derick chukua vijana twende fukayose “ aliongea kimbona na derick alichukua vijana na safari ya kwenda fukayose ikaanza , na hapakuwa mbali sana kwani sehemu walikuwepo kwene chimbo lao ilikuwa ni bunju .
Nusu saa tu walikuwa wameshafika na jambo la kwanza kimbona kuona ni moshi mzito , walisogea mpaka eneo hilo na hapo ndipo walipopigwa butwaa kwani kontena walilikuta likiwa tupu lakini pia walijua kuwa mzigo wote uliteketezwa kwa moto , kimbona alijikuta akikaa chini kwani hakuamini kama tani nzima ya madawa ya kulevya iliokuwa ikiingia nchini ndio hio imeteketezwa yote , ilikuwa ni hasara kubwa kwake kupata , kwani ni mzigo ambalo ulikuwa umemgharimu pesa nyingi mno .
Wakati akiwa kwenye majuto simu yake ilitoa mlio kuwa kuna mtu aliekuwa akipiga , aliichukua na kuona ni sam aliekuwa akipiga simu
“vipi umefanikiwa ?”
“ hapana ni majanga mzigo wote umeteketezwa “”
“unamaanisha mzigo wote “
“ ndio na mtu aliefanya hivyo naonekana kutujua kwani ndio kanitumia ujjumbe kuwa mzigo upo huku shambani na ndipo nilipoukuta umeunguzwa wote “.
“ kimbona hio ni hatari kubwa sana na hasara kwa ujumla , nimehangaika mwezi mzima kuusubiria huo mzigo ufike nchini , inaonekana hakuwa makini na vijana wako “.
‘ nilikuwa makini sana sam , huu sio mzigo wa kwanza kupokea”
“ unafikiri nani katufanyia hivyo “
“ kuna ujumbe ambao kaniachia ngoja ni kufowadie “
“ sawa “.
“ derick huyu mtu inabidi akamatwe haraka wasiliana na carlos tumpe kazi ya kumfatilia “ aliongea kimbona na derick aliwasiliana na carlos Cardoso na kumpa maelekezo .
*****
Suzzane alikuwa ni mwenye hasira sana juu ya mtu aliekuwa anajiita mzalendo , aliapia kumuonyesha siku akimtia kwenye mikono yake , upelelezi wake ulikuwa ukifanyika kwa kina kweli , hakutaka kukurupuka kwani aliamini kuwa mtu ambae alikuwa akideal nae alikuwa ni mtu mwenye akili na hivyo hata yeye alipaswa kutumia akili vile vile , alijiapiza kumkamata mtu anaejiita mzaelndo , hakujua mtu huyu ni nani japo kuna muda hisia zake zilimwambia kuwa mtu huyo alikuwa ni damiani lakini hakutaka kuamini kabisa , wakati kontena la madawa ya kulevya linashushwa bandarini alikuwepo na hata vijana wa kimbona walivyochezewa mchezo wa kubadilishiwa kontena pia aliliona jambo hilo , ila kwakuwa halikuwa likimuhusu aliona sio kazi yake , Zaidi ya yote yeye alitaka kujua ni mtu gani yupo nyuma ya vijana waliofanya mchezo wa kubadilisha kontena , kwanza mwanzoni zilikuwa ni hisia zake tu ambazo zilimpeleka bandarini mara baada ya kupata taarifa hio ya kushushwa kwa mzigo wa madawa kutoka kwa mtu wake aliekuwa ndani ya TISS kuna hisia zilimwambia lazima kuna jambo lingetokea na ndio maana aliingia ndani ya eneo hilo tokea muda wa saa kumi akiangalia kila mtu aliekuwa akiiaangia bandarini hapo na kutoka na alijikuta akitabasamu mara baada ya kubaini mchezo uliokuwa ukifanyika bandarini mpaka vijana wa kimbona ambao alikuwa akiwajua vyema kubadilishiwa kontena , na hata kontena hilo la madawa lilivyotolewa hapo bandarini , hakuwa nyuma na gari yake aina ya brevis nyeupe , alifatilia mpaka linafika kidomole na kuingizwa kwenye karakana hakutaka kuwa na papara kwani alirudi barabarani na kisha alipaki gari lake kwenye duka moja la jumla na kununua soda na kukaa huku akinywa akiangalia upande wa barabara ambao gari lile lililokuwa na kontena lililoambatana na vijana wale ambao hakuwajua , alikuwa ameweka umakinni wa hali ya juu , alikaa hapo Zaidi ya lisaa na ndipo alipo ona gari moja la kifahari likipita na kukunja upande ule ule , alijikuta akichanua kwa tabasamu pana mara baada ya kuona gari hio kwani aliamini kabisa aliekuwa ndani ya gari hio alikuwa ni mtu anaemtaka , alitulia kama nusu saa na akanyanyuka na kisha alilisogelea gari lake na kuingia ndani na kuliwasha , lakini ile anakanyaga mafuta alishuhudia ile benz ikitoka na safari hii ikikunja kuelekea kiwangwa msata , alijikuta akisubiria kama dakika moja , na gari iliokuwa imebeba kontena ile aliona na yenyewe ikifuatia , aliacha imuache mbali mita kadhaa na ndipo alipowasha gari yake na kufatilia kwa nyuma mpaka gari ile ilipokunja kwenye shamba yeye alipitisha gari na kwenda kupaki mbele na kisha alirudi kwa miguu na hapo ndipo aliposhuhudia madawa yale yakiteketezwa , jambo hilo kidogo lilimshangaza , kwani aliamiani mtu ambae alifanya mchezo hu huenda alikuwa akiwazunguka wenzake na kutaka kuyauza madawa hayo lakini alichoshangazwa ni kuteketezwa kwa madawa yale .
“ hawa watu ni wakina nani ?” lilikuwa ni swali ambalo lilizunguka ndani ya kichwa chake huku akimwangalia mwanamke ambae alionekana kuwa ndio kiongozi wa kuchoma madawa hayo mpaka pale walipomaliza na kuondoka , na yeye haraka haraka alikimbilia gari lake na kuingia kwenye gari na kulifatilia lile benz.
“Nataka tuingie mapinga kwanza kwenye nyumba yangu ‘aliongea janeth .
“ kuna mishe gani ?”
“ kuna mtu nataka kuoanana nae “
“ poa “ .
Gari waliopanda janeth na abasi mara baada ya kufika mapinga ilikunja kushoto na kuchukua barabara ya zamani na kuja kupita kituo cha polisi mwisho zahanati ya mapinga na ikaja kutokea kwa mbele kabisa kwenye shule ya msingi mapinga , ilienda mbele kidogo na kusimama nje ya nyumba iliokuwa na ukuta , na abasi alishuka na kisha alifungua geti na gari ile ikaingia ndani.
Suzzane yeye hakutaka kabisa kuwapoteza watu hao , alidhamiria kabisa kuwajua na mpango wake ilikuwa ni kuwavamia usiku na ndio maana mara baada kuona gari ile imeingia ndani ya geti lile , alirudi na kwenda kupark kwenye moja ya duka la madawa huku akiangalia nyumba ile , muda huo giza lilikuwa limeingia kwani ilikwa ni kama muda wa saa moja hivi , wakati akiwa amesimama simu yake ilitoa mlio kuwa inaita , aliitoa mfukoni na na kuangalia mpigaji na aliona alikuwa ni mheshimiwa raisi .
“ hellow mheshimiwa “
“ ndio suzzane , uko wapi ?”
“ nipo bagamaoyo , kuna nini mheshimiwa ?”
“ kuna mzigo wetu umeibiwa bandarini na mtu anaejiita mzalendo , na mpaka sasa tumefatilia na tumegundua umechomwa moto ‘ aliongea mheshimiwa na kumfanya suzzane abenue midomo kwa dharau .
“ kwahio unataka nifanye nini muheshimiwa “
“ nataka uwakamate hao watu inawezekana akawa damiani “
“ sawa muheshimiwa “ aliongea suzzane na kukata simu na kisha hakutaka kuchelewa , kwani hisia zake zilimwambia kabisa kuwa watu walioingia kwenye nyumba ile mmoja wapo ni yule anae muwinda kwa udi na uvumba .
Alilisogelea geti kama mtu anaepita , huku akiangalia kama kuna kamera lakini hakuona hata moja na hapo aliona jambo lake lingeweza kuwa rahisi , alizunguka upande wa nyuma na kuangalia urefu wa ukuta huo na kisha aliangalia kushoto na kulia na kama paka aliparamia ukuta hu na kwenda kutua ndani ya nyumba hio nyuma kabisa ya tank la maji .
Alishika kiuno kuangalia bastora yake na kuitoa kisha akaangalia risasi zilizokuwemo na baada ya kuona anazo zakutosha alitembea kwa kuinama na kwenda kujibanza kwenye kona ya ukuta karibu na mlango , aliangalia usalama na kisha alitembea kwa kasi ya ajabu na kwenda kutua kwenye kibaraza karibu kabisa na mlango wa kuingilia , aliusogelea mlango i kama mtu aliekuwa akisikilizia sauti kutoka ndani lakini hakuna sauti iliosikika japo taa zilikuwa zikiwaka , akili yake ilikuwa ikifanya kazi kwa kasi mno , hakutaka kuingia kizembe zembe , alitaka ajihakikishie kuwa yupo salama .
Alishika kitasa cha mlango na kukinyonga kwa utaaramu wa hali ya juu pasipo kelele na akafungua mlango kidogo na alitumia mwanya huo kuangalia eneo la ndani , aligudnua kuwa ene hilo lilikuwa na sable lakini ambayo haikuwa na mtu .
Aliamua kuingia ndani kabisa kwa tahadhari kubwa mpaka kwenye sable kubwa pana iliojaa masofa huku TV ikiwa inawaka .
“ karibu , nilikuwa nakusubiri “ ilikuwa ni sauti nyororo ilimshitua suzzane kwa nyuma na kugeuka kwa kasi lakini ile anageuka bastora ilipigwa teke na kwenda kudondokea mbali. .
ITAENDELEA
SEHEMU YA 36
Suzzane baada ya kuona bastora yake imeenda mbali , hakutaka kuzembea , japo mbele yake alionekana mwanamke mrembo lakini jinsi bastora yake ilivyopigwa teke alijua kuwa mtu anaepambana nae sio mtu wa kawaida kabisa .
“wewe ndio mzalendo wa nchi hii “ aliongea suzzane kwa dharau akimwangalia janeth uson
“ wewe unanionaje , unafikiri mimi ni kama wewe unaowasaidia waharifu , mpaka kumuua mpenzi wako danieli ‘ aliongea janeth na kumfanya suzzane apandwe na hasira na kumfata janeth huku akidhamiria kumpiga pigo , lakini na janeth ni kama na yeye alikuwa akimsubiria kwani ile suzzane anarusha ngumi janeth aliikwepa , kushoto , lakini suzzane alikuwa mwepesi kweli kwani ile anahepa kushoto tayari alikuwa amechia teke la mbavu lililompata kisawasawa janeth na kuugumia maumivu , huku suzzane akimfata kwa kasi yake , lakini hilo lilikuwa kosa kwa suzzane kwani ni kama janeth alikuwa akimtegea kwani ile anafika alipigwa bonge la mtama na kwenda chini na hapo hapo janetha akaachia front kick , lakini suzzane aliona hilo kwani alibiringita kushoto na kwenda kutua kwenye friji huku akijinyanyua , ulikuwa ni mtanange , janeth alijnekana mtaalamu na pia suzzane alikuwa ni komandoo mbobezi , zilianza kupigwa ngumi hapo huku kila mtu akijaribu kuwekpa na kupangua za mwenzake , kiufupi japo janeth alikuwa yuko vizuri lakini kwa suzzane alikuwa mtoto tu , kwani kadri muda unavyoenda ndio alipokua anachoka na alianza kuchezea mapigo na moja kubwa lilimpeleka chini ni teke la roundhouse lililimpiga tumboni na kwenda kutua kwenye sofa , suzzane alikuwa na hasira kama mbogo kwani alimfata huku akidhamiria kumzimisha , lakini alijikuta akutulizwa na sauti nyuma ikumuarisha asimame hivyo hivyo kabla hajachanguliwa ubongo , lakini abasi alikuwa amechelewa kwani suzzane kama chui alikuwa asharukia mlango na kuchomoka nje kabisa na hakutaka kubaki ndani hapo kwani aliona si salama kwake , aliruka ukuta na kutoa nje kabisa kisha alienda mpaka barabarani na kupanda gari yake huku akijifuta jasho , alionekana alikuwa akisikiliza baadhi ya maumivu .
“ pumbavu nitawakamata tu , walikuwa wakinisubiria , kama nisingekuwa mweepesi wangenikamata “ aliongea suzzane huku akijikuta akitoa machozi mara baada ya kukumbuka kauli ya mwanadada jaenth iliokuwa ikumuhusu Daniel
Jinsi alivyokuwa abaendesha gari alikuwa ni kama mwehu maana alikuwa kwenye spidi kali mno , madakika kadhaa tu alikuwa ndani ya jogoo na kukunja kushoto na kupeleka gari mpaka nje ya nyumba kubwa iliokuwa na geti kisha alifungua kwa rimoti na kuingiza gari ndani .
“angeniua mshenzi yule “ aliongea janeth huku akionekana kuwa kwenye maumivu makali
‘”suzzane ni komandoo yule anambinu nyingi za kivita si rahisi kushindana nae kwenye ulingo ukashinda “
“ ni kweli lakini lazima tumpate lasivyo kazi zetu zitakuwa ngumu sana “.
*******
KIA ( KILIMANJARO INTERNATIONA AIRPORT )
Ilikuwa ni ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro ilionekana ndege ya shirika la KLM ikisimama eneo lake kwa ajili ya kushusha abiria mara baada tu ya kutua ndani a uwanja huo wa ndege , dakika kadhaa mbele alionekana mwanaume mmoja wa kizungu mwenye mwili wa mazoezi alievalia tisheti ilimbana vyema na kufanya mwili wake kujichora , mwanaume huyu alikuwa amevalia miwani .
“naweza pata ndege ya kunipeleka dar asubuhi hii “ aliuliza mwanaume huyu .
“ ndio ipo inayotoka saa nne ya shirika la ATCL”
“ nipe ticket ya daraja la kwanza “ aliongea bwana huyu na kisha mwanadada aliekuwa hapo uwanjani alifanya kama alivyoambiwa na kumpatia ticket mara baada ya malipo kufanyika kwa njia ya kadi .”
Saa tano na nusu bwana huyu alionekana akitoka ndani ya uwanja wa kimataifa wa mwalimu nyerere mara baada tu ya kutoka alionana na mwanamama aliekuwa anamjua vyema na kumsoggelea .
“ Rebecca ‘
“ za siku nyingi ?” mwanaume huyu japo ya kuwa na rangi ya kizungu lakini alionekana kukijua vizuri Kiswahili .
“ nzuri kabisa bwana stephano lamberk “ aliongea Rebecca na kumfanya bwana stephano lamberk kutabasamu huku wakilisogelea gari aina ya ford na bwana stephano aliingiza begi lake ndani na kisha alifungua mlango wa mbele na gari liliondoshwa .
Ni mwendo kama wa lisaa hivi gari ile ilikuwa ikipita maeneo ya kawe na kuja kutokezea lugalo na kuingia taki bovu na iliendeshwa na kukunja kushoto barabara ya kwenda makongo juu na kwenda kusimama kwenye moja ya jumba la kifahari kabisa ndani ya eneo hilo lililokuwa limezungukwa na ukuta mrefu .
Baada ya kuingia ndani ya jumba hili gari ilikweda kupark na stephano alitoka kwenye gari na hap ndipo alijikuta akichanua tabasamu na hio ni mara baada ya kuonana na mtu aliesimama mbele yake .
“luang shu “ aliongea Stephan na kumfanya luang shu atabasamu na kisha walikumbatia .
“ ni muda wa miezi sasa tokea uniache china “
“ ni kweli karibu tena Tanzania “ aliongea
“ asante sana nimefika kwa mara nyingine baada ya miaka miwili sasa tokea niondoke “ aliongea bwana stephano huku akitabasamu na waliongozana mpaka ndani huku wakifatiwa na Rebecca nyuma .
“china umeionaje ?”
“ nchi yenu ni endelevu sana katika mambo mengi huamini nimeingia nchini bila mtu kunijua kabisa hahaha “
“yeah kwa staili hio hakuna mtu wa kukufahamu kabisa “ aliongea stephano huku akichukua begi lake na kuelekea chumbani akiwa ameongozana na luangshu huku Rebecca akibaki sebleni , baada ya kufika ndani , walitoa nguo zote kwenye lile begi na kuzibwaga kitandani na kisha stephano alitoa kijidude kama chaja na ukichomeka ukutani kwenye soketi ya umeme na baada ya hapo alifungua lile begi na kuingiza miguu ndani na kusimama , kilikuwa ni kitendo cha sekunde kadhaa tu kulitokea kama moto uliokuwa unatokea kwenye lile begi na ni kama ulikuwa ukimuunguza bwana Stephano na hapo hapo ngozi yake ikabadililka na kuwa ya kiafrika kabisa na wala sio ya kizungu tena
‘ karibu damiani Tanzania kwa mara nyingine “ aliongea luangshu na kumfanya damiani atabasamu na kisha alivaa nguo na kutoka mpaka sebleni na hapo ndipo rebeka alishangaa.
“ rebbecca ogopa sana Mungu na teknolojia hahaha “ aliongea damiani na umfanya Rebecca kushangaa tu kwani mtu alieingia hapo akiwa na ngozi ya kizungu sasa anatoka akiwa na ngozi ya kiafrika .
“ kweli kabisa inapaswa tuogope mungu na teknolojia “ .
*****
Ni siku ambayo damiani anaingia nchini katika geti la ikulu kulionekana magari mawili ya aina ya range yakitoka na kuingia barabarani na kuchukua barabara salenda , na nusu saa mbele gari zile mbili zilionekana zikipita mwenge hatimae zilipita mbezi beach , tegeta na kuingia barabara iliokuwa ikielekea ununio dyanstry beach . dakika kadhaa gari zile zilikuwja kusimama kwenye jumba la kifahari la mrembo janeth , geti lilifunguliwa na gari ziliingizwa ndani kabisa na mwanadada aliekuwa mkakamavu alitoka na kumfungulia mke wa raisi , huku na gari ya nyuma wakitoka wadada wawili waliokuwa wamevalia suti na walikuwa mhali hapo kwa ajili yakuimarisha ulinzi .
Mara baada ya mke wa raisi kutoka kwenye magari hayo moja kwa moja aliingia ndani ya jumba hilo , mpaka sebleni na hapo ndipo alipomuana janeth na janeth mara baada ya kumuaona mke wa riais alimkimbilia n kwenda kumhug.
“mom nimekumis sana “ aliongea janeth akijidekeza kwa wema .
“ ni mekumis pia mwanangu “
“ lakini mama haya maisha mpaka lini ya kujificha ficha “
“sikia janeth najua unateseka sana , lakini vumilia mambo yakiwa sawa utanichoka mwenyewe “
“ mhmh mom kila siku unaniambia mambo yakiwa sawa , nimekuwa mtu wa kufichwa tokea nimezaliwa mpaka sasa “
“ ni kwa usalama wako mwanangu sina jinsi “.
“sawa mama lakini nakumiss sana “
“ nakumiss pia mwanangu mmefikia wapi ?”
“ jana tulifanikiwa kukamata kontena ya madawa ya kulevya na tumeyachoma yote “
“ safi sana , nataka kila madawa yanayoingia hapa nchini yachomwe , sipo tayari kuona taifa ambalo raisi bendera alilipigania kwa nguvu zake zote likiharibiwa tena “
“ nitapambana mama “
“ haya niambie kuna lingine limetokea ?”
“ ndio mama jana suzzane nilipambana nae “
“nini , ilikuwaje ukapambana na suzzane “
“ nadhani jana alikuwa akitufatilia kwa muda mrefu kwani gari yake niliiona kidomole na hata wakati wakurudi pia niliona nikajua tu kuna mtu anatufatilia japo sikujua ni nani na ndipo nilipomuambia abasi tuingie mapinga kumsubiri , na kweli saa moja kama na nusu aliingia ndani hapo kwa lengo la kutukamata , ndipo tulipo pambana nae mpaka akakimbia “
“ kuwa makini sana na suzzane , anaroho mbaya sana yule mwanamke , hashindwi kukuoa duniani , kama ameweza kumuua danny sembuse wewe na isitoshe ni mtiifu sana kwa mheshimiwa raisi “
“ ni kweli sema nimegundua jambo hilo linamuuma sana “
“ hahaha hana lolote huyo namjua sana tu kwa usaliti wake “ aliongea mke wa raisi huku akionesha kufurahishwa sana na uwepo wa mahali hapo kwani meno yote nje
“ mimi naondoka janeth kabla mheshimiwa hajaanza kuchezwa na machale , maana namjua sana mambo yake “ aliongea mke wa raisi .
“ sawa mama nitakuwa nawasiliana na wewe kwa kupita sabi “.
“ sawa hakuna shaka, shika hiki kiboksi kitunze sana , ndio kilichonifanya leo nije hapa , usikifungue mpaka pale nitakapokuambia na kukupa ufunguo wake “
‘ kina nini mama? “
“ wewe kitunze utajua baadae kina nini “ aliongea mke wa raisi na kisha aliagana na mtoto wake
Dakika chache mbele gari za mke wa raisi zilitoka ndani ya jumba hilo na kuingia barabarani , lakini wakati huo huo gari ya brevis nyeupe ya suzzane ilionekana ikiwa nyuma ya gari hizo .
“ hizi gari mbona ni za ikulu zinafanya nini hapa “ ni swali alililojiuliza suzzane na aliona majibu yake ni kumpigia raisi simu
ITAENDELEA
SEHEMU YA 37
Wazo namba moja ambalo alikuwa nalo agent z ni kumjua kwa undani bruno lamberk ,aliamini kwa kumjua bwana huyo angeweza kufahamu baadhi ya mambo ambayo yangemsaidia kujua baadhi ya mambo katika misheni yake , alikuwa akimjua kimbona na mheshimiwa raisi kama watu waliokuwa wakimtafuta kijana damiani lakini alikuwa akiamini kabisa kwamba kuna mengi ya kuyajua yaliokuwa yakihusiana kati ya damiani na bruno , ambayo kidogo yangemletea mwanga wa kazi yake , kazi hii ilionekana ngumu kwake kutokana na mpangilio wake , maana alijua kama damiani angekuwa nchini thailland kama uchunguzi wake wa mara ya kwanza, basi kazi ingekuwa ngumu kidogo kupata ukweli , lakini kwakuwa wakuu wake wa kazi walikuwa wamempatia kazi ya kufahamu tu kama kijana huyo bado yuko huru au yupo kwenye mikono ya mheshimiwa , aliona pia kuna urahisi wa kazi hio .
Siku hio alikuwa ndani ya jumba lake la kifahari lililokuwepo ndani ya eneo la kigamboni , alikuwa amekaa chini akijaribu kufatilia habari zinazomuhusu bwana bruno lamberk , aliangalia kwanzia mali zake mpaka makampuni yake , na hapo alijikuta akipata wazo la kufanya siku ya kesho , kwani muda huo ilikuwa tayari ni jioni kabisa .
“ kesho inanibidi kwenda kwenye moja ya kampuni zake , naamini kuna kitu naweza kukipata pale “ aliongeaa huku akigagua baadhi ya makaratasi yake , mpaka pale alipokuja kushituliwa na honi ya gari getini , alifata kamera na kuangalia ni nani aliekuwa akipiga honi na alitabasamu mara baada ya kuona ni mpenzi wake mellisa .
Siku iliofata bwana zakayo hakutaka kabisa kuchelewesha kazi kwani huo ndio uliokuwa moto wake wa kazi , aliamini kumaliza kazi haraka ndio kupata kazi nyingine na kutengeneza pesa Zaidi , siku hio asubuhi alikuwa amevalia kinadhifu sana kama kawaida yake , huku akiwa kwenye gari yake aina ya roll Royce , muda huo alikuwa akikatiza mtaa wa magomeni akiiendea morocco na moja ya nia yake kubwa ilikuwa ni kwenda mpaka mikocheni , dakika chache mbele alikuwa mbele kidogo ya jengo la airtel alikunja kushoto kwa mbele na kuingia kwenye jengo ambalo ndani yake kulikuwa na makao makuu ya kampuni ya bruno enterprises .
Baada ya kuegesha gari yake alitoka na moja kwa moja alieelekea mpaka ndani ya jengo hilo , aliangalia kwenye screen kujua flour ambayo kampuni ya bruno ilipokuuwa ikifanya kazi, aliipata ilikuwa ni ghorofa ya 10 , aliingia kwenye lift na moja kwa moja alienda mpaka ndani ya flour hio na hapo ndipo alipopigwa na mshangao kwani alikuta wafanya kazi wakifanya usafi na hali iliiokuwepo humo ndani iliashiria kabisa kampuni imefungwa , alimsogelea mdada mmoja aliekuwa akikusanya baadhi ya maboksi na kumsalimia .
“samahani naulizia nini kinaendelea hapa , maana nilikuja kwajili ya kuonana na meneja wa kampuni ya bruno “.
“ pole kaka kumbe huna taarifa , kampuni ya bruno saivi imefungwa rasmi , na kubashilishwa jina , kwa sasa inajulikana kwa INNOVA “
“ INNOVA ?””
“ ndio kaka , kwa taarifa ni kwamba kampuni imeuzwa kwa kampuni ya INNOVA ya Italy na sasa wamehamia jengo la PSPF posta “ aliongea mwanadada huyo huku akiendelea na kazi .
Zakayo alitoka ndani ya jengo hilo huku akiwa na mawazo ya hapa na pale , alikuwa akiwaza ni nani alieuza kampuni hii ilihali mhusika mkuu alikuwa hana ndugu hapa nchini , hio ilikuwa ni kazi nyingine kwake ambayo aliona anapaswa kuitafutia jibu asubuhi hio .
Jambo hilo aliona ni ngumu kulipatia majibu na hapo ndipo jina la rafiki yake irene aliekuwa ni moja ya wana usalama ndani ya kitengo cha TISS liliibuka kwenye kichwa chake , alitoa simu yake wakati huo akiwa ndani ya gari yake na kuanza kupiga , na sekunde chache tu simu hio ilipokelewa .
“ nambie mwana mitindo”
“ safi za masiku Irene ?“
“ poa umenisusa kweli zakayo “
“ sio kweli mambo ni mengi tu “
“ mhmh haya , niambie lakini “
“ fresh , kuna jambo nataka unisaidie Irene “
“ jambo gani hilo ?”
“ kuna taarifa naihitaji , naamini lazima mtakuwa nayo kitengoni hapo “
“taarifa gani “
“ bruno interprises nafikiri hii taarifa mnayo juu ya hii kampuni kuuzwa “
“hahaha zakayo sisi tunahusikaje na maswala ya mauzo ya kampuni “
“ come on Irene , kuna mambo ya kiusalama yanaendelea ndani ya ile kampuni , na naamini lazima kuna mambo mnayajua , mimi nataka unisaidie kujua ni nani alierithi mali za bruno “.
“mhmh , inaonekana upo kazini kama kawaida yako “
“ yeah kuna kazi naifanya na ndio maana nahitaji hio taarifa “
“ sawa ngoja niangalie kama kweli kutakuwa na taarifa nitakupatia “
“ hayo ndio maneno “
“ ukifanikisha hilo uje mjengoni ni kupe gauni la bure “
‘ hahaha … haya bwana na nitakuja kweli “.
Zakayo baada ya kuona ashapata sehemu ya kupatia taarifa yake , hakuona haja ya kuzunguka jiji hilo kwa siku hio na moja kwa moja alienda mpaka kwenye kampuni yake mtaa wa mlimani city ili kumsubiria Irene afanye kazi yake .
“kuna mtu lazima hapa nchini alimsaidia damiani kufika nchini thailland , nikimpta huyu nitajua wapi alipo damiani na kama yupo hai au hayupo hai “ aliongea zakayo huku akiingia kwenye lift akiingia ndani ya jengo lake la biashara la PSSSF commercial tower .
Baada ya kufika ndani hakukaa sana , aliingia secretary wake akimtaarifu kuna mgeni anashida naye , kwani alikuwa akihitaji vazi .
“sasha mruhusu aingie , si unajua utaratibu “
“ ndio lakini kagoma anasema uende upande wa maduka anataka ukamchagulie nguo “ aliongea sasha na kumfanya zakayo ainuke kwenye kiti chake na kutoka ofisini ili kwenda kuonana na mteja jeuri , alisogea mpaka kwenye maduka yake maduka yake ya nguo na hapo ndipo alipojikuta jicho likimtoka .
“ janeth !” aliongea zakayo kwa mshangao akimwangalia mlimbwende aliekuwa mbele yake ,
“ zakayoo “ aliongea janeth na kisha walikumbatiana kwa furaha .
“ nimekumis sana bro “. Aliongea janeth kwa mapozi na kumfanya zakayo atabasamu kwani alikuwa akimjua vyema huyo mwanamke aliekuwa mbele yake .
“ umerudi lini ?”
“ nina miezi sasa tokea nirudi “
“ ndio ukashindwa hata kuniambia kama umerudi “.
“ mambo mengi , ila jana baada ya kujua jina la kampuni yako nikaona ni vyema leo nije hapa unichagulie nguo “.
Aliongea janeth kimapozi , maana janeth na yeye alikuwa mzuri mno , na ni kwa kipindi kirefu sana zakayo alikuwa akimpenda huyo mwanamke tokea siku ya kwanza kukutana nae nchini indonesia katika mashindano ya mitindo , na siku alipokuja kugundua kuwa mwanamke huyo alikuwa ni mtanzania ndio alipojenga nae urafiki , lakini bahati mbaya kwake ni kwamba mrembo huyo hakuwa mwepesi kabisa , kwani hata baada ya kurusha ndoano , aliishia kuambiwa kuwa wawe marafiki na huku janeth akipigilia msumari kwa kumuita zakayo kaka jambo ambalo kwa zakayo aliona kama tusi . .
Baada ya kumchagulia gauni , waliongozana na kurudi ofisini , zakayo alimkaribisha na kisha waliketi , na muda huo huo simu yake ilitoa mlio wa sauti kuashiria ilikuwa ikiita , aliitoa mfukoni na kisha aliangalia jina la mpigaji na kukutana alikuwa ni Irene , alimwangalia janeth na kisha alipokea simu hio
“ niambie irene”
“ poa, nishafanikisha kazi yako “
“ enhe niambie “
“ mmiliki wa mali za bruno mpaka sasa ni bwana stephano lamberk “
‘ stephano lamberk ?”
“ ndio inasemekana ni mtoto wake na kwa taarifa nilizo nazo ni kwamba tayari yupo hapa jijini dar es salaam “
“ sawa asante Irene nashukuru kwa msaada wako “
“ naja kuchukua gauni langu nikitoka kazini ndio nitapokea asante yako “
“ hahaha .. wewe njoo tu “
Alikata simu na kumwangalia janeth aliekuwa bize na simu .
“ sasa bro mimi naondoka “
“ hivi janeth utaacha lini kuniita bro “
“ hahahah.. basi zakayo mimi naondoka “
“ aliongea janeth na kisha alinyanyuka na kuaga na kuondoka huku akimuacha zakayo akimwangalia kwa nyuma kwa masikikitiko “
“ abasi kuna jina nakutumia hebu jaribu kufatilia taarifa zake “ aliongea janeth mara baada ya kufika kwenye gari yake .
“ jina gani ?”
“ stephano lamberk”
“ sawa “
Aliingia kwenye gari na kisha kusepa bila kujulikana alikuwa akielekea wapi muda huo
******
Ilikuwa ni siku nyingine muda wa asubuhi kabisa mwanadada merina siku hio kazini aliletwa na Patrick , walikumbatiana mara baada ya kufika kwenye maegesho na kisha Patrick aliwasha gari yake na kuondoka , wakati huo Patrick anaondoka kwenye mapokezi ya magari , kuna gari nyingine ilio onekana kumfatilia , kwani Patrick alivyo ondoka tu na gari ile iliondoka .
Ni gari iliokuwa ikiendeshwa na mwanume mmoja wa makamo miaka si chini ya ishirini na nne mrefu mweupe , mara baada ya kusogea umbali wa mita kadhaa kutoka kwenye jengo la SWIFT TRANSIT , alitoa simu yake na ,kupiga mahali .
“ vipi hassani “
“ madam kama ulivyo niagiza nimewaona wako pamoja , asubuhi hii Patrick kamleta hadi kazini kwake “
“ sawa , endelea kuwafatilia “
“ sawa madam “ aliongea bwana yule na kisha alitoka eneo lile kwa spidi
Upande wa ofisini mara baada ya kuingia tu na kuketi kwenye kiti chake , aliingia afisa masoko .
“Madam kuna tenda hapa imetufikia “
“ inatoka wapi? “
“ kampuni ya NEXT LEVEL TECH (NLT )”
“ ni kampuni gani? “
“ ni kampuni ya maswala ya utengenezaji vifaa vya simu na innovation (uvumbuzi )
Aliongea mwanaume huyo wa makamo alikuewa akifahamika kwa jina la sogone wambura , ambaye alikuwa ni afisa masoko , alimpatia merina tenda hio na kuanza kuipitia kwa umakini mkubwa .
“ kuna maelezo mengine ?“
“ ndio kasema atakuja CEO kusaini mwenyewe hio tenda , pia anasema kuna mambo mengine ya kibiashara ya kuzungumza “.
“ sawa hakuna shaka mpe maelekezo secretary wangu amuwekee appointment “ aliongea merina huku akionekana kuangalia baadhi ya makabrasha yaliokuwa hapo ndani , lakini dakika chache tu simu yake ya mezani iliita .
“ kuna nini monica ?” alikwa ni secretary .
“ kuna mgeni wako anasema anamaswala binafsi ya kuzungumza na wewe “
Merina alijikuta akiwasha kamera ya mapokezi kumuangalia mgeni mwenyewe , alijikuta akifikiria kidogo na kisha alimwambia amruhusu .
Alikuwa ni mwanaume mrefu mweusi alievalia suti iliomkaa vyema , miaka yake si chini ya therathini mwenye ndevu za kiuchebe .
“ karibu “
“ asante sana merina , mimi sio mkaaji lakini kuna ujumbe wako hapa nimekuletea kutoka ikulu “.
“ ujumbe gani?? “.
“ madam wema anataka kuonana na wewe siku ya leo saa kumi kamili jioni hoteli ya serena “
Merina alijikuta akishangaa , hakuelewa kuna sababu gani ya yeye kukutana na mke wa raisi alijifikiria kwa dakika chache .
“ sawa nitaonana nae “ aliongea merina
“ hakuna shaka , lingine amesema usimwambie Patrick swala hili “
Jambo hilo pia lilimshangaza merina , lakini alijikuta akishangaa Zaidi , na pia waswasi ulichukua nafasi yake , kwani hakujua ni kwanini kuonana na mwanamama huyo kulikuwa na masharti kama ni mambo ya kawaida tu , aliamini kuna jambo , lakini hakutaka Zaidi kuweka mambo mabaya katka kichwa chake aliona ni bora atii wito kwanza .
Siku yake ilikuwa ni bize siku nzima kwani alikuwa akikutana na watu mbali mbali ambao siku hiio , muda kama wa saa saba muda ambao alikuwa ndio anataka kutoka kwa ajili ya kwenda kupata chakula ndio muda ambao secretary aliingia ndani ya ofisi yake akimtaarifu kuwa kuna mgeni anataka kuonana nae
“ anaitwa nani “
“ kajjitambulisha kwa jina la stephano lamberk kutoka kampuni ya NLT “
“ okey sawa mruhusu “
Alijiweka sawa kumsubiria bwana huyo kwani kwa tenda ambayo aliacha asubuhi , ilikuwa ni moja ya tenda yenye pesa nyingi mno ambazo angeingia nae mkataba , kampuni yake ingeneemeka .
“ karibu “ aliongea merina akimkaribisha bwana stephano lamberk ambae aliachia tabasamu mwanana baada ya kumuona mwanamke huyo mbele yake.
“ kitendo cha merina na yeye kukutanisha macho na mwanaume huyo alievalia kinadhifu kabisa suti yake na tai alijikuta akiganda kwa dakika “
“ asante “ ilikuwa ni sauti iliomshitua sana merina , ni sauti ambayo alikuwa akiijua vyema , japo mtu aliekuwa mbele yake hakuwa na sura ya mtu mwenye sauti hio kwani aliekuwa mbele yake alikuwa ni mzungu .
CNTINUARA .
SEHEMU YA 38
Japo mwanaume aliekuwa mbele yake alikuwa mzungu lakini sauti yake iliendana vyema na ya damiani , hakujua ni kwanini anamawazo hayo lakini ukweli ni kwamba alikuwa akiikumbuka vyema sauti ya damiani, sauti ambayo alikuwa akitamani sana kuisikia katika maisikio yake kwa mara nyingine .
Upande wa bwana stephano alikuwa akimwangalia mlimbwende huyo huku akitamani hata kusema neno tofauti na jambo lililomleta , lakini kwake aliona ni jambo la hatari sana kufanya hivyo japo mara kwa mara alikuwa hamkumbuki mlimbwende huyo lakini siku hio alivyopata kuonana nae alijikuta akishangaa , kwanza kilichomshangaza ni juu ya mrembo huyo kuwa CEO wa kampuni hio , kwani mara ya kwanza kwake kuonana na mrembo huyo ni siku ambayo alikuwa ndani ya kampuni hio kwa ajili ya kuomba kazi na merina na yeye akiwa mmoja ya waombaji kazi , jambo hilo lilimshangaza kidogo , fikra zake hazikumuacha kwenye jambo hilo tu , lakini alikumbuka vyema siku walipo kuwa ndani ya wilaya ya lushoto hospitalini , siku alipofungua macho yake na kuonana na merembo huyo , fikra hizo zilimfanya aanze kuvuta hata picha ya kupigwa busu kwenye paji la uso wake , japo tukio hili alikuwa amelisahau kwa miaka kadhaa , lakini kulikumbuka jambo hilo tena , aliona ni kama lilitokea jana yake , alijikuta akitabasamu huku akishindwa kuzuia mshangao wake mpaka pale alipo karibshwa kiti ndani ya ofisi hio .
“ naitwa stephano lamberk ni kurugenzi mtendaji wa kamouni ya NLT “ alijitambusha huku akipeana mkono na merina .
“ karibu bwana stephano , kwa majina naitwa merina sosteness ni mkurugenzi mtendaji wa kamuni ya SWIFT TRANSIT LIMITED “.
“ nashukuru kukufahamu merina , nipo hapa kwa ajili ya business proposal , nimejaribu kuangalia baadhi ya makampuni ya usafirishaji hapa nchini yene mafanikio na nimeona kampuni hii imefanya vizuri Zaidi , hongera sana “
Aliongea bwana stephano na kumfanya merina atabasamu , huku akipenda sauti ya bwana stephano , alitamani aendelee kuongea .
“ asante sana karibu SWIFT TRANSIT”
“ nashukuru sana , labda niende moja kwa moja ili nisichukue muda mrefu , nadhani nishatanguliza tenda kwenye kampuni hii “
“ ndio nimeiangalia , na niseme asante sana kwa kuchagua kampuni yetu “
“kama nilivysema mwanzo sikuchagua kampuni hii kwa sababu za kiupendeleo ni kutokana na vigezo vya kupokea tenda kama hii “ aliongea huku akitoa karatasi baadhi na kumpatia merina .
“ kampuni yangu kwa sasa inahitaji malighafi nyingi kutoka nje ya nchi ,kwa ajili ya maswala ya kiteknolojia , hivyo nimeona mizigo yangu yote ya kampuni yapitie kwenye kampuni yenu , huo ni mkataba ambao utakuwa ni wa miaka miwili ya mwanzo , na utaongezeka kutokana na ufanisi wa huduma kutoka kwenye kampuni yako “.
“ nashukuru bwana stephano kwa kuchagua kampuni yetu , na nimeangalia vipengele vya mkataba huu viko vizuri na vinaendana na utendaji wa kampuni yetu hivyo nakubali mkataba huu “. Aliongea na kisha alisaini mkataba huo na kupeana mikono na kisha stephano aliaga na kuondoka huku akionekana kuwa na tabasamu pana usoni .
Alienda moja kwa moja mpaka kwenye gari yake aina ya benz new model na kuwasha gari na kuondoka .
“ she is beutifull as always” stephano alijikuta akitamka hayo maneno huku akiwasha gari yake na muda huo nia yake ni kwenda kurasini
Upande wa merina , alijikuta kumbukumbu zake zikimrudisha nyuma , siku aliokuwa akiongea na damiani nje ya kampuni yake , kuna vitu alikiri anaweza kuvisahau katika maisha yake lakini sio sauti ya kijana damiani , sauti hio hakuweza kuisahao kabisa katika , kwani kwake ni kama kumbukmbu aliokuwa nayo juu ya damiani , na hata mwanaume aliengia hapo na kusaini nae mkataba alikiri kwamba alikuwa na sauti iliokuwa ikiendana kwa kila kitu na ya damiani , alijikuta akiinuka na kuangalia upande wa nje wa jengo hilo akimwangalia mwanaume huyo akiingia kwenye gari yake na kuondoka , alirudi kwenye kiti chake mara baada ya kuvuta pumzi ndefu mno , na kukaa kwenye kiti chake lakini bado sauti haikumtoka , alijikuta akichukua simu yake na kuanza kutafuta jina la stephano lamberk kwenye mitandao .
“stephano lamberk ni mtoto wa marehemu bruno lamberk amezaliwa mwaka 1996 ni mmiliki wa kampuni changa ya teknojia ijulikanayo kwa jina la NEXT LEVEL TECH yenye makazi yake nchini Tanzania ana utajiri wa dollar millioni 400 zinazotokana na umiliki wa hisa wa asilimia 23 ndani ya kampuni ya HUAWEI “
Ilikuwa ni taarifa ambayo ilimuacha mdomo wazi merlina , mambo mawili yalimfanya ashangae , jambo la kwanza ni kuwa mtoto wa bruno , jambo la pili ni utajiri aliokuwa nao , mambo hayo mawili kwa wakati mmoja yalimfikirisha kwa wakati mmoja , kumbukumbu za mama yake damiani kuuliwa kikatili na watu waliokuwa maadui wa bruno lamberk ziliijaza fikra yake mara moja .
“ this is serious “ ni nenno aliloongea merina akimaanisha jambo hilo sio la kawaida.
Upande wa stephano na yeye alikuwa kwenye mawazo ya aina moja na merina alikuwa akimuwazia mrembo huyo tokea anatoka ndani ya kampuni hio mpaka anafika kurasini , jambo lililompa fikra fikirishi ni juu ya mrembo huyo mara yake ya kwanza kukutana nae kujitambulisha kwake kama mtu ambae alikuwa akifanya interview kama yeye.
“ who is merina ?” ni moja ya swali lililokuwa ndani ya kichwa chake , alienda moja kwa moja mpaka ndani ya kiwanda , mtu wa kwanza kukutana nae alikuwa ni Rebecca , mwanamama ambae anaishi maisha ya kifahari jijini lakini haikujulikana alikuwa akifanya kazi gani .
“ luang shu yupo wapi ?” lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa damiani ama stephano .
“ yupo ofisini “..
Damiani aliaenda moja kwa moja mpaka upande wa jengo moja refu lilikuwa limejengwa kwa usanifu wa hali ya juu ambapo pembeni kulikuwa na kiwanda cha uzalishaji , aliingia moja kwa moja kwenye lift ambayo ilimpeleka mpaka ghorofa ya nane .
Baada ya kufika alisalimiana na dada mmoja hivi mweusi sio mrembo sana lakini alionekana kuwa mrembo kutokana na mavazi yake na pia na miwani yake ya macho aliovalia ilimfanya apendeze .
“damiani karibu boss mkubwa “
“ vipi maendeleo “.
“ bado tupo kwenye mwanzo wa kudraft mapendekezo na idea mbalimbali “
“ namaanisha DREAMER T
“ twende ukajionee mwenywe kila kitu kipo sawa kwa sasa “.
Walitokana kuingia kwenye lift iliokuwa na vibonyeze kumi na moja yaani kuanzia ground flour mpaka gorfa ya kumi , baada ya kuingia ndani ya hii lift , luangshu alibonyeza namba moja mara mbili na lift ilianza kushuka kwenda chini na walikuja kutokea kwenye vyumba vya chini ya Ardhi lakini huwezi jua kama walikuwa kwenye ardhi kwani ndani yake hakukuwa kukitofautiana sana na vyumba vya juu tofauti mkubwa ndani ya flour hii ya chini ya ardhi ni mwanga, mwanga wake ulikuwa ni wa rangi ya blue tupu , na pia ilionekana sehemu kama maabara flani hivi , lakini pia ili uweze kuingia ndani ya flour hii baada ya kutoka kwenye lift lazima uvuke four layers of protection (deterrence , access control ,detection and identification aka four layers )hivi ni vizuizi vya kiulinzi kwa mtu kuingia ndani ya eneo hilo .
Basi baada ya kupita kwenye vizuizi hivyo vyote moja kwa moja waliingia kwenye chumba ambacho kilikuwa na maandishi makubwa ya DREAMER T ROOM .
“ ding!!! WELCOME MISTER DAMIANI RABANI AND LUANG SHU IN DREAMER T ROOM “.
Ilikuwa ni sauti flani ya kike ya kuvutia iliosikika kwenye sauti zamasikio ya damiani , alijikuta akishangaa , japo alikuwa muwezeshaji wa project nzima ya ujenzi wa chumba hicho lakini hakuamini kutakuwa na mafanikio ya aina hio , kwa mtu wa kawaida usingejua chumba hicho kinahusu nini , kwani hakikuwa na kiti chochote Zaidi ya mwanga wa blue na taa flani za mfano wa projector rangi ya blue .
“ unaweza kuuliza chohote “ aliongea luang shu na damiani alijjifikiria na likaja jambo kwenye kichwa chake .
“DREAMER T who is merina sosteness CEO of swift transit limited ?“(dreamer t nataka kumjua merina sosteness ni nani )
“Dingg !!!” MERINA SOSTNESS IS THE FOUNDER AND CEO OF SWIFT TRANSIT LIMITED, BORN IN 1996 IN SINGIDA , HAS STUDIED AT HARVARD UNIVERSITY TAKING A COURSE IN ECONOMICS HER MOTHER AND FATHER ARE OWNERS OF ATPAY , A CANADIAN BASED COMPANY , HER FORTUNE IS US$10 MILLION. MANY LIKE TO TEASE HER BY CALLING HER A RICH BEUTY .
ARE YOU SATISFIED OR NEED MORE INFORMATION ABOUT MERINA MISTER DAMIANI ?”
(merina sosteness ni mwanzilishi na mmiliki wa kampuni ya SWIFT TRANSIT Limited , amezaliwa mwaka 1996 ndani ya mkoa wa singida amesomea maswala ya uchumi ndani ya chuo cha Harvard , mama yake na baba yake ni wamiliki wa kampuni ya ATPAY lampuni yenye makao yake makuu ndani ya canada , utajiri wake ni dolla milioni kumi (bilioni ishirini na tatu za kitanzania ) wengi wanapenda kumtania kwa kumuita mrembo tajiri . , vipi unahitaji taarifa Zaidi kumuhusu merina au umeridhika bwana damiani rabani )
“ No thank you ( hapana asante )
“ WELCOME AGAIN”(karibu tena )
Damiani alijikuta akitabasamu na kuamuangalia luang shu , aliona hela zake alizotoa kwajili ya kujengewa DREAMER T hazikwenda bure kabisa .
*******
MIEZI KADHAA NYUMA
SHENZHEN –CHINA
Ilikuwa sku ya kipekee sana kwa bwana damiani rabani kutambulishwa kama moja ya wamiliki wa kampuni ya HUAWEI jambo kwake lilikuwa ni kama ndoto , hakuamini katika maisha yake angekuja kukaa na watu wakubwa na wenye pesa zao kama ilivyokuwa siku hio , hata CEO wa kampuni ya HUAWEI alipomtaka kunyanyuka kwa ajili ya kusalimiana na wakurugenzi wa bodi ,kwake aliona ni kama alikuwa ndotoni , makofi aliopigiwa na watu hao kuonyesha ishara ya kumkaribisha katika familia hio, kwake aliona akiamka asubuhi atakuta ni ndoto , lakini haikuwa ndoto , kila kitu kilichokuwa mbele yake kilikuwa ni uhalisia , damiani alikuwa sio damiani wa miaka ya nyuma huyu alikuwa ni damiani mwingine , damiani tajiri, damiani anaye miliki hisa ndani ya kampunni kubwa nchini china katika maswala ya teknolojia .
Hata baada ya kikao hicho cha wakurugenzi kuisha na kuanza kuonyeshwa mazingira ya hapo ndani , alizidi kushangaa , alikiri kwamba kampuni hio ilikuwa ni kampuni iliokuwa imeendelea sana katika swala zima la kiteknolojia .
Alizungushwa kwenye baadhi ya sehemu ndani ya jengo hizo , sehemu ambazo ilikuwa ni baadhi tu ya viwanda vilivyokuwemo vikitengeneza baadi ya bidhaa ikiwemo simu alishangaa mno , lakini ulikuwa ni mshangao ulioambatana na mafunzo ndani yake , alitamani sana mambo kama hayo yangekuwepo ndani ya taifa lake la Tanzania , japo taifa lake lilikuwa masikini , lakini alijivunia sana kuwa mtanzania na aliona maendeleo waliokua nayo wachina hata Tanzania wanaweza pia kuwa nayo kama tu wakiwa na uongozi thabiti na sera imara .
Wakati akiongozwa na CEO wa kampuni hio akielezwa jinsi ya utendaji wa kampuni hio ,ndio alikuja bwana mmoja wa kichina na kuongea maneno machache na CEO wa kampuni hio aliekuwa akijulikana kwa jina la shang lee .
“ mister damiani , huyu ni luang shu ni mtoto wa waziri wa mambo ya ndani ya uchina “ alitambulishwa kwa bwana luang shu na damiani alitabasamu huku wakiongea kimombo na bwana luang shu .
“damiani nimefika hapa kukupa mwaliko maalumu wa kukutana na baba yangu kwa ajili ya chakula cha jioni “ aliongea bwana luang shu na kumfanya damieni aendelee kushagaa , kila jambo kwake lililokuwa likiendelea ndani ya nchi hio mengi yalikuwa ni ya mshangao , kualikwa na waziri wa nchi hio lilikuwa ni jambo kubwa mno na sio kubwa tu , ni heshima kubwa sana , japo alikuwa na mawazo kwanini anataka kuonana na waziri huyo lakini aliona kuna sababu ya kutii wito .
Damiani alikubaliana na bwana luang shu kwa ajili ya kuonana na baba yake , muda wa saa mbili kamili za jioni , ndio muda ambao damiani alikuja kuchukuliwa ndani ya hoteli ilioko ganzhou na kwenda kwenye miadi yake , na mtu aliekuja kumchuku alikuwa ameagizwa na waziri huyo .
Gari iliyoyoma mpaka ndani ya hoteli kubwa ya kimataifa iliokuwa ndani ya jiji la Shenzhen iliokuwa ikifahamika kwa jina la four season , ni hoteli kubwa sana iliokuwa na mazingira ya kuvutia .
Mara baada ya kufika ndani ya hoteli hii alipelekwa moja kwa moja mpaka kwenye vyumba vya VIP kwa ajili ya kuonana na mheshimiwa , kwake yeye aliendelea kushagaa mandhari ya hoteli hio kama kawaida yake , lakini wakati anaingia ndani ya flour hio ndefu yenye mazingira ya kuvutia ndipo kidogo tu apigane kikumbo na mwanamke mmoa mrembo wa kiafrika , mpaka mwanadada ambae alikuwa amemtangulia damiani alitabasamu .
Damiani aliangalia na mwanadada huyo kisha aliomba msamaha na akapishana nae na kuendelea na safari
Waziri wa mambo ya ndani ya uchina alikuwa ndani ya eneo hilo tayari kwa ajili ya kuonana na damiani rabani , hakuwa peke yake kwani pia alikuwa na mwanae luang shu , damiani aliasalimiana na mheshimiwa huyo kwa heshima zote na kisha alikaribishwa .
“ bwana rabani kwa jina naitwa shu liang lee ni waziri wa mambo ya ndani ya uchina , nadhani unamaswali mengi unayo jiuliza kwanini ghafra tu nimekuita kwa ajili ya kuonana na wewe “ aliongea waziri wa mambo ya ndani , aliekuwa amevalia suti yake , alikuwa ni bwana mmoja mwenye kipara cha umri , alionekana tayari alikwisha uvuka ujana mpaka wakati huo .
“ ni kweli mheshimiwa , kwanza kwangu imekuwa heshima kubwa sana , japo wito wako niliupkea kwa mshangao , kwani sikuwahi tegemea katika maisha yangu kuja kuonana na kiongozi mkubwa kama wewe ndani ya taifa hili “
“ haha ni kweli uyazungumzayo , lakini kila jambo linatokea kwa sababu maalumu , labda nijitambulishe kuwa mimi ni moja ya watu wa karibbu na marafiki wakubwa wa marehemu raisi bendera lakini pia kupitia bendera nimefahamiana na mfanya biahsara bruno lamberk “ .
“nashukuru sana mheshimiwa kwa kujua kuwa wewe ni moja ya marafiki wa raisi bendera , kiufupi mimi pia ni mmoja ya watu ambao nilikuwa nikimpenda sana raisi bendera na kifo chake kilinigusa sana “.
Walikuwa wakiongea huku chakula tayari kikiwa kishaletwa , kilikuwa ni chakula cha ki VIP kweli kwa rabani alikuwa mshamba lakini hakutaka kuonekana mzembe kabisa , alijitahidi kuendana na mazingira .
“ bwana rabani kama nilivyojitambulisha kwako juu ya uhusiano wangu na bendera pamoja na bruno , nataka niseme kwamba kabla ya raisi bendera hajafariki aliniomba kuisaidia Tanzania katika maswala ya kiteknolojia , na mpaka sasa ninapo zungumza kuna vijana ambao wamemaliza kusoma hapa china Katika maswala mbali mbali ya kiteknolojia na kwa sasa wapo kwenye moja ya kampuni baadhi kwa ajili ya kupata uzoefu , lakini kwa bahati mbya ni kwamba mpango huu tuliufanya kuwa binafsi mimi na bendera mpaka pale vijana hao watakapo maliza masomo yao , lakini ndio hivyo mheshimiwa amekwisha tangulia mbele za haki , na ni jukumu langu kuangalia ni namna gani vijana hawa kama ilivokuwa nia ya mheshimiwa kuhakikisha wanarudi na kuendeleza teknolojia ndani ya taifa la Tanzania , kwani naamini hio itakuwa ni moja ya jambo ambalo kwangu mimi ndio nitalifanya kuenzi kifo chake “ alinyamaza kisha akaendelea na wakati huo damiani hakuwa na jambo la kuongea Zaidi ya kushangazwa na maneno ya waziri .
“ hivyo bwana rabani kwakua sasa ushajulikana kama mfanya biashara rasmi na mrithi wa mali zote za bruno , wewe kama mfanya biashara nataka tuambizane katika kuhakikisha teknolojia ndani ya Tanzania inakuwa , kwa kunzisha kampuni ya kiteknolojia nchini Tanzania , na vijana wote wa kitanzania walio chini yangu nitawaweka chini yako , naamini wewe ni mzalendo wa kweli kwa taifa lako hivyo swala hili sio gumu lako kulifanyia maamuzi “
Swala hilo kwa damiani lilimpa furaha , na furaha aliopata ni kuona kwamba kuna watu waliokuwa wakiitakia mema nchi yake kama ilivyokuwa kwa waziri wa viwanda , lakini jambo moja ambalo lilikuwa likimpa mashaka mpaka kwa wakati wake ni watu wanaomtafuta , pia kisasi alichokuwa akitaka kukikamilisha juu ya wote waliohusika na kifo cha mama yake .
itaendelea ......

USISITE KUWASILIANA NAMI WATSAPP KWA NAMBA 0687151346
AU UNAWEZA GUSA LINK HIO HAPO CHINI CHINI ITAKULETA MOJA KWA MOJA WATSAPP
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom