HereMAWASILIANO : 0687151346
ILIPOISHIA SEHEMU YA SITA
Iliishia ndani ya miaka mitano nyuma kipindi ambacho raisi bendera anapewa madaraka rasmi na kutangaza vita zidi ya wauzaji wa madawa ya kulevya
“mimi nafikiri kwa sasa hakuna swala la kuogopa kwani mtandao wetu una mizizi mirefu sana na hata kwa washirika wake pia ni waaminifu , kinachotakiwa kwasasa ni kuangalia upepo kwanza na kuzuia mzigo wowote kuingia nchini kwa muda huku tukitafuta ni mbinu gani raisi anaipanga “ aliongea Bruno kwani ndie aliekuwa kiongozi mkuu wa umoja wa wauza madawa nchini..
“ mkuu ulichosema ni sahihi kabisa lakini swala hili ili lifanikiwe lazima tuwe na mtandao wetu pale ikulu ambao utakuwa unatupatia taarifa “ wakati wakiendelea na kikao mlango ulifunguliwa na aliingia mwanadada aliekuwa amevalia suti ya zambarau mwenye rangi nyeupe mrefu mrembo. Alimsogelea bwana Bruno na akamuinamia na alionekana kuna jambo alilokuwa akimwambia na hapo Bruno alijikuta akitoa macho .
SEHEMU YA SABA
“ kuna nini mkuu ?” aliuliza mkuu wa majeshi .
“washa televisheni hio “ aliongea Bruno .
Ilikuwa ni taarifa ya mkuu wa police akitangaza rasmi kuvunjwa kwa kamati ya ulinzi wa kamati ya maswala ya upambanaji ya madawa ya kulevya (DCEA).
“ hili ni swala ambalo tulilitegemea raisi kulifanya “ aliongea athumani .
“ sio hilo tu kuna kubwa Zaidi “
“ lipi hilo Bruno? “
“ mheshimiwa raisi kavunja kamati zote za ulinzi , chakula , mpaka usafi ikulu “ aliongea Bruno na hapo kila mmoja alitoa leso yake na kufut jasho .
“ naona mambo yanazidi kuwa magumu na tunahitaji kulifaanyia kazi hili haraka iwezekanavyo maana mpaka sasa hatuna mtandao wa kutupatia taarifa kwa kile kinachoendelea ikulu “ aliongea sam.
“ mkuu tunafanyaje? “
“ hapa hakuna cha kufanya inabidi tuhold biashara kwa sasa , nitaandaa ripoti na nitaituma makao makuu ya U-97 , nyie wengine inabidi muwaambie washirika wenu kusimamisha biashara na kufuta ushahidi .”
Na kikao kilifungwa huku kila mmoj akitoka , hakuna hata mmoja kati yao aliekuwa kwenye hali nzuri kiumunekano kwani wote walionekna walikuwa kwenye frustration ( waswasi ).
****
Zikiwa zimepita siku mbili mbele , raisi bendera alisaini sheria mpya ya ubadilishaji fedha za kigeni , uliowasilishwa na gavana wa benki , sheria hio ilikuwa ikizuia taasisi zote na maduka yaliokuwa yakibadilisha fedha kutokubali au kufanya mabadilishano ya pesa za kigeni juu ya kiwango cha dollar elfu kumi yaani milioni ishirini na Zaidi , pili sheria ya kuzuia wasafiri kuingia nchini na kiasi cha pesa juu ya dollar elfu kumi bila kutolewa maelezo TRA .
Sheria hio mpya ilikuwa ni mwiba kwa wafanya biashara wa madawa ya kulevya nchini , na hilo walilipokea kama pigo lingine .
Baada ya mswada huo wa sheria raisi aliendelea na pangua pangua yake kwanzia ngazi za juu bandarini mpaka ngazi za chini alimteua mkuu wa mkoa mpya wa dar es salaam , mtwara , mwanza , tanga , katavi , na kigoma , lakini hakuishia hapo tu aliunda baraza jipya la mawaziri huku pia akimteua waziri mkuu mpya , jamnbo ambalo liliacha wananchi mdomo wazi pamoja na washirika wake kwani mtu alieteuliwa hakutegemewa .
Bwna hamduni saidi rajabu ndie aliekuwa waziri mkuu mpya , mwanzoni akiwa ni katibu ofisi ya waziri mkuu .
Baada ya teuzi hizo raisi aliitisha kikao kingine huku kikao hiki kikiwa na watu wengi Zaidi , alikuwemo waziri mkuu wakuu wote wa idara ya usalama , mkuu wa DCEA mpya alieteuliwa , waziri wa mambo ya ndani bwana rajabu ngasu , waziri wa katiba na sheria alfred peter na waziri wa fedha bwna innocent mushi .
“ hongereni waheshimiwa kwa kuteuliwa kwa kila mtu na nafasi yake , lakini niseme kwamba pia niwapongeze kwa uzalendo wenu kwa nchi hii , kwani kupitia hilo ndio leo hii linatufanya tuwepo mahali hap kwenye hiki kikao , simaanishi kwamba sisi ndio wazalendo tu wa nchii hii , wapo wazalendo wengine lakini sisi ndio wawakilishi wao , na naamini huko nje kwa sasa wanamatumaini makubwa sana juu yetu katika ufanyaji maamjuzi yenye maslahi mapana ya nchi hii .” alitulia kidogo kisha akaendelea
“ nafasi mlizopo zinasababu kubwa sana , na niseme kwamba ni nafasi ngumu sana kwani zina majukumu makubwa sana ambayo mnakwenda kuyatimiza kwa maslahi mapana ya nchi hii nyie kama wazalendo , kama mnavyo jua taifa hili lipo kwenye wakati mgumu sana na kipinid tulichopo sasa ni kibaya sana kwani vijana wanadhidi kuangamia kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya , hivyo basi nimewaita ndugu zangu hapa kwa nia kuu moja ya kuwaapa muelekeo wa serikali yangu , pili kuweka na kuwapa mpango wa hatua za mapambno ya madawa ya kulevya .
“ bwana lazaro kitwana “ (huyu alikuwa ndio mkuu wa DCEA mpya ) kazi yako kuanzia sasa ni kuunda timu ambayo itakuwa na polisi watakao kuwa na kazi moja maalumu ya kukamata kila mshukiwa yoyote wa biashara ya madawa ya kulevya hapa nchini .” aliendelea
“ mkuu wa TISS , mkuu wa majeshi na IGP nadhani faili langu lipo tayari “
“ ndio mkuu “
“ good nikitoka hapa nitalihitaji “.
“hivyo basi kwa umoja wetu hapa ndani nataka nitangaze kwamba kuanzia sasa nyie ni wajumbe wa mamlaka ya kupambana na madawa ya kulevya nchini , mamlaka hii itaongozwa na makamu wa raisi na mwenendo mzima wa maswala haya mtahusika , niwaamnbie tu kuwa vita imeanza na ndani ya mwezi ujao sihitaji kunusa harufu ya aina yoyote ya madawa ya kulevya .” aliongea muheshimiwa na kisha kikao kiliisha lakini mkuu wa majeshi , mkuu wa usalama wa taifa na IGP walibaki .
“ waheshimiwa nadhani kazi mmeimaliza , hivyo nahitaji orodha ya vijana wa kazi .
“Danieli mtalemwa mwenye namba ya utambulisho N00D)( huyu ni komandoo daraja la kwanza amepata mafunzo yake nchini CUBA , china na Thailand , huku elimu yake ya kipelelezi na ujasusi akiichukua nchini Israeli , mafanikio yake ni makubwa sana katika operesheni alizo fanya hapa nchini ikiwemo ya ambone tanga , kibiti na rusumo ni mhitimu wa chuo kikuu UDSM ngazi ya shahada , monash nchni Australia akisomea maswala ya uinjinia .
Suzzane rashidi ( aka miss k) namba za utambulisho N02S huyu ni komandoo daraja la kwanza , lakini pia amefudhu mafunzo ya kipelezi kwasasa yuko nchini urusi kama undercover agent katika misheni ya umoja wa taifa , mafunzo yake kachukua CUBA na thailland huyu ni hatari Zaidi katika udunguaji , lakini pia ni mbobezi katika maswala ya computer (IT).
Zakayo yakobo( agent z ) mwenye namba za utambulisho N01Z huyu ni pia ni komandoo , lakini pia ni mhitimu wa maswala ya kipelelezi ni mhitimu wa chuo cha uigizaji nchini marekani elimu yake ya kimapigano kamalizia nchini china ,, kwasasa yupo chini Indonesia kwenye mashindano ya mitindo .
Wengine ni Irene joseph , martine sheiza na abasi ndumbalo hawa wote ni wana usalama chini ya kitengo cha TISS .”
Alimaliza mkuu wa TISS na kisha alimkabishi mheshimiwa faili hilo .
“ kazi nzuri naamini upembuzi wenu ni yakinifu mkuu wa idara kazi ya kwanza anayotakiwa kufanya agent Z ni ya abduction(utekaji) .
“ unamaanisha nini mheshimiwa kuhusu utekaji , ni nani anapaswa kutekwa?? “
“hio ndio kazi ya kwanza itakayotuingiza katika mtandao wa madawa ya kulevya nikimaanisha mtu anayetakiwa kutekwa ni weak point(sehemu yenye udhaifu ) na tunatakiwa kuitumia kikamilifu , target yetu kwa sasa ni bwana Bruno lamberk” akanyamaza kisha akaendelea .
“ kwa taarifa nilizo nazo ni kwamba huyu ndio mkuu wa usambazaji wa madawa ya kulevya hapa nchini na afrika mashariki kwa ujumla , chini yake anawashirika wengi ambao hawajulikani na wapo hapa nchini , tukifanikiwa kumpata Bruno basi na washirika wake tunaweza kuwapata , lakini kazi hio sio rahisi kwani hakuna ushahidi wa moja kwa moja , na ili kufanikiwa katika hilo inatupasa kumgeuza mshirika wetu .
wazee walichoka maana walikuwa wakimjua huyo mzungu alikuwa ni mwekezaji mkubwa hapa nchini , na ukiachana na uwekezaji wake alikuwa pia ni moja ya watu waliokuwa wakisaidia jamii sana , sasa kutajwa kwake kama muuza ngada mkubwa nchini jambo hilo lilikuwa ni kubwa na la kuogopesha, na kustajabisha kwa wakati mmoja , lakini ndio hivyo bwana huyu alikuwa akijizificha biashara zake haramu kwa kujivika ngozi ya chui .
“mheshimiwa kama uzungumzalo ni kweli , swala hilo linahusiana vipi na misheni unayotaka aifanye agent Z “
“safi iko hivi , Bruno ana mtoto wake wa siri sana kwa taarifa nilizo nazo na mtoto huyo inasemakana bwana huyu anampenda sana huyo mtoto na anaweza kufanya kitu chochote kile ilimradi mtoto huyo asidhurike kwani ndio anatarajia kuwa mrithi wake , nadhani mpaka hapo mnaelewa kwamba udhaifu mkubwa wa Bruno ni huyo mtoto, lakini jambo la kushangaza mpaka sasa ni kwamba bwana Bruno hamfahamu huyo mtoto kwani mwanamke aliezaa nae kaamua kumficha , na anachojua bruno ni kitu kimoja tu kuwa ana mtoto wa kike .
“ sasa kama hamjui mtoto wake sisi tutafanikiwa vipi kumshawishi aamini kwamba huyo ni mtoto wake? “
“hio kazi niachieni mimi mpango huu haujaanza kusukwa leo tu umeanza muda mrefu mimi ni mtekelezaji tu na nyie pia mnatakiwa kutekeleza swala hilo “
Baada ya msheshimiwa kutoa maagizo hayo zakayo alitumiwa ujumbe wa misheni ambayo alitakiuwa kuifanya nchini marekani, huku akipokea maagizo ya moja kwa moja kutoka ofisi ya raisi .
“ unapaswa kupiga picha baada ya kumteka cheni alio vaa hakikisha sura haionekani mtoto huyo yuko chuo x na picha yake ni hio .
******
Tajiri lamberk alikuwa kwenye wakati mgumu sana wakati huo wa kiuongozi katika umoja wao walio upa jina la UNITY 97(U-97) , aliandaa ripoti na kuikamilisha kisha aliituma makao makuu ya umoja huo yaliokuwa nchini mexico , ripoti hio ilikuwa imejumuisha mwenendo wa maswala ya kibiashara kwa ujumla nchini Tanzania .
Baada ya kutuma ripoti hio masaa machache alipokea ujumbe kutoka makao makuu .
“ we received your report and level 01 unity leader conceded with your recommendations until further notice. “ akimaanisha kwamba kiongozi wa juu kabisa wa U-97 amepokea na kukubaliana na mapendekezo yake mpaka pale taarifa nyingine Zaidi itakapo tolewa .
Baada ya kupokea feedback alisambaza kwa wakubwa walio chini yake huku akitoa onyo la kuchukua tahadhari mapema kwani muda wowote hali inaweza kubadilika.
Siku mbili mbele baada ya kutoa ripoti hio , ilikuwa muda wa saa mbili usiku akiwa kwenye jumba lake la kifahari eneo la mbezi beach , alipokea simu kutoka kwa mtu asiemfahamu , simu hio ilimtaka kuingia upande wa watsapp kwani kuna zawaid yake .
Bruno hakuamini macho yake , mapigo ya moyo yalipiga kite kitu alichokiona na taarifa alio iona ilikuwa ni mwiba kwake .
Kilikuwa ni kidani flani ambacho kilitengenezwa kwa madini ya almasi na kidani hicho kumbukumbu zake zilimpeleka miaka ishirini nyuma , ndani ya miaka miwili tu tokea aanzishe makazi yake nchini Tanzania , miaka hio mara baada ya kuanzisha makazi yake nchini Tanzania akiwa kwenye mawazo sana ya familia yake aliokuwa akiishi nayo katika jiji la new York kuuwawa kikatili sana na hio ilitokana na ugomvi mkubwa aliokuwa nao na wauza madawa ya kulevya wenzake , huku akituhumiwa kuwasaliti, ndipo mkuu wa kikundi hicho alipotuma watu wake na kuiteketeza familia yake na yeye baada ya tukio hilo la kusikitisha katika maisha yake alikimbilia nchini Tanzania , na kwanzia siku hio aliishi akiwa na kisasi moyoni , na kupitia tukio hilo alikuja kujiapia hata kuja kutengeneza familia katika maisha yake yote , lakini baada ya kupita miaka miwili ndipo alipo kutana na mwanamke wa kitanzania kabila la kinyaturu , mwanamke huyu alikuwa ni mfanya kazi wa hoteli ya singita grumet iliokuwa ndani ya mbuga ya wanyama serengeti , ulianza urafiki ndani ya hoteli hio na mwishowe ukazaa mapenzi , kutokana na hali ya kulewa ya bwana Bruno siku hio alijikuta akifanya mapenzi na mwanamke huyo aliejitambulisha kwake kwa jina la wema sufiani , kulivyokucha ndipo alipokuja kushituka akiwa kalaliwa na mrembo huyo , kuanzia siku hio bwana Bruno kila akifika kwenye hoteli hio lazima afanye mapenzi na wema , baada ya mwaka mmoja kupita wa mahusiano yake na wema ndipo siku alipo fika ndani ya hoteli hio kukutana na habari za wema kuwa mjamzito .
Ilikuw ni habari mbaya sana kwake kwani alikuwa ashaweka nadhiri ya kutokuja kutengeneza familia katika maisha yake yote lakini pia aliogopa jambo lililomtokea miaka ya nyuma kujirudia kwa mwanamke wema na mtoto atakaezaliwa , hakutaka kumuonesha wema ni jinsi gani habari hio ilikuwa mbaya kwake , alichokifanya yeye ni kumuonesha kuwa kafurahia habari hio huku kichwani akipanga yake .
Baada ya miezi tisa hatimae wema alijifungua na wakati huo alikuwa ashaacha kazi yake ya uhudumu wa hoteli na alikuwa nyumbani kwao singida , Bruno alipata taarifa ya wema kujifungua mtoto wa kike , iilikuwa habari ya kufurahisha kwake , lakini ya kuogopesha siku mbili mbele ndio siku alio fika singida kwa siri sana na akakutana na wema na hapo ndipo alipo fanya jambo ambalo kwa wema lilikuwa na majonzi sana na kuhudhunisha , kwani alimpa kadi ya benki huku akimwambia hela iliokuwemo humo ilikuwa ni kwa ajili ya matunzo ya mtoto na yake lakini pia alimpa kidani cha almasi kikiwa na cheni , kilikuwa kimetengeneza kwa muundo wake wa kipekee sana .
“ wema consider me I am dead from now on , I have family and I don’t need trouble with your baby , my family will not accept her , and I cant do anything about it, for child safety and yours don’t ever ever look for me .( akimaanisha kwamba kwanzia siku hio amchukulie kama amekufa kwani familia yake haingeweza kumkubali huyo mtoto , na akimwambia kuwa asije akamtafuta tena “
“ kwa wema ilikuwa ni kilio lakini baada ya siku alikubaliana na swala hilo , alikiangalia ile cheni na kisha akamvalisha mwanae , huku akienda benki na kuangalia kiasi cha pesa alichoachiwa na mzungu huyo , zilikuwa ni pesa nyingi sana kwa wakati huo , na kwakuwa mwanamke huyo alikuwa na akili ya maisha basi aliweza kufanya biashara , na biashara hio ikamtambulisha rasmi na kuwa mwanamke mashuru ndani ya nchi , na hio ilikuwa ni baada ya miaka kumi mbeleni , katika wakati wote huo alikuwa akisikia habari za Bruno na kwa Bruno pia alikuwa akisikia habari za wema , baadae wema alikuja kuolewa na henry mushi , kipindi hicho bwana huyo akiwa ni waziri wa maliasili na utalii, lakini jambo ambalo lilimshangza bwana Bruno ni kwamba hakuwahi kumuona mtoto wake kabisa , na hata kwenye familia ya henry na wema hakukuwa na jina la mtoto wake swala hilo lilikuwa likimuumiza kichwa sana na kutaka kujua ni wapi mtoto wake alipo lakini liligonga mwamba , kwani japo alijaribu kuongea na mwanamke huyo hakupata ushirikiano kabisa kwani jibu lake lilikuwa moja kuwa asahau kuwa ana mtoto kwenye maisha yake yote na akiendelea kumfatilia atampoteza , na kwakuwa Bruno hakutaka ugomvi na mwanamke huyo ukizingatia kipindi hicho mwanamama huyo alikuwa na nguvu sana nchini , na mume wake walikuwa ni watu wenye msimamo ndani y serikali hakutaka kabisa purukushani .
Upande pia wa henry hakuwahi kujua kuwa mke wake wema ashawahi kuwa na mtoto , kwani wema hakuwahi kumtambulisha mtoto wake kwake, miaka kadha mbele walifanikiwa kupata watoto pia . kwa hio hio ilikuwa ni kumbukumbu ya miaka ishirini iliopita .
Basi turudi kwenye mika mitano nyuma siku hio ndio siku ambayo bwana Bruno anatumiwa picha na mtu asiemjua ikionesha kidani hicho ,huku chini ikiambatana na maelezo
“ ukitaka ukweli juu ya mahali alipo mtoto wako fika new Africa hoteli chumba namba 108 siku ya ijumaa saa nne kamili usiku hakikisha jambo hili linakuwa siri yako kosa moja tu utampoteza mtoto wako” huku video ya mtoto wake ikimuonesha katekwa .
inaendelea,...... ..
SafiVipi wadau niweke Seadon 2 yotee
Unatakiwa kuwa mvumilivu kweli ukitaka kusomahii riwaya iliisha?