SEHEMU YA 26
MWAKA MMOJA NYUMA
BANGKOK THAILLAND
“Welcome in thailland damiani”. Karibu thailland damiani .
“ thank you “ alijibu damiani na kisha bwana yule ambaye bado hakujitambulisha jina kwa damiani walitoka pale uwanje wa ndege wa survanabhumi kwa gari moja nyeusi aina ya MBW X7 , damiani ilikuwa ndio mara yake ya kwanza kufika katika hili jiji kwa huo muda wote alikuwa akishangaa sana mazingira , yalikuwa ni mazingira ya kuvutia kwakweli tofauti na jiji la dar , waliingia barabara ya suan luang , wakapita siratil express , hapa ilikuwa ni barabara ya juu kama pale ubungo lakini daraja hili lilikuwa limejengwa kwa usanifu mzuri mno , baada kama ya nusu saa hivi wakaja kukunja kwenye barabara iliokuwa ikielekea wilaya ya pathum wan gari iliendelea kuyoyoma huku kwenye gari hakuna aliekuwa akimuongelesha mwenzake kila mu alikuwa akiwaza yake , baadae kidogo walipita lumphing park , hapa ni moja ya sehemu za bata sana ndani ya jiji la Bangkok. Baada ya madakika kadhaa ndipo walipo ingia kwenye jengo ambalo mbele lilikuwa na jina MUAY THAI ACADEMY (MTI).
Hiki ni moja ya vyuo vinavyo fundisha mafunzo ya ngumi vikubwa ndani ya jiji la Bangkok , ni sehemu ambayo kulikuwa na mazoezi mengi ya kujifunza kuna gym kama gym , lakini kuna wale ambao wapo mahali hapo kwa ajili ya kuweka miili yao fit(body fitness) , pia kuna wale waliokuwa wakipigana kwa kulipwa , lakini ukiachana na hao wote kuna ambao wanafundishwa private , yaani mafunzo ya ziada na hawa wengi ndio wanakuwa wanatoka mataifa ya nje .
Basi bwana damiani alifikishwa ndani ya camp hio na kisha bwana yule alimkaribisha na moja kwa moja alimuongoza mpaka ofisini kwa bwana zaripov ambae ndie aliekuwa mkuu wa kambi hio ya kimapigano , Sasa damiani kuna jambo ambalo lilimshangaza , kwani tokea anatoka Tanzania alikuwa akijua kuwa alikuwa anakuja kukutana na mtu aliempigia simu , lakini kitu cha kushangaza ni kwamba mara jamaa ya kuingizwa kwenye kambi hio alianza kupewa sheria za kambi , na kuambiwa hapo tayari ashafika kwa hio ajiandae kwa mazoezi makali . uvumilivu ulimshinda na kutaka kujua kwanini yuko hapo na ndipo alipo omba kuuliza swali kwanini yupo hapo na jibu alilopewa lilimchosha .
" Damiani kazi yetu hapa nikuwafundisha watu ngumi wanapofika hapa , na wewe tulipokea usajili wako na tukapewa maelekezo utafika hapa hivyo tukaja kukupokea kwa hio hatujui zaidi ya hilo " aliongea bwana huyo kwa kingereza kwa lafudhi yake ya Thai.
hakukuwa na maelezo mengi charn chai ambae ndie bwana aliempokea aurport alipewa maelekezo ya kumuonesha mazingira ya hapo ndani baada ya kuandikishwa rasmi kuwa mwanafunzi wa chuo hicho , muda huo ilikuwa ni saa kumi na moja kwenda na nusu .
" Utakaa hapa kambini kwa muda wa miezi mitatu kwa gharama za hapa , then utatafuta makazi " aliongea charn chai , muda huo walikuwa wakipita kwenye moja ya sehemu za kimapigano ' ARENA ' kulikuwa na uwanja kabisa sehemu ya kushuhudia mapambano .
Baada ya kufanyiwa orientation alipelekwa hadi kwenye hostel za camp hio na kuonyeshwa kitanda chake , hostel hizo zilikuwa ni kama ‘hall’(eneo la moja kwa moja ) moja ambao lilikuwa na vitanda kushoto na kulia vingi , muda huo humo ndani hakukua na mtu ilionesha watu walikuwa wametoka kwani kulikuwa na mabegi na baadhi ya vitu , vikionesha kwamba kuna watu waliokuwa wakiishi ndani ya eneo hilo .
Baada ya kupewa kitanda charn chai alimwambia watoke waende upande ambao watu wanafanya mazoezi na pia amuoneshe canteen ilipo ,.
Ilikuwa ni mshangao kwa damiani kwani watu waliokuwepo hapo ndani walikuwa wakijifua kimazoezi hatari , wengi wao miili yao imetuna kwa mazoezi makali walio kuwa wakipewa , kuna waliokuwa wakipigana , kuna waliokuwa wakifundshwa kwanni kuna walimu kabisa walionekana kuwaelekeza na haikuwa wanaume tu pia mpaka wanawake walionekana wakiwa wanachukua mazoezi ya kimapigano .
Basi mwezi wa kwanza ukapita na hapo kijana damiani alikuwa akifundishwa muda wote huo na master zaripov , alikuwa jamaa mmoja mwenye misuli ambaye hakuwa na utani kabisa , damiani alianza kukolea mazoezi japo mwanzoni ilikuwa ngumu kwake , lakini kila akikumbuka mama yake alivyouliwa kikatili alizidi kujifua kimazoezi ,juhudi zake zilizaa matokeo maatokeo mazuri , kwani ndani ya mwezi huo hakuwa yule damiani mnyonge tena , alikuwa anajua kukwepa kupangua pigo kuruka sarakasi kiufupi mapigano ya muay thai yalikuwa yashaanza kumuingia akililini vizuri jambo lililomfurahisha sana zaropov , kwa kipindi chote hicho hakuwa na marafiki wengi zaidi ya salamu tu ,kwa hostel aliokuwa akiishi kulikuwa na mchanganyiko wa watu kutoka mataifa mbalimbali .
Mtu ambae alikuwa amemzoea alikuwa ni charn chai pekee , charn chai yeye alikuwa ni mkufunzi wa mafunzo ya fitness na alikuwa akijihusisha na wale watu matajiri waliokuwa wakija kufundishwa kuwa fit kimwili .
Mwezi wa pili ndio mwezi ambao sasa kijana damiani ndio alianza kujulikana , kwani kipindi chote cha mafunzo alikuwa akifundishwa peke yake na master zaropov , sasa siku moja ndio alipelekwa ulingoni ndani ya kumbi hio kwa ajili ya kuchuana na bwana mmoja aliekuwa akitokea uingereza , bwana huyu alikuwa ana miezi sawa na ya damiani tokea kuingia kwenye chuo hicho lakini alikuwa pia ni moja ya mpiganaji aliefuzu na aliekuwa akizijua vyema kuzipiga kithai thai .
wenzao siku hio walikuwa wakishuhudia pambano , walitoa heshima kwa kithai , siku hio watu wengi walionekana kumshangilia bwana james ( muingereza ) na hio ni kutokana na jamaaa huyu alikuwa akijulikana na alikuwa ashapigana na watu kibao hapo ndani na kuwapiga , kwa damiani wala hakuwa na wasiwasi kabisa , kwani na yeye alikuwa yupo vizuri sana na alikuwa moja ya wanafunzi waliokuwa wakizingatia kile alichokuwa akifundishwa .
Basi mpambano ulianza , kila mtu alirusha ngumi teke na kupangua , huku kila mtu akionekana hakuna aliye kuwa na presha na kila mtu alikuwa akimsoma mwenzake mchezo , damiani na yeye mwili wake ulikuwa umetuna kwa siku hizo chache alizokaa hapo kambini .
James aliruka pigo la kushitukiza ambalo kwa muay thai linafahamika kama kradit te ( jump kick ) pigo hili lilimyumbisha damiani na kurudi nyuma huku akijipamga upya , lakini james alikuwa ni mtu ambae sio mcheleweshaji wa muda kwani alileta tena pigo la kradot thip na awamu hii damiani alimsoma vyema kwani alikwepa na kumrudisha nyuma na pigo takatifu la Te trong ( front kick ) na kumpepesua nyuma james huku watu wakishangilia na hali hio ilimpa hasira kwani alianza kurusha mapigo mfululizo lakini damiani alikuwa akijitahidi kuyapangua , kuna muda damiani alizidiwa na kupigwa pigo takatifu la roundhouse kick na kumpeleka chini na kufanya watu wamshangilie james , Damiani alihisi maumivu ila hakutaka kiyapa nafasi , alijipanga upya na sasa ni kama kashituliwa kwani na yeye alianza kuonesha ujuzi wake katika Kuzipiga kithai thai , james alikuwa akipangua kitaalamu kila pigo , lakini alijikuta akishindwa kupangua pigo moja la teke lililokuwa lilikujilana kama Axe kick na yeye kwenda chini na hapo watu walishangilia , na ilionekana ngoma droo , james aliona akizembea lazima ataibika siku hio hivyo ile dharau aliokuwa akimletea Damiani aliacha na jambo hilo damiani aliliona na kimfanya atabasamu kwani aliona hio ni fair play , zilipigwa kweli siku hio huku kila mtu akimbahatisha mwenzake na yeye lazima abahatishwe hivyo hivyo mpaka mwisho wa mchezo hakuna alieshinda pambano hilo kwani wote walitoka droo na walikuwa wamechoka , lakini hilo kwa james aliona kama dharau kubwa kwake kwani aliona kwanzia siku hio tayari ashapata mshindani wake ambae ni damiani n ahata kuwa na ile heshima aliokuwa nayo tokea mwanzo ..
Kwa upande wa damiani watu walianza kumfahamu sasa , maana kitendo cha kutoka droo na james , ambae alikuwa ndio mpiganaji wa level za juu kushinda wote kilimpa umaarufu ,
Master zaropov alimpa hongera na kumfundisha zaidi mbinu mpya ,mwezi wa tatu ulikatika na ndipo damiani rasmi alitoka camp na kwenda kuishi kwenye apartment . , alikuja kupata apartment ya dollar 500 iliokuwa ikijulikana kwa jina la V apartment karibu kabisa na shopping mall ya Emsquare ni eneo moja la kifahari .
Kutoka hapo mpaka camp ni mwendo wa nusu saa kwa kutembea ila ukipitia shortcut ni kama dakika ishirini , kwa taks ni dakika kumi tu kufika na hio ni kutokana na kuwa barabara ilikuwa ni ya mzunguko , sasa mweizi wa kwanza akiwa apartment ulipita na hapo jumla alikuwa na miezi minne , katika mwezi huo ndio siku alipokutana na kijana sabi katika mall ya Emsqure .
Kwanza siku ya kwanza kukutana waliangaliana kama watu waliokuwa wakifahamiana , lakini haikuwa hivyo , hio ikikuwa ni kutokana na lafudhi yao pamoja na rangi kwani sehenu waliokutana ni sehemu ya malipo(cashier) , kwani baada ya manunuzi Damiani alitoa kadi ya CRDB tanzanite card , kadi ambayo sabi aliona kabisa nembo ya benki hio na kwa haraka haraka alijua kadi hio ilikuwa ikipatikana kwenye taifa la Tanzania tu , baada ya dada aliekuwa hapo mapokezi kuswipe kadi ile na kumrudishia damiani , aliondoka huku sabi na yeye akiripia kwa njia ya cash yaani Thai baht ( pesa inayotumika thailland ) .
Baada ya kulipia alitoka haraka haraka mpaka nje ya mall ile huku akizumgusha kichwa kulia na kushoto , na alifanikiwa kumuona Damiani kwa mbali akizunguka nyuma ya mall hio
" Wewe mtanzania " aliongea kwa sauti sabi kwa kuita sauti iliosikika vyema kwa damiani lakini sio kwa wathailland kwani hawakuwa wakielewa lugha ya kiswahili waliishia tu kumwangalia sabi ila hawakumuelewa , kwani lugha yao kubwa ilikuwa ni Thai , ilibidi Damiani asimame ..
"Vipi bro "
" Freh vipi " hapo sabi alitabasamu kwani kujibiwa kwa kiswahili alijua kabisa yupo na mbongo halisi tena wa bara .
Basi kuanzia hapo Sabi na damiani walifahamiana rasmi , sabi yeye alikuwa ashamaliza mafunzo yake ya kimapigano tayari kwani alikuwa ndani ya jiji hilo kwa muda wa miezi sita na siku na alikuwa amemalizia katika chuo kilichokuwa kikifahamika kwa jina la black camp .
Tokea wawili hawa wakutane hakuna hata mmoja aliefunguka kwa mwenzake jinsi alivyo ingia ndani ya nchi hio zaidi ya kusema kuwa walifika kwa ajili ya mafunzo basi , Sabi yeye alikuwa akiishi victory monument , mbali kidogo na alipokuwa akiishi damini lakini kwa treni ya umeme ilikuwa ni mwendo wa kama dakika kumi hivi kufika .
Urafiki kati ya sabi na damiani ulizaliwa kwanzia siku hio damiani kila akitoka camp anasafiri kwa sabi victory monument village kwenda kumsalimia wakati huo sabi na yeye alikuwa ni mtaalamu wa mapigano ya Muay Thai kutoka black camp , lakini pia alikuwa akisomea cozi ya upelelezi katika chuo cha International detective university & college , kilikuwa hapo hapo bangkok .ilikuwa ni kozi ya miaka miwili .
Basi siku moja ilikuwa ni muda wa jioni hivi , muda ambao sabi alifika V apartment kwa ajili ya kumsalimia rafiki yake , kama kawaida alipanda ghorofa ya kumi kwemda juu na kufika nje ya chumba alibonyeza kengere na dakika chache damiani alimkaribisha kwa furaha , huku jamaa alionekana kuwa ndio alikuwa akirudi kutoka camp maana alikuwa ndio kwanza anaenda bafuni .
Hii apartment aliokuwa akiishi damiani ilikuwa ni ya kishua tofauti na ya sabi ile ya kule victory manument , hii ilikuwa ina seble ,balcony , jiko na chumba cha kulala , sasa wakati sabi amekaa hapo sebleni huku damiani akiwa bafuni ndipo alipoona laptop ya HP ikiwa na flashdisk , aliiangalia ile flashdisk na wakati huo Damiani na yeye anafika kutoka bafuni akijifuta maji na taulo .
"kaka naona unatumia flash ya kijasusi , halafu umeichomeka kwenye HP ndogo kama hio , inasoma kweli ??" aliongea sabi.
"haha .. mbona ya kawaida hii " .
" kaka nina degree ya computer science ujue , hio flash hapo inaweza kusoma lakini sio mafaili yote , mpaka uwe na computer yenye uwezo mkubwa na program yake ndio utaona mafaili yote " aliongea sabi na hapo damiani alipata mshangao kwani flash hio ni ile aliopewa na bruno , na kama kweli maneno anayo zungumza sabi yalikuwa na ukweli basi huenda kukawa na zaidi ya taarifa kwenye hio flash aliwaza damiani huku akiingalia ile flash .
" unasema kweli " mimi sijui kuna mtu tu kanipa .
" Aliekupa atakuwa mwanausalama kama sikosei , hizo kama hutaziona TISS basi CIA au wewe ni mwana usalama ndugu yangu " akiongea kwa utani lakini alikuwa ashahisi kitu alijua kuna uwezekano wa damiani kuwa mwanausalama kwani alijua mara nyingi wattu wanao safri kutoka mataifa ya mbali kuja ndani ya nchi ya thailland mara nyingi wanakuwa ni wanajeshi au wanausalama ..
Mimi sio mwanausalama , ila nina ndugu yangu alinipa nitumie sasa sijajua kama ni ya kijasusi , aliongea damiani na kumfanya sabi atabasamu , sabi alikuwa mwepesi sana kwenye kumsoma mtu na alijua kabisa damiani alikuwa anamficha kitu ,
SEHEMU YA 27
Damiani hakutaka kabisa kumuamini sabi nakumueleza maswala yake ukizingitaia pia walikuwa ndio kwanza wamejuana , ndio maana alikataa kabisa kukubali flash ile kama ilikuwa ya kijasusi , japo kuna kitu alikifahamu na kupitia maaelezo ya sabi lakini hakutaka kabisa kumpa nafasi ya kujua historia yake ya nyuma mpaka kuja kufikia hapo nchini thailland .
Upande wa sabi pia aliligundua jambo hilo na kuona kabisa damiani alikuwa akimficha kitu ila hakutaka kumlazimisha kukubali ukweli kuwa flashdisk ile ilikuwa ni ya kijasusi japo alikuwa na uhakika sana , na pia hata yeye kwa upande wake hakuwa akmuamini damiani kwa undani Zaidi , kwani hata yeye alikuwa amemficha mambo mengi lakini jambo lililowafanya kuwa marafiki ni kutoka nchi moja .
Basi walipotezea swala lile na kuendelea na mishe zao zingine , siku hio walikuwa wamepanga waende kula bata usiku huo , na kwa damiani hakuwa mpenzi wa hayo mambo lakini kwa ushawishi wa sabi , damiani alikubali ,maana tokea aingie ndani ya jiji hilo hakuwahi kutoka na kwenda maeneo ya starehe kama club na sehemu zingine .
Saa mbili kamili usiku ndio walitoka eneo hilo , na siku hio sabi alimwambia damiani walikuwa wakienda club moja maarufu iliokuwa ikifahamika kwa jina la thailland night life , hii ni club moja maarufu sana iliokuwa ikipatikana kilomita kadhaa kutoka sehemu anayo ishi damiani mtaa huo huo ulio kuwa ukijulikana kwa jina la sukhumvit soi nyuma kidogo ya mji wa korea town unakunja kulia ndio unakutana na club hii , unaambiwa hii sehemu kama umeoa usiende maana huko lazima ufanye usaliti kwani watoto warembo wa kithai hawatakuacha salama tena hutumiii nguvu wanajileta wenyewe .
Basi baada ya kutoka barabarani walichukua taksi mpaka kwenye hii club , siku hio damiani ndio alijua kuwa alikuwa haijui thailland vizuri , kwani warembo aliokuwa akiwaona mchana akipishana nao wakiwa kwenye shughuri zao za kawaida alikuwa akiwaona wa kawaida na walikuwa hawampi hamasa , lakini alipo ingia kwenye hii club ndio alijikuta akisisimka mwili sana kwani warembo wamekaa kihasara hasara tu huku ngoma zinazo chezwa hapo ndani zilikuwa sio za kitoto , kwa sabi alionaekana alikuwa mzoefu sana wa hayo maeneo.
Aliishia kujisemea kweli hii ni night life , basi walisogea mpaka upande wa pili kushoto kwenye moja ya viti virefu na kukaa hapo huku kuna waliokuwa wakiburudika kwa kucheza go go dance , kuna waliokuwa wakinywa , kuna waliokuwa na wapenzi wao , fujo tu ilimradi kila mtu alikuwa akihakikisha usiku wake unakuwa ni wa furaha .
Hawakuchukua muda tayari walikuwa washasogelewa na mrembo mmoja sana alievalia nusu uchi
“ swasdiii” alisalimia mrembo huyo kwa kithai akimaanisha ( hi )..
“ chung sung “ alijibu sabi na kumfanya damiani ashangae kwani hakujua kuwa mwenzake alikuwa akijua kuongea kithai ..
“sah wah dee khrap “ aliongea kimapozi huyo mrembo akimsalimia damiani ila damiani hakuelewa maana alimwangalia sabi , na sabi alitabasamu ..( hapoalikuwa akimaanisha kwamba rafiki yake ni mkimya na anaonekana mgeni )
“khea mi phud thiy “ sabi hapo alijibu akimaanisha kwamba mwenzake hajui kithai laabda kingereza .
Lakini wakati wakiendelea kuongea na mrembo huyo alikuja mrembo mwingine na kukaa kwenye meza yao , na wakati huo tayari muhudumu ashakuja na kuchukua oda yao , na kwa sabi kama kawaida aliagiza pombe ila kwa damiani bado alikuwa akishangaa agize nini mpaka pale alipo muuliza rafiki yake kama kuna kinywaji tofauti na pombe akaambiwa vipo pepsi , fanta nk.
Damiani aligiza fanta , wale warembo walishangaa kwa kutabasamu m ,uzuri ni kwamba ndani ya hii club ni kwamba mara nyingi watu wanaokuja hayo maeneo mara nyingi ni watalii , hivyo hata wadada wengi warembo wanaoingia hizo sehemu wanajua kuongea kingereza .
Hivyo waliendana vyema na damiani katika maongezi , watu walikuwa wakicheza kweli moja ya ya staili pendwa ndani ya club nyingi ndani ya jiji la Bangkok hususani sukhumvit soi, papaya club ni go go dance , ilikuwa ni moja ya mziki wa kuamsha vibe , damiani alianza kunywa pepsi lakini rafiki yake alimladhimisha kunywa bia , na pia kwa ushawishi wa wale warembo pia ulimfanya damiani kunywa bia , japo mwanzo aliona kama chungu lakini baadae alijikuta ashamaliza chupa , akaongezewa ya pili na hapo ndipo akili iliingia mdudu kwani alianza kuchangamka na kuongea maneno yasio eleweka kwani alikuwa akichangya kisambaa , Kiswahili na kingereza kwa wakati mmoja jambo ambalo liliwafurahisha sana wale wadada , lakini japo alilewa ila alikuwa akijielewa , ila sasa hakuacha kuwashika shika wale wadada .
Lisaa limoja mbele mizuka ilikuwa imepanda kwani damiani aliomba kutoka na yule dada aliekuja nae mara ya kwanza na dada kwakuwa alikuwa hapo kwa kazi hio basi hakukataa , hata kwa sabi hivyo hivyo baada ya wote kulipia walitokana warembo hao na kutokomea , sabi haikueleweka hata alienda upande upi ila kwa damiani yeye alienda mpaka sehemu anayoishi .
Saa mbili kamili asubuhi ndio damiani alikuwa akishtuka kutoka usingizini huku kichwa kikimuuma , alinyanyuka na wakati huo kitandani hapo hakukua na mtu na hata hakumbuki kilichotokea usiku , alichokuwa akikumbuka ni kwamba alikuwa bar usiku uliopita lakini jinsi alivyo rudi hakukumbuka kabisa . , aliingia baufuni huku akiwa na maswali mengi na kujiapia hatokuja kunywa pombe tena , baada ya kujimwagia maji huku akivuta kumbukummbu za jana yake , kuna mambo yalikuwa yakipita katika kichwa chake kama picha za kuja na kupotea , na hapo ndipo kumbukumbu za kuja na mwanamke hapo ndani zilijirudi, ni kama mtu aliekurupuka usingizini , alioga na kisha alitoka akiwa anajifuta maji mpaka sebuleni na hapo ndipo alipopigwa na mshangao kwani begi lake ambalo alikuwa ameliweka chumbani lilikuwa sebleni huku nguo zikiwa zimetapakaa , kengele ya hatari iligonga kwenye kichwa chake alikimbilia begi na kulifungua na kuangalia baadhi ya vitu vyake , aliviona aligeuka akitafuta laptop na flash hakuiona na hapo ndipo alipo data , kwani laptop na flash alikumbuka kabisa aliacha sebuleni hapo lakini sasa asubuhi hii hakuiona.
Alijikuta akikaa chini na kuwaza huku akiwa mtu kama aliekuwa amechanganyikiwa , kuna hisia zilikuwa zikimwambia kuwa mwanamke aliekuwa amekuja nae usiku mahali hapo alikuwa ndio alie chukua laptop yake , lakini kuna hisia pia za sabi kuchukua laptop yake , aliona ni ufala kubaki hapo sebleni akiwaza aliona jambo hilo anapaswa kulitafutia ufumbuzi mapema , kwani maneno ya sabi ya kwamba flash disk ile ni ya kijasusi na huenda ikawa na Zaidi ya taarifa liligonga kwenye kichwa chake , alikimbia mpaka chumbani kwake na kisha alichukua nguo haraa haraka akavaa kisha akatoka na safari ikaanza , alifika mpaka kituo cha kupandia treni na kisha safari ya victory monument ikaanza , dakika kumi tu tayari alikuwa eneo hilo , baada ya kushuka alikunja kushoto na kuingia mtaa wa makazi ya watu na akakunja kulia na kukutana na jengo ambalo ndio sehemu aliokuwa akiishi sabi .
Sabi na yeye muda huo alikuwa ndio kwanza anaamka usingizini na pembeni yake alikuwa amelaliwa na mwanamke aliekuwa mtupu bila kuwa na nguo hata moja , alimsogeza taratibu nakisha alinyanyuka na kwenda maliwato na kujisaidia , lakini ile anamaliza alisikia mlango ukigongwa alitoka na kwenda kufungua na alikutana na sura ya damiani .
“ vipi mzee mapema yote hii , halafu unaonekana unawasiwasi “ aliongea sabi kivivu huku akionekana bado alikuwa na usingizi .
“jana hujaja kule getto kwangu usiku “
“ sijaja , jana si baada ya kukupandisha kwenye taksi na yule mrembo nikapanda na mimi ya kuja huku “ aliongea sabi na kumfanya damiani akae kwenye kiti kilichokiuwepo hapo ndani , na wakati wanaongea yule membo na yeye alitoka huku hakuwa hata na nguo na wala hakuwa na wasiwasi alitoka mpaka sebleni .
Na alionekana na sabi alimwambia avae asepe , alivaa na kisha alikuja na kuomba hela na sabi alimpa baht 400 akasepa .
“ niambie mzee kuna inshu gani kwani ?”
“ ile flash na lamptop nadhani yule ghashi kaondoka navyo “.
“ ile niliokwambia ya kijasusi ?”
“ ndio hio mzee nimeamka nimesachiwa kwenye begi na baadhi ya sehemu zingine , lakini hela zipo kisichokuwepo ni laptop na ile flash .”
“ sasa jambo hilo dogo tu mbona limekufanya unakuwa na wasiwasi hivyo , kwani kuna cha maana gani kwenye ile flash? “.
“ sabi sikia niambie tunawezaje kumpata yule mwanamke , wewe unaudhoefu , ile flash ni muhimu sana ni ya kijasusi kama ulivyo sema na kama kweli ulivyosema jana kama inatumika kuficha mafaili basi kuna umuhimu wa kuipata
“ aliongea damiani na kumfanya sabi amwangalia kisha na yeye alikaa chini na kumwangalia damiani na akafikiria kidogo .
“ tnaweza kama tukimtafuta , lakini nataka kujua kilichopo kwenye flash kina umuhimu gani , na kwanini achukue flash na laptop “.
“ kuna mambo sijakuambia , ila nitakuambia kama tutampata kwanza yule mwanamke na kuchukua ile flashdisk , na hapo nitakuambia kila kitu , kiufupi ni kwamba mtu kapoteza maisha kunikabidhi ile flash “ aliongea damiani na kwa sabi kwa udhoefu na mafunzo yake ya muda mfupi ya kiupelelezi aligundua jambo kutoka kwa damiani .
“ ngoja tutamtafuta naaamini bado atakuwa kwenye jiji hili , tutaanzia pale kwako si kuna camera kwenye lile jengo ?”
“ ndio zipo “
“ basi tuelekee huko tukacheki “ aliongea sabi na kisha aliingia na kujiandaa haraka haraka na kisha walitoka na kuelekea sukhumviti soi , dakika kadhaa walikuwa tayari nje ya Emsqure shopping mall , walikata kushoto na kuja kuingia kwenye geti la apartment hizi .
Walienda kwa mlinzi wa apartment na kisha walieleza shida yao , japo waliulizwa maswali mengi lakini mwishowe walikubaliwa kuangalia zile camera , ubaya ni kwamba hakukuwa na camera za ndani ya chumba cha damiani , kiufupi vyumba vyote hakukuwa na utaratibu wa ufunga camera ila nje ya chumba zilikuwepo , waliangalia na kweli walimshuhudia mrembo huyo akitoka na kuingia kwenye lift na kitoka kabisa nje .
“namjua huyu dada “ aliongea mtaalamu yule wa camera na kuwafanya sabi na damiani wamwangalie .
“ unamjuaje ??”
“ anafikaga hapa mara kwa mara , na anasemaga ana ndugu yake “ aliongea mlinzi yule mwenye kofia na mavazi yake ya kiulinzi , na alikuwa akiongea kingereza vizuri .
“ unaweza kukumbuka siku mara ya mwisho aliokuja ?”.
“ jana alikuja” aliongea mlinzi na hapo aliwafanya washangae .
“ alikuja saa ngapi ?”
“ alikuja kwenye saa kumi na moja hivi alipaki gari yake hapo nje ya geti na akaingia “ aliongea mlinzi na sabi aliomba kuonyeshwa camera za nje na kweli walimshuhudia akishuka kwenye gari aina ya nissani Almera , sabi alichukua namba zile na kuzinakili kwenye simu yake kisha aliomba aonyeshwe camera za ndani , walionyeshwa camera za ndani na hapo ndipo walipo pigwa na mshangaoo kwani yule dada alionekana akifungua chumba alichokuwa akiishi damiani na alitumia madakika kadhaa ndani ya chumba hicho na kutoka , huku akiwa amejifunika kichwa , wakati anatoka , na damiani alionekana kuingia kwenye jengo hilo na walipishana kwenye lift, kwenye floor ya chini kabisa kwani damiani wakati anasubiria kuingia kwenye lift hio na mwanadada huyo alikuwa akitoka kwenye lift hio ila kwa damiani hakumwangalia .
“ inaonekana alikuwa anakufatilia kwa muda mrefu , na kama alikuwa akija hapa mara kwa mara basi kuna kitu alikuwa akitafuta “ aliongea sabi na muda huo walikuwa washatoka kwenye chumba cha camera na kuingia ndani kwenye chumba cha damiani .
“ na anaonekana ni mtaalamu katika kazi yake “ aliongezea damiani .
“ inawezekana , maana kama alikuwa anaingia na kupekuwa na siku zote hujui kama kuna mtu anaingia kwenye chumba chako basi anaonekana ni mtaalamu , lakini pia huenda na wewe haupo makini na chumba chako maana huna mafunzo ya kijasusi .”.
“ daah !wamekuja mpaka huku “ aliongea damiani huku akioneakana alikuwa na wasiwasi .
“ wakina nani ??”.
“ ni stori ndefu sana ,ila kwasasa naamini atarudi kwani kitu alichochukua huenda hakitamsaidia , kwani wanachokitafuta nakijua na uzuri ni kwamba nilikificha sehemu salama kabisa “.
“ najua huniamini bado , ila hata mimi ninahistoria yangu yakuumiza , ila kwakuwa swala hili linakugusa sana , niambie hata kama ni stori ndefu na hapo ndio nitajua jinsi yakukusaidia “ aliongea sabi na kumfanya damiani amwangalie sabi usoni , na damiani hakuwa na jinsi na hapo ndipoalipo anza kumwambia historia nzima ya maisha yake kuanzia mama yake kufa kifo cha kikatili mpaka kufikia siku anafika thailland , ilikuwa ni simulizi iliomsisimua sana sabi .
“Aisee damiani pole sana , umepitia magumu mengi , na pia hongera sana kwa kufikia hapa , nimekuzidi umri lakini unaonekana umexperience magumu kuliko mimi , lakini kuna sababu ya sisi kukutana , kwa sababu umeniamini na kuniambia historia yako ngoja na mimi nikusimulie yakwangu “ aliongea sabi na kuanza kumsimulia mwanzo hadi mwisho na kumfanya damiani na yeye swala hilo limshangaze sana , na kilichomshangaza ni namna wote walivyoingia ndani ya nchi hio .
“ lakini mpaka sasa kinachonisumbua kichwa na mtihani baba alionipa , ni kwamba wakati naingia ndani ya hii nchi nilidhani nakuja kukutana na mtu , lakini nilishangaa nilipelekwa kwenye camp ya mafunzo ya ngumi , na nilipowauliza kuhusu mtu alienileta hapa walikuwa hawanielewi Zaidi ya kuambiwa walipokea usajili wangu tu” .
“ hata mimi pia waliniambia swala kama hilo hilo , na siku nyingi natamani kumjua mtu alienileta mahali hapa , lakini niliona kuna sababu ya kuletwa kwenye chuo cha mapigano ‘ aliongea damiani .
“ stori yako na yangu zinafanana kabisa na ndio maana nasema kuna sababu kubwa ya sisi kuwepo ndani ya nchi hii na kukutana , ninaweza kusema mpaka sasa tuna adui wa aina moja , na kama nilivyo sema, ile flash tukiipata inaweza kutupelekea kujua ukweli au kupata pakuanzia , kwani naamini inayo taarifa , maana nazijua sana zile flash ni za kijasusi na kuna namna ya ku extract taarfa zake . aliongea sabi .
“TUKO PAMOJA BRO “ . aliongea damiani na wakapeana mikono na kukubaliana waanze msako wa kumkamata mrembo wa kithai usisahau hapo kwamba ni miezi minne ya damiani kuwa ndani ya Bangkok na sabi miezi yake saba ya kuwa ndani ya jjiji hilo .
SEHEMU YA 28
Siku ambayo damiani aliibiwa flash ile ilikuwa ni siku ya jumamosi kwenda jumapili , na uzuri ni kwamba siku hio hakuwa na ratiba za kwenda camp , baada ya sabi na damiani kukubaliana , sabi hakutaka kubaki hapo kwa damiani , moja kwa moja alitoka na kuelekea kwenye apartment yake victory monument , hii ni sehemu moja ambayo ilikuwa ipo kimya sana , na kwa wenyeji waliokuwa wakiishi maeneno hayo hawakuwa kabisa na kero na mtu , kila mtu alikuwa na mambo yake , hakuna aliekuwa akimfatilia mwenzake , haikuwa sehemu ya kitajiri sana kama kule alikokuwa akiishi damiani , sehemu hio walikuwa wakiishi watu wa kawaida yaani nikimaanisha wenye kipato cha kawaida , basi dakika kumi tayari sabi alifika kwake ,aliingia mpaka kwenye chumba chake hicho na kisha alijibwaga chini .
“ kuna sababu kubwa ya mimi kukutana na damiani ndani ya jiji hili , japo mwanzoni nilimhofia kwa kutokumuamini lakini historia yake imenigusa sana , kifo cha baba kilikuwa ni cha kikatili sana na hakika watu waliohusika watakuwa ni watu wazito sana , kwani sumu iliomuua baba ni sumu ambazo hazipatikani kwa mtu wa kawaida , naamini baba kuna jambo alikuwa akilijua au huwenda aliingia katika vita na hawa watu , lakini kwa kulinganisha historia ya damiani na yangu , zinalingana kabisa , naamini kwa kumtumia damiani nitajua vitu vingi hususani waliohusika na kifo cha baba yangu , kuna ulazima wa kuipata ile flash , lakini je yule mwanamke ni nani inaonekana alikuwa akimfatilia sana damiani kwa muda mrefu kama ni kweli basi inapaswa kuwa makini “ alijifikiria wakati huo akiwa ameangalia huu ya ceiling board .
Huku upande wa damiani na yeye alikuwa kwenye mawazo mengi , alikuwa amejilaza lakini muda wote alikuwa na waswasi , swala la mwanamke kuingia kwenye chumba chake na kumkagua pasipo yeye kujua lilikuwa ni swala la hatari sana .
“ nilifanya akili kubwa wa kutohifadhi zile document kwenye hii apartment , kama nisinge pata wazo la kuzipeleka benki , huenda sasa ingekuwa shida kwangu , na ningepoteza muongozo wote ambao ungeniwezesha kuwajua wabaya wangu lakini naamini atarudi kwani najua wanachokihitaji sio flash bali ni nyaraka ambazo hawajazipata bado , ningekuwa makini swala hili lisingefikia hapa , lakini huu ni mwanzo mzuri na ni bahati kwani nishajua watu hawa washanifata mpaka huku , nilikuwa simwamini sabi , lakini sasa kwa historia yake nadhani anafaa kabisa kuwa partner “ aliwaza damiani na yeye huku akiwa amejilaza , alikuwa pia akijilaumu kwa kulaghaiwa na kunywa pombe , aliona anapaswa kuwa makini kwanzia muda huo kwani aliamini kabisa watu aliokuwa akishindana nao ni watu hatari na wenye mikono mirefu .
****
Ilikkuwa ni muda wa saa moja kwa saa za thailland , ndio muda ambao sabii walitoka hapo kwa ajili ya kuanza upelelezi , siku hio sabi alikuja na gari aina ya ISUZU D MAX ambayo ni aina ya pickup nyekundu .
“ hii gari umeipatia wapi ?” aliuliza damiani na kumfanya sabi atabasamu ‘ ‘ kuna rafiki yangu mmoja amenisaidia kwa leo , nilimwambia nina kazi ngumu leo akanipatia “ aliongea .
“ umefanya poa itaturahisishia , sasa tunaanzia wapi maana sielewi kabisa ramani inaendaje “ aliongea damiani maana ni kweli kwakuwa hakuwa na mafunzo yoyote ya kiupelelezi hakuelewa .
“ usiwaze upo na mpelelezi , nishapata location ya ile nissani almera ilipo kwa kutumia namba zake .
“ iko wapi ?”.
“ phra nakhon district , sijawahi kufika ila kwakutumia ramani kwenye hii tablet naamini tutafika “ aliongea huku akimpatia tablet ile .
“ hio sehemu yenye kidot chekundu ndio tutaipata “ aliongea sabi huku akiwa makini na usukani , walipita road 7 , na hio sehemu ilikuwa na umbali wa masaa mawili kuendesha kwa gari , walipita pataya city , wakapita chori bur beach wakakunja kushoto baada ya masaa mawili walikuwa ndani ya wilaya hii .
Ilikuwa ni moja ya wilaya ambazo zilikuwa zikitembelewa sana na watalii kwani kulikuwa na moja ya kivutio maarufu sana kilichokuwa kikijulikana kwa jina la ‘GIANT SWING’ , majengo yake katika hili eneo ni ya kizamani zamani , ni majengo ambayo kwa bongo huwezi ya kuta , lakini ni moja ya majengo imara sana .
Waliendesha gari kwa kuelekezwa na ile ramani , muda huo ni giza na mwanga wa makazi ya watu na taa za barabarani ndio zilizokuwa zikiwaongoza , wakati wanaikaribia sehemu ambayo gari ile ilikuwepo , gari ile ilikuwa inakuja upande wao kwani kidoti kile kilionekana kikisogea .
“ anakuja upande wetu ngoja tusimamishe gari kwanza “ aliongea sabi na kusimisha gari kando , na kweli ndani ya dakika tano waliona ile gari , waligeuza gari harakaharaka na kuanza kuifatilia , hawakuweza kuona aliekuwepo ndani ya gari maana kulikuwa na giza , waliungia kwa nyuma gari ile uzuri ni kwamba hawakuwa na wasiwasi kwani walikuwa na ramani iliokuwa ikiwaonesha sehemu ilipo na hata haikueleweka walikuwa wakitumia technolojia gani kuifatilia .
Walifatilia kwa muda mrefu sana gari ile na lisaa limoja mbele ilikuja kusimama ndani ya club ya pataya , ni moja ya club hot sana ndani ya jiji hili kwa wale ambao washawahi kutembelea , sabi alsimamisha gari yake karibu kabisa na gari na mwanamke mmoja mrembo wakithai alishuka huku akiwa ameongozana na mwanamme mwingine , huyu hakuwa yule ambae walikuwa wakimtafuta , waliwaangalia mpaka wakiingia club, na walivyo ona wametokomea ndani na wao walishuka na kuingia ndani ya club hio .
Damiani aliishia kujisemea tu kuwa jiji hili watu wanakula bata maana idadi ya watu waliokuwepo humo ndani na shughuli iliokuwa ikifanyika , hao watu ni hakika huwezi waambia kama kuna mungu na wakakuamini ,lakini pia asilimia kubwa ya wathailland hawaamini kuna mungu kama ilivyokuwa kwa wakristo na waislamu kwani asilimia kubwa wanasalia budha .
Basi sabi waliingia ndani ya club ile huku wakiangalia upande wa wale watu walikopitia , waliwaona kwa mbele upande wa kulia wakiwa wamezungukwa na wanawake wengine .
“ sikia hapa inabidi tujigawe , wewe utakaa upande ule wa kushoto na mimi upande huu , agiza hata pepsi uzuge nayo “ aliongea sabi na wakagawana huku wakiwa wanawasiliana kwa meseji , huku shauku yao kubwa ilikuwa ni kumpata yule mrembo , walitumia Zaidi ya lisaa limoja kuwafatilia wale watu mpaka muda ambao wanatoka waliwaona na walipeana ishara wawafate , waliingia kwenye gari a safari ikaanza muda huu hawakuelekea tena walikotoka bali walichukua road 8 na damiani na wao wakawafatilia kiakili wasijue kuwa wanafatiliwa .
Kilichowashangaza ni kwamba walienda kusimamisha mita kadhaa karibu kabisa na apartment ya vision aliokuwa akiishi damiani katika eneo la sukhumvit soi hii apartrment ilikuwa ikijulikana kwa jina la ASPIRE ni moja a apartment za bei ghali , na pia ulinzi wake ulikuwa ni wa hali ya juu yaani huwezi ingia getini bila ruhusa ya mwenyeji .
Walisimamisha gari pembeni kabisa na lango la kuingilia huku wakikaa hapo na baada kama ya dakika kumi na tano kulitoka gari nyingine , ilikuwa gari moja nyeusi roll royce black badge cullinan , ni moja ya ghari za kifahari sana ndani ya thailland .
Kuna kitu sabi alikigundua kwenye ile gari lakini hana uhakika nacho ,
“ unajua kuendesha gari ?” aliuliza sabi
“ ndio nikofit “
“ shika usukani fuatilia hio gari mimi niangalie utaratibu wa kuingia kwenye hili jengo bila kushitukiwa “ aliongea sab na wakaachana huku damiani akianza kufatilia ile gari kwa nyuma , ilikuwa imemiacha mbele kidogo lakini alikuwa anaiona , na kwakuwa muda ulikuwa umeenda gari hazikuwa nyingi barabarani basi hakupata shida .
Gari ilikuwa ikiendeshwa kwa speed kweli na hata damiani na yeye alihakikisha gari ile haimuaichi kwa namna yoyote ile , uzuri ni kwamba gari ile ilikuwa ikielekea upande waliokuwa wameenda mwanzoni phra nakhon , baada ya masaa kama mawili ya kufatilia gari ile ilikunja kushoto na kuingia sehemu moja palikuwa pakiitwa suangluang rama IX ni sehemu moja kulikuwa na kajimsitu lakini kulikuwa na majumba ya kifahari yaliokuwa yamejengwa katika eneo hilo , gari ile ilisimamishwa na akashuka mwanamke na kwakupita mwanga hafifu wa baadhi ya taa za majumba yale aliweza kumjua , alikuwa yule msichana , alishuka haraka haraka , lakini ile anafungua mlango kuna jambo alihisi kwa nyuma yake na hio ni kutokana na mafunzo ya hisia aliokuwa amejifunza , alijifanya kama mtu anaefungua mlango kama mtu asiekuwa na umakini lakini haikuwa hivo kwani ile anafungua mlango alijirusha na kuchia teke moja la round na kama vile alitegemea kwani alijikuta akipiga mtu mtama na mtu yule alionekana mwepesi kwani alidondoka lakinni aliruka na kusimama tena , alikuwa jamaa mmoja mwenye mwili mkubwa hivi wa kimazoezi aliekuwa amevalia tisheti nyeupe , jamaa aalikuwa akirusha ngumi mfululizo na kumfanya damiani atabasamu kwani aligundua jamaa alikuwa akirusha ngumi pasipo kuwa makini na mwili wake na hilo likawa kosa kwani hakujisumbua alikwepa kila pigo na jamaa na yeye aliendelea kurusha na damiani alivyo ona mwenzake ashachoka alianza kurudisha mapigo , jamaa na yeye hakuwa haba kwenye kuyapangua lakini alianza kuzidiwa kwani damiani alianza kumpiga maeneo nyeti kama shingoni na kwenye viwiko vya mkono halafu akamlamba mtama jamaa alitua kama gunia na damiani hakutaka kumpa nafasi ya kunyanyuka alimpiga fly kick ilimgonga shingoni na jamaa yule akaenda chini na kuzima .
Na hapo akasikia makofi yakipigwa kwa nyuma yake kama mtu aliekuwa akimpongeza , alikuwa ni yule mwanadada aliekuwa amelala nae usiku wa jana .
Damini hasira zilimpanda na kumfata na muda huo huyu dada alikuuwa amevalia suruali ya jeans na viatu vya high heals , ulikuwa ni moto yule mrembo alikuwa ni mtaalamu maana alikuwa amesimama eneo moja hasogei na aliweza kupangua kila pigo lililokuwa likirushwa na damiani , kiufupi ni kama alikuwa akicheza na mtoto , damiani alijikuta akipatwa na hasira Zaidi na kuleta aina nyingine ya kimapigano , jambo ambalo mrembo yule alitabasamu na muda huu alishindwa kusimama kama alivyo kuwa amesimama mwanzo kwani mapigo aliokuwa akiletewa sio ya kitoto , alisogea hatua moja nyuma na damiani akarusha roundhouse kick iliomfanya mrembo yule ainame mpaka mikono kushika chini kwa nyuma na damiani hakufanya ajizi , alirusha sweep round kick , lakini ni kama aliotewa kwani yule mrembo aliruka sarakasi aina ya acrobatic flip na kutua kwa nyuma , lakini awamu hii aliona anazidiwa hapo ndipo alipo anza na yeye kuleta mashambulizi kwa damiani , damiani alijitahidi kupangua na alizidiwa kwani aligundua bidada huyo mapaigo yake sio ya kithai thai , hakujua ni aina gani ya mapigano lakini aligundua anapigana na mtu wa level ambayo sio yake .
Dakika mbili nyingi damiani alipigwa teke la mbavu akajikunja kidogo akaguswa shingoni na akaenda chini mzima mzima .
Upande wa sabi aliweza kuingia ndani ya jengo lile , lakini aliishia kukata tamaa mara baada kuingia ndani ya lile jengo kwani lilikuwa na vyumba vingi na ilikuwa ni ngumu kujua watu wale walienda chumba gani , alichokifanya alirudi mpaka kwenye maegesho ya magari na aliiona ile nissani almera na kisha aliisogelea na alitoa kitu kama sindano huku akiwa amechuchumaa na akachokonoa mlango na kisha ukafunguka na alizama ndani ya gari hilo siti za nyuma na kutulia .
SEHEMU YA 29
Ni baada ya masaa mawili ya damiani kuzimishwa na mrembo wa kithai , ndani ya masaa hayo ndio fahamu zilimrejea huku akihisi maumivu makali ya kichwa , alifungua macho huku akijaribu kupepesa kulia na kushoto ili kupata kujua sehemu aliopo maana alikuwa akikumbuka vyema tukio lililomtokea saa chache nyuma .
Kilikuwa ni chumba chenye kitanda cha chuma , chumba ambacho kilikuwa na dirisha moja dogo upande wa juu sana lakini pia kilikuwa na feni ambayo kwa wakati huo linazunguka , damiani alijaribu kuvuta mikono yake , lahaulah ! hapo ndipo alipojua kuwa alikuwa amefungwa mikono yake kwa pingu ,alijaribu kuvuta miguu lakini pia alijua miguu nayo ilikuwa imefungwa kisawa sawa na kwa mantiki hio aligundua kuwa sehemu aliokuwepo sio salama kwake na ni swala la muda tu kwa mtu aliemfunga hapo kurudi .
Alijaribu kujinasua kwa kuvuta mikono na miguu , lakini haikuwezekana , kiufupi kitanda kile kilikuwa ni kizito mno na aliemfunga alikuwa kamfunga kitaalamu , alijitahidi kadri ya uwezo wake lakini alishindwa , muda huo kwa makadirio ya haraka ilikuwa imetimu saa tisa kwenda kumi usiku .
Taa ya mwanga hafifu iliokuwa ikikimulika chumba hicho ilionesha dhahiri kuwa wakati huo kulikuwa ni giza nje , damiani alijitahidi kujivuta lakini hakukuwa na matumaini ya kujiokoa katika eneo hilo .
Alijikuta akijikatia Tamaa huku mawazo ya mwanadada yule yakimrejea , alikumbuka wakati akipigana nae .
" Yule sio mtu wa kawaida kabisa , ana mapigo ya hali ya juu , ni mwanamke lakini nisingefua dafu mbele yake ,anaonekana kunizidi vitu vingi katika swala la mapigano , huyu mwanadada ni nani kanifahamu vipi? "
Yote hayo yalikuwa ni baadhi tu ya mawazo yaliokuwa yakizunguka katika kichwa cha kijana damiani , hakuwa na jinsi tena aliemfunga kamfunga vyema na hakuwa na uwezo tena wakujifungua ili ajiokoe , nafasi aliokuwa nayo kwa muda huo ilikuwa ni moja tu yaani kusubiri .
Lisaa la kwanza likapita , la pili mpaka matatu yote ya damiani kusubiri , ila hakukuwa na mtu alieingia , muda huo alifahamu fika nje kushapambazuka kwani mwanga hafifu kupitia chumba kile uliingia na kumulika ukutani .
Nusu saa mbele mlango wa chumba kile ulifunguliwa , damiani macho yote yalikuwa mlangoni kutaka kushuhudia ni nani aliekuwa akiingia eneo
hilo ,hakuwa mwingine alikuwa ni yule mrembo wa kithai huku awamu hii akiwa ameshikiria bilauli mkononi iliokuwa ikionekana na kilevi .
Alisogea mpaka kwenye kijimeza kilichopo humo ndani na kukalia na kufanya mapaja yake yote yalio nona kuonekana wazi huku kijigauni kikipanda juu , mwanadada huyu alionekana kutokuwa kabisa na waswasi , kwani alimuangakia damiani na kisha akatabasamu na ni kama ni mtu aliekuwa akimtega .
" Niambie Damiani handsome boy kutoka Tanzania , naona uko kwenye mshangao " .aliongea kwa mapozi , lakini kwa damiani ilikuwa si kitu .
" Wewe ni nani??"..
" your one night stand remember ," mwanamke ulie lala nae usiku wa juzi kumbuka vizuri " .
" I am asking , who are you ?(Nauliza wewe ni nani una nifahamu vipi ?..)
" you don’t have to panic damianni you will know me slowly but for now you can call me marie ( Huna haja ya kupaniki damiani utanifahamu taratibu , ila kwa sasa unaweza niita Maria au chae charoen (thai name))” ".
********
MWAKA MMOJA NYUMA .
OSLO INTERNATIONAL AIRPORT -NORWAY
Ilikiwa ni kipindi cha kati ya mwezi wa kumi kwenda wa kumi na moja mwishoni mwaka 2018 ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa ilitua ndege ya shirika la etihad , iliokuwa ikitokea jijini lagos nigeria , baada kama ya nusu saa katika mlango wa kutokea , alionekana bwana mmoja mrefu saizi ya kati mwenye umri kimakadirio kati ya miaka 35 kwenda 40 hivi aliekuwa amevalia suti nyeusi ilio mkaa vyema mwilini , alikuwa ni mwafrika huyu bwana , baada ya kutoka kabisa nje ya jengo hilo la terminal huku mkononi akiwa ameshikilia kijibegi kidogo cheusi mfano wa briefcase lakini haikuwa briefcase , basi jamaa huyu aliingia ndani ya moja ya Taksi zilizokuwepo hapo uwanjani .
" where are you going mister (Wapi mister) " aliuliza jamaa mmoja wa kizungu kwa lugha ya kingereza
" continental hotel " aliongea na gari hapo hapo iliwashwa na kuondoka , kutoka airport kwenda kwenye hii hotel ni sehemu ya dakika kama arobaini hivi , ila itategema unatumia usafiri gani , maana ndani ya jiji hili usafiri haukuwa shida , kulikuwa na train za umeme , buses kama za mwendo kasi , taksi , pia magari ya kukodi yanapatikana hapo hapo airport .
Basi ndani ya madakika kadhaa gari ile ilikuja kusimama nje kabisa ya hoteli hio kubwa ya nyota tano , bwana yule alitoa noti ya dollar mia na ya dollar hamsini kulipia usafiri yaani jumla ilikuwa ni dollar 150 ukizileta kitanzania si chini ya laki tatu , unaweza shangaa lakini wenzetu wameendelea sana ndani ya jiji hili kila kitu kinauzwa kwa bei ya juu lakini kwao ni bei ya kawaida kutokana na hali halisi ya uchumi wao .
Basi bwana huyu baada ya kuingia ndani ya hoteli hii , muda huo ilikuwa ni kama saa kumi hivi jioni kwenda kumi na moja , alienda mpaka mapokezi na kisha aliongea shida yake .
"I am going to room number 150 ( Naelekea chumba namba 150) " Aliongea huku akimuangalia mwanadada huyo wa kizungu .
" Do you have appointment ( je unayo miadi naye ?)"
"yes you cana just make a call and tell him its Samuel saitoto ( Ndio unaweza kupiga simu , jina samueli Saitoto " aliongea bwana huyu na hapo ndipo tunamjua huyu ni sam ( Rich sam ) .
Mwadada yule alipiga simu na sekunde chache tu alimruhusu sam nakuondoka eneo hilo na kuingia kwenye lift , sekunde chache alikuwa ndani ya floor namba 11 alitembea kwenye vyumba hivi huku akiangalia namba zilizobandikwa mlangoni , ilikuwa ni moja ya hoteli nzuri sana ya kimataifa ilikuwa ikivutia sana .
Hatimae alikifikia chumba hichi na kisha aligonga mlango na kufunguliwa na mzungu mmoja mwenye kipara , lakini pia umri wake ulionekana umeenda kama sio miaka 60 basi ni kwenda 70 hakuwa na utofauti na raisi wa marekani Biden .
" Karibu sana sam " aliongea yule mzungu , wakati huo alikuwa amevalia nguo za kulalia rangi nyeupe , chumba kilikuwa chumba kweli , kilikuwa na kila kitu ndani , masofa tv na mengine mengi ya kivutia na kukifanya kiitwe VIP room.
" Nashukuru sana mister charles .."
" how long have you been since you moved to USA (una muda gani tokea utoke nyumbani nakuhamia USA ??) " .
"four to five years now ( nina miaka minne kwenda mitano sasa) " .
" okey I think you have been given practical instruction in lagos (okey nadhani , umepewa maelekezo yakinifu , nchini Lagos) " .
" yes " aliongea huku akiifungua kile kijibegi alichokuwa ameshikilia mkononi na kutoa baadhi ya karatasi na kumkabidhi yule mzungu , alizifungua na kisha aliziangalia , na akamuomba karamu sam na akatoa na kumkabidhi mister charles na alionekana kusaini karatasi zile .
" congratulation mister samueli saitoto now you are the owner of all asset of bruno lamberk this agreement will be valid when bruno dies , I also congratulate you for being leading member of U-97 in Tanzania ( sasa wewe ni mmiliki wa mali zote za bruno lamberk , mkataba huu utakuwa valid pale bruno atakapo fariki , piki nakupongeza kwa kuwa mwanachama kiongozi wa U-97 ndani ya Taifa la Tanzania ." aliongea huku akinyanyuka na kuendea begi dogo la plastic na kulifungua na kutoa picha .
"after one year starting today count twelve months forward , then it will be time for you to return Tanzania about other instructions you will be notified , the person in the picture you should look for him as soon as you arrives , the rest you will do at your own will.( Baada ya mwaka huu kupita , nikimaanisha kwanzia siku hii ya leo uhesabu miezi kumi na mbili ndio unatakiwa kurejea Nchini Tanzania , utaratibu mwingine utapewa , mtu wa kwenye hio picha unatakiwa kumtafuta mara baada ya kuingia Tanzania , mengine utayafanya kwa utashi wako " akaongea halafu akanyanyuka tena na kutoa picha ya bruno lamberk .
"that person its your first mission when you get there , I know you know what you are supposed to do (hio ndio kazi yako ya kwanza kufanya ukiingja ndani Ya tanzania , najua unafahamu cha kufanya " aliongea mzungu jwa msisitizo huku akiwa siriasi na sam aliitika kwa kichwa kuwa anajua) .
" Then you are good to go " .
Basi baada ya sam kutoka hapo alirudi nchini marekani ambako ndio familia yake ilipo , alianza kuhesabu miezi kumi na mbili kwanzia siku hio na ndani ya mwezi wa kumi na moja ukienda wa kumi na mbili ndipo alipo pata taarifa za kifo cha bendera raisi wa Tanzania , alishangazwa sana na taarifa ile , hata kwa familia yake pia , baada ya siku kadhaa baada ya taarifa ndio aloingia nchini rasmi huku siku alio ingia nchini akipokea maagizo mengine kutoka nchini Nigeria makao makuu ya U-97 ndani ya Afrika .
Baada ya kufika nchini hapo alimtafuta raisi athumani ndalu na waka ahidiana kukutana ndani ya siku hizo , baada ya kukutana ndio siku aliokutanishwa na raisi Henry , raisi ambaye aliapishwa siku kadhaa kuwa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania , alitambulishwa kwake kama mwanachama aliejiunga miaka mitatu iliopita kwenye U-97 , lakini hakuwa huyo tu kulikuwepo pia na waziri wa mambo ya ndani bwana musiba na yeye pia alitambulishwa kama mwanachama mwingine ambae na yeye alikuwa na miaka miwili ya uanachama ndani ya U-97 .
Hivyo sam akatambulishwa kama mkuu wa U-97 mpya nchini akichukua nafasi ya bruno , baada ya sam kutambulishwa rasmi , ndio swala la kumuua bruno likawekwa mezani na watu wanne , yaani sam , raisi mstaafu Ndalu , musiba (waziri wa mambo ya ndani) na Raisi henry wakalijadili jinsi ya kulitekeleza .
katika kikao hiko hitimisho likawa ni jina la Kimbona kuingizwa katika umoja huo yaani U-97 huku wakidhamilia kumtumia kimbona kwa ajili ya kumuua bruno na kuhakikisha mali zote za bruno zinarudi kwenye mikono ya U-97 .
****** kitendo cha kimbona kushindwa kumpata Damiani ikawa mwiba mkali kwa sam yeye kama kiongozi wa U-97 , sam anamlazimisha kimbona kujua ni mahari gani Damiani alipo kwa uwezo wake wote , kimbona swala hilo linamuumiza kichwa sana na ndipo anaomba ushauri kwa raisi henry , Raisi henry anampa ushauri kimbona kumtafuta mpelelezi wa kimataifa ambae anaweza akaifanya hio kazi , huku akimpa mapendekezo ya kazi hio kumpa komandoo jasusi aliefahamika kwa jina la agent Z (kumbuka huyu ndie moja ya wanausalama waliokuwa chini ya bendera , lakini pia huyu ahent Z ndio ambae anaenda kupewa kazi ya kumtafuta Damiani , kazi anayopewa na mkuu wa TISS mstaafu matinde huku mfadhili akiwa ni mfanya biashara mwanadada Merina ).
basi kwa msaada wa raisi kimbona anafanikiwa kumpata zakayo( agent Z) mwanamitindo maarufu Tanzania , wakati huo huyu bwana alikuwa ni moja ya watu maarufu Tanzania na alikuwa ni moja ya wanamitindo waliokuwa na mafanikio sana na alikuwa akimvalisha moja ya msanii mkubwa nchini .
kimbona anafika ndani ya kampuni ya Z - styllish wear iliokuwa ikipatikana mlimani city anafika ofisini hapo na anaomba kuonana na zakayo mkurugenzi na mtendaji wa Z styllish wear ..
kimbona kwakuwa na yeye alikuwa mfanya biashara mkubwa tu haikuwa shida kwake kuonana na bwana huyu , zakayo alikuwa ni kijana mwenye mwili wa kawaida wa mazoezi mrefu maji ya kunde , alikuwa ni Handsome kweli , na mtanashati haswa hakuna mtu ambae anaweza kudhania kuwa bwana huyo alikuwa akifanya kazi ya usalama wa taifa chini ya TISS undercover agent .
SEHEMU YA 28
Basi baada ya kimbona kuonana na zakayo alitoa karatasi iliokuwa ikionesha utambulisho wa kimbona lakini pia karatasi hio ilikuwa imesainiwa na raisi huku ikiwa imeambatana na barua yake ya kumsaodia kimbona .
Baada ya zakayo kusoma barua hio alimwangalia kimbona na kisha alivuta pumzi na kumtaka aseme shida yake , na kimbona hakutaka kuzunguka alitoa picha na kisha kumkabidhi zakayo .
" nahitaji kujua huyo kijana alipo ".
" na baada ya kujua alipo " .
" kazi yako itaishia hapo , na malipo yako yataingia kwenye akaunti .' .
Zakayo alijifikiria kwa muda na kisha alikubaliana na kazi hio huku malipo nusu kiasi cha milioni kumi kiliingizwa kwenye akaunti yake , huku zakayo akimpa siku kumi kazi hio kukamilika .
Baada ya kimbona kumaliza kumpa kazi hio sam , alipokea simu kutoka kwa sam ikitaka kumpa feedback ya maendeleo ya kazi na hapo ndipo alipo muambia mpango uliopo .
" sasa hio kazi baada ya kukamilika , namaanisha akijua sehemu huyo damiani alipo nitaendelea mimi mwenyewe kufatilia na kumkamata " aliongea sam na kimbona alikubakiana nae .
Siku kumi mbeleni zakayo alikuwa na ripoti kamili , ripoti ya hatua kila hatua ya damiani alikopitia kwanzia Tanga , balozi ya kenya mpaka alipo ondoka nchini kuelekea Thailland , ripoti hio ilikuwa ya kushangaza kwa kimbona , lakini pia hata ilipo mfikia sam alishangazwa na ripoti hio , moja kwa moja waliamini kwamba damiani alikuwa na mtu aliekuwa akimpa sapoti , kwani ni ngumu kwa damiani kufahamiania na balozi wa kenya tena kwa muda mfupi .
" sasa kimbona mpaka hapa kazi yako ishaisha , palipo baki nitaendelea mimi mwenyewe , lakini pia kama ulivyo ona kwamba kuna uwezekano wa damiani kuwa na mtu anaemsaidia hivyo swala hili liwe siri kwanza baina yetu , mheshimiwa akikuuliza mwambie uchunguzi haujakamilika bado na hata kwa zakayo mpe taarifa mapema " aliongea sam na akakubaliana na kimbona .
siku chache sam tokea apate taarifa ya Damiani kuwa nchini thailland , siku hio akiwa ofusini kwake mikocheni ndio ikaingia Email ..
Marie Alberto CIA agent in Thailland contact info .. ******* Give her the mission " ilikuwa ndio email hio .
Na sam l hakuchekewa kwa kutumia mawasiliano aliopewa aliwasiliana na Marie na alimpata na kumpa misheni ya kumtafuta Damiani.
" And if I find him what follows (Baada ya kumpata natakiwa kufanyaje ?? )".
" make shure he gives you the documents then kill him (hakikisha anakupa nyaraka kisha unaweza kumuua , usimuache akaishi )" hio ndio misheni aliopewa Maria huku akipewa majina kamili ya damiani .
*****
Basi tukirudi nchini Thailland damiani alikuwa akimwangalia mwanadada maria kwa hasira kali mno hakujua wakati huo ni kipi akifanye kwani ashajua mwanadada huyo hakuwa na nia nzuri kwake .
" marie what do you want from me and why you have been following me (Maria unataka nini kwangu , na kwanini unanifatilia ?" .
" I think you know what I want up to this point ( Ninachokitaka kutoka kwako nadhani unakijua mpaka sasa ) ".
" I don’t know just tell me what you want from me and who sent you ( sijui niambie unachotaka kutoka kwangu na nani kakutuma ?)".
" I have been following you for long until now , its three month now and today I want to end my mission by taking the document you have (Nimekufatikia kwa muda mrefu sana ni miezi mitatu sasa , na leo nataka nihitimishe kazo yangubya kukufatilia , nahitaji nyaraka ukizo nazo) ".
" I don’t have any document , and even if I do I would not be able to give someone like you prostitute (Sina nyaraka mimi , nahata ningekuwa nazo nitakupaje malaya kama wewe) " .
" ahahaha,.. ah .. ahahaha I think you got wrong about me damiani , sleeping with you doesn1t give you credibility to call me a prostitute , but I will forgive you , your were amaizing how you *****d me , so here I don’t give a *** just tell me where is document I need (hahahahaha... ah. ahaha..ahahahaha , nadhani hujanijua vizuri damiani , kukupa mwili wangu sio kigezo cha wewe kuniita malaya , nitakusamehe kwa hilo maana ulijua kunifikisha ninapotaka siku ya juzi , hivyo naomba unipe nyaraka ulizo nazo tuachane kabisa ".
" I already told you , I don’t have the documents you prostitute , and if there is something you wish to do just go ahead but know this , you and those who sent you there is nothing you can get from me .(Nishakwambia sina nyaraka wewe kahaba na kama kuna kitu unapanga kufanya fanya utakalo ila unachokitaka kutoka kwangu na hao waliokutuma jueni hamtaoata kitu hapa ".
" damiani do you think talking with the same girl you fucked now I am at work not doing pet talk with you I need documents and about you life I will reconsider Damiani hivi unadhani unaeongea nae leo ni yuke uliekuwa ukimto**ba juzi , now nipo kazini sipo hapa kwa ajili ya kujadiliana na wewe , nahitaji nyaraka kuhusu maisha yako naweza kukufikiria "
" kama una nyege kwaninj usinifungulie nikakutoa hamj zako zote , kuliko kujihangaisha na kitu ambacho hutopata " aliongea damiani kwa dharau na kumfanya maria apandwe na hasira na kutoka nje ya hiko chumba na dakika kadhaa alirudi akiwa na kisu , huku mkononi akiwa na funguo za pingu aliziweka juu ya kimeza na kisha alivua gauni na kubakiwa na chupi , jambo hilo hata kwa damiani lilimshangaza lakini kwa maria hakuwa na wasiwasi , alivuta droo kwenye kile kimeza na kisha akatoa kikopo kama cha babycare ndogo , alikiweka juu ya kimeza na kisha alivua kile kijibikini , na kisha akachukua yale mafuta na kupaka mikononi na akaanza kumsogelea damiani ambae muda wote huo alikuwa akimshangaa , maria alivuta mkanda wa suruali alio vaa damiani na kisha alimvua suruali , mpaka boksa mpaka miguuni , kisha alishika mb*o na kuisiliba na yale mafuta , haikueleweka yalikuwa mafuta gani ila yalisababisha msisimko wa hali ya juu kwa damiani , msisimko ambao hakuwahi kuuhulisi katika maisha yake , mb* o ilisimama wima kama mshale , maria hakuwa akiongea alitoka kitandani na kusogelea yale mafuta na kuchukua mengine na kuanza kujiapka sehemu zake za siri .
na kisha alipanda tena kwenye kitanda na kusugua tena kwa mafuta yale mb** o ya damiani , kitu ambacho kilimfanya damiani atoe macho maana utamu alio kuwa akisikia ulikuwa wa aina yake ukizingatia ikikuwa mara yake ya kwanza kufanyiwa vile .
Baada ya kazi ile maria alikalia mb**o ya damiani na kisha akajilengesha kitu kilichomfanya afumbe macho kwa kusikilizia msisimko , kwa damiani nako alikuwa yupo ulimwengu mwingine na hio ni baada ya maria kutumbukiza naniliu yake ambayo ilimbana vyema na kusababisha msisimko zaidi , maria aliendelea kukata viuno huku akiwa amefumba macho akisikilizia utamu .
Ni kitendo kilichodumu kwa muda wa nusu saa hivi ndio maria akatoka katika mwili wa damiani , huku mb**o ya damiani ikiwa imesimama mpaka inauma , damiani alikuwa akitaka mlimbwende huyo aendelee na hakuelewa ni dawa gani aliokuwa amempaka kwani msisimuko ulikuwa wa hali ya juu .
" is it sweat ?umesikia utamu wee " aliongea maria huku akiwa na kile kisu mkononi .
"what do you want to do ( unataka kufanya nini?)" aliongea damiani kwa kubabaika .
" nimekupa utamu kwanza ili uone uchungu nikiikata hio mb**o yako kama hutoniambia ziko wapi nyaraka ninazo hitaji ambazo umepewa na bruno ".
" Aliongea merina na wakati huu tayari alikuwa ameishikilia mb** o ya damiani huku akiisugua kitendo ambacho kwa damiani kilizidi kumsisimua maradufu na akili yake haikueleweka ilikuwa inawaza nini muda huo alichokuwa akitaka ni mlimbwende huyo kumpa utamu tena .
" Arghhh... marie.aa nipe kwanza utamu nitakwambia zilipo ...asii tafadhari weka kisu chini " aliongea damiani kwa tabu sana maana alikuwa amezidiwa na hisia za kutaka kitumbua , maria alitabasamu kwani aliona kabisa zoezi lake lilikuwa likifanya kazi kikamilifu .
Marie na yeye kila akiangalia mkuyenge wa damiani , nyege zinampanda kwani na yeye alikosa uvumilivu na kujikuta awamu hii akiinuka na kuchukua funguo na kufunga kile chumba kwa ndani na kisha alisogelea zile za pingu na kuzichukua kisha akamfungulia Damiani .
Damiani baada ya kufunguliwa alikuwa kama nyati aliejeruhiwa kwani alimuanza maria kwa kumuweka mbuzi kagoma na kumkunja kisawa sawa na kuanza kupamp , ilikuwa ni mpata shike wa aina yake kwani maria alibadilishwa kila aina ya staili huku akilalama na damiani alimtaiti vizuri kwani hakutaka hata kidogo achoropoke kwenye mikono yake .
haikujulikana ni mafuta gani damiani aliopakwa kwani hakujielewa kwa wakati huo ,
" nyaraka ziko wapi ?"
Aliuliza marie huku akiwa amemkalia damiani anakata viuno kwa spidi ya 4G , damiani wakati huo hakuwa akijielewa maana alikuwa kwenye ulimwengu mwingine kabisa , lakini hakuwa tayari kusema ni wapi nyaraka zilikuwepo , na marie baada ya kuona bado damiani alikuwa mgumu hapo ndipo alipo fanya kitendo cha kifilauni .
Kwani kitendo hicho kilimfanya damiani apate msisimko kiasi cha kutoa machozi , kwani joto liliongezeka na mkuyenge kubanwa zaidi , marie alikuwa kabadilisha njia kwani muda huu alikuwa ameingiza mku** ni huku akikata mauno .
" Damiani nyaraka ziko wapi ?" " RHB bank " .
" Box number ngapi "
" Arghhh... siiiii.. namba ..namba 2060 " .
" pasword ni nini ?? " ...
" Argh .. ni SARAH " aliongea Damiani pasipo kujielewa na dakika kadhaa marie alimgusa shingoni na hapo hapo akazima na kufungwa kama mwanzo na marie aliweka funguo zile kwenye meza na akavaa nguo akatoka kwenye chumba hicho .
Baada ya dakika kadhaa alionekana kuvaa na kupendeza na usinge jua kama ndie alietoka kufanya ufilauni muda mfupi uliopita , aliingia kwenye gari na kusepa kuchukua nyaraka .
SEHEMU YA 30
Sabi baada ya kuingia kwenye lile gari hakutaka kutoka mpaka ahakikishe watu wake anao wafatilia ana wapata , alikaa kabisa kiti cha nyuma na kuegamia kwenye kiti , masaa yalienda bila kuona watu wale kutoka , aliamini kabisa kuna uwezekano wa watu wale kulala kabisa eneo hilo kwenye hizo apartment , lakini pia hakutaka kukata tamaa alikuwa na uchungu wa kupata flash ambayo kwa maelezo ya damiani aliona kabisa ilikuwa muhimu kwake kwani aliamini ingempa muongozo wa kujua ni nini kilisababisha baba yake kuchomwa sindano ya sumu mpaka kufa .
Aijaribu kutoa simu na kumtafuta damini lakini hakukuwa na majibu ya aina yoyote jambo ambalo lilimpa mashaka lakini hakutaka kabisa kuruhusu mawazo mabaya katika kichwa chake .
Alijikuta akipitiwa usingizi na kuja kushituka ikiwa ni saa moja kamili asubuhi na kilichomshitua ni kelele za magari zilizokuwa zikitoka kaatika parking hioo , alijitahidi kujificha ili aisonekane katika gari hio , masaa machache mbele ndio yule mwanamke waliomuona na bwana wake wakiingia hapo kwenye hzio apartment akitoka , na awamu hii alikuwa peke yake .
Alitoa kisu chake kidogo alichokuwa amefunga kwenye ufunguo na kisha akajiandaa kwa makabiliano na mrembo huyo na asubuhi alionekana kupendeza , mrembo yule wala hakuwa na wasiwasi na laiti kama angejua kwenye gari kulikuwa na mtu anamsubiri asingeingia , alicho kifanya sabi ni kulala kabisa kwenye siti ili asionekane .
Mrembo yule aliingia kwenye gari na kuwasha gari na kisha alitoa gari hilo pasipo kujua kuwa kwenye siti ya nyuma kulikuwa na mtu , gari ilitoka mpaka ikaingia kwenye barabara ya sukhumviti soi hapo ndipo sabi alipotokeza na kumuwekea kisu shingoni , jambo ambalo lilisababisha gari liyumbe lakini sabi alimtuliza vizuri .
“ endesha gari mpaka sehemu anayo ishi rafiki yako aliekuwa anatumia gari hii jana “ aliongea sabi kwa msisitizo na mdada yule alionesha kabisa woga machoni . “ wewe ni nani simjui mimi mtu unayemzungumzia gari nilikuwa nalo siku nzima
“.
“ usiteke tubishane , naomba simu yako “ aliongea sabi na mrembo yule kwa mkono wa kushoto alimpa simu
“ taja password “
Baada ya sabi kutajiwa password aliingia kwenye picha na kukuta picha ya mtu ambae alikuwa akimtafuta akiwa amepiga na huyo membo .
“endesha gari mpaka kwa huyo rafiki yako na usilete utani kwani nitakudhuru
“ aliongea sabi na kwa mrembo yule alitii maana alijua kabisa mtu huyo hana utani na pia ni ngozi nyeusi watu ambao hakuwa akiwajua vizuri , masaa mawili mrembo yule aliingiza gari mtaa wa suang luan park na kukunja kulia na hapo ndipo sabi aliposhuhudia gari waliokuwa wakitumia na rafiki yake damiani siku ya jana . na hapo ndipo alipo jua lazima kuna kitu kimetokea , mrembo yule kwa hali ya kutetemeka alisimamisha gari ,
“ toka nje taratibu na usilete ujinga maana nitakudhuru “ aliongea sabi mara baada ya gari kusimamishwa na mrembo huyo .
“ tangulia mbele “ aliongea sabi na muda huo hakuwa na masihara hata kidogo alionekana kuwa katika hali ya hasira kweli .
Baada ya kuufikia mlango , sabi alimuamrisha yule mdada afungue mlango lakini hakufunguka kwani ulikuwa umefungwa kwa nje , sabi alimwamrisha atafute funguo , na kweli dada yule alimuonyesha funguo inapopatikana kwenye chungu cha maua na kusha sabi aliinama na kumpatia kisha akafungua na wakaingia ndani .
Nyumba ilikuwa kubwa ya gorofa moja kwenda juu , chini kulikuwa na masofa na baadhi ya samani za gharama wakati huo sabi hakutaka kucheza mbali na yule mwanamke , kwani aliamini kitendo kidogo cha kijinga anaweza akamkosa .
Sabi aliangalia kila kona lakini hakuona dalili ya kumuona damiani . walianzia kukagua upande wa juu ya gohoroa na kisha wakashuka chini kwenye vyumba vilivyokuwepo chini .
Baada ya kukagua vyumba kadhaa napasipokuona dalili ya mtu sabi alikata tamasa na kuona huenda rafiki yake hakuwa eneo hilo.
Lakini wakati akiwaza kuna mlango aliuona na hakukiangalia hiko chumba , alimwangalia yule mrembo aliekuwa na hali ya waswasi huku akihangaika kujaribu kupiga simu ila sabi alimuona na kumpokonya simu ,alimwambia aongoze njia kuelekea kwenye hiko chumba , walijaribu kusukuma na kweli mlango haukuwa umefungwa kwa funguo Zaidi ya komeo kwa nje tu. “ damiani ! aliongea sabi mara baada ya kumuona damiani akiwa amefungwa kwenye kitanda huku akiwa uchi wa mbuzi na gobore likiwa bado lipo wima , sabi hakutaka kupoteza muda alimpiga pigo yule mrembo na kumfanya alegee aende chini lakini kabla ya kutua chini alimdaka na kumuweka chini , alisogelea funguo na kisha akazichukua na akamfungulia damiani .
“ vipi nini kimetokea ?”.
“ wewe acha tu mzee yule mwanamke alichonifanyia , ni dhaidi ya ushetani “ aliongea damiani huku akivaa suruali lakini ilimpa shida maana bado dhakari yake ilikuwa wima .
“ yaani yule sio mwanamke wa kawaida , anapigana hatari na mapigo yake sijui ni ya aina gani , unavyo niiona hapa kidogo tu anikate mashine yangu “
“ anataka nini kutoka kwako ?”
“ nyaraka nilizokuambia nimepewa na bruno “.
“kwa hio ikawaje ushampa? “.
“ hahahaha.. nina kichaa ule ndio uhai wangu nampaje kwa mfano , nimemdanganya nimeweka benki ya RHB , ila kidogo tu nimpatie maana alichokuwa ananifanyia kama ni mtu mwingine uvumilivu ungenishinda na ungechelewa kidogo tu angerudi angenikuta hapa na kunimaliza “ “ vipi kuhusu flash “.
“ sijaipata ila nina wazo “.
“ wazo gani ?”
“ kwakuwa nimemdanganya kuhusu sehemu nilizoweka nyaraka akifika akikosa atarudi sasa akirudi inabidi tumbananishe atupe kila kilichokuwa chetu na tusepe “ aliongea damiani na wote walikubaliana , walimbeba yule msichana na kisha walimuweka kwenye kitanda na kumfunga kama alivyokuwa amefungwa damiani na wakati huo hajitambui , damiani alimwangalia kwa uchu maana muda huo bado hali yake haikuwa sawa .
“ sabi ngoja nipige hata kimoja nitulieze hali yanguu sijielewi hapa kabisa “.
“ acha hizo , huo utakuwa ubakaji , kumbuka sisi tunaitafuta haki hatutakiwi kuwa na dosari “
“ sio hivyo lakini sijui huyu mwanamke kanipaka nini “ aliongea huku akishika kile kichupa chenye yale mafuta na kumpa sabi akakiangalia .
“nenda kajioshe tu na sabuni hali inatulia “ aliongea sabi baada ya kusoma maelekezo juu ya kile kichupa na damiani hakautaka kuchelewa alitafuta bafu lilipo na alikwenda akajiosha na wote wakafunga ule mlango na kutoka nje ya kile chumba na kuanza kukagua kila kona ya chumba walijaribu kuitafuta ile flash, walipanda mpaka kwenye vyumba vya juu ya ghorofa wakijaribu kutafuta lakini walichofanikiwa kuona ni laptop ya damiani lakini hakukuwa na flash , walijaribu kutafuta chini ya kitanda na hapo ndipo sabi alitabasamu kwani aliona bastora .
Hii itafanya kazi yake “ aliongea sabi huku akijaribu kuingalia kama ilikuwa na risasi na aliona ilikuwa full , walijaribu kupekua pekua lakini hawakuambulia kile walichokuwa wakitafuta .
“ sasa hapa inabidi tumuwekee mtego , muda si mrefu naamini atarudi “ aliongea damiani na sabi alikubaliana nae .
Yalipita masaa mawili ndio gari ya marie iliingia , alishangaa kuona gari ya mdogo wake iliokuwa imesimamishwa na aliamini kabisa kuwa mdogo wake atakuwa ndani , japo hakujua ni kwanini mdogo wake kaja eneo hilo kwani alitakuwa muda huo awepo chuo , lakini alipuuzia na kwenda ndani huku akiwa makini kwani kuna dalilimbaya aliziona na hapo ndipo aliposhitukaa kwani alimkuta damiani yupo kwenye sofa kajipumzisha huku akiwa na glasi mkononi yenye juisi .
“ karibu sana mke wangu , naona umekuja muda muafaka maana nina ny**ge “ aliongea damiani huku akiwa hana wasiwasi kabisa .
“mdogo wangu yuko wapi “. Aliuliza huku akionekana kuwa na hasira kweli .
“ aranya !!” aliita huku akimwangalia damiani na damiani aliishia kutabasamu .
“ kumbe anaitwa aranya , mdogo wako nimemtuma sokoni , ili atupatie uwanja nikusugue mpaka akirudi umekuwa mwepesi “ aliongea damiani na hapo ndipo alipopampansiha hasira marie .
“ utanikoma leo wee hayawani kama umemgusa mdogo wangu utakiona cha mtema kuni na utanitambua kwa kunipotezea muda wangu wa kwenda mpaka sukhumvit soi , kumbe unanidanganya “ aliongea marie huku akimfata damiani kwa hasira na kurusha ngumi ambayo damiani aliiona vyema na kuhepa kushoto ikapita , lakini hakupumzishwa kwani ile anahepa kushoto marie asharusha front kick iliomfanya gauni lake alilovalia kumuacha wazi kabisa , teke lile lilimpata damiani kwenye kifua , damiani na yeye hakutaka kuzembea kama jana yake , alitaka kumuonesha mwanamke huyo kwamba hata yeye alikwa vizuri kwenye mapigano .
Marie alikuja na teke lingine akidhamiria kumfyeka mtama damiani lakini damiani alikuwa mwepesi na alishaigundua dhamira ya mhasimu wake kwani aliruka juu na alivyorudi chini alikuwa ameachia teke lililompata marie tumboni na kupepesuka kurudi nyuma .
Na hapo ni kama aligusa mzinga wa nyuki kwani marie alianza kumletea mapigo ya karate hapo ndio damiani aligwaya , japo alijitahidi kupangua kila pigo lakini aliona kuzidiwa , hakutaka kupigwa kizembe kwa mara ya pili na yeye aliitumia muay thai vizuri , damiani alipangua karate huku akijjiweka sawa , kuna kosa alilolifanya marie na damiani aliona hio kama ushindi kwake kwani alimkanyaga kwa nguvu kwenye goti la mkuu na hapo alimfanya marie atoe ukulele maana mauamivu yalikuwa makali , damiani hakutaka kumchelewesha aliruka tena juu akimdhamiria kumzimisha kabisa , lakini pigo hilo marie aliliona vyema na kulikwepa huku akirudisha ngumi iliompata vyema damiani kifuani .
Marie alisimama tena wima japo alikuwa akyumba maana mguu bado ulikuwa na maumivu , na hapo ndipo damiani aliposhuhudia kitu ambacho aliwahi tu kukiona kwenye movie , ilikuwa ni kung fu , marie alikuwa airudisha miguu nyuma kwa mbwembwe , huku damiani akiwa anamshangaa kufumba na kufumbua hata damiani hakujua alifkiwaje maana alijikuta akipokea ngumi mfululizo na akaongezewa na teke lililompeleka kwenda kutua kwenye sofa huku akisikilizia maumivu , na marie hakutaka kumpa nafasi anyanyuke kwani alimfata kwa kukimbia lakini alijikuta bila kupenda akisimama na hio ni mara baada ya risasi kupuliza kwenye sikio lake .
“ simama hivyo hivyo na nyoosha mikono juu “ aliongea sabi na marie alitii
“ damiani kachukupe pingu mbili kule ndani uje umfunge “ aliongea sabi na damiani kwa maumivu makali alisimama na kwenda walikomfunga charanya mdogo wake marie na alimfungua mguu mmoja na mkono mmoja na kisha alirudi sebleni na kumfunga nayo marie , halafu wakamuongoza hadi kwenye kile kile chumba .
“charanya “ aliongea marie huku akitokwa na machozi baada ya kumuona mdogo wake alivyokuwa amefungwa , alionekana kumpenda sana mdogo wake .
“ dadaaaa “ aliongea huku kakitoa machozi .
“ mfungulieni mdogo wangu hata uadui na nyie nasema “ aliongea kwa hasira marie akimwangalia damiani , lakini kwa damiani wala hakuwa na hata huruma . “ damiani mfunge kwenye hiko kitanda mfungulie huyo dogo “ aliongea sabi na damiani alimfungulia charanya na kumfunga pingu mikononi kama muhalifu na kisha damiani alimpadisha marie kwenye kitanda na kumfunga kama alivyokuwa amefungwa yeye .
“nina maswali makuu mawili tu ya kukuuliza mrembo na sipo hapa kwa ajili ya kupoteza muda kabisa , swali la kwanza ni wapi flash yetu ilipo , swali la pili wewe ni nani na nani kakutuma “.
Aliongea sabi huku akimwangalia marie , na marie alimwangalia kwa hasira sana sabi huku akionesha kiburi cha kutotaka kuongea na hapo ndipo sabi alitabasamu na kumvuta charanya na kumuwekea bastora kwenye kichwa .
“ nahesabu mpaka tatu , usipo nijibu utashuhuida ubongo wa mdogo wako ukitapakaa hapa ndani , moja mbili tatu .
“ flash ipo kwenye gari “ aliongea bila kupenda huku akitoa machozi na jambo hilo lilinfaya sabi atabasamu na kumpa ishara damiani akaangalie kwenye gari kama ni kweli.
Damiai dakika tatu tu alirudi akiwa ameishikilia mkononi huku akionesha kutabasamu hakuamini kama flash ile ilikuwa mikononi mwake tena . “ swali la pili hujajibu mrembo , ila kwakuwa umejibu swali langu la kwanza , nitampunguzia adhabu mdogo wako na kumfaya kilema kama tu hautotaka kuniambia ukweli “.
“ wewe ni nani ?” awamu hii alieuliza ni damiani lakini kwa marie hakutaka kabisa kuongea , na hapo ndipo alipomikoki bastora na kuiweka kwenye paja la charanya aliekuwa akilia huku akiongea kithai .
“ nimetumwa na samiueli saitoto kutoka Tanzania “ aliongea marie na kuwafanya waangaliane damiani na sabi
“ samueli saitoto ni nani ?”
“ simjui samueli ni nani , ila nilipokea maagizo kutoka HQ nitiii maagizo yake
“.
“HQ gani ??”
“CIA “ aliongea na kuwafanya sabi na damianni watumbue macho “ huyo samueli anapatikana wapi “.
“ yupo Tanzania , nadhani nimeibu maswali yenu yote naombeni mumuachie mdogo wangu “ aliongea marie .
Baada ya kumhoji marie kwa muda mrefu hawakuwa na haja nae teana kwani waliona kabisa waliochokuwa wakikitafuta tayari washakipata , damini alienda kuchuku laptop yake na kisha waliwazimisha na kuondoka .
Baada ya kuutoka huko moja kwa moja walielekea kwa damiani sehemu aliokuw na apartment yake na kisha alichkua vitu vyake muhimu na alienda mpaka kwa sabi kukaa kwa muda kwani aliamini lazima marie angemtafuta kwa namna yoyote ile .
******
Basi baada ya damini kutoka nyumbani kwa marie walienda moja kwa moja mpaka kwenye apartment ya damiani na baada ya kufika sabi alimwambia damini kwamba hio sehemu sio salama tena anatakiwa kuondoka kuelekea anakoishi yeye na damini alikubaliana na sabi na baada ya muda mfupi wa damini kuchukua vitu vilivyo muhimu walitoka na kuelekea victory monument
Hatimae sabi na damiani wanafanikiwa kuipata flash waliokuwa wakiitafuta , kila mmoja alijawa na shauku ya kutaka kujua kama kweli flashi hio ilikuwa na taarifa Zaidi ya zile anazo zijua damiani , hawakautaka kuchelewa Zaidi kwani mara baada tu ya kutulia waliona jambo la kufanya ni kuhakiki ile shauku yao kama ni kweli .
Basi sabi alichukua laptop yake na kisha alifanya utundu wake kwenye computer hio na ndani ya madakika kadhaa alichomeaka flashi ile , na akaaanza kufanya mautundu mengine kwa kubonyeza keyboard na ndani ya madakika kadhaa alikuwa amefanikiwa kuona kilichokuwa kwenye flashi , na kama ilivyokuwa mategemeo yao walikuta flash ile ikiwa na faili ambalo lilikuwa zipped ( yaani faili lilokuwa likihitahi uwekaji wa nywira ili kulifungua .
Sabi alimwangalia damiani usoni na hivyo hivyo kwa damiani alimwangalia sabi usoni ni kama kuna taarifa mabayo walikuwa wanapeana lakini la hasha , sabi alikuwa ni kama mtu ambaye alikuwa akihitaiji ruhusa kutoka kwa damianii kwani damiani alitingisha kichwa chake na ikawa kama ruhusa kwa sabi ..
“ faili hili limefungwa , ili kulifungua tunahitaji nywira “ aliongea sabi huku akimwangalia damiani usoni .
“ kwa hio tunafanyaje ?” aliuliza sabi kwa mhamaniko .
“ inabidi nivunje vunje ili kulifungua “
“ sawa wewe fanyya uwezalo lilolamsingi tuweze kuona ni nini kimehifadhiwa kwenye hilo faili “ aliongea damiani na sabi alianza kazi yake ya kulifungua faili hilo kwa njia anazo zijua yeye , kwakuwa alikuwa mtaalamu wa maswala ya computer swala hilo kwake halikumpa shida kabisa , kwani ndani ya sekunde kadhaa alikuwa ashaweza kulifungua faili hilo .
Ndani ya faili hilo kulikuwa na video na ilikuwa ni video hio moja tu ambayo ilikuwepo , video ambayo ilikuwa na megabyte kumi(MB 10) , sabi alimwangalia damiani na damiani alimwangalia sabi na damiani alitingisha kichwa na kumruhusu sabi aiplay hio video .
“HELLOW , NAFIKIRI NI MOJA YA VIDIO YANGU YA PILI UNAIONA , KWANZA NIKUPE HONGERA KWA KUFANIKIWA KUIONA VIDIO HII , KWANI NAAMINI MPAKA SASA UMEKWISHA PITIA HATUA YA KWANZA NA SASA UNAWEZA KUJILINDA .
DHUMUNI LA KUREKODI VIDIO HII NI KUKUPA MUONGOZO WA
BIASHARA ZANGU ZOTE NINAZO ZIMILIKI ILI UWE MRITHI KAMILI
NA KUENDELEA KUENDELEZA BISHARA HIZO , UNACHOPASWA
KUFANYA NI KUPIGA NAMBA HIZI 098765***** TAJA NAMBA YA UTAMBULISHO 145S01 HAPO UTAPOKEA MAAGIZO MENGINE .” na
video ikaishia hapo , hakukuwa na kingine Zaidi na aliekuwa akiongea ni bruno . .
Kwa vijana hao jambo hilo hawakuwa wakilitegemea kwani mategemeo yao ilikuwa ni zaidi ya taarifa hio .
Kutokana na kwamba washaonekana na ilikuwa Dhahiri kwamba damiani lazima angekamatwa ndani ya nchi hio ukizingatia watu waliokuwa wakimtafta walikuwa na ushirika mpaka CIA basi hakutaka kuchelewa tena kupiga namba hio , alicho kifanya ni kuchukua simu yake na kuingiza namba aliotajiwa na kisha alipiga .
“ please specify your identification number “ ilikuwa ni sauti ya kike iliotulia ikimuhitaji kuingiiza namba ya utambulisho na damiani ilikuwa mara yake ya pili kuisikia sauti hio
“one four five ‘S’ zero one “ alitaja damiani
“ please wait for identification “ tafadhari subiri kwa ajili ya utambulisho
“identification complete please wait to be reconnected to the person you are loking for “ akimaanisha kwamba asubiri kwa ajili ya kuunganishwa na mtu ambae anamtafuta .
Kila mmoja alipatwa na mshangao na mhamaniko wa aina yake , kwani kinacho tokea hapo ni kile kile kilichotokea nyuma wakati wanapiga namba hizo na hapo swali linaibuka je mtu huyo ni nani ambae kila siku wanaambiwa wanaunganishwa nae lakini hawamjui na wala hajitambulisihi kwao , kila mtu hakuwa na jibu .
Baada ya dakika kadhaaa simu iliita tena na awamu hii ilikuwa ni namba mpya lakini iliokuwa ni private yaani haikuwa na utambulisho kuwa ilikuwa ikipiga kutoka wapi .
Damini aliipokea na kisha aliweka simu sikioni .
“ una karamu pembeni ?” ilikuwa ni sauti nzito mara baada tu ya damiani kupokea simu hio .
“ ndio nunayo “
“ andika hio namba “ aliambiwa na kisha alitajiwa namba na kuiandika
“ safari kutoka sehemu uliopo nenda mpaka china mtafute mtu mwenye hio namba atakupa maelekezo “ na simu ilikatwa hapo hapo hata damiani alipo taka kuuliza mtu huyo ni nani alikwisha chelewa kwani ishakata na asingekuwa na uwezo wa kuipiga namba hio kwani ilikuwa ni namba ambayo ni private na usingeweza kuipigia labda akupigie kwa mwenye namba .
“ vipi tunafanyaje ?” aliuliza sabi huku akimwangalia mwenzake usoni akitarajia jibu .
“ inabidi twende china “ aliongea damiani na sabi alijifikiria kwa muda.
“ inabidi wewe uwende china “ aliongea sabi na kumfanya damiani ashangae .
“ wewe unabaki ?”.
“ ndio kuna mambo sijayakamilisha , lakini pia kozi yangu ya upelelezi sijaimaliza , nikiikamilisha inabidi nirudi nyumbani “ aliongea sabi na damiani alijikuta akiwa mnyonge lakini hakuwa na la kufanya
Basi hatimae damiani alifanya tararibu zote za kusafiri mpaka china siku moja tu ilimtosha kukamilisha taratibu hizo na siku iliofuata saa nane kamili mchana aliingia kwenye ndege na kusafiri , huku nyaraka zake akizipost kwenda benki ya china kwani aliona sio salama kama angetembea nazo hivyo njia ya salama ilikuwa ni kwa njia ya posta .
WELCOME TO GANZHOU CHINA
Ni maandishi makubwa yaliosomeka mara baada ya ndege hio kutua ndani ya jiji hilo la kibisahara la nchini china jiji ambalo limejengeka haswa .
SEHEMU YA 31
TURUDI SASA JIJI DAR ES SALAAM PRESENT
Naam ni dani ya jiji la dar es salaam ndani ya jengo la PSSSF tower jengo moja refu sana lililokuwa likipatikana mlimani city , ndani ya sehenu ya kuingilia ndani ya jengo hiLi alionekana mkuu mstaafu wa TISS bwana elly matinde akitoka kwenye gari nyeusi aina ya jaguar , bwana huyu baada ya kutoka kwenye gari alinyoosha moja kwa moja mpaka ndani ya jengo hili , aliingia kwenye lift na dakika chache tu alikuwa kwenye flour kubwa iliokuwa imependezeshwa, aliFika mapokezi huku akiona bango kubwa limeandikwa Z STYLISH WEAR .
Ndio ni ndani ya kampuni ya mwana mitindo maarufu aliyejizokea jina kwa kushinda mataji mbali mbali katika swala zima la uwana mitindo na huyu hakuwa mwingine alikuwa ni zakayo , kijana machachari mwenye muonekano wa kuwanasa warembo wengi wa jiji hili hasa wale wanaotaka kutoka na wanaume wazuri na waliofanikiwa .
" nimemkuta CEO " aliongea bwana matinde mara tu baada ya kufika mapokezi akiongea na mwanadada aliekuwa amependeza kweli kweli na hii ni moja ya kazi ya zakayo kwani wafanya kazi wake wote walikuwa wanapendeza na hio aliona ni moja ya njia ya kutangaza bidhaa zake .
" Ndio ana mgeni kwa sasa , unayo appointment ya kukutana nae siku ya leo ?" .
" sina appointment , lakini unaweza mwambia mkurya amefika atakuelewa " aliongea huku akiweka tabasamu usoni na dada yule naye alipokea tabasamu hilo huku akitingisha kichwa na kukubaliana na matinde na kisha alitoka eneo hilo la mapokezi huku akimuonesha matinde sehemu ya kusubiria .
Dakika chache tu alirudi mwanadada yule na kisha alimwambia kwamba mzee asubiri dakika kadhaa kuna mteja anamalizana nae , ndani ya dakika kumi alitokea zakayo alietangulizama na moja ya msanii maarufu wa kike nchini na kumlaki matinde na kisha waliongozana mpaka kwenye ofisi yake .
" Ofisi yako nzuri sana , hongera ".
" Nashukuru sana mheshimiwa karibu sana ".
" nishakaribia , nafurahi kijana kama wewe umefikia mafanikio kama haya , vijana wengi mtaani wanahangaika kwa kukosa ajira ".
" Unajua maisha ili ufanikiwe kuna sifa lazima uwe nazo , ukikosa sifa hizo utaishia kulalamika kwamba serikali haitoi ajira "
" ni kweli kabisa , sasa sitaki kupoteza muda , nadhani mpaka sasa ushajua kilichonileta hapa ".
" nishajua ndio " aliongea huku akijiweka vizuri .
" kuna kazi nataka mnifanyie " .
" Tukufanyie au nikufanyie ??".
" haha naona uko makini ,nimesema mnifanyie kwakua haupo peke yako " .
" nipo na nani ?" " undercover nwenzako ".
" unamaanisha doris??".
" Ndio " .
" malipo yapo ??".
" nisingefika hapa ilihali najua TISS hawakulipi na kwasasa ni kama unajitolea tu , nimekuja nikiwa kamili " . " Basi hakuna shida nipe kazi ".
Aliongea na kisha matinde alitoa picha na kumpatia , na zakayo aliipokea na kisha akaingalia na alijikuta akikazia macho na kitendo hicho matinde alikiona .
" huyu mtu mbona kila mtu anamtafuta ni nani "?.
" Unamaanisha unamjua ??".
" Ndio , mkuu japo swala hili ni siri lakini kwakuwa ushawahi kuwa mkubwa wangu naomba nikwambie " aliongea zakayo na kumfanya matinde amwangalie .
" Mheshimiwa raisi kupitia kwa mfanya biashara mmoja ajulikanaye kwa jina la Kimbona ashawahi kuniletea kazi kama hii na nilishafanyaga ".
" unamaanisha kimbona mmilikiwa KILAC ??" " Ndio huyo ".
" ni kazi gani alikuletea ??"
" kumtafuta huyu bwana kwenye hii picha " Aliongea na hapo ndipo matinde alishangaa zaidi .
" Na ulifanikiwa kumpata ??"
" kazi yangu ilikuwa ni kujua kijana huyo yuko wapi , na nilifanikisha hilo na kazi yangu iliishia hapo na nikapewa malipo yangu na sikufatilia zaidi.” "Yuko wapi kwa sasa " aliuliza kwa mhamaniko .
" hahaha..mheshimiwa ukitaka details zote inabidi nikuuzie taarifa si unajua naishi kwa njia hii " aliongea zakayo na kumfanya matinde atabasamu na kisha akitoa simu na kupiga namba ya kizito na kumpa maelekezo .
" Taja namba ya akaunti ?" aliongea matinde na zakayo alitaja huku akiachia tabasamu kwani kwake hela ilikuwa kipaumbele zaidi , alikuwa ni jasusi wa hali ya juu na kwa utanashati wake usingedhania kwamba bwana huyo ashawahi pitia mafunzo ya kikomandoo , alikuwa akiweka maslahi mbele zaidi , na ashafanya kazi nyingi za waheshimiwa na kuzifanikisha na malipo hake kulipwa na ndio kazi iliomfanikisha mpaka kufungua kampuni hio kubwa na japo alikuwa mwanamitindo lakini alikuwa akipenda sana kazi ya upelelezi .
" hazikupita dakika hata tano meseji iliingia kwenye simu yake , ikionesha muamala wa shillingi milioni kumi . " alitabasamu na kumwangalia matinde .
" nipe ripoti " .
" iko sehemu salama ni ndefu kidogo , utanambia sehemu ambayo tunaweza kukutana na nikuletee " aliongea zakayo na matinde hakubisha na alitoka hapo baada ya wawili hao kuagana .
******
Saa tatu kamili usiku ndani ya hoteli ya nyota tatu ilio kuwa ikijulikana kwa jina la golden tulip iliokuwa ikipatikana msasani sekou drive road , ilionekana gari ya mrembo merina aina ya AUD ikiingia ndani ya eneo la maegesho , dakika chache tu alitokezea kwenye gari hio huku kama kawaida yake akiwa amependeza sana .
Alitembea kwa mwendo wa madaha kabisa kuingia ndani ya jengo hilo na moja kwa moja alielekea hadi kwenye lift na kubofya kitufe namba tano , lift hio ikamchukua moja kwa moja mpaka floor namba tano , alitoka huku akitembea akijaribu kuzungusha macho kulia na kushoto mita kadhaa mbele aliona sehemu aliokuwa akiendea " meeting hall " baada ya kuufikia mlango huo hatimae aliufungua na hapo ndipo alipo kutana sura tofauti za aina tano .
" karibu sana merina " aliongea kizito huku akimkaribisha kabisa kwenye kiti na merina alitabasamu akashukuru na kukaa ndani hapo kulikuwa ni wanaume tupu huku sura hizo akiwa hazijui .
Walikuwa ni kizito , mkuu wa majeshi , katibu mkuu mstaafu wa chama tawala NLP , Matinde na mkuu wa polisi kanda maalumu ya Arusha amabe kwenye utawala wa bendera alikuwa ni mkuu wa polisi kadna maalumu ya dar es salaam. .
" Jamani kwanza nataka niwatambulishe kwenu mfadhili wetu , anaitwa nerina sostenessi ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya SWIFT TRANSIT LIMITED " . aliongea kizito na wote walipiga makofi na kumkaribisha .
“Japo ya kuwa ni mkurugenzi lakini pia ni moja ya watu wa karibu wa kijana damiani , sitopenda kuweka ukaribu wao wazi lakini niseme tu kwamba ni mtu ambaye tunaweza tukamwamini " aliongea na hapo alimkaribisha matinde .
" jamani kama tulivyokubaliana katika kikao chetu kilichopita juu ya dhamira ya kumpata kijana damiani , niseme kwamba kazi haikuwa ngumu kwani mpaka sasa ninayo ripoti inayomuhusu " aliongea na kisha aliinua tablet yake na kuanza kusoma .
" Jina lake kamili anaitwa Damiani rabani , ana miaka 25 hadi sasa ni mzaliwa wa lushoto Tanga kijiji kinavhojulikana kwa jina la mkuzi . alinyamaza kisha akaendelea
“mnamo tarehe tajwa ,wala 2019 mama yake alishambuliwa kwa risasi na watu ambao mpaka sasa haifahamiki ni wakina nani lakini ni ni maadui wa bwana bruno lamberk , siku kadhaa mbele kijana damiani baada ya kimaliza kumpumzisha ya mama yake katika nyumba yake ya milele ,alitekwa na watu wasio julikana mpaka alipokuja kupewa msaada na merina , huyu alieoko mbele yenu ,alimsaidia kwa kumfikisha hospitalini lushoto mjini , alikaa kwa siku mbili ndipo alipo rejewa na fahamu lakini katika harakati za kimtafuta daktar kijana damiani alitekwa tena nah ii taarifa ya polisi kituo cha polisi lushoto mjini ." Alitulia hadi hapo na kisha akaendelea .
Hio ni taarifa ya awali kutoka kwa polisi , lakini taarifa ya zakayo tuliempa kazi nitaisoma .
“kwa taarifa za kuanzia hospitalini uchunguzi aliofanya amebaini , damiani hakutekwa " aliongea hapo na merina alijikuta akitoa macho kwa mshangao , akaendelea .
“Taarifa zinaonesha suzzane ndie aliemtoa hapo hospitalini kwa maagizo ya marehemu danny mtalemwa na hii ilikuwa ni kwa ajili ya kuhakikisha usalama wake , alipelekwa korogwe mara naada ya kutoka hospitali ya wilaya ya lushoto , siku moja baada ya kupelekwa korogwe ndio siku ambayo danieli aliuwawa ndani ya kijiji cha mkuzi na kuhusu watu waliofanya tukio hilo hawakujulikana , kuhusu damiani hakujulikana pia alipo elekea , lakini kwa uchunguzi wa zakayo alibaini kijana huyo alifika mjini tanga ,akawasiliana kwa namba 06***** kwenda kwa namba ambayo haikufahamika ni namba gani mpaka sasa kwani kwenye kumbukumbu za kimitandao haikuwepo na siku alio wasiliana na hio namba ndio siku aliotoka katika lodge ya FURAHA inn , uchunguzi ulibainika kwa kutumia kamera za ulizi wa benki ya CRDB kijana huyo alionekana akiingia kwenye gari aina ya mercedez benz , baada ta kuingia katika gari hio , jasusi wetu mbobezi zackayo aligundua uelekeo wa gari hio ukikuwa ni kuelekea jijini dar es salaam na hilo aliligundua kwa kupitia camera zilizofungwa daraja la wami , kibo complex na palm beach shopping malls , baada ya upelelezi aligundua bwana damiani kupitia ubalozi wa kenya alifanikiwa kutoka nchini na kuelekea kenya na hatimae Thailland ." Alimaliza na kila mtu alishngazwa na uhodari wa upelelezi wa zakayo kupiia ripoti hio , lakini pia swala la damiani kwenda nchini Thailland .
" inamaana hakutaka hata kunitafuta , alifika mpaka dar jamani " yalikuwa moja ya mawazo ya mrembo merina aliekuwa pia kwenye mshangao wa taarifa hio .
" kabla ya maswali naomba niendelee " aliongea matinde na walimwangalia wakisubiri aendelee .
" kilichomfanya zakayo afanye upelelezi huu ni kwasababu raisi henry kupitia mfanya biashara kimbona anaemiliki kampuni ya KILAC (KIMBONA
INTERNATIONAL LINK AND COMPANY ) ndie alieomba kazi hii ifanyike '.
" Unamaanisha kwa huyo kimbona anashirikiana na raisi ?".
" Inawezekana kwa asilimia mia moja ,lakini pia kazi ilikuwa ni kujua tu mahali alipo damiani na kazi iliishia hapo .”
" mheshimiwa matinde mpaka hapo nimegundua mambo mawili makubwa , la kwanza kuna uwezekano huyo damiani kuna mtu anamsaidia , maana kutokana na background yake ya maisha asingeweza kukutana na balozi wa kenya , la pili kuna uwezekano wa kimbona kwa kushirikiana na mheshimiwa raisi wanaweza wakawa wamempata damiani au bado wanaendelea kumtafuta ".
" Ni kweli kabisa kizito naunga mkono swala hilo , lakini sasa kwa taarifa hio ni kipi kinakwenda kufanyika kwanzia sasa ,naomba swala hilo tulijadiri kwa pamoja ili tuone muafaka .". aliongea matinde
" Mimi nadhani swala hili tumpe tena mpelelezi zakayo afuatilie na tujue kama Damiani yupo mikononi mwa raisi au bado wanamtafuta na kama wanamtafuta na sisi tuongeze juhudi zetu za kumpata kabla ya wao , kwani tunaamini ana taarifa muhimu tunazo hitaji " aliongea mkuu wa majeshi na wote walikubaliana .
Merina alijikuta moyo ukimuuma baada ya kikao hicho , mapenzi yake kwa damiani ni kama yalikuwa yamerudi upya , hakuamini kama damiani alofika dar mpaka kusafiri lakini hakumtafuta , lakiniswala la damiani kufatiliwa aliona huenda ikawa sababu ya yeye kuondoka bila kimtafuta , lakini pia mambo mengi yalikichanganya kichwa chake hakuelewa kwanini raisi henry anamtafuta damian?i , ni kipi damiani anacho ambacho kinasababisha maisha yake yanakuwa ni ya kutangatanga ?, ni nani damiani anamsaidia mpaka akafikia hatua ya kwenda nchini thailland? , thailland amekwenda kufanya nini ? kuna mambo mengi ambayo yeye alikuwa akitaka kuyafahamu kujua ukweli wake kwani muda huo alionekana kuchanganyikiwa ukijumlisha na mapenzi aliokuwa nayo juu ya damini hali ilizidi kuwa mbaya Zaidi .
" Nitakupata tu damiani nimekumis sana " aliongea merina wakati huo tayari alikuwa nje ya jumba lake la kifahari , jumba ambalo ungeambiwa kuwa nni yeye tu na mdogo wake wanaoishi ndani ya jumba hilo usingeweza kuamini .
.********
IKULU DAR ES SALAAM
Zikiwa zimepita siku mbili baada ya mheshimiwa henry kumtembelea sabi hospitalini aghakani , siku hio kijana sabi alionekana akitoka kwenye gari aina ya V8 XR nyeusi baada ya kufunguliwa mlango na bwana mmoja alievalia suti , ndani ya eneo la maegesho ndani kabisa ya ikulu dar es salaam .
Baada ya kutoka aliongozwa na mwanadada alivalia kinadhifu kabisa kama ilivyo desturi kwa wafanya kazi wa ikulu kuvaa suti , siku hio kijana sabi alivalia suti iliomkaa vyema kwenye mwili wake , suti ya rangi ya blue .
" Karibu sana sabi alikuwa ni patrick aliekuwa amesimama mbele yake akionesha tabasamu huku akimlaki rafiki yake ." " Asante rafiki yangu ".
waliongozana mpaka ndani kabisa na kuingia kwenye dining hall na hapo alikutana na mama yake patrick mke wa raisi miss wema akiwa anaandaa chakula .
" Karibu sana sabi , jisikie huru " aliongea mke wa raisi huyo huku akiachia tabasamu lililomfanya kuonekana mzuri japo umri umeenda .
Ilikuwa ni chakula cha mchana na siku hio sabi alikuwa amealikwa rasmi na mheshimiwa raisi hapo ikulu kwa chakula cha pamoja .
" karibu sana sabi " aliongea henry mara baada ya kufika mezani na wote wakakaaa na kuanza kula huku wakipiga stori .
" sabi una mchumba kweli ?" aliuliza raisi na sabi akitabasamu .
" bado sijabahatika kuwa nae mheshimiwa " aliongea sabi .
" vijana wa siku hizi mnachelewa sana , patrick nilitarajia mchumba wako.ungekuja nae hapa " .
" Yupo na majukumu mengi sema alitamani kuja " aliongea patrick na jambo hilo lilimfanya mke wa raisi kukunja sura .
" patrick yule ni.mchumba wako kweli ?" aliuliza mke wa raisi .
" kitu kama hicho mama , mama nipo kwenye hatu ya kumhalalisha " ..
" mhmh haya , ila mwanagu hujaona wanawake wengine mpaka yule " " kwanini unasema hivyo mama ?" .
"sabi unampango gani kwa sasa ? " aliuliza mheshimiwa ili kupotezea mazungumzo ya mke wake na patrick .
" kwa sasa sijafikiria bado maana ndio kwanza nimerudi nchini ".
"mimi nataka nikupe kazi inayoendana na wewe na itakayo kulipa vizuri maana kitendo ulichofanya kinastahili zawadi kubwa sana lakini,mimi naona nikupe kazi ambayo unaendana nayo ila nitakulipa.pesa nzuri ".
" nitashukuru muheshimjwa japo naomba isiwe kwasababu nimekuokoa ila naomba iwe kwasababi nastahili kazi hio kutokana na elimu yangu maana kitendo kile hata kwa mtu mwingine ningefanya “.
" ondoa shaka juu ya hilo "
Basi baada ya mheshimiwa kumaliza.kula.,.aliongozana na sabi mpaka.ofisini , lakini ile anakaribia ofisi yake alikutana na suzzane akiwa ana msubiri , sabi baada ya kumuona suzzane alimkonyeza na suzzane alitabasamu.
" suzzane karibu ".
" Asante mheshimiwa nahitaji kuongea na wewe " .
" sawa hakuna shida " aliongea huku akimwambia sabi asubiri dakika chache aongeee na suzzane .
Suzzane baada ha kuingia ndani alitoa barua na kumpa.mheshimiwa na raisi aliisoma .
" kwani unataka kuacha kazi suzzane ?".
" Mheshimiwa kuna uwezekano damiani akawa tayari nchini na ninataka kufanya upelelezi nikiwa chini ya TISS ilo kumkamata kwani kuna hisia zinaniambia swala la wewe kushambuliwa anahusika kwa namna moja ama nyingine na kama nni kweli basi atakuwa mtu hatali kweli na kama kweli amepewa waraka wa raisi bendera na hatujui unahusu nini basi kuna uwezekano mkubwa akawa tishio kwako muheshimiwa ".
" What !!! , unayoyasema ni kwrli suzzane ??."
" mheshimiwa swala hilo sina uhakika nalo ila naamini kwa asilimia kubwa damiani yupo ndani ya Tanzania nataka swala hilo nilifanyie kazi kabla mambo hayajaharibika , hivyo nataka nijipunguzie majukumu niwe na swala moja la kumtafuta damiani ." aliongea suzzane na raisi aliekuwa kwenye mshituko hakuwa na lakusema kwani hata yeye pia alikuwa anahitaji swala hilo lifanyike kwa umakini .
" sawa shzzane hakikisha this time unamkamata na unachukua nyaraka na kumuhoji kile anachojua , kisha nitata maagizo ya kipi kifanyike , hakikisha unanipa taarifa kila hatua unayo pitia , nakukumbusha nyaraka ambayo inatoka kwa raisi bendera kama kweli kijana huyo anayo jua itakuwa nni hatari sana kama ataamua kuitumia kwani utakuwa ni udhaifu wangu mkubwa " aliongea raisi na suzzaene alipiga salute na kutoka .
" Sabi unesema huna kazi maalumu , na umesomea maswala ya computer " nataka nikupe kazi ya mkurugenzi wa mawasiliano ikulu , lakini pia msemaji mkuu wa serikali " aliongea raisi na kumpagawisha sabi kwani ilikuwa ni nafasi kubwa sana kitaifa .
" Nashukur sana muheshimiwa kwa kuniamini lakini naona ni nafasi kubwa sana
" .
" usijali kijana wangu nakuamini sana isitoshe umeyaokoa maisha yangu , unastahiki zaidi ya haya " aliongea raisi na kupeana mkono na sabi.
Siku mbili mbele mheshimiwa henry alimteua sabi mboneche kuwa mkurugenzi wa mawasiliano ikulu , na pia kuwa msemaji mkuu wa serikali .
“MISSION COMPLETE SABI SEE YOU SOON IN NEXT MISSION –by mzalendo “ulikuwa ni ujumbe ulioingia kwenye simu ya sabi .
Wakati sabi akifurahia uteuzi huo raisi henry alipokea simu kutoka kwa mkuu wa U-97 kuwa kuna kikao , kwani bwana huuyo ashatua nchini na ana mengi ya kuongea .
END OF SEASON ONE .
THANK YOU.