Ujasusi - Umoja namba 97

Ujasusi - Umoja namba 97

Suzzane hakutaka kukurupuka katika kufanya kazi yake , alikuwa na kazi mbili za kufanya kwa wakati huo ili kujua ukweli anaotaka kuujua , mtu wa kwanza aliekuwa akimfatilia , alikuwa ni janeth , na wa pili alikuwa ni stephano lamberk alikuwa makini kweli na kazi yake hakutaka kabisa kuwapa nafasi watu anaowafatilia wajue kama wanafatiliwa , na ndio maana alikuwa akitumia akili sana katika kuwafatiilia , hata ile alipogundua kuwa kuna uhusiano kati ya mke wa raisi na janeth hakutaka kumwambia mheshimiwa raisi , kwani aliona kabisa anapaswa kujua kabisa kile kinacho endelea na ndipo atoe taarfa hio kwa mkuu wake .
Siku hio ilikuwa ulikuwa ni muda wa saa mbili kamili akiwa ametoka kwenye mihangaiko yake ya kiuchunguzi , alikuwa amekaa mezani akijaribu kuunganisha matukio.
Jina la janeth bendera na jina la stephano lamberk ni majina ambayo yalikuwa kwenye akili yake .alikuwa na picha zilizokuwa zikiwaonesha wawili hao kuchekeana kabisa , picha alizochukua siku hio mchana ndani ya makao makuu ya kampuni ya NLT .
Alikuwa akiangalia picha ya stephano akiwa ameshikana mkono na janeth , na muda huo walionekana walikuwa wakiagana , tabasamu lililokuwepo kwenye uso wa janeth na pia kwenye uso wa bwana stephano lamberk vilimfanya aje na hitimisho kuwa wawili hao walikuwa wanafahamiana .
Lakini jambo la pili lililomchanganya ni jina la janeth “janeth bendera ‘ ni jina ambalo lilimchangaya sana , kilicho mchanganya Zaidi ni mwanadada huyo kuwa na elimu kubwa mno tena akiwa na umri mdogo , hakuamini kwamba mwanadada huyo ni kweli alikuwa na PHD kwa umri aliokuwa nao , jambo hilo kwake pia lilikuwa likimpa maswali mengi ambayo kuna muda yalikuwa yakigongana .
“ kama janeth ana PHD inawezekana pia alienda kwenye kampuni ya NLT kwa ajili ya biashara kwani wote wapo kwenye fani moja , lakini pia nina hisia wawili hawa wanaonekana kufahamiana kwa muda mrefu japo ni hisia zangu lakini naamini uwezekano huo upo , na kama watakuwa washakutana kabla kuna uwezekano pia wakawa wanashirikiana pia katika maswala mengine , ikiwemo la janeth kuchoma madawa ya kimbona , lakini bado kuna jambo linanichanganya na natakiwa kulifania uchunguzi , inawezekanaje huyu anae jiita mzalendo kutumia sura za watu wengine katika matukio yake ya nyuma , inatakiwa ni ujue ukweli lakini ukweli nitaujua vipi ?” hayo yote yalikuwa ni mawazo ya mwanadada suzzane , jasusi mbobezi aliekuwa akimtii sana mheshimiwa raisi katika kazi zake nyingi .
*****
Ni siku ambayo ndani ya kampuni ya NLT kulikuwa na kikao cha wakurugenzi wa bodi , yaani wale wamiliki wate wa kampuni walikuwa wapo kwa ajili ya kujadiliana mustakabali wa kampuni hio mpya tanzania katika maswala ya teknolojia kwa ujumla wake.
Kwa damiani hata yeye pia alifurahishwa sana na muamko wa watanzania , kwani kitendo cha kutangaza kuuza hisa asilimia ishirini na hisa hizo kununuliwa zote , aliamini sana watanzania wanaipenda teknolojia na wapo tayari kwa ajili ya kuona taifa lao likiwa linaendelea katika swala zima la teknolojia
Siku hio mda wa asubuhi ndio muda ya watu mbali mbali waliokuwa ni wamiliki wa hisa za kampuni ya NLT waliingia ndani ya ukumbi wa mikutano ndani ya jengo hilo la NLT , moja ya watu waliongia eneo hilo alikuwa ni Patrick mtoto wa mheshimiwa raisi .
Patrick alikuwa ni mmoja ya mmiliki wa hisa katika kampuni hio na haikueleweka kwanini alivutiwa na kampuni hio mpaka kununua hisa , kwani hata yeye pia alikuwa ni moja ya watu waliokuwa wamkimiliki kampuni inayo endana na hio ya NLT lakini pia alikuwa ni adui mkubwa wa kampuni hio .
Kilichomshangaza Patrick ni mara baada ya kuingia ndani ya ukumbi wa mikutano ni kumuona merina , hakujua kuwa na merina alikuwa ni mmiliki wa asilimia kadhaa ndani ya kampuni hio sio kwake tu lakini pia kwa merina pia alishangazwa na uwepo wa Patrick ndani ya ukumbi huo kwani pia hata yeye hakujua kuwa patrick alikuwa mmiliki wa hisa ndani ya kampuni hio .
Nusu saa baada ya watu wote kuingia ndani ya ukumbi huo , akiwemo janeth , na mainjinia wengine , rebbecca , luang shu hakuwepo kwani alikuwa tayari amekwisha rudi nchi kwao china .
Basi damiani aliingia huku akiwa amevalia suti yake safi kabisa ya bei mbaya , alikwenda moja kwa moja kuketi katika kiti chake maaulumu kama kurugenzi wa kampuni hio , lakini pia kama mmiliki wa kampuni kwani yeye ndie aliekuwa anahisia nyingi katika kampuni hio ( major share holder ).
Damianni ama stephano na yeye pia alijikuta akishangazwa na uwepo wa merina ndani ya eneo hilo , alikuwa akimjua merina kama mteja wake , lakini hakujua kuwa mwanadada huyo alikuwa amekwisha kununua hisa katika kampuni yake , alijikuta moyo wake ukifurahi , hali ambayo hata yeye hakujua kwanini alikuwa akifurahi , aligeuza upande wa janeth na wakagongana macho na kila mmoja alitabasamu .
Basi kikao icho kilianza kwa kutambulisha watu mbali mbali waliokuwa wakimiliki hisa zao kwa asilimia zao na Patrick alikuwa akimiliki asilimia kumi na merina pia alikuwa akimiliki asilimia kumi , pia kikao kiliambatana na moja ya malengo ya kampuni siku za usoni .
MASAA MACHACHE NYUMA .
Kitendo cha stephano kuitwa jina lake halisi na mrembo janeth kilimchanganya na kumshitua kwa wakati mmoja , hakujua ni kwa namna gani mrembo huyo alimjua , japo alikuwa akikumbuka kuwa mrembo huyo kuna sehemu ashawahi kukutana nae , lakini swala la kumjua kuwa amevaa ngozi feki lilimchanganya .
“ usiwe na waswasi siri yako ipo salama “ aliongea janeth kwa mapozi .
“ wewe ni nani ?”
“ mimi ni janeth mfanyakazi wako “ aliongea janeth kwa mapozi huku akizunguka ndani ya ofisi hio kama mtu aliekuwa akiichunguza na alionekana alikuwa akijiamiani sana mbele ya damiani .
Stephano japo mwanadada huyo alikuwa ameonesha kujua siri yake lakini hakutaka kabisa kuwa mwepesi aliweka ngumu
“ sijui unacho ongea kuhusu siri “
“ hahahaha… kwa hio unamaanisha ninayo ongea hapa ni uongo “
“ ndio ni uongo , inakuwaje unaniita jina ambalo sio la kwangu na huyo damiani ni nani ?”
“ damiani ni jina lako halisi nakujua A to Z najua unaweza ukawa umenisahau , au unataka nikukumbushe tulipokutana mara ya kwanza “.
“ sijawahi kukutana na wewe mimi “ aliongea stephano kwa kujiamini huku akiangalia tarakishi yake “
“ naona umesahau siku ile ulivyogongana na mimi ndani ya hoteli ya four season china wakati unaenda kuonana na waziri wa china “
Hapo ndipo stephano alipokumbuka sehemu aliokutana na mwanadada huyo , alijikuta akijilaumu kwa kutomkumbuka mapema , alimkumbuka mwanadada huo alipogongana nae wakati anaingia kwenye lift .
“ naona umenikumbuka sasa “
“ janeth nina kazi kwasasa naomba tuishie hapa kwa leo “ aliongea stephano kwa sauti ambayo ilionesha kuwa na waswasi ndani yake .
“ usijali damiani , kwanza unaelewa kuwa hio ngozi ndio mimi nilioitengeneza , au luang shu hajakwambia “
Kauli hio ndio iliomfanya stephano kushangaa Zaidi , na hapo hakuwa na ujanja kabisa , mpaka hapo alijikuta akikumbuka kauli ya luang shu kumwambia kuwa mtu alieitengeneza FULL BODY MASK alikuwa ni mtanzania mwenye phd yake , mpaka hapo alijua kuwa mtu aliekuwa akiongea nae alikuwa akimjua vyema .
“ wewe ndio uliotengeneza full body mask “.
“ ndio ni mimi damiani “ aliongea janeth huku akikaa kwenye sofa huku akimwangalia damiani akiwa ameachia tabasamu
“ ila sikujua kuwa unatumia jina la stephano lamberk mpaka nilipo kuona , nikajua umevaa ngozi bandia “
“ sina hoja , ila nasema hongera sana “
“ asante damiani , ila nilikuwa nikikutafuta sana tokea siku ile ulionigonga “
“ ulikuwa ukinitafuta!! , kwa ajili ya nini ulikua ukinitafuta ?”
“ nitakuambia siku nyingine damiani , kwasasa kuna majukumu yangu nataka kwenda kuyashughulikia lakini nisindikize basi “ aliongea mrembo huyo na kisha damiani alinyanyuka na kutoka na janeth mpaka eneo la kupark magari na walipeana mkono kwa bashasha kubwa , na wakati wanapeana mkono ndio wakati ambao suzzane alikuwa akiwapiga picha .
*****
Mheshimiwa raisi japo swala la uwekezaji wa Stephano lamberk lilikuwa swala lenye tija kwa nchi , lakini kwake aliliona wala hilo kama mwiba katika maendeleo yake mwenyewe , alijua kuwa kampuni ya INNOVA na kampuni ya NLT kuingia nchini na kuwekeza inamaanisha yeye kampuni yake kufa kabisa , kwani aliamini asingeweza kabisa kushindana na INNOVA na NLT, alikuwa akiwaza mambo kadha wa kadha ni kwa namna gani angeishi pasipo kupata hasara Zaidi . mchaga huyu japo ya kuwa raisi lakini alikuwa akipenda pesa pia , na ndio maana alikuwa tayari kufanya lolote kwa ajili ya kujiingizia pesa .
Siku hio ni baada ya kuonana na bwana stephano na kufanya mazungumzo nae , alikuwa ameshikilia karatasi ya asilimia za hisa ambazo zilikuwa zikiuzwa na kampuni hio ya NLT alikuwa amekaa chini akiwaza ni maamuzi gani afanye , lakini pia upande wa pili pia alikuwa akiwazia uwekezaji wa kampuni ya INNOVA ambayo pia ilikuwa ikiuza asilimia za hisa zao .
Baada ya kuwaza muda wa masaa kadhaa , ndipo alipokuja kufanya maamuzi ya kununua hisa katika makampuni hayo yote mawili kwa wakati mmoja , alitoa simu yake na kupiga mahali .
“ nataka kununua hisa zote za kampuni ya NLT na INNOVA “ aliongea mheshimiwa .
“ mheshimiwa hisa zilizobaki ni asilimia kumi tu kwa kampuni zote mbili “”
“ hizo zingine zimeenda wapi “
“ zimekwisha kununuliwa na SWIFT TRANSIT “
“ okey sawa nitanunua hizo zilizobaki nafanya muamala sasa “ aliongea na kisha alikata simu .
“ huyu ni merina mchumba wake Patrick huyu , mwanamke anaakili sana huyu sijui Patrick anakwama wapi kumuoa huyu mwanamke , inabidi nimuite nifanye nae mazungumzo “ alijifikiria huku akiendelea kuchezesha simu yake , na dakika kadhaa alikuwa ashanunua hisa zote .
Mara baada ya kufanikisha hilo ndipo alipoendelea na majukumu yake , mpaka muda wa kutoka ofisini.
Lakini kabla ya kutoka aliingia kijana wake ambae alikuwa akimfanyia baadhi ya shughuli zake binafsi , kijana huyu aikuwa akijulikana kwa jina la talimba , alikuwa ni kijana msomi mno aliekuwa ni mwanausalama kitengo cha ikulu , na moja ya kazi kubwa ambayo alikuwa amempa kijana huyu kuifanya ni kumfatilia mke wake , kwani mheshimiwa raisi japo alikuwa akimpenda sana mke wake lakini hakuwa akimuamini hata kidogo , haikujulikana ni sababu gani hakuwa akimuamini mke wake
“ vipi talimba kuna habari yoyote “
“ ndio muheshimiwa na ndio maana niko hapa “ aliongea talimba , alikuwa ni kijana mojamfupi maji ya kunde mwenye macho makubwa hivi na mwili wake mnene kiasi .
Muda huo mheshimiwa alikuwa amesimama nje ya ofisi na alikuwa akitaka kuelekea upande wa familia yake , lakini ilibidi aghaili na kurudi ndani ya ofisi kuongea na talimba , kwani alijua kabisa kila talimba anapofika anayo taarifa , basi jua ni taarifa ya siri ambayo hakutaka mtu oyote yule ndani ya ikulu aifahamu
“ mheshimiwa madam siku mbili zilizopita kakutana na mwanadada anaefahamika kwa jina la janeth bendera muda wa jioni maeneo ya ununio ndani ya nyumba moja ambayo kwa kufatilia niligundua kuwa inamilikiwa na msichana huyo , pia siku ya jana yake alikutana na mwanadada merina muda wa saa kumi kamili ndani ya hoteli ya serena “
‘’umesema janeth , huyo janeth ni nani “
“ janeth kwa taarifa nilizo nazo ni mwanasayansi aliengia nchini miezi kadhaa iliopita akitokea china , kiwango cha elimu yake ni PHD “”alijjibu talimba na kumfanya bendera ashangae na awaze kidogo na majina hayo mawili yalipita ndani ya kichwa chake yaani ‘merina na janeth’.
“ safi endelea kuwafatiilia na unipe taarifa Zaidi “
“ sawa muheshimiwa “
Baada ya mheshimiwa kupewa taarifa hio na talimba alitoka ofisini na kwenda upande wa familia yake na kuonana na mke wake aliekuwepo sebleni akiangalia tamthilia , wema mara baada ya kumuona mme wake , aliinuka na kumkumbatia
Mheshimiwa alioga na kisha alimua kupumzika huku akijaribu kuwaza jambo la mke wake kukutana na merina na janeth hakujua ni kwanini wamekutana ila aliamini kama kuna mpango unaendelea ambao yeye haujui basi angeujua tu , muda wa saa mbili kwenda tatu ndipo alipo mkumbuka patrick na kumpigia simu na kumpa maagizo ya kufika ikulu siku inayo fata .
Ilikuwa siku nyingine siku ya asubuhi na mapema ndio siku Patrick alifika kwa ajili ya kuonana na baba yake na walianza mazungumzo
“ kesho nataka ukahudhurie kikao cha wana hisa ndani ya kampuni ya NLT , nimenunua hisa asilimia kumi ndani ya kampuni ile japo nilihitaji kununua zote ila inaonekana mkwe kanizidi ujanja “
“ mkwe gani baba “
“ si merina au kuna mwingine ?”
“ inamaana merina kanunua hisa kwenye kampuni ya NLT “
“ ndio , inakuwaje merina ni mpenzi wako na hujui hilo “
“ baba mimi na merina hatuzungumzi sana maswala ya kazi “
“ anhaa sawa .. ila patrIck kuna kitu sikielewi , hivi unaamini kweli yule mwanamke anakupenda ?”
“ baba hata mimi mpaka wakati huu nachanganyikiwa kabisa , nampenda sana merina , lakini merina kuna mtu anampenda “
“ kuna mtu anampenda , unamaanisha sio wewe “
“ ndio baba kuna kijana mmoja anafahamika kwa jina la damiani , ndio merina anampenda lakini mpaka sasa kijana huyo hajawahi kuonekana tokea atekwe”
“ unasema damiani?? “
“ ndio mbona umeshituka unamfahamu ??“
“ hapana lakini ni kama nishawahi kulisikia hilo jina “
‘ yawezekana baba kwani ni moja ya watu waliokuwa wakihusiana na bruno , kwani mama yake alipigwa risasi na mahasimu wa bruno “
“ kwa hio unamaanisha merina na damiani wanafahamiana , na walifahamiana vipi ?”
“ hata mimi swala hilo linanichanganya , sijui wapi walikutana ila najua wanafahamiana kwani merina alilia sana siku ambayo alitekwa “ aliongea Patrick huku akimuhadithia baba yake tukio la damiani kutekwa ndani ya hosputali ya lushoto “
“kweli inaonekana wanafahamiana , sasa unamaamuzi gani juu ya merina maana hata mimi nimetokea kumpenda yule mwanamke , ana akili sana za kimaisha na kama atakuwa mke wako atakusaidia sana “
“ baba hata mimi mpaka sasa sijui nifanyeje kumteka merina kihisia kwani nampenda sana “
“ hahaha kijana wangu wanawake ni viumbe dhaifu sana , hakikisha merina anakuwa mke wako , usikubali mtu mwingine akimchukua kutoka kwako “ aliongea raisi na kumfanya Patrick atabasamu .
“ baba umenitia nguvu sana , na mimi lazima merina awe mke wangu sitoruhusu mtu yoyote amchukue “
“ safi sana kijana wangu , pia hakikisha bishara zinaenda vizuri “
‘ sawa baba “
Itaendelea
SEHEMU YA 42
Zakayo alikuwa mtu mjanja sana katika kufanya uchunguzi , na kilichokuwa kinampa uwezo wa kujua jambo hata kama limejificha ni kutodharau kila taarifa inayomfikia , kwani baada ya kupata taarifa aliokuwa akiitaka kutoka kwa Irene basi aliona ni mwanzo mzuri wa kuendelea na uchunguzi wake .
‘stephano lamberk ‘ ni jina lililomvutia sana jasusi huyu , aliamini kabisa kuna taarifa iliokuwa Imejificha juu ya bwana stephano lamberk , kwani kupita taarifa za maisha ya nyuma ya bwana bruno kutokuwa na mtoto wa kiume wala ndgu yoyote , aliamini lazima kuna jambo nyuma ya stephano lamberk .
Jambo la kwanza ambalo aliona anapaswa kulijua undani wake, ni swala zima la bruno lamberk kupigwa risasi na kuuwawa , aliamini kwa kulifanyia swala hilo uchunguzi , angejua ni watu gani walimuua na swala hilo huenda lingepelekea kujua ni wapi alipo damiani .
Mwanzoni kazi hio aliona ni nyepesi sana , lakini sasa aliona ni kazi ngumu mno kwake , hata waliompa kazi walipomuuliza maendeleo ya uchunguzi wake aliishia kuwaambia kuwa wampe muda wa kulifanyia uchunguzi swala hilo kwa undani zaidi .
Siku hio alikuwa ndani ya jiji la Arusha , haikujulikana alikuwa ndani ya jiji hilo kwa ajjili ya nini , lakini aliamini kuna kitu angekipata ndani ya jiji hilo ambacho kingemsaidia katika upelelezi wake, alienda mpaka ndani ya hoteli moja kubwa ya kitalii iliokuwa ikipatikana ndani ya jiji hilo iliokuwa ikifahmika kwa jina la gran melia .
baada ya kuweka mizigo yake michache ndani ya chumba hiko alijipumzisha , na muda huo ilikuwa yapata saa kumi za jioni , alikuja kushituka kutoka usingizini muda wa saa mbili za usiku , na kilizho mshitua ni mlio wa simu .
“ vipi uko wapi “
“ ilikuwa ni sauti iliosiikika katika masikio yake “
“ niko hotelini “
“ mtu wako nimemuona sasa hivi hapa triple A “
“nakuja sasa hivi , hakikisha humpotezi “ aliongea zakayo na alianza kujiandaa haraka haraka na kisha alitoka ndani ya hoteli hio na kuchukua usafiri wa taksi uliomfikisha mpaka triple A
Ni moja ya sehemu ambazo zilikuwa zimechangamka sana , watu walikuwa wengi wakiwa wanakunywa bia , na wengi wao walikuwa ni machalii wa miaka ya ujana .
Baada ya kuingia eneo hili la club alitoa simu yake na kupiga na dakika kadhaa alitoka mwanaume mmoja mnene kiasi mwenye miaka kati ya miaka ishirini na nane hivi aliekuwa amevalia kinadhifu kabisa , bwana huyu alikuwa akifahamika kwa jina la godlove .
Baada ya kuonana na godi waliingia wote ndani ya club hio na kuchagua sehemu na kuketi na god love alimuonesha mtu ambae alikuwa anamtafuta , na zakayo alijikuta akitabasamu baada ya kuona kuwa mtu anaemtafta alikuwa mwenyewe .
“unataka tufanyeje , maana jamaa anaishi kwa machale sana “
“ nataka nimteke kibabe , lakini sina shemu ya kumpeleka “
“ kuna karakana moja hivi nahifadhia kahawa tunaweza mpaleka “ aliongea
“ hapo fresh , ngoja niendelee kumlia timing , si umekuja na gari yako ?”
“ ndio ipo “
Basu baada ya masaa kadhaa hivi kupita , ikiwa imetimu saa nne kamili mtu waliekuwa wanamfatilia alionekana kunyanyuka kwenye kiti chake akiingia kati ya watu waliokuwa wanacheza mziki , na kuanza na yeye pia kucheza , jambo hilo ni kama zakayo alikuwa akilisubiria , kwani alitabasamu na kisha alinyanyuka.
“ nisubirie kwenye gari yako “ aliongea zakayo na kisha god alitoka na zakayo kuingia kati ya watu na kuanza kucheza huku target yake ilikuwa ni kumpata mwanaume huyo aliekuwa akicheza hapo ndani , alijua sio jambo rahisi kwani mtu aliekuwa akimsogelea alikuwa ni mtu hatari mno , na alijua kosa moja tu anaweza kumkosa na hilo hakutaka litokee kwani alikuwa akimtafuta mno .
Baada ya kumfikia akiwa bize , mara alijikuta akizongwa na watu ambao walimfanya kumzibia kwa mbele , aliwapangua na kupita na hapo ndipo alipo pigwa na mshangao kwani mtu aliekuwa akimtafuta hamuoni tena , alijikuta akianza kujipenyeza kwenye watu huku akizungusha shingo , lakini hakumuona , alichoka , alijua tayari ashashitukiwa tayari na mtu ashapotea , na kama alivyosema god kuwa mtu huyo alikuwa ni mtu anaeishi kwa machale aliona jambo hilo ni la kweli , wakati akiwa anaendelea simu yake ilivibrate na haraka aliitoa na kuangalia meseiji .
“ mtu wako huyu huku anasepa “ ilikuwa ni meseji iliomkurupusha zakayo na haraka alielekea upande wa kutokea nje , na ile anafika tu aliingia ndani ya gari la god .
‘ kaelekea wapi ?”
“ katoka saivi na gari ya Subaru “ aliongea na kisha walianza kulitafuta gari hilo uelekeo wake , na uzuri ni kwamba walikuwa wakitumia range . hivyo zakayo aliamini kwamba kama wangemfukuzia wangempata kiurahisi muda huo walikuwa ndani ya barabara ya kaloleni na mbele kidogo walikuta wakiiona gari hio na hapo zakayo alitabasamu , uzuri ni kwamba muda huo hakukuwa na magari mengi hivyo jambo lao lilionekna kuwa rahisi , lakini pia gumu kwani mtu waliekuwa wanamfatilia alionekana kujua kabisa kuwa anafatiliwa maana spidi alikuwa anatembea nayo ilikua juu , dakika chache gari ile ilikunja simeon road , na wakina zakayo hawakutaka kabisa kuipoteza kwani muda huo walikuwa wameikaribia kabisa , walikuja kufanikiwa kuipita kwa mbele na kuizuia gari hio nyuma kidogo na barabara ya kwenda njiro .
Baada ya kuizuia bwana huyo alitoka kwenye gari na kutoka nduki na zakayo hakutaka kabisa na yeye kubaki nyuma kwani kama mshale alichomoka na kuanza kumfukuza kwa nyuma , jamaa alikuwa kwenye spidi ya hali ya juu lakini pia zakayo vile vile, alikuja kumkamatia kwenye kona ya kuingia vijana rd. lakini bado jamaa huyo hakutaka kukamatwa kizembe kwanni alianza kupambana na zakayo , lakini zakayo alionekana kuwa imara kwenye mapambo kwani mapigo mawili tu yalikuwa yamemdondosha chini , kuna baadhi ya watu walijikuta wakivutiwa na tukio hilo , lakini zakayo hakutaka kuwapa nafasi kwani alimbeba mtu wake na kuondoka eneo hilo , mpaka alipo kuja kukutana na god na kumpakia mtu wake na safari ya kuelekea kwenye karakana ya god ikaanza , dakika chache walikuwa kijenge , gari ilikunja kulia na kwenda kusimama kwenye jengo moja kuu kuu, alitoa ufunguo na kufungua mlango na kumuingiza ndani mtu wake na kisha alimzindua .
“ nyie ni wakina nani , kwanini mnanifatilia ?”
“ na wewe ni nani kwanini unatukimbia “
“siawakimbia mimi “
“sikia bwana mdogo sipo hapa kwa ajili ya kukudhuru ila kuna taarifa naihitaji kutoka kwako “
“ taarifa gani unataka kutoka kwangu ukiwa umenifunga”
“sikia najua ulikuwa moja ya walinzi wa bwana bruno lamberk “ aliongea zakayo na kumfanya bwana huyo ashituke .
“ simfahamu mtu huyo “
“ najua ungejibu hivyo , kama nilivyo kuambia sipo hapa kwa ajili ya kukudhuru ukinipatia taarifa yangu nnayo hitaji nakuachia huru “
Aliongea zakayo na kisha alitoa kitambulisho bandia chenye jina tofauti na kumuonesha bwana huyo , na jamaa alishangaa baada ya kuona kitambulishho hicho kilichomuonesha kuwa mtu huyo alikuwa ni mwanausalama , alijikuta akivuta pumzi nyingi na alionekana kama mtu alieshukuru “
“ ni kweli mimi nilikuwa mlinzi wa bruno lakini sina taarifa yoyote kwenu ”
“ sasa mbona unaonekana kuwa na waswasi “
“ lazima niwe na waswasi maana tokea kifo chake maisha yangu yamekuwa yakujificha “
“ kwanini unasema ni yakujificha ?”
“ walinzi wote wa bruno wameshakufa nilepo hai ni mimi tu “
“ unaamaanisha wenzako wote walikufa na kwanini wafe “
“ sijui sababu “
“ ulianza kuwa mlinzi wa bruno kwanzia lini ?”
“ miaka nane sasa “
“unafikiri ni kwanini wenzako wamepoteza maisha “
“nadhani ni maadui wa bruno “.
“ wee unwafahamu maadui wa bruno ?”
“hapana siwafahamu wote ila kuna baadhi nawafahamu aliokuwa anafanyanao biashara “
“kwanini wawe maadui wakati alikuwa akifanya nao kazi “
“braza nakujibu tu kwasababu wewe ni mwanausalama , lakini maisha yangu yapo hatarini naomba unisaidie hata nitoke nje ya hii nchi “
“ kama unataka kuwa salama na nikusaidie nipe taarifa muhimu ambayo itanishawishi” aliongea zakayo huku akimwangalia kijana huyo .
“ ninayo ndio , lakini lazima unihakikishe kuwa nipo salama “
“ mpaka sasa upo salama bwana mkubwa , kwanza jina lako nani “
“ Herbert sheiza “
“ wewe ni mwenyeji wa wapi “
“ lushoto “
“nipe hio taarifa “
“kuna mpango wa siri boss aliuandaa kabla ya kifo chake “ aliongea Herbert na kumfanya zakayo atabasamu .
“ mpango gani?? “
“damiani “
“ damiani ni nani ?”
“ damiani ndio mpango wenyewe “
“ unamaanisha nini kusema damiani ndio mpango wenyewe “
“ boss alimchagua damiani katika kutimiza mpango huo , na hata mama yake damiani kuuwawa ulikuwa mpango wa boss “ zakayo alijikuta akitoa jicho kwa mshangao
“unamaanisha nini kusema hivyo “.
“ “mimi najua hivyo tu kuwa mama yake damiani kuwawa ulikuwa mpango wa boss , na pia walikuwa wakimfatilia damiani tokea akiwa chuo na aliepewa kazi hio alikuwa ni danieli ambae ashakufa “
“Nipe taarifa nyingine hio bado haitoshi kukusaidia nataka uniambie kila unachokijua kuhusu boss wako “.
“ boss alikuwa anauza madawa ya kulevya , mpaka pale alipowasaliti wenzake na kuungana na raisi bendera , na mpaka sasa sisi tulishangaasababu ya boss kuwasaliti wenzake , lakini moja ya mlinzi mwenzetu alituambia kuwa boss kashikwa pabaya na raisi bendera merehemu na wote tulikubaliana na hilo , lakini mpaka sasa hatukujua ni nini kinaendelea kwani boss aliongezewa ulinzi “.
“.unajua aliemuua boss wako “.
“ sifahamu ila kuna watu wawili nawahisi kuhusika “.
“ nani na nani “
“ suzzane “
“ suzzane ndio nani ?”
“ ni moja ya walinzi walikuwa wametumwa na mheshimiwa raisi kumlinda boss “
“ sasa kama suzzane alikuwa anamlinda boss kwanini useme kuwa ndio kamuua boss huyo huyo “.
“ kwasababu suzzane ndie aliemuua danny “. Aliongea bwana Herbert na kumfanya zakayo ashangae , kilicho mfanya ashangae ni kwamba alikuwa akiwajua vyema suzzane na danieli kama moja ya makomandoo wenzake , lakini pia alifahamu fika kuwa danny na suzzane walikuwa wakivunja sheria za usalama wa taifa kwa kuwa wapenzi , lakini kuambiwa kuwa suzzane ndio aliemuua danny swala hilo lilimshangaza “
“ wee ulijuaje haya yote ?”
“ siku ambayo danny anapigwa risasi nilishihudia kwa macho yangu”
“umesema umeshuhudia kwa macho yako hebu niambie kilichotokea “
“ siku hio baada ya kifo cha boss kila mlinzi alitawanyika , kimya kimya kwani tulijua hali isingekuwa salama tena , mimi sehemu nilio fikiria kujificha ni kwenda kujificha kwa bibi mkuzi , siku ambayo damiani anaingia ndani ya mkuzi akiwa na danny niliwashuhudia , lakini jambo lililo nishangaza ni mara baada ya danny kupigwa risasi na mtu aliejificha juu ya mti mwanzoni sikuwa nimemuona vizuri mpaka pale aliposhuka chini na hapo ndipo nilipomuaona suzzane , lakini hakuwa peke yake , alikuwa na bwana mmoja hivi mzungu mzungu hivi “.
“ na damiani je ?”
“ damiani alikimbia na mimi pia nilikimbia na sikukaa tena kwa bibi ndio nilikuja huku Arusha kwanzia siku hio , lakini bado kuna watu walikuwa wakinifatilia kwanzia siku hio na ndio maana maisha yangu yalikuwa ya kujificha sana , na hata nilivyowaona pale club niliwagundua tu ni walewale “.
Zakayo aliridhshwa na maneno ya Herbert mno , lakini pia ni nameneno ambayo yalimuacha kwenye mashangao , baada ya mahojiano yake kumalizika , hakuona sababu tena kubaki eneo hilo , god aliondoka na Herbert na zakayo alienda hotelini .
“ mama yake damiani kuuwawa na bruno , linawezekanaje hili , na ni mpango gani huo ulikuwa ukisukwa , najua suzzane kumuua danny ni lazima itakuwa ni oda kutoka kwa raisi lakini hili la mama yake damiani kuuwawa linanichanganya “ aliongea zakayo mara baada ya kufika hotelini akiwa amejilaza akiwaza mambo hayo , alijikuta akianza kuunganisha matukio ya upelelezi wake wote “
“kwanini bruno amuue mama yake damiani ni mpango gani bruno alikuwa nao , na kwanini bruno afie nyumbani kwa damiani , watu wawili waliokuwa ndani ya nyumba ya wakina damiani walikuwa ni wakina nani, je mpango huo suzzane alikuwa akiujua , ni nani aliemsaidia damiani kwenda thailland je ndio mpango wenyewe wa bruno, lakini hata kama bruno ashakufa tayari , aisingeweka mpango ambao na yeye anakufa , ni Dhahiri kabisa kuwa mpango wake ulifeli , lakini hata kama umefeli , damiani ni nani anaemsaidia?, sehemu ni moja tu ya kupata jibu na sehemu hio ni ndani ya ubalozi wa kenya , balozi wa kenya lazima atakuwa anajua kinacho endelea maana si rahisi kwa mtu mkubwa kumsafirisha damiani pasipo ya kufahamiana nae “ hayo ndio maswali alio ona kwamba anapaswa kuyajibu kwani muda huo hakuwa na jibu hata moja “.
*******
Carlos Cardosso muuaji huyu wa kimataifa , mara baada ya kushindwa kazi yake ya kwanza aliokuwa amepewa na kimbona , kazi ya kupata nyaraka alizoacha bruno kutoka kwenye mikono ya damiani , kazi ambayo alifiifanya akiwa na suzzane , mkataba wake na kimbona ulivunjika , lakini pia japo mkataba wake na bwana huyo ulivunjika , lakini pia hakutaka kurudi gerezani na ndio maana aliamua kumuomba bwana huyo kuendelea kuishi uraiani huku akiahidi kufanyakazi zote ambazo atakuwa anampa.
Kambi yake rasmi ilikuwa ni ndani ya jiji la lushoto tanga ndani ya mlalo , sehemu ambayo ndio kulikuwa na kambi ya kimbona , lakini taarifa ya mzigo wa madawa ya kulevya wa mabilioni uliokuwa ukimilikiwa na boss wake huyo kupotea , jambo hilo lilimshangaza sana , na hata pale alipopewa taarifa ya kufika dar kwa ajili ya kulifanyia uchunguzi swala hilo , aliamini kabisa mtu ambae anamfanyia uchunguzi alikuwa ni mtu wa hatari sana , kwani kitendo cha dawa hizo kutolewa bandarini mpaka kupelekwa bagamoyo na kuteketezwa alikiri kuwamtu huyo alikuwa ni mwenye welevu mkubwa wa akili katika kupanga mipango yake na yeye pia aliona ili kufanikisha kazi ya boss wake bila makossa ni kuhakikisha kuwa na yeye anakuwa na akili vile vile katika kupanga mipango yake .
Mara baada tu ya kufika ndani ya jiji la dar mtu aliemkumbuka alikuwa ni suzzane , na kwakuwa alikuwa anamawasiliano na mrembo huyo hakupata shida ya kuonana nae , suzzane ndie aliempa taarifa zote za muhusika mkuu anaemtafuta , jambo hilo lilionekana kumfurahisha sana carlos , lakini pia lilimrahishia kazi yake .
Siku hio alikuwa makini sana kumfatilia janeth , alitaka kujua ratiba yake yote , lakini pia kuwa na tahadhari atakapotaka kumfanyia tukio mrembo huyo , kwani kama alivyopewa maelezo na suzzane kuwa mrembo huyo ni hatari kimapigano .
Siku hio alipanga kufanya tukio la kumteka janeth , ili akampe mateso kama alivyo ambiwa na boss wake ili kujua ni nani aliechini yake .
Saa saba kamili za usiku ndio muda ambao aliingia ununio , mbele kabisa ya jumba analoishi janeth huku akiwa na taarifa za muonekano wote na ramani nzima ya nyumba hio mpaka chumba anacholala mlimbwende huyo .
ITAENDELEA
NILIKUWA NIMESHIKWA NA MALARIA WADAU TOKEA JUMAPILI NILISHINDWA KUANDIKA KABISA HATA KUWAJIBU. .
SEHEMU YA 43
Carlos alikuwa amezamilia kuhakikkisha tukio la kumteka janeth linafanikiwa kwa asilimia mia , na ndio maana alifanya uchunguzi wa ratiba zote za mwanadada huyo kwanzia muda anaolala , chumba anacholala , walinzi wanaolinda nyumba hio , watu wanaoishi nao na ramani nzima ya nyumba jinsi ya kuingia na kufanya tukio lake pasipo kukwama haikueleweka utafiti huo alifanya saa ngapi , lakini kila kitu kilikuwa kipo mikononi mwake na jambo lilokuwa limebaki ni kukamilisha tu kazi yake .
Muda huo wa saa saba aliofika ndani ya jengo hilo alizunguka mpaka nyuma ya ukuta na kama chui aliparamia ukuta na kutua ndani pasipo kushitukiwa wala kupigisha kelele , na jinsi alivyoruka na ukuta ule ulivyokuwa na umeme aliruka kitaalamu sana .
Mara baada ya kutua ndani pambeni kabisa ya swimming pool alianza kuangaza kulia na kushoto kuangalia usalama , baada ya kuona hali ikoshwari alitembea kuelekea upande wa nyumba ambayo walikuwa wakilala walinzi , akiwa na bastora yake mkononi aina ya pistol F3 blaser na usoni akiwa amejiziba vyema kuzuia sura yake kuonekana .
Basi kama mwanajeshi wa navy alivyofika kwenye mlango aligonga kama mara tatu kwa nguvu lakini sio kwa kelele sana na kisha alijibanza pembeni ya mlango , na zilipita kama sekunde sitini tu mlango ulifunguliwa , na mtu wa kwanza kutoka alikuwa ameshika bastora huku akiwa na kifua wazi , lakini uzembe wa mtu huyo ni kutoka bila tahadhari na hio ilikuwa fursa moja kwa carlos kwani alimvuta kwa staili moja ya kijeshi na kumzimisha na kisha kumlaza chini , baada ya kuona zoezi lake limefanikiwa alichokifanya ni kufunga kiwambo cha kuzuia sauti kwenye pistol yake na kisha alizama kama kinyonga ndani ya nyumba hio , ilikuwa na vyumba kadhaa ambavyo kwa haraka haraka alijua kuwa kila chumba kilikuwa na walinzi wamelala , alisukuma kitasa cha mlango wa kwanza na kikakubali na jamboo hilo lilimfanya apate tumaini kwani aliingia kiulaini na kuzama ndani na hapo ndipo alipokutana na vitanda viwli kimoja kina mtu kalala na kingine kilionekana hakina mtu na hapo hisia zake zilimwambia kuwa chumba hicho kilikuwa ndio chumba anacholala mlinzi aliemzimisha nje .
Ni mvumo wa risasi ndio uliosikika kwa mbaali na kukifumua kichwa chamlinzi aliekuwa akikoroma huku damu zikitapakaa , baada ya kuona zoezi hilo limefanikiwa alitoka taratibu na kwenda kwenye chumba kinachofata kisha aligonga mlango maana chumba hicho kilikuwa kimefungwa kwa ndani na mara baada ya kugonga mlango ulifunguliwa na jamaa mmoja mnene alitokezea uso na hapo hapo carlos alitokea kwa mbele yake na kumnyooshea bastora huku akimpa ishara atokea nje ya chumba hicho na bwana yule kwa kutetemeka sana alitoka nje pasipo kelele na hakuchelewesha alitwangwa risasi na kisha carlos akaingia ndani kwa spidi , lakini bahati haikuwa yake kwani ile anaingia alijikuta akilambwa teke lililomyumbisha pembeni na bastora yake kudondoka , na hapo ndipo aliposhudia mwanaume alikuwa amevaa boksa akiwa amekunja ngumi , lakini usoni akionesha hali ya hofu mno jambo ambalo kwa carlos alilichukulia kama udhaifu .
“ wewe ni nani ?” lilikuwa swali kutoka kwa bwana huyo lakini carlosa aliona swali hilo alijibu kwa vitendo kwani alimsogelea bwana huyo kwa kasi na hakuchelewa alimpiga mapigo mawili yaliomzimisha chini , hakuwa na muda wa kupoteza maana alikuwa na dakika kadhaa za kufanya tukio la kumteka janeth kabla hajashtukiwa , aliinama na kuchukua bastora yake na kisha alimpiga risasi ya kichwa yule mlinzi na kusababisha damu kuruka mpaka kwenye mapazia .
Baada ya kuona zoezi lake limefanikiwa alirudi kwenye chumba cha kwanza na alipekuwa pekuwa na akaja kuibuka na rimoti moja ya rangi ya majivu na kutoka nayo nje na mara baada ya kutoka na kumpita mlinzi aliemzimisha ni kama alikumbuka kitu kwani aliangalia nyuma na kisha alimchapa risasi yule mlinzi na kisha alitembea kuelekea mlango mkubwa wa kuingilia ndani ya nyumba kubwa , alifika na kuminya kitasa na alikuta kilifungwa kwa ndani na kwa kutumia utundu wake sekunde chache tu tayari mlango ulikuwa umefunguliwa , alizama ndani na kukutana na sable huku mwanga wa taa za nje ukimulika ndani ya sable ile , hakutaka kwenda kwenye vyumba vingine kwani alikuwa akijua ni chumba gani janeth alikuwa analala .
Alitembea kama mwanajeshi komandoo na kufikia mlango wa chumba cha janeth juu ya floor ya kwanza ya nyumba hio na kisha alishika kitasa na kukinyonga na uzuri ni kwamba mlango haukufugwa kwa ndani alizama taratibu huku akiona mtu alielala kwenye kitanda na jambo hilo lilimfurahisha kwani kazi yake aliona inakwenda kuwa nyepesi , aliingia ndani lakini ni kama alikuwa anasubiriwa kwani ile anaingia tu kwa utaalamu wa hali ya juu mno janeth alimrushia shuka carlos na kumziba uso huku akitanguliza na front kick iliompata vyema carlos , lakini hakuwa mzembe kwani aliyumba nyuma kidogo mpaka kwenye kabati huku shuka akiwa amelitupa pembeni .
Sifa moja kuu ya carlos ilikuwa ni kuchukia kupigana na mwanamke halafu amshinde na ndio maana alivyo ona mpinzani wake yupo vizuri alitupa bastora nje kabisa ya mlango na wakaaza kuzipiga , janeth alionekana kuwa vyema kujihami na mapigo ya carlos lakini pia carlos na yeye alikuwa makini mno, wa kwanza kupigwa pigo mshitukizo ni carlos , kwani ile anakwepa teke la mrembo janeth , alijikuta akipigwa teke lingine lililounganishwa na roundhouse (pigo la kung fu ) na kumpeleka carlos chini , lakini carlos aliinuka kama mwanariadha na hapo aliona asipokuwa makini lazima azidiwe , jenth alimsogelea carlos kwa kasi lakini bahati haikuwa yake kwani ni kama carlos alikuwa akimsubiri kwani alivutwa mbele na kutua kwenye kifua na bila kuchelewesha alipigwa kwenye shingo na hapo hapo akalegea na kudondoka chini huku nguo yake ya kulalia ikiusaliti mwili .
Carlos alimwangalia janeth kwa uchu , lakini hakutaka kufanya ujinga , alimbeba begani na kisha kutoka hadi nje , kwa kutumia rimoti aliokuwa amechukua kwa mlinzi alifungua geti na kutoka mpaka nje na kisha alilifunga na kurusha rimoti ndani na kisha akaenda kumpakia janeth kwenye gari yake akiwa hajitambui kabisa na kutokomea , akiwa amekamilisha kazi yake kwa asilimia mia moja .
******
Asubuhi siku nyingine kabisa mtu wa kwanza kufika nje ya nyumba ya janeth alikuwa ni abasi lakini kilicho mshangaza abasi ni mara baada ya kupiga honi mfululizo pasipo kupata majibu , hali hio kidogo ilimtia hofu kwani nyumba hio ilikuwa na walinzi alishuka kwenye gari yake na kulisogelea geti na kisha aligonga lakini bado hakupata mafanikio , akiwa amesimama nje anawaza alikuja mwanamama mmoja ambae abasi alimtambua , kwani alikuwa ni mfanyakazi aliekuwa akihusika na maswala ya upishi na usafi wa nyumba hio .
“ kuna nini ?”
“ hakuna anaeitika nimegonga mara kibao “.
“ kwahio tunafanyaje “
“ngoja nijaribu kupiga simu “ aliongea abasi na kuingia kwenye gari yake na kuchukua simu na kuanza kupiga , lakini simu iliita bila kupokelewa , alipiga simu kwa moja ya walinzi lakini pia simu iliita bila kupokelewa na hapo kengele ya hatari iligonga kwenye kichwa chake , alizunguka hadi nyuma ya ukuta na kisha aliuparamia na kwenda kutua chini ,na kusogelea upande wa getini na kitu cha kwanza kukutana nacho ni rimoti ya geti , alisogea zaidi na hapo ndipo moyo wake ulipiga kite na hio ni ,mara baada ya kumuona mlinzi akiwa amechanguliwa kichwa vibaya , alijikuta akisahau hata kufungua geti ili mwanamke aliepo nje aingie ndani kwani alikimbilia ndani huku akiita jina la janeth , lakini alikuta nyumba imetulia , alienda mpaka kwenye chumba cha janeth na kukuta patupu huku simu yake ikiwaipo kwenye ‘bedside’.
Hapo moja kwa moja akili yake ilimwambia kuwa tayari janeth alikuwa amekwisha kutekwa , alijikuta akikaa chini huku akitamani kulia , alichokumbuka muda huo ni kwenda upande wa kamera na kuangalia kilichorekodiwa , alitoka na kwenda moja kwa moja upande wa kushoto mita kadhaa na chumba cha janeth na kufungua mlango na kisha aliwasha laptop na kuanza kuangalia matukio ya siku hio na hapo ndipo aliposhuhudia mwanaume akiingia ndani ya nyumba hio kwanzia mlango mkubwa ambapo ndipo sehemu ambako kulikuwa na kamera mpaka kwenye cchumba cha janeth , mpaka alipomuona mtu huyo aliejiziba uso akitoka huku akiwa amembeba janeth , hakujua mtu huyo ni nani kwani mwanga ulikuwa hafifu mno kwani taa zilikuwa zimezimwa , lakini alichogundua kuwa mtu alietekeleza jambo hilo alikuwa ni mwanaume .
Alijikuta akitoa simu yake ya mkononi na kupiga , na dakika chache simu ilipokelewa .
“ sabi upo wapi ?”
“ nipo na mheshimiwa ndio tunaelekea uwanja wa ndege nasafiri kwenda marekani sasa hivi kuna nini? “
“ janeth “
“ kafanya nini “
“ katekwa “
“ nini? “
“ ndio yaani na sijui ni nani kafanya tukio hilo kwani ni mwanaume aliekuwa amejiziba uso “.
“sasa abasi nakusaidiaje , maana ndio nafika airport hapa na mheshimiwa “
“ wewe nenda tu nitajua cha kufanya , ila inabidi swala hili tulifanye kimya kimya madam asijue “
“ hakuna shida , hakikisha unanipa kinachoendelea , ukijua alipo wataarifu polisi pia “
“ poa “
*****
Saa moja kamili ndio muda ambao jeneth alizinduka , hakujua ni eneo gani alipo , ila alikuwa akikumbuka tukio la jana lote lililotokea , chumba alichokuwepo kulikuwa na kitanda na godoro ambalo halina shuka akiwa amefungwa mikono na miguu , huku mwanga hafifu ulioashiria kuwa muda huo ni asubuhi ulimurika ndani ya chumba hicho .
Janeth alijaribu kujinasua lakini aliona ugumu wa aina yake , na hapo hakuwa na jinsi kabisa , aliona siku hio kakamatika kweli .
Dakika chache mbele mlango ulifunguliwa na aliingia carlos cardosso awamu hii alikuwa hajajifunika kabisa uso wake .
“ wewe ni nani ?”
“ you fuk__ng bitch , stay quite before I lose my patient “ wewe kunguni tulia kimya kabla sijapoteza uvumilivu wangu
“ who are you “
“you don`t need to know who I am , what you need to know is that your day to go to hell are numbered “ huna haja ya kunijua mimi ni nani , unachopaswa kufahamu ni kwamba siku zako za kwenda kuzimu zinahesabika “ aliongea carlos huku akiwa amemsogelea kabisa usoni janeth akiwa amemkazia uso , lakini kwa janeth na yeye hakumchelewesha kwani alimtemea mate usoni na kumfanya carlos anyanyuke na kuyafuta huku akiwa kama hajakasirika , lakini fasta janeth alipokea kibao cha uhakika kilichomgeuza upande mwingine na hapo simu ya carlos ilitoa mlio kuashiria ilikuwa inaita aliangalia na kuona ni boss aliekuwa anapiga , alitoka mpaka nje ya chumba hicho na kuja kutokelezea kwenye moja ya sable kubwa kubwa yenye makochi ya mbao, huku kukiwa na baadhi ya wanaume wenye miili ya mazoezi wakiwa wanavuta sigara .
“ yess boss “
“ carlos make sure that bitch talks aboaut her boss, proceed with first class torture if she doesn’t cooperate “ carlos hakikisha huyo Malaya anaongea ni nani boss wake , akikataa kuongea mpe mateso daraja la kwanza .”
“okey boss “
Ilikuwa ni simu kutoka kwa kimbona aliekuwa akimpa maelekezo ya kipi carlos alichotakiwa kufanya , mara baada ya simu ile kukatika , carlos alimpa ishara moja ya wanaume wale waliokuwa wakivuta sigara na dakika kadhaa mwanaume yule alitoka na kuja na box kama la huduma ya kwanza na kisha aliongozana na carlos kwenda kuingia kwenye hiko chumba na kisha janeth alifunguliwa kwenye kile kitanda na kisha alifungwa kwenye kiti kwa ajili ya zoezi la mateso kuanza baada ya kumfunga jeneth huku kigauni chake kikiacha mapaja yake yalionona nje jambo ambalo wale wanaume waliangalia kwa matamanio.
“ boss can we talk out there “.boss tunaweza ongea kidogo hapo nje “ aliongea yule mwanaume mweusi kama mkaa akimpa ishara carlos , na carlos aliitika na wakatoka hadi nje kidogo “”
“what do you want to talk about Dario “ unataka kuongea nini Dario .
“how do you think if we *** her first , she is hot I cant stand it “unaonaje tukijilia vyetu kwanza kabla ya kumpa mateso mtoto mrembo mno siwezi vumilia “ aliongea Dario huku pepo la ngono likiwa linafanya kazi yake kwa kiwango cha 4G .
“ I think you have made a point but I will be the first to *** bcoz I did all the work myself and don’t tell the boys until we finish “nadhani umeongea point ila nitakuwa wakwanza kufanya maana nimehaingaika mimi mwenyewe na usiwaambie vijana mpaka tumalize “ aliongea na hapo darius alitoa jino lake lenye kutu kwa furaha .
“ you wait here until I finish the first round “ wewe suubiri hapa mpaka nimalize round ya kwanza “ aliongea carlos na darius alimuonesha alama ya dole gumba kukubaliana nae na carlos akazama .
Janeth alikuwa na wasiwasi mno , hisia zake zilimwambia tu kwa vyovyote lazima abakwe siku hio , kwani macho ya uchu alioyaona kutoka kwa watekaji wale alijua tu lazima huko nje walipokuwa wameenda kuongea ni kwenda kujadili mpango huo .
Na kama alivyotegemea ndivyo kilichokwenda kufanyika , kwani baada ya carloss kuingia alimtoa janeth kwenye kile kiti na kumrudisha kitandani na kumfunga mikono vizuri na mguu mmoja akaufunga mashariki na mwininge magharibi , na alivyoona zoezi lake limefanikiwa alilegeza mkanda wa suruali yake ya jeans ,ilishuka na kubaki na boksa tu , hakutakka kuvua yote maana alijua kuwa pia yupo kazini , janeth alishuhudia mdubwana wa carlos ulivyotuna ,hakuweza kupiga kelele kwani muda huo alikuwa ameshindiliwa matambala mdomoni , carlos alisogea na kupanda juu ya kitanda na kisha alikipandisha kigauni cha janeth .
Janeth hakuamini kama siku hio ndio anakwenda kuliwa tunda lake alilolitunza kwa miaka mingi pasipo kukutana na mwanaume yoyote yule , kwake aliamini baada ya kitendo hicho hatakuwa na thamani tena , kitendo cha kubakwa kwake ni Zaidi ya kuuliwa kuliko kufanyiwa kitendo hicho , kwa jinsi alivykuwa amefungwa hakujua kama anakupona siku hio , alichokifanya ni kufumba macho ili kusubiria unyama unaoenda kutendeka hhuku akimuomba mungu kutokee muujiza .
ITAENDELEA
SEHEMU YA 44
Carlos alitoa mhogo wake na kisha alitema mate na kuupaka vizuri kwa ajili ya kazi yake , lakini ile anavuta nguo ya ndani ya janeth , mara mlango uligongwa kwa nguvu , kitendo kilichomkasirisha na kutoka nje kwa hasira na alijua yote hayo ni wivu wa dario na alidhamiria kumfanyia mbaya , ile kutoka na mihasira yake lilikuwa ni kosa kubwa sana kwani alijikuta akilwamba risasi mbili kifuani na kwenda mkumku chini huku damu zikitapakaa mlangoni .
Mtu aliekuwa ameshika bunduki alikuwa ni damiani mwenyewe , tena huyu akiwa ni yule original asie na ngozi feki , sebleni hapo zilionekana damu zilizokuwa zimetapakaa kila kona , huku mwili wa dario ukionekana ukiwa chini huku dudu yake ikiwa nje kabisa na alionekana kabisa wakati mwenzake akiwa ndani basi na yeye alikuwa akipooza pooza dudu yake .
Damiani hakutaka kuchelewa , alikuwa amecahafukwa na roho ya kikatili mno , hakuonesha huruma hata kidogo , kwani damu zilizotapakaa eneo hilo zilionesha kuwa mtu alieingia eneo hilo alikuwa ni Zaidi ya hayawani .
Aliingia ndani ya chumba alichokuwemo janeth , na kumfanya jenth atoe machozi mara baada ya kumuona mwanaume damiani akiwa mbele yake , damiani alimfungulia na kumtoa matambara , , kitendo cha janeth kufunguliwa tu alijikuta akimkumbatia damiani kwa nguvu huku akilia kwa kwikwi , damiani alimbembeleza jeneth na kisha walitoka eneo hilo m mpaka upande wa barabarani na kuingia kwenye gari .
****
MASAA TISA NYUMA
Kwa janeth ilikuwa ni kama ndoto , kwani wakati huo alipkuwa usingizini alikuwa akiota kabisa kuna mtu kavamia nyumba yake , alijikuta akikurupuka , lakini wakati huo anakurupuka ndio wakati ambayo mlango wa nje ndio ulikuwa ukifunguliwa kwani alisikia ufunguo ukidondoka chini , alijikuta akipatwa na waswasi , na kukimbilia dirishani na kuangalia getini na hapo ndipo alipomshuhudia mlinzi akiwa chini alikimbilia simu yake na kutafuta namba ya abasi na kuipiga lakini haikupatikana kitendo kilichomfanya aachie tusi , hakujua ni mtu gani wa kumpigia muda huo na alijikuta akiwa amepiga namba ya damiani , lakini kabla hata hajaongea tayari kitasa cha mlango kilikuwa kishashikwa na hapo hapo alitupa simu pembeni huku simu ikipiga na kujifunikashuka gubigubi .
Huku upande wa damiani kama ilivyo kawaida yake ya kuchelewa kulala , saa sita kama na robo ndio aliingia kwenye chumba cha kulala , masaa machache mara baada ya kulala simu yake ilitoa mlio ikiashiria kuwa inaita , jambo ambalo lilimkurupusha na pia kumshangaza , hakujua ni nani anaweza kumpigia simu usiku huo maana haikuwa kawaida . .
Alijikuta akipokea simu mara baada ya kuona aliekuwa akipiga ni janeth , sauti ya kwanza kusikia , ilikuwa ni kishindo na hapo hapo akasikia sauti ya janeth “ wewe ni nani “ hapo hapo kwa akili yake ya haraka alikuwa ashajua kuwa kuna jambo la hatari lililokuwa linamtokea mrembo huyo , alijikuta akitoka kitandani mkumku huku simu bado ikiwa sikioni , sauti ya mwisho kuisikia , ilikuwa ni mguno wa wa mwanaume na hapo hapo hakusikia tena sauti .
Kilicho mchanganya kwa wakati huo hakujua ni wapi nyumbani kwa janeth kwani hakuwa na mazoea na mrembo huyo ya kujua ni mahali gani anaishi na laiti angekuwa anapajua basi angeendesha gari yake moja kwa moja mpaka eneo hilo .
Angekuwa na utaalamu wa wa komputa huenda na program kadhaa huenda kwake ingekuwa rahisi, lakini sasa uwezo huo hakuwa nao kabisa , alichokumbuka ni bastora yake aina S&W Model 12-9 aliokuwa ameihifadhi kwenye kabati , aliichomoa na kuvaa suruali yake ya jeansi na tisheti ya timberland na koti,na kutoka nje na kuingia kwenye gari yake aina ya BMW X8 , wazo alilokuwa nalo muda huo lilikuwa ni kwenda kurasini , lakini kuna wazo jipya lilimjia na wazo hilo ni kumpigia simu luangshu kwani aliamini muda huo china itakuwa ni muda wa asubuhi .
Dakika kadhaa tu simu ilipokelewa.
“ hello luang shu I am in very urgent emergency and I want to acces dreamer T by phone to find someone location “ habari luang shu nina dharula ya muhimu mno , nauliza kama ninaweza kupata mawasiliano na dreamer T kwa kutumia simu kujuaa mtu alipo “
“ yes its very simple dial the number I refer to in the usual way 0001” ndio ni rahisi sana piga namba ninazo kutajia kwa njia ya kawaida sifuri sifuri sisfuri moja “ aliongea na hapo hapo damiani alipiga namba zile na kuweka sikioni na hazikupita hata sekunde tayari simu ishapokelewa .
“welcome to DREAMER T global service , how may I help you ?” karibu kwenye DREAMER T huduma kwa ulimwengu , je unataka nini nikusaidie “
“ I need to locate someone, janeth bendera “ nataka kujua mtu alipo , anaeitwa janeth bandera .
“please wait our T to process your request “.tafahari subiri T akijaribu kufanyia kazi ombi lako “
“your request has been approved , a messege has been sent with a link that will direct you to the location where janeth bendera is “.ombi lako limefanikiwa meseji imetumwa kwako iliambatana na link ambayo itakuunganisha na mtu unaemtafuta .
“okey thank you “
Damiani alifungua ujumbe ule na kisha alifungua link ambayo moja kwa moja ilimpeleka mpaka kwenye google map iliokuwa ikionenyesha kialama chekundu kilichokuwa kikitembea , aliangalia eneo husika aliona janeth muda huo alikuwa anapita bunju na yeye wakati huo alikuwa yupo anatokelezea mbezi huku akifatilia mshale uliokuwa ukionesha uelekeo .
Masaa machache baadae ndio muda alifanikiwa kufika mpaka mwisho wa mshale ulipokuwa ukimpeleka , na alikuja kusimamisha gari barabarani eneo moja lililokuwa likifahamika kwa jina la kerege bagamoyo , alipita kanisa moja la roman na kusonga mbele huku akipata uelekeeo kupitia simu yake na mpaka anakuja kusimama kwenye nyumba moja kubwa iliokuwa na ukuta ndipo alipo pozi hapo , aliangalia hapo na kuona kuwa huo sio muda sahihi wa kuvamia eneo hilo kwani alijua kuwa lazima watu hao watakuwa wapo makini kwa muda huo , alichofanya ni kurudi barabara kuu na kuingia ndani ya gari na kwenda kusimamisha gari yake kwenye ofisi moja ya kata na kutulia hapo .
Saa moja kamili ndio muda ambao alikuwa akivamia eneo hilo na a aliingia kiulaini kupitia getini baada ya kumpiga pigo takatifu mtu aliekuwa akilinda geti baada ya kutoka kizembe na kisha alizama ndani na hapo ndipo alipochapa watu risasi bila huruma , alikuwa akipiga risasi huku akikumbuka tukio la mama yake kuuwawa kikatili na wala hakuogopa kabisa damu ambazo zilikuwa zikirukia kwa muda huo aliamini akileta uchungaji/ushekhe tu basi watu hao wangesmhambulia yeye ..
******
Moja ya watu ambao walikuwa na taarifa ya kutekwa kwa janeth alikuwa ni suzzane(miss k agent) , kwani tukio zima yeye mwenyewe alikuwa akilijua na hata mipango yote ya carlos alikuwa akiijua , alitaka kumtumia carlos kutekeleza jambo hilo ili iwe kwake rahisi kupata kujua kuwa janeth ni nani kupitia kwa carlos .
Hata taarifa za vyombo vya usalama vilivyoripoti tukio hilo kwake alitabasamu na kuona kuwa carlos alikuwa amefanya kazi kikamilifu kama alivyotegemea na ndio maana asubuhi hio aliongea na carlos wakutane eneo la bagamoyo kwa ajili ya kumfanyia mahojiano janeth .
Alikuja kupishana na gari alililopanda damiani akiwa na janeth karibu kabisa na shue ya sekondari baobab , na wala hakujua kuwa ndio aliikuwa anapishana na mtaalamu damiani ambae ametoka kufanya mauaji ya majambazi sugu au washirika wake .
Dakika tano pekeee alikuwa akikatiza kweye njia ya vumbi upande wa kushoto mkabala na kanisa la romani akielekea mafichoni alipokuwa ameelekezwa na carlos , baada ya kufika eneo hilo alisimamisha gari nje ya geti na kisha akaingia ndani pasipo kugonga na hapo ndipo aliponusa hali isio ya kawaida , maana komandoo huyu na jasusi alikuwa na machale balaa , alitoa bastora yake na kuiweka mkononi na kisha alifungua mlango wa sebleni na hapo ndipo alipopigwa na mshangao wa aina yake kwani damu zilikuwa zimetapakaa kila mahali , aliangalia kulia na kushaoto lakini hakuona alichokuwa akitafuta na alijikuta kwa umakini wa hali ya juu akitembea kuelekea mbele upande wa kulia na hapo ndipo alipokuja kukutana na maiti ya dario , na baada ya kuangalia upande wa kulia mlangoni ndipo alipomuona carlos , alimkimbilia na kisha alimwinamia huku akivaa gloves zake na kisha alimshitua na hapo kwa hali ya taabu sana carlos alifumbua macho .
“ carlos what happened here?? “
“daa.. daa.. miani “ aliongea carlos na hapo hapo akakata moto na kuwa wa baridi “ .
Suzzane hakutaka tena kubaki eneo hilo alitoka huku akiwataarifu polisi juu ya tukio hilo huku akiendesha gari lake kurudi alikotoka .
‘damiani .. inamaana damiani amerudi , kwa hali ile nilioikuta damiani atakuwa ni hatari na mkatili mno , anafanana na carlos tu “ aliongea suzzane huku aking`ata meno yake kwa hasira wakati huo akipishana na diffenda ya polisi iliokuwa ikielekea eneo la tukio ikitokea kituo cha polisi mapinga .
Tukio la kutekwa kwa janeth na kuwawa kwa walinzi wake lilisambaa kwa kasi sana kwenye vyombo vya habari na hio ni baada ya tukio hilo kuthibitishwa na mkuu wa polisi kanda maalumu ya dar es salaam , tukio hilo halikuishia kwa wananchi tu pia lilimfikia mke wa raisi wema au mama Patrick .
Jambo hilo lilimpelekea mshituko mno mama huyo kiasi cha kuanza kupumua kwa shida na mtu aliemuona kwa mabadiliko hayo alikuwa ni mfanyakazi wao wa ndani aitwae zainabu , alimtuliza kwa kumpa maji na hapo kidogo hali yake ilikaa sawa alichukua simu yake na kupiga kwa abasi .
“abasi unafanya kazi gani , nimekupa kazi ya kumlinda mwanangu , mpaka anatekwa wewe ulikuwa wapi ??“ .
“ nisamehe madam , jana nilipata dharula sikuwepo”.
“hayo sio mambo ya kuniambia mimi , namtaka mwanangu akiwa hajadhurika lasivyo utanitambua mimi ni nani “ aliongea mke wa rasi kwa jazba kweli huku akikata simu na kukaa kwenye sofa akihema kwa nguvu .
Polisi walikuwa wakifatilia kwa ukaribu sana tukio hilo akiwepo DCP (deputy commissioner) bwana barangwa mahimbo bwana huyu alikuwa na usongo kweli na kuhakikisha kuwa anawapata wahalifu akiongozwa na mwanadada aliepokea cheo cha usajini wa polisi (seargent )hawa takamoyo , wengi polisi wanamuita sajini au sajent taka vya moyo jina lake la utani .
Hawa baada ya kufika eneo la tukio kwa kuongozwa na abasi waliweza kufatilia kamera za ulinzi ndani ya eneo hilo , na hawakuambilia sura ya mtu huyo japo waliweza kipata muonekano wa mtu huyo , kamishina msaidizi alitoa maagizo wa sajent takamoyo kuhakisha ufatiliaji unafanyika kwa umakini wa hali ya juu mno .
“sajent hakikisha watu hawa tunawakamata mara moja , fanyeni upekuzi wa kila mahali kumbaini mhusika wa hili , kazi hii nataka isifike saa sita mchana iwe ishakamilika na proffesa janeth awe amepatikana na wahusika wafikishwe mbele za sheria “
“ sawa afande “ alipiga saluti na kazi ya msako ikaendelea , vijana waligawanyika kila kona ya jiji kuhakikisha kuwa wahusika wanapatikana , lakini sajenti nusu saa baada ya kuagana na kamishna msaidizi wa polisi bwana barangwa , alipokea simu kutoka kwa kamishna mwenyewe kumtaarifu kuhusu mauaji yaliofanyika bagamoyo .
Mara baada ya sajenti kupokea taarifa hio aliingia kwenye difenda na kuelekea eneo la tukio , dakika arobaini ziliwatosha kabisa kufika ndani ya eneo hilo na kuanza kupiga picha na kuchukua baadhi ya vielelezo ambavyo vingewasaidia katika upelelezi wao .
“carlos cardosso “ ni jina lililotamkwa na sajenti takamoyo mara baada ya kumgundua ,alikuwa akimfahamu vyema mtu huyo kwani anakumbuka tukio la kushambuliwa eneo la mikese na mtu huyo kutoroshwa wakati akisafirishwa kwenda gereza la morogoro , na kuanzia siku hio sajent takamoyo japo ya kuambiwa kesi hio isifatiliwe lakini kwake jambo hilo halikuwa swala la kulifumbia macho kwani kimya kimya alilikuwa akifanya upelelezi wa kujua kwanini siku ile walisahambuliwa kwa sindano za usingizi na mfungwa huyo kutoroshwa na pia isitoshe maagizo kutoka kwa wakubwa yakimtaka swala hilo liwe siri na lisifatiliwe , sintofahamu ya jambo hilo ndio iliomsukuma kutaka kujua Zaidi , maana kati ya moja ya polisi waliokuwa wazalendo na taifa basi ni mwanadada huyu sajenti takamoyo , ukimuona njiani akiwa na mavazi ya kawaida hutoamini kuwa alikuwa ni sajent wa polisi , maana alikuwa ameumbika haswa na sura yake ya kirangi , sura nyeupe , na umbo lake namba nane vilimfanya we mzuri kweli , lakini licha ya uzuri huo alipenda kazi ya polisi mno , alikuwa akipenda kukamata sana waharifu na kutokana na tabia yake alikuwa amefanikiwa kutokomeza sana uhalifu ndani yajiji la dar mpaka kupelekea kazi yake kuonekana kwa wakubwa na kupandishwa cheo na kuwa sajent .
Carlos cardosso ni jina lililomjia mara baada ya kuona sura hio ya mwanaume wa kibrazili akiwa amefumba macho akiwa mfu , kitendo cha kumkuta mwanaume huyo kuwa mfu aliamini kabisa mtu aliengia ndani ya eneo hilo na kutekeleza mauji ya carlos alikuwa ni mtu hatari sana .
Alichokifanya ni kuanza kuangalia mazingira ya hapo ndani na hapo ndipo alipokuta Kamba kwenye kitanda na kwenye kiti na pia vifaa vya kutesea watu alijaribu kuvuta picha ya eneo hilo na hapo alijua kabisa kuna mtu alikuwa amefungwa kwenye kitanda , alizidi kuvuta picha na hapo aligundua kuwa kuna mtu mwingine alieingia na kumuokoa mtu aliefungwa kwenye kitanda , hapo hapo alikumbuka video ya kamera alizochukua kwenye nyumba ya janeth za mwanaume alieingia ndani akiwa amejiziba uso , na hapo ndipo alipo jaribu kufananisha mwili wa carloss na jibu moa kwa moja likaja uwa mtekaji alikuwa ni carlos, na pia alijua kabisa kuwa janeth alikuwa ameokolewa na mtu aliefanya mashambulizi na kuuwa majambazi hayo .
Alipiga simu moja kwa moja kwa kamishina na kumpa maelezo ya tukio zima na pia uwezekano wajaneth kuwepo kwenye eneo hilo .
“ kama hayo usemeyo ni kweli , sasa hivi hakikisheni mnajua ni wapi janeth alipo maana yeye ndie atatoa maelezo kamili ya tukio zima “
“ sawa afande “
ITAENDELEA .
SEHEMU YA 45
“ulijuaje niko pale “ lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa janeth kwenda kwa damiani aliekuwa akitengeneza kifungua kinywa wakati huo janeth alikuwa amevaa tracksuti aliopewa na damiani alikuwa amesimama akimwangalia damiani aliekuwa bize .
“si ulinipigia simu jana wewe “
“kumbe ulisikia?? “
“ ndio , nilisikia purukusahani ndio nikajua kuwa upo kwenye hatari “
Aliongea damiani pasipo kugeuka nyuma , huku upande wa janeth alikuwa akimwangalia damiani hammalizi alikuwa akitabasamu , na kushukuru kwa wakati mmoja ,, kwani akikumbuka tukio lile la kutaka kubakwa , lilikuwa likimsisimua sana na kufanya nywele zake zisimame kwa woga na mwili kuwa wabaridi .
“asante sana damiani , ungechelewa kidogo tu nadhani sasa nisingekuwa janeth tena “.
“njoo chukua haya mayai tukanywe chai , kwanza sahau yaliopita yatakuumiza kichwa sawa “ aliongea damiani huku wakielekea dining na kutenga chai na kuanza kunywa , janeth tabasamu lililokuwa usoni mwake usingeamini kuwa ni mtu aliekuwa ametoka kuekolewa muda mfupi uliopita , alikuwa akinywa chai huku akimwangaia damiani na kutabasamu .
Baada ya kumaliza kunywa chai ndipo janeth alipomkumbuka mama yake na pia abasi kwani aliamini sasa hivi watu hao wangekuwa kwenye tafrani isio kifani ya kutaka kujua usalama wake , alimuomba damiani simu yake na kwakua namba alizokukuwa akikukumbuka ni za mama yake basi ndio mtu alieona ampigie .
Madam wema ama first lady alikuwa kwenye wasiwasi mmno , kila saa alikuwa akimpigia simu abasi kujua kinacho endelea , lakini taarifa zilikuwa zikimvunja moyo mno hakujua mwanae kama yupo salama , hata chai hakuweza kunywa kabisa siku hio inapitaje kwa mfano sasa mtoto unaempenda katekwa .
Muda wa saa nne kamili ndio namba mpya ilipopiga na kwa haraka haraka aliipokea na kuweka sikioni .
“ mom “ ilikuwa sauti ilisikika kwenye masikio ya mwanamama huyo .
“janeth uko wapi mwanangu , uko salama , uko wapi nitakufa mimi mama yako “
“niko sawa mama nilitekwa ila nimeokolewa mom niko salama usiwe na wasiwasi “
“ uko wapi kwasasa nataka kukuona “
“mama tunataonana niko sehemu salama , mwambie na abasi atakuwa na waswasi “ aliongea upande wa pili na kumfanya mama huyo kuhema kwa nguvu na kukaa chini ya sofa na kumshukuru mungu na simu ilikatwa .
“asante mungu , bendera mtoto wetu kapona “ aliongea mama huyo huku akionekana kuwaza mbali mno na kukumbuka maisha yake ya nyuma .
*****
HISTORIA YA MKE WA RAIS
Ni kipindi cha miaka yangu ya nyuma , kipindi hicho nikiwa binti mdogo kabisa wa miaka kumi na sita , nikiwa katika umri wa kuvunja ungo , kipindi hichi nilikuwa nikisoma shule ya sekondari songea girls,nilikuwa moja ya wasichana wapole sana wenye nidhamu ya hali ya juu ndani yashule yetu , japo sikujaliwa akili sana kama wanafunzi wengine lakini kwa uwezo mdogo niliokuwa nao nilikuwa nikijitahidi sana kusoma ili kufaulu katika masomo yangu hususani kipindi hicho nikiwa nipo kidato cha nne , kipindi hicho kufaulu kwenda kidato cha sita ilikuwa kazi ngumu mno kwa miaka yetu , kwani ilikuwa ikihitajika kazi kubwa ya kujisomea hasa kwa baadhi ya watu kama sisi ambao hatukua na iq kubwa kama wengine .
Licha ya kuwa mpole , nadhifu na nidhamu lakini pia nilikuwa moja ya wasichana ambao niseme kuwa tulikuwa tumejaaliwa uzuri , sio kama najisifu lakini huo ulikuwa ni ukweli , na mimi mwenyewe nilikuwa nikikiri hilo , lakini uzuri kwangu kuna muda mwingine niliona kama mateso , kwani ni mara nyingi nilikuwa anikitongozwa mpaka na baadhi ya walimu ndani ya shule yetu , jambo hilo lilikuwa ni changamoto kubwa sana kwangu kwani baadhi ya walimu ambao niliwakatalia walikuwa wakinitishia kunifelisha katika masomo yangu , moja ya walimu hao alikuwa ni mwalimu mmoja aliekuwa akifahamika kwa jina la mwalimu rama au mwalimu pengo kama alivyokuwa akifahamika kwa jina lake la utani kwani alikuwa na pengo , mwalimu huyu alikuwa akinitaka kwa muda mrefu sana lakini nilikuwa nikimkataa , sikua nikimpenda hata kidogo lakini pia sikutaka kujiharibia mimi mwenyewe kwa tamaa za mwalimu huyo , kwani nilijua madhara yake , lakini mwanzo wa kumkatalia mwalimu huyo ndio ukawa mwiba kwangu kwani alikuwa akiniferisha makusudi kabisa katika masomo yake aliokuwa akifundisha , hali hio ilinitia mawazo sana mpaka baadhi ya marafiki zangu wakaniambia nimkubalie lakini kwangu nilikataa katakata , nilitamani kwenda kusema ngazi za juu , lakini mtu aliekuwa huko ngazi za juu na yeye alikuwa akinitaka kimapenzi ,jambo ambalo niliona hakuna msaada wowote ambao ningepata , niliishi hivyo hivyo kwa kusoma kwa bidii huku nikiamini kuwa mtihani wa mwisho kwakuwa mwalimu huyo sio yeye anayehusika na kusahihisha basi niliamini hata afanyeje nisingeweza feli .
Mwezi wa tisa ndio mwezi ambao watu wengi walikuwa kwenye harakati za kujiandaa na mtihani wa moko , siku hio nikiwa ninajisomea na marafiki zangu alikuja headgirl wetu aliekuwa akifahamika kwa jina la mary singano , alikuja mpaka tulipokua tunasomea na kuniomba nikaongee nae pembeni , sikujua alikuwa na jambo gani la kuongea na mimi kwani kipindi hicho sikuwa na mazoea naye kabisa .
“wema nimekuita hapa kuna jambo nimelisikia kutoka kwa moja ya marafiki zako”
“ rafiki yangu nani na ni jambo gani? “
“hilo sio la msingi lakini naomba unisikilize “
“ndio nakusikiliza “
“ni kweli mwalimu rama anakufelisha masomo yako makusudi kwasababu ulimkatalia “ nilijikuta nikimwangalia headgirl kwa mshangao lakini wakati nikimwangalia nilijikuta machozi yakiwa yamenijaa mashavuni na hatimae kilio kabisa .
“ mbona unalia sasa wema , nimekuuliza naomba uniambie nataka kukusaidia “
“ ni kweli mary“ niliongea huku nikiwa na uchungu moyoni kwani ni kipindi kirefu nilikuwa nikivumilia jambo hilo na ni kama leo nimepata sehemu ya kulisemea , nilimwambia kila kitu headgirl juu ya jambo hilo .
“kuna mtu anataka kuonana na wewe “
“ nani ?“
“ utamjua ila ni kiongozi pia kutoka shule ya songea boys ni kaka mkuu kule “ aliongea mary na kunifanya nikae nifikirie .
“ kwanini anataka kuonana na mimi ??“.
“nimemwambia kuhusu swala lako mimi kama kiongozi na kwakuwa yeye kapewa jukumu hilo na mkuu wa wilaya ndio anataka akusaidia kufikisha malalamishi yako “
“ sawa nipo tayari kuonana nae “ niliongea huku nikijikuta nikipata tumaini .
Siku moja mbele nilikutana na kiongozi huyo , kwakweli siku hio baada ya kuonana nae nilijikuta mapigo yangu ya moyo yakibadilika , nilikuwa nimevutiwa mno na kaka huyo , kwa muoenekano wake alikuwa ni moja ya watu waliokuwa wakionekana kujiamini mno .
“naitwa john bendera ni headboy kutoka shule ya sekondari songea boys , nimefika hapa kwa ajili ya kuongea na uongozi wa shule yenu na hii ni mara baada ya mkuu wa wilaya kusikia tetesi juu ya wanafunzi kutumikishwa kingono katika mashule mengi yaliopo songea , hivyo nikawa moja ya watu ambao nimeteuliwa kufanyia uchunguzi swala hilo ndani ya shule hii , nishaelezwa kwa kifupi na headgirl hivyo nataka pia unipe maelezo yako wewe mwneyewe “ basi japo alikuwa akiongea ila kwangu mawazo yalikuwa kwingine kabisa , sijui ni kwa jinsi nilivyokuwa nikitongozwa na wanuume au laah kwani nilitamani bendera aniambie kuwa ananipenda ila sio kumwambia maswaibu yangu , alivyoniona nipo mbali kimaawazo ndipo aliponirudisha kwenye mstari na hapo ndipo nilipomueleza mkasa wangu wote na kuahidi kuwa atalifanyia kazi .
Siku nne mbele yaani ijumaa ndio siku ambayo mkuu wa wilaya alifika ndani ya shule yetu , alikuwa ni mwanamama mmoja mnene alievaa wigi , alifika ofisini kwa mkuu wa shule na mimi nikaitwa , lakini huwezi amini nilikutana na wadada watano wakiwa na malalamiko sawa na yangu wakimtuhumu mwalimu rama kuwatongoza nilijikuta nikizidi kumchukia mwalimu rama , japo alikuwa akinitongoza lakini nilitamnani yale aliokuwa akiniambia kuwa ananipenda kuwa yana ukweli wake lakini kumbe nia yake ilikuwa ni tamaa tu .
Basi mwalimu rama mbele ya mkuu wa wilaya na afisa elimu aliambiwa ajitetee . lakini maji yalikuwa yamemfika shingoni kwani mwisho wa siku alionekana kabisa hatukuwa tukimsingizia maana mashahidi walikuwa wengi , hivyo alifukuzwa shule rasmi .
Kitendo kile kwakweli shujaa wangu alikuwa ni bendera kwani niliamini pasipo yeye nisingetoka katika kifungo kile cha kufelishwa mitihani makusudi kabisa , kwanzia siku hio hisia zangu za kimapenzi juu ya bendera zikachipuka , zikamea na hatimae kukomaa ndani ya moyo wangu , ilikuwa kila jumapili nikipata nafasi lazima nikamuone bendera, mwanzoni ilikuwa ni kama nikienda kumshukuru lakini mwisho wa siku nilishindwa kujizuia mbele yake na jambo hilo aliligundua vyema , lakini jambo la ajabu ni kwamba kwanzia siku hizo bendera alianza kuniepuka jambo hilo liliniumiza na kunifanya nishindwe hata kuwa makini na masomo yangu kwani ni muda mwingi nilikuwa nikimfikiria bendera tu .
Mpaka tunakuja kufanya mahafali ya mwisho ya kidato cha nne mwezi wa tisa mwishoni ndipo nilipo pata nafasi ya kuonana na bendera kwa mara nyingine na kilichonifurahisha siku hio ni kuhudhuria kwake na kuniletea zawadi pamoja na ua jekundu nilifurahi sana siku hio , japo wazazi wangu walikuwepo lakini sikuwa na habari nao mimi nilikuwa na habari na bendeera tu , kwani kila picha nilitaka nipigwe na bendera , kiasi kilichowashangaza mpaka ndugu zangu akiwemo dada yangu .
Baada ya mahafali kuisha ndipo nilipo onana na bendera nilianza kumlaumu kwa kitendo chake cha kuniepuka , lakini huwezi amini nilikuwa nishamsamehe muda mrefu tu , yaani kitendo cha kuja kwenye mahafali yangu ndio kilichonifanya nimsahemehe kwani kipindi alichokuwa ananikwepa nilikuwa nishamshemea mpaka maneno mabaya ya kumchukia .
Basi kwanzia siku hio penzi langu na bendera likazaliwa rasmi , na kuuanza haatua za awali za ukuaji na ukomavu , siku ya mahafali ya bendera ndio siku yenyewe ambayo bendera alinitoa usichana wangu na kuniingiza kwenye raha ya mapenzi , nakumbuka ni kwenye moja ya guest house iliokuwa ikipatikana eneo la bomba mbili usiku ndipo nilipovuliwa nguo ya ndani na bendera na kunitoa usichana wangu .
Kwanzia siku hio ndio nikawa nimekufa nimeoza kwa bendera , yaani nilikuwa siambiwi wala sisikiii muda wote kichwa changu ni bendera tu.
Basi mwisho wa kumaliza mitihani yetu ndio siku ambayo nililala mpaka kukakucha na bendera , ilikuwa ni moja ya siku moja ya furaha sana katika maisha yangu , maana raha nilioisikia siku hio na Amani moyoni mwangu naweza sema kwamba haitoweza jirudia maana nilikuwa wamoto kweli , siku hio ilikuwa ni kupika na kupakua .
“ bendera ndoto yako ni kuja kuwa nani baadae “
“mimi “
“ ndio wewe mpenzi kwani kuna mwingine humu ndani “
“ mimi nataka kuja kuwa raisi “.
“hahaha … ndoto kubwa hio mpenzi sidhani kama itakuja kutimia “
“ lazima itimie mimi nakuhakikishia hilo kabla sijafa lazima niitimize na wewe umekuwa mtu wa kwanza kujua ndoto yangu lakini pia utakuwa wakwanza kushuhudia kile nisemecho “.
“ ukiwa raisi na mimi nitakuwa mke wa raisi si ndio “
“ ndio kwanzia sasa hivi wewe ni first lady mtarajiwa“
“ hahaha .. jamani “nilijikuta nikifurahi mno kwa maneno ya bendera .
“ nakupenda sana bendera usije ukaniacha “
“ siwezi kukuacha mpenzi nakupenda pia “
Basi niseme kwamba siku ambayo kilamtu anapanda gari la kwenda kwao kwangu ilikjuwa huzuni mno ni kama niliona sitokuja tena kuonana na bendera , japo tulijiwekea ahadi kibao lakini bado niliona haitoshi , tuliahidiana kupendana daima lakini niliona bado nilimtaka bendera mimi .
ITAENDELEA
SEHEMU YA 46
Basi siku hatimae mwezi ukapita bila kuonana wala kuwasiliana na bendera kipindi hicho nikiwa nyumbani kwetu singida , lakini huwezi amini nilianza kupata mabadiliko ya mwili kuchoka kwa mara kwa mara na kula vitu vichachu na hata muda mwingine asubuhi kutapika ninaposkia harufu ya mayai , mtu wa kwanza kuona jambo hilo alikuwa ni mama yangu , alijua kabisa kuwa nina mimba na hata mimi kwa hali hio nilijua kabisa nina mimba .
Baada ya mama kujua hali yangu alinichukua mkuku mkuku mpaka hospitalini huku akiwa amechukia mno , nilipimwa na nikagundulika nina mimba , kwangu swala hilo lilikuwa la furaha sana japo nilikuwa nalia lakini nilikuwa na furaha moyoni nilikuwa nikilia kinafiki tu sikuamini kama nilikuwa na kiumbe cha bendera tumboni kwangu , nilijiliza mbele ya mama baada ya kunigombeza sana huku akitaka nimtaje muhusika , lakini mimi sikutaka kabisa kumtaja bendera nilijua lazima bendera angefungwa maana nilikuwa nikimjua vyema mama yangu kwa misimamo yake .
Mwisho wa siku nilimdanganya kuwa nimebakwa nikajiliza liza kwake mwisho wa siku akahudhunika lakini baada ya siku akazoea , lakini kimbembe kilikuja kwa baba sasa baada ya kurudi kutoka migodini kahama huko buzwagi akiwa na mali , baada ya kunigungua mjamzito alimshutumu sana mama kwamba alikuwa ananilea kwa kunidekeza na mwishowe ndio kasababisha mimi kupata ujauzito na kwanzia siku hio akampa mama yangu talaka rasmi , huku yeye akienda kuishi na mwanamke mwingine huko mwanza .
Sikuwa na mawasiliano kabisa na bendera tokea aende kwao geita na kipindi hicho njia kubwa ya mawasiliano ilikuwa ni barua , akukuwa na simu za mkononi .
Basi maisha yangu na mama yalikuwa magumu kwani mama hakuwa na ajira ya kuaminika , alikuwa akifanya viabarua vya hapa na pale ili kuhakikisha mimi mwanae sikosi kula na kuvaa , uzuri ni kwamba nilikuwa mimi tu kwani dada alikuwa amekwisha kuolewa Iringa huko .
Maisha yalienda mpaka nilipojifungua mtoto wa kike , nakumbuka kipindi nilichojifungua matokeo yalikuwa yashatoka , na kwa taarifa tu ni kwamba nilifaulu kwa daraja la nne ambalo halikuwa likiniwezesha kwenda kidato cha tano , kwa bendera nae niliambiwa na rafiki yake kuwa alipata daraja la tatu alama ambazo zilikuwa zikimuwezesha kwenda chuo , nilishangaa kwani moja ya watu waliokuwa ni majiniasi basi alikuwa bendera kwani hata kwenye moko alikuwa amepata daraja la kwanza akiwa amewaongoza wenzake wote na wilaya , lakini matokeo ya mwisho ndio hivyo alikuwa na daraja la tatu , nilijiuliza ilikuwaje na hapo ndipo nilipokuja kuujua ukweli lakini baadae kabisa kuwa bendera alikuwa akiniwaza sana hahaha… kumbe wakati mimi nateseka juu yake na yeye alikuwa akiteseka juu yangu , na hayo yote nilikuja kuyafahamu kutoka kwa rafiki yake ambae nilikutana nae kipiindi nikiwa nipo jijini dar nikisomea masomo ya hotel management , lakini pia nilikuja kusikia kuwa bendera anayachukia mapenzi balaa na pia ananichukia hataki hata kunisikia , jambo hilo lilinikosesha raha na nilijua yote hayo ni juu ya kufeli kwake na ndoto yake ya kuwa raisi , na mimi baada ya kusikia hivyo sikutaka hata kumwambia kuwa nina mtoto wake .
Basi mtoto wangu nilimpa jina la janeth , japo mama aligoma kwani alitaka nimpe jina la kiislamu , lakini mimi nilikadhania hilo , mpaka nikapelekea mama kunihoji upya juu ya baba wa mtoto na hapo ndipo nilipomuambia ukweli kuwa mtoto alikuwa ni wa bendera na bendera ni mkristo hivyo siwezi kumpa jina la kiislamu na mama yangu alikubali .
Basi janeth akiwa na miaka minne mbeleni nilimuacha kwa bibi yake na mimi nikaenda kusomea masomo yangu ya hoteli management ndani ya jiji la dar , masomo ambayo yalinichukua miaka miwili na nikafanikiwa kupata cheti changu na kurudi singida , nilifurahi kumuona janeth kakuwa huyo kwani kipindi hicho alikuwa darasa la pili , lakini pia kilichonifurahisha ni kwamba hakuchukua akili ya mama yake bali alichukua ya baba yake japo sura kachukua yangu na rangi ka ujumla wake , shuleni alikuwa ni jiniasi sana alikuwa ndio namba moja , nilikuwa nikimpenda sana mwanangu .
Basi baada ya kukaa nyumbani miezi miwili na mtoto wangu ndipo nilipokuja kupata nafasi ya kazi Serengeti kwenye hoteli moja ya kitalii ndani ya mbuga za wanyama , kwanzia siku hio nilikuwa nimeamua kufanya kazi kwa bidi kwa ajili ya matunzo ya janeth, sikuwahi kujua bendera yuko wapi na sikujihangaisha kumtafuta , japo moyoni mwangu alikuwa amejaa tele , yaani nilikuwa nikitamani kumuona lakini sikuwa nikitaka kumtafuta .
Miezi sita ya kazi ndipo nilipokuja kukutana na mzungu mmoja aliekuwa akija hotelini hapo kama mtalii mwanzoni tulianza mazoea ya kawaida , kiasi hata cha wafanya kazi wenzangu kuanza kunishawishi nimchune huyo mzungu pesa , lakini kwangu sikutaka kujihusisha na mapenzi kabisa , moyoni mwangu alikuwepo bendera tu , lakini kila siku ambayo mzungu yule akija pale hotelini alikua akiniachia kiasi kukubwa cha pesa kiasi kwamba hata ushuari wa marafiki zangu ulianza kuniingia akilini .
“ yaani wewe wema mtu sio mtu wako anakupa mihela yote hii ukimpa je si atakutoa kwenye umasikini “ yalikuwa ni maneno ya rafiki yangu julita siku hio nikiwa nimetoka kumhudumia mzungu huyo niliekuwa nikimjua kwa jina la bruno , kwa mbaali nilianza kuona ushauri wa julitha una maana na kwanzia siku hio nilijiapiza kwamba siku nyingine akija lazima nimpe tunda , nilikuwa nimesahau kabisa ahadi zangu kwa bendera na pia kila nikikumbuka kuwa bendera alikuwa hanitaki kuniona kwa kisingizo cha kwamba nimemfelisha basi nilipata msukumo Zaidi wa kugawa tunda kwa bruno .
Baada ya miezi kadhaa bruno alifika tena , na siku hio ndio nilipopata nafasi ya kuongea nae bruno , alikuwa akionekana mtu wa mawazo sana kuna siku nilimkuta akiwa amekaa kwenye bustani akilia kwa kilio cha kwikwi kabisa , jambo ambalo liliniumza sana ukizingatia na kwa namna alivyokuwa akinijali kwa kunipa pesa zake ,.
Siku hio ndio niliodhamiria kumpa penzi kwani niliamiani kwamba alikuwa akihitaji faraja , sikujali tena bendera sijui flag kwenye moyo wangu nilichokuwa nikijali kwa muda huo ilikuwa ni furaha ya bruno , siku hio alilewa sana kiasi kwamba hakuwezaa hata kwenda chumbani kwake na ikabidi nimkokote mpaka ndani kwake , lakini kitendo cha mimi kuingia nae tu ndio alianza kuninyonya midomo na kunipapasa kitu kilichofanya kikunde changu kusimama na kuhisi wadudu wakinitambalia mwilini huku shoti kuanzia kwenye maziwa mpaka kwenye kitumbua zikinisumbua , madakika kadhaa nilikuwa mweupe kama nilivyozaliwa na nilikuwa nikiusikilizia mwiko wa mzungu bruno , nilijkikuta nikifurahia mchezo ule na hio ilitokana na kwamba nilikuwa sijafanya muda mrefu na naweza sema ilikuwa ni mara yangu yatatu kufanya mapenzi katika maisha yangu .
Basi kuanzia siku hio ndio ikawa ni bruno kuwa mwiko na mimi kuwa chungu ilikuwa ni mwendo wa kukaanga mboga tu , kitendo hicho niliona kikirudisha furaha kwa bruno kiasi kwamba kama marafiki zangu walivyokuwa wkainiambia ni kweli nilianza kupewa pesa za kumwaga kiasi kilichonifanya kuanza kupendeza lakini pia matunzo ya janeth yakiongezeka , kutokana na ufaulu mzuri wa janeth niliamua kumhamisha shule kipindi hicho akiwa darasa la nne na nilimpelaka kenya shule moja iliokuwa ikifahamika kwa jina la hillcrest international shule nilioifahamu kutoka kwa rafiki yangu mkenya aliekuwa akifanya kazi hapo singita .
Baada ya miezi ya kupakua na kupika ndipo nilipojikuta nina ujauzito jambo ambalo kwangu sikulitarajia kabisa , kwani katika maisha yangu sikutaka kabisa kuwa na mtoto tofauti na wa bendera , lakini I nigesemaje sasa kwani pesa zilininogea nikajisahau sikua na jinsi tena , nilimsubiri bruno aje tena nimwambie juu ya ujauzito huo
Na kweli baada ya miezi alikuja na nikamueleza , japo nilikuwa nina tabasamu usoni lakini sikuwa nikimpenda kabisa bruno , yaani nilitamani hata kiumbe kilichoko tumboni nikitoe , lakini l niliogpa hio dhambi kabisa , basi baada ya kumwambia vile alionyesha kufurahi tu jambo ambalo lilinipa matumaini na alinishauri niache kazi nirudi nyumbani na atakuwa ananitumia pesa za matumizi , kwakua nilikuwa nikimuamini basi niliamua kuacha kazi na kurudi nikiwa na kiasi cha kutosha cha pesa , mama alishangaa mno baada ya kumwambia ni mjamzito , lakni nilimuelewesha kuwa mwanaume alienipa ujauzito ndie alienifanya hata kumpeleka janeth hillcrest , zilikuwa ni pesa za huyo mwanaume na nilimwaminisha kuwa alikuwa akinipenda , na kadri siku zilivyokuwa zikienda ndio mama aliamini maneno yangu kwani bruno hakukoma kunitumia pesa na kipindi hicho aliniambia kuwa alikuwa amehamia nchini rasmi na kuanzisha biashara zake .
Baada ya miezi tisa nilijifungua salama mtoto mwenye asili mbili yaani mzungu na mwafrika , alikuwa ni mtoto mzuri mno wa kike baada ya kujifungua bruno alikuja kisiri sana muda wa usiku na kuomba kuonana na mtoto na baada ya kumuona alimwangalia na kisha alitabasamu na kumbusu kwenye shavu kulia na kushoto then kwenye paji la uso kisha akanipa mtoto na katoa kidani flani hivi cha almasi na kumvalisha na hapo ndipo bruno alipo niambia maneno ambayo yalinifanya mpaka leo hii kumchukia milele lakini haikunifanya kumchukia yeye tu pia nilijikuta nikimchukia mwanangu wa kumzaa .
“ madam madam “.
Ilikuwa sauti ya zainabu ndio iliomtoa wema kwenye mawazo ya kumbukumbu yake ya nyuma
“ naam “
“ amka ule hata kidogo mama yangu “
“ sawa “,
*****
Baada ya janeth kuwasiliana na mama yake kimbembe kilibaki kwa janeth na damiani kwani damiani hakutaka kujulikana kama ndie aliemuokoa janeth , walikaa wakajadiliana ni kwa namna gani wanaweza wakalitatua hilo swala ndipo janeth alipomwambia neno moja damiani ambae mwenyewe hakujua ni kwa jinsi gani mwanadada huyo anakwenda kulifanya .
“ damiani I want you to trust me , as I said you won`t be involved “ damiani nataka uniamini katika hili niamini kabisa hutohusika .
“okey sawa janeth nakuamini , lakini nataka uniruhusu nikupeleke mwenyewe mpaka kituo cha polisi “ aliongea damiani na kumfanya janeth atabasamu na furaha kumjaa tele mbele ya mwanaume huyo .
“ okey damiani “.
Basi baada ya wawili hao kukubaliana , moja kwa moja walienda mpaka kituo cha polisi cha osterbay kuripoti na hapo ndipo walipokutana na waandishi kibao waliokuwa wakihitaji kujua mwenendo huo wa utekaji , kitendo cha janeth kutokezea tu alianza kuzongwa na waandishi wa habari , lakini damiani aliwazuia na mwishoe alitoa maelezo ya kueleweka ndani ya kituo hicho huku sajent takamoyo akiandika kila kilichokuwa kikisemwa na janeth .
“ kwa hio unamaanisha aliekuokoa hukumuona ?”
“ ndio sikumuona ila aliniambia jina lake nimwite mzalendo tu basi inatosha “.
“ na baada ya kutoka hapo ndani ulifikaje mpaka mjini “
“ nilipewa lift na mzungu mmoja hivi anajulikana kwa jina la stephano lamberk “.
“ unamaanisha huyo mtoto wa bruno lamberk aliekuja nchini hivi karibuni “
“ ndio “
“okey naona ndio amekuleta hapa”
“ ndio”
“ pole sana professor janeth , kwasasa sina mengine ya kukuuliza ila pale tutakapokuhitaji tutakuita mahali hapa “
“ nashukuru sajenti takamoyo”.
Baada ya maelezo hayo kamanda wa jeshi la dar es salaam aliongea na waandishi wa habari na kueleza mtiririko mzima wa kesi hio .
“ ndugu waandishi wa habari mnamo saa mbili ya leo tulipokea taarfia ya kutekwa kwa proffessa janeth bendera na baada ya taarifa wanausalama wetu walifika eneo la tukio na kufanya uchunguzi , lakini tukiwa katika uchunguzi huo ndipo tulipopokea simu ya majambazi kuuwawa na mtu aleijitambulisha kwa jina la mzalendo , ambae kwa taarifa alizonazo proffesa ni kwamba mtu huyo hakupata kumuona sura ni hayo tu waandishi “ aliongea kamishina ba baada ya hapo na janeth alihojiwa .
“ proffessa inasemekeana kwamba una umri wa miaka ishirini na saba ni kweli kwamba wewe ni proffessa na uliwezaje kupata uproffesa wako ukiwa na umri mdogo “ aliuliza mwandishi mmoja naefahamika kwa jina la chakunyegera
“ kuwa proffessa kwa umri huu sio jambo la kushangaza sana kama utakuwa na juhudi katika masomo, lakini pia vile vile napenda kusema mungu amenijalia na uwezo wa kuweza kusoma na kuelewa haraka naweza sema ndio kitu kilichoniwezesha kuyapata mafanikio haya kwa haraka “
“ proffessa janeth bendera , jina lako la mwisho linaonesha kuwa linafanana na la marehemu raisi wa tanzania bwana john bendera , je una uhusiano wowote na na yeye?? “
“hapana nadhani kama ningekuwa na mahusaiano ya karibu nayeye ningeweza kufahamika katika jamii ya watanzania , hivyo hakuna mahusiano yoyote kati yangu na ya marehemu raisi bendera “
“tumesikia kwamba umefanya tafiti mbali mbali katika maswala ya teknolojia katika vyuo ulivyopitia je umerudi nchini au umekuja kusalimia na kuondoka kwenda kufanya kazi nchi za nje ka ?” aliuliza mwandishi kimbembe .
“ kwasasa nimerudi kikamilifu nchini na sijarudi peke yangu , nimerudi na timu kamili ambayo kwanzia sasa na kupita kampuni ya NLT tunakwenda kuindeleza Tanzania katika swala zima la maendeleo ya kiteknolojia kwa ujumla wake , ili kuhakikisha Tanzania ya viwanda ambayo mheshimiwa bendera na mheshimiwa raisi wa sasa waliookuwa wakiiota inakwenda kufanikiwa na hatimae taifa letu kusonga katika swala zima la uchumi kwani viwanda kwa sasa ni teknolojia , ukiwa na teknoojia nzuri utadhalisha bidhaa bora kwa muda mfupi ambazo zitaingia kwenye ushindani na bidhaa za nje na ile hali ya watanzania kudharau bidhaa zetu za ndani itakwenda kutoweka kabisa “
Maneno alioongea yaliwafanya waandishi kuridhika lakini pia damiani aliekuwa pembeni na ngozi yake ya kistephano lamberk au kizungu alitabasamu , kwani maneno hayo yalimgusa sana .
Baada ya mazungumzo hayo waandishi waliomba kuongea damiani ama stephano lamberk lakini alikataa kwa kuwaambia kuwa anawaalika rasmi katika siku ya ufunguzi wa kampuni yake wiki moja mbeleni .
ITAENDELEA
SEHEMU YA 47
Taarifa ya kuwawa kwa carlos cardosso ilimfikia kimbona akiwa ofisini kwake , ilikuwa ni moja ya taarifa mbaya kwake , hakuamini kabisa kuwa jambazi hatari wa kimataifa ambaye alikuwa akimuamini sana katika kazi zake na kazi zinazofata alikuwa ameuawa kwa kupigwa na risasi na mtu anaejiita MZALENDO , kwake swala hilo lilikuwa ni pigo , lakini pia kwa vijana wake wengine ambao walikuwa wakimfanyia kazi kwani wote waliuwawa , jina la mzalendo lilizidi kumuumiza kichwa mno na hakujua ni maamuzi gani achukue kwa wakati huo , lakini pia alishukuru kwani pia hakukuwa na mtu ambae amekuwa hai kwani lazima wangebanwa lazima angabainika kwamba yeye ndie aliekuwa nyuma ya vijana hao na hata jambazi hilo .
Wakati akiwa kwenye mawazo simu yake iliita na aliekuw akipiga alikuwa ni sam , alipokea na kuweka sikioni na neno la kwanza kusikia lilikuwa :
“ uko wapi “
“ niko ofisini “
“ nakuja “
“ poa “
Nusu saa tu sam au rich sam alifika ndani ya ofisi hio ya kimbona ndani ya kampuni yake ya KILAC , alionekana na yeye alikuwa na wasiwasi kweli .
“ nimeona taarifa ya kifo cha carlos cardosso kwenye vyombo vya habari “
“ ndio hivyo hata mimi habari hio ndio kwanza nimeipata na mpaka sasa sijajua cha kufanya “
“ sasa una la kufanya lipi na wakati wa kufa washakufa , wewe waache wafu wazike wafu wao sisi tuendelee na mipango mingine , uzuri ni kwamba huyo mzalendo kaua kila mtu “
“ ni kweli kabisa na mimi kanirahishia kazi kweli kwani angemuacha hata mmoja na polisi wangefika huenda wangetutaja “
“ hata wangekuwa hai tungemmaliza kabla hajapanua mdomo wake tuna koneksheni nyingi ndani ya taifa hili , au usahasahau kuwa sisi ndio tunao liongoza taifa “
“ ndio najua , lakini waswasi ndio lazima uwepo “
“ ni kweli “
“ unasema tuongee mpango mwingine ni upi huo ?”
“ marie yupo nchini “
“ marie yupi “
“ nawewe ushasahau si nilikwambia yule jasusi wa CIA anaetokea thailland “
“ anhaa nimekumbuka daah , kichwa kimevurugwa saivi yaani “
“ haha .. pole lazima uvurugwe najua vjana uliwapoteza wanakuumiza “
“ ndio hivyo , kwa hio anasemaje “
“anasema uchunguzi nchini china amegundua kuwa damiani yupo hapa nchini “.
“ unamaanisha damiani karudi “
“ ndio na inaonekana amerudi muda mrefu , si unaona hali yahewa ilivyombaya “
“ inawezekana , lakini sasa huyo damiani yuko wapi “
“ anasema kuna uwezekano wa mambo mawili , damiani anaweza akawa stephano lamberk au stephano lamberk anafahamiana na damiani “
“ hapo stephano kufahamiana na damiani nakubali , ila swala la stephano lamberk kuwa damiani sikubali hata mje na mzimu wa mama yangu “
“ hahaha … hata mimi nimemwambia hivyo ila kasema speculations zake zinaweza zikazaa majibu kati ya hayo na kwasasa anaingia kazinia kulifatilia hilo “
“inabidi umpe na kazi ya kufatilia na hili la huyu mzalendo “
“ ndio maana nimekuja hilo ni moja wapo “
“ na lingine ni lipi “.
“ death notice from U-97 “
“ inamuhusu nani hio “
“ julieth , stephano lamberk ,sabi mboneche na wema sufiani wanatakiwa wauwawe tumemepwa siku kumi kulikamilisha hilo “.
“ huyo sabi ni nani “
“ ni mtoto wa marehemu brigedia mboneche saivi ni mkurugenzi wa ikulu mawasiliano “
“nini , sasa kwanini wauwawe na hilo la mke wa raisi linakaa vipi “
“ hata mimi sielewi yaani nimechanganyikiwa , nilichoambiwa ni kwamba hao wanahatarisha umoja wetu ndani ya Afrika kwa ujumla “.
“mhmh ! aisee sielewi “
“ mimi kuna picha inanijia hapa “
“ picha gani “
“brigedia mboneche aliuliwa na U-97 “
“kwanini auliwe “ alingea kwa mshangao .
“ sijajua taarifa hio kwa undani wake ila ni kweli kauliwa na U-97 na taarifa hio nasikia mwendazake alikuwa nayo , jambo ambalo mpaka sasa linanipa mashaka huenda hata mwendazake kauliwa na U-97 “
“mhmh na wema je ?”
“ inawezekana pia kuna mambo anayafanya pasipo ya uelewa wetu yanayohatarisha umoja , level za juu za uongozi wanaijua tanzania kuliko tunavyo ijua sisi “
“ unamaanisha sisi ni kama mashushu tu “
“ ndio maana yake , ninahisi U-97 sio madawa ya kulevya tu kuna ya ziada ila sitaki hata kuyajua mimi mimi najari pesa tu “
“ umeongea point sam , sisi tudiri na njururu tu “.
“ hahaha.. eti njururu , ndio maana nakukubali kimbona , njururu ndio kila kitu siku ya kwenda mars nataka niwe na nauli “
“ hahaha .. kumbe unampango wa kwenda mars “
“haha ndio , sema kuna hili swala la kufa linaninyima raha kabisa “.
“ haha .. mimi hata siliwazii saivi nakula maisha tu , nikifa mimi vijana wataniwakilisha “
“ kweli kabisa , tunawekeza kwa watoto “
“ ndio , halafu hujaniambia hao wanakufaje na nani anafanya hayo”
“hio ndio kazi yetu kimbona , nina mpango wa kwenda kuwakodi al shabab “
“uatawapatia wapi wanamgambo hao “
“ mawasiliano yao yapo ndani ya umoja wetu “
“ unamaanisha U-97 “
“ ndio kwani kuna umoja gani mwingine , yaani mpaka sijui boko haram islamic state , alqaida sijui waasi gani wote wapo chini ya ufadhili wa U-97 , mambo haya ni siri kimbona acha uropoke uone na wewe death notice yako nisipotumiwa “
“siwezi ropoka , yaani huu umoja kuna muda unaniogopesha ila hela zikiingia kwenye kaunti nasahau hofu “
“ hahaha hfu ndio adui yetu kimbona , ukiwa na hofu umekwisha utakuwa masikini wa kutupwa “
“ ni kweli kabisa “
“sasa nimekuja kukuambia pia kuwa kesho nitakuwa na kikao na wakuu wa U-97 , japo mheshimiwa yupo nje ya nchi , ajenda ya kikao hicho nishatumiwa , hili la sabi , wema , stephano na janeth ni siri yetu mimi na wewe “
“ hakuna shida “
Basi sam aliondoka na kumuacha kimbona akiwaza .
*****
Basi hatimae giza liliingia muda wa saa mbili kamili za usiku ndani ya hoteli ya regency Kilimanjaro ilionekana gari ya merina ikipark katika eneo hilo na akatoka mrembo huyo akiwa amependeza kweli , baada ya yeye kutoka na kuingia ndani , iliingia tena gari aina ya V8 XR nyeusi na alitoka mkuu wa majeshi bwana abdallaha khalifa bwana aliefika akiwa amevalia suti yake na miwani na akaingia ndani ya jengo hilo la hoteli .
Nusu saa mbele ndani ya ukumbi mdogo wa mikutano eneo la VIP meza ilionekana ikiwa imezungukwa na watu wasiopungua watano yaani bwana kizito kabwela , merina sostness , Abdallah khallifa , bwana elly matinde, zakayo au agent Z na CP (commissioner police ).
“ jamani za saa hizi “ aliongea matinde kiongozi wa kikosi hicho cha watu watano ukimtoa zakayo maana zakayo yeye hapo alikuwa yupo kwa ajili ya maslahi tu .
“ salama “
“ kwanza nawashukuru sana kwa kufika wote bila kukosa katika kikao hichi cha dharula na hii imetokana na jambo ambalo lilikuwa nje ya uwezo wangu, kulitokea maamuzi hivyo kuhitaji ushauri wenu juu ya hilo , lakini pia tutasikia ripoti fupi ya pale upelelezi wetu ulipofikia mpaka sasa “ aliongea matinde na kisha alimkaribisha zakayo pasipo kupoteza muda .
“mpaka sasa naweza sema kwamba upelelezi wangu haujafikia mwisho , lakini kuna hatua kubwa ambayo mpaka sasa nimefikia ambayo inanipa matumaini ya asilimia kubwa ya kuikamilisha muda mfupi ujao
Mpaka sasa nimefanikiwa kujua kifo cha mama yake damiani kilivyotokea na kifo hicho kilitokea mnamo tarehe tajwa huku jeshi la polisi kukamilisha upelelezi huo kwa kuutangazia umma kwamba tukio hilo lilikuwa ni la kijambazi ambalo walijaribu kuwahusisha majambazi hao na majamazi waliovamia chuo cha SEKOMU (SEBASTIANI KOLOA MEMORIAL UNIVERSITY ) lakini taarifa hio ni ya uongo na ya kweli ni hii “ alitulia kidogo akaendelea .
“Kifo cha sarah rabani hakikuwa kifo cha bahati mbaya ila kilikuwa kifo cha kupangwa na ni mpango wa muda mrefu ulioandaliwa na bwana bruno lamberk , lakini licha ya kwamba bruno alipanga kufanya mauaji haya lakini inaibuka sintofahamu kutokana na kwamba siku ya tukio la kuwawa kwa sarah rabani , bruno lamberk alikuwa amejeruhiwa kwa risasi , mpaka pale kijana damiani kumfikisha nyumbani kwao kwa ajili ya msaada na hapo kukutwa na mauti , lakini licha ya kwamba siku ya tukio hilo bruno lamberk alikuwa na jereha la risasi, lakini pia kuwa na dhamira ama mpango wa kumuuwa mama rabani, ni kwamba tukio hilo linaweza likawa limefanikiwa ama halikufanikiwa, na hili ni kutokana na uchunguzi nilioufanya na kubaini kuwa siku ya tukio nyumbani kwa sarah kulikuwa na watu wanne yaani saraha marehemu , bruno marehemu , muaji namba moja na muaaji namba mbili, najaribu kuwaita kwa namba kutokana na kwamba mpaka sasa sijapata kuwafahamu majina yao , naendelea.. , muaaji namba moja alikuwa ndani ya nyumba wakati damiani na mzee kivinje (mganga wa kijiji wa tiba za asili )walipo fika nyumbani kwa sarah , mzee kivinje alimshuhudia muuaji namba mbili aliekuwa ameshika bastola na akivuja damu kwenye bega akitokomea huku akiwa ametoka ndani ya nyumba ya sarah lakini pia huyo huyo kivinje aliweza kumshuhudia muuaji namba moja akiwa ndani ya nyumba ,nyuma ya mlango akiwa amejiziba uso , nadhani mpaka hapo mmepata picha kuwa kuna watu wanne ambao wana majibu tunayoyatafuta , lakini wawili tunawatoa kwani washatangulia mbele za haki na sasa waliobaki ni wawili yaani muuaji namba moja na namba mbili , lakini kwanini mpango huo umuhusu sarah , ni kwamba kwa taarifa za awali ni kwamba damiani alikuwa ni chaguo la bruno katika kukamilisha mpango X nimeupa mpango X kwani mpaka sasa sijajua unahusu nini, ni jambo ambalo nitalifatilia kiundani Zaidi,mahusiano ya mambo haya na kujua mahali alipo damiani ni kama ifuatavyo , kama tulivyoona mambo haya yalivyotekelezwa ni kwamba danieli mtalemwa aliuliwa na carlos cardosso akishirikiana na agent miss k (suzzane ) paisina shaka naamini miss k kapokea maagizo kutoka kwa raisi , lakini pia bila shaka pia carlos cardosso aliachiwa huru kwa ajili ya kummaliza danieli kwasababu danieli alikuwa ni komandoo namba moja na hakuwa na mpinzani hapa chini katika mapambano Zaidi ya carloss hilo ni A , B ni kwamba target ya kuuliwa kwa danieli ni kutokana na taarifa nyeti aliokuwa danieli ambayo ni nyaraka zilizoachwa na bruno , lakini ikatokea kwamba nyaraka hizo hakuwa nazo danny ila alikuwa nazo damiani hivyo suzzane alikuwa akitaka nyaraka hizo kutokana na oda ya raisi , lakini kitendo cha kukimbia kwa damiani hii inakuja sasa kwenye ripoti yangu ya nyuma tuliona damiani akipata msaada ambao tunaamini kwamba bila kuwa na koneksheni asingefanikiwa kupata msaada huo hadi kwenda thailland hio inaniaminisha kwamba koneksheni hio ilitengenezwa na bruno mwenyewe au vininginevyo katika mpango x na kwa maneno hayo nasema kwamba moja ya mtu ambae yupo kwenye mpango x ni balozi wa kenya bwana njiroge japo swala hilo suna uhakika nalo , bwana njiroge atatufahamisha ilikuwaje akakubali kumsafirisha damiani mpaka kenya .
Pili uchunguzi hautaishia hapo naamini kati ya muuaji namba moja na namba mbili mmoja wapo anaweza akawa uraiani au wote wakawa uraiani hivyo taarifa za bwana njiroge zitakuwa muhimu na pia za aidha muaji namba mbili au namba moja zitakuwa muhimu .
Mwisho nihitimishe kwa kusema kuwa mpaka sasa carlos Cardoso keshapoteza maisha kwa kuuliwa na mtu anaejiita mzalendo ninayo taarifa ya awali kutoka kituo cha polisi magogoni zinazoainisha kwamba hili sio tukio namba moja la mtu anaejiita mzalendo , pili pia taarifa kutoka TISS inasema kuwa huenda mzalendo akawa anahusika na shambulio la raisi pale serena.”
“ ni kupongeze sana bwana zakayo kwa ufanisi wako katika uchunguzi wako lakini nina swali moja , kuna uwezekano wa mzalendo kuwa na koneksheni na mzalendo “.
“ mheshimiwa kizito hilo ndio swala ambalo nitalifanyia uchunguzi wa kina na kama kuna muunganiko naamini tutafahamu “
“mimi nina swali moja kama ulivyodema mpango x , je unaamini kuwa mpango huu unaendelea na kama unaendelea je damiani anaweza akawa ndio anaendeleza mpango huo “aliuliza merina
“ naamini mpango huo unaendelea m, kama damiani aliweza kufika nchini thailland naamini hivyo , lakini pia naamini anaweza akawa anafanya mambo ambayo hajui asili yake huku akiwa amemezezwa udanganyifu “ .
“nataka kuongezea hapo kwa miss merina kuhusu huo mpango x , vipi unaamini swala hili ni rahisi kupata majibu yote tukiwa ndani ya taifa la Tanzania bila kupitia katika nyayo ambazo amepita damiani ili kujua mpango huo x “aliuliza CP
“ hilo nalo ni swala ambalo nilikuwa nikilifikiria na pia nilitamani kuliweka wazi , kuna mawili kwa mambo ambayo yanaendelea hapa nchini kuna hisa zinaniambia kuwa yanaweza yakawa yanahusika na mpango x moja ya jambo hilo ni juu ya swala la bwana stephano lamberk kufika hapa nchini na kuanza swala la uwekezaji , mali za bruno kwenda kwa innova , mzalendo haya ni mamb ambayo mpaka sasa yananifikirisha nab ado sina majibu sahihi kama mnavyojua sisi wenyewe tulimjua bruno kwa Zaidi ya miaka ishirini iliopita , na hatukuwahi kusikia kuwa ana mtoto basi kuna majibu ambayo yanaweza yakatupa majibu Zaidi “
“ nikushukuru sana bwana zakayo kwa upelelezi wako , sasa nirudi kwa sisi wana jumuia yetu hii ambayo mpaka sasa hatujaipa jina , swala nililoshindwa kulitolea maamuzi ni swala la huyu balozi wa kenya , zakayo katoa pendekezo la kumteka , lakini kwangu mimi nimeona ni jambo la hatari kwa nchi na ushirikiano wa kimataifa vilevile kwani mpango wetu sio kuiharibu Tanzania ila ni kuijenga hivyo nilikuwa nahitaji mawazo yenu katika jambo hilo “ aliongea matinde
“ mimi nina wazo moja , nadhani tutafute footage ambazo zitatapelekea kuwa ushahidi ili pale tutakapoenda kumhoji bwana huyu njiroge asije akakataa kutohusika , na kama akikubali basi ni lazima atatupa majibu sahihi “
“ naunga mkono hja ya bwana kizito “
“Tunaunga mkono wote hoja “
“ kama tunaunga mkono wote hoja , basi naamini swala hilo halitakuwa na ugumu nitakachotakiwa kufanya ni kumpatia kitambulisho ambacho kitamuwezesha bwana zakayo kufanya pelelezi ndani ya balozi na pia ndani uwanja wa ndege , labda kama zakayo una jambo la kuongea “
“ ndio ninalo la kuongea ambalo pia naamini litanisaidia katika uchunguzi wangu “
“ni lipi hilo “
“ waheshimiwa nadhani tunakumbuka miaka ya nyuma nyie ndio mlikuwa wateule wa mheshimiwa bendera , na pia kwa taarifa ni kwamba ninnyi ndio mliohusika katika biashara nzima ya kutokomeza dawa za kulevya , lakini nikiwa nchini Indonesia nilipokea mission iliopewa jina la 0404 na nilikamilisha hio na mission hio ilitoka kwa raisi mwenyewe nataka kujua ni kwa namga gani raisi bendera aliweza kusaliti biashara yake ya madawa ya kulevya na kuunga juhudi za kukomesha madawa ya kulevya hapa nchini kwani moja ya vijana wa bruno walinipa taarifa kwamba bruno hakufanya kwa mapenzi yake ila ni kwamba raisi alimshika pabaya , nataka kujua huenda likanisaidia kujua mpango x “ aliongea zakayo na kuwafanya wazee hao washangae ni kama waliokuwa wakijuliza na kizito alitingisha kichwa na kumuashiria matinde kuwa anaweza kuongoza .
“ mission 0404 ilikuwa inahusika na mtoto wa bruno na mheshimiwa hakuweza kutuweka wazi sana ila hio ilikuwa ni weak point ambayo ilituwezesha kumfanya brunoo cooperate”
“ mpaka hapo nimepata picha , lakini kuna jambo linanichanganya kidogo kama ni hivyo basi bruno atakuwa na watoto wawili , kwani niliemteka mimi alikuwa ni mwanamke “
“inawezekana “
“ waheshimiwa kabla hamjaendelea nina swali kidogo “ aliongea merina na kuwafanya wote wamwangalie .
“ mmesema mission 0404 nataka kujua ilikuwa inahusu nini “
“ilikuwa ni abduction miss merina “
“ abduction , ilitokea wapi hio ?”
“USA” aliongea zakayo na hapo ndipo alipo mfanya merina atoe jicho huku machozi yakianza kuloanisha mashavu yake na kuwafanya wote washangae .
ITAENDELEA .
SEHEMU YA 48
“ miss merina vipi mbona unatoa machozi”.lilikuwa ni swali kutoka kwa kizito kwenda kwa merina , na merina haraka haraka alijikuta akifuta machozi .
“ hakuna muheshimiwa kuna tukio nimelikumbuKa miaka ya nyuma kidogo limenifanya hisia zangu zizamie huko “ aliongea merina huku akijiweka sawa na hakukuwa na mazungumzo mengi ndani ya kikao hicho kwani kilifungwa rasmi na kila mtu akatawanyika .
Upande wa kutokea nje kabisa ya maegesho alionekana matinde akiwa ametangulizana na zakayo .
“ mheshimiwa huyu merina wazazi wake ni wakina nani ?”
“nasikia wanaishi canada huko kwanini unauliza ?“.
“anafanana na yule msichana niliemteka miaka ya nyuma “
“ unasema kweli?? “
“ ndio tena nilishangaa sana baada ya kumuona “
“ kwa hio unataka kumaanisha kwamba merina ni mtoto wa bruno? “
“ siwezi jua labda wamfanana tu ila sina uhakika “
“ haiwezekani watakuwa wamefanana kwani merina nimejaribu kufatilia habari zake ni kweli wazazi wake wapo Canada ni wamiliki wa kampuni ya ATPAY “
Aliongea matinde na kumfanya zakayo akubaliane , muda huo walikuwa wakiingia kwenye gari , lakini wakati wakiwa wanaingia kulionekana mtu kwa upande wa kushoto akiwapiga picha , alikuwa kijana mdogo alievalia kofia huku akiwa ameshikilia kamera yenye lensi kubwa .
Upande wa merina alijikuta akiendesha gari huku akiwa na mawazo ya hapa na pale , alijikuta akikumbuka na yeye tukio la kutekwa akiwa chuoni nchini marekani , tukio hilo japo hakupata madhara yoyote lakini alikuwa akiliogopa sana kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kutokewa na tukio la aina hio .
“ nimewakumbuka mom and dad” aliongea huku akiongeza mwendo kuwahi nyumbani kwake , lakini mawazo yake hayakuishia kwenye kuwakumbuka wazazi tu alikuwa pia akikumbuka ripoti nzima ya zakayo , alikiri kuwa zakayo alikuwa vyema katika kufanya upelelezi lakini kwa upande mwingine aliona kama zakayo alikuwa akifanya upelelezi ambao haukuwa ukimuhusu damiani .
“ stephano anaweza akawa anajua ni wapi damiani alipo lazima nikamuulize kesho yake huu uchunguzi wa zakayo unachukua muda mrefu mno kuliko nilivyotegemea “ alijiongelesha merina huku akiingia mtaa wa masaki
******
Mheshimiwa raisi japo alikuwa safarini lakini alikuwa akifatilia kila kilichokuwa kikiendelea ndani ya taifa la tanzania , , japo bwana huyu alikuwa na madhaifu yake lakini likija swala la maslahi ya taifa alikuwa akipigania sana , na katika kipindi kifupi cha uongozi wake alikuwa amefanya mengi ya kuwafanya watanzania wajivunie .
Muda huo alikuwa ndani ya hoteli ya kitalii ndani ya jiji la Washington DC akiwa anaangalia baadhi ya taarifa kutoka Tanzania , moja ya taarifa iliokuwa gumzo ni ya proffessa janeth kutekwa na mpaka kupatikana kwake , huku akiwa kivutio kwa kuwa proffesa kwa umri mdogo tu jambo ambalo liliwashangaza sana watanzania .
“ janeth bendera “ alijikuta akitamka jina hilo huku akuwa ameshikilia mvinyo wake akiwa amekaa kwenye sofa huku akionekana kuwaza mbali mno na hapo kumbukumbu zake zilimpeleka nyuma miaka kadhaa .
***
Ni baada ya miezi kadhaa baada ya kurudi nchini kutokea kenya ambako nilikuwa nilienda kumwakilisha mheshimiwa raisi katika kikao cha wakuu wa nchi za afrika mashariki , kwangu ndani ya kipindi cha miezi hio kilikuwa ni kipindi ambacho kwa namna moja ama nyingine nilikuwa nikisumbuliwa na mawazo ya hapa na pale , maneno alioniambia mheshimiwa ndalu nikiwa ndani ya jiji la Nairobi yalikuwa yakijirudia rudia mara kwa mara ndani ya kichwa changu , na kuongeza shauku yangu ya kutaka kujua baadhi ya mambo yanavyokwenda , kwani nilijihisi kabisa nilikuuwa kwenye kiza kinene , furaha yangu mbele ya bendera ilianza kupungua , udhaifu mkubwa ambao niilikuwa nao katika maisha yangu ilikuwa ni familia nilikuwa nikiipenda sana familia yangu kiasi kwamba sikupenda jambo lolote liikumbe familia yangu , maneno ya mheshimiwa ndalu kuhusisha na familia yangu kidogo nilipata mashaka , lakini si mashaka tu lakini pia nilitaka kujua kwa undani maneno yake kama yana ukweli ndani yake, maana mpaka mtu kuja mpaka hotelini kwangu tena nje ya nchi ilimaanisha kwamba kuna jambo alikuwa akitaka nilifahamu ambalo ameona kabisa sikuwa na ufahamu nalo .
Sikuona haja ya kujiumiza tena na mawazo ya aina hio , jambo nililoamua siku hio nilivyokuwa nikitoka nyumbani kwangu nikielekea ofisini, ni kulifatilia swala hilo , mara baada ya kufika ofisini nilikaa nikaanza kuwaza ni kwa namna gani ninaweza kulifatilia jambo hilo kwa undani, na kwakuwa mimi mwenyewe sikuwa na uzoefu na kazi hio na pia nisingeweza kuifanya miimi mwenyewe niliona kulikuwa na ulazima wa kupata mtu ambae anaweza akalifanya jambo hilo , nilianza kuwaza na kuwapambua walinzi wangu mmoja baada ya mwingine , wapo niliokuwa nikiwaamini sana lakini pia niliamini wasingeweza kuifanya kazi hio kwani walikuwa na ujuzi wa kawaida sana ambao wasingeendana na kazi yangu , kazi nyingine iliibuka hapo , niliwaza ni nani anaeweza kunifanyia kazi hio akili yangu ilikwama , nilijikuta nikipotezea kwanza swala hilo na kufanya majukumu yangu ya kiofisi na baada ya kumaliza majukumu yangu ya kiofisi ndipo nilipokea simu kutoka kwa muheshimiwa , wakati huo alikuwa makao makuu ya nchi na mimi nilikuwa ndani ya jiji la dar es saalam , nilipokea simu ya muheshimiwa .
“habari za kazi muheshimiwa “
“ salama henry , unaendeleaje na familia na majukumu yako kwa ujumla “
“ mheshimiwa namshukuru mungu familia inaendelea vizuri lakini pia na majukumu yangi ya kiofisi yapo vizuri “
“ nafurahi kusikia hivyo henry , sasa nimekupigia kuna jambo nataka nikwambie , umoja wa wafanyabishara wa dar es salaam mwezi uliopita waliniomba nihudhurie katika mkutano wao walioupa jina la ‘get together ‘ na waliniomba kuwa mgeni rasmi , lakini kutokana na ratiba zangu na tarehe tajwa mambo yamebanana kwani siku hio nina ugeni kutoka china, waziri wa mambo ya ndani ya uchina atakuwa hapa nchini hivyo naomba uniwakilishe “
“ hakuna shaka muheshimiwa nitakusaidia katika hilo “.
“shukrani sana henry , kuhusu hotuba ya siku hio na maelekezo mengine nitakutumia kwa njia ya email “
“ sawa muheshimiwa “.
Baada ya kupokea simu hio kwangu niliona ni jambo jema kwani na mimi pia nilikuwa mfanya biashara , hivyo kumuwakilisha mheshimiwa katika kikao hicho kwangu ilikuwa ni fursa nyingine ya kufahamiana na wafanya biashara wakubwa nchini ambao sijawahi kukutana nao .
Basi siku yenyewe ilifika na nilifanikiwa kuhudhuria kikamilifu katika mkutano huo ambao nilikuwa mgeni rasmi nikimuwakilisha mheshimiwa raisi , ulikuwa ni mkutano uliokuwa umejaaa mengi ya faida kwa Tanzania na kwa wafanya biashara pia .
Moja ya wafanya biashara waliokuwepo katika kikao hicho alikuwepo bruno lamberk akiwa na walinzi wake , alikuwa ni moja ya wafanya biashara waliokuwa na ulinzi mkubwa sana nchini na hio yote ilikuwa ni kutokana na mchango wake katika swala zima la kutokomeza madawa ya kulevya , mchango ambao ulitokana na kuwasaliti wenzake na kupelekea kuwa na maadui wengi nchini na hivyo ulinzi wake kuwa ni moja ya jukumu la kiserikali .
Moja ya walinzi wake ndie alienivutia mno kwa kazi yangu hakuwa mwingine bali alikuwa ni suzzane , nilikuwa nikizijua sifa zake nyingi japo ya kuwa komandoo lakini pia alikuwa na mafunzo ya kiintellijensia , jambo ambalo lilinifanya nimuone moja ya watu ambao kama angeaminika angekuwa ni perfect candidate (mtu sahihi) kwa kazi yangu , wazo hilo liliibua changamoto nyingine ndani ya kichwa changu , nilijua kabisa mwanadada huyo alikuwa ni mlinzi wa bruno , lakini pia ni moja ya vijana waliokuwa wakiaminiwa na mheshimiwa raisi , kwangu changamoto ilikuwa ni kwa jinsi gani ninaweza kumshawishi kunifanyia kazi yangu na pili kumwamini kwa kutotoa siri juu ya kazi nirakayompa .
Baada ya kurudi nyumbani kwangu wazo moja lililonijia ilikuwa ni kutafuta wakati wa kuongea na suzzane kwa siri sana pasipo ya kushitukiwa , jambo nililokuwa nikitaka kulifanyia uchunguzi lilikuwa likimuhusu bruno pia ndio maana niliona natakiwa kumshawishi suzzane kwa namna yoyote ile anifanyie kazi yangu.
Siku ya jumamosi ndio siku niliofanikiwa kuandaa appointment meeting na suzzane katika hoteli ya colleseum ndani ya masaki , nilichagua hoteli hio kutokana na kwamba siku hio bwana bruno alikuwa ndio mahali pake pakufanyia mazoezi kwani matajiri wengi walikuwa wakipapenda kutokana na kuwepo kwa club ya mazoezi (body fitness club) na mimi pia nilikuwa mwanachama wa club hio .
Jambo ambalo nimefanikiwa ni kuonana na suzzane , lakini jambo ambalo sikuwa na uhakika nalo ni kumshawishi mwanamke huyo kunifanyia kazi yangu , na ndio maana nilikuwa ninataarifa nyingi sana zilizokuwa zikimuhusu suzzane , nilikuwa na taariifa zilizokuwa zikiihusu mpaka familia yake kwa ujumla , niliona nivyema kujiandaa kwa namna yoyote ile .
Siku hio hakukuwa na shida sana ya kuonana nae kwani alikuwa ni moja ya walinzi ambao walikuwa zamu katika kumlinda bwana bruno , hivyo alichokifanya suzzane ni kuwaachia wenzake majukumu kwa muda wakati boss waka akichukua mazoezi .
“ nadhani umepata mshangao uliojaa maswali suzzane mara baada ya kupata ujumbe wangu “
“ ndio muheshimiwa nilipatwa na mshangao huo kwani naamini hatupokei maagizo kutoka kwako “
“ napenda ulivyo na maneno ya moja kwa moja suzzane na mimi nitakuwa na meneno ya moja kwa moja ili tuweze kuelewana kwa haraka “
“ hakuna shaka muheshimiwa , maana pia nipo kazini “
“ kuna kazi nataka unifanyie suzzane , ambayo ina malipo makubwa sana kama utaikamilisha “
“ mheshimiwa kama nilivyosema awali ni kosa kubwa kwa mimi kupokea kazi binafsi zinazohusu malipo pasipo ruhusa ya wakuu wangu wa kazi . kwani endapo itafahamika kwa mheshimiwa raisi ninaweza kuipoteza kazi yangu lakini pia ni kosa la kuvunja kiapo changu”
“ nalielewa hilo suzzane kabla hata sijakuita hapa , lakini pia naelewa familia yako kwa ujumla ni kwa jinsi gani unahitaji pesa za kutosha kuitunza , kutokana na baba yako kufilisika kwa kushindwa kulipa kodi na hatimae kuwa gerezani kwa kesi ya uhujumu uchumi “
“ mheshimiwa ulikuwa ukiifatilia familia yangu ?”
“sio kuifatilia suzzane najua mengi kuhusu yanayoendelea katika familia yako , lakini yote nimeayafanya ili kujenga Imani yangu kwako , juu ya kazi ambayo nataka kukupatia unifanyie “
“ mheshimiwa kama unataka kunipa kazi kutokana na hali ya maisha ya familia yangu , basi naomba kazi hio umtafute mtu mwingine akufanyie “
“suzzane sio nia yangu ya kuifatilia familia yako ,lakini niimefanya hivyo kutokana na umuhimu wa kazi yangu lakini pia kujilinda mimi mwenyewe , najua huajamtembelea muda mrefu baba yako gerezani ,nataka kukuambia kuwa anateseka sana na mimi ndio mtu pekee ambae naweza nikamtoa gerezani “
Suzzane alijikuta akikumbuka kuwa ni kweli hajawahi kumtembelea baba yake gerezani muda mrefu , tokea apatikane na kesi ya uhujumu uchumi , alikaa huku akimwangalia mheshimiwa kwa hasira .
“ naomba nikalifikirie hili muheshimiwa nipe muda “ aliongea suzzane huku akinyanyuka .
“ sawa suzzane unasiku mbili tu za kufikiria , kama upo tayari utanipigia kwa hii namba na utaletewa taarifa za kazi yenyewe ambayo unatakiwa kuifanya , siku utakayokamilisha kazi yangu ndio siku ambayo nitamtoa baba yako gerezani “. Aliongea makamu wa raisi , na kisha aliagana na suzzane huku akiamini kwa asilimia mia maongezi hayo yamefanikiwa , kwani alishajua udhaifu wa suzzane uko wapi hasa pale alipo litamka jina la baba yake , hizo zote zilikuwa ni hila za henry katika kumpata suzzane , aliamini misimamo ya wanajeshi ndio maana alichukua tahadhari mapema sana na hata gerezani alitoa amri ya baba yake suzzane kuongezewa mateso makali mno , huku akiamini kabisa suzzane lazima angefika gerezani kwa ajili ya kumuona baba yake kabla ya kufanya maamuzi .
Basi baada ya mimi kuagana na suzzane sikuwa na lingine zaidi ya kusubiria jibu langu kutoka kwa suzzane , jibu ambalo niliamini kwa asilimia mia moja kwamba lazima suzzane akubali , kwani kama mheshimiwa andalu alivyotumia udhaifu wangu kwa kutaja familia yake katika kufikisha ujumbe wake na hivyo hivyo na mimi nilitumia udhaifu wa suzzane katika kufikisha ujumbe wangu ili akubali kunifanyia kazi yangu .
Siku moja mbele nilipokea simu kutoka kwa mkuu wa magereza kuwa suzzane alifiika kumuona baba yake , jambo lililonifanya kutabasamu mno , kwani niliamini kwa hali ambayo atakuwa amemkuta nayo baba yake , basi lazima angenitafuta , na kweli nilikaa Zaidi ya masaa mawili tu ndipo nilipo pokea simu kutoka kwa suzzane akitaka kazi huku akihitaji nimtoe baba yake gerezani , ule msemo wa damu nzito kuliko maji ulichukuwa nafasi yake.
Basi nilimpa suzzane kazi kuu mbili , kazi ya kwanza ilikuwa ni kuchunguza maisha ya bruno kwanzia akiwa nchini kwa mara ya kwanza mpaka siku ambayo anausaliti umoja wake , pili nilihitaji kujua mwenendo mzima uliofanyika mpaka raisi bendera kuwa raisi wa Tanzania .
Baada ya kumpa kazi hio suzzane , wiki hatimae mwezi ulitimia na ndipo suzzane alipo nitaarifu kuwa anataarifa kamili ya kazi niliokuwa nimempatia , na mimi kwa hamu kubwa sana ya kujua ripoti hio sikukawia kwani nilipanga sehemu ya kuonana nae , sehemu yenyewe ilikuwa ni ndani ya hoteli ya new Africa hoteli muda wa saa tatu kamili za usiku ndio suzzane alipofika ndani ya chumba ambacho nilikuwa nimekichukuwa kwa ajili ya kuonana nae.
“ enhe niambie suzzane ripoti inasemaje “
“ suzzane kwanza alitabasamu jambo ambalo lilinishangaza sana , lakini sikutaka kuuliza maswali mengi Zaidi ya kutaka kusikiliza ripoti hio .
“ mheshimiwa una moyo wa kusikiliza ?”
“ suzzane niambie acha kunitisha , nimepitia magumu mengi bhna “
“ mheshimiwa katika uchunguzi wangu , mkeo pia emejitokeza katika ripoti yangu , je unaniruhusu niendelee ?”
Nilijikuta moyo ukipiga paa , baada ya kusikia jina la mke wangu , kwa jinsi suzzane alivyokuwa ananinagalia niliamini kabisa ripoti hio haikuwa na mazuri kabisa ya kuyasikia , nilikuwa nikimpenda sana mke wangu na Zaidi ya yote nilikuwa nikimuamini pia .
“ suzzane naomba usome ripoti hio tafadhari inanihusu mimi sio wewe ndio maana nakulipa “
“sawa muheshimiwa , aliongea kisha akapozi na akaangalia faili lake . na kisha akaendelea , mheshimiwa kutokana na maelezo ya kazi ulionipa nilifanikiwa kufanya utafiti wangu kwa kina Zaidi na ni mengi ambayo nimeyafahamu ambayo pia yanamuunganisha mkeo katika ripoti hii , labda kwa kuanzia nianze na ripoti ya mkeo , mkeo alisoma songea girls , lakini alipofikia kidato cha nne ndipo alipokutana na mpenzi wake wa kwanza ( first love) anajulikana kwa jina la john bendera “
“ unasemaje suzzane ?”
“ ndio mheshimiwa , si umesema nisome , mkeo mpenzi wake wa kwanza , namaanisha madam wema kipenzi chake cha kwanza ni mheshimiwa bendera “ kwa jinsi alivyokuwa akiongea suzzane nadhani alikuwa akifurahia taarifa hio , na hii niliamini huenda ni kwa jinsi nilivyompa kazi hio hivyo alikuwa akilipiza kisasi , nilipata mshituko wa aina yake , moyo uliniuma hatari na hasira zilianza kupanda huku presha nayo haikuniacha salama , pumzi zilinikatika ghafra , na suzzane aliliona hilo na alinipa maji na kidogo hali yangu ikatulia .
“ mheshimiwa niendelee?”
“endelea tu suzzane nipo tayari kusikiliza “
“ mheshimiwa kama nilivyosema mkeo ashawahi kutoka kimapenzi na bendera kuhusu taarifa nyingine jinsi walivyo achana sina , ila waliachana baada tu ya kumaliza kidato cha nne na kila mtu kurejea nyumbani kwao , na kuanzia hapo bendera hakuwahi kuonekana kuwa na mahusiano tena na wema na hio nikutokana na ufaulu mdogo ambao alipata kidato cha nne , huku akiamini aliechangia matokeo yake mabaya alikuwa ni wema , hilo ni la kwanza ,la pili ni mkeo pia ashawahi kutoka kimapenzi na bruno lamberk na inasemekana wema ashawahi kubeba mimba ya bruno mpaka kujifungua lakini haikujulikana mahali mtoto alipo mpaka sasa hivi , hivyo nilishindwa kupata taarifa juu ya mtoto “ suzzane wakati akisoma hakujua kuwa nilikuwa kwenye hali gani kwani neno la mwisho kusikia lilikuwa ni ‘wema ashawahi kubeba mimba ya bruno ‘ hapo hapo ndipo nilikata moto nilikuja kuamka siku nyingine kabisa nikiwa hospitalini , mwanzoni baada ya kufungua macho yangu sikukumbuka ya jana lakini nilijishangaa kwanini nilikuwa ndani ya hospitali , na hapo ndipo nilipo anza kuvuta kumbukumbu zangu nyuma na kuanza kukumbuka wakati suzzane akinisomea ripoti ile , machozi ya kiume ndio yalio anza kunitoka tena mbele ya mke wangu , nijilikuta nikimwangalia kwa hasira mno huku macho yakiwa yameloana machozi .
“ kuna nini mume wangu , mbona uko hivi jamani “ aliongea wema , nilijikuta nikitamani kuongea chochote lakini nilijizuia lkuongea neno , moyo ndio uliokuwa ukiniuma mno , nilikaa hospitalini huku dokta akimwambia mke wangu kuwa nilipata mshituko wa moyo , wema alitaka kujua ni kipi kilichonifanya kuwa na mshituko moyo lakini sikutaka kabisa kuongea kitu , jambo ambalo nimeligundua lilikuwa likiniumiza sana moyo , kuna muda niliona bora hata nisingefatilia ya nyuma kwani yamekuja kuniumiza tu .
Baada ya hali yangu kuonekana ipo kidogo imetulia ndipo niliporudi nyumbani na mtu wa kwanza kuja kuniona alikuwa ni raisi bendera , nakumbuka hio ndio siku ambayoo nilithibitisha maneno ya suzzane na hio ni mara baada ya mheshimiwa bendera kusalimiana na mke wangu , wote walikuwa wakiangaliana kwa macho ya kuongea kabisa , mapenzi yanauma nyie yasikilizieni tu kwa wengine , jinsi moyo ulivyokuwa ukiniuma haikuwa na mfano , chuki yangu dhidi ya mheshimiwa bendera iliibuka kwa kasi ya ajabu sana , japo nilivumilia sana , lakini nilitamani kumkaba na kumuuliza kwanini alikuwa akinificha mambo , nilikuwa nikimwamini sana rafiki yangu bendera lakini kitendo cha kunificha juu ya uhusiano wake wa nyuma na wema liliniuma sana , lakini sikuwa na jinsi kabisa , nilichokuwa nikiwaza kwa wakati huo ni kutaka kujua kama walikuwa wakiendeleza mapenzi yao pasipo ya mimi kujua na hapo ndipo nilipo mpa moja ya vijana wangu kazi ya kumfatilia mke wangu .
Baada ya siku kadhaa kutengemaa nilimpigia tena suzzane nikitaka aje animalizie ripoti yangu na awamu hii sikutaka kabisa kwenda hata hotelini kwani nilimuita ofisini kwangu kabisa , sikujali tena juu ya usalama wake au nini .
“ suzzane nataka uniambie kuhusu mtoto wa bruno na mke wangu yuko wapi “.
“ mheshimiwa kwa taarifa nilizo nazo ni kwamba mkeo alijifungua salama mkoani singida , lakini baada ya hapo hakuwahi kuonekana kabisa kuwa na mtoto “.
“ kwa maana hio kuna uwezekano mtoto huyo kuwepo mahali anaishi na je alikuwa ni jinsia gani ?”
“ alikuwa ni mtoto wa kike “
“ na bruno alikuwa akijua juu ya hilo “
“ ndio muheshimiwa , kwani alienipa taarifa alisema bruno ndie aliemshawishi wema kuacha kazi mara baada ya kupata ujauzito “.
“wanawake wauji kabisa , nimekaa miaka yote hio pasipo kujua kuwa mke wangu ashawahi kujifungua bullshit .“
Nilijikuta nikiongea kwa hasira mno
ITAENDELEA
 
Suzzane hakutaka kukurupuka katika kufanya kazi yake , alikuwa na kazi mbili za kufanya kwa wakati huo ili kujua ukweli anaotaka kuujua , mtu wa kwanza aliekuwa akimfatilia , alikuwa ni janeth , na wa pili alikuwa ni stephano lamberk alikuwa makini kweli na kazi yake hakutaka kabisa kuwapa nafasi watu anaowafatilia wajue kama wanafatiliwa , na ndio maana alikuwa akitumia akili sana katika kuwafatiilia , hata ile alipogundua kuwa kuna uhusiano kati ya mke wa raisi na janeth hakutaka kumwambia mheshimiwa raisi , kwani aliona kabisa anapaswa kujua kabisa kile kinacho endelea na ndipo atoe taarfa hio kwa mkuu wake .
Siku hio ilikuwa ulikuwa ni muda wa saa mbili kamili akiwa ametoka kwenye mihangaiko yake ya kiuchunguzi , alikuwa amekaa mezani akijaribu kuunganisha matukio.
Jina la janeth bendera na jina la stephano lamberk ni majina ambayo yalikuwa kwenye akili yake .alikuwa na picha zilizokuwa zikiwaonesha wawili hao kuchekeana kabisa , picha alizochukua siku hio mchana ndani ya makao makuu ya kampuni ya NLT .
Alikuwa akiangalia picha ya stephano akiwa ameshikana mkono na janeth , na muda huo walionekana walikuwa wakiagana , tabasamu lililokuwepo kwenye uso wa janeth na pia kwenye uso wa bwana stephano lamberk vilimfanya aje na hitimisho kuwa wawili hao walikuwa wanafahamiana .
Lakini jambo la pili lililomchanganya ni jina la janeth “janeth bendera ‘ ni jina ambalo lilimchangaya sana , kilicho mchanganya Zaidi ni mwanadada huyo kuwa na elimu kubwa mno tena akiwa na umri mdogo , hakuamini kwamba mwanadada huyo ni kweli alikuwa na PHD kwa umri aliokuwa nao , jambo hilo kwake pia lilikuwa likimpa maswali mengi ambayo kuna muda yalikuwa yakigongana .
“ kama janeth ana PHD inawezekana pia alienda kwenye kampuni ya NLT kwa ajili ya biashara kwani wote wapo kwenye fani moja , lakini pia nina hisia wawili hawa wanaonekana kufahamiana kwa muda mrefu japo ni hisia zangu lakini naamini uwezekano huo upo , na kama watakuwa washakutana kabla kuna uwezekano pia wakawa wanashirikiana pia katika maswala mengine , ikiwemo la janeth kuchoma madawa ya kimbona , lakini bado kuna jambo linanichanganya na natakiwa kulifania uchunguzi , inawezekanaje huyu anae jiita mzalendo kutumia sura za watu wengine katika matukio yake ya nyuma , inatakiwa ni ujue ukweli lakini ukweli nitaujua vipi ?” hayo yote yalikuwa ni mawazo ya mwanadada suzzane , jasusi mbobezi aliekuwa akimtii sana mheshimiwa raisi katika kazi zake nyingi .
*****
Ni siku ambayo ndani ya kampuni ya NLT kulikuwa na kikao cha wakurugenzi wa bodi , yaani wale wamiliki wate wa kampuni walikuwa wapo kwa ajili ya kujadiliana mustakabali wa kampuni hio mpya tanzania katika maswala ya teknolojia kwa ujumla wake.
Kwa damiani hata yeye pia alifurahishwa sana na muamko wa watanzania , kwani kitendo cha kutangaza kuuza hisa asilimia ishirini na hisa hizo kununuliwa zote , aliamini sana watanzania wanaipenda teknolojia na wapo tayari kwa ajili ya kuona taifa lao likiwa linaendelea katika swala zima la teknolojia
Siku hio mda wa asubuhi ndio muda ya watu mbali mbali waliokuwa ni wamiliki wa hisa za kampuni ya NLT waliingia ndani ya ukumbi wa mikutano ndani ya jengo hilo la NLT , moja ya watu waliongia eneo hilo alikuwa ni Patrick mtoto wa mheshimiwa raisi .
Patrick alikuwa ni mmoja ya mmiliki wa hisa katika kampuni hio na haikueleweka kwanini alivutiwa na kampuni hio mpaka kununua hisa , kwani hata yeye pia alikuwa ni moja ya watu waliokuwa wamkimiliki kampuni inayo endana na hio ya NLT lakini pia alikuwa ni adui mkubwa wa kampuni hio .
Kilichomshangaza Patrick ni mara baada ya kuingia ndani ya ukumbi wa mikutano ni kumuona merina , hakujua kuwa na merina alikuwa ni mmiliki wa asilimia kadhaa ndani ya kampuni hio sio kwake tu lakini pia kwa merina pia alishangazwa na uwepo wa Patrick ndani ya ukumbi huo kwani pia hata yeye hakujua kuwa patrick alikuwa mmiliki wa hisa ndani ya kampuni hio .
Nusu saa baada ya watu wote kuingia ndani ya ukumbi huo , akiwemo janeth , na mainjinia wengine , rebbecca , luang shu hakuwepo kwani alikuwa tayari amekwisha rudi nchi kwao china .
Basi damiani aliingia huku akiwa amevalia suti yake safi kabisa ya bei mbaya , alikwenda moja kwa moja kuketi katika kiti chake maaulumu kama kurugenzi wa kampuni hio , lakini pia kama mmiliki wa kampuni kwani yeye ndie aliekuwa anahisia nyingi katika kampuni hio ( major share holder ).
Damianni ama stephano na yeye pia alijikuta akishangazwa na uwepo wa merina ndani ya eneo hilo , alikuwa akimjua merina kama mteja wake , lakini hakujua kuwa mwanadada huyo alikuwa amekwisha kununua hisa katika kampuni yake , alijikuta moyo wake ukifurahi , hali ambayo hata yeye hakujua kwanini alikuwa akifurahi , aligeuza upande wa janeth na wakagongana macho na kila mmoja alitabasamu .
Basi kikao icho kilianza kwa kutambulisha watu mbali mbali waliokuwa wakimiliki hisa zao kwa asilimia zao na Patrick alikuwa akimiliki asilimia kumi na merina pia alikuwa akimiliki asilimia kumi , pia kikao kiliambatana na moja ya malengo ya kampuni siku za usoni .
MASAA MACHACHE NYUMA .
Kitendo cha stephano kuitwa jina lake halisi na mrembo janeth kilimchanganya na kumshitua kwa wakati mmoja , hakujua ni kwa namna gani mrembo huyo alimjua , japo alikuwa akikumbuka kuwa mrembo huyo kuna sehemu ashawahi kukutana nae , lakini swala la kumjua kuwa amevaa ngozi feki lilimchanganya .
“ usiwe na waswasi siri yako ipo salama “ aliongea janeth kwa mapozi .
“ wewe ni nani ?”
“ mimi ni janeth mfanyakazi wako “ aliongea janeth kwa mapozi huku akizunguka ndani ya ofisi hio kama mtu aliekuwa akiichunguza na alionekana alikuwa akijiamiani sana mbele ya damiani .
Stephano japo mwanadada huyo alikuwa ameonesha kujua siri yake lakini hakutaka kabisa kuwa mwepesi aliweka ngumu
“ sijui unacho ongea kuhusu siri “
“ hahahaha… kwa hio unamaanisha ninayo ongea hapa ni uongo “
“ ndio ni uongo , inakuwaje unaniita jina ambalo sio la kwangu na huyo damiani ni nani ?”
“ damiani ni jina lako halisi nakujua A to Z najua unaweza ukawa umenisahau , au unataka nikukumbushe tulipokutana mara ya kwanza “.
“ sijawahi kukutana na wewe mimi “ aliongea stephano kwa kujiamini huku akiangalia tarakishi yake “
“ naona umesahau siku ile ulivyogongana na mimi ndani ya hoteli ya four season china wakati unaenda kuonana na waziri wa china “
Hapo ndipo stephano alipokumbuka sehemu aliokutana na mwanadada huyo , alijikuta akijilaumu kwa kutomkumbuka mapema , alimkumbuka mwanadada huo alipogongana nae wakati anaingia kwenye lift .
“ naona umenikumbuka sasa “
“ janeth nina kazi kwasasa naomba tuishie hapa kwa leo “ aliongea stephano kwa sauti ambayo ilionesha kuwa na waswasi ndani yake .
“ usijali damiani , kwanza unaelewa kuwa hio ngozi ndio mimi nilioitengeneza , au luang shu hajakwambia “
Kauli hio ndio iliomfanya stephano kushangaa Zaidi , na hapo hakuwa na ujanja kabisa , mpaka hapo alijikuta akikumbuka kauli ya luang shu kumwambia kuwa mtu alieitengeneza FULL BODY MASK alikuwa ni mtanzania mwenye phd yake , mpaka hapo alijua kuwa mtu aliekuwa akiongea nae alikuwa akimjua vyema .
“ wewe ndio uliotengeneza full body mask “.
“ ndio ni mimi damiani “ aliongea janeth huku akikaa kwenye sofa huku akimwangalia damiani akiwa ameachia tabasamu
“ ila sikujua kuwa unatumia jina la stephano lamberk mpaka nilipo kuona , nikajua umevaa ngozi bandia “
“ sina hoja , ila nasema hongera sana “
“ asante damiani , ila nilikuwa nikikutafuta sana tokea siku ile ulionigonga “
“ ulikuwa ukinitafuta!! , kwa ajili ya nini ulikua ukinitafuta ?”
“ nitakuambia siku nyingine damiani , kwasasa kuna majukumu yangu nataka kwenda kuyashughulikia lakini nisindikize basi “ aliongea mrembo huyo na kisha damiani alinyanyuka na kutoka na janeth mpaka eneo la kupark magari na walipeana mkono kwa bashasha kubwa , na wakati wanapeana mkono ndio wakati ambao suzzane alikuwa akiwapiga picha .
*****
Mheshimiwa raisi japo swala la uwekezaji wa Stephano lamberk lilikuwa swala lenye tija kwa nchi , lakini kwake aliliona wala hilo kama mwiba katika maendeleo yake mwenyewe , alijua kuwa kampuni ya INNOVA na kampuni ya NLT kuingia nchini na kuwekeza inamaanisha yeye kampuni yake kufa kabisa , kwani aliamini asingeweza kabisa kushindana na INNOVA na NLT, alikuwa akiwaza mambo kadha wa kadha ni kwa namna gani angeishi pasipo kupata hasara Zaidi . mchaga huyu japo ya kuwa raisi lakini alikuwa akipenda pesa pia , na ndio maana alikuwa tayari kufanya lolote kwa ajili ya kujiingizia pesa .
Siku hio ni baada ya kuonana na bwana stephano na kufanya mazungumzo nae , alikuwa ameshikilia karatasi ya asilimia za hisa ambazo zilikuwa zikiuzwa na kampuni hio ya NLT alikuwa amekaa chini akiwaza ni maamuzi gani afanye , lakini pia upande wa pili pia alikuwa akiwazia uwekezaji wa kampuni ya INNOVA ambayo pia ilikuwa ikiuza asilimia za hisa zao .
Baada ya kuwaza muda wa masaa kadhaa , ndipo alipokuja kufanya maamuzi ya kununua hisa katika makampuni hayo yote mawili kwa wakati mmoja , alitoa simu yake na kupiga mahali .
“ nataka kununua hisa zote za kampuni ya NLT na INNOVA “ aliongea mheshimiwa .
“ mheshimiwa hisa zilizobaki ni asilimia kumi tu kwa kampuni zote mbili “”
“ hizo zingine zimeenda wapi “
“ zimekwisha kununuliwa na SWIFT TRANSIT “
“ okey sawa nitanunua hizo zilizobaki nafanya muamala sasa “ aliongea na kisha alikata simu .
“ huyu ni merina mchumba wake Patrick huyu , mwanamke anaakili sana huyu sijui Patrick anakwama wapi kumuoa huyu mwanamke , inabidi nimuite nifanye nae mazungumzo “ alijifikiria huku akiendelea kuchezesha simu yake , na dakika kadhaa alikuwa ashanunua hisa zote .
Mara baada ya kufanikisha hilo ndipo alipoendelea na majukumu yake , mpaka muda wa kutoka ofisini.
Lakini kabla ya kutoka aliingia kijana wake ambae alikuwa akimfanyia baadhi ya shughuli zake binafsi , kijana huyu aikuwa akijulikana kwa jina la talimba , alikuwa ni kijana msomi mno aliekuwa ni mwanausalama kitengo cha ikulu , na moja ya kazi kubwa ambayo alikuwa amempa kijana huyu kuifanya ni kumfatilia mke wake , kwani mheshimiwa raisi japo alikuwa akimpenda sana mke wake lakini hakuwa akimuamini hata kidogo , haikujulikana ni sababu gani hakuwa akimuamini mke wake
“ vipi talimba kuna habari yoyote “
“ ndio muheshimiwa na ndio maana niko hapa “ aliongea talimba , alikuwa ni kijana mojamfupi maji ya kunde mwenye macho makubwa hivi na mwili wake mnene kiasi .
Muda huo mheshimiwa alikuwa amesimama nje ya ofisi na alikuwa akitaka kuelekea upande wa familia yake , lakini ilibidi aghaili na kurudi ndani ya ofisi kuongea na talimba , kwani alijua kabisa kila talimba anapofika anayo taarifa , basi jua ni taarifa ya siri ambayo hakutaka mtu oyote yule ndani ya ikulu aifahamu
“ mheshimiwa madam siku mbili zilizopita kakutana na mwanadada anaefahamika kwa jina la janeth bendera muda wa jioni maeneo ya ununio ndani ya nyumba moja ambayo kwa kufatilia niligundua kuwa inamilikiwa na msichana huyo , pia siku ya jana yake alikutana na mwanadada merina muda wa saa kumi kamili ndani ya hoteli ya serena “
‘’umesema janeth , huyo janeth ni nani “
“ janeth kwa taarifa nilizo nazo ni mwanasayansi aliengia nchini miezi kadhaa iliopita akitokea china , kiwango cha elimu yake ni PHD “”alijjibu talimba na kumfanya bendera ashangae na awaze kidogo na majina hayo mawili yalipita ndani ya kichwa chake yaani ‘merina na janeth’.
“ safi endelea kuwafatiilia na unipe taarifa Zaidi “
“ sawa muheshimiwa “
Baada ya mheshimiwa kupewa taarifa hio na talimba alitoka ofisini na kwenda upande wa familia yake na kuonana na mke wake aliekuwepo sebleni akiangalia tamthilia , wema mara baada ya kumuona mme wake , aliinuka na kumkumbatia
Mheshimiwa alioga na kisha alimua kupumzika huku akijaribu kuwaza jambo la mke wake kukutana na merina na janeth hakujua ni kwanini wamekutana ila aliamini kama kuna mpango unaendelea ambao yeye haujui basi angeujua tu , muda wa saa mbili kwenda tatu ndipo alipo mkumbuka patrick na kumpigia simu na kumpa maagizo ya kufika ikulu siku inayo fata .
Ilikuwa siku nyingine siku ya asubuhi na mapema ndio siku Patrick alifika kwa ajili ya kuonana na baba yake na walianza mazungumzo
“ kesho nataka ukahudhurie kikao cha wana hisa ndani ya kampuni ya NLT , nimenunua hisa asilimia kumi ndani ya kampuni ile japo nilihitaji kununua zote ila inaonekana mkwe kanizidi ujanja “
“ mkwe gani baba “
“ si merina au kuna mwingine ?”
“ inamaana merina kanunua hisa kwenye kampuni ya NLT “
“ ndio , inakuwaje merina ni mpenzi wako na hujui hilo “
“ baba mimi na merina hatuzungumzi sana maswala ya kazi “
“ anhaa sawa .. ila patrIck kuna kitu sikielewi , hivi unaamini kweli yule mwanamke anakupenda ?”
“ baba hata mimi mpaka wakati huu nachanganyikiwa kabisa , nampenda sana merina , lakini merina kuna mtu anampenda “
“ kuna mtu anampenda , unamaanisha sio wewe “
“ ndio baba kuna kijana mmoja anafahamika kwa jina la damiani , ndio merina anampenda lakini mpaka sasa kijana huyo hajawahi kuonekana tokea atekwe”
“ unasema damiani?? “
“ ndio mbona umeshituka unamfahamu ??“
“ hapana lakini ni kama nishawahi kulisikia hilo jina “
‘ yawezekana baba kwani ni moja ya watu waliokuwa wakihusiana na bruno , kwani mama yake alipigwa risasi na mahasimu wa bruno “
“ kwa hio unamaanisha merina na damiani wanafahamiana , na walifahamiana vipi ?”
“ hata mimi swala hilo linanichanganya , sijui wapi walikutana ila najua wanafahamiana kwani merina alilia sana siku ambayo alitekwa “ aliongea Patrick huku akimuhadithia baba yake tukio la damiani kutekwa ndani ya hosputali ya lushoto “
“kweli inaonekana wanafahamiana , sasa unamaamuzi gani juu ya merina maana hata mimi nimetokea kumpenda yule mwanamke , ana akili sana za kimaisha na kama atakuwa mke wako atakusaidia sana “
“ baba hata mimi mpaka sasa sijui nifanyeje kumteka merina kihisia kwani nampenda sana “
“ hahaha kijana wangu wanawake ni viumbe dhaifu sana , hakikisha merina anakuwa mke wako , usikubali mtu mwingine akimchukua kutoka kwako “ aliongea raisi na kumfanya Patrick atabasamu .
“ baba umenitia nguvu sana , na mimi lazima merina awe mke wangu sitoruhusu mtu yoyote amchukue “
“ safi sana kijana wangu , pia hakikisha bishara zinaenda vizuri “
‘ sawa baba “
Itaendelea
SEHEMU YA 42
Zakayo alikuwa mtu mjanja sana katika kufanya uchunguzi , na kilichokuwa kinampa uwezo wa kujua jambo hata kama limejificha ni kutodharau kila taarifa inayomfikia , kwani baada ya kupata taarifa aliokuwa akiitaka kutoka kwa Irene basi aliona ni mwanzo mzuri wa kuendelea na uchunguzi wake .
‘stephano lamberk ‘ ni jina lililomvutia sana jasusi huyu , aliamini kabisa kuna taarifa iliokuwa Imejificha juu ya bwana stephano lamberk , kwani kupita taarifa za maisha ya nyuma ya bwana bruno kutokuwa na mtoto wa kiume wala ndgu yoyote , aliamini lazima kuna jambo nyuma ya stephano lamberk .
Jambo la kwanza ambalo aliona anapaswa kulijua undani wake, ni swala zima la bruno lamberk kupigwa risasi na kuuwawa , aliamini kwa kulifanyia swala hilo uchunguzi , angejua ni watu gani walimuua na swala hilo huenda lingepelekea kujua ni wapi alipo damiani .
Mwanzoni kazi hio aliona ni nyepesi sana , lakini sasa aliona ni kazi ngumu mno kwake , hata waliompa kazi walipomuuliza maendeleo ya uchunguzi wake aliishia kuwaambia kuwa wampe muda wa kulifanyia uchunguzi swala hilo kwa undani zaidi .
Siku hio alikuwa ndani ya jiji la Arusha , haikujulikana alikuwa ndani ya jiji hilo kwa ajjili ya nini , lakini aliamini kuna kitu angekipata ndani ya jiji hilo ambacho kingemsaidia katika upelelezi wake, alienda mpaka ndani ya hoteli moja kubwa ya kitalii iliokuwa ikipatikana ndani ya jiji hilo iliokuwa ikifahmika kwa jina la gran melia .
baada ya kuweka mizigo yake michache ndani ya chumba hiko alijipumzisha , na muda huo ilikuwa yapata saa kumi za jioni , alikuja kushituka kutoka usingizini muda wa saa mbili za usiku , na kilizho mshitua ni mlio wa simu .
“ vipi uko wapi “
“ ilikuwa ni sauti iliosiikika katika masikio yake “
“ niko hotelini “
“ mtu wako nimemuona sasa hivi hapa triple A “
“nakuja sasa hivi , hakikisha humpotezi “ aliongea zakayo na alianza kujiandaa haraka haraka na kisha alitoka ndani ya hoteli hio na kuchukua usafiri wa taksi uliomfikisha mpaka triple A
Ni moja ya sehemu ambazo zilikuwa zimechangamka sana , watu walikuwa wengi wakiwa wanakunywa bia , na wengi wao walikuwa ni machalii wa miaka ya ujana .
Baada ya kuingia eneo hili la club alitoa simu yake na kupiga na dakika kadhaa alitoka mwanaume mmoja mnene kiasi mwenye miaka kati ya miaka ishirini na nane hivi aliekuwa amevalia kinadhifu kabisa , bwana huyu alikuwa akifahamika kwa jina la godlove .
Baada ya kuonana na godi waliingia wote ndani ya club hio na kuchagua sehemu na kuketi na god love alimuonesha mtu ambae alikuwa anamtafuta , na zakayo alijikuta akitabasamu baada ya kuona kuwa mtu anaemtafta alikuwa mwenyewe .
“unataka tufanyeje , maana jamaa anaishi kwa machale sana “
“ nataka nimteke kibabe , lakini sina shemu ya kumpeleka “
“ kuna karakana moja hivi nahifadhia kahawa tunaweza mpaleka “ aliongea
“ hapo fresh , ngoja niendelee kumlia timing , si umekuja na gari yako ?”
“ ndio ipo “
Basu baada ya masaa kadhaa hivi kupita , ikiwa imetimu saa nne kamili mtu waliekuwa wanamfatilia alionekana kunyanyuka kwenye kiti chake akiingia kati ya watu waliokuwa wanacheza mziki , na kuanza na yeye pia kucheza , jambo hilo ni kama zakayo alikuwa akilisubiria , kwani alitabasamu na kisha alinyanyuka.
“ nisubirie kwenye gari yako “ aliongea zakayo na kisha god alitoka na zakayo kuingia kati ya watu na kuanza kucheza huku target yake ilikuwa ni kumpata mwanaume huyo aliekuwa akicheza hapo ndani , alijua sio jambo rahisi kwani mtu aliekuwa akimsogelea alikuwa ni mtu hatari mno , na alijua kosa moja tu anaweza kumkosa na hilo hakutaka litokee kwani alikuwa akimtafuta mno .
Baada ya kumfikia akiwa bize , mara alijikuta akizongwa na watu ambao walimfanya kumzibia kwa mbele , aliwapangua na kupita na hapo ndipo alipo pigwa na mshangao kwani mtu aliekuwa akimtafuta hamuoni tena , alijikuta akianza kujipenyeza kwenye watu huku akizungusha shingo , lakini hakumuona , alichoka , alijua tayari ashashitukiwa tayari na mtu ashapotea , na kama alivyosema god kuwa mtu huyo alikuwa ni mtu anaeishi kwa machale aliona jambo hilo ni la kweli , wakati akiwa anaendelea simu yake ilivibrate na haraka aliitoa na kuangalia meseiji .
“ mtu wako huyu huku anasepa “ ilikuwa ni meseji iliomkurupusha zakayo na haraka alielekea upande wa kutokea nje , na ile anafika tu aliingia ndani ya gari la god .
‘ kaelekea wapi ?”
“ katoka saivi na gari ya Subaru “ aliongea na kisha walianza kulitafuta gari hilo uelekeo wake , na uzuri ni kwamba walikuwa wakitumia range . hivyo zakayo aliamini kwamba kama wangemfukuzia wangempata kiurahisi muda huo walikuwa ndani ya barabara ya kaloleni na mbele kidogo walikuta wakiiona gari hio na hapo zakayo alitabasamu , uzuri ni kwamba muda huo hakukuwa na magari mengi hivyo jambo lao lilionekna kuwa rahisi , lakini pia gumu kwani mtu waliekuwa wanamfatilia alionekana kujua kabisa kuwa anafatiliwa maana spidi alikuwa anatembea nayo ilikua juu , dakika chache gari ile ilikunja simeon road , na wakina zakayo hawakutaka kabisa kuipoteza kwani muda huo walikuwa wameikaribia kabisa , walikuja kufanikiwa kuipita kwa mbele na kuizuia gari hio nyuma kidogo na barabara ya kwenda njiro .
Baada ya kuizuia bwana huyo alitoka kwenye gari na kutoka nduki na zakayo hakutaka kabisa na yeye kubaki nyuma kwani kama mshale alichomoka na kuanza kumfukuza kwa nyuma , jamaa alikuwa kwenye spidi ya hali ya juu lakini pia zakayo vile vile, alikuja kumkamatia kwenye kona ya kuingia vijana rd. lakini bado jamaa huyo hakutaka kukamatwa kizembe kwanni alianza kupambana na zakayo , lakini zakayo alionekana kuwa imara kwenye mapambo kwani mapigo mawili tu yalikuwa yamemdondosha chini , kuna baadhi ya watu walijikuta wakivutiwa na tukio hilo , lakini zakayo hakutaka kuwapa nafasi kwani alimbeba mtu wake na kuondoka eneo hilo , mpaka alipo kuja kukutana na god na kumpakia mtu wake na safari ya kuelekea kwenye karakana ya god ikaanza , dakika chache walikuwa kijenge , gari ilikunja kulia na kwenda kusimama kwenye jengo moja kuu kuu, alitoa ufunguo na kufungua mlango na kumuingiza ndani mtu wake na kisha alimzindua .
“ nyie ni wakina nani , kwanini mnanifatilia ?”
“ na wewe ni nani kwanini unatukimbia “
“siawakimbia mimi “
“sikia bwana mdogo sipo hapa kwa ajili ya kukudhuru ila kuna taarifa naihitaji kutoka kwako “
“ taarifa gani unataka kutoka kwangu ukiwa umenifunga”
“sikia najua ulikuwa moja ya walinzi wa bwana bruno lamberk “ aliongea zakayo na kumfanya bwana huyo ashituke .
“ simfahamu mtu huyo “
“ najua ungejibu hivyo , kama nilivyo kuambia sipo hapa kwa ajili ya kukudhuru ukinipatia taarifa yangu nnayo hitaji nakuachia huru “
Aliongea zakayo na kisha alitoa kitambulisho bandia chenye jina tofauti na kumuonesha bwana huyo , na jamaa alishangaa baada ya kuona kitambulishho hicho kilichomuonesha kuwa mtu huyo alikuwa ni mwanausalama , alijikuta akivuta pumzi nyingi na alionekana kama mtu alieshukuru “
“ ni kweli mimi nilikuwa mlinzi wa bruno lakini sina taarifa yoyote kwenu ”
“ sasa mbona unaonekana kuwa na waswasi “
“ lazima niwe na waswasi maana tokea kifo chake maisha yangu yamekuwa yakujificha “
“ kwanini unasema ni yakujificha ?”
“ walinzi wote wa bruno wameshakufa nilepo hai ni mimi tu “
“ unaamaanisha wenzako wote walikufa na kwanini wafe “
“ sijui sababu “
“ ulianza kuwa mlinzi wa bruno kwanzia lini ?”
“ miaka nane sasa “
“unafikiri ni kwanini wenzako wamepoteza maisha “
“nadhani ni maadui wa bruno “.
“ wee unwafahamu maadui wa bruno ?”
“hapana siwafahamu wote ila kuna baadhi nawafahamu aliokuwa anafanyanao biashara “
“kwanini wawe maadui wakati alikuwa akifanya nao kazi “
“braza nakujibu tu kwasababu wewe ni mwanausalama , lakini maisha yangu yapo hatarini naomba unisaidie hata nitoke nje ya hii nchi “
“ kama unataka kuwa salama na nikusaidie nipe taarifa muhimu ambayo itanishawishi” aliongea zakayo huku akimwangalia kijana huyo .
“ ninayo ndio , lakini lazima unihakikishe kuwa nipo salama “
“ mpaka sasa upo salama bwana mkubwa , kwanza jina lako nani “
“ Herbert sheiza “
“ wewe ni mwenyeji wa wapi “
“ lushoto “
“nipe hio taarifa “
“kuna mpango wa siri boss aliuandaa kabla ya kifo chake “ aliongea Herbert na kumfanya zakayo atabasamu .
“ mpango gani?? “
“damiani “
“ damiani ni nani ?”
“ damiani ndio mpango wenyewe “
“ unamaanisha nini kusema damiani ndio mpango wenyewe “
“ boss alimchagua damiani katika kutimiza mpango huo , na hata mama yake damiani kuuwawa ulikuwa mpango wa boss “ zakayo alijikuta akitoa jicho kwa mshangao
“unamaanisha nini kusema hivyo “.
“ “mimi najua hivyo tu kuwa mama yake damiani kuwawa ulikuwa mpango wa boss , na pia walikuwa wakimfatilia damiani tokea akiwa chuo na aliepewa kazi hio alikuwa ni danieli ambae ashakufa “
“Nipe taarifa nyingine hio bado haitoshi kukusaidia nataka uniambie kila unachokijua kuhusu boss wako “.
“ boss alikuwa anauza madawa ya kulevya , mpaka pale alipowasaliti wenzake na kuungana na raisi bendera , na mpaka sasa sisi tulishangaasababu ya boss kuwasaliti wenzake , lakini moja ya mlinzi mwenzetu alituambia kuwa boss kashikwa pabaya na raisi bendera merehemu na wote tulikubaliana na hilo , lakini mpaka sasa hatukujua ni nini kinaendelea kwani boss aliongezewa ulinzi “.
“.unajua aliemuua boss wako “.
“ sifahamu ila kuna watu wawili nawahisi kuhusika “.
“ nani na nani “
“ suzzane “
“ suzzane ndio nani ?”
“ ni moja ya walinzi walikuwa wametumwa na mheshimiwa raisi kumlinda boss “
“ sasa kama suzzane alikuwa anamlinda boss kwanini useme kuwa ndio kamuua boss huyo huyo “.
“ kwasababu suzzane ndie aliemuua danny “. Aliongea bwana Herbert na kumfanya zakayo ashangae , kilicho mfanya ashangae ni kwamba alikuwa akiwajua vyema suzzane na danieli kama moja ya makomandoo wenzake , lakini pia alifahamu fika kuwa danny na suzzane walikuwa wakivunja sheria za usalama wa taifa kwa kuwa wapenzi , lakini kuambiwa kuwa suzzane ndio aliemuua danny swala hilo lilimshangaza “
“ wee ulijuaje haya yote ?”
“ siku ambayo danny anapigwa risasi nilishihudia kwa macho yangu”
“umesema umeshuhudia kwa macho yako hebu niambie kilichotokea “
“ siku hio baada ya kifo cha boss kila mlinzi alitawanyika , kimya kimya kwani tulijua hali isingekuwa salama tena , mimi sehemu nilio fikiria kujificha ni kwenda kujificha kwa bibi mkuzi , siku ambayo damiani anaingia ndani ya mkuzi akiwa na danny niliwashuhudia , lakini jambo lililo nishangaza ni mara baada ya danny kupigwa risasi na mtu aliejificha juu ya mti mwanzoni sikuwa nimemuona vizuri mpaka pale aliposhuka chini na hapo ndipo nilipomuaona suzzane , lakini hakuwa peke yake , alikuwa na bwana mmoja hivi mzungu mzungu hivi “.
“ na damiani je ?”
“ damiani alikimbia na mimi pia nilikimbia na sikukaa tena kwa bibi ndio nilikuja huku Arusha kwanzia siku hio , lakini bado kuna watu walikuwa wakinifatilia kwanzia siku hio na ndio maana maisha yangu yalikuwa ya kujificha sana , na hata nilivyowaona pale club niliwagundua tu ni walewale “.
Zakayo aliridhshwa na maneno ya Herbert mno , lakini pia ni nameneno ambayo yalimuacha kwenye mashangao , baada ya mahojiano yake kumalizika , hakuona sababu tena kubaki eneo hilo , god aliondoka na Herbert na zakayo alienda hotelini .
“ mama yake damiani kuuwawa na bruno , linawezekanaje hili , na ni mpango gani huo ulikuwa ukisukwa , najua suzzane kumuua danny ni lazima itakuwa ni oda kutoka kwa raisi lakini hili la mama yake damiani kuuwawa linanichanganya “ aliongea zakayo mara baada ya kufika hotelini akiwa amejilaza akiwaza mambo hayo , alijikuta akianza kuunganisha matukio ya upelelezi wake wote “
“kwanini bruno amuue mama yake damiani ni mpango gani bruno alikuwa nao , na kwanini bruno afie nyumbani kwa damiani , watu wawili waliokuwa ndani ya nyumba ya wakina damiani walikuwa ni wakina nani, je mpango huo suzzane alikuwa akiujua , ni nani aliemsaidia damiani kwenda thailland je ndio mpango wenyewe wa bruno, lakini hata kama bruno ashakufa tayari , aisingeweka mpango ambao na yeye anakufa , ni Dhahiri kabisa kuwa mpango wake ulifeli , lakini hata kama umefeli , damiani ni nani anaemsaidia?, sehemu ni moja tu ya kupata jibu na sehemu hio ni ndani ya ubalozi wa kenya , balozi wa kenya lazima atakuwa anajua kinacho endelea maana si rahisi kwa mtu mkubwa kumsafirisha damiani pasipo ya kufahamiana nae “ hayo ndio maswali alio ona kwamba anapaswa kuyajibu kwani muda huo hakuwa na jibu hata moja “.
*******
Carlos Cardosso muuaji huyu wa kimataifa , mara baada ya kushindwa kazi yake ya kwanza aliokuwa amepewa na kimbona , kazi ya kupata nyaraka alizoacha bruno kutoka kwenye mikono ya damiani , kazi ambayo alifiifanya akiwa na suzzane , mkataba wake na kimbona ulivunjika , lakini pia japo mkataba wake na bwana huyo ulivunjika , lakini pia hakutaka kurudi gerezani na ndio maana aliamua kumuomba bwana huyo kuendelea kuishi uraiani huku akiahidi kufanyakazi zote ambazo atakuwa anampa.
Kambi yake rasmi ilikuwa ni ndani ya jiji la lushoto tanga ndani ya mlalo , sehemu ambayo ndio kulikuwa na kambi ya kimbona , lakini taarifa ya mzigo wa madawa ya kulevya wa mabilioni uliokuwa ukimilikiwa na boss wake huyo kupotea , jambo hilo lilimshangaza sana , na hata pale alipopewa taarifa ya kufika dar kwa ajili ya kulifanyia uchunguzi swala hilo , aliamini kabisa mtu ambae anamfanyia uchunguzi alikuwa ni mtu wa hatari sana , kwani kitendo cha dawa hizo kutolewa bandarini mpaka kupelekwa bagamoyo na kuteketezwa alikiri kuwamtu huyo alikuwa ni mwenye welevu mkubwa wa akili katika kupanga mipango yake na yeye pia aliona ili kufanikisha kazi ya boss wake bila makossa ni kuhakikisha kuwa na yeye anakuwa na akili vile vile katika kupanga mipango yake .
Mara baada tu ya kufika ndani ya jiji la dar mtu aliemkumbuka alikuwa ni suzzane , na kwakuwa alikuwa anamawasiliano na mrembo huyo hakupata shida ya kuonana nae , suzzane ndie aliempa taarifa zote za muhusika mkuu anaemtafuta , jambo hilo lilionekana kumfurahisha sana carlos , lakini pia lilimrahishia kazi yake .
Siku hio alikuwa makini sana kumfatilia janeth , alitaka kujua ratiba yake yote , lakini pia kuwa na tahadhari atakapotaka kumfanyia tukio mrembo huyo , kwani kama alivyopewa maelezo na suzzane kuwa mrembo huyo ni hatari kimapigano .
Siku hio alipanga kufanya tukio la kumteka janeth , ili akampe mateso kama alivyo ambiwa na boss wake ili kujua ni nani aliechini yake .
Saa saba kamili za usiku ndio muda ambao aliingia ununio , mbele kabisa ya jumba analoishi janeth huku akiwa na taarifa za muonekano wote na ramani nzima ya nyumba hio mpaka chumba anacholala mlimbwende huyo .
ITAENDELEA
NILIKUWA NIMESHIKWA NA MALARIA WADAU TOKEA JUMAPILI NILISHINDWA KUANDIKA KABISA HATA KUWAJIBU. .
SEHEMU YA 43
Carlos alikuwa amezamilia kuhakikkisha tukio la kumteka janeth linafanikiwa kwa asilimia mia , na ndio maana alifanya uchunguzi wa ratiba zote za mwanadada huyo kwanzia muda anaolala , chumba anacholala , walinzi wanaolinda nyumba hio , watu wanaoishi nao na ramani nzima ya nyumba jinsi ya kuingia na kufanya tukio lake pasipo kukwama haikueleweka utafiti huo alifanya saa ngapi , lakini kila kitu kilikuwa kipo mikononi mwake na jambo lilokuwa limebaki ni kukamilisha tu kazi yake .
Muda huo wa saa saba aliofika ndani ya jengo hilo alizunguka mpaka nyuma ya ukuta na kama chui aliparamia ukuta na kutua ndani pasipo kushitukiwa wala kupigisha kelele , na jinsi alivyoruka na ukuta ule ulivyokuwa na umeme aliruka kitaalamu sana .
Mara baada ya kutua ndani pambeni kabisa ya swimming pool alianza kuangaza kulia na kushoto kuangalia usalama , baada ya kuona hali ikoshwari alitembea kuelekea upande wa nyumba ambayo walikuwa wakilala walinzi , akiwa na bastora yake mkononi aina ya pistol F3 blaser na usoni akiwa amejiziba vyema kuzuia sura yake kuonekana .
Basi kama mwanajeshi wa navy alivyofika kwenye mlango aligonga kama mara tatu kwa nguvu lakini sio kwa kelele sana na kisha alijibanza pembeni ya mlango , na zilipita kama sekunde sitini tu mlango ulifunguliwa , na mtu wa kwanza kutoka alikuwa ameshika bastora huku akiwa na kifua wazi , lakini uzembe wa mtu huyo ni kutoka bila tahadhari na hio ilikuwa fursa moja kwa carlos kwani alimvuta kwa staili moja ya kijeshi na kumzimisha na kisha kumlaza chini , baada ya kuona zoezi lake limefanikiwa alichokifanya ni kufunga kiwambo cha kuzuia sauti kwenye pistol yake na kisha alizama kama kinyonga ndani ya nyumba hio , ilikuwa na vyumba kadhaa ambavyo kwa haraka haraka alijua kuwa kila chumba kilikuwa na walinzi wamelala , alisukuma kitasa cha mlango wa kwanza na kikakubali na jamboo hilo lilimfanya apate tumaini kwani aliingia kiulaini na kuzama ndani na hapo ndipo alipokutana na vitanda viwli kimoja kina mtu kalala na kingine kilionekana hakina mtu na hapo hisia zake zilimwambia kuwa chumba hicho kilikuwa ndio chumba anacholala mlinzi aliemzimisha nje .
Ni mvumo wa risasi ndio uliosikika kwa mbaali na kukifumua kichwa chamlinzi aliekuwa akikoroma huku damu zikitapakaa , baada ya kuona zoezi hilo limefanikiwa alitoka taratibu na kwenda kwenye chumba kinachofata kisha aligonga mlango maana chumba hicho kilikuwa kimefungwa kwa ndani na mara baada ya kugonga mlango ulifunguliwa na jamaa mmoja mnene alitokezea uso na hapo hapo carlos alitokea kwa mbele yake na kumnyooshea bastora huku akimpa ishara atokea nje ya chumba hicho na bwana yule kwa kutetemeka sana alitoka nje pasipo kelele na hakuchelewesha alitwangwa risasi na kisha carlos akaingia ndani kwa spidi , lakini bahati haikuwa yake kwani ile anaingia alijikuta akilambwa teke lililomyumbisha pembeni na bastora yake kudondoka , na hapo ndipo aliposhudia mwanaume alikuwa amevaa boksa akiwa amekunja ngumi , lakini usoni akionesha hali ya hofu mno jambo ambalo kwa carlos alilichukulia kama udhaifu .
“ wewe ni nani ?” lilikuwa swali kutoka kwa bwana huyo lakini carlosa aliona swali hilo alijibu kwa vitendo kwani alimsogelea bwana huyo kwa kasi na hakuchelewa alimpiga mapigo mawili yaliomzimisha chini , hakuwa na muda wa kupoteza maana alikuwa na dakika kadhaa za kufanya tukio la kumteka janeth kabla hajashtukiwa , aliinama na kuchukua bastora yake na kisha alimpiga risasi ya kichwa yule mlinzi na kusababisha damu kuruka mpaka kwenye mapazia .
Baada ya kuona zoezi lake limefanikiwa alirudi kwenye chumba cha kwanza na alipekuwa pekuwa na akaja kuibuka na rimoti moja ya rangi ya majivu na kutoka nayo nje na mara baada ya kutoka na kumpita mlinzi aliemzimisha ni kama alikumbuka kitu kwani aliangalia nyuma na kisha alimchapa risasi yule mlinzi na kisha alitembea kuelekea mlango mkubwa wa kuingilia ndani ya nyumba kubwa , alifika na kuminya kitasa na alikuta kilifungwa kwa ndani na kwa kutumia utundu wake sekunde chache tu tayari mlango ulikuwa umefunguliwa , alizama ndani na kukutana na sable huku mwanga wa taa za nje ukimulika ndani ya sable ile , hakutaka kwenda kwenye vyumba vingine kwani alikuwa akijua ni chumba gani janeth alikuwa analala .
Alitembea kama mwanajeshi komandoo na kufikia mlango wa chumba cha janeth juu ya floor ya kwanza ya nyumba hio na kisha alishika kitasa na kukinyonga na uzuri ni kwamba mlango haukufugwa kwa ndani alizama taratibu huku akiona mtu alielala kwenye kitanda na jambo hilo lilimfurahisha kwani kazi yake aliona inakwenda kuwa nyepesi , aliingia ndani lakini ni kama alikuwa anasubiriwa kwani ile anaingia tu kwa utaalamu wa hali ya juu mno janeth alimrushia shuka carlos na kumziba uso huku akitanguliza na front kick iliompata vyema carlos , lakini hakuwa mzembe kwani aliyumba nyuma kidogo mpaka kwenye kabati huku shuka akiwa amelitupa pembeni .
Sifa moja kuu ya carlos ilikuwa ni kuchukia kupigana na mwanamke halafu amshinde na ndio maana alivyo ona mpinzani wake yupo vizuri alitupa bastora nje kabisa ya mlango na wakaaza kuzipiga , janeth alionekana kuwa vyema kujihami na mapigo ya carlos lakini pia carlos na yeye alikuwa makini mno, wa kwanza kupigwa pigo mshitukizo ni carlos , kwani ile anakwepa teke la mrembo janeth , alijikuta akipigwa teke lingine lililounganishwa na roundhouse (pigo la kung fu ) na kumpeleka carlos chini , lakini carlos aliinuka kama mwanariadha na hapo aliona asipokuwa makini lazima azidiwe , jenth alimsogelea carlos kwa kasi lakini bahati haikuwa yake kwani ni kama carlos alikuwa akimsubiri kwani alivutwa mbele na kutua kwenye kifua na bila kuchelewesha alipigwa kwenye shingo na hapo hapo akalegea na kudondoka chini huku nguo yake ya kulalia ikiusaliti mwili .
Carlos alimwangalia janeth kwa uchu , lakini hakutaka kufanya ujinga , alimbeba begani na kisha kutoka hadi nje , kwa kutumia rimoti aliokuwa amechukua kwa mlinzi alifungua geti na kutoka mpaka nje na kisha alilifunga na kurusha rimoti ndani na kisha akaenda kumpakia janeth kwenye gari yake akiwa hajitambui kabisa na kutokomea , akiwa amekamilisha kazi yake kwa asilimia mia moja .
******
Asubuhi siku nyingine kabisa mtu wa kwanza kufika nje ya nyumba ya janeth alikuwa ni abasi lakini kilicho mshangaza abasi ni mara baada ya kupiga honi mfululizo pasipo kupata majibu , hali hio kidogo ilimtia hofu kwani nyumba hio ilikuwa na walinzi alishuka kwenye gari yake na kulisogelea geti na kisha aligonga lakini bado hakupata mafanikio , akiwa amesimama nje anawaza alikuja mwanamama mmoja ambae abasi alimtambua , kwani alikuwa ni mfanyakazi aliekuwa akihusika na maswala ya upishi na usafi wa nyumba hio .
“ kuna nini ?”
“ hakuna anaeitika nimegonga mara kibao “.
“ kwahio tunafanyaje “
“ngoja nijaribu kupiga simu “ aliongea abasi na kuingia kwenye gari yake na kuchukua simu na kuanza kupiga , lakini simu iliita bila kupokelewa , alipiga simu kwa moja ya walinzi lakini pia simu iliita bila kupokelewa na hapo kengele ya hatari iligonga kwenye kichwa chake , alizunguka hadi nyuma ya ukuta na kisha aliuparamia na kwenda kutua chini ,na kusogelea upande wa getini na kitu cha kwanza kukutana nacho ni rimoti ya geti , alisogea zaidi na hapo ndipo moyo wake ulipiga kite na hio ni ,mara baada ya kumuona mlinzi akiwa amechanguliwa kichwa vibaya , alijikuta akisahau hata kufungua geti ili mwanamke aliepo nje aingie ndani kwani alikimbilia ndani huku akiita jina la janeth , lakini alikuta nyumba imetulia , alienda mpaka kwenye chumba cha janeth na kukuta patupu huku simu yake ikiwaipo kwenye ‘bedside’.
Hapo moja kwa moja akili yake ilimwambia kuwa tayari janeth alikuwa amekwisha kutekwa , alijikuta akikaa chini huku akitamani kulia , alichokumbuka muda huo ni kwenda upande wa kamera na kuangalia kilichorekodiwa , alitoka na kwenda moja kwa moja upande wa kushoto mita kadhaa na chumba cha janeth na kufungua mlango na kisha aliwasha laptop na kuanza kuangalia matukio ya siku hio na hapo ndipo aliposhuhudia mwanaume akiingia ndani ya nyumba hio kwanzia mlango mkubwa ambapo ndipo sehemu ambako kulikuwa na kamera mpaka kwenye cchumba cha janeth , mpaka alipomuona mtu huyo aliejiziba uso akitoka huku akiwa amembeba janeth , hakujua mtu huyo ni nani kwani mwanga ulikuwa hafifu mno kwani taa zilikuwa zimezimwa , lakini alichogundua kuwa mtu alietekeleza jambo hilo alikuwa ni mwanaume .
Alijikuta akitoa simu yake ya mkononi na kupiga , na dakika chache simu ilipokelewa .
“ sabi upo wapi ?”
“ nipo na mheshimiwa ndio tunaelekea uwanja wa ndege nasafiri kwenda marekani sasa hivi kuna nini? “
“ janeth “
“ kafanya nini “
“ katekwa “
“ nini? “
“ ndio yaani na sijui ni nani kafanya tukio hilo kwani ni mwanaume aliekuwa amejiziba uso “.
“sasa abasi nakusaidiaje , maana ndio nafika airport hapa na mheshimiwa “
“ wewe nenda tu nitajua cha kufanya , ila inabidi swala hili tulifanye kimya kimya madam asijue “
“ hakuna shida , hakikisha unanipa kinachoendelea , ukijua alipo wataarifu polisi pia “
“ poa “
*****
Saa moja kamili ndio muda ambao jeneth alizinduka , hakujua ni eneo gani alipo , ila alikuwa akikumbuka tukio la jana lote lililotokea , chumba alichokuwepo kulikuwa na kitanda na godoro ambalo halina shuka akiwa amefungwa mikono na miguu , huku mwanga hafifu ulioashiria kuwa muda huo ni asubuhi ulimurika ndani ya chumba hicho .
Janeth alijaribu kujinasua lakini aliona ugumu wa aina yake , na hapo hakuwa na jinsi kabisa , aliona siku hio kakamatika kweli .
Dakika chache mbele mlango ulifunguliwa na aliingia carlos cardosso awamu hii alikuwa hajajifunika kabisa uso wake .
“ wewe ni nani ?”
“ you fuk__ng bitch , stay quite before I lose my patient “ wewe kunguni tulia kimya kabla sijapoteza uvumilivu wangu
“ who are you “
“you don`t need to know who I am , what you need to know is that your day to go to hell are numbered “ huna haja ya kunijua mimi ni nani , unachopaswa kufahamu ni kwamba siku zako za kwenda kuzimu zinahesabika “ aliongea carlos huku akiwa amemsogelea kabisa usoni janeth akiwa amemkazia uso , lakini kwa janeth na yeye hakumchelewesha kwani alimtemea mate usoni na kumfanya carlos anyanyuke na kuyafuta huku akiwa kama hajakasirika , lakini fasta janeth alipokea kibao cha uhakika kilichomgeuza upande mwingine na hapo simu ya carlos ilitoa mlio kuashiria ilikuwa inaita aliangalia na kuona ni boss aliekuwa anapiga , alitoka mpaka nje ya chumba hicho na kuja kutokelezea kwenye moja ya sable kubwa kubwa yenye makochi ya mbao, huku kukiwa na baadhi ya wanaume wenye miili ya mazoezi wakiwa wanavuta sigara .
“ yess boss “
“ carlos make sure that bitch talks aboaut her boss, proceed with first class torture if she doesn’t cooperate “ carlos hakikisha huyo Malaya anaongea ni nani boss wake , akikataa kuongea mpe mateso daraja la kwanza .”
“okey boss “
Ilikuwa ni simu kutoka kwa kimbona aliekuwa akimpa maelekezo ya kipi carlos alichotakiwa kufanya , mara baada ya simu ile kukatika , carlos alimpa ishara moja ya wanaume wale waliokuwa wakivuta sigara na dakika kadhaa mwanaume yule alitoka na kuja na box kama la huduma ya kwanza na kisha aliongozana na carlos kwenda kuingia kwenye hiko chumba na kisha janeth alifunguliwa kwenye kile kitanda na kisha alifungwa kwenye kiti kwa ajili ya zoezi la mateso kuanza baada ya kumfunga jeneth huku kigauni chake kikiacha mapaja yake yalionona nje jambo ambalo wale wanaume waliangalia kwa matamanio.
“ boss can we talk out there “.boss tunaweza ongea kidogo hapo nje “ aliongea yule mwanaume mweusi kama mkaa akimpa ishara carlos , na carlos aliitika na wakatoka hadi nje kidogo “”
“what do you want to talk about Dario “ unataka kuongea nini Dario .
“how do you think if we *** her first , she is hot I cant stand it “unaonaje tukijilia vyetu kwanza kabla ya kumpa mateso mtoto mrembo mno siwezi vumilia “ aliongea Dario huku pepo la ngono likiwa linafanya kazi yake kwa kiwango cha 4G .
“ I think you have made a point but I will be the first to *** bcoz I did all the work myself and don’t tell the boys until we finish “nadhani umeongea point ila nitakuwa wakwanza kufanya maana nimehaingaika mimi mwenyewe na usiwaambie vijana mpaka tumalize “ aliongea na hapo darius alitoa jino lake lenye kutu kwa furaha .
“ you wait here until I finish the first round “ wewe suubiri hapa mpaka nimalize round ya kwanza “ aliongea carlos na darius alimuonesha alama ya dole gumba kukubaliana nae na carlos akazama .
Janeth alikuwa na wasiwasi mno , hisia zake zilimwambia tu kwa vyovyote lazima abakwe siku hio , kwani macho ya uchu alioyaona kutoka kwa watekaji wale alijua tu lazima huko nje walipokuwa wameenda kuongea ni kwenda kujadili mpango huo .
Na kama alivyotegemea ndivyo kilichokwenda kufanyika , kwani baada ya carloss kuingia alimtoa janeth kwenye kile kiti na kumrudisha kitandani na kumfunga mikono vizuri na mguu mmoja akaufunga mashariki na mwininge magharibi , na alivyoona zoezi lake limefanikiwa alilegeza mkanda wa suruali yake ya jeans ,ilishuka na kubaki na boksa tu , hakutakka kuvua yote maana alijua kuwa pia yupo kazini , janeth alishuhudia mdubwana wa carlos ulivyotuna ,hakuweza kupiga kelele kwani muda huo alikuwa ameshindiliwa matambala mdomoni , carlos alisogea na kupanda juu ya kitanda na kisha alikipandisha kigauni cha janeth .
Janeth hakuamini kama siku hio ndio anakwenda kuliwa tunda lake alilolitunza kwa miaka mingi pasipo kukutana na mwanaume yoyote yule , kwake aliamini baada ya kitendo hicho hatakuwa na thamani tena , kitendo cha kubakwa kwake ni Zaidi ya kuuliwa kuliko kufanyiwa kitendo hicho , kwa jinsi alivykuwa amefungwa hakujua kama anakupona siku hio , alichokifanya ni kufumba macho ili kusubiria unyama unaoenda kutendeka hhuku akimuomba mungu kutokee muujiza .
ITAENDELEA
SEHEMU YA 44
Carlos alitoa mhogo wake na kisha alitema mate na kuupaka vizuri kwa ajili ya kazi yake , lakini ile anavuta nguo ya ndani ya janeth , mara mlango uligongwa kwa nguvu , kitendo kilichomkasirisha na kutoka nje kwa hasira na alijua yote hayo ni wivu wa dario na alidhamiria kumfanyia mbaya , ile kutoka na mihasira yake lilikuwa ni kosa kubwa sana kwani alijikuta akilwamba risasi mbili kifuani na kwenda mkumku chini huku damu zikitapakaa mlangoni .
Mtu aliekuwa ameshika bunduki alikuwa ni damiani mwenyewe , tena huyu akiwa ni yule original asie na ngozi feki , sebleni hapo zilionekana damu zilizokuwa zimetapakaa kila kona , huku mwili wa dario ukionekana ukiwa chini huku dudu yake ikiwa nje kabisa na alionekana kabisa wakati mwenzake akiwa ndani basi na yeye alikuwa akipooza pooza dudu yake .
Damiani hakutaka kuchelewa , alikuwa amecahafukwa na roho ya kikatili mno , hakuonesha huruma hata kidogo , kwani damu zilizotapakaa eneo hilo zilionesha kuwa mtu alieingia eneo hilo alikuwa ni Zaidi ya hayawani .
Aliingia ndani ya chumba alichokuwemo janeth , na kumfanya jenth atoe machozi mara baada ya kumuona mwanaume damiani akiwa mbele yake , damiani alimfungulia na kumtoa matambara , , kitendo cha janeth kufunguliwa tu alijikuta akimkumbatia damiani kwa nguvu huku akilia kwa kwikwi , damiani alimbembeleza jeneth na kisha walitoka eneo hilo m mpaka upande wa barabarani na kuingia kwenye gari .
****
MASAA TISA NYUMA
Kwa janeth ilikuwa ni kama ndoto , kwani wakati huo alipkuwa usingizini alikuwa akiota kabisa kuna mtu kavamia nyumba yake , alijikuta akikurupuka , lakini wakati huo anakurupuka ndio wakati ambayo mlango wa nje ndio ulikuwa ukifunguliwa kwani alisikia ufunguo ukidondoka chini , alijikuta akipatwa na waswasi , na kukimbilia dirishani na kuangalia getini na hapo ndipo alipomshuhudia mlinzi akiwa chini alikimbilia simu yake na kutafuta namba ya abasi na kuipiga lakini haikupatikana kitendo kilichomfanya aachie tusi , hakujua ni mtu gani wa kumpigia muda huo na alijikuta akiwa amepiga namba ya damiani , lakini kabla hata hajaongea tayari kitasa cha mlango kilikuwa kishashikwa na hapo hapo alitupa simu pembeni huku simu ikipiga na kujifunikashuka gubigubi .
Huku upande wa damiani kama ilivyo kawaida yake ya kuchelewa kulala , saa sita kama na robo ndio aliingia kwenye chumba cha kulala , masaa machache mara baada ya kulala simu yake ilitoa mlio ikiashiria kuwa inaita , jambo ambalo lilimkurupusha na pia kumshangaza , hakujua ni nani anaweza kumpigia simu usiku huo maana haikuwa kawaida . .
Alijikuta akipokea simu mara baada ya kuona aliekuwa akipiga ni janeth , sauti ya kwanza kusikia , ilikuwa ni kishindo na hapo hapo akasikia sauti ya janeth “ wewe ni nani “ hapo hapo kwa akili yake ya haraka alikuwa ashajua kuwa kuna jambo la hatari lililokuwa linamtokea mrembo huyo , alijikuta akitoka kitandani mkumku huku simu bado ikiwa sikioni , sauti ya mwisho kuisikia , ilikuwa ni mguno wa wa mwanaume na hapo hapo hakusikia tena sauti .
Kilicho mchanganya kwa wakati huo hakujua ni wapi nyumbani kwa janeth kwani hakuwa na mazoea na mrembo huyo ya kujua ni mahali gani anaishi na laiti angekuwa anapajua basi angeendesha gari yake moja kwa moja mpaka eneo hilo .
Angekuwa na utaalamu wa wa komputa huenda na program kadhaa huenda kwake ingekuwa rahisi, lakini sasa uwezo huo hakuwa nao kabisa , alichokumbuka ni bastora yake aina S&W Model 12-9 aliokuwa ameihifadhi kwenye kabati , aliichomoa na kuvaa suruali yake ya jeansi na tisheti ya timberland na koti,na kutoka nje na kuingia kwenye gari yake aina ya BMW X8 , wazo alilokuwa nalo muda huo lilikuwa ni kwenda kurasini , lakini kuna wazo jipya lilimjia na wazo hilo ni kumpigia simu luangshu kwani aliamini muda huo china itakuwa ni muda wa asubuhi .
Dakika kadhaa tu simu ilipokelewa.
“ hello luang shu I am in very urgent emergency and I want to acces dreamer T by phone to find someone location “ habari luang shu nina dharula ya muhimu mno , nauliza kama ninaweza kupata mawasiliano na dreamer T kwa kutumia simu kujuaa mtu alipo “
“ yes its very simple dial the number I refer to in the usual way 0001” ndio ni rahisi sana piga namba ninazo kutajia kwa njia ya kawaida sifuri sifuri sisfuri moja “ aliongea na hapo hapo damiani alipiga namba zile na kuweka sikioni na hazikupita hata sekunde tayari simu ishapokelewa .
“welcome to DREAMER T global service , how may I help you ?” karibu kwenye DREAMER T huduma kwa ulimwengu , je unataka nini nikusaidie “
“ I need to locate someone, janeth bendera “ nataka kujua mtu alipo , anaeitwa janeth bandera .
“please wait our T to process your request “.tafahari subiri T akijaribu kufanyia kazi ombi lako “
“your request has been approved , a messege has been sent with a link that will direct you to the location where janeth bendera is “.ombi lako limefanikiwa meseji imetumwa kwako iliambatana na link ambayo itakuunganisha na mtu unaemtafuta .
“okey thank you “
Damiani alifungua ujumbe ule na kisha alifungua link ambayo moja kwa moja ilimpeleka mpaka kwenye google map iliokuwa ikionenyesha kialama chekundu kilichokuwa kikitembea , aliangalia eneo husika aliona janeth muda huo alikuwa anapita bunju na yeye wakati huo alikuwa yupo anatokelezea mbezi huku akifatilia mshale uliokuwa ukionesha uelekeo .
Masaa machache baadae ndio muda alifanikiwa kufika mpaka mwisho wa mshale ulipokuwa ukimpeleka , na alikuja kusimamisha gari barabarani eneo moja lililokuwa likifahamika kwa jina la kerege bagamoyo , alipita kanisa moja la roman na kusonga mbele huku akipata uelekeeo kupitia simu yake na mpaka anakuja kusimama kwenye nyumba moja kubwa iliokuwa na ukuta ndipo alipo pozi hapo , aliangalia hapo na kuona kuwa huo sio muda sahihi wa kuvamia eneo hilo kwani alijua kuwa lazima watu hao watakuwa wapo makini kwa muda huo , alichofanya ni kurudi barabara kuu na kuingia ndani ya gari na kwenda kusimamisha gari yake kwenye ofisi moja ya kata na kutulia hapo .
Saa moja kamili ndio muda ambao alikuwa akivamia eneo hilo na a aliingia kiulaini kupitia getini baada ya kumpiga pigo takatifu mtu aliekuwa akilinda geti baada ya kutoka kizembe na kisha alizama ndani na hapo ndipo alipochapa watu risasi bila huruma , alikuwa akipiga risasi huku akikumbuka tukio la mama yake kuuwawa kikatili na wala hakuogopa kabisa damu ambazo zilikuwa zikirukia kwa muda huo aliamini akileta uchungaji/ushekhe tu basi watu hao wangesmhambulia yeye ..
******
Moja ya watu ambao walikuwa na taarifa ya kutekwa kwa janeth alikuwa ni suzzane(miss k agent) , kwani tukio zima yeye mwenyewe alikuwa akilijua na hata mipango yote ya carlos alikuwa akiijua , alitaka kumtumia carlos kutekeleza jambo hilo ili iwe kwake rahisi kupata kujua kuwa janeth ni nani kupitia kwa carlos .
Hata taarifa za vyombo vya usalama vilivyoripoti tukio hilo kwake alitabasamu na kuona kuwa carlos alikuwa amefanya kazi kikamilifu kama alivyotegemea na ndio maana asubuhi hio aliongea na carlos wakutane eneo la bagamoyo kwa ajili ya kumfanyia mahojiano janeth .
Alikuja kupishana na gari alililopanda damiani akiwa na janeth karibu kabisa na shue ya sekondari baobab , na wala hakujua kuwa ndio aliikuwa anapishana na mtaalamu damiani ambae ametoka kufanya mauaji ya majambazi sugu au washirika wake .
Dakika tano pekeee alikuwa akikatiza kweye njia ya vumbi upande wa kushoto mkabala na kanisa la romani akielekea mafichoni alipokuwa ameelekezwa na carlos , baada ya kufika eneo hilo alisimamisha gari nje ya geti na kisha akaingia ndani pasipo kugonga na hapo ndipo aliponusa hali isio ya kawaida , maana komandoo huyu na jasusi alikuwa na machale balaa , alitoa bastora yake na kuiweka mkononi na kisha alifungua mlango wa sebleni na hapo ndipo alipopigwa na mshangao wa aina yake kwani damu zilikuwa zimetapakaa kila mahali , aliangalia kulia na kushaoto lakini hakuona alichokuwa akitafuta na alijikuta kwa umakini wa hali ya juu akitembea kuelekea mbele upande wa kulia na hapo ndipo alipokuja kukutana na maiti ya dario , na baada ya kuangalia upande wa kulia mlangoni ndipo alipomuona carlos , alimkimbilia na kisha alimwinamia huku akivaa gloves zake na kisha alimshitua na hapo kwa hali ya taabu sana carlos alifumbua macho .
“ carlos what happened here?? “
“daa.. daa.. miani “ aliongea carlos na hapo hapo akakata moto na kuwa wa baridi “ .
Suzzane hakutaka tena kubaki eneo hilo alitoka huku akiwataarifu polisi juu ya tukio hilo huku akiendesha gari lake kurudi alikotoka .
‘damiani .. inamaana damiani amerudi , kwa hali ile nilioikuta damiani atakuwa ni hatari na mkatili mno , anafanana na carlos tu “ aliongea suzzane huku aking`ata meno yake kwa hasira wakati huo akipishana na diffenda ya polisi iliokuwa ikielekea eneo la tukio ikitokea kituo cha polisi mapinga .
Tukio la kutekwa kwa janeth na kuwawa kwa walinzi wake lilisambaa kwa kasi sana kwenye vyombo vya habari na hio ni baada ya tukio hilo kuthibitishwa na mkuu wa polisi kanda maalumu ya dar es salaam , tukio hilo halikuishia kwa wananchi tu pia lilimfikia mke wa raisi wema au mama Patrick .
Jambo hilo lilimpelekea mshituko mno mama huyo kiasi cha kuanza kupumua kwa shida na mtu aliemuona kwa mabadiliko hayo alikuwa ni mfanyakazi wao wa ndani aitwae zainabu , alimtuliza kwa kumpa maji na hapo kidogo hali yake ilikaa sawa alichukua simu yake na kupiga kwa abasi .
“abasi unafanya kazi gani , nimekupa kazi ya kumlinda mwanangu , mpaka anatekwa wewe ulikuwa wapi ??“ .
“ nisamehe madam , jana nilipata dharula sikuwepo”.
“hayo sio mambo ya kuniambia mimi , namtaka mwanangu akiwa hajadhurika lasivyo utanitambua mimi ni nani “ aliongea mke wa rasi kwa jazba kweli huku akikata simu na kukaa kwenye sofa akihema kwa nguvu .
Polisi walikuwa wakifatilia kwa ukaribu sana tukio hilo akiwepo DCP (deputy commissioner) bwana barangwa mahimbo bwana huyu alikuwa na usongo kweli na kuhakikisha kuwa anawapata wahalifu akiongozwa na mwanadada aliepokea cheo cha usajini wa polisi (seargent )hawa takamoyo , wengi polisi wanamuita sajini au sajent taka vya moyo jina lake la utani .
Hawa baada ya kufika eneo la tukio kwa kuongozwa na abasi waliweza kufatilia kamera za ulinzi ndani ya eneo hilo , na hawakuambilia sura ya mtu huyo japo waliweza kipata muonekano wa mtu huyo , kamishina msaidizi alitoa maagizo wa sajent takamoyo kuhakisha ufatiliaji unafanyika kwa umakini wa hali ya juu mno .
“sajent hakikisha watu hawa tunawakamata mara moja , fanyeni upekuzi wa kila mahali kumbaini mhusika wa hili , kazi hii nataka isifike saa sita mchana iwe ishakamilika na proffesa janeth awe amepatikana na wahusika wafikishwe mbele za sheria “
“ sawa afande “ alipiga saluti na kazi ya msako ikaendelea , vijana waligawanyika kila kona ya jiji kuhakikisha kuwa wahusika wanapatikana , lakini sajenti nusu saa baada ya kuagana na kamishna msaidizi wa polisi bwana barangwa , alipokea simu kutoka kwa kamishna mwenyewe kumtaarifu kuhusu mauaji yaliofanyika bagamoyo .
Mara baada ya sajenti kupokea taarifa hio aliingia kwenye difenda na kuelekea eneo la tukio , dakika arobaini ziliwatosha kabisa kufika ndani ya eneo hilo na kuanza kupiga picha na kuchukua baadhi ya vielelezo ambavyo vingewasaidia katika upelelezi wao .
“carlos cardosso “ ni jina lililotamkwa na sajenti takamoyo mara baada ya kumgundua ,alikuwa akimfahamu vyema mtu huyo kwani anakumbuka tukio la kushambuliwa eneo la mikese na mtu huyo kutoroshwa wakati akisafirishwa kwenda gereza la morogoro , na kuanzia siku hio sajent takamoyo japo ya kuambiwa kesi hio isifatiliwe lakini kwake jambo hilo halikuwa swala la kulifumbia macho kwani kimya kimya alilikuwa akifanya upelelezi wa kujua kwanini siku ile walisahambuliwa kwa sindano za usingizi na mfungwa huyo kutoroshwa na pia isitoshe maagizo kutoka kwa wakubwa yakimtaka swala hilo liwe siri na lisifatiliwe , sintofahamu ya jambo hilo ndio iliomsukuma kutaka kujua Zaidi , maana kati ya moja ya polisi waliokuwa wazalendo na taifa basi ni mwanadada huyu sajenti takamoyo , ukimuona njiani akiwa na mavazi ya kawaida hutoamini kuwa alikuwa ni sajent wa polisi , maana alikuwa ameumbika haswa na sura yake ya kirangi , sura nyeupe , na umbo lake namba nane vilimfanya we mzuri kweli , lakini licha ya uzuri huo alipenda kazi ya polisi mno , alikuwa akipenda kukamata sana waharifu na kutokana na tabia yake alikuwa amefanikiwa kutokomeza sana uhalifu ndani yajiji la dar mpaka kupelekea kazi yake kuonekana kwa wakubwa na kupandishwa cheo na kuwa sajent .
Carlos cardosso ni jina lililomjia mara baada ya kuona sura hio ya mwanaume wa kibrazili akiwa amefumba macho akiwa mfu , kitendo cha kumkuta mwanaume huyo kuwa mfu aliamini kabisa mtu aliengia ndani ya eneo hilo na kutekeleza mauji ya carlos alikuwa ni mtu hatari sana .
Alichokifanya ni kuanza kuangalia mazingira ya hapo ndani na hapo ndipo alipokuta Kamba kwenye kitanda na kwenye kiti na pia vifaa vya kutesea watu alijaribu kuvuta picha ya eneo hilo na hapo alijua kabisa kuna mtu alikuwa amefungwa kwenye kitanda , alizidi kuvuta picha na hapo aligundua kuwa kuna mtu mwingine alieingia na kumuokoa mtu aliefungwa kwenye kitanda , hapo hapo alikumbuka video ya kamera alizochukua kwenye nyumba ya janeth za mwanaume alieingia ndani akiwa amejiziba uso , na hapo ndipo alipo jaribu kufananisha mwili wa carloss na jibu moa kwa moja likaja uwa mtekaji alikuwa ni carlos, na pia alijua kabisa kuwa janeth alikuwa ameokolewa na mtu aliefanya mashambulizi na kuuwa majambazi hayo .
Alipiga simu moja kwa moja kwa kamishina na kumpa maelezo ya tukio zima na pia uwezekano wajaneth kuwepo kwenye eneo hilo .
“ kama hayo usemeyo ni kweli , sasa hivi hakikisheni mnajua ni wapi janeth alipo maana yeye ndie atatoa maelezo kamili ya tukio zima “
“ sawa afande “
ITAENDELEA .
SEHEMU YA 45
“ulijuaje niko pale “ lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa janeth kwenda kwa damiani aliekuwa akitengeneza kifungua kinywa wakati huo janeth alikuwa amevaa tracksuti aliopewa na damiani alikuwa amesimama akimwangalia damiani aliekuwa bize .
“si ulinipigia simu jana wewe “
“kumbe ulisikia?? “
“ ndio , nilisikia purukusahani ndio nikajua kuwa upo kwenye hatari “
Aliongea damiani pasipo kugeuka nyuma , huku upande wa janeth alikuwa akimwangalia damiani hammalizi alikuwa akitabasamu , na kushukuru kwa wakati mmoja ,, kwani akikumbuka tukio lile la kutaka kubakwa , lilikuwa likimsisimua sana na kufanya nywele zake zisimame kwa woga na mwili kuwa wabaridi .
“asante sana damiani , ungechelewa kidogo tu nadhani sasa nisingekuwa janeth tena “.
“njoo chukua haya mayai tukanywe chai , kwanza sahau yaliopita yatakuumiza kichwa sawa “ aliongea damiani huku wakielekea dining na kutenga chai na kuanza kunywa , janeth tabasamu lililokuwa usoni mwake usingeamini kuwa ni mtu aliekuwa ametoka kuekolewa muda mfupi uliopita , alikuwa akinywa chai huku akimwangaia damiani na kutabasamu .
Baada ya kumaliza kunywa chai ndipo janeth alipomkumbuka mama yake na pia abasi kwani aliamini sasa hivi watu hao wangekuwa kwenye tafrani isio kifani ya kutaka kujua usalama wake , alimuomba damiani simu yake na kwakua namba alizokukuwa akikukumbuka ni za mama yake basi ndio mtu alieona ampigie .
Madam wema ama first lady alikuwa kwenye wasiwasi mmno , kila saa alikuwa akimpigia simu abasi kujua kinacho endelea , lakini taarifa zilikuwa zikimvunja moyo mno hakujua mwanae kama yupo salama , hata chai hakuweza kunywa kabisa siku hio inapitaje kwa mfano sasa mtoto unaempenda katekwa .
Muda wa saa nne kamili ndio namba mpya ilipopiga na kwa haraka haraka aliipokea na kuweka sikioni .
“ mom “ ilikuwa sauti ilisikika kwenye masikio ya mwanamama huyo .
“janeth uko wapi mwanangu , uko salama , uko wapi nitakufa mimi mama yako “
“niko sawa mama nilitekwa ila nimeokolewa mom niko salama usiwe na wasiwasi “
“ uko wapi kwasasa nataka kukuona “
“mama tunataonana niko sehemu salama , mwambie na abasi atakuwa na waswasi “ aliongea upande wa pili na kumfanya mama huyo kuhema kwa nguvu na kukaa chini ya sofa na kumshukuru mungu na simu ilikatwa .
“asante mungu , bendera mtoto wetu kapona “ aliongea mama huyo huku akionekana kuwaza mbali mno na kukumbuka maisha yake ya nyuma .
*****
HISTORIA YA MKE WA RAIS
Ni kipindi cha miaka yangu ya nyuma , kipindi hicho nikiwa binti mdogo kabisa wa miaka kumi na sita , nikiwa katika umri wa kuvunja ungo , kipindi hichi nilikuwa nikisoma shule ya sekondari songea girls,nilikuwa moja ya wasichana wapole sana wenye nidhamu ya hali ya juu ndani yashule yetu , japo sikujaliwa akili sana kama wanafunzi wengine lakini kwa uwezo mdogo niliokuwa nao nilikuwa nikijitahidi sana kusoma ili kufaulu katika masomo yangu hususani kipindi hicho nikiwa nipo kidato cha nne , kipindi hicho kufaulu kwenda kidato cha sita ilikuwa kazi ngumu mno kwa miaka yetu , kwani ilikuwa ikihitajika kazi kubwa ya kujisomea hasa kwa baadhi ya watu kama sisi ambao hatukua na iq kubwa kama wengine .
Licha ya kuwa mpole , nadhifu na nidhamu lakini pia nilikuwa moja ya wasichana ambao niseme kuwa tulikuwa tumejaaliwa uzuri , sio kama najisifu lakini huo ulikuwa ni ukweli , na mimi mwenyewe nilikuwa nikikiri hilo , lakini uzuri kwangu kuna muda mwingine niliona kama mateso , kwani ni mara nyingi nilikuwa anikitongozwa mpaka na baadhi ya walimu ndani ya shule yetu , jambo hilo lilikuwa ni changamoto kubwa sana kwangu kwani baadhi ya walimu ambao niliwakatalia walikuwa wakinitishia kunifelisha katika masomo yangu , moja ya walimu hao alikuwa ni mwalimu mmoja aliekuwa akifahamika kwa jina la mwalimu rama au mwalimu pengo kama alivyokuwa akifahamika kwa jina lake la utani kwani alikuwa na pengo , mwalimu huyu alikuwa akinitaka kwa muda mrefu sana lakini nilikuwa nikimkataa , sikua nikimpenda hata kidogo lakini pia sikutaka kujiharibia mimi mwenyewe kwa tamaa za mwalimu huyo , kwani nilijua madhara yake , lakini mwanzo wa kumkatalia mwalimu huyo ndio ukawa mwiba kwangu kwani alikuwa akiniferisha makusudi kabisa katika masomo yake aliokuwa akifundisha , hali hio ilinitia mawazo sana mpaka baadhi ya marafiki zangu wakaniambia nimkubalie lakini kwangu nilikataa katakata , nilitamani kwenda kusema ngazi za juu , lakini mtu aliekuwa huko ngazi za juu na yeye alikuwa akinitaka kimapenzi ,jambo ambalo niliona hakuna msaada wowote ambao ningepata , niliishi hivyo hivyo kwa kusoma kwa bidii huku nikiamini kuwa mtihani wa mwisho kwakuwa mwalimu huyo sio yeye anayehusika na kusahihisha basi niliamini hata afanyeje nisingeweza feli .
Mwezi wa tisa ndio mwezi ambao watu wengi walikuwa kwenye harakati za kujiandaa na mtihani wa moko , siku hio nikiwa ninajisomea na marafiki zangu alikuja headgirl wetu aliekuwa akifahamika kwa jina la mary singano , alikuja mpaka tulipokua tunasomea na kuniomba nikaongee nae pembeni , sikujua alikuwa na jambo gani la kuongea na mimi kwani kipindi hicho sikuwa na mazoea naye kabisa .
“wema nimekuita hapa kuna jambo nimelisikia kutoka kwa moja ya marafiki zako”
“ rafiki yangu nani na ni jambo gani? “
“hilo sio la msingi lakini naomba unisikilize “
“ndio nakusikiliza “
“ni kweli mwalimu rama anakufelisha masomo yako makusudi kwasababu ulimkatalia “ nilijikuta nikimwangalia headgirl kwa mshangao lakini wakati nikimwangalia nilijikuta machozi yakiwa yamenijaa mashavuni na hatimae kilio kabisa .
“ mbona unalia sasa wema , nimekuuliza naomba uniambie nataka kukusaidia “
“ ni kweli mary“ niliongea huku nikiwa na uchungu moyoni kwani ni kipindi kirefu nilikuwa nikivumilia jambo hilo na ni kama leo nimepata sehemu ya kulisemea , nilimwambia kila kitu headgirl juu ya jambo hilo .
“kuna mtu anataka kuonana na wewe “
“ nani ?“
“ utamjua ila ni kiongozi pia kutoka shule ya songea boys ni kaka mkuu kule “ aliongea mary na kunifanya nikae nifikirie .
“ kwanini anataka kuonana na mimi ??“.
“nimemwambia kuhusu swala lako mimi kama kiongozi na kwakuwa yeye kapewa jukumu hilo na mkuu wa wilaya ndio anataka akusaidia kufikisha malalamishi yako “
“ sawa nipo tayari kuonana nae “ niliongea huku nikijikuta nikipata tumaini .
Siku moja mbele nilikutana na kiongozi huyo , kwakweli siku hio baada ya kuonana nae nilijikuta mapigo yangu ya moyo yakibadilika , nilikuwa nimevutiwa mno na kaka huyo , kwa muoenekano wake alikuwa ni moja ya watu waliokuwa wakionekana kujiamini mno .
“naitwa john bendera ni headboy kutoka shule ya sekondari songea boys , nimefika hapa kwa ajili ya kuongea na uongozi wa shule yenu na hii ni mara baada ya mkuu wa wilaya kusikia tetesi juu ya wanafunzi kutumikishwa kingono katika mashule mengi yaliopo songea , hivyo nikawa moja ya watu ambao nimeteuliwa kufanyia uchunguzi swala hilo ndani ya shule hii , nishaelezwa kwa kifupi na headgirl hivyo nataka pia unipe maelezo yako wewe mwneyewe “ basi japo alikuwa akiongea ila kwangu mawazo yalikuwa kwingine kabisa , sijui ni kwa jinsi nilivyokuwa nikitongozwa na wanuume au laah kwani nilitamani bendera aniambie kuwa ananipenda ila sio kumwambia maswaibu yangu , alivyoniona nipo mbali kimaawazo ndipo aliponirudisha kwenye mstari na hapo ndipo nilipomueleza mkasa wangu wote na kuahidi kuwa atalifanyia kazi .
Siku nne mbele yaani ijumaa ndio siku ambayo mkuu wa wilaya alifika ndani ya shule yetu , alikuwa ni mwanamama mmoja mnene alievaa wigi , alifika ofisini kwa mkuu wa shule na mimi nikaitwa , lakini huwezi amini nilikutana na wadada watano wakiwa na malalamiko sawa na yangu wakimtuhumu mwalimu rama kuwatongoza nilijikuta nikizidi kumchukia mwalimu rama , japo alikuwa akinitongoza lakini nilitamnani yale aliokuwa akiniambia kuwa ananipenda kuwa yana ukweli wake lakini kumbe nia yake ilikuwa ni tamaa tu .
Basi mwalimu rama mbele ya mkuu wa wilaya na afisa elimu aliambiwa ajitetee . lakini maji yalikuwa yamemfika shingoni kwani mwisho wa siku alionekana kabisa hatukuwa tukimsingizia maana mashahidi walikuwa wengi , hivyo alifukuzwa shule rasmi .
Kitendo kile kwakweli shujaa wangu alikuwa ni bendera kwani niliamini pasipo yeye nisingetoka katika kifungo kile cha kufelishwa mitihani makusudi kabisa , kwanzia siku hio hisia zangu za kimapenzi juu ya bendera zikachipuka , zikamea na hatimae kukomaa ndani ya moyo wangu , ilikuwa kila jumapili nikipata nafasi lazima nikamuone bendera, mwanzoni ilikuwa ni kama nikienda kumshukuru lakini mwisho wa siku nilishindwa kujizuia mbele yake na jambo hilo aliligundua vyema , lakini jambo la ajabu ni kwamba kwanzia siku hizo bendera alianza kuniepuka jambo hilo liliniumiza na kunifanya nishindwe hata kuwa makini na masomo yangu kwani ni muda mwingi nilikuwa nikimfikiria bendera tu .
Mpaka tunakuja kufanya mahafali ya mwisho ya kidato cha nne mwezi wa tisa mwishoni ndipo nilipo pata nafasi ya kuonana na bendera kwa mara nyingine na kilichonifurahisha siku hio ni kuhudhuria kwake na kuniletea zawadi pamoja na ua jekundu nilifurahi sana siku hio , japo wazazi wangu walikuwepo lakini sikuwa na habari nao mimi nilikuwa na habari na bendeera tu , kwani kila picha nilitaka nipigwe na bendera , kiasi kilichowashangaza mpaka ndugu zangu akiwemo dada yangu .
Baada ya mahafali kuisha ndipo nilipo onana na bendera nilianza kumlaumu kwa kitendo chake cha kuniepuka , lakini huwezi amini nilikuwa nishamsamehe muda mrefu tu , yaani kitendo cha kuja kwenye mahafali yangu ndio kilichonifanya nimsahemehe kwani kipindi alichokuwa ananikwepa nilikuwa nishamshemea mpaka maneno mabaya ya kumchukia .
Basi kwanzia siku hio penzi langu na bendera likazaliwa rasmi , na kuuanza haatua za awali za ukuaji na ukomavu , siku ya mahafali ya bendera ndio siku yenyewe ambayo bendera alinitoa usichana wangu na kuniingiza kwenye raha ya mapenzi , nakumbuka ni kwenye moja ya guest house iliokuwa ikipatikana eneo la bomba mbili usiku ndipo nilipovuliwa nguo ya ndani na bendera na kunitoa usichana wangu .
Kwanzia siku hio ndio nikawa nimekufa nimeoza kwa bendera , yaani nilikuwa siambiwi wala sisikiii muda wote kichwa changu ni bendera tu.
Basi mwisho wa kumaliza mitihani yetu ndio siku ambayo nililala mpaka kukakucha na bendera , ilikuwa ni moja ya siku moja ya furaha sana katika maisha yangu , maana raha nilioisikia siku hio na Amani moyoni mwangu naweza sema kwamba haitoweza jirudia maana nilikuwa wamoto kweli , siku hio ilikuwa ni kupika na kupakua .
“ bendera ndoto yako ni kuja kuwa nani baadae “
“mimi “
“ ndio wewe mpenzi kwani kuna mwingine humu ndani “
“ mimi nataka kuja kuwa raisi “.
“hahaha … ndoto kubwa hio mpenzi sidhani kama itakuja kutimia “
“ lazima itimie mimi nakuhakikishia hilo kabla sijafa lazima niitimize na wewe umekuwa mtu wa kwanza kujua ndoto yangu lakini pia utakuwa wakwanza kushuhudia kile nisemecho “.
“ ukiwa raisi na mimi nitakuwa mke wa raisi si ndio “
“ ndio kwanzia sasa hivi wewe ni first lady mtarajiwa“
“ hahaha .. jamani “nilijikuta nikifurahi mno kwa maneno ya bendera .
“ nakupenda sana bendera usije ukaniacha “
“ siwezi kukuacha mpenzi nakupenda pia “
Basi niseme kwamba siku ambayo kilamtu anapanda gari la kwenda kwao kwangu ilikjuwa huzuni mno ni kama niliona sitokuja tena kuonana na bendera , japo tulijiwekea ahadi kibao lakini bado niliona haitoshi , tuliahidiana kupendana daima lakini niliona bado nilimtaka bendera mimi .
ITAENDELEA
SEHEMU YA 46
Basi siku hatimae mwezi ukapita bila kuonana wala kuwasiliana na bendera kipindi hicho nikiwa nyumbani kwetu singida , lakini huwezi amini nilianza kupata mabadiliko ya mwili kuchoka kwa mara kwa mara na kula vitu vichachu na hata muda mwingine asubuhi kutapika ninaposkia harufu ya mayai , mtu wa kwanza kuona jambo hilo alikuwa ni mama yangu , alijua kabisa kuwa nina mimba na hata mimi kwa hali hio nilijua kabisa nina mimba .
Baada ya mama kujua hali yangu alinichukua mkuku mkuku mpaka hospitalini huku akiwa amechukia mno , nilipimwa na nikagundulika nina mimba , kwangu swala hilo lilikuwa la furaha sana japo nilikuwa nalia lakini nilikuwa na furaha moyoni nilikuwa nikilia kinafiki tu sikuamini kama nilikuwa na kiumbe cha bendera tumboni kwangu , nilijiliza mbele ya mama baada ya kunigombeza sana huku akitaka nimtaje muhusika , lakini mimi sikutaka kabisa kumtaja bendera nilijua lazima bendera angefungwa maana nilikuwa nikimjua vyema mama yangu kwa misimamo yake .
Mwisho wa siku nilimdanganya kuwa nimebakwa nikajiliza liza kwake mwisho wa siku akahudhunika lakini baada ya siku akazoea , lakini kimbembe kilikuja kwa baba sasa baada ya kurudi kutoka migodini kahama huko buzwagi akiwa na mali , baada ya kunigungua mjamzito alimshutumu sana mama kwamba alikuwa ananilea kwa kunidekeza na mwishowe ndio kasababisha mimi kupata ujauzito na kwanzia siku hio akampa mama yangu talaka rasmi , huku yeye akienda kuishi na mwanamke mwingine huko mwanza .
Sikuwa na mawasiliano kabisa na bendera tokea aende kwao geita na kipindi hicho njia kubwa ya mawasiliano ilikuwa ni barua , akukuwa na simu za mkononi .
Basi maisha yangu na mama yalikuwa magumu kwani mama hakuwa na ajira ya kuaminika , alikuwa akifanya viabarua vya hapa na pale ili kuhakikisha mimi mwanae sikosi kula na kuvaa , uzuri ni kwamba nilikuwa mimi tu kwani dada alikuwa amekwisha kuolewa Iringa huko .
Maisha yalienda mpaka nilipojifungua mtoto wa kike , nakumbuka kipindi nilichojifungua matokeo yalikuwa yashatoka , na kwa taarifa tu ni kwamba nilifaulu kwa daraja la nne ambalo halikuwa likiniwezesha kwenda kidato cha tano , kwa bendera nae niliambiwa na rafiki yake kuwa alipata daraja la tatu alama ambazo zilikuwa zikimuwezesha kwenda chuo , nilishangaa kwani moja ya watu waliokuwa ni majiniasi basi alikuwa bendera kwani hata kwenye moko alikuwa amepata daraja la kwanza akiwa amewaongoza wenzake wote na wilaya , lakini matokeo ya mwisho ndio hivyo alikuwa na daraja la tatu , nilijiuliza ilikuwaje na hapo ndipo nilipokuja kuujua ukweli lakini baadae kabisa kuwa bendera alikuwa akiniwaza sana hahaha… kumbe wakati mimi nateseka juu yake na yeye alikuwa akiteseka juu yangu , na hayo yote nilikuja kuyafahamu kutoka kwa rafiki yake ambae nilikutana nae kipiindi nikiwa nipo jijini dar nikisomea masomo ya hotel management , lakini pia nilikuja kusikia kuwa bendera anayachukia mapenzi balaa na pia ananichukia hataki hata kunisikia , jambo hilo lilinikosesha raha na nilijua yote hayo ni juu ya kufeli kwake na ndoto yake ya kuwa raisi , na mimi baada ya kusikia hivyo sikutaka hata kumwambia kuwa nina mtoto wake .
Basi mtoto wangu nilimpa jina la janeth , japo mama aligoma kwani alitaka nimpe jina la kiislamu , lakini mimi nilikadhania hilo , mpaka nikapelekea mama kunihoji upya juu ya baba wa mtoto na hapo ndipo nilipomuambia ukweli kuwa mtoto alikuwa ni wa bendera na bendera ni mkristo hivyo siwezi kumpa jina la kiislamu na mama yangu alikubali .
Basi janeth akiwa na miaka minne mbeleni nilimuacha kwa bibi yake na mimi nikaenda kusomea masomo yangu ya hoteli management ndani ya jiji la dar , masomo ambayo yalinichukua miaka miwili na nikafanikiwa kupata cheti changu na kurudi singida , nilifurahi kumuona janeth kakuwa huyo kwani kipindi hicho alikuwa darasa la pili , lakini pia kilichonifurahisha ni kwamba hakuchukua akili ya mama yake bali alichukua ya baba yake japo sura kachukua yangu na rangi ka ujumla wake , shuleni alikuwa ni jiniasi sana alikuwa ndio namba moja , nilikuwa nikimpenda sana mwanangu .
Basi baada ya kukaa nyumbani miezi miwili na mtoto wangu ndipo nilipokuja kupata nafasi ya kazi Serengeti kwenye hoteli moja ya kitalii ndani ya mbuga za wanyama , kwanzia siku hio nilikuwa nimeamua kufanya kazi kwa bidi kwa ajili ya matunzo ya janeth, sikuwahi kujua bendera yuko wapi na sikujihangaisha kumtafuta , japo moyoni mwangu alikuwa amejaa tele , yaani nilikuwa nikitamani kumuona lakini sikuwa nikitaka kumtafuta .
Miezi sita ya kazi ndipo nilipokuja kukutana na mzungu mmoja aliekuwa akija hotelini hapo kama mtalii mwanzoni tulianza mazoea ya kawaida , kiasi hata cha wafanya kazi wenzangu kuanza kunishawishi nimchune huyo mzungu pesa , lakini kwangu sikutaka kujihusisha na mapenzi kabisa , moyoni mwangu alikuwepo bendera tu , lakini kila siku ambayo mzungu yule akija pale hotelini alikua akiniachia kiasi kukubwa cha pesa kiasi kwamba hata ushuari wa marafiki zangu ulianza kuniingia akilini .
“ yaani wewe wema mtu sio mtu wako anakupa mihela yote hii ukimpa je si atakutoa kwenye umasikini “ yalikuwa ni maneno ya rafiki yangu julita siku hio nikiwa nimetoka kumhudumia mzungu huyo niliekuwa nikimjua kwa jina la bruno , kwa mbaali nilianza kuona ushauri wa julitha una maana na kwanzia siku hio nilijiapiza kwamba siku nyingine akija lazima nimpe tunda , nilikuwa nimesahau kabisa ahadi zangu kwa bendera na pia kila nikikumbuka kuwa bendera alikuwa hanitaki kuniona kwa kisingizo cha kwamba nimemfelisha basi nilipata msukumo Zaidi wa kugawa tunda kwa bruno .
Baada ya miezi kadhaa bruno alifika tena , na siku hio ndio nilipopata nafasi ya kuongea nae bruno , alikuwa akionekana mtu wa mawazo sana kuna siku nilimkuta akiwa amekaa kwenye bustani akilia kwa kilio cha kwikwi kabisa , jambo ambalo liliniumza sana ukizingatia na kwa namna alivyokuwa akinijali kwa kunipa pesa zake ,.
Siku hio ndio niliodhamiria kumpa penzi kwani niliamiani kwamba alikuwa akihitaji faraja , sikujali tena bendera sijui flag kwenye moyo wangu nilichokuwa nikijali kwa muda huo ilikuwa ni furaha ya bruno , siku hio alilewa sana kiasi kwamba hakuwezaa hata kwenda chumbani kwake na ikabidi nimkokote mpaka ndani kwake , lakini kitendo cha mimi kuingia nae tu ndio alianza kuninyonya midomo na kunipapasa kitu kilichofanya kikunde changu kusimama na kuhisi wadudu wakinitambalia mwilini huku shoti kuanzia kwenye maziwa mpaka kwenye kitumbua zikinisumbua , madakika kadhaa nilikuwa mweupe kama nilivyozaliwa na nilikuwa nikiusikilizia mwiko wa mzungu bruno , nilijkikuta nikifurahia mchezo ule na hio ilitokana na kwamba nilikuwa sijafanya muda mrefu na naweza sema ilikuwa ni mara yangu yatatu kufanya mapenzi katika maisha yangu .
Basi kuanzia siku hio ndio ikawa ni bruno kuwa mwiko na mimi kuwa chungu ilikuwa ni mwendo wa kukaanga mboga tu , kitendo hicho niliona kikirudisha furaha kwa bruno kiasi kwamba kama marafiki zangu walivyokuwa wkainiambia ni kweli nilianza kupewa pesa za kumwaga kiasi kilichonifanya kuanza kupendeza lakini pia matunzo ya janeth yakiongezeka , kutokana na ufaulu mzuri wa janeth niliamua kumhamisha shule kipindi hicho akiwa darasa la nne na nilimpelaka kenya shule moja iliokuwa ikifahamika kwa jina la hillcrest international shule nilioifahamu kutoka kwa rafiki yangu mkenya aliekuwa akifanya kazi hapo singita .
Baada ya miezi ya kupakua na kupika ndipo nilipojikuta nina ujauzito jambo ambalo kwangu sikulitarajia kabisa , kwani katika maisha yangu sikutaka kabisa kuwa na mtoto tofauti na wa bendera , lakini I nigesemaje sasa kwani pesa zilininogea nikajisahau sikua na jinsi tena , nilimsubiri bruno aje tena nimwambie juu ya ujauzito huo
Na kweli baada ya miezi alikuja na nikamueleza , japo nilikuwa nina tabasamu usoni lakini sikuwa nikimpenda kabisa bruno , yaani nilitamani hata kiumbe kilichoko tumboni nikitoe , lakini l niliogpa hio dhambi kabisa , basi baada ya kumwambia vile alionyesha kufurahi tu jambo ambalo lilinipa matumaini na alinishauri niache kazi nirudi nyumbani na atakuwa ananitumia pesa za matumizi , kwakua nilikuwa nikimuamini basi niliamua kuacha kazi na kurudi nikiwa na kiasi cha kutosha cha pesa , mama alishangaa mno baada ya kumwambia ni mjamzito , lakni nilimuelewesha kuwa mwanaume alienipa ujauzito ndie alienifanya hata kumpeleka janeth hillcrest , zilikuwa ni pesa za huyo mwanaume na nilimwaminisha kuwa alikuwa akinipenda , na kadri siku zilivyokuwa zikienda ndio mama aliamini maneno yangu kwani bruno hakukoma kunitumia pesa na kipindi hicho aliniambia kuwa alikuwa amehamia nchini rasmi na kuanzisha biashara zake .
Baada ya miezi tisa nilijifungua salama mtoto mwenye asili mbili yaani mzungu na mwafrika , alikuwa ni mtoto mzuri mno wa kike baada ya kujifungua bruno alikuja kisiri sana muda wa usiku na kuomba kuonana na mtoto na baada ya kumuona alimwangalia na kisha alitabasamu na kumbusu kwenye shavu kulia na kushoto then kwenye paji la uso kisha akanipa mtoto na katoa kidani flani hivi cha almasi na kumvalisha na hapo ndipo bruno alipo niambia maneno ambayo yalinifanya mpaka leo hii kumchukia milele lakini haikunifanya kumchukia yeye tu pia nilijikuta nikimchukia mwanangu wa kumzaa .
“ madam madam “.
Ilikuwa sauti ya zainabu ndio iliomtoa wema kwenye mawazo ya kumbukumbu yake ya nyuma
“ naam “
“ amka ule hata kidogo mama yangu “
“ sawa “,
*****
Baada ya janeth kuwasiliana na mama yake kimbembe kilibaki kwa janeth na damiani kwani damiani hakutaka kujulikana kama ndie aliemuokoa janeth , walikaa wakajadiliana ni kwa namna gani wanaweza wakalitatua hilo swala ndipo janeth alipomwambia neno moja damiani ambae mwenyewe hakujua ni kwa jinsi gani mwanadada huyo anakwenda kulifanya .
“ damiani I want you to trust me , as I said you won`t be involved “ damiani nataka uniamini katika hili niamini kabisa hutohusika .
“okey sawa janeth nakuamini , lakini nataka uniruhusu nikupeleke mwenyewe mpaka kituo cha polisi “ aliongea damiani na kumfanya janeth atabasamu na furaha kumjaa tele mbele ya mwanaume huyo .
“ okey damiani “.
Basi baada ya wawili hao kukubaliana , moja kwa moja walienda mpaka kituo cha polisi cha osterbay kuripoti na hapo ndipo walipokutana na waandishi kibao waliokuwa wakihitaji kujua mwenendo huo wa utekaji , kitendo cha janeth kutokezea tu alianza kuzongwa na waandishi wa habari , lakini damiani aliwazuia na mwishoe alitoa maelezo ya kueleweka ndani ya kituo hicho huku sajent takamoyo akiandika kila kilichokuwa kikisemwa na janeth .
“ kwa hio unamaanisha aliekuokoa hukumuona ?”
“ ndio sikumuona ila aliniambia jina lake nimwite mzalendo tu basi inatosha “.
“ na baada ya kutoka hapo ndani ulifikaje mpaka mjini “
“ nilipewa lift na mzungu mmoja hivi anajulikana kwa jina la stephano lamberk “.
“ unamaanisha huyo mtoto wa bruno lamberk aliekuja nchini hivi karibuni “
“ ndio “
“okey naona ndio amekuleta hapa”
“ ndio”
“ pole sana professor janeth , kwasasa sina mengine ya kukuuliza ila pale tutakapokuhitaji tutakuita mahali hapa “
“ nashukuru sajenti takamoyo”.
Baada ya maelezo hayo kamanda wa jeshi la dar es salaam aliongea na waandishi wa habari na kueleza mtiririko mzima wa kesi hio .
“ ndugu waandishi wa habari mnamo saa mbili ya leo tulipokea taarfia ya kutekwa kwa proffessa janeth bendera na baada ya taarifa wanausalama wetu walifika eneo la tukio na kufanya uchunguzi , lakini tukiwa katika uchunguzi huo ndipo tulipopokea simu ya majambazi kuuwawa na mtu aleijitambulisha kwa jina la mzalendo , ambae kwa taarifa alizonazo proffesa ni kwamba mtu huyo hakupata kumuona sura ni hayo tu waandishi “ aliongea kamishina ba baada ya hapo na janeth alihojiwa .
“ proffessa inasemekeana kwamba una umri wa miaka ishirini na saba ni kweli kwamba wewe ni proffessa na uliwezaje kupata uproffesa wako ukiwa na umri mdogo “ aliuliza mwandishi mmoja naefahamika kwa jina la chakunyegera
“ kuwa proffessa kwa umri huu sio jambo la kushangaza sana kama utakuwa na juhudi katika masomo, lakini pia vile vile napenda kusema mungu amenijalia na uwezo wa kuweza kusoma na kuelewa haraka naweza sema ndio kitu kilichoniwezesha kuyapata mafanikio haya kwa haraka “
“ proffessa janeth bendera , jina lako la mwisho linaonesha kuwa linafanana na la marehemu raisi wa tanzania bwana john bendera , je una uhusiano wowote na na yeye?? “
“hapana nadhani kama ningekuwa na mahusaiano ya karibu nayeye ningeweza kufahamika katika jamii ya watanzania , hivyo hakuna mahusiano yoyote kati yangu na ya marehemu raisi bendera “
“tumesikia kwamba umefanya tafiti mbali mbali katika maswala ya teknolojia katika vyuo ulivyopitia je umerudi nchini au umekuja kusalimia na kuondoka kwenda kufanya kazi nchi za nje ka ?” aliuliza mwandishi kimbembe .
“ kwasasa nimerudi kikamilifu nchini na sijarudi peke yangu , nimerudi na timu kamili ambayo kwanzia sasa na kupita kampuni ya NLT tunakwenda kuindeleza Tanzania katika swala zima la maendeleo ya kiteknolojia kwa ujumla wake , ili kuhakikisha Tanzania ya viwanda ambayo mheshimiwa bendera na mheshimiwa raisi wa sasa waliookuwa wakiiota inakwenda kufanikiwa na hatimae taifa letu kusonga katika swala zima la uchumi kwani viwanda kwa sasa ni teknolojia , ukiwa na teknoojia nzuri utadhalisha bidhaa bora kwa muda mfupi ambazo zitaingia kwenye ushindani na bidhaa za nje na ile hali ya watanzania kudharau bidhaa zetu za ndani itakwenda kutoweka kabisa “
Maneno alioongea yaliwafanya waandishi kuridhika lakini pia damiani aliekuwa pembeni na ngozi yake ya kistephano lamberk au kizungu alitabasamu , kwani maneno hayo yalimgusa sana .
Baada ya mazungumzo hayo waandishi waliomba kuongea damiani ama stephano lamberk lakini alikataa kwa kuwaambia kuwa anawaalika rasmi katika siku ya ufunguzi wa kampuni yake wiki moja mbeleni .
ITAENDELEA
SEHEMU YA 47
Taarifa ya kuwawa kwa carlos cardosso ilimfikia kimbona akiwa ofisini kwake , ilikuwa ni moja ya taarifa mbaya kwake , hakuamini kabisa kuwa jambazi hatari wa kimataifa ambaye alikuwa akimuamini sana katika kazi zake na kazi zinazofata alikuwa ameuawa kwa kupigwa na risasi na mtu anaejiita MZALENDO , kwake swala hilo lilikuwa ni pigo , lakini pia kwa vijana wake wengine ambao walikuwa wakimfanyia kazi kwani wote waliuwawa , jina la mzalendo lilizidi kumuumiza kichwa mno na hakujua ni maamuzi gani achukue kwa wakati huo , lakini pia alishukuru kwani pia hakukuwa na mtu ambae amekuwa hai kwani lazima wangebanwa lazima angabainika kwamba yeye ndie aliekuwa nyuma ya vijana hao na hata jambazi hilo .
Wakati akiwa kwenye mawazo simu yake iliita na aliekuw akipiga alikuwa ni sam , alipokea na kuweka sikioni na neno la kwanza kusikia lilikuwa :
“ uko wapi “
“ niko ofisini “
“ nakuja “
“ poa “
Nusu saa tu sam au rich sam alifika ndani ya ofisi hio ya kimbona ndani ya kampuni yake ya KILAC , alionekana na yeye alikuwa na wasiwasi kweli .
“ nimeona taarifa ya kifo cha carlos cardosso kwenye vyombo vya habari “
“ ndio hivyo hata mimi habari hio ndio kwanza nimeipata na mpaka sasa sijajua cha kufanya “
“ sasa una la kufanya lipi na wakati wa kufa washakufa , wewe waache wafu wazike wafu wao sisi tuendelee na mipango mingine , uzuri ni kwamba huyo mzalendo kaua kila mtu “
“ ni kweli kabisa na mimi kanirahishia kazi kweli kwani angemuacha hata mmoja na polisi wangefika huenda wangetutaja “
“ hata wangekuwa hai tungemmaliza kabla hajapanua mdomo wake tuna koneksheni nyingi ndani ya taifa hili , au usahasahau kuwa sisi ndio tunao liongoza taifa “
“ ndio najua , lakini waswasi ndio lazima uwepo “
“ ni kweli “
“ unasema tuongee mpango mwingine ni upi huo ?”
“ marie yupo nchini “
“ marie yupi “
“ nawewe ushasahau si nilikwambia yule jasusi wa CIA anaetokea thailland “
“ anhaa nimekumbuka daah , kichwa kimevurugwa saivi yaani “
“ haha .. pole lazima uvurugwe najua vjana uliwapoteza wanakuumiza “
“ ndio hivyo , kwa hio anasemaje “
“anasema uchunguzi nchini china amegundua kuwa damiani yupo hapa nchini “.
“ unamaanisha damiani karudi “
“ ndio na inaonekana amerudi muda mrefu , si unaona hali yahewa ilivyombaya “
“ inawezekana , lakini sasa huyo damiani yuko wapi “
“ anasema kuna uwezekano wa mambo mawili , damiani anaweza akawa stephano lamberk au stephano lamberk anafahamiana na damiani “
“ hapo stephano kufahamiana na damiani nakubali , ila swala la stephano lamberk kuwa damiani sikubali hata mje na mzimu wa mama yangu “
“ hahaha … hata mimi nimemwambia hivyo ila kasema speculations zake zinaweza zikazaa majibu kati ya hayo na kwasasa anaingia kazinia kulifatilia hilo “
“inabidi umpe na kazi ya kufatilia na hili la huyu mzalendo “
“ ndio maana nimekuja hilo ni moja wapo “
“ na lingine ni lipi “.
“ death notice from U-97 “
“ inamuhusu nani hio “
“ julieth , stephano lamberk ,sabi mboneche na wema sufiani wanatakiwa wauwawe tumemepwa siku kumi kulikamilisha hilo “.
“ huyo sabi ni nani “
“ ni mtoto wa marehemu brigedia mboneche saivi ni mkurugenzi wa ikulu mawasiliano “
“nini , sasa kwanini wauwawe na hilo la mke wa raisi linakaa vipi “
“ hata mimi sielewi yaani nimechanganyikiwa , nilichoambiwa ni kwamba hao wanahatarisha umoja wetu ndani ya Afrika kwa ujumla “.
“mhmh ! aisee sielewi “
“ mimi kuna picha inanijia hapa “
“ picha gani “
“brigedia mboneche aliuliwa na U-97 “
“kwanini auliwe “ alingea kwa mshangao .
“ sijajua taarifa hio kwa undani wake ila ni kweli kauliwa na U-97 na taarifa hio nasikia mwendazake alikuwa nayo , jambo ambalo mpaka sasa linanipa mashaka huenda hata mwendazake kauliwa na U-97 “
“mhmh na wema je ?”
“ inawezekana pia kuna mambo anayafanya pasipo ya uelewa wetu yanayohatarisha umoja , level za juu za uongozi wanaijua tanzania kuliko tunavyo ijua sisi “
“ unamaanisha sisi ni kama mashushu tu “
“ ndio maana yake , ninahisi U-97 sio madawa ya kulevya tu kuna ya ziada ila sitaki hata kuyajua mimi mimi najari pesa tu “
“ umeongea point sam , sisi tudiri na njururu tu “.
“ hahaha.. eti njururu , ndio maana nakukubali kimbona , njururu ndio kila kitu siku ya kwenda mars nataka niwe na nauli “
“ hahaha .. kumbe unampango wa kwenda mars “
“haha ndio , sema kuna hili swala la kufa linaninyima raha kabisa “.
“ haha .. mimi hata siliwazii saivi nakula maisha tu , nikifa mimi vijana wataniwakilisha “
“ kweli kabisa , tunawekeza kwa watoto “
“ ndio , halafu hujaniambia hao wanakufaje na nani anafanya hayo”
“hio ndio kazi yetu kimbona , nina mpango wa kwenda kuwakodi al shabab “
“uatawapatia wapi wanamgambo hao “
“ mawasiliano yao yapo ndani ya umoja wetu “
“ unamaanisha U-97 “
“ ndio kwani kuna umoja gani mwingine , yaani mpaka sijui boko haram islamic state , alqaida sijui waasi gani wote wapo chini ya ufadhili wa U-97 , mambo haya ni siri kimbona acha uropoke uone na wewe death notice yako nisipotumiwa “
“siwezi ropoka , yaani huu umoja kuna muda unaniogopesha ila hela zikiingia kwenye kaunti nasahau hofu “
“ hahaha hfu ndio adui yetu kimbona , ukiwa na hofu umekwisha utakuwa masikini wa kutupwa “
“ ni kweli kabisa “
“sasa nimekuja kukuambia pia kuwa kesho nitakuwa na kikao na wakuu wa U-97 , japo mheshimiwa yupo nje ya nchi , ajenda ya kikao hicho nishatumiwa , hili la sabi , wema , stephano na janeth ni siri yetu mimi na wewe “
“ hakuna shida “
Basi sam aliondoka na kumuacha kimbona akiwaza .
*****
Basi hatimae giza liliingia muda wa saa mbili kamili za usiku ndani ya hoteli ya regency Kilimanjaro ilionekana gari ya merina ikipark katika eneo hilo na akatoka mrembo huyo akiwa amependeza kweli , baada ya yeye kutoka na kuingia ndani , iliingia tena gari aina ya V8 XR nyeusi na alitoka mkuu wa majeshi bwana abdallaha khalifa bwana aliefika akiwa amevalia suti yake na miwani na akaingia ndani ya jengo hilo la hoteli .
Nusu saa mbele ndani ya ukumbi mdogo wa mikutano eneo la VIP meza ilionekana ikiwa imezungukwa na watu wasiopungua watano yaani bwana kizito kabwela , merina sostness , Abdallah khallifa , bwana elly matinde, zakayo au agent Z na CP (commissioner police ).
“ jamani za saa hizi “ aliongea matinde kiongozi wa kikosi hicho cha watu watano ukimtoa zakayo maana zakayo yeye hapo alikuwa yupo kwa ajili ya maslahi tu .
“ salama “
“ kwanza nawashukuru sana kwa kufika wote bila kukosa katika kikao hichi cha dharula na hii imetokana na jambo ambalo lilikuwa nje ya uwezo wangu, kulitokea maamuzi hivyo kuhitaji ushauri wenu juu ya hilo , lakini pia tutasikia ripoti fupi ya pale upelelezi wetu ulipofikia mpaka sasa “ aliongea matinde na kisha alimkaribisha zakayo pasipo kupoteza muda .
“mpaka sasa naweza sema kwamba upelelezi wangu haujafikia mwisho , lakini kuna hatua kubwa ambayo mpaka sasa nimefikia ambayo inanipa matumaini ya asilimia kubwa ya kuikamilisha muda mfupi ujao
Mpaka sasa nimefanikiwa kujua kifo cha mama yake damiani kilivyotokea na kifo hicho kilitokea mnamo tarehe tajwa huku jeshi la polisi kukamilisha upelelezi huo kwa kuutangazia umma kwamba tukio hilo lilikuwa ni la kijambazi ambalo walijaribu kuwahusisha majambazi hao na majamazi waliovamia chuo cha SEKOMU (SEBASTIANI KOLOA MEMORIAL UNIVERSITY ) lakini taarifa hio ni ya uongo na ya kweli ni hii “ alitulia kidogo akaendelea .
“Kifo cha sarah rabani hakikuwa kifo cha bahati mbaya ila kilikuwa kifo cha kupangwa na ni mpango wa muda mrefu ulioandaliwa na bwana bruno lamberk , lakini licha ya kwamba bruno alipanga kufanya mauaji haya lakini inaibuka sintofahamu kutokana na kwamba siku ya tukio la kuwawa kwa sarah rabani , bruno lamberk alikuwa amejeruhiwa kwa risasi , mpaka pale kijana damiani kumfikisha nyumbani kwao kwa ajili ya msaada na hapo kukutwa na mauti , lakini licha ya kwamba siku ya tukio hilo bruno lamberk alikuwa na jereha la risasi, lakini pia kuwa na dhamira ama mpango wa kumuuwa mama rabani, ni kwamba tukio hilo linaweza likawa limefanikiwa ama halikufanikiwa, na hili ni kutokana na uchunguzi nilioufanya na kubaini kuwa siku ya tukio nyumbani kwa sarah kulikuwa na watu wanne yaani saraha marehemu , bruno marehemu , muaji namba moja na muaaji namba mbili, najaribu kuwaita kwa namba kutokana na kwamba mpaka sasa sijapata kuwafahamu majina yao , naendelea.. , muaaji namba moja alikuwa ndani ya nyumba wakati damiani na mzee kivinje (mganga wa kijiji wa tiba za asili )walipo fika nyumbani kwa sarah , mzee kivinje alimshuhudia muuaji namba mbili aliekuwa ameshika bastola na akivuja damu kwenye bega akitokomea huku akiwa ametoka ndani ya nyumba ya sarah lakini pia huyo huyo kivinje aliweza kumshuhudia muuaji namba moja akiwa ndani ya nyumba ,nyuma ya mlango akiwa amejiziba uso , nadhani mpaka hapo mmepata picha kuwa kuna watu wanne ambao wana majibu tunayoyatafuta , lakini wawili tunawatoa kwani washatangulia mbele za haki na sasa waliobaki ni wawili yaani muuaji namba moja na namba mbili , lakini kwanini mpango huo umuhusu sarah , ni kwamba kwa taarifa za awali ni kwamba damiani alikuwa ni chaguo la bruno katika kukamilisha mpango X nimeupa mpango X kwani mpaka sasa sijajua unahusu nini, ni jambo ambalo nitalifatilia kiundani Zaidi,mahusiano ya mambo haya na kujua mahali alipo damiani ni kama ifuatavyo , kama tulivyoona mambo haya yalivyotekelezwa ni kwamba danieli mtalemwa aliuliwa na carlos cardosso akishirikiana na agent miss k (suzzane ) paisina shaka naamini miss k kapokea maagizo kutoka kwa raisi , lakini pia bila shaka pia carlos cardosso aliachiwa huru kwa ajili ya kummaliza danieli kwasababu danieli alikuwa ni komandoo namba moja na hakuwa na mpinzani hapa chini katika mapambano Zaidi ya carloss hilo ni A , B ni kwamba target ya kuuliwa kwa danieli ni kutokana na taarifa nyeti aliokuwa danieli ambayo ni nyaraka zilizoachwa na bruno , lakini ikatokea kwamba nyaraka hizo hakuwa nazo danny ila alikuwa nazo damiani hivyo suzzane alikuwa akitaka nyaraka hizo kutokana na oda ya raisi , lakini kitendo cha kukimbia kwa damiani hii inakuja sasa kwenye ripoti yangu ya nyuma tuliona damiani akipata msaada ambao tunaamini kwamba bila kuwa na koneksheni asingefanikiwa kupata msaada huo hadi kwenda thailland hio inaniaminisha kwamba koneksheni hio ilitengenezwa na bruno mwenyewe au vininginevyo katika mpango x na kwa maneno hayo nasema kwamba moja ya mtu ambae yupo kwenye mpango x ni balozi wa kenya bwana njiroge japo swala hilo suna uhakika nalo , bwana njiroge atatufahamisha ilikuwaje akakubali kumsafirisha damiani mpaka kenya .
Pili uchunguzi hautaishia hapo naamini kati ya muuaji namba moja na namba mbili mmoja wapo anaweza akawa uraiani au wote wakawa uraiani hivyo taarifa za bwana njiroge zitakuwa muhimu na pia za aidha muaji namba mbili au namba moja zitakuwa muhimu .
Mwisho nihitimishe kwa kusema kuwa mpaka sasa carlos Cardoso keshapoteza maisha kwa kuuliwa na mtu anaejiita mzalendo ninayo taarifa ya awali kutoka kituo cha polisi magogoni zinazoainisha kwamba hili sio tukio namba moja la mtu anaejiita mzalendo , pili pia taarifa kutoka TISS inasema kuwa huenda mzalendo akawa anahusika na shambulio la raisi pale serena.”
“ ni kupongeze sana bwana zakayo kwa ufanisi wako katika uchunguzi wako lakini nina swali moja , kuna uwezekano wa mzalendo kuwa na koneksheni na mzalendo “.
“ mheshimiwa kizito hilo ndio swala ambalo nitalifanyia uchunguzi wa kina na kama kuna muunganiko naamini tutafahamu “
“mimi nina swali moja kama ulivyodema mpango x , je unaamini kuwa mpango huu unaendelea na kama unaendelea je damiani anaweza akawa ndio anaendeleza mpango huo “aliuliza merina
“ naamini mpango huo unaendelea m, kama damiani aliweza kufika nchini thailland naamini hivyo , lakini pia naamini anaweza akawa anafanya mambo ambayo hajui asili yake huku akiwa amemezezwa udanganyifu “ .
“nataka kuongezea hapo kwa miss merina kuhusu huo mpango x , vipi unaamini swala hili ni rahisi kupata majibu yote tukiwa ndani ya taifa la Tanzania bila kupitia katika nyayo ambazo amepita damiani ili kujua mpango huo x “aliuliza CP
“ hilo nalo ni swala ambalo nilikuwa nikilifikiria na pia nilitamani kuliweka wazi , kuna mawili kwa mambo ambayo yanaendelea hapa nchini kuna hisa zinaniambia kuwa yanaweza yakawa yanahusika na mpango x moja ya jambo hilo ni juu ya swala la bwana stephano lamberk kufika hapa nchini na kuanza swala la uwekezaji , mali za bruno kwenda kwa innova , mzalendo haya ni mamb ambayo mpaka sasa yananifikirisha nab ado sina majibu sahihi kama mnavyojua sisi wenyewe tulimjua bruno kwa Zaidi ya miaka ishirini iliopita , na hatukuwahi kusikia kuwa ana mtoto basi kuna majibu ambayo yanaweza yakatupa majibu Zaidi “
“ nikushukuru sana bwana zakayo kwa upelelezi wako , sasa nirudi kwa sisi wana jumuia yetu hii ambayo mpaka sasa hatujaipa jina , swala nililoshindwa kulitolea maamuzi ni swala la huyu balozi wa kenya , zakayo katoa pendekezo la kumteka , lakini kwangu mimi nimeona ni jambo la hatari kwa nchi na ushirikiano wa kimataifa vilevile kwani mpango wetu sio kuiharibu Tanzania ila ni kuijenga hivyo nilikuwa nahitaji mawazo yenu katika jambo hilo “ aliongea matinde
“ mimi nina wazo moja , nadhani tutafute footage ambazo zitatapelekea kuwa ushahidi ili pale tutakapoenda kumhoji bwana huyu njiroge asije akakataa kutohusika , na kama akikubali basi ni lazima atatupa majibu sahihi “
“ naunga mkono hja ya bwana kizito “
“Tunaunga mkono wote hoja “
“ kama tunaunga mkono wote hoja , basi naamini swala hilo halitakuwa na ugumu nitakachotakiwa kufanya ni kumpatia kitambulisho ambacho kitamuwezesha bwana zakayo kufanya pelelezi ndani ya balozi na pia ndani uwanja wa ndege , labda kama zakayo una jambo la kuongea “
“ ndio ninalo la kuongea ambalo pia naamini litanisaidia katika uchunguzi wangu “
“ni lipi hilo “
“ waheshimiwa nadhani tunakumbuka miaka ya nyuma nyie ndio mlikuwa wateule wa mheshimiwa bendera , na pia kwa taarifa ni kwamba ninnyi ndio mliohusika katika biashara nzima ya kutokomeza dawa za kulevya , lakini nikiwa nchini Indonesia nilipokea mission iliopewa jina la 0404 na nilikamilisha hio na mission hio ilitoka kwa raisi mwenyewe nataka kujua ni kwa namga gani raisi bendera aliweza kusaliti biashara yake ya madawa ya kulevya na kuunga juhudi za kukomesha madawa ya kulevya hapa nchini kwani moja ya vijana wa bruno walinipa taarifa kwamba bruno hakufanya kwa mapenzi yake ila ni kwamba raisi alimshika pabaya , nataka kujua huenda likanisaidia kujua mpango x “ aliongea zakayo na kuwafanya wazee hao washangae ni kama waliokuwa wakijuliza na kizito alitingisha kichwa na kumuashiria matinde kuwa anaweza kuongoza .
“ mission 0404 ilikuwa inahusika na mtoto wa bruno na mheshimiwa hakuweza kutuweka wazi sana ila hio ilikuwa ni weak point ambayo ilituwezesha kumfanya brunoo cooperate”
“ mpaka hapo nimepata picha , lakini kuna jambo linanichanganya kidogo kama ni hivyo basi bruno atakuwa na watoto wawili , kwani niliemteka mimi alikuwa ni mwanamke “
“inawezekana “
“ waheshimiwa kabla hamjaendelea nina swali kidogo “ aliongea merina na kuwafanya wote wamwangalie .
“ mmesema mission 0404 nataka kujua ilikuwa inahusu nini “
“ilikuwa ni abduction miss merina “
“ abduction , ilitokea wapi hio ?”
“USA” aliongea zakayo na hapo ndipo alipo mfanya merina atoe jicho huku machozi yakianza kuloanisha mashavu yake na kuwafanya wote washangae .
ITAENDELEA .
SEHEMU YA 48
“ miss merina vipi mbona unatoa machozi”.lilikuwa ni swali kutoka kwa kizito kwenda kwa merina , na merina haraka haraka alijikuta akifuta machozi .
“ hakuna muheshimiwa kuna tukio nimelikumbuKa miaka ya nyuma kidogo limenifanya hisia zangu zizamie huko “ aliongea merina huku akijiweka sawa na hakukuwa na mazungumzo mengi ndani ya kikao hicho kwani kilifungwa rasmi na kila mtu akatawanyika .
Upande wa kutokea nje kabisa ya maegesho alionekana matinde akiwa ametangulizana na zakayo .
“ mheshimiwa huyu merina wazazi wake ni wakina nani ?”
“nasikia wanaishi canada huko kwanini unauliza ?“.
“anafanana na yule msichana niliemteka miaka ya nyuma “
“ unasema kweli?? “
“ ndio tena nilishangaa sana baada ya kumuona “
“ kwa hio unataka kumaanisha kwamba merina ni mtoto wa bruno? “
“ siwezi jua labda wamfanana tu ila sina uhakika “
“ haiwezekani watakuwa wamefanana kwani merina nimejaribu kufatilia habari zake ni kweli wazazi wake wapo Canada ni wamiliki wa kampuni ya ATPAY “
Aliongea matinde na kumfanya zakayo akubaliane , muda huo walikuwa wakiingia kwenye gari , lakini wakati wakiwa wanaingia kulionekana mtu kwa upande wa kushoto akiwapiga picha , alikuwa kijana mdogo alievalia kofia huku akiwa ameshikilia kamera yenye lensi kubwa .
Upande wa merina alijikuta akiendesha gari huku akiwa na mawazo ya hapa na pale , alijikuta akikumbuka na yeye tukio la kutekwa akiwa chuoni nchini marekani , tukio hilo japo hakupata madhara yoyote lakini alikuwa akiliogopa sana kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kutokewa na tukio la aina hio .
“ nimewakumbuka mom and dad” aliongea huku akiongeza mwendo kuwahi nyumbani kwake , lakini mawazo yake hayakuishia kwenye kuwakumbuka wazazi tu alikuwa pia akikumbuka ripoti nzima ya zakayo , alikiri kuwa zakayo alikuwa vyema katika kufanya upelelezi lakini kwa upande mwingine aliona kama zakayo alikuwa akifanya upelelezi ambao haukuwa ukimuhusu damiani .
“ stephano anaweza akawa anajua ni wapi damiani alipo lazima nikamuulize kesho yake huu uchunguzi wa zakayo unachukua muda mrefu mno kuliko nilivyotegemea “ alijiongelesha merina huku akiingia mtaa wa masaki
******
Mheshimiwa raisi japo alikuwa safarini lakini alikuwa akifatilia kila kilichokuwa kikiendelea ndani ya taifa la tanzania , , japo bwana huyu alikuwa na madhaifu yake lakini likija swala la maslahi ya taifa alikuwa akipigania sana , na katika kipindi kifupi cha uongozi wake alikuwa amefanya mengi ya kuwafanya watanzania wajivunie .
Muda huo alikuwa ndani ya hoteli ya kitalii ndani ya jiji la Washington DC akiwa anaangalia baadhi ya taarifa kutoka Tanzania , moja ya taarifa iliokuwa gumzo ni ya proffessa janeth kutekwa na mpaka kupatikana kwake , huku akiwa kivutio kwa kuwa proffesa kwa umri mdogo tu jambo ambalo liliwashangaza sana watanzania .
“ janeth bendera “ alijikuta akitamka jina hilo huku akuwa ameshikilia mvinyo wake akiwa amekaa kwenye sofa huku akionekana kuwaza mbali mno na hapo kumbukumbu zake zilimpeleka nyuma miaka kadhaa .
***
Ni baada ya miezi kadhaa baada ya kurudi nchini kutokea kenya ambako nilikuwa nilienda kumwakilisha mheshimiwa raisi katika kikao cha wakuu wa nchi za afrika mashariki , kwangu ndani ya kipindi cha miezi hio kilikuwa ni kipindi ambacho kwa namna moja ama nyingine nilikuwa nikisumbuliwa na mawazo ya hapa na pale , maneno alioniambia mheshimiwa ndalu nikiwa ndani ya jiji la Nairobi yalikuwa yakijirudia rudia mara kwa mara ndani ya kichwa changu , na kuongeza shauku yangu ya kutaka kujua baadhi ya mambo yanavyokwenda , kwani nilijihisi kabisa nilikuuwa kwenye kiza kinene , furaha yangu mbele ya bendera ilianza kupungua , udhaifu mkubwa ambao niilikuwa nao katika maisha yangu ilikuwa ni familia nilikuwa nikiipenda sana familia yangu kiasi kwamba sikupenda jambo lolote liikumbe familia yangu , maneno ya mheshimiwa ndalu kuhusisha na familia yangu kidogo nilipata mashaka , lakini si mashaka tu lakini pia nilitaka kujua kwa undani maneno yake kama yana ukweli ndani yake, maana mpaka mtu kuja mpaka hotelini kwangu tena nje ya nchi ilimaanisha kwamba kuna jambo alikuwa akitaka nilifahamu ambalo ameona kabisa sikuwa na ufahamu nalo .
Sikuona haja ya kujiumiza tena na mawazo ya aina hio , jambo nililoamua siku hio nilivyokuwa nikitoka nyumbani kwangu nikielekea ofisini, ni kulifatilia swala hilo , mara baada ya kufika ofisini nilikaa nikaanza kuwaza ni kwa namna gani ninaweza kulifatilia jambo hilo kwa undani, na kwakuwa mimi mwenyewe sikuwa na uzoefu na kazi hio na pia nisingeweza kuifanya miimi mwenyewe niliona kulikuwa na ulazima wa kupata mtu ambae anaweza akalifanya jambo hilo , nilianza kuwaza na kuwapambua walinzi wangu mmoja baada ya mwingine , wapo niliokuwa nikiwaamini sana lakini pia niliamini wasingeweza kuifanya kazi hio kwani walikuwa na ujuzi wa kawaida sana ambao wasingeendana na kazi yangu , kazi nyingine iliibuka hapo , niliwaza ni nani anaeweza kunifanyia kazi hio akili yangu ilikwama , nilijikuta nikipotezea kwanza swala hilo na kufanya majukumu yangu ya kiofisi na baada ya kumaliza majukumu yangu ya kiofisi ndipo nilipokea simu kutoka kwa muheshimiwa , wakati huo alikuwa makao makuu ya nchi na mimi nilikuwa ndani ya jiji la dar es saalam , nilipokea simu ya muheshimiwa .
“habari za kazi muheshimiwa “
“ salama henry , unaendeleaje na familia na majukumu yako kwa ujumla “
“ mheshimiwa namshukuru mungu familia inaendelea vizuri lakini pia na majukumu yangi ya kiofisi yapo vizuri “
“ nafurahi kusikia hivyo henry , sasa nimekupigia kuna jambo nataka nikwambie , umoja wa wafanyabishara wa dar es salaam mwezi uliopita waliniomba nihudhurie katika mkutano wao walioupa jina la ‘get together ‘ na waliniomba kuwa mgeni rasmi , lakini kutokana na ratiba zangu na tarehe tajwa mambo yamebanana kwani siku hio nina ugeni kutoka china, waziri wa mambo ya ndani ya uchina atakuwa hapa nchini hivyo naomba uniwakilishe “
“ hakuna shaka muheshimiwa nitakusaidia katika hilo “.
“shukrani sana henry , kuhusu hotuba ya siku hio na maelekezo mengine nitakutumia kwa njia ya email “
“ sawa muheshimiwa “.
Baada ya kupokea simu hio kwangu niliona ni jambo jema kwani na mimi pia nilikuwa mfanya biashara , hivyo kumuwakilisha mheshimiwa katika kikao hicho kwangu ilikuwa ni fursa nyingine ya kufahamiana na wafanya biashara wakubwa nchini ambao sijawahi kukutana nao .
Basi siku yenyewe ilifika na nilifanikiwa kuhudhuria kikamilifu katika mkutano huo ambao nilikuwa mgeni rasmi nikimuwakilisha mheshimiwa raisi , ulikuwa ni mkutano uliokuwa umejaaa mengi ya faida kwa Tanzania na kwa wafanya biashara pia .
Moja ya wafanya biashara waliokuwepo katika kikao hicho alikuwepo bruno lamberk akiwa na walinzi wake , alikuwa ni moja ya wafanya biashara waliokuwa na ulinzi mkubwa sana nchini na hio yote ilikuwa ni kutokana na mchango wake katika swala zima la kutokomeza madawa ya kulevya , mchango ambao ulitokana na kuwasaliti wenzake na kupelekea kuwa na maadui wengi nchini na hivyo ulinzi wake kuwa ni moja ya jukumu la kiserikali .
Moja ya walinzi wake ndie alienivutia mno kwa kazi yangu hakuwa mwingine bali alikuwa ni suzzane , nilikuwa nikizijua sifa zake nyingi japo ya kuwa komandoo lakini pia alikuwa na mafunzo ya kiintellijensia , jambo ambalo lilinifanya nimuone moja ya watu ambao kama angeaminika angekuwa ni perfect candidate (mtu sahihi) kwa kazi yangu , wazo hilo liliibua changamoto nyingine ndani ya kichwa changu , nilijua kabisa mwanadada huyo alikuwa ni mlinzi wa bruno , lakini pia ni moja ya vijana waliokuwa wakiaminiwa na mheshimiwa raisi , kwangu changamoto ilikuwa ni kwa jinsi gani ninaweza kumshawishi kunifanyia kazi yangu na pili kumwamini kwa kutotoa siri juu ya kazi nirakayompa .
Baada ya kurudi nyumbani kwangu wazo moja lililonijia ilikuwa ni kutafuta wakati wa kuongea na suzzane kwa siri sana pasipo ya kushitukiwa , jambo nililokuwa nikitaka kulifanyia uchunguzi lilikuwa likimuhusu bruno pia ndio maana niliona natakiwa kumshawishi suzzane kwa namna yoyote ile anifanyie kazi yangu.
Siku ya jumamosi ndio siku niliofanikiwa kuandaa appointment meeting na suzzane katika hoteli ya colleseum ndani ya masaki , nilichagua hoteli hio kutokana na kwamba siku hio bwana bruno alikuwa ndio mahali pake pakufanyia mazoezi kwani matajiri wengi walikuwa wakipapenda kutokana na kuwepo kwa club ya mazoezi (body fitness club) na mimi pia nilikuwa mwanachama wa club hio .
Jambo ambalo nimefanikiwa ni kuonana na suzzane , lakini jambo ambalo sikuwa na uhakika nalo ni kumshawishi mwanamke huyo kunifanyia kazi yangu , na ndio maana nilikuwa ninataarifa nyingi sana zilizokuwa zikimuhusu suzzane , nilikuwa na taariifa zilizokuwa zikiihusu mpaka familia yake kwa ujumla , niliona nivyema kujiandaa kwa namna yoyote ile .
Siku hio hakukuwa na shida sana ya kuonana nae kwani alikuwa ni moja ya walinzi ambao walikuwa zamu katika kumlinda bwana bruno , hivyo alichokifanya suzzane ni kuwaachia wenzake majukumu kwa muda wakati boss waka akichukua mazoezi .
“ nadhani umepata mshangao uliojaa maswali suzzane mara baada ya kupata ujumbe wangu “
“ ndio muheshimiwa nilipatwa na mshangao huo kwani naamini hatupokei maagizo kutoka kwako “
“ napenda ulivyo na maneno ya moja kwa moja suzzane na mimi nitakuwa na meneno ya moja kwa moja ili tuweze kuelewana kwa haraka “
“ hakuna shaka muheshimiwa , maana pia nipo kazini “
“ kuna kazi nataka unifanyie suzzane , ambayo ina malipo makubwa sana kama utaikamilisha “
“ mheshimiwa kama nilivyosema awali ni kosa kubwa kwa mimi kupokea kazi binafsi zinazohusu malipo pasipo ruhusa ya wakuu wangu wa kazi . kwani endapo itafahamika kwa mheshimiwa raisi ninaweza kuipoteza kazi yangu lakini pia ni kosa la kuvunja kiapo changu”
“ nalielewa hilo suzzane kabla hata sijakuita hapa , lakini pia naelewa familia yako kwa ujumla ni kwa jinsi gani unahitaji pesa za kutosha kuitunza , kutokana na baba yako kufilisika kwa kushindwa kulipa kodi na hatimae kuwa gerezani kwa kesi ya uhujumu uchumi “
“ mheshimiwa ulikuwa ukiifatilia familia yangu ?”
“sio kuifatilia suzzane najua mengi kuhusu yanayoendelea katika familia yako , lakini yote nimeayafanya ili kujenga Imani yangu kwako , juu ya kazi ambayo nataka kukupatia unifanyie “
“ mheshimiwa kama unataka kunipa kazi kutokana na hali ya maisha ya familia yangu , basi naomba kazi hio umtafute mtu mwingine akufanyie “
“suzzane sio nia yangu ya kuifatilia familia yako ,lakini niimefanya hivyo kutokana na umuhimu wa kazi yangu lakini pia kujilinda mimi mwenyewe , najua huajamtembelea muda mrefu baba yako gerezani ,nataka kukuambia kuwa anateseka sana na mimi ndio mtu pekee ambae naweza nikamtoa gerezani “
Suzzane alijikuta akikumbuka kuwa ni kweli hajawahi kumtembelea baba yake gerezani muda mrefu , tokea apatikane na kesi ya uhujumu uchumi , alikaa huku akimwangalia mheshimiwa kwa hasira .
“ naomba nikalifikirie hili muheshimiwa nipe muda “ aliongea suzzane huku akinyanyuka .
“ sawa suzzane unasiku mbili tu za kufikiria , kama upo tayari utanipigia kwa hii namba na utaletewa taarifa za kazi yenyewe ambayo unatakiwa kuifanya , siku utakayokamilisha kazi yangu ndio siku ambayo nitamtoa baba yako gerezani “. Aliongea makamu wa raisi , na kisha aliagana na suzzane huku akiamini kwa asilimia mia maongezi hayo yamefanikiwa , kwani alishajua udhaifu wa suzzane uko wapi hasa pale alipo litamka jina la baba yake , hizo zote zilikuwa ni hila za henry katika kumpata suzzane , aliamini misimamo ya wanajeshi ndio maana alichukua tahadhari mapema sana na hata gerezani alitoa amri ya baba yake suzzane kuongezewa mateso makali mno , huku akiamini kabisa suzzane lazima angefika gerezani kwa ajili ya kumuona baba yake kabla ya kufanya maamuzi .
Basi baada ya mimi kuagana na suzzane sikuwa na lingine zaidi ya kusubiria jibu langu kutoka kwa suzzane , jibu ambalo niliamini kwa asilimia mia moja kwamba lazima suzzane akubali , kwani kama mheshimiwa andalu alivyotumia udhaifu wangu kwa kutaja familia yake katika kufikisha ujumbe wake na hivyo hivyo na mimi nilitumia udhaifu wa suzzane katika kufikisha ujumbe wangu ili akubali kunifanyia kazi yangu .
Siku moja mbele nilipokea simu kutoka kwa mkuu wa magereza kuwa suzzane alifiika kumuona baba yake , jambo lililonifanya kutabasamu mno , kwani niliamini kwa hali ambayo atakuwa amemkuta nayo baba yake , basi lazima angenitafuta , na kweli nilikaa Zaidi ya masaa mawili tu ndipo nilipo pokea simu kutoka kwa suzzane akitaka kazi huku akihitaji nimtoe baba yake gerezani , ule msemo wa damu nzito kuliko maji ulichukuwa nafasi yake.
Basi nilimpa suzzane kazi kuu mbili , kazi ya kwanza ilikuwa ni kuchunguza maisha ya bruno kwanzia akiwa nchini kwa mara ya kwanza mpaka siku ambayo anausaliti umoja wake , pili nilihitaji kujua mwenendo mzima uliofanyika mpaka raisi bendera kuwa raisi wa Tanzania .
Baada ya kumpa kazi hio suzzane , wiki hatimae mwezi ulitimia na ndipo suzzane alipo nitaarifu kuwa anataarifa kamili ya kazi niliokuwa nimempatia , na mimi kwa hamu kubwa sana ya kujua ripoti hio sikukawia kwani nilipanga sehemu ya kuonana nae , sehemu yenyewe ilikuwa ni ndani ya hoteli ya new Africa hoteli muda wa saa tatu kamili za usiku ndio suzzane alipofika ndani ya chumba ambacho nilikuwa nimekichukuwa kwa ajili ya kuonana nae.
“ enhe niambie suzzane ripoti inasemaje “
“ suzzane kwanza alitabasamu jambo ambalo lilinishangaza sana , lakini sikutaka kuuliza maswali mengi Zaidi ya kutaka kusikiliza ripoti hio .
“ mheshimiwa una moyo wa kusikiliza ?”
“ suzzane niambie acha kunitisha , nimepitia magumu mengi bhna “
“ mheshimiwa katika uchunguzi wangu , mkeo pia emejitokeza katika ripoti yangu , je unaniruhusu niendelee ?”
Nilijikuta moyo ukipiga paa , baada ya kusikia jina la mke wangu , kwa jinsi suzzane alivyokuwa ananinagalia niliamini kabisa ripoti hio haikuwa na mazuri kabisa ya kuyasikia , nilikuwa nikimpenda sana mke wangu na Zaidi ya yote nilikuwa nikimuamini pia .
“ suzzane naomba usome ripoti hio tafadhari inanihusu mimi sio wewe ndio maana nakulipa “
“sawa muheshimiwa , aliongea kisha akapozi na akaangalia faili lake . na kisha akaendelea , mheshimiwa kutokana na maelezo ya kazi ulionipa nilifanikiwa kufanya utafiti wangu kwa kina Zaidi na ni mengi ambayo nimeyafahamu ambayo pia yanamuunganisha mkeo katika ripoti hii , labda kwa kuanzia nianze na ripoti ya mkeo , mkeo alisoma songea girls , lakini alipofikia kidato cha nne ndipo alipokutana na mpenzi wake wa kwanza ( first love) anajulikana kwa jina la john bendera “
“ unasemaje suzzane ?”
“ ndio mheshimiwa , si umesema nisome , mkeo mpenzi wake wa kwanza , namaanisha madam wema kipenzi chake cha kwanza ni mheshimiwa bendera “ kwa jinsi alivyokuwa akiongea suzzane nadhani alikuwa akifurahia taarifa hio , na hii niliamini huenda ni kwa jinsi nilivyompa kazi hio hivyo alikuwa akilipiza kisasi , nilipata mshituko wa aina yake , moyo uliniuma hatari na hasira zilianza kupanda huku presha nayo haikuniacha salama , pumzi zilinikatika ghafra , na suzzane aliliona hilo na alinipa maji na kidogo hali yangu ikatulia .
“ mheshimiwa niendelee?”
“endelea tu suzzane nipo tayari kusikiliza “
“ mheshimiwa kama nilivyosema mkeo ashawahi kutoka kimapenzi na bendera kuhusu taarifa nyingine jinsi walivyo achana sina , ila waliachana baada tu ya kumaliza kidato cha nne na kila mtu kurejea nyumbani kwao , na kuanzia hapo bendera hakuwahi kuonekana kuwa na mahusiano tena na wema na hio nikutokana na ufaulu mdogo ambao alipata kidato cha nne , huku akiamini aliechangia matokeo yake mabaya alikuwa ni wema , hilo ni la kwanza ,la pili ni mkeo pia ashawahi kutoka kimapenzi na bruno lamberk na inasemekana wema ashawahi kubeba mimba ya bruno mpaka kujifungua lakini haikujulikana mahali mtoto alipo mpaka sasa hivi , hivyo nilishindwa kupata taarifa juu ya mtoto “ suzzane wakati akisoma hakujua kuwa nilikuwa kwenye hali gani kwani neno la mwisho kusikia lilikuwa ni ‘wema ashawahi kubeba mimba ya bruno ‘ hapo hapo ndipo nilikata moto nilikuja kuamka siku nyingine kabisa nikiwa hospitalini , mwanzoni baada ya kufungua macho yangu sikukumbuka ya jana lakini nilijishangaa kwanini nilikuwa ndani ya hospitali , na hapo ndipo nilipo anza kuvuta kumbukumbu zangu nyuma na kuanza kukumbuka wakati suzzane akinisomea ripoti ile , machozi ya kiume ndio yalio anza kunitoka tena mbele ya mke wangu , nijilikuta nikimwangalia kwa hasira mno huku macho yakiwa yameloana machozi .
“ kuna nini mume wangu , mbona uko hivi jamani “ aliongea wema , nilijikuta nikitamani kuongea chochote lakini nilijizuia lkuongea neno , moyo ndio uliokuwa ukiniuma mno , nilikaa hospitalini huku dokta akimwambia mke wangu kuwa nilipata mshituko wa moyo , wema alitaka kujua ni kipi kilichonifanya kuwa na mshituko moyo lakini sikutaka kabisa kuongea kitu , jambo ambalo nimeligundua lilikuwa likiniumiza sana moyo , kuna muda niliona bora hata nisingefatilia ya nyuma kwani yamekuja kuniumiza tu .
Baada ya hali yangu kuonekana ipo kidogo imetulia ndipo niliporudi nyumbani na mtu wa kwanza kuja kuniona alikuwa ni raisi bendera , nakumbuka hio ndio siku ambayoo nilithibitisha maneno ya suzzane na hio ni mara baada ya mheshimiwa bendera kusalimiana na mke wangu , wote walikuwa wakiangaliana kwa macho ya kuongea kabisa , mapenzi yanauma nyie yasikilizieni tu kwa wengine , jinsi moyo ulivyokuwa ukiniuma haikuwa na mfano , chuki yangu dhidi ya mheshimiwa bendera iliibuka kwa kasi ya ajabu sana , japo nilivumilia sana , lakini nilitamani kumkaba na kumuuliza kwanini alikuwa akinificha mambo , nilikuwa nikimwamini sana rafiki yangu bendera lakini kitendo cha kunificha juu ya uhusiano wake wa nyuma na wema liliniuma sana , lakini sikuwa na jinsi kabisa , nilichokuwa nikiwaza kwa wakati huo ni kutaka kujua kama walikuwa wakiendeleza mapenzi yao pasipo ya mimi kujua na hapo ndipo nilipo mpa moja ya vijana wangu kazi ya kumfatilia mke wangu .
Baada ya siku kadhaa kutengemaa nilimpigia tena suzzane nikitaka aje animalizie ripoti yangu na awamu hii sikutaka kabisa kwenda hata hotelini kwani nilimuita ofisini kwangu kabisa , sikujali tena juu ya usalama wake au nini .
“ suzzane nataka uniambie kuhusu mtoto wa bruno na mke wangu yuko wapi “.
“ mheshimiwa kwa taarifa nilizo nazo ni kwamba mkeo alijifungua salama mkoani singida , lakini baada ya hapo hakuwahi kuonekana kabisa kuwa na mtoto “.
“ kwa maana hio kuna uwezekano mtoto huyo kuwepo mahali anaishi na je alikuwa ni jinsia gani ?”
“ alikuwa ni mtoto wa kike “
“ na bruno alikuwa akijua juu ya hilo “
“ ndio muheshimiwa , kwani alienipa taarifa alisema bruno ndie aliemshawishi wema kuacha kazi mara baada ya kupata ujauzito “.
“wanawake wauji kabisa , nimekaa miaka yote hio pasipo kujua kuwa mke wangu ashawahi kujifungua bullshit .“
Nilijikuta nikiongea kwa hasira mno
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 49
“ pole sana mheshimiwa “
“ sina haja ya pole yako suzzane najua unanikejeli tu “
“ hapana mheshimiwa namaanisha kutoka moyoni “
“kama unamaanisha nieleze maengine nisio yajua kuhusu mke wangu , maana inaonekana naishi na mtu ambae simjui kabisa “
“ ni hayo tu mheshimiwa “
“ nipe yanayomuhusu raisi bendeera “
“ kuhusu raisi bendera pia nilijua kuwa, uraisi ilikuwa ni moja ya ndoto yake ya muda mrefu tokea akiwa sekondari “.
“ wewe umejuaje hayo mambo ya zamani suzzane “
“ mheshimiwa si uliniambia nifatilie maisha ya watu hao kwanzia mambo yao ya nyuma “
“ ndio nilikuambia lakini wewe umeyajuaje “
“ nimehoji watu wa karibu na bendera waliokuwa wakimjua na hili nimeambiwa hata mkeo alikuwa analijua “
“ unamaanisha mke wangu alikuwa anajua ndoto ya bendera ya kuwa raisi? “.
“ bendera na mke wangu wanafiki sana sijapata ona , huenda yapo mengi ambayo siyafahamu , enhe wewe nani kakupa hizi habari “
“ mtu wa kwanza kunipa taarifa za bendera ni rafiki yake aliesoma nae songea boys na kwa upande wa madam nilipata nafasi ya kuwajua marafiki zake wawili mmoja alikuwa ni mfanyakazi hoteli ya singita grumeti iliopo serrengeti na mwinginge alikuwa ni mwanafunzi mwenzake “
“ endelea “
“ kama nilivyosema kuwa maisha ya bendera ndoto yake kubwa ilikuwa ni kuwa raisi , zipo juhudi mbali mbali alizozifanya mpaka kupata nafasi hio , akianzia kuwa diwani mbunge , waziri na hatimae raisi , katika safari yake hio ..”
“vipi kuhusu kuchukua fomu ya uraisi ?”
“ swala la kuchukua fomu bado sijalifatilia kwa undani wake na hii ni kutokana na kukosa taarifa , lakini miezi mitatu kabla ya uchaguzi alikutana mara kadhaa na waheshimiwa wastaafu wa wamu ya nne , awamu ya tano na ya sita , lakini pia alikuwa na ukaribu na mkuu wa kitengo cha TISS bwana ngalu aliekuwa chini ya mheshimiwa ndalu raisi wa awamu ya saba “.
“ kwa hio wewe suzzane unaonaje kuhusu hilo swala , unadhani mheshimiwa bendera alikuwa ni moja ya watu ambao walichukua fomu pasipo kuwa na nia “
“ mheshimiwa siamini katika hilo “
“ good suzzane kwa kazi yako , niliokuahidi nitayatendea kazi , lakini niseme kuanzia sasa wewe ni mfuasi wangu na unayajua mengi kuhusu mimi pamoja na familia yangu , hivyo tulioongea hapa ni siri yangu mimi na wewe na pia nitatimiza niliokuahidi , lakini nikikuhitaji katika kazi yoyote ile utanifanyia , tumeelewana suzzane ?”
“ mheshimiwa nadhani hilo ni swala ambalo hatukuahidiana , kazi yangu nishafanya na sitaki kazi nyingine kutoka kwako “.
“ suzzane nadhani kuna kitu hukielewi , mimi sio mjinga wa kukuacha hivi hivi , unayajua mengi kuhusu mimi nikikuachia ukiwa upande wa bendera kuna mambo mawili unaweza ukanisaliti au ukatoa siri zangu hivyo njia ni moja tu ukubali kuwa mshirika wangu kwanzia sasa , au nikupoteze wewe pamoja na familia yako , moyo wangu saivi haumwamini mtu kabisa kwa haya yote nilioyasikia na roho yangu imekuwa mbaya mno hivyo ni wewe kuchagua “
Suzzane hakuwa na ujanja tena na alionekana kuniogopa hivyo hakuwa na namna ya kukataa kile nilichokuwa nataka , na kwanzia siku hio suzzane alikuwa akifanya kazi zangu nyingi na nyingine hata hakuwa akizitaka alikuwa akizifanya na hio ni kutokana na nguvu niliokuwa nayo , nilikuwa na pesa za kutosha na pia nilikuwa makamu wa raisi , hivyo ilikuwa ni rahisi kwangu kumpoteza yeye na familia yake , hivyo salama yake ilikuwa ni kuwa mshirika na mimi .
Baada ya ripoti ya suzzane , nilijikuta nikiweka kisasi juu ya mheshimiwa bendera , bruno , na mtoto aliemzaa na wema , mapenzi yangu kwa wema hayakupungua japo ya kuujua ukweli kuwa alikuwa akinidanganya nilimpenda sana lakini sikumuaimini tena .
Kiufupi kwanzia siku hio mfumo wangu wa maisha ulibadilika kabisa , ila hali ya kuwa na roho ya kipadri ilinipotea kabisa , nilikuwa na moyo mgumu na muda wowote nilikua nikitamani hata mtu aingie kwenye kumi na nane zangu nimtolee hasira.
Siku mbili mbele baada ya kuujua ukweli ndipo nilipo pokea simu kutoka kwa mheshimiwa ndalu , jambo ambalo hata mimi limenishangaza nakumbuka mara baada ya kupokea simu alianza na kicheko .
“ hahahaha .. hahaha .. bwana henry swali langu naomba sasa ulijibu , je unamwamini bendera ?” hio ndio ilikuwa sauti yake baada ya kupokea , ilikuwa ni sauti iliokuwa ikiashiria ushindi
“mheshimiwa mheshimiwa “ ni sauti iliomshitua mheshimiwa bendera kutoka kwenye kumbukizi yake ya miaka ya nyuma kumbukumbu ambayo iliayabadilisha maisha ya mheshimiwa henry kabisa .
Madam wema aliwezaje kuyaficha maisha ya wanae wote wawili yaani janeth na mtoto wa bruno , mtoto wa bruno yuko wapi , ni kweli mheshimiwa bendera alilazimishwa kuchukua fomu ya uraisi tuendelee wapenzi wasomaji
*******
“Uhalisia wa mambo” . Moja ya watu maarufu ambao wanaelezea maana ya uhalisia wa mambo ni bwana dean radin , , kupitia kitabu chake cha ‘ entangled mind’ yaani akili iliokwama bwana huyu anajaribu kuonesha utofauti kati ya zama zilizopita na zama za sasa (past reality and new reality) katika mwanzo kabisa wa kitabu chake anasema kwamba neno ukweli limekuwa ni jambo la kuwahangaisha wana historia wengi mno duniani na yote hayo ni juu ya ukweli wa zamani na ukweli wa zama za sasa , huku wengi ya wana historia hao wakishindwa kujua ni kipindi gani kweli hio ya zamani ilibadilika , kila mmoja anasema ukweli ulibadilika mwaka Fulani lakini mwingine pia anasema ukweli ulibadilika mwaka Fulani , lakini katika mwenendo mzima wa kubadilika kwa uhalisia kwa ujumla wake , ni wachache sana ambao waliweza kushuhudia ukweli huo ukibadilika huku wengi wao wakishindwa kujua , na hata wale ambao waliweza kujua waliishia kunong`ona wao kwa wao wakishindwa kuyasema yale ambayo wanayaona ,hizi ndio zama za sasa , yaliokuwa zamani sio ya sasa , mambo mengi yamebadilika kuanzia mitazamo ya kimaisha mpaka tabia binafsi za watu haziendani na zile za zama zilizopita , zama za sasa yapo mengi watu wanafichwa , wengine wanaoficha wanayaficha na yanakuwa ni mambo ambayo hayajulikani kwa kipindi cha muda mrefu,huku wale ambao wanaujua ukweli juu ya dunia inavyoenda ndio wanazidi kutufanya kutokujua uhalisia wa mambo , U-97(UMOJA NAMBA TISINI NA SABA ) , naam ni umoja namba tisini na saba tunaendelea .
*****
Merina alikuwa mwenye mawazo mno juu ya hatima ya maisha yake , kwani umri aliokuwa nao alikuwa akitamaani na yeye kuwa na furaha kama watu wengine walivyokuwa na furaha , wengi wao wakiwemo baadhi ya marafiki zake walikuwa wakiyafurahia mapenzi lakini yeye japo ya kuwa mzuri na mungu kumbariki na uzuri wa ajabu lakini alikuwa hana furaha kabisa na hajawahi kujua furaha ya penzi , na hio ni kutokana na kungojea penzi la mtu ambae hajulikani alipo yaani damiani , pasipo kujua kwamba mtu anaemuwaza na kumuota usiku na mchana ni mtu ambae amekutana nae Zaidi ya mara moja pasipo kumjua .
Siku hio wakati kulivyokucha hisia zake zilikuwa zikimwambia kwenda kwenye kampuni ya mtoto wa bruno , aliamini huenda bwana huyo alikuwa na ukaribu na damiani , huenda pia angekuwa na taarifa iliokuwa ikimuhusu damiani , kwani kama alivyosikia kutoka kwa zakayo katika ripoti yake ya kumtaja damiani kuwa na nyaraka ambazo zilikuwa za bruno basi kuna uwezekano bwana huyo akawa amekutana na damiani .
Asubuhi na mapema tu gari yake ya kifahari ilionekana ikitoka eneo hilo la nyumbani kwake ikielekea upande wa Morocco , ni muda wa dakika arobaini tu alikuwa ndani ya jengo la kampuni ya NLT na ile anaingiza gari maegesho , huku upande wa kuingilia alionekana bwana Stephan mzungu feki akiingia na gari yake ya BMW X8 na kwenda kulisimamisha katika maegesho na kwa spidi ya haraka bwana huyu alitoka na kuzunguka upande wa mwingine na kumfungulia proffessa janeth mlango , proffessa mrembo kuwahi kutokea ndani ya taifa la Tanzania , yote hayo wakati yakifanyika mwanadada mrembo Zaidi ya janeth yaani merina alikuwa akiangalia wawili hao, wa kwanza kumuona merina alikuwa ni damiani , alijikuta akichanua tabasamu mno baada ya kumuona mwanamke huyo mbele yake kitendo ambacho kwa janeth alikishuhudia wakati akiwa bize na simu yake na ilimbidi ageuke kuangalia mbele ni nani huyo kamfanya mzungu huyo feki kutabasamu kwa namna hio , na hapo ndipo alipokutana na mwanadada ambae kama ni kukutana nae alikutana nae mara moja , alikiri mwenyewe kuwa merina alikuwa mzuri mno Zaidi yake .
“habari za asubuhi stephano “.
“ salama merina hali yako vipi “
“ hali yangu nzuri tu namshukuru mungu , mambo poffesa”
“ poa za kwako “
“ salama “
“ sasa stephano nimefika hapa nina maongezi kidogo na wewe “
“ hakuna shaka , nadhani tuongozane mpaka ofisini “.
Basi waliongozana kuelekea ofisini huku stephano akitangulia akifatia merina na wa mwisho walikuwa ni janeth aliekuwa akimwangalia merina kwa wivu , kuna dalili mbaya aliziona kabisa za kuzidiwa kete , maana hata yeye ni siku chache japo kwake aliziona nyingi za kuwa na hisia na kijana damiani ama mzungu feki bwana stephano lamberk , janeth hata yeye alikuwa akimpenda damiani kama damiani na sio stephano , tokea siku aonane nae nchini china , hisia zake juu ya kijana huyo zilikuwa juu na hata pale alipoambiwa kuwa anatakiwa atoke nchini chna na kurudi Tanzania kwake hakuwa na kipingamizi kwani aliona ndio atapata wakati mzuri wa kuwa na ukaribu na bwana damiani .
Basi hatimae walifika ofisini na damiani ama stephano alimkaribisha merina na merina akaketi , huku upande wa ofisini kwa janeth moyo wake ulikuwa juu juu mno , wivu ulimshika , hata yeye mwenyewe alikuwa akijishangaa kwanini kapatwa na hali hio , alitamani kujua ni kipi amacho damiani anaongea na merina , kila akikumbuka uzuri wa merina hali yake ilikuwa mbaya mno .
“ karibu sana merina , kwanza sikupata nafasi ya kukushukuru kwa kuiamini kampuni yetu na kununua hisa “
“ huna haja ya kunishikuru sana stephano mimi nawekeza sehemu ambayo naamini lazima nitapata faida “
“ hahahaha,… hizo ndio kauli za wafanya biashara bwana , anyway karibu sana , ulisema unajambo wataka kuongea karibu “ aliongea damiani huku akiwa na shauku ya kujua ni kipi merina alitaka kuongea , lakini wakati huo pia kwa merina kila alivyokuwa akislikiliza sauti ya bwana huyo , ilionekana kuwa halisi kabisa katika masikio yake , yaani sauti ya damiani .
“ kwanza ni kupe pole kwa kifo cha baba yako stephano “
“ asante merina kishapita “
“ kuna jambo kidogo halipo sawa , sina dhumuni la kuyarudisha maumivu yako yaliopita lakini kuna jambo kwangu nataka kulifahamu “
“ jambo gani merina”
“ nafikiri unajua sababu ta kifo cha baba yako “
“ ndio nafahamu vyema “
“je unafahamu lingine Zaidi ukiachana na kifo cha baba yako”
“ hapana sifahamu merina , kwani kuna Zaidi “
“ ndio namaanisha watu waliohusika na kifo cha baba yako “
“ mhmh kwa kweli sijafahamu mpaka sasa ila nipo hapa nchini kwa ajili ya kulifatilia hilo “
“ Zaidi na maadui hao je unafahamu lingine lililotokea siku ya tukio “”
“hapana “
“kupitia tukio hilo mama yake mpenzi wangu aliuwawa kikatili na watu walimuua baba yako , lakini pia kutokana na tukio hilo mpenzi wangu amepotea mpaka sasa sijui alipo “
Mapigo ya moyo ya damiani yalikuwa juu mno , japo maswali yote ya merina alikuwa akyajibu kinafiki , lakini swala la kuitwa mpenzi na mwanamke huyo liliupeleka spidi moyo wake , japo alijua kuwa mwanamke huyo alikuwa akimpenda lakini hakuwahi kulifikiria swala hilo , kumbukumbu zilimrudisha mpaka siku aliokuwa ndani ya hospitali ya lushoto , mpaka kuja kuchukuliwa na suzzane, na akaunganisha na maneno haya ya merina ya sasa na hapo ndipo alipojua ni kweli mwanamke huyo alikuwa akimaanisha anachoongea .
“ pole sana merina , mpenzi wako alikuwa anaitwa nani “
“damiani “
“ najua swali hili linaweza kuwa nje ya mada lakini unaweza kuniambia ulikutanaje na damiani ??“
“nilikutana na damiani wakati alipokuja kwenye interview kwenye kampuni yangu ndio tulipo anana na mara ya mwisho tulionana lushoto “
“pole sana , kwa hio mpaka sasa unamsubiria damiani ?” bwana stephano au damiani alikuwa akiuliza maswali ya kijinga ambayo kwa merina hayakuwa na msingi , lakini kwake yeye yalikuwa na msingi .
“ndio , na ndio maana niko hapa , kwani sababu yote yanayotokea ni kwasababu ya bruno “
“ unamaanisha nini kusema ni sababu ya bruno ?”.
Swali hilo ndilo swali ambalo kidogo lilimpa wakati mgumu merina , hakujua ajibu kama uchunguzi wa zakayo wa juu ya bruno kuwa na mpango wa kumuua mama yake damiani au ajibu tofauti .
“ nataka kujua kama ushawahi kuonana na damiani “ kibao kiligeukia kwa damiani hakujua na yeye ajibu nini swali hilo , kwani hata yeye alikuwa akimpenda merina , japo hakuwa na uhakika na hisia zake , lakini alikiri kuwa kila amuonapo mwanamke huyo moyo wake ulikuwa ukijawa na mshituko , sasa mawazo ya aina mbili yaliitawala akili yake aliaminni akijibu hapana anaweza akamkatisha tamaa mrembo huyo na hatimae huenda mwanadada huyo angemove on na maisha yake , lakini wazo la pili aliona ni kumwambia ndio amekutana nae , kumpa moyo , lakini pia jibu lake lingedhalisha maswali mengine Zaidi , alijikuta akiwa kwenye dilemma ….
******
Ilikuwa ni siku ya saa nne kamili ndani ya hoteli ya kimataifa ya serena ndani ya ukumbiwa VIP , ndani ya eneo hili kulikuwa na watu waliokuwa wamezunguka meza , watu hawa hawakuwa wengine bali walikuwa ni wanachama wa umoja namba tisini na saba U-97.
Jumla ya watu hao walikuwa ni kumi na moja wengine wakiwa ni wafanyabiashara mbali mbali ambao walikuwa wamejiunga ndani ya umoja huo , waliokuwa maarufu zaidi alikuwa ni mheshimiwa ndalu , alikuwa ni mheshimiwa wa mambo ya ndani , kulikuwepo na mheshimiwa wa waziri wa fedha , alikuwepo waziri mkuu , mkuu wa TISS alikuwepo waziri wa mambo ya nje , alikuwepo kimbona na sam, hawa walikuwa ni baadhi ya wanachama wa umoja huu, japo kulikuwepo na wanachama wengi ambao walikuwa wapo ngazi ya chini ambao hawakuwa wakihusika katika vikao hivyo , wakiwemo wasanii mbalimbali ..
Siku hio ajenda kubwa iliotangazwa na kiongozi wa U-97 ndani ya Tanzania bwana Samuel saitoto ni juu ya kutambulishwa kwa muwakilishi mpya wa mpango zero , mpango ambao utakuwa katika kukamilishwa na muwakilishi huyo ambae alikuwa akisubiliwa kwani bado hajafika .
Lakini pia bwana Samuel saitoto alitoa maagizo ya kwamba ili utekelezaji huo uanze kila mwanachama anapaswa kusaini karatasi ambayo itapitishwa , lakini kabla ya kuendelea bwana mmoja hivi ambae alikuwa akijulikana kwa jina la abduli sheriff alinyoosha mkono na akaruhusiwa .
“ mheshimiwa umesema mpango zero , je tunaweza kufahamu ni mpango unao husu nini ?”
“bwana sheriif hata mimi sijafahamu juu ya mpango zero unahusu nini , ila kwakua mwakilishi anakuja basi inapaswa tuwe na subira”
Baada ya kusema hayo aliingia mwanadada mmoja mrefu maji ya kunde alievalia suti na kumnong`oneza sam na kisha alitoka .
“ jamani mwakilishi keshafika hivyo ni wakati wetu sasa kumpokea “ aliongea sam na mlango ulifunguliwa na akaingia bwana mmoja wa kizungu hivi mzee kidogo mwenye kijipara na kuoneshwa mahali pake na kisha aliruhusiwa kujitambulisha .
“ naitwa davinc Leonardo ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya INNOVA nimefika nchini kwa ajili ya kukamilisha mpango zero wa U-97”
ITAENDELEA
SEHEMU YA 50
MIAKA ISHIRINI NYUMA
ANASIMULIA MAREHEMU RAISI BENDERA KABLA YA KIFO CHAKE .
Katika maisha yangu sikuwahi kuja kuwaza kwamba nitakuja kupenda mapema , unaweza ukajjiuliza kwanini nilikuwa na mawazo ya namna hii , hio yote nilikuwa ni moja ya watu ambao nilikuwa nikijiona mgumu sana, marafiki zangu wengi walikuwa wakinitania kama mgumu na hio ni kutokana nilikuwa moja ya watu makaudhu sana , kwaniza msingi mpaka sekondari sikuwa na ile hali ya kutaka kuwa katika mapenzi kama wengine walivykuwa wakiwaza , kwani wengi waliona kwa miaka hio kuwa na wanawake ilikuwa ni fasheni , ila kwa upande wangu niliona ni kutokujielewa na nilijiwekea ahadi katika maisha yangu kwamba sitoruhusu hisia zangu kupenda mpaka nafika chuo kikuu .
Kipindi hicho nilipokuwa ndani ya shule ya songea boys nilikuwa moja ya wanafunzi wenye juhudii sana katika masomo , nilikuwa nikiongoza kila mtihani lakini licha ya yote nilikuwa headboy ndani ya shule hio , nilikuwa nikiheshimika kwanzia kwa wanafunzi mpaka kwa walimu na hio ilitokana na misimamo yangu isio yumbishwa , nilikuwa nikisema moja basi ni moja hakuna wakuweka mbili , hio ndio ilikuwa tabia yangu .
Richa ya yote hayo nilikuwa na ndoto kubwa mno ya kuja kuitimiza katika maisha yangu hapo baadae , ndoto hio ilikuwa ni kuja ku waraisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania , nilikuwa na msukumo mkubwa sana katika swala zima la kuongoza taifa hili , moja ya watu wangu ambao walikuwa wakinivutia katika maswala ya uongozi alikuwa ni mheshimiwa raisi wa awamu ya kwanza mheshimiwa nyerere na waziri mkuu Edward moringe sokoine , hao ndio walikuwa wanasiasa niliokuwa nikiwapenda .
Miezi kadhaa ya kidato cha nne ndio miezi iliobadilisha misimamo yangu yote niliokuwa nayo juu ya mapenzi , na nikawa moja ya watu waliokuwa wakiunukuu mstari kitabu anafahamika kwa jina la Charles dickens katika kitabu chake alichokitta jina la A tale of two cities (hadithi ya miji miwili ), moja ya msamiati wake uliokuwa ukisomeka kwa lugha ya kingereza “ I wish you know that you have been the last dream of my soul “akimaanisha kwamba ‘ natamani ujue kuwa umekuwa ndoto yam wisho katika roho yangu .
Basi habari ya hadithi ya miji miwili ikawa wimbo katika ubongo wangu , yote haya ni baada ya kukutana na msichana wema kutoka songea girls , msichana ambae nilimsaidia kufikisha malalamishi yake kwa mkuu wa wilaya juu ya kunyanyaswa na mwalimu rama wa shule hio ya songea girls , ule msemo wa becky Andrews katika kitabu chake cha forgotten night ,’ love has no time constraints ‘(mapenzi hayana muda maalumu ) ukatimia katika maisha yangu na hio yote ni baada ya kukutana na mrembo wema , kauzu mimi niliokuwa nikiwaona waliokuwa wapo kwenye mapenzi walikuwa wakipoteza muda na mimi nilikuwa nimeshikika vyema .
Mapenzi yangu kwa wema yalikuwa ni makubwa mno , lakini baade nilikuja kugundua kuwa wema alikuwa ni distractions(alikuwa akitoa kwenye mstari kimasomo ) na hio ni baada ya matokeo yangu kuwa mabaya mno kidato cha nne .
Ndipo nilifanya maamuzi ya kutokuonana na wema kabisa kwenye maisha yangu mpaka pale nitakapo maliza masomo yangu , kwani niliamini kama nitaendelea na penzi hilo basi ndoto zangu nyingi zingeishia njiani lakini kumbe kwangu ilikuwa moja ya kosa kubwa sana mabalo ningerudisha muda nyuma ningelisahihisha , kwani ni kosa lililonifanya niiumie sana moyo na hio ni mara baada ya kwenda nyumbani kwa wema na kumkuta akiwa mjamzito , kilichonifanya mpaka kufunga safari ya kwenda nyumbani kwa wema nibaada ya taarifa kutoka kwa rafiki yangu kuwa wema ni mjamzito na hapo na mimi niliona nikajioneee mwenyewe na ni kweli siku hio niliofika ndani ya mji wa singida ndipo nilipomshuhudia kipenzi changu wema akiwa mjamzito , mwanaume niliishia kutoa machozi tu na kugeuza njia na kurudi nyumbani , , njia nzima nilikuwa nikiwaza ahadi nilizowekeea na mwanamke huyo .
Baada ya miezi kadhaa ya maumivu niliamua kukomaa kiume , japo sikuweza kumsahau wema hata kidogo kwenye maisha yangu , nilikuwa nikimpenda sana mwanamke huyo na hata soma yangu chuoni ilikuwa ya taabu sana kipindi nilipokuwa sina mawasiliano na wema .
Maamuzi niliokuwa nayo kwa wakati huo ni kutaka kumuonesha wema kwamba alifanya kosa kubwa kuwa na mwanaume mwingine , huku akivunja kiapo chake cha kunisubiri , jambo nilillkuwa nimenuia kwa wakati huo ilikuwa ni kuwa raisi wa Tanzania jambo ambalo nilikuwa nikikumbuka kumwambia kabisa wema na kumwahidi kumfanya first lady , nia yangu ilikuwa kumkomoa tu .
*****
Bwana stephano lamberk jambo aliloona linafaa ni kumpa matumaini mrembo merina kumsubiria damiani .
“ nishakutana na damiani nchini china “.
“ what ! , unasema ukweli stephano ?”
“ ndio na muda si mrefu atafika nchini “
“ anafanya nini china , ashawahi kunitaja ?”
“ sijawahi kumsikia , ila ashawahi kuniambia kuwa anamwanamke anampenda ambae ashawahi kumsaidia akiwa kwenye hali mbaya mno , huku ikawa kama miujiza “
“ oooh my gosh, so muda wote ulikuwa unanichora tu stephano na maswali yako ?”
“ sikuwa nikikuchora ila nilitaka kuthibitisha kama kweli wewe ndie “
Merina alionekana kuwa na furaha mno juu ya jambo hilo , lakini wakati akiwa na furaha hio huku upande wa janeth alikuwa na hali mbaya , kwani proffesa huyo baada ya kuona wawili hao wameingia ofisini alitamani kujua ni kipi walichokuwa wakiongea , shauku yake ilimmsfanya atumie akili yake ya kiproffessa na hapo ndipo alipokumbuka kuwa anaweza kunasa sauti kwa kutumia network fiber ., hivyo alisikia kila kitu kilichokuwa kikizungumzwa na damiani .
Pande wa merina alijikuta akijawa na furaha mno , aliuliza kila aina ya swali ili mradi tu kukidhi shauku yake , jambo ambalo lilimfurahisha sana damiani .
*****
SEHEMU YA HAMSINI B
MIEZI SITA NYUMA
LAGOS -NIGERIA .
Ni ndani ya jiji la lagos Nigeria ndani ya makao makuu ya U-97 Africa yaliokuuwa yakifahamiaka kwa jina la ‘RITUAL OBSERVERS’ yaani waangalizi wa tamaduni , makao makuu yaliokuwa yakipatikana katika mtaa wa ‘ikorodu’ . katikati ya Nigeria na pembezoni mwa fukwe .
Ndani ya jengo hili ndio sehemu aliokuwa akipatikana kiongozi mkubwa wa U-97 yaani ‘level -6’ , na ndani ya eneo hilo la waangalizi wa tamaduni (ritual observers ) ndio alipokuwa akiishi , kiongozi huyu ambae hakuwa akifamika Zaidi ya kujulikana kwa cheo chake cha ‘level 6 alikuwa na mamlaka makuu ndani ya Africa , lakini pia alikuwa na mamlaka makuu ndani ya jumuia hii ya U-97 duniani kwani kiongozi mkuu kabisa alikuwa ni level one , huyu makao makuu yake yalikuwa ni ndani ya jiji la virginia marekani , sehemu iliokuwa ikiitwa ‘ Drome heaven class’ au darasa la mbingu la drome wafuasi wenyewe walikuwa wakiita hii sehemu kama D heaven .
Viongozi wakuu katika umoja huu ni wale waliokuwa wakitawala ndani ya mabara husika ukimtoa level one , wengine wote makao makuu yao yalikuwa katika mabara kwa mfano Afica makao makuu yake yalikuwa ndio ndani ya jiji la lagos Nigeria ndani ya mtaa wa ikorodu sehemu iliopewa jina kama ‘ritual observers’ bara la Australia lilikuwa likitawaliwa na level 04 huyu makao mako yake makuu yalikuwa ndani ya jiji la syndney sehemu moja iliokuwa ikijulikana kama ‘Reveletion park’ au kwa Kiswahili hifadhi ya ufunuo , bara la ASIA makao makuu yake yalikuwa ndani ya Singapore , makao makuu yake yalikuwa yakifahamika kwa jina la ‘soul classifier lab ‘ yaani maabara ya kupanga roho na hapa kiongozi wake alikuwa ni level 03,, kwa bara la amerika yaani kusini na kaskazini makao makuu yake yalikuwa ndani ya D heaven na kiongozi alikuwa ni level 05 , bara la ulaya makao makuu yake yalikuwa ujerumani ndani ya mji wa berlin sehemu moja iliokuwa ikifahamika kwa jina la mitte , makao makuu yake yalikuwa ya kifahamika kwa jinal la ‘Arc trust lord ‘ au tao Imani bwana hapa kingozi wake alikuwa ni level 02 .
Huo ni mchanganuo uliokuwa umetokana na taarifa aliotoa bwana bruno lamberk miaka michache nyuma ,taarifa aliokabidhiwa kwa raisi bendera .
Basi tukirudi sasa kwenye makao makuu ya U-97 lagos ‘ritaul abservers ‘ siku hio kulikuwa na kikao kizito kilichokuwa kikifanyika , kikao hichi kilikuwa kikihusu maendeleo ya umoja namba tisini na saba ndani ya mataifa ya Afrika na hali kinzani kwa kuenea kwa umoja huu , watu ndani ya eneo hili wote walikuwa wamevalia suti na ndala au kanda mbili rangi nyeupe na soksi nyeupe mikononi huku wakiwa wamekaa kwenye viti flani hivi aina ya vigoda lakini vilikuwa na foronya , upande wa mbele wa jengo hilo , sehemu ambayo ilikuwa ni kama ‘madhabahu’ kuu ya waangalizi wa tamaduni kulikuwa na kitu kama spika , spika ndogo ambayo ilikuwa ikitoa sauti ya maagizo kutoka kwa level 06 kwani hakuwa akionekana .
“hali kinzani ya umoja wetu ndani ya bara hili hairidhishi kwa ujumla wake , tunataka umoja huu uenee sio kwa viongozi wa juu tu tunataka mpaka katika jamii ya kawaida ya wananchi wawe wanafata tamaduni zetu “.ilisika sauti ya level 6
“ nimewaita hapa kutokana na taarifa muhimu juu ya mpango zero utakao tekelezwa ndani ya taifa la Tanzania , lakini mpango huu ili ufanikiwe kuna hali kinzani ndani ya taifa la Tanzania , hali ambayo inaweza kuchelewesha mpango wetu kutimia , hivyo kuanzia sasa , majina yafuatayo yamewekewa alama nyekundu kwanzia sasa ndani ya taifa la Tanzania , na majina hayo ni stephano lamberk , wema sufiani na janeth bendera na sabi mboneche , kazi hio nataka imalizike mapema na ‘submissive quest’oda wakilishi ipelekwe ‘soul classifier lab ‘.” Ilikuwa ni sauti ya level 06 akitoa maagizo sauti ambayo ilikuwa ni nzito kweli , kila mtu hap ndani ilikuwa ni ndio ndio tu hakuna ambae alikuwa na uwezo wa kusema hapana .
“mpango zero utafanikishwa na kampuni ya INNOVA “.
Kikao hicho kilifanyika kabla ya death notice kutumwa Tanzania na kumfikia mwakilishi wa umoja wa U-97 bwana Samuel saitoto
ITAENDELEA
SEHEMU YA 51
Ndani ya kikao alicho itisha sam hakuna mshirika ambae alipata kuambiwa ni nini maana ya mpango zero , hakuna alieweza kujua Zaidi ya kuambiwa kuwa watoe ushirikiano kwenda kwa kampuni ya INNOVA.
Upande mwingine baada ya damiani kuongea na mwanadada merina na kuona mwanadada huyo kufurahi kwa kile ambacho amemwambia , siku hio kuna wazo ambalo damiani alikuwa nalo kichwani .
Bwana huyu japo alikuwa amepewa mali nyingi na bruno lakini kisasi chake kilikuwa pale pale , siku hio alikuwa akiwaza mtu ambae alikuwa akiwasiliana nae mara kwa mara kabla hajaenda thailland na baada ya kwenda thailland , mtu ambae alikuwa akimpa maelekezo ndio mtu ambae alikuwa akikisumbua kichwa chake .
Siku hio aliwahi kurudi kweli ndani ya nyumba yake iliokuwa ikipatikana eno la makongo juu , , kazi zote za usimamizi wa kampuni alimwachia mwanadada janeth na Rebecca kwa ajili ya kuendeleza majukumu ya kampuni , kwani ni muda mchache sana walikuwa nao mpaka tarehe ya ufunguzi wa kampuni hiyo utakapo timia , ufunguzi ambao ulikuwa ukifanyika wiki moja mbeleni .
Damiani mara baada ya kufika ndani ya nyumba yake hio alisogea mpaka upande wa ‘safe box’ na kisha alitoa bahasha , bahasha ambayo ilikuwa ni ile aliopewaga na bwana bruno miaka kadhaa nyuma kabla ya kifo chake na kabla ya damiani kwenda nhini thailland , damiani aliikumbuka bahasha hio siku hio , na jambo lililomfanya akumbuke mengi juu ya bahasha hio ni mara baada ya kukutana na mwanadada merina , alikiri kwamba alikuwa akimpenda mwanadada huyo , kwani furaha aliomuona nayo merina muda mchache uliopita ndio furaha ambao alihisi katika mtima wake , lakini kinachomuumiza moyo lilikuwa ni jambo la kumdanganya mwanadada huyo ya kwamba damiani anakuja muda si mrefu kwa ajili ya kukutana na merina , aliona kuwa huo ni mtego kwake na lazima merina angefika baada ya muda kutaka kuunganishwa na damiani na yeye kwakua ndie damiani , aliona kuna ugumu wake kwani alikuwa na kazi ngumu sana mbele yake ya kuwatafuta maadui wa bruno ambao anaamini ndio waliokuwa wamehusika na kifo cha mama yake .
Baada ya kufungua bahasha hio , karatasi moja aliochukua ni ile ambayo ilikuwa na kama ramani yenye sehemu ambazo zilikuwa zimewekewa alama nyekundu , aliangalia ndani ya ramani hio ili kujua ni kipi bwana bruno alikusudia mpaka kumpa hio karatasi .
Aliangalia sana , lakini kila alipokuwa akipekecha kichwa chake , akili yake ilikuwa ikikwama , alijua kabisa hio karatasi inaonesha ramani , lakini muundo wa ramani hio haukuweleka kama ni ramani ya sehemu gani , hilo ndio tatizo la kwanza kwake alilokuwa nalo kwa wakati huo na aliona alitakiwa kulitafutia ufumbuzi kwani aliamini kuna taarifa ya kuitafuta .
Baada ya kuona jambo hilo limeshindikana , alitoa ile flash disk na kisha alichukua laptop yake na kuanza kuangalia video ya bruno , ambayo kama ni kuiangalia video hiyo , basi hio ilikuwa ni mara ya pili ama ya tatu , kwani mara ya kwanza alikumbuka kuwa aliiangalia ndani ya jiji laa lushoto akiwa nyumbani kwao siku chache baada ya kifo cha mama yake .
Aliangalia video hiyo kwa umakini kama amtu ambae alikuwa akijaribu kutafuta kitu flani , na hapo kitu hicho alikiona na kuisimamisha ile video na kuangalia mkufu ambao ulikuwa ukionesha kwenye video hio
“ NADHANI UNAANGALIA VIDIEO HII HUKU NIKIWA SIPO TENA DUNIANI , INAWEZEKANA SIKUJUI NA TUMEKUTANA MUDA MFUPI , HILO HALIJALISHI ILIMRADI ULICHONACHO MIKONONI MWAKO KIPO SALAMA , DHUMUNI YA KUREKODI VIDIO HII NI KUKUAMBIA KWAMBA NAFURAHI KUKUAMBIA KUWA WEWE NDIO MRITHI HALALI WA MALI ZANGU ZOTE NINAZO MILIKI , LAKINI ILI KUMILIKI MALI ZANGU HIZO KUNA HATUA ZA KUPITIA NA ILI KUJUA HATUA HIZO NI LAZIMA UWE JASIRI , MTAFUTE MTU MWENYE NAMBA O713**** ATAKUPA MAELEKEZO YA KILE UNACHOTAKIWA KUFANYA , MWISHO MTAFUTE MTU MWENYE HIKI KIDANI ( ALIKIONYESHA ) KISHA MUONYESHE KIDANI KILICHOKUWA KWENYE MKEBE HUYO ATAKUWA NI MWANANGU NA NAOMBA UKIFANIKISHA HILO CHUKUA KIDANI HICHO NA KITAKUWA UFUNGUO NA KINAELEKEZA ENEO NILILOACHA HAZINA YANGU NA HATI INAYOKURUHUSU KUMILIKI MALI ZANGU ZOTE.”
“ mtoto wa bruno , kidani “ yalikuwa ni maneno ya damiani mara baada ya kuangalia vidio hio , kuna jambo lilimjia akilini alihitaji kumshirikisha mtu juu ya swala hilo , lakini kwa wakati huo hakuona mtu sahihi kwake ambae angemshirikisha .
“ nampata wapii mtoto wa bruno ?” ni swali la kwanza ambalo lilikuwa ndani ya kichwa chake , damiani hakuwa na ujuzi wa aina yoyote ule wa maswala ya kumtafuta mtu kwani yeye alikuwa na elimu ya uhasibu elimu ambayo haikuwa na msaada kwenye shida yake aliokuwa nayo kwa wakati huo , hapo ndio akili yake ikaanza kuload kwa nguvu na jina la sabi liliibuka kwenye kichwa chake , aliamini sabi anaweza akamsaidia katika shida yake , lakini swala la sabi kufanya kazi ikulu hakuwa na maelezo nalo , kwani ni kipindi cha muda mrefu hajawasiliana na sabi na hakujua kwa wakati huo sabi alikuwa upande wa nani , hakujua kuwa sabi alikuwa upande wa serikali ambayo damiani aliamini ndani ya serikali hio ndio kuna maadui zake , ama sabi yupo upande wake alama ya kuuliza iliibuka kwenye kichwa chake , alishindwa kumtafsiri sabi kwa wakati mmoja .
Jambo lililomjia akilini kwa wakati huo ni kupiga namba kwa hatua alizo pitia siku za nyuma alivyofika ndani ya jiji la tanga , aliamini huenda angeweza kupokelewa , alitoa simu yake na kisha alinakiri namba zile na kisha alianza kupiga , lakini bahati mbya ni kwamba namba ile haikuwa ikipatikana alichukua namba zingine zile alizozigundua kuwemo kwenye flash kipindi akiwepo chini thailland na rafiki yake sabi na kisha alizijaribu lakini pia namba hizo hazikuwa zikipatikana , kichwa kilianza kupata moto , hakujua ni kwa namna gani anaweza akalitatua tatizo alilokuwa nalo , alikuwa akitaka kujua ni mtu gani aliekuwa akiwasiliana nae mara kwa mara mpaka kumpa maelekezo ya kufika thailland na mpaka kufika nchini china na hatimae kukabidhiwa hisa asilimia ishirini na tatu za kampuni ya ya huawei .
“ngoja DREAMER T inaweza kunisaidia “ aliongea damiani na kisha alitoka ndani ya chumba chake akiwa na ile karatasi ambyao ilikuwa na ramani na wazo lake la kwanza lilikuwa ni kwenda kwenye kampuni yake ili kuingia kwenye chumba cha dreamer T.
****
Upande mwingine zakayo ama jasusi wa kimataifa alikuwa kwenye kazi yake kama kawaida , alikuwa aktaka kujua ni nani alikuwa akimsaidia kijana damiani mpaka kufika nchini thailland , siku hio alikuwa nje kabisa ya ubalozi wa kenya akiwa na bahasha yake mkononi , alifika getini na kujitambulisha kwa kutoa kitambulisho chake na mlinzi wa getini alikiangalia kisha alimruhusu kupita .
Baada ya kufika ndani ya eneo hilo la balozi ya kenya , aliingia mapokezi na kupokelewa na mwanadada mmoja hivi mweusi na kwa haraka haraka bwana zakayo aligundua mwanadada huyo alikuwa mkenya , kwani rafudhi yake ya kiswahili ilidhhirisha .
“ how may i help you “ ni kusaidie nini ?”
“ naahitaji kuoanana na balozi “
“ una miadi nae “
“ hapana ila ninashida ya muhimu mno “ aliongea zakayo huku akimpa mwanadada huyo kitambulisho chake na mwanadada huyo alimwangalia zakayo kama kumsanifu na kisha akatabasamu .
“ subiri kuna wageni yupo nao kwa sasa “
“ hakuna shida “
Baada ya kusubiri kwa madakika kama arobaini hivi ndipo wanaume wawili wa kizungu aliwaona wakitoka ndani ya ofisi ambayo aliamini kuwa ilikuwa ni ya balozi .
“ unaweza kwenda kaka balozi anakusubiri “ aliongea mwanadada huyo baada ya kuweka simu yake ya mezani chini na alionesha alikuwa akimtaariafu balozi kuhusu ujio wa bwana zakayo jasusi asie fahamika kwamba ni jasusi yaani ‘undercover agent ‘.
“ karibu bwana zakayo “ aliongea bwana huyo kwa kutabasamu baada ya zakayo kujitambulisha kwake .
“ asante mheshimiwa , nina shida ilionileta hapa ya kiusalama , kuna mtu namtafuta , lakini katika uchunguzi wangu wa awali nimegundua mtu huyo ashawahi kupokea msaada kwako “
“ unasema mtu ashapokea msaada kutoka kwangu , je mtu huyo ni nani ?” aliuliza bwana njoroge na zakayo hakuwa na presha , alitoa baadhi ya picha za daamiani na kisha aliziweka mezani na kumfanya balozi huyo atoe macho .
“ nafikri mheshimiwa balozi unatambua mtu huyo “ aliongea zakayo na balozi aliinua picha moja kama mtu ambae alikuwa akiiangalia kwa umakini hivi na kisha alitingisha kichwa kuwa hamfahamu .
“ sijawahi kumuona kabisa , huyu ndio unaesema amepata msaada kutoka kwangu ?”
“ ndio mheshimia , “ aliongea zakayo na kisha alitoa picha nyingine na kuiweka mezani na balozi aliichukua na kuiangalia na hapo ndipo aliposhituka , kwani picha hio ilikuwa ikimuonesha balozi akiwa na damiani wakiwa uwanja wa ndege .
“ mheshimiwa nadhani umemsahau kidogo , nadhani kupitia picha hio utamjua mtu huyo “ aliongea zakayo kwa kujiamini kabisa , huku akiamini kwamba wakati huo alikuwa amempata pazuri balozi huyo na asingechomoka kwenye mtego wake .
“ wewe ni nani ?”
“ nadhani nishajitambulisha mheshimiwa kwako “. Aliongea zakayo na kumfanya bwana njiroge apumue kwa nguvu .
“ nilijua tu haya yatatokea , na nakiri kweli nilimsaidia mtu huyu kwenda nchini kenya ., lakini sikuwa nikimfahamu “
“utampelekaje mtu kenya pasipo kumfahamu “
“ niliombwa kufanya hivyo na mimi nilifanya “.
“ uliombwa na nani mheshimiwa ?”. swali hilo lilionekana gumu kutoka kwa bwana njiroge kwani hakutaka kulijibu kiurahisi .
“ na first lady ?”.
“ first lady ? , unamaanisha mke wa raisi “.
“ ndio alienipigia simu kuwa kuna kijana anaomba nimsaidie kumfikisha kenya”.
“ wewe una mahusiano gani na mke wa raisi madam wema “ aliuliza zakayo kwa mhamaniko kwani mpaka hapo alikuwa na mshangao kweli .
“sina mahusiano yoyote na mheshimiwa zaidi ya kibiashara na yeye ni mke wa raisi “
“ swala hili raisi alikuwa akilijua? “
“ kwanzia hapo sijui “
“ okey nashukuru sana mheshimiwa kwa ushirikiano wako “
“ hahahahaha ,... agent z nakujua vyema ndio maana nimekusaidia kujibu maswali yako kwa sheria za balozi huna mamlaka ya kunihoji pasipo kibali “ aliongea balozi na kumfanya zakayo ashangae .
“ unanifahamu kivipi ?”
‘ nakufahamu kwa muda mrefu sana na hata ulipo ingia nilikujua kabla hata hujajitambulisha “
“ ndio unanifahamu kivipi ?”
“ nakufahamu kuwa wewe ni ‘undercover agent’ wa TISS ambae kwa sasa upo huru kufanya kazi mwenyewe na najua kazi hii ni nani unamfanyia “ aliongea balozi huyo na kisha aliinuka na kutoa picha na kuziweka mezani na hapo ndipo zakayo alishangaa kwani picha hio ilikuwa ni picha ikimuonesha akiwa ndani ya eneo la serena akiagana na mheshimiwa matinde .
“ ulionekana ulikuwa ukitufatilia ?”
“ndio nilihitaji kujua mambo kadhaa kuhusu wewe kwani kuna kazi pia nataka nikupe “ aliongea njoroge na kumfanya zakayo apumue kidogo .
“ kazi , kazi gani mheshimiwa “
“ kazi ilio ndani ya utaalamu wako , hakuna kazi nyingine zaidi ya hio “
“ naomba uiweke waza juu ya hio kazi “.
“ nataka unifanyie uchunguzi wa kumjua bwana stephano lamberk ni nani “
“ stephano lamberk ?”
“ ndio “
“ kwanini unaitaji kumjua stephano lamberk ??“
“ nitalijibu hilo siku ukija na ripoti kamili ya stephanno lamberk ni nani “ aliongea njoroge huku akionesha kutabasamu kabisa , na zakayo hakutaka kukaa tena ndani ya ofisi hio kwani aliaga na kisha aliondoka .
Baada ya kuingia kwenye gari lake , alijikuta akivuta pumzi , na mawazo kadha wa kadha yalianza kupita ndani ya kichwa chake , wazo la kwanza ni la mke wa raisi kumsaidia damiani , lakini wazo la pili likawa ni juu ya sababu ya bwana njiroge kutaka kumjua stephano lamberk bila kuweka sababu ya kwanini anataka taarifa ya bwana huyo .
“ huyu stephano , kila mtu anataka kumjua , ni nani huyu ?” ni swali lililomfikirisha jasusi huyu wa kimataifa ‘ agent z’ .
Upande mwingine baada ya damiani kutoka ndani ya nyumba yake aliingia barabarani na kisha kuendesha upande wa kuelekea mwenge huku akidhamiria kurudi ofisini kwani kuna jambo lake alikuwa akihitaji kulifanyia uchambuzi . alitoa simu yake akijaribu kupiga namba ya janeth kumuuliza sehemu alipo na hap ndipo alipo ambiwa kuwa ashatoka kazini na sasa yupo posta .
Baada ya kujibiwa hivyo alimwambia kuwa’ basi ‘ janeth kwani alidhani kuwa alikuwa ofisini .
Wakati akiwa anaendesha gari yake upande wa nyuma kulikuwa na mwanadada hatari sana , mwanadada huyu tulimuoana miezi kadhaa ndani ya jiji la thailland , hakuwa mwingine bali alikuwa ni jasusi wa CIA mwanadada marie , alikuwa akimfatilia damiani hatua kwa hatua , kona kwa kona , na siku hio alionekana kuna jambo alilokuwa amelidhamitia kwenye roho yake .
ITAENDELEA
SEHEMU YA 52
Rafaeli aliendesha gari yake pasipo kujua kuwa anafatiliwa mpaka alipo fika ndani ya kiwanda chake , baada ya kuingia ndani ya kiwanda hichi alinyoOsha moja kwa moja mpaka kwenye jengo ambalo ni la utawala na kisha aliingia kwenye lift , na kubonyeza namba kumi na moja na liFt ilianza kushuka chini mpaka kwenye floor iliokuwa na taa za blue , alitumia taratibu zote za kupita katika ‘ four layer zone of protection ‘ na kuingia ndani ya chumba cha DREMER T
“ welcome again mister damiani rabani in dreamer T “ karibu rabani katika chumba cha dreamer T .
“ thank you “ alijibu na kisha alitoa ile karatasi yenye ramani na kisha aliifungua kwa mbele na kuishikilia vizuri .
“ i want to know what this map means ,(nataka kujua ramani hii inamaanisha nini) “
“please wait for our T recognition system to proccess your request (tafadhari subiri kwa mfumo wetu wa utambuzi kuiangalia “)
“your request has been succesfull , this map is coding system known as GEO SCAD , is a system used to hide location information , discovered in 2011 by SCAD (ombi lako limefanikiwa , hio karatasi inamfumo wa kodi unajulikana kwa jina la ‘GEO-SCAD’ ni mfumo unaotumika kuficha taarifa uliogunduliwa na kampuni ya SCAD “ danieli alijikuta akishangaa jibu hilo .
“can i identify the information hidden in the map ?( naweza kufahamu taarifa hio iliofichwa kwenye hio ramani “)
“ SCAD company after discovering this kind of encryption , they did not disclose publicly on how to interpret the information for security reason, thus its beyond T abililty ”( kampuni ya SCAD baada ya kugundua jinsi ya kuficha aina hio ya taarifa hawakutaka kutangaza hadharani namna ya kutafisiri taarifa hio , hivyo ni jambo lilolopo nje ya T)
“ shit” tusi
“thank you mister damiani , do you need more help for T to help you (“asante mister damiani unahitaji msaada mwingine damiani ?”)
“ hapana asante “ aliongea huku akitoa ndani ya chumba hicho , japo hakupata msaada anaotaka , lakini aliona kuna mwanga baada ya kuambiwa kuwa hizoo ni kodi .
Hapa mtu anaeweza kunisaidia , ni janeth , huyu ni mtaalamu anaweza akawa na ufahamu na hio GEO –SCAD “ aliongea huku akitoka mpaka nje na kuondosha gari yake , na wakati anaondoka hapo , gari aina ya toyota clown nyeupe ilimuungia kwa nyuma , ni gari aliokuwa amepanda mwanadada marie , alikuwa akimfatilia stephano lamberk kila hatua , alitaka kujua ratiba zake zote , ili akimfanyia tukio lifanikiwe kwa asilimia mia moja , damiani aliendesha gari yake na kuingia bagamoyo road , alitembeza gari mpaka mbezi beach na kisha alikata kona na kuingia njia ya mkato iliookuwa ikielekea makongo juu na alikuja kusimamisha gari yake kwenye get la nyumba yake ambapo sekunde kadhaa geti lilifunguka na kisha aliingiza gari yake .
Baada ya kufika ndani hakutaka kukawia na jambo lake kichwani , kwani alitoa simu yake na kisha alimpigia janeth simu , na mwanamke huyo alimwambia analala kwa rafiki yake masaki .
“ kuna picha nakutumia nataka unisaidie kuitambua “
“ sawa “
Alikata simu na kisha alipiga nusu karatasi ile picha kwa tahadhari kwani hakuwa akimwamini sana janeth na kisha alimtumia .
“ hii ni ramani ya GEO –SCAD i can tell just by looking” aliongea janth baada ya dakika tano ya kutumiwa ile picha .
“ unaweza kuitafsiri ?”
“ siwezi sina elimu yake ya kutosha , ila kwa ninavyo jua unaweza ukawasiliana na SCAD wakakusaidia “
“ inawezekana?? “
“ ndio mara nyingi inafanyika hivyo , ukitaka taarfa ya eneo husika kuificha kwa mfumo wao wa kodi , unaingia kwenye websitie na unawasiliana nao kupitia email , hivyo hivyo ukitaka tafsiri yao “
“ okey asante “ aliongea damiani haraka haraka na akaingia kwenye website ya SCAD alipata email na kisha alituma ujumbe na dakika kama tatu hivi ujumbe wake ulijibiwa na aliambiwa aweke attachment(hio karatasi) aliipiga picha na kisha akatuma na akaambiwa asubirie dakika chache kwa ajili ya majibu .
Huku upande wa nje mwanadada marie baada ya kuhakikisha kazi yake imeenda sawa alitoa gari yake na kundoka.
*****
Mke wa raisi madam wema alikuwa kwenye mawazo makali sana , alikuwa muda wote akifikiria usalama wa mwanae janeth , kwani aliaminii watu waliofanikisha tukio la kumteka lazima wangemfata tena , kwani aliamini waliokufa kwenye tukio walikuwa wakimfanyia mtu kazi aliewatuma kwa ajili ya kumteka mwanae na jambo hilo alikuwa akiliwazia sana , alikuwa yupo chumbani kwake akiwa amepumzika , hakujua ni jambo gani kwa wakati huo alifanye ,alichofanya ni kumpigia simu abasi huku akimpa maagizo ya kumlinda janeth kila hatua na sehemu anayo enda .
Alijikuta akianza kuwaza mambo yanavyo enda ndani ya nchi ya tanzania , kumbukumbu nazo hazikumuacha salama kwani alijikuta akikumbuka miaka yake ya ujana .
*****
Ni mwaka ambao nilijifungua mtoto wa kike ndani ya hospitali ya kiomboi pale singida , na kurudi nyumbani na mpaka kuonana na bruno baba wa mtoto wa kike niliekuwa nimejifungua .
Siku hio nilikuwa na hasira mno na hio ni mara baada ya kukutana na bruno na kuniambia maneno ambayo hayakuwa yakieleweka katika kichwa changu , nilijikuta nikimchukia sana mwanaume huyo .
Nilimlaumu kwa kuniambia maneno yale ya kwamba hakuwa akimtaka mtoto tena , jambo hilo liliniuma kweli nilimwangalia mwanangu aliekuwa kwenye mikono yangu akinyonya , nilijikuta nikiwa katika wakati mgumu mno , sikujua kwa wakati huo nifanye nini .
Wakati nikiwa nawaza mara alikuja rafiki yangu mmoja hivi niliekuwa nikifanya nae kazi singita , siku hio alikuja kunisalimia alikuwa ni rafiki yangu kweli .
Baada ya kufika alifurahi sana kumuona mtoto wangu na kumsifia kwakuwa mzuri , na hata mimi pia nilikiri kuwa mtoto wangu huyo alikuwa mzuri kweli na nywele zake za kizungu .
Basi baada ya maongezi ya kimbea ya hapa na pale na habari za kazini ndio hapo rafiki yangu huyo alivyoniambia kuhusu wagenia aliokutana nao wanatafuta mtoto wa kumlea (adoption ) huku kazi hio akiwa amepewa rafiki yangu huyo aliekuwa akifahamika kwa jina la bahati .
“ rafiki yangu hii ni bahati , waliniambia watanipa pesa nyingi kama nitawatafutia mtoto “ aliongea bahati
“ sasa huyo mtoto utampatia wapi ?”.
“ nataka niende vituo vya kulelea watoto , pia nikikosa mtoto huko naenda hata kuiba hospiutalini pacha mmoja na wapelekea “ aliongea kwa usiriasi jambo ambalo lilinifanya nicheke .
Basi tulipiga stori pale za hapa na pale na kisha aliaga na kuelekea kwao , hakuwa akiishi mbali na kwetu ni kijiji cha tatu tu .
Basi siku ya pili kupita baada ya kukutana na rafiki yangu bahati , siku hio nilikuta nikitoka clinic ya kwanza kwa ajili ya mwanagu kuchomwa sindano ndipo nilipo kutana na rafiki yake bendera , kumbuka kipindi hicho sikuwa na mawasiliano kabisa na bendera na sijawahi kabisa kuonana na mtu hata anaefahamiana na bendera , hivyo sikujua kwa wakati huo bendera alikuwa wapi au anafanya nini .
“johson , niliita kwa mshangao mara baada ya kumuona “ na yeye alshangaa na kima mtu aliekuwa akitafuta kumbukumbu na hapo ndipo alipo tabasamu na kuniita jina langu .
“ za masiku ?”
“ “ nzuri wema “
“ naona mwenzetu ushaitwa mama tayari “
“ hahaha ndio , kumbe unaishi hapa singida? “
“ hapana kuna mjomba wangu nimempitia kuna dawa nimekuja kuzichukua “
“ dawa !unaumwa ?”
“ ni stori ndefu wema , ila kiufupi naumwa sana na sidhani kama nina maisha marefu “ aliongea na kweli alikuwa amekonda sana .
“ nini zaidi “
“figo zangu zote zinafeli “
“ masikini pole “
“ asante”
“ unamawasiliano na rafiki yako ?”
“ nani , bendera ?”
“ ndio “
“ mara ya mwisho nilikutana nae wakati anarudi kutoka kwenu “
“ kutoka kwetu ?” niliuliza kwa mshangao .
“ ndio kutoka kwenu , si alikuja kukuona baada ya kusikia wewe mjamzito “ moyo wangu ulijikuta ukipiga paah .
“ ni kipindi gani ?”
“ juzi juzi tu hapa sidhani hata mwezi umepita , nasikia noeli alikuona ukiwa mjamzito na akamwambia bendera na bendera alifunga safari ya kuja huku kushuhudia kwa macho yake .
Sikuamini maneno hayo kutoka kwa johnson moyo wangu uliuma kwa kweli , sikujua kama bendera alifika singida na kunishuhudia nikiwa na mimba ya bruno , kwakeli roho iliniuma , nilikuwa nikimpenda sana bendera , nilijikuta hata nikishindwa kuagana vizuri na johsnoni na kuondoka huku nikitoa machozi , nilifika nyumbani na kuanza kulia , nililia sana siku hio , kila nilipokuwa nikikumbuka ahadi nilizoahidiana na bendera moyo uliuma .
Baada ya siku hio ndio nilianza kupata msongo wa mawazo , hata mama yangu alinishangaa kwa hali hio kwani hata sikumpenda tena mwanangu ambae kwa wakati huo nilikuwa nimempa jina la jenny .
Siku mnyonyesha kabisa , hasira zilikuwa juu kweli , mama alinichukua na kunipeleka hospitalini na huko nako niliambiwa ni ‘postpartum blue ‘ dokta akisema ni hali tu ambayo inawakumba wanawake baada ya kujifungua na inaisha yenyewe , kipindi hicho mama yangu nilikuwa sijamweleza chochote juu ya bendera , hivyo na yeye aliamini maelezo ya daktari .
Siku moja mbele mama alienda kwenye vibarua vyake , nakumbuka ni siku ambayo akili zangu zilirudi kuwa sawa siku hio kutokana na jambo ambalo lilinitokea , nakumbuka siku hio nilipitiwa na usingizi mzito hata mimi nilijishangaa , kwani nilijika kuamshwa na baba baadae kabisa jioni ya saa kumi na moja , nilishangaa kweli kwani nakumbuka nililala saa tatu za asubuhi , swali la kwanza kutoka kwa mama lilikuwa ni sehemu alipo mtoto .
Mwanzoni nilishangaa , swali hilo lakini akili iliponikaa sawa ndio nilikumbuka kuwa nilikuwa nimemlaza mtoto chumbani , nilinyanyuka na kwenda chumbani na hapo ndipo nilipopigwa na mshangao , kwani sikumkuta mtoto , tulianza kutafuta huku na kule , lakini sikuweza kabisa kumuona mwanangu , nilijikuta nikianza kulia kilio ambacho ni kama mtu aliefiwa , ile hali ya mawazo ilikuwa imenitoweka ghafra na sasa nilikuwa nikimaka mwanangu tu jenny .
Masaa mawili tulitafuta bila mafanikio , mama na watu walichanganyikiwa kwa tukio hilo , nililia mpaka koo likauma , akili haikuwa ikifanya kazi kwa wakati huo , mtoto alikuwa ameibiwa baada ya kama saa mbili za usiku ni kama akili ndio ilikaa sawa na hapo ndipo nilipokumbuka maneno ya bahati kutafuta mtoto wa kupelekea wazungu .
“mamaaa , bahati bahati “ niliongea kwa kukurupuka na kuropoka kwa wakati mmoja na kumshitua mama yangu .
“ bahati kafanya nini “
Nilimsimulia kwa ufupi na hapo ndipo tulipotoka na moja kwa moja kuelekea nyumbanni kwa bahati , na usiku huo mkuku mkuku .
Palikuwa ni sehemu ya nusu saa ila sisi tulitumia dakika kumi na tano tu kufika nyumbani kwa bahati tulibisha hodi na alitoka bibi yake bahati kwani ndio mtu pekee aliekuwa akiishi nae .
“ tunamuulizia bahati “ mama aliongea .
“ bahati bahati kaenda ulaya kaniaga jana kaacha tu barua hata kusoma sijui kasema nimpe wema mtoto wa marehemu sufiani “
Moyo ulipiga paa , baada ya kusikia maneno hayo , nilijua kama ni kwei bahati ameenda ulaya basi ni hakika kwamba alikuwa amepata mtoto , wazo la kwamba mtoto alieondoka nae alikuwa ndie mtoto wangu zilinzia hapo hapo na nilijikuta nikikaa chini na kuanza kulia .
‘ tunaomba hio barua “ aliongea mama nakuchukua barua na kutumia mwanga wa kandili aliisoma .
Mama alikuwa mtu mzima ila alilia siku hio , haikuwa barua ilikuwa ni ujumbe tu mdogo .
“ utanisamehe sana rafiki yangu wema , nimemchukua jenny nadhani ukisoma barua hii nitakuwa tayari nipo kwenye ndege kuelekea ulaya , najua nilichokifanya si sahihi na mungu ataniadhibu kwa uovu wangu “ ilikuwa ni maandishi hayo tu ndio yalionifanya nilie sana , nililia mno jamani , japo nilikuwa nikimchukia mwanagnu lakini nilikuwa nikimpenda , nakumbuka nilizimia siku hio na nilikuja kushituka kesho yake na kilio kiliendelea .
Mama yangu alifikisha taarifa polisi , lakini siku zilizidi kwenda pasipo ya jenny wala bahati kupatikana , baada ya miezi kadhaa mwanangu janeth alirudi kutoka shuleni na kidogo kupitia yeye ndipo akili ilirudi rudi na kidogo nilianza kupotezea mawazo ya jenny .
Siri ya kumpoteza mwanangu ilibaki kwa watu wachache sana , ilikuwa ni aibu kwangu , kwani lawama zote nilijibebesha mimi nilijiapia siku nitakapo kutana na bahati atanitambua , lakini pia nilijiapia kumtafuta mwanangu kwa hali na mali , ndio kwanzia siku hio nilipo anza kufanya bishara na hela alionipa bruno huku malengo yangu yalikuwa ni kutaka kumtafuta mtoto wangu tu , nilifanya sana biashara na ziliniendea vizuri mno kwani mtaji ulikuwa mkubwa , nilimpeleka janeth masomoni nchini marekani.
Mke wa raisi alijikuta akishituka kwenye kumbukumbu hio , kumbukumbu ambayo ilimtoa machozi sana , kwani alionekana kumkumbuka mwanae jenny .
JE MTOTO HUYO ALIPATIKANA BAADA YA JENNY KUMUIBA ?
ITAENDELEA .

MWENDELEZO :0687151346
 
Kazi nzuri sana, inareflect maisha ya viongozi flani flani hapa nchini kuanzia miaka ya 2005 mpaka sasa.
 
Table content ya season 3 hio usiku huu namalizia season 2 yotee
Screenshot_20211224-215939.jpg
 
EHEMJU YA 53
Ujio wa damiani ndani ya tanzania ulimchanganya mno mwanadada suzzane , ni siku kadhaa sasa alikuwa kwenye kuchunguza ni kwa namna gani damiani aliingia nchini pasipo kujulikana , kwani ndani ya viwanja vyote vya kimataifa kulikuwa na usalama wa taifa ambao walikuwa wakiifatilia sura ya damiani , ili pale atakapo taka kuingia ndani ya tanzania tu akamatwe .
Siku hio alikuwa amechoka mno na hio ni baada ya kutoka arusha , sehemu ambayo alienda kwa ajili ya kufatilia kamera za ulinzi ili kujihakikishia kama ni kweli damiani aliingia nchini , lakini ajabu ni kwamba hakuweza kuona sura ya damiani katika viwanja vyote vya kimataifa , na hata alipotuma taaifa songwe , pia aliambiwa picha hio haikuonekana .
Moja kwa moja aliamiani huenda damiani aliingia nchini kwa kutumia njia za barabara , ama njia sizizo rasmi , jambo moja alililoliona ni la kulifanya kwa wakati huo ni kumsaka damiani popote pale kabla hata ya mheshimiwa raisi hajarudi chini kutokea marekani .
Njia moja ya kumtafuta damiani ilikuwa ni kwa kupitia bwana stephano lamberk , aliamini kabisa kuwa bwana huyo huenda ndie aliehusika na kumuingiza damiani nchini na damiani sasa yupo kwa ajili ya kulipiza kisasi , ni jambo ambalo kwake halikumshangaza kwani swala la damiani kulipiza kisasi ni swala ambalo alilitegemea sana , lakini damiani alikuwa na nyaraka ambazo alilikuwa akizihitaji .
Aliamini damiani na stephano walikuwa wakifahamiana kwa nama yoyote ile , na aliamiani kwamba huenda wakawa wanashirikiana katika mambo mengi , kichwa chake kilikuwa kikizongwa na mamabo mengi , kwani upande huu alikuwa akimtafuta mtu anaejiita mzalendo , mtu ambae alikuwa akijibadilisha sura kila baada ya kufanya tukio , pia upande huu swala la damiani , kwake aliona kazi zinazidi kuwa ngumu mno na hapo ndipo alipo ona swala la msaada kwake ni muhimu zaidi , alikuwa na watu ambao alikuwa amewapa kazi maalumu za kufanya watu waliokuwa wapo chini ya kitengo cha usalama wa taifa , na aliona hao ndio waliokuwa wanafaaa kwa ajili ya kumsaidia kazi yake .
“ damiani nitakupata tu “ aliongea suzzane huku akijiegamiza kwenye sofa akiangalia runinga .
****
Damiani alisubiri dakika kadhaa na kweli baada ya dakika hizo majibu ya email yake kutoka SCAD yalirudi na hapo ndipo ilipo rudishwa ramani ya tanzania nzima lakini sehemu moja ya eneo la kibaha likiwa limezungushiwa alama kubwa , aliangalia maneno ya kibaha na hapo ndipo alipo ona neno la kibaha kwa mathias.
Japo karatasi hio ilikuwa ikionesha ramani lakini hakuelewa moja kwa moja ilikuwa ikimaanisha nini haswa , na pia muda ulikuwa umeenda hivyo alipumzika huku akidhamiria siku ya kesho yake kwenda kibaha .
Siku ya pili yake muda wa saa moja damiani alikuwa kwenye gari yake akielekea kibaha ,alikuwa keshatoa taarifa zote kwa rebecca kwa ajili ya kumsaidia kazi zake siku hio .
Lisaa limoja na nusu alisimamisha gari lake upande wa kulia ndani ya eneo la kwa mathias , na kisha alitoa karatasi ile na kuangalia kwa makini na aliona kabisa alikuwa eneo husika , aliangalia tena karatasi ile na aliona kijialama cha rangi ya njano kimewekewa mshale , halafu mbele yake kuna alama ya herufi kubwa ya N , aliangalia tena kwa kutumia elimu yake ya geofrafia na hapo alitoka kwenye gari na kuvuka barabara upande wa pili , aliingia ndani ya eneo hilo na kukutana na soko dogo , watu walikuwa wapo , alisogelea mpaka kwenye kibanda cha tigo pesa na kisha alisalimiana na jamaa mmoja aliekuwa akifanya kazi hapo .
“ vipi kaka “
“ safi karibu “
“ asante , ila nina shida ndugu yangu “
“ karibu “
“ unaweza kutambua hii alama “ aliongea huku akimuonesha alama ile kwenye ile ramani
“ inapatikana maeneo haya ya kwa mathias”
“ kaka kwa kweli mimi sina siku nyingi haya maeneo labda uende pale juu kwenye lile duka la magodoro kuna mzee pale ni mwenyeji sana wa hili eneo “
“ sawa shukrani “ alitembea na kuvuka barabara ya vumbi na kwenda upande wa juu kidogo sehemu flani ina gema hivi na kupandisha , alisalimiana na mwenye duka lile la magodoro na kisha alimuonesha .
“yeah nakumbuka kuiona mahali hii alama “ aliongea mzee yule huku akionesha kukisumbua kichwa chake , lakini bado hakukumbuka ni wapi .
“ sele hebu njoo mara moja “ aliita mzee huyo na kijana mmoja wa maji ya kunde hivi alievalia kanzu alifika .
“ hivi hii alama unaijua , mimi nakumbuka kuiona mahali ila nimesahau “ aliongea mzee huyo na sele alishika ile karatasi na kuiangalia .
“ ndio naifahamu sana , ipo pale wanapo paita precious center”
“ yeah nimekumbuka , kwa mwingira pale efatha sio “ aliongea mzee huyo kuonesha kukumbuka vyema .
“ ni wapi hapo jamani? “.
“ eneo la efatha kulia kwako kuna nyumba kubwa ina hio alama kwenye geti “ aliongea sele , na damiani siku hio hakuwa amevaa ‘full body mask ‘ alikuwa na sura yake yenyewe .
“ sipajui wazee wangu mimi mgeni hapa “ aliongea damiani na wale wazee waliangaliana na kisha waliita boda upande wa kushoto na ilifika na walimpa maelekezo ya sehemu hio ilipo na hapo damiani alishukuru na kisha alipanda boda hio na kakunja kushoto barabara ya vumbi , ikipita baadhi a maduka kadhaa na kuelekea uelekeo wa wa kushoto .
Dakika kumi na tano tu mtu wa kwanza kuiona hio nyumba alikuwa ni damini , tena haikuwa nyumba , kilikuwa kama ni kiwanda hivi chenye geti kubwa sana kwa nje jeusi na ilikuwa na hio alama ilioandikwa kwa maadnishi meupe , alitoa elfu moja na kumkabidhi mtu wa boda huku akimwambia amsubiri.
Aligonga geti dakika kadhaa tu mlango ulifunguliwa na bwana mmoja alieshika kirungu , na damiani alimjua mtu huyo alikuwa ni mlinzi .
“ wewe ni nani ?”
“ nimeelekezwa kuja hapa na marehemu bruno “ bwana yule alishangaa
“Subiri hapa hapa “ aliongea mlinzi na kisha aliingia ndani na dakika kadhaa tu alitoka mwanaume mmoja wa makamo hivi si chini ya miaka arobaini mweupe alieshika mkasi wa kutengenezea bustani .
“ karibu “ aliongea bwana yule na damiani aliingia ndani na geti kufungwa , lakini kufumba na kufumbua damiani alijikuta akipigwa pigo takatifu la shingo na hapo hapo aliona nyota nyota na kuzimia .
Huku upande mwingine masaa kadhaa nyuma , mwanadada marie , jasusi huyu wa CIA aliekuwa akifanya kazi zake chinii ya umoja wa U-97 alikuwa hatua hatua akimfatilia damiani kwa nyuma , kilichomfanya siku hio atabasamu ni baada ya kumuona laivu damiani , yaani yule damiani aliekuwa akimtafuta alimuona kwenye gari , kazi yake ilikuwa rahisi mno , wakati analifatilia gari la damiani wakati huo linatoka alikuwa na kamera yake kubwa mkononi , hakuwa na shaka kwani alikuwa akimfatilia mtu wake pasipo kujua , mpaka damiani anaingia kibaha kwa mathias marie alikuwa nyuma yake , hata wakati damiani alipo shuka kwenye gari alikuwa akimwangalia tena alimpiga picha kabisa , huku yeye akiwa amepark upande wa kulia wa gari lake karibu na gari ya damiani huku damiani alikuwa upande wa kulia akiongea na mzee mmoja hivi , yeye alikuwa akifailia na alikuwa akichukua picha za damiani .
Wakati akiendelea kufatilia alitoa simu yake na kumpigia boss wake kimbona na kumwambia kuwa mtu wake ashampata na muda huo alikuwa eneo la kibaha .
“ suzzane hakikisha unamkamata na nitatuma vijana waje wakulekeze wapi pa kumpeleka “ aliongea kimbona upande wa pili wa simu kwa lugha ya kingereza .” okey “
“ welldone suzzane “ kimbona alimwagia sifa suzzane , lakini suzzane alikata kabla haja jibu na hio ni mara baada ya kumuona damiani akipanda boda boda , alitoka kwenye gari na kisha alivuka upande wa kulia na yeye akaita boda na akatoa maagizo ya kuifatilia boda boda hio .
Walikuja kukutana na boda boda nyingine ambayo ilikuwa imemleta suzzane .“ vipi ernest ?“ huyo ni ernest muendesha boda aliemleta damiani
“ poa , namsubiria mteja wangu hapa nirudi nae “.
“aliongea ernest “
Marie aliwageukia wale boda boda na kisha kwa kutumia lugha yake ya kiswahili kibovu aliwapa elfu kumi na kuwaambia kuwa waondoke kwani mtu alieingia ndani ya nyumba hio ni mtu ambae alikuwa akimjua , wale boda boda hawakua na mashaka walifurahia pesa waliopewa na kisha wao waliondoka na kumuacha marie akiwa amesimama akiliangalia geti hilo aliangalia kulia na kushoto , na hakukuwa na watu wengi zaidi ya gari la wanafunzi wa chekechea lililopita na kumtimulia vumbi na gari hio ilitoka ndani ya geti la efatha precious centre sehemu ambayo mara nyingi wana efatha hukusanyika kila mwaka na kufanya mikutano yao ya kikanisa ndani ya hilo eneoo , ni sehemu ambayo haikuwa bush sana .
Ukuta ulikuwa mrefu na marie alikuwa akiangalia ni kwa namna gani anaweza kuingia ndani ya hio nyumba bila kushitukiwa , kwani mtu anaemtaka alikuwa ndani ya hio nyumba ., alitembea mpaka nyuma kabisa kwenye shamba na kuangalia sehemu ambayo alikuwa anaweza kuruka , na bahati ilikuwa yake kwani nyuma kabisa kulikuwa na mnazi mrefu mita kadhaa na ukuta , alipiga mahesabu yake na kisha alirudi hatua kadhaa akiwa na raba zake mguuni aina ya converse alifunga vizuri na kisha alikimbilia mnazi ule na kama mwanaridha alikuwa ashauparamia robo yake na kisha alijibingirisha kwa kuruka na kwa utalaamu wa juu kabisa alitokomea ndani ya ukuta.
******
Wakati yote hayo yanaendelea upande wa pili , siku hio hio na muda huo huo , ndani ya eneo la kampuni , alionekana suzzane upande wa kulia akiwa kwenye gari , lakini pia upande wa kushoto alionekana zakayo akiwa kwenye gari , na walionekana wote walikuwa na nia moja ya kufika ndani ya eneo hilo , wote walikuwa wakimfatilia bwana stephano lamberk .
Walikaa hapo kwa masaa kadhaa lakini mtu ambae walikuwa wakikusudia kumuona wala hakuonekana kabisa , kwani mtu wa kwanza kuingia ndani ya eno hilo alikuwa ni janeth , zakayo alimshuhudia janeth , na kisha alitabasamu , aliona jambo lake lingeweza kutimia kama angemtumia mwanamke huyo , wakati huo hakuwa amemuona suzzane kama alikuwa ndani ya eneo hilo , walisubiria kwa masaa kama mawili bila ya stephano lamberk kuonekana , zakayo aliona anapoteza muda na suzzane nae alikuwa akitaka kuondoka , lakini kuna kitu kilimvutia suzzane ni baada ya kumuona zakayo akiingia ndani ya kampuni hio .
Alikuwa akimjua vyema zakayo kwani na yeye alikuwa mwana usalama mwenzake , huku zakayo akiplay undercover na alikuwa akifanya kazi ambazo zilikuwa ni special tu na kwa malipo maalumu , alijikuta akitabasamu , alijua huyo muhuni hapo yupo kwa kusudi maalumu , alimiani lazima kuna uchunguzi aliokuwa akifanya , aliona hio ni nafasi ya kumsubiria zakayo ili ajaribu kumuuliza , japo alijua ugumu wake lakini aliona atatumia mbinu ambazo zitamfanya aingie kwenye kumi na nane zake .
Zakayo mara baada ya kuingia ndani ya kampuni ile alienda mpaka mapokezi na kisha alijieleza pale kutaka kuonana na mwana dada janeth , dada wa mapokezi alipiga simu kwa janeth na dakika chache tu zakayo alikuwa akielekezwa ofisi ambayo janeth alikuwa akifanyia kazi .
“ proffessa “ aliongea zakayo kwa kutabasamu na kisha alienda kuketi kwenye kiti .
“ karibu broo “.
“ ushaanza mambo yako sasa “
“ hahaha .. karibu baby zakayo “
“ hilo ndio neno sasa ila sema tu kavu halina nyama nyama na kachumbari “
“ hahaha niambie ?”
“ safi , unajua nilikuwa siamini kabisa kuwa wewe ni proffessa kwani nilijua wewe ni mwanamitindo na mrembo alieushika moyo wangu “.
“ looh ! kumbe ulikuwa hujui m siku ile tunakutaka indonesia nilikuwa kwenye kukiwakilisha chuo changu kama mwanamitindo “.
“ kumbe , kuna mengi nadhani siyafahamu kuhusu wewe , inabidi ukaribu uongezeke tufahamiane vizuri “.
“ hahaha kweli , ila sijui kama utajua mengi yanayonihusu “.
“ kwanini nisijue , labda ushindwe kunipa nafasi hio ya kukufahamu “.
“ nafasi unayo zakayo “
“ shukrani , anyway mimi sio mkaaji hapa , nimekuja kukutana na boss mkubwa wa kampuni , lakini niliona nianze kwako kabla ya boss”
“ stephano , bado leo hatofika kazini “.
“ unaonekana kufahamiana na stephanno vyema “.
“ sana nimekutana nae mbali na niseme ndie alienileta tanzania “
“ ni boyfriend wako ?”
“ kitu kama hicho , ila tupo kwenye stage za ukuaji “.
“ kumbe ndio maana unanikataa “.
“ sikukatalia ila wewe ni too much kwangu “
“ how “
“ ni handsome , unapesa , halafu unagombaniwa na kila mwanamke mimi siwezi “
“ aah wapi sema tu hunitaki una mtaka damiani “
“ damiani ?” aliongea janeth kwa mshangao na jambo hilo lilimfurahisha sana zakayo , alifanya makusudi kulitaja ili kuangalia reaction ambayo atakuwa nayo janeth , na jibu lake alikuwa ashalipata .
“ nimekosea namaanisha stephano , lakini mbona umeshangaa “
“ noo.. umenichanganya ulipotaja hilo jina , “
“ unamfahamu damiani? “
“ yeah , ninae rafiki yangu anaitwa damiani “
|” sawa siku moja nitaomba nikutane nae “
“usijali”
Basi zakayo aliaga na kutoka nje huku akiwa na tabasamu pana usoni , jasusi huyu alikuwa na mbinu nyingi za kiujasusi na ndio maana alikuwa akimuuliza janeth maneno ya kimitego , alitabasamu kwa kuona kuwa janeth alikuwa akimfahamu damiani na hapo aliamini lazima damiani hatokuwa mbali na hii nchi , aliamini lazima damiani yupo tanzania , alitoka mpaka kwenye parking na kisha aliingia na kutoka eneo hilo taratibu mpaka akatoka kwenye kizuizi na , muda ambao anatoka suzzane hakuwa eneo hilo , lakini ile anakata kulia tu kuna gari ilimzibia kwa mbele na nusu aigonge , kilichosikika hapo ilikuwa mikwaruzo ya tairi na breki , zakayo alijikuta akitoa tusi na kufungua mlango na kulisogelea gari suzzane .
“suzzane ! “ aliongea zakayo baada ya kuiona sura ya mwanamke huyo .
“ nikajua haunifahamu agent z “
“na mimi nilijua haunifahamu , lakini unashida gani mpaka kunizibia “.
“ nilitaka tuongeee “
“ ndio mpaka utake kunisababishia ajali “
“ lakini haijatokea ,ingia tuongee “
“ sio sasa suzzane , panga siku tuonane nina haraka “.
“ najua una haraka , lakini ninataarifa unayo itaka “
“ hahaha ... acha utani wako suzzane , unadhani nahitaji taarifa gani kutoka kwako “.
“damiani i know where he is “ aliongea akimaanisha kuwa damiani anajua alipo “
“you cant be serious suzzane , and how do i know damian and who is he “ huwezi kuwa sirious suzzane na mimi namjua vipi damiani na ni nani .
“ hahaha and the same goes of you, can`t be serious enough to apply espionage tactic infront of me and you know who i am ,, hata wewe pia huwezi kuwa siriasi , huwezi kutumia mbinu za kijasusi mbele yangu na unanijua mimi ni nani “ zakayo alijikuta akigwaya , hakuona haja ya kubishana na huyo mwanamke kwani alikuwa akizisikia tabia zake japo hakuwahi kufanya nae kazi .
“tutafute sehemu ya kuongea suzzane sio hapa “
“ hakuna shida , pale kwenye ule mgahawa panatufaa “ aliongea suzzane na zakayo hakuwa mbishi alisogelea gari lake lililokuwa likinguruma kisha alilisogeza na kuliweka pembeni na kisha aliongozana na suzzane .
Baada ya kufika tu walikaa kwenye mgahawa huo uliokuwa upande wa pili wa barabara na suzzane aliagiza chapati na zakayo pia alifanya hivyo hivyo .
“ unataka kuongea na mimi nini suzzane “
“ zakayo nakujua wewe unafanyia watu mbalimbali wakiweka pesa mezani , na nilikuona ndani ya kampuni ya NLT na nilijua tu kuna uchunguzi unaufanya “
“ hayo umeyasikia wapi suzzane , najua haunifahamu vizuri “
“ nakujua A to Z ,jana nimepata taarifa ulikuwa balozi ya kenya na ulikuwa ukiuliza kuhusu damiani “
“ nani kakuambia yote hayo “
“ njoroge , nishawahi kufika pale kwa uchunguzi wangu na pia nilimpa maagizo ya mtu yoyote akifika akimuulizia damiani anipe taarifa “
“ fu*ck you njoroge”
“ hahaha .. mwanamitindo bhana you real know how to play undercover “
“ suzzane niambie unataka nini kutoka kwangu ?”.
“unamfanyia nani kazi “
“ ili ukamwambie muheshimiwa raisi kibaraka wako “. Aliongea na kumfanya suzzane atabasamu .
“ siwezi kumwambia ila ukinilazimisha nitafanya hivyo “.
“ suzzane huwezi ni tisha kwa trick za kitoto namna hio , i know what you did to daniel “
“ sishangai zakayo , juu ya uwezo wako na ndio maana nimevutiwa na wewe unipe mawili matatu “
“ kuhusu nini ?”
“who you are working for? Nani unamfanyia kazi “.
“ je travaille pour personne, c`est juste mon intuition a faire ,mais je suis le serviteuro patriotique de ce pays , simfanyii kazi mtu yoyote silika yangu ndio inanivuta kufanya hivyo ,hata hivyo mimi ni moja ya watumishi wazalendo wa nchi hii “ aliongea zakayo na kubadilisha lugha kwenda kifaransa mara baada ya watu kukaa pembeni yao na kumfanya suzzane atabasamu .
“ vipi hutaki kujua damiani alipo “.
“ sihitaji , na siwezi kushirikiana na wewe kwa ulichomfanyia danieli tena mtu ambae alikuwa anakupenda , bullshit suzzane i dont give a f*ck about what you know , besides i will find everything on my own so dont try to get into my ways “ aliongea zakayo na alionekana kukasirika mno , kwani baada ya kuongea maneno hayo alinyanyuka na kuweka hela chini ya sahani na kusepa .
INAENDELEA
SEHEMU YA 54
Wakati hayo yanaendelea , dakika chache mbele , ziliingia gari za serikali mbili gari aina ya V8 na baada ya gari hizo kusimama , alionekana mke wa raisi akiingia ndani ya kampuni hio ya NLT , huku akiwa ameongozana na walinzi wake wa kike , mama huyu kwa jinsi alivyokuwa akionekana , utadhani hakuwa mtu mzima , kwani alikuwa na ngozi changa kabisa .
Alitembea mpaka kwenye lift na kisha aliingia ndani mpaka mapokezi na baada ya kufika mapokezi dada aliekuwa hapo alianza kutetemeka , ila alitulizwa baada ya kuulizwa ofisi ya janeth .
Walinzi walibaki nje na mama huyo aliingia ndani ya ofisi ya janeth mwanae na kisha walikumbatiana kwa furaha na kisha aliketi .
“ nina wasiwasi janeth juu ya usalama wako ?”
“ mom najua wasiwasi wako lakini huna haja ya kuogopa “.
“ lazima , nchi kwa sasa haijatulia kabisa “.
“ najua kujilinda mama na isitoshe abasi anafanya kazi hio kwa siri sana , hivyo ni rahisi kujua ni nani ananifatilia “
“ kuwa makini janeth “
“ sawa mama , lakini mbona umekuja hapa? “
“ kuna mzigo nilikupa unihifadhie nimekuja kuuchukua , unakumbuka ?”
“ ndio nakumbuka si kiboksi kile “
“ ndio , mmiliki wa kile kiboksi ashafika nataka nikamkabidhi “.
“ okey mama , lakini kipo nyumbani “
“ tuondoke sasa hivi nikakichukue “
“ sawa , lakini mama nina swali “
“ uliza tu mwanangu “
“ nimekuwa nikiambiwa kuwa na mimi nipo kwenye mpango wa kizalendo , na nikapewa jina hilo la namba linahusiana na nini ?“
“ janeth hilo swala najilaumu kwa kuingizwa kwenye mpango huo , kwani nadhani sasa ndio linakuweka kwenye hatari zaidi , ila mapema utajua ni mpango wa aina gani “.
“ natamani iwe mapema sitaki kuwa blackmailled(kufichwa) nakufanya vitu ambavyo sivijui “
“ nakujua mwanangu “
“ how about sister , kuna hope ya kumpata “.
“ bado , but i promise soon utampata dada yako “ waliongea na kisha walitoka na kuingia kwenye gari baada ya janeth kutoa maagizo kwa rebecca .
“ umekuja ofisini si watakuwa na maswali wafanyakazi “.
“ najua , lakini hio ndio njia ya kukufanya ujulikane , siwezi kukuficha milele , so nivumilie mwanangu “
“naelewa mom “
Ni dakika chache tu walikua ununio , kani hakukuwa na foleni kubwa janeth na madam wema waliingia ndani na kisha alimsubiri janeth , na sekunde chache tu alitoka na kiboksi na kumkabidhi mama yake na kisha waliondoka .
*****
MIAKA ISHIRINI NYUMA .
Ni mwaka ambayo wema alimpoteza mwanae jenny , mwanadada huyu alifanya kazi kwa bidii sana , huku kila akikumbuka mwanae ameibiwa , alizidi kujituma huku akiwa na malengo ya kupata hela na kumtafuta jenny , moyo ulikuwa ukimuuma sana mara kwa mara kila alivyokuwa akimkumbuka mwanae jenny , kwani anakumbuka siku ambayo anaibiwa hakuwa hata amenyonyesha , alijiona mkosaji sana , lakini pia alimlaumu sana rafiki yake bahati , alijuta katika maisha yake kumjua bahati , rafiki ambaye alikuwa akithamini maslahi zaidi kuliko utu .
Basi miaka ilisonga , na mafanikio yake katika biashara hayakufichika tena , watu walimjua kama mwanamke mpambanaji , kwani watu wengi ndani ya singida na mikoa ya jirani walianza kumfahamu boss wema .
Lakini licha ya yote mwanamke huyu alikuwa kwenye majonzi mengo sana , alikuwa akipitia magumu mengi mno huku kila jambo ambalo alikuwa akipitia aliamini yeye ndie aliekuwa chanzo hivyo alitakiwa kuwajibika na yale aliyoyasababisha .
Kilichoongeza maumivu yake ni baada ya kusikia mpenzi wake na mtu aliekuwa amemuhifadhi katika mtima wake ‘john bendera’ kufunga ndoa na mwanamke mwingine , kwake ilikuwa ni zaidi ya majuto , lakini kila alipokuwa akikumbuka kuwa yeye ndie aliekuwa chanzo alijikuta akishindwa kumlaumu bendera , lakini licha ya yote hayo pia alitamani kupata walau nafasi ya kuongea na bendera ili amuombe msamaha kwa kile alicho mfanyia kwa kuvunja ahadi yake , aliamini kwamba huenda mwanaume huyo aliumia sana siku ambayo aligundua kuwa alikuwa mjanzito wa mwanaume mwingine yaani bruno , kwani maumivu aliokuwa akipita kwa wakati huo kwa kuwapoteza watu aliokuwa akiwapenda alijua ni kiasi gani na bendera alijisikia , lakini hakuwa na jinsi , yaliokwisha kutokea yalikuwa yashatokea na hakuwa na uwezo wa kuyarudisha nyuma tena , aliamua kuangalia mbele na sio nyuma tena , maumivu yaliokuwa ndani ya mtima wake yalikuwa ndio chachu kwake ya kufanya kazi kwa bidii zote .
“ nitakupata tu mwanangu jenny siku moja “ aliongea siku hio akiwa ndio amefika ndani ya jiji la dar kwa ajjili ya semina ya wafanya biashara , siku hio akiwa ndani ya hoteli ya new africa .
Japo mwanadada huyu alikuwa ameamua kusonga mbele lakini alikuwa na dhumuni la kuongea na bendera , kwani hatia ilikuwa ikimlima ndani ya moyo wake , wakati huo bendera hakuwa na mafanikio makubwa kama aliokuwa nayo wema , kwani alikuwa ni mbunge wa kuteliwa kijana kabisa .
Siku ya semina hio ndipo alipopata kukutana na bruno , lakini hakutaka hata kuongea na mwanaume huyo , alimchukia na aliona yote yaliokuwa yakitokea na yeye pia alikuwa chanzo , na kwa bruno nae hakutaka kujishughulisha na wema kabisa .
Semina hio iliokuwa imedumu muda wa siku nne , huku mgeni rasmi akiwa ni mheshimiwa kingoi , raisi wa awamu ya nne .
Siku ya mwisho ya semina ndipo wema alikutana na henry ambae kwa kipindi hicho alikuwa ni mbunge wakuteuliwa lakini pia alikuwa mfanya biashara na hapo kwenye semina alifika kibiashara ila sio ki ubunge .
Mmhesimiwa henry alitokea kumpenda sana wema mara baada tu ya kumuona , lakini pia baada ya kufatilia taarifa zilizokuwa zikimuhusu mwanamke huyo mrembo , kwake aliona jambo la maana ni kutupa ndoano kwa mwanadada huyo , alivutiwa sana na uongeaji wa kujiamini wa wema hasa pale alipopewa nafasi kama mfanya bishara chipukizi , ongea yake , kujiamini kwa wema na urembo wake kulimvutia sana henry .
Henry hatua ya kwanza ya kumpata mwanadada huyo ni kuweka ukaribu wa kiurafiki , alitaka kumjua vyema wema na pia alitaka kumpa nafasi wema ya kumjua yeye vyema , aligundua kuwa mwanadada huyo alikuwa na mawazo mengi na hio kwake ilikuwa kama nafasi kwake , na kweli kadri siku zilivyokuwa zinaenda alianza kuirudisha furaha yake.
Hakutaka kuchelewa alianza kumtongoza wema , lakini mwanadada huyo alinekana kuwa mgumu mno , kuna kipindi henry alitamani kabisa kujikatia tamaa , lakini kila alipokuwa akimwangalia mwanadada huyo alijikuta akiyumbishwa na msimamo wake na alianza upya kutongoza .
Henry na bendera walikuwa marafiki , na urafiki wao ulianzia bungeni mara baada ya kuteuliwa na wote kuwekwa viti vya nyuma sana , bendera alikuwa akimtania sana henry kwa kumwambia aoe na henry alimwambia wakati utafika tu .
Siku moja henry alimualika wema bungeni na wema alikubali kwenda , lakini akiwa na lake kichwani , alitaka kutumia nafasi hio kuonana na bendera na kuongea nae , henry yeye alikuwa amemwalika bungeni kwa ajili ya kumtambulisha kwa rafiki yake .
Baada ya vikao vya bunge kuisha , henry na bendera walipanga kwenda kupata chakula kwenye moja ya hoteli , huku henry akinuia kumtambulisha wema kwa bendera , bendera hakukataa wito huo .
Muda wa saa mbili kamili usiku meza ilionekana ikiwa na watu watatu , yaani bendera , henry na wema , bendera alishangaa uwepo wa wema , lakini pia alizidi kushangaa pale alipotambulishwa na henry kuwa wema alikuwa mpenzi wake , kwa upande wa wema hakutaka aina hio ya utambulisho lakini alikubali kinafiki , kwa bendera hasira zilikuwa waziwazi lakini alikuwa akijiuzia mno .
Baada ya chakula , hatimae nafasi ambayo wema alikuwa akiitaka ilitokea na hilo ni baada ya henry kutoka kwenda msalani .
“ john naomba unisamehe “ ilikuwa ni sauti iliotoka kwa wema na kwenda kwa bendera .
“ kwa lipi juu ya usaliti wako nishasahau na haina haja ya kuyaleta ya nyuma hapa isitoshe unaempenzi wako , mwanamke msaliti sana wewe “ aliongea bendera kwa hasira mno na ilikuwa hulka yake .
“ naomba unipe nafasi ya kuonana tuongee john please “
“ sina huo muda na kwasasa nishaoa , au huoni pete kidoleni “
“ najua jonh lakini nakupenda bado john kumbuka uliniacha mwenyewe bila taarifa nikakusubiri hukuonekana “.
“ sina haja ya kuonana na wewe tena msaliti , hujui tu nilivoumia kwa ajili yako “
“ nataka tuongee kidogo kilicho tokea baada ya sisi kuachana “
“ hahaha.. juu ya kubeba ujauzito wa bruno sahau “
“ noo wa kwako “
“ nini !! tumia sababu nyingine sio hio “
“mimba ya bruno ilikuwa bahati mbaya na nilifanya vile kwa kukosa matumizi ya mtoto wako janeth “ aliongea wema lakini kwa mbali walimuona henry anakuja na wakakanyamaza huku janeth akijiweka sawa maana alikuwa akitoa machozi .
Baada ya chakula bendera aliondoka huku akiwa na mawazo juu ya maneno aliokuwa ameongea wema , kuna nafsi ilikuwa ikitaka kuyaamini maneno hayo , na pia kuna nafasi ilikuwa ikikataa maneno hayo , hakuwa akimwamini tena mwanamke huyo na pia hakutaka kurudishwa na wema nyuma tena kwani alikuwa na mke , lakini upande uliokuwa na nguvu ni ule wa kujua kama kweli wema alikuwa akimaanisha juu ya mtoto .
Wote walilala hoteli moja lakini kila mtu chumba tofauti , wema alilala cha kwake na henry cha kwake na pia bendera , muda wa saa sita mlango wa chumba cha bendera uligongwa na bendera akiwa na bukta lake kifua wazi alienda kufungua na baada ya kufungua tu aliingia wema bila hata ya kuruhusiwa .
“ unafanya nini hapa wema “
“ nimekuja tuongee john , kwanini unanifanyia hivyo hutaki kunisikiliza ulifikiri sikusikia marafiki zako walivyokuwa wakiniambia juu ya maneno yako “
“ hukuwaambia wewe kuwa unanichukia , je unajua ni mangapi nilikuwa napitia na mama yangu baada ya kumaliza masomo “
“ sitaki kujua mimi , maana yote yanaumiza ulikuwa unalala na wanaume kupata pesa , si ndio unavyotaka kusema “
“ john acha kuniumiza , uliwaambia marafiki zako unanichukia na huku na mpango na mimi , ulifikiri mimi niliekuwa nikikupenda kwa mapenzi ya dhati nilijisikiaje “
“ na wewe ukawaamini sio na ndio maana ukalala na bruno akakuzalisha , kwanini upo hapa na sio kwa huyo bwana wako , mwenye pesa , au umeona na henry anapesa umeona ujiweke karibu “
“ john haya yote ninayo pitia kwenye maisha yangu ni sababu yako na hupaswi kunitukana , nimekuja kukuambia tu siku tulioachana nilikuwa na ujauzito , na nilijifungua mtoto wa kike yupo marekani masomoni , hio ndio picha yake “ aliongea wema kwa hasira kisha akamrushia chini na kisha wema aliondoka na kurudi kwenye chumba chake akilia , bendera alichukua picha ile na kuiangalia na kweli aliamini maneno yale , maana mtoto japo alichukua sura ya mama yake , lakini alikuwa akifanana nae , alijikuta ni kama mtu aliekuwa ameshituka kwani alitoka mbio na kwenda kwenye chumba cha wema , alikuwa akikijua vyema , na hapo alikaa akagonga sana lakini wema hakufungua , wema alikuwa ndani amejifungia alikuwa akilia , laiti ungemuona wema alivyokuwa anatoa machozi na uzuri aliokuwa nao ungeshamgangaa bendera , baada ya bendera kuomba kufunguliwa kwa sauti ya chini ili asije akamshitua henry hatimae , wema alifungua .
Hapo ndipo bendera alimpa nafasi wema ya kumuhadithia kilichotokea , wema alimuhadithia kila kitu mpaka alivyokutana na bruno na mpaka kumpoteza mtoto wake aliezaa na bruno , bendera alijikuta akimhurumia sana wema , alijua kama mama ni kipindi kigumu sana kwake , bendera nae alimuhadithia maisha yake jinsi alivyosoma kwa mawazo , huku akimwambia kutoshindwa kumsahau katika maisha yake , mpaka siku anafika singida kwa ajili ya kuonana nae , kila mtu alikuwa akitokwa na machozi , walijikuta wote wakifarijiana , mwisho wa siku na hisia hazikuwaacha salama , , wote walikuwa wakipendana kwa dhati na hisia hazikuwa mbali baina yao .
Usiku ulikuwa wakufarijiana , mno , ulichezwa mchezo wa kikubwa mpaka wote wakapitiwa na usingizi , walikuja kushituka kukiwa kumekucha kabisa na hio ni baada ya mlango kugongwa na henry , wema ndie aliekuwa wakwanza kushituka na alieuendea mlango na kufungua kidogo .
“ umeamkaje ?”
“ safi za kwako “
“ salama , mimi najiandaa kwa ajili ya kwenda bungeni tutaonana baadae unywe chai sawa “ aliongea henry kwa heshima zote kwani alikuwa akimheshmu mno wema japo alikuwa akimpenda na hio ni kutokana na mwanadada huyo heshima aliokuwa amejijengea.
“ ameshaondoka “”
“ lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa bendera “
“ ndio , wewe huendi “ aliongea
“ siendi mimi , nimechoka leo au unataka niende ? “ aliongea na kumfanya wema atabasamu .
“ nop”
Wawili hao baada ya kuoga walianza upya , , walifanya na kufanya , kila wakiongea kidogo walikuwa wakifanya ,, baada ya kumaliza ndipo bendera alipo anzisha mazungumz na wema .
‘ una mahusiano gani na henry “
“ ni rafiki yangu kwa sasa , ila ananitongoza “
“unampenda ?”
“ nadhani unajua jibu bendera?”
“anakufaa “
“ unamaanisha nini ?”
“namaanisha henry anakufaa anasifa zote za kuwa mme wako “
“siwezi “
“ huwezi nini ?”
“moyo wangu wote upo kwako nitaolewaje nae “
“ wema sikiliza , mwenyewe nakupenda sana , tena sana , najilaumu kwa makosa yangu lakini pia una makosa yako , sasa inapaswa maisha yasonge , nina mke tena mjamzito , siwezi kuwa na wewe tena unapaswa sasa furaha yako iwe kipaumbele , jiufunze kumpenda henry atakufanya uwe na furaha , sipendi tena utoe machozi , kwani utanipa wakaati mgumu sana , nakupenda wema lakini nadhani hatukuandikiwa kuwa pamoja am sorry . aliongea wahenga walisema mapenzi hayana mwenyewe , jinsi alivyokuwa akiongea bendera huwezi mdhania jinsi anavyo changia hoja bungeni wala akiwa kazini kwake .
Je baada ya wema kuolewa na henry hawakupasha kiporo ???”.
Damiani nae kaingia cha kike , ?? noja tuone.
KESHO NAMALIZIA MPAKA EPSODE YA 60 KUKAMILISHA SEASON TWO STAY TUNED , PIA TUVUMILIANE JAMANI KUANDIKA NI KUGUMU MNO NA KUNACHUKUA MUDA MREFU NA MIMI PIA NINA MISHE ZINGINE ZA KIMAISHA ZA KUJIINGIZIA KIPATO
SEHEMU YA 55
Marie kitendo cha kutua ndani ya nyumba ile , tayari alikuwa ashaonekana na yule mzee ambae ndio alimkaribisha damiani ndani .
Muoneknao wa eneo la hapo ndani ulikuwa ni wa kipekee sana , upande wa kulia wa nyumba hio kulikuwa na bustani ya maua yaliochongwa vizuri mno , upande wa kushoto kulikuwa na tanki la maji , na mbele kidogo kulikuwa na swimmingi pool , kwa nje muonekan wa nyumba hio kwa macho ya haraka haraka ungesema ni kiwanda , lakini ukiingia ndani mazingira yake ya hapo ndani yalivyokuwa masafi , ungepata kuamini vinginevyo kwani eneo hilo lilionekana kama hosteli .
Basi mwanadada huyu baada ya kutua kishujaa kabisa , hali iliofanya mlinzi wa geti na yule mzee , wamwangalie kwa macho ya mshango , kwani ni kama swala alieingia ndani ya zizi la simba , mzee aliamini mwanadada huyo hakuwa mtu wa kawaida , kwa jinsi alivyoweza kuruka ukuta huo mrefu , alimini mwanadada huyo alikuwa na mafunzo ya kijeshi , lakini kwake hilo halikumuogopesha sana zaidi ya kutabasamu na kumsogelea .
“ who are you ?”
“ no one “.
Lilikuwa ni swali moja na jibu moja tayari ngumi zishaanza hapo ndani , yalikuwa ni mapigano ya kwenye movie za kizungu au za kichina , kwani mzee yule mweupe japo umri ulionekana kwenda lakini alionekana kuwa ameiva haswa kimapigano , kwani alikuwa mwepesi mno , lakini haikuwa kwake tu kwa marie nae hakuwa haba , alikuwa akimchanganyia mzee wa watu mapigo ya kithai , kung fu , karate , ili mradi tu kumletea mzee tafrani na mwisho wa siku kumuangusha chini na kutimiza azima yake , pasipo kujua kuwa muda ambao walikuwa wanapigana kuna baadhi ya watu walikuwa wamekaa kabisa pembeni wakiangalia mpambano huo tena mmoja ya watu aliekuwa ndani ya eno hilo alionekana kutoka akiwa ameshikilia juice yake na wala alionekana kabisa hakuwa na waswasi , wote walionekana walikuwa wakimuamini mzee huyo .
“ wow ! master p that is one smart kick “ alisikika bwana mmoja pembeni aliekuwa na manywe ya kirastafali akimaanisha kumpa sifa mzee huyo ambae jina sasa tunamjua kwa jina la master p .
Kwa mapigo aliokuwa akirusha marie yalikuwa ni ya kiume , kuna muda master p alionekna kuzidiwa , kwani kuna muda master p alilete pigo la kung fu la shingo kwenda kwa marie , na marie akadank na kutumia mguu wa kushoto aliushitua mguu wa master p kwa nguvu na master p kukosa balance na kudondokea ua , lakini ile marie anakuja kwa kasi kumuadhibu na teke la tumboni master p alijinyanyua na sarakasi ya kiupande upande ya kimzunguko na kama pia na kutua sehemu nyingine na kwa wepesi wa hali juu alipelka ngumi mbili mfululizo na marie alizipangusa zote , hapo ndipo mwanadada huyu alipo anza mapigo ya aina nyingine , kwani alikuwa ashamsoma master p alikuwa akicheza karate na moja aina ya mapigano yaliokuwa yakipendwa sana na wabrazili na alikuwa akiyajua udhaifu wake , lakini pia kwa upande wa master p alikuwa ashausoma udhaifu wa mwenzake , kwa hio hapo ilikuwa ni kulindana kila mtu udhaifu wake .

Kwa upande wa marie alijua kabisa ndani ya hio nyumba hauna kupona , kwani kwa nyuso zilizokuwa zikimwangalia aliamini kabisa hapo ndani huenda kuna kambi ya kijeshi au chuo cha kimapigano , hivyo muda wpte alikuwa akiangalia nafasi ya kutoroka .
Basi mpambano wa kuviziana uliendelea , lakini kwa marie tayari alikuwa tayari ashaiona njia yake ya kusepa , katika hali ya mshangao kama nyani na hii ni mara baada ya kumpumbaza master p na pigo la ‘round sweep ‘ pigo lililomfanya aruke beki , ‘acrobatic back flip’ hapo ndipo marie aliwashangaza kwani alikanya ukuta , tank la maji ukutana tena beki , lakini kabla hajatua upande wa pili wa ukutana , mlio usioumiza masikio ulisikika , ilikuwa ni risasi ambayo haikueleweka ilimpiga marie sehemu gani , kwani ile anapigwa tayari dondokea upande mwingine .
“ james na rashidi mfateni “ ilikuwa ni kauli moja tu ya master p na vijana walikuwa nje ya geti , huku master p akinawa maji ya bomba , lakini pia upande wa kulia , alionekana jamaa aliekuwa ameshika mtutu wake wa bunduki lake aina ya SMG akilibusu ile sehemu ya kutolea moshi alionekana kujivunia kwa kitendo alichokuwa amekifanya , na master p alimwangalia bwana huyo na kutabasamu
Upande wa nje baada ya vijana wale kutoka sehemu ambayo waliamini ndio marie alidondokea , walipigwa na mshangao , kwani marie hakuonekana kabisa eneo hilo , zaidi ya samu zilizosambaa , walianza kuzunguka kila kona na kuangalia kwa mbele lakini hakukua na mtu kabisa zaidi ya miti ya miembe na baadhi ya minazi michache .
“master , hatujampata “ ilikuwa ni kauli ya james baada ya masaa mawili ya kuznguka huku na huko kumtafuta marie .
*****
Damiani alishituka masaa kadhaa mbele kabisa akiwa ndani ya chumba ambacho kilikuwa na kitanda tupu na godoro , na dirisha la aluminium lakini lililokuwa limewambwa vizuri na chuma kwa upande wa ndani .
Alizungusha macho kulia na kushoto na hapo ndipo alipogundua kuwa alikuwa amefungwa mkono mmoja na pingu , kumbukumbu zake ,zilimrudisha muda alioingia hapo ndani mpaka kupigwa na kupoteza fahamu , alitingisha kwa nguvu lakini hakuna lolote ambalo angefanya angeweza kujiokoa .
Lisaa limoja la kubaki hapo ndani , hatimae mlango ulifunguliwa na yeye alijikuta akipata nafuu , kwani aliona angejibiwa maswali yake , lakini licha ya kujibiwa maswali yake alijikuta akipatwa na mshangao mkuu .
“ elvis !!! , ni jina alilotamka baada ya kumuona mtu aliekuwa akimfahamu ,alikuwa ni rafiki yake elvis , mngoni wa songea aliekuwa akipenda sana warembo , rafiki yake aliekuwa amemuacha chuoni pale TIA .
“ damiani !” aliongea na elvis huku akiweka tabasamu usoni mwake , lakini kabla hajaongea sana , aliingia master p na mwanamaa mmoja hivi aliekuwa amevalia kombati za jeshi , huku kwenye bega lake alikuwa na ngao yaani meja .
“Ndio mwenyewe ?” lilikuwa swali kutoka kwa mister p kwenda kwa elvis
“ yes ndio mwenyewe afande . “ aliongea elvis .
“ karibu bwana damiani kwenye kambi ya ‘ wazalendo camp ‘ you made it back hongera sana , mimi ni master p , ila unaweza niita afande paul ni luteni kanal wa jeshi la wananchi mstaafu , huyu ni afande lissa ni meja , kwasasa yupo pale makongo sekondari kama mgavi .
Damiani alijikuta akishangaa mno , hakuelewa maana ya wazalendo ilikuwa ikimaanisha nini , na pia swala la yeye kukaribishwa , alikuwa ashasahau kuwa ramani ya bruno ndio iliomleta mahali hapo .
“ master p “ ilikuwa nisauti nyingine iliosikika kutoka nje na alikuwa ni rashidi .” kuna nini ?”
‘ tumempata ila kazima , anaonekana kupoteza damu nyingi sana .
******
MIAKA ISHIRINI NYUMA .
wema japo bendera alimwambia maneno ya yeye kumpa ruhusu ya kuolewa na henry , lakini moyo wake ulikuwa kwa bendera tu , mheshimiwa bendera , alikuwa na msimamo mkali sana , japo alikuwa akimpenda mwanadada huyo lakini hakutaka kuruhusu hisia zake zifanye maamuzi , kwani aliruhusu akili yake ndio ifanye maamuzi .
japo ya wema kujiliza mbele ya bendera , lakini hakuweza kubadilisha mtazamo wa bendera , kwani mwana huyo alikuwa amedhamiria , na alienda mbali na kumwambia wema kwamba siku nyingine wakionana sio wapenzi tena bali wataheshimiana kama kitu na shemeji yake .
maneno hayo yalitoka kirahisi sana katika mdomo wa bendera , lakini yalikuwa yanamuumiza sana bwana huyo , kwani alichokuwa akikiongea alikuwa ni kumpigia chapuo rafiki yake henry , aliamini kwa wema kuolewa na henry kidogo angepata nafasi hata ya kumuona kwa mbali .
hatimae siku zilipita tokea bendera aongee na wema , kuna muda alikua akijilaumu kwa kukimbilia kuoa haraka ilihali moyoni mwake alikuwa kuna mwanamke aliekuwa akimpenda , lakini kwakuwa alikuwa akiyajua maumizu ya mapenzi hakutaka kumsababishia mke wake , hivyo aliamua kumsahau wema .
upande wa wema hakuonekana sawa , henry alijitahidi sana kumuweka wema sawa , japo alifanikiwa , lakini haikuwa kwa asilimia zote wema naye baada ya kuona ni kweli bendera amedhamiria ndipo alipoamua kukubaliana na henry na mapenzi yake na henry yakaanzia hapo , lakini japo alikuwa kwenye penzi jipya , lakini hakuacha kumpenda bendera , alikuwa akiona wivu mwingi mara baada ya kumuona bendera na mke wake .
siku zilipita na hatimae , bendera na wema walikutana tena kwa ajili ya kuongea juu ya mustakabali wa mtoto wao janeth .
“ wema najua hili ninalokwenda kukuambia litakuwa gumu kwako , lakini naomba unisikilize “
“ nakusikiliza “
“ naomba uwepo wa janeth uwe siri yako mimi na wewe “.
“kwanini , unamaana gani bendera “
“ namaanisha kwanzia sasa hivi nitahusika na janeth kwa kila kitu , na wewe hakikisha henry hajui katika hili , kwani mpaka sasa tumemdanganya mengi “
“lakini siwezi kuishi mbali na mwanangu “
“ najua wema , lakini kama nilivyokuambia kwa ajili ya henry lazima tulifiche hili , najua unampenda mwanao “
“ ni ngumu sana kwangu kunitenganisha na mwanangu na sitoweza “
“ inawezekana , utakuwa ukimuona mwanao kama kawaida , mwakani naenda masomoni marekani hivyo nitaonana na janeth nitatumia muda huo kuongea na janeth “
Maneno hayo yalionekana kuwa magumu sana kwa wema , lakini mwisho wa siku alikuja kukubaliana na bendera juu ya kumficha henry , ulikuwa ni uamuzi ambao wao wenyewe hawakujua ni sahihi , lakini walichofikiria kwa muda huo ni kuacha kwanza henry amuoe wema .
Janeth alikutana na baba yake bendera , na alipata kufahamiana nae , lakini kwanzia siku hio alianza kuishi nchini marekani , kwa mzungu mmoja ambae alikuwa ni rafiki yake bendera , rafiki ambae alikutana nae ndani ya chuo cha bostoni , mzungu huo alikuwa ni proffessa ndani ya chuo hicho katika maswala ya electronics , na alifurahishwa sana na uwezo wa janeth na ndio maana alikubari mara moja kumlea .
Wema alikuja kuolewa na henry na miaka kadhaa alimzaa mtoto wake wa kike aliempa jina la jenista , kwa upande wa henry jenista hakuwa mtoto wake wa kwanza kulikuwa na patrick ambae alikuwa akiishi na bibi yake mkoani arusha na hio ni mara baada ya mama yake kufariki baada ya kuzaliwa, hivyo na wema alimpokea patrick kama mwanae wakati huo alikuwa na umri sawa na wa janeth .
Henry hakuwahi kugundua wala kujua kuwa wema ashawahi kuwa na mapenzi na bendera wala bruno , pia hakujua kuwa wema alikuwa na watoto wawili yaani janeth aliekuwa nchini marekani anaelelewa na jenny ambae aliibiwa na bahati na wazungu .
Raisi bendera baada ya masomo yake nje ya nchi ya ngazi ya shahada hatimae alirudi nchini na kuanza harakati za siasa , miaka mitatu mbeleni aliweza kupata nafasi ya ubunge jimbo la geita mjini, hatimae pia alipata nafasi ya kuteuliwa naibu waziri na mwishowe waziri kabisa , huku upande wa henry na yeye aliweza kupata ubunge na hatimae uwaziri .
Wema nae aliendeleza bishara zake na alizidi kujipanua kimataifa zaidi , kipindi hicho na patrick mtoto ambae alikuwa amechukua kama mwanae wa kumzaa alikuwa ndio yupo masomoni .
Mara chache wema aliweza kuongea na mtoto wake kwa siri sana , na hata mara nyingine kwenda nchini marekani kuonana nae pasipo mume wake kujua , janeth alikuwa na akili sana m kiufupi alikuwa ni genius na proffes crispin ambae ndie aliekuwa mwangalizi wa janeth alimsifu janeth kwa uwezo wake na pia alimwambia rafiki yake bendera kuwa amebarikiwa kuwa na mtoto mwenye akili , janeth alirushwa madarasa na hatimae miaka michache tu aliweza kuapta shahada yake ya kwanza .
Upande wa raisi bendera na henry urafiki wao uliendelea pasipo kuwa na dosari , bendera aliweza kuyatuliza mapenzi yake juu ya wema na kuwa bize na mke wake , lakini hio haikuwa hivyo kwa upande wa wema , kwani siku zote alikuwa akimpenda mwanaume huyo japo kuwa alikuwa ameolewa , lakini licha ya wema kuwa na mapenzi na bendera , lakini pia aliitahidi kuhakisha kumuoneshea mume wake mapenzi aliokuwa akistahili kuoneshewa ,alikuwa pia akimpenda henry kwani ndie aliemsadia katika kuirudisha furaha yake .
Familia hizo mbili yaani familia ya bendera na familia ya henry zilikuwa karibu mno na kupelekea hata wake zao kujenga urafiki , mke wa bendera aitwae maria alijenga urafiki na wema , pasipo kujua kuwa mme wake alishawahi kutoka kimapenzi na wema .
Kadri urafiki wao ulivyokuwa unakuwa ndio walipojikuta wakiaminiana mpaka kuanza kuambiana mambo ya kifamilia na hapo ndipo maria alipo mwambia mipango ya bendera kuwa raisi wa tanzania , swala hilo lilimfurahisha sana wema , kwani aliamini ndoto ya bendera ilikuwa ikienda kutimia , lakini pia wema alijikuta akipata mshangao mara baada ya mume wake pia kumwambia kuwa anandoto ya kuwa raisi na atahakikisha kuwa anaitimiza , jambo hilo lilimshangaza , bendera alikuwa na ndoto ya kuwa raisi ilihali pia henry alikuwa na ndoto ya kuwa raisi .
Tabia moja aliokuwa nayo henry ilikuwa ni uwazi , nia yake ya kuwa raisi aliiweka wazi mapema mno mara baada tu ya kupata uwaziri , na mtu wa kwanza wa kumwambia juu ya jambo hilo alikuwa ni rafiki yake bendera , bendera alishangazwa na nia hio ya rafiki yake kwani pia hata yeye alikuwa na nia hio hio ya kuwa raisi , kwake ilimuia ngumu sana bendera kufanya maamuzi , aliamiani akiweka na yeye nia yake wazi ya kuwa raisi basi urafiki wake yeye na henry ungeisha , kwani wangekuwa wapinzani .
Bendera alianza kuwaza juu ya jambo hilo , hakuishia kwenya jambo hilo tu lakini pia aliwaza mambo kadha wa kadha ambayo alikuwa amemfanyaia rafiki yake , aliamini henry alikuwa akimpenda yeye kwa dhati , roho yake juu ya dhuluma waliomfanyia henry yeye na wema ilianza kuinguza nafsi yake na kujutia , ukubwa wa hatia hio ndio uliomfanya kughairi juu ya yeye kuwa raisi na kuamua kumsapoti rafiki yake kwa moyo mkunjufu kwanzia siku hio , huku akiamini inaweza kusaidia kupunguza ile hatia aliokuwa nayo juu ya henry .
Upande wa wema na yeye alijikuta akimuonea sana huruma mume wake , alijua henry alikuwa akimpenda sana na hio ndio ilioibua huruma juu yake , henry alikuwa amemfanyia mengi sana wema ya kudhihirisha kwamba alikuwa akimpenda .
Wema alijikuta na yeye kuingia katika mgogoro wa nafsi wa kuchagua ni yupi wa kumsapoti kati ya mume wake au mpenzi wake wa zamani katika kuwania uraisi , kipindi hichi chaguzi nyingi zilikuwa zishapita na raisi ambae alikuwa madarakani kwa wakati huo alikuwa ni mheshimiwa ndalu .
Baada ya kufikiria sana kwa wema , mwisho wa siku aliamua kumsapoti mume wake kwa asilimia mia moja juu ya kuwa raisi wa tanzania na swala hilo pia aliliweka wazi kwa bendera , na bendera pia alimuweka wazi wema kwamba na yeye anamsapoti henry katika safari ya kuelekea ikulu .
INAENDELEA
 
SEHEMU YA 56
Miaka kadhaa baada ya mheshimiwa athumani ndalu baada ya kuchukua madaraka ,ufisadi ulikithiri sana ndani ya taifa la tanzania huku hali ya chama cha NLM kikidhidi kupeoteza wafuasi kwa kasi kubwa na hio ni mara baada ya vyama vya upinzani kuunganisha nguvu ili kukipindua chama kilichopo madarakani .
Katika kipindi cha muhula wa pili wa uongozi wa muheshimiwa ndalu japoo ya kupita katika muhula wake wa pili , lakini nguvu ya chama ilikuwa imeshuka mno , lakini pia katika kipindi hicho biashara ya madawa ya kuelvya ilikuwa imetamalaki nchini kwa kiasi kikubwa mno .
Lakini pia licha ya serikali yake kukosa muelekeo mheshimiwa huyu alikuwa amefanya na yeye maendeleo kwa namna yake ..
Katika kipindi hichi, chama kilikuwa kimegawanyika katika makundi mawili , kuna kundi lililokuwa likiongozwa na waheshimiwa wastaafu wa awamu ya tano ya nne na ya pili , lakini pia kuna kundi ambalo lilikuwa likimpa nguvu mheshimiwa ndalu na kundi hili lilikuwa likiongozwa na mheshimiwa ndalu mwenyewe na wastaafu wa awamu ya sita na ya saba .
Alichokuwa anaamini mheshimiwa ndalu ni juu ya imani ya kwamba kundi lake ndani ya chama lilikuwa na nguvu kubwa tofauti na kundi la wapinzani wake ndani ya chama , na hivyo aliamini mtu atakae pokea kijiti ni mtu ambae atampendekeza yeye .
“vipi uchaguzi ujao unaona nani anafaa kwa ajili ya kukurithi “ ni swali kutoka kwa mke wake bi saida wakiwa wamepumzika .
“ henry ananifaa “ aliongea mheshimiwa huyu huku akiangalia dari .
“ unaona anaweza ?”
“ sana , henry ni mkomavu kisiasa , ana ushawishi mkubwa hivyo anaweza “
“ lakini hali ya chama sasa kuamini kwa wananchi ni mbaya kwani wanaonekana kuokuwa na imani na chama chetu tena “
“ hahahaha.. mke wangu , hilo linakuogopesha nini , katiba inatulinda sana hata kwa goli la mkono sisi tunashinda , wapinzani nawachukulia kama watu wanao nipa hamasa tu na sio kushinda “
Hivyo ndivyo alivyokuwa akiamini bwana athumani , lakini pia sio kuamini tu , hivyo ndivyo chama kilijengwa , katiba ilikuwa ikipendelea chama kilichokuwa madarakani , uchaguzi ulikuwa ukifanyika lakini hakukuwa na usawa wa kuhesabu kura .(no free and fair election ) kwani waliokuwa wakiongoza tume ya kuhesabu kura walikuwa ni wanachama , hivyo ilikuwa ni ngumu sana kwa chama pinzani kushinda chama tawala .
*****
Upande mwingine wa kundi la wakongwe wa chama , miaka kadhaa nyuma , walikuwa na kikao , kikao hicho kilimuhusisha mkuu wa usalama mstaafu wa taifa bwana marko ngalu , mstaafu wa awamu ya nne , awamu ya tano na awamu ya tatu na awamu ya pili , na baadhi ya makatibu wa chama na wenyeviti mikoani .
Kikao hiki wakati kinafanyika ni ndani ya miaka miwili kabla ya uchaguzi mkuu , waheshimiwa hawa baada ya kukutana walianza mazungumzo yao .
“ waheshimiwa kama nilivyotangulia kusema , nchi kwa sasa ina hali mbaya sana “.
“ ni kweli muheshimiwa , hali hairidhishi kwa sasa , taifa linadidimia , na hatua zinapaswa kuchukuliwa “ aliongea mstaafu wa awamu ya nne .
“ unafikiri ni hatua gani tunaweza kuzichukua ?”
“ mheshimiwa mstaafu wa awamu ya tatu nadhani unafahamu kwamba sisi japo tunaonekana hatuna nguvu ndani ya chama ila tuna ushawishi wa hali ya juu , nadhani hilo ndio swala la sisi kufanya kwa sasa “
“ ni kweli tunaushawishi , kwani mitazamo yetu sisi kama wakongwe inasikilizwa sana “
“nadhani sisi kwa sasa ili kuiepusha serikali yetu katika kudidimia , lakini pia kukiokoa chama , ni kuhakikisha raisi ajae atarudisha heshima ya chama “
“ naunga mkono hoja “ aliongea wa awamu ya tano .
“ hivyo mnataka tufanyeje ?”
“ lazima tuanza maandalizi mheshiwa wa awamu ya pili “
“ ndio najua tunapaswa kuanza maandalizi , lakini maandalizi bila plan hakuna la maana “
“ ndio maana tupo hapa mheshimiwa wa awamu ya nne au unasemaje mkuu wa usalama “
“mimi nalia na maswala ya madawa ya kulevya , lakini mpaka sasa kuna umoja upo nchini ambao ndio wanaamua nani awe raisi nani asiwe raisi “.
“ umoja gani ?” aliongea mheshimiwa wa awamu ya pili , huyu alikuwa mzee kweli kweli .
“U-97 , japo sina uhakika ila ninaamini umoja huu upo ndani ya taifa la Tanzania , kwani mara ya mwisho taarifa nilizopata niliambiwa unaushawishi mkubwa ndani ya taifa la kenya “
“ unahusu nini huu umoja ?”
“ ni juu ya maswala ya madawa ya kulevya “.
“ hahahaha,, sasa hao wanaingilia vipi maswala ya uchaguzi wa tanzania na hio nguvu wanaitoa wapi “
“ waheshimiwa nadhani siwezi kulizungumzia hili sana kwani naamini mpaka sasa huenda kuna baadhi yetu wamepokea fomu kutoka kwa umoja huo au huenda kuna wanachama kabisa hapa “ wote waliangaliana .
“jamani kama kuna mwanachama wa huo umoja ajitokeze hapa “ aliongea awamu ya pili na wote kimya “
“jamani nauliza tena kama kuna ambae ni mwanachama wa huo umoja ?”
“ mheshimiwa wa wamu ya pili umekadhania juu ya mwanachama je wewe sio ?”
“ mimi nilipokea fomu lakini sikujiunga , japo nilipokea vitisho sana lakini kipindi changu cha uongozi umoja huu hakuw ana nguvu sana kama ilivyo sasa “
“ hahahahaha.. kwa hio mheshimiwa ulikuwa ukiuliza maswali gani wakati unaujua “
“ nilikuwa nikitaka kufahamu zaidi juu ya umoja huu mheshimiwa wa awamu ya tatu “
“ mimi pia nilipokea fomu ila sikujiunga “ aliongea wa awamu ya tatu na baadae kila mtu waliongea hivyo hivyo na kutokana na hali hio ya kutokuaminiana kikao hicho kilifungwa na kusubiriwa siku nyingine .
Siku nazo hazikukawia , hatimae waliweka kikoa hicho tena watu wale wale , na siku hio ajenda ilikuwa ni kumchagua mtu ambae walikuwa wakimtaka wao , kwa ajili ya kurudisha heshima ya chama .
Waheshimiwa hawa , hakuna hata mmoja wao ambae alikuwa ni U-97 na nadhani pia umoja huo uliwadharau kutokana na nafasi zao kisiasa .
Baada ya kuchambua na kuchambua ndipo jina la mheshimiwa bendera liliibuka .
“ waheshimiwa najua mna nia nzuri lakini kwa bendera hapana , yule hajui siasa “aliongea wa awamu ya tano .
“ndio maana tumemchagua , huyo ili heshima ya chama ipande lazima tuweke mtu ambae anayatamguliza maslahi ya wananchi mbele “
“ kweli kabisa naunga mkono hoja |”
“ mimi pia naunga mkono hoja “
Mheshimiwa bendera waziri alikuwa akipigiwa chepuo bila yeye kujijua , wazee hawa walikuwa ni wenye wingi wa mbinu , kwani ndani ya hio miaka miwili walikuwa ni kama kunguni , kila mtu aliekuwa na ushawishi katika chama walikuwa wakimwingia kwa namna yake na kumshawishi , na wakati mambo hayo yanaendelea , mheshimiwa ndalu na washirika wake hawakujua kila kilichokuwa kikiendelea , walikuwa washajiaminisha kwamba wao walikuwa na nguvu katika chama hivyo hakuna wakuwashinda na hilo ndilo likawa kosa lao kubwa.
Moja ya watu waliopewa jukumu la kumshawishi bendera kuwa raisi alikuwa ni bwana marko ngalu , bwana huyu mara baada ya kikao hicho miezi miwili mbele ndipo alipomfata bendera kumwambia azima ya wakongwe wa chama kutaka kumuweka ikulu , lakini pasipo kutegemea bendera aliwaambia kuwa hakuwa na mpango wa kuwa raisi na kwa wakati huo alikuwa akimsapoti rafiki yake .
Jambo hilo lilimpa wakati mgumu bwana ngalu , kwani hakujua ni kwa namna gani angemshawishi mheshimiwa bendera , wenzake walimwambia kuwa ahakikishe anamshawishi bendera juu ya jambo hilo.
Hapo ndipo bwana huyu alipo anza mbinu zake za kiujasusi za kutaka kujua ni udhaifu gani wa bendera ambao angeweza kuutumia ili kumshawishi , na hapo ndipo alipo anza kufatilia maisha ye bendera , na ndipo alipo kuja kujua mahusiano yaliokuwepo katika ya bendera na wema mke wa henry .
Siku kadhaa mbele mara baada ya kupata taarifa hio , aliamua moja kwa moja kuomba kuongea na wema yaani mke wa henry , aliamini kuwa wema ndie aliekuwa udhaifu mkubwa wa bendera na kama angeweza kumshawishi mwanamke huyo juu ya dhamira waliokuwa nayo wakongwe hao wa nchi basi ingekuwa ni rahisi pia kumshawishi bendera .
Kwa bwana huyu ngalu mwanausalama , alikuwa akiamini kulikuwa na ugumu pia wa kumshawishi wema , kwani alijua kuwa mwanamama huyo mme wake pia alikuwa na nia ya kuwania uraisi ,
Basi mara baada ya wema kuonana na ngalu waliongea
“ samahani kama utanifikiria vibaya , ila sina nia mbaya juu ya neno lolote nitakalolisema hapa “ aliongea ngalu .
“ hakuna shida mheshimiwa na kusikiliza “
“ nafahamu uhusiano wako wa nyuma na henry , lakini kama nilivyosema sina nia mbaya juu ya kujua huko , ila kuna mambo ambayo nataka kuyajua kuhusu bendera kwani najua alikuwa akikupenda sana hivyo sina shaka kwamba alikuwa akikuambia mambo yake “ wema alishangaa na kisha alivuta pumzi na kumwangalia mheshimiwa ngalu .
“ ni kweli usemayo , lakini pia nimeshangazwa na ulivyofatilia mambo yangu mimi na bendera , ni jambo gani hilo unalitaka kulijua kutoka kwangu maana mimi na bendera sasa hatuna tena uhusiano .”
“bendera alishawahi kukuambia ana ndoto gani katika maisha yake ?”
“ yeah ashawahi kuniambia kuwa ana ndoto ya kuwa raisi , lakini kwa sasa ndoto hio hana tena kwani anamsapioti rafiki yake ambae ni mme wangu , nafikiri unalijua hilo “
“ yeah nalifahamu hilo na pia nimefurahishwa na jibu , kwanza kabisa nadhani unaelewa ni kiasi gani nchi kwa sasa ilipofikia , najua unaweza usitambue hilo kutokana na kwamba wewe sio mwanasiasa , lakini nchi sasa ipo kwenye hali mbaya sana na sisi kama wakuu wa hii nchi hatuwezi kukaa kimya kuangalia nchi hii inayumba “
“ unataka kumaanisha nini muheshimiwa ?”
“ tunataka raisi ajae asiwe na siasa nyingi tunataka raisi ambaye atairudisha hii nchi katika mstari na mtu mmoja pekee anaweza kufanya hilo ni bendera , najua mme wako pia ana nia ya kuwa raisi , lakini henry ni mwanasiasa , na pia tukimpa nchi sisemi kwamba atashindwa kuongoza , ila mambo yanaweza yakawa yale yale “
“ kwanini unaniambia haya wakati ninyi ndio mmeamua hayo , kwani kwa ninavyo ona ni swala la ninyi kuamua kama viongozi wa chama , mimi naingiaje hapo “
“bendera kakataa kuwa raisi anasema anampa sapoti rafiki yake kwa sasa “.
“ mh kwa hio unatakaje “
“ umshawishi bendera akubaliane na sisi , henry atampokea bendera baada ya kustaafu kwani wote ni vijana ila tunataka nchi irudi kwenye mwelekeo “.
“ lakini nadhani kwa sasa unafahamu kwamba mimi simsapoti tena bendera , kwani mimi nimeolewa na siwezi kumsaliti mume wangu na kumpa sapoti bendera “.
“ najua unachomaanisha , lakini haya hatuyafanyi kwa faidi yetu sisi wenyewe tunayafanya kwa taifa la kesho , hivyo wewe kumshawishi bendera sio kwasababu ushawahi kuwa nae katika mahusiano au sio kwasababu unamsaliti mmeo , ila ni kwa ajili ya taifa hili na swala hilo lipo mikononi mwako “
“kama bendera kakataa kushawishika unaaminije kuwa mimi nitaweza kulifanikisha hilo “
“ utaweza , bendera anakusikiliza sana wewe “ wema alijikuta akivuta pumzi kwa nguvu na kisha alimwangalia mheshimiwa ngalu .
“ naomba kufikiria swala hili kwanza “
“ hakuna shida juu ya hilo , unaweza ukafikria , lakini ukumbuke maamuzi utakayo yafanya ni juu ya taifa hili “.
Wema alijikuta akiwa kwenye wakati mgumu mno , aliwaza na kuwaza juu ya maamuzi yake atakayo yafanya , alikuwa akipenda kusapoti ndoto za mume wake , lakini pia maneno ya ngalu yalikuwa yanamaana kubwa , kwani ni kweli nchi ilikuwa na hali mbaya , alikuwa kwenye kuchanganyikiwa lakini mwishowe alijikiuta akikubaliana na swala la bendera kuwa raisi .
Wema alijaribu kumshawishi bendera kwa mara ya kwanza , lakini kazi hio ilikua ngumu , kwani msimamo wake ulikuwa vile vile , na hakupenda kuyumbishwa kabisa na maamuzi aliokuwa nayo .
Siku nazo hazikuwasubiria , muda ulisonga na miaka ikakatika pasipo ya bendera kukubaliana na wakongwe wa chama juu ya yeye kuchukua kijiti cha uraisi kutoka kwa ndalu , wema alijitahidi kwa sehemu yake lakini mwisho wa siku aliachana na kumshauri bendera baada ya kumuona msimamo wake na akaamua kumpa sapoti mme wake .
Wakati hayo yanafanyika na henry na yeye hakuwa nyuma katika kuhakikisha kuwa anafanikiwa katika azma yake ya kuwa raisi wa jamuri ya muungano wa tanzania , lakini pia hakujua kuwa wakongwe wa chama walikuwa na mtu wao waliokuwa wakimpa sapoti , pia hakujua kuwa mkwe wake alikuwa akilijua hilo .
Upande wa bendera , alijikuta akiwa kwenye wakati mgumu sana hakujua afanye maamuzi gani ni kweli maneno ya mstaafu ngalu yalikuwa yanamgusa sana , lakini akimfikiria rafiki yake henry pia kulikuwa na uzito wake , siku nazo zilikuwa zimesonga , kwani siku ya kuchukua fomu ilikuwa imekaribia na alikuwa bado hajaamua ni jambo gani anaweza akalifanya kwa wakati huo.
Bendera japo alikuwa akiwaamini wakongwe wachama kama watu ambao wana ushawishi , lakini pia alikuwa akiamini kwamba hata kama angechukua fomu asingeweza kupita katika halmashauri kuu ya chama na kuwa mgombea , aliijua vyema nguvu aliokuwa nayo henry kwani alikuwa na sapoti kubwa kutoka kwa mheshimiwa ndalu , lakini kutokana na kwamba alikuwa akiwaheshimu wazee hao ndipo siku alipo amua kwenda kuchukua fomu huku dhumuni lake kubwa ilikuwa ni kuwaridhisha wakongwe wa chama .
ITAENDELEA
SEHEMO YA 57
Tukirudi kutoka kwenye kumbukumbu hio ya miaka ya nyuma
“ hapa kuna fanyika nini ?” lilikuwa ni swali kutoka kwa damiani kwenda kwa mister p ambae alikuwa akimtembeza hapo ndani , damiani alikuwa akishangaa sana , kwani kulikuwa kadhaa hapo ndani ambao walikuwa wakifanya mazoezi .
“ hii ni kambi ya mafunzo ya kiintellijensia bwana damiani , ilijengwa na mheshimiwa bendera kabla umauti haujamkuta “.
“ mheshimiwa bendera ?”
“ yeah ndie aliejenga kambi hii na kuipa jina la wazalendo , hii sehemu ni ya siri mno hata mheshimiwa henry hafahamu uwepo wake “.
“ ni kipi kinafanyika hapa ?”
“tunafundisha vijana kuhusu elimu ya kiintellijensia ili kupambana na U-97”
“ U-97 ndio nini ??”
“ utaelewa baadae baada ya kiongozi wetu wa kambi akifika “
“ ni nani huyo kiongozi “
“ utamjua baada ya yeye kufika “
Damiani alijikuta akiridhika na jibu lile kishingo upande , huku akiendelea kuoneshwa maeneno tofauti ndani ya kambi hio , alionyeshwa sehemu ambazo zilikuwa na siraha za kila aina jambo lililomshangaza pia , lakini pia alionyeshwa sehemu ambapo kulikuwa na tarakishi za mawasiliano .
Kiufupi ni eneo ambalo lilikuwa limejengwa kiufundi sana , kwani kama ungeiingia hapo ndani usingejua kuwa eneo hilo lina vyumba chini ya ardhi ni eneo ambalo lilikuwa limeficha siri nyingi sana .
Muda wa saa moja kamili za jioni iliingia gari moja aina ya landcruiser ya rangi ya majivu na alishuka mwanamama mmoja mrembo na hakuwa mwingine alikuwa ni mke wa raisi henry , kwa jinsi alivyojiweka ilikuwa ni ngumu sana kujulikana.
Baada ya kufika alisalimiana na master p kisha waliongozana ndani na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye moja ya ofisi ndogo .
“nahitaji kuoana na kijana luteni “ aliongea madam wema .
“ sawa madam “ aliongea luten paul au master p na kupiga saluti kisha akatoka nje na sekunde chache tu , aliingia damiani na kushangazwa na uwepo wa mke wa raisi walisalimiana kisha wakaketi .
“karibu sana kijana kwenye umoja wetu wa wazalendo “
“ nashukuru madam “
“tulikuwa tukikusubiri kwa muda mrefu “
“ mlikuwa mkinisubiri?”
“ ndio kwani ndani ya mpango wa uzalendo wewe ni moja ya kiini chake “
“ ni mpango gani huo wa uzalendo “
“ ni kuitoa U-97 ndani ya nchi hii “
“ni mara yangu kuisikia hii U-97 inahusu nini “
“ ni umoja wa uliongizwa hapa nchini na wazungu ambao hawana nia nzuri na nchi hii , kuhusu taarifa zake zote utazipata na utaelewa juu ya umoja huu japo sio mambo yote , kwani mpaka sasa tunaamini umoja huu ni zaidi ya tunavyo ufahamu “
“ kwa hio ninakuwaje nipo kwenye mpango wa kizalendo “.
“hilo hatujui kwanini upo kwenye mpango wa kizalendo , kwasababu kwenye majina ambayo mheshimiwa bendera alieyaleta kwetu ni jina lako la damiani rabani lilikuwepo “
“ unamaanisha mheshimiwa bendera alikuwa ananifahamu ?”
“ndio bwana rabani “
“ ananifahamu vipi ?”
“ sina jibu juu ya hilo ila naamini utapata majibu yako jinsi mpango wetu unavyoendelea na hii ni flash alionikabidhi bruno na alinipa maagizo ukifika kwenye hii kambi tu nikukabidhi” aliongoea maadam na kisha alimpatia damiani .
“la mwisho kambini hapa huruhusiwi kufika tena mpaka pale tutakapo kuhitaji” mke wa raisi baada ya kuongea maneno hayo aliingia kwenye gari yake na kisha aliondoka.
“ master p nataka kuondoka “
“kabla ya kuondoka kuna mtu nataka uonane nae kama utamtambua “.
“ sawa “ aliongea damiani na kisha waliongozana na kukunja kushoto na kuingia kwenye chumba ambacho mara baada ya damiani kuingia alijua kabisa kuwa sehemu hio ilikuwa ni sehemu ya wagonjwa kwani kulikuwa na vitanda .
Walisogelea mpaka kwenye kitanda kimoja ambacho kulikuwa na mtu ambae ametundikiwa dripu ya damu .
“ unamfahamu huyu “ aliongea master p na kumfanya damiani amwangalie kwa umakini na hapo ndipo alipojikuta akipigwa na mshangao .
“ marie!!!”
“unamfahamu ?”
“ ndio nishwahi kukutana nae thailland ni CIA agent “
“ CIA??”
“ nishawahi kupambana nae na aliniambia kuwa alikuwa ametumwa na samueli saitoto “
“ samueli saitoto ?”
“ ndio , ni tajiri mmoja hivi aliekuwa nje ya nchi na kaingia nchini baada ya mheshimiwa raisi bendera kufariki wanapenda kumuita rich sam “
“ nishamjua huyo , kwanini alikuwa ana kufatilia “
“ nyaraka alizonipa bruno , na bado hakuzipata nadhani ndio maana kamleta tanzania kwa kazi hio “
“huyu samueli saitoto ni hatari sana , lazima tumfatilie tujue kwa undani ni nani haswa na kwanini ana nguvu mpaka za kuwatumia CIA “
“ni kweli na huenda akawa ndani ya huo umoja wa U-97 kama mlivyo niambia “
“ inawezekana kwani mpaka sasa hatujui kiongozi wa umoja huo ni nani kwani ni siri kubwa hata wakati wa vikao vyao “.
Damiani aliongea na master p na baada ya muda kidogo alitoka ndani ya eneo hilo na moja kwa moja alienda upande alipo kuwepo rafiki yake elvis na kumsalimia .
“ inakuwaje uko hapa elvis , ni miaka tokea tumeachana “
“ ni kweli nilivyomaliza nilienda jeshini na ndipo nilipokutana na master p ni stori ndefu kidogo ila ndie alienileta hapa “
“ hahaha .. lakini nakumbuka kuna kipindi uliniambia hupendi kwenda jeshini “
“ ni kweli nilikuambia kuwa sipendi kwenda jeshini , lakini baada ya kumaliza chuo na pia nilivyosikia taarifa kuwa umepotea ndio nilipata msukumo wa kwenda jeshini ili nipate uwezo wa kukutafuta “
“ elvisi nashukuru sana kwa kunijali kama rafiki , hakika nimeguswa na maneno yako “
“ usiseme hivyo damiani , mimi ni rafiki yako , kumbuka ni mambo mengi sana tumefanya pamoja “
“ ni kweli kabisa , hata mimi nilikuwa nikikumbuka sana , na nilikuwa nikitafuta muda wa kukutafuta “.
“ kweli ulikuwa unataka kunitafuta ?”
“ ndio kuna kazi nilitaka nikupe kwenye kampuni yangu ya maswala ya uhasibu “
“daah ! nashukuru kwa kuniatambua kama mtu mwenye elimu ya uhasibu , lakini kwasasa ndio nipo hapa na kuna kazi nyingi ambazo tunazifanya “
“ ni kweli kabisa , na pia naamini tutazidi kuonana “ “
“ ni kweli “
Basi damiai baada ya kuongea na elvis aliondoka ndani hapo na kwakutumia boda boda aliweza kufanikiwa kulifikia gari lake na kisha aliondoka huku akiwa na swala jingine ndani ya kichwa chake la kulifanyia kazi swala la U-97 lakini pia na kifaa cha flash disk alichopewa na madam wema kwani aliamini lazima kuna maelekezo ya hatua inayofata . .
******
Mrembo merina alikuwa kwenye tabasamu muda wote , maneno aliokuwa ameambiwa na bwana stephano lamberk yalikuwa yakijirudia kwenye kichwa chake mara kwa mara , hakuamini kwamba mtu aliekuwa anampenda na yeye alikuwa akimfikiria tena , siku hio alikuwa amelala akiangalia juu akionesha tabasamu mwanana kabisa , huku akiwaza siku ambayo atakuja kuonana na damiani , hakupata picha siku hio itakuwaje kwa furaha ambayo atakuwa nayo.
“ lakini kwanini sauti ya stephano inafanana na ya damiani ?” merina alijikuta akijiuliza swali hilo pasipo kujijibu , alifikiria na kufikiria na aliona tu labda ni kufanana tu hakuna lingine , alijikuta akipitwa na usingizi na kuja kuamka saa , moja kamili asubuhi muda ambao alijiandaa haraka haraka kwa ajili ya kuwahi kazini.
Saa mbili kamili ndio muda mwanadada huyu alikuwa akitoka kwenye nyumba yake kuelekea mjini posta kwenye majukumu yake , aliendesha gari kwa mwendo wa taratibu kwani pia barabara ilikuwa na magari mengi , saa mbili na dakika arobaini alikuwa nje ya jengo la ofisi yake , alipaki gari na kisha alitoka na hapo ndipo aliposhangazwa na uwepo wa patrick eneo hilo .
“ mambo pat , nimeshangaa kukuona hapa leo “
“ nimekufata merina , vipi uko poa ?”
“ ndio niko poa “
“mbona siku hizi unaniepuka mpenzi , ni nini shida ?”
“ sijakuepuka patrick , ni majukumu ya kikazi tu ndio yananifanya niwe bize “
“majukumu gani hayo merina hata kunitumia ujumbe wa meseji , au kuninijibu”.
“pat kuna sababu “
“ sababu “
“ ndio , ni damiani “
“ damiani !!!??”
“ ndio damiani anarudi , nimeongea na stepahano “.
“kwa hio damiani akirudi inamaana mimi na wewe basi , kwanini unataka kunifanyia hivyo merina “
“ patrick , muda huu ni wa kazi , tutaongea kwa kirefu tafadhari “ aliongea merina akimuacha patrick nyuma akimwangalia kwa huzuni mno , lakini baada ya merina kuondoka alijikuta akipandisha maruhani yake baaada ya kuingia garini .
“ fuc**k you damiani , bora usiingie nchini lazima ni kuuwe “ aliongea na kisha aliwasha gari yake na kuondoka .
*****
Samweli saitoto mwakilishi mkuu wa umoja namba tisini na saba(U-97) , alikuwa kwenye wakati mgumu sana , na hio ni mara baada ya kuwasiliana na kimbona na kupewa taarifa kwamba gari ya marie imekutwa eneo la kibaha kwa mathiasi ikiwa haina mtu huku mawasiliano na jasusi huyo yakikosekana , alikuwa ni mwenye wasiwasi mkubwa sana wakati huo .
Aliinnua simu yake na kisha alitafuta namba ya kimbona na kisha alipiga , na ndani ya masekunde kadhaa namba hio ilipokelewa .
“ “ vipi maendeleo kimbona , mmeweza kumpata alipoelekea /”
“ hapana , ila kuna taarifa kwamba alielekea upande wa precieos center kwa mwingira na sasa vijana wangu wanafatilia huko “
“ lakini uliesema damiani alionekana eneo hilo ?”
“ ndio alionekana ndani ya eneo hilo . na ninawasiwasi huenda akawa amekwamatwa na damiani au kuna lingine lilo tokea “
“ sawa vijana wakifanikiwa kumpata utanitaarifu “.
“hakuna shida “.
Vijana wa kimbona walifika ndani ya eneo la kibaha kwa matiasi na kukuta gari ya marie ikiwa imepaki bila ya marie mwenyewe kutokuwepo na hapo ndipo walipo toa taarifa kwenda kwa bosi wao wakimtaarifu juu ya jambo hilo , lakini katika kuulizia ndipo walipoambiwa kuwa alionekana akielekea upande wa precios centre akiwa ndani ya bodaboda , vijana hao baada ya kupewa maelekezo y hayo hawakutaka kuzubaa walitafuta mtu wa boda aliempeleka , bahati mbaya ni kwamba mtu huyo alikuwa amepeleka kichwa(mteja) , kwa hio hawakuwa na jinsi zaidi ya kusubiri , na ndani ya nusu saa boda huyo alikuja na hapo ndipo walipopewa maelekezo , na vijana hao hawakutaka tu kuelekezwa bali walimuomba boda huyo awapeleke ndani ya eneo hilo .
Ni madakika kadhaa tu walikuwa washafika , huku wakiwa kwenye gari yao aina ya noah , kijana baada ya kufika kwenye lango la nyumba alioingia marie , walisimamisha gari na kisha walimruhusu yule boda kurudi .
Muda huo ilikuwa ni saa kumi na moja kama na nusu hivi , walizunguka ndani ya ukuta huo na hawakuona namna ya kuingia ndani na hapo ndipo waliposhauriana kusubiri mpaka kagiza kaingine ndipo waingie ndani hapo ili wakafanye jambo lao , na kwa wakati huo walisogeza gari lao mbele kabisa ili wasishitukiwe na kisha walisimamisha hapo huku wakiangalia upande wa getini , ilivyofika muda wa saa kumi na mbili kama na nusu hivi ndipo walipozishuhudia gari aina ya landcruiser ikiingia ndani ya geti hilo lakini pia kuna gari nyingine nyeusi aina ya range ilikuwa imesimama mita chache kutoka upande wa kulia wa geti hilo , walikuwa wakiangalia kwa umakini kwa kila kiu kilichokuwa kinaendelea kwani hawakutaka kabisa kufanya uzembe , walitaka kukamilisha kazi ambayo walikuwa wamepewa na bosi wao kikamilifu na timu yao ilikuwa ikiongozwa na derick .
Walijiuliza gari zile zilikuwa ni za nini na kwanini gari moja ipaki nje , ila hawakupata jibu , na ndio wasingeweza kupata jibu kwani hawakuwa na aina ya mafunzo yoyote ya kiupelelezi , kwani waliokotwa tu na kimbona na kupewa mafunzo ya kutumia bunduki .
Nusu saa mbele gari ile ya landcruiser , ilitoka na hawakutaka kuzubaa kwani walishauriana waifatilie gari hio huku wakimuacha kijana mmoja alifahamika kwa jina la kipisi aendelee kuangalia mienendo ya eneo hilo mpaka pale watakapo rudi .
Gari ile ambayo ilikuwa ikiongozwa na derick , ilikuwa kwenye mwendo ikifatilia magari hayo yaliokuwa yapo kwenye mwendo pia , na walihakikisha kwamba hawayapotezi kwenye macho yao , lakini pia walitumia akili zao za kuzaliwa kuzuga ili wasishitukiwe kama walikuwa wanafatilia magari hayo , gari la nyuma iilikuwa ni ile range nyeusi na gari ya mbele ilikuwa ni ile land cruiser.
Dakika chache walikuwa wakipita kibaha stand kuu , na waliendelea kufatilia na gari zile zilionesha kuzidi kuchanja mbuga , kwani ziliweza kupita mbezi na wao walikuwa nyuma tu hatimae zilipita ubungo , na hawakuzipoteza , mpaka zinapita magomeni walikuwa wapo nazo sambamba, kwanza walikuwa wakijiuliza watu wale walikuwa ni wakina nani , lakini pia wakati wanaendelea kufatilia walikuwa wakiwasiliana moja kwa moja na kimbona na sam .
Walikuja kushangazwa baada ya gari zile kuingia barabara ya ikulu , barabara ambayo magari ya kawaida hayakuruhusiwa kuingia , walikwenda kupaki gari yao karibu na barabara ya barack obama na kisha mmoja wao alishuka na kuangalia upande wa geti la kuingilia ikulu na hakuweza kuziona zile gari tena , alirudi kwenye gari na kuwataarifu wenzake .
Lakini wakati wanasubiria , simu ya derick ilitoa mliokuwa ilikuwa ikiita na alipo angalia aliekuwa akipiga alikuwa ni kipisi .
“ vipi kipisi “
“ nimemuona damiani anatoka kwenye ile nyumba , nipo nyuma namfatilia “
“ uko wapi sasa “
“ kibaha “
“ endelea kumfatilia tunakuja “
“ sawa “
ITAENDELEA
SEHEMU YA 59
Kimbona japo alikuwa amewapa kazi vijana wake , ila hakuwa akiwaamini kwa asilimia mia moja , kwani alikuwa akiamini hawakuwa na uzoefu kabisa wa kazi na ndio maana mchana hio baada ya kuona marie hakuwa akipatikana kama alivypokea maagizo kutoka kwa sam ndipo waliposhauriana kumtafuta zakayo kwa ajili ya kuwasaidia kazi hio , kwani walikuwa wakiamini kwamba jasusi huyo alikuwa akifanya kazi kwa pesa na lazima angewafanyia kazi yao , wazo hilo liliungwa mkono na sam na moja kwa moja waliwasiliana na zakayo kwa ajili ya kuonana na zakayo hakuwa na shaka alimwambia kimbona afike ndani ya ofisi yake eneo la mlimani .
Kimbona alikuwa akijiamini sana na aliamini kwa namna moja ama nyingine lazima amshawishi kijana zakayo kufanya kazi hio kwani anakumbuka ashawahi kumpa kazi kwa msaada wa kuunganishwa na raisi , na hapo alikuwa akitabasamu kwenye gari yake mara baada ya kuangalia briefcase iliokuwa imejaa mahela pembeni yake .
“ utatufanyia tu kazi , najua unapenda sana hela na nikikupa hizi utaifanya kaziyetu leo leo “ aliongea kimbona huku akizidi kuongeza kasi ya gari yake kuelekea mtaa wa mlimani na muda huo alikuwa akipita mwenge mataa na alikunja kushoto na kuingia barabaa ya samu nujoma na ndani yadakika kadhaa tu alikuwa nje ya jengo la PSSF .
“ karibu bwana kimbona “ aliongea zakayo mara baada ya kuingia ndani ya ofisi ya zakayo .
“ leo umechelewa kuondoka ?”
“ ndio kuna mambo kidogo ya kazi yalikuwa yananichelewesha “ aliongea zakayo .
“pole sana na majukumu , nimekuja hapa nina kazi nataka unifanyie “
“ kazi gani”
“ kuna jasusi ambaye alikuwa akifanya upelelezi amepotea wakati akimfatilia damiani “
“ akimfatilia damiani , damiani si amepotea?”
“ hapana hajapotea damiani yupo nchini na nilitumiwa na picha hizi hapa za damiani “ aliongea kimbona na kumuonesha zakayo na hapo ndipo alipopigwa na mshangao , alikuwa ni kweli ni damiani , na japo hajawahi kukutanana na kijana huyu anakwa ana lakini kupigia picha alimfahamu vyema .
“ ni kweli ndio yeye “
“ sasa nataka umkamate damiani akiwa hai , ukifanikiwa kumkamata najua lazima nitampata marie “
“ marie ndio huyo jasusi “
“ ndio , nataka kujua kama upo tayari kwa ajili ya kufanya kazi “
“ pesa kwanza “
“ hahahaha... nakufahamu bwana zakayo nimejiandaa vya kutoasha “ aliongea huku akifungua briefcase yake na kuweka mezani na hapo ndipo zakayo alipojikuta akitoa macho kwani hela hizo zilikuwa ni dollar mia mia zilizofungwa kwa rababend, kimbon alitoa mabunda kama kumi na kumuwekea mbele zakayo .
“ hizo ni milioni hamsini , ukifanikiwa na kuongeza ishirini “ aliongea kimbona na kumfanya zakayo atabasamu .
“nipe sehemu pa kuanzia “ aliongea zakayo huku akitabasamu .
“ ameonekana kibaha kwa mathias na hata marie pia kaonenakana na kupotelea ndani ya eneo hilo “
“ okey nitalifanyia kazi “
Zakayo na kimbona walikubariana na zakayo muda huo huo wa saa kumi na moja na yeye alikuwa akielekea kibaha kwa ajili ya uchunguzi wake .
Upande mwingine wakati kimbona anaingia ndani ya jengo hilo la psssf mwanadada suzzane alikuwa upande wa kulia akiangalia watu waliokuwa wakiingia na kutoka ndani ya jengo hilo , na dhumuni la kukaa eneo hilo alikuwa akitaka kujua ni nani zakayo alikuwa akimfanyia kazi , kiasi cha kwenda mpaka kwenye kampuni ya NLT , aliamini huenda jasusi huyo alikuwa akijua mambo mengi sana , na hilo ndilo lililomsukuma kumfatilia zakayo na hio ni mara baada ya zakayo kumtolea nje ombi lake la kushirikishana taarifa na pia kumwambia ni nani aliekuwa akimfanyia kazi .
Sasa wakati kimbona anaingia ndani ya jengo hilo suzzane alimuona na alikuwa akimtambua sana , na jambo hilo ndilo lililomfanya suzzane atabasamu na aliamini kabisa , kimbona kafika eneo hilo kwa ajjili ya kuonana na zakayo .
Muda mchache baada ya kimbona kuingia ndani ya jengo hilo na kutoka ndipo alipomuona zakayo akitoka na kuingia kwenye gari yake , jambo ambalo lilimfanya anyanyuke alipokuwa amekaa na kisha aliingia kwenye gari yake na kuanza kuifatilia gari ya zakayo .
Kama ilivyokuwa kwa vijana wa kimbona na kwa akina zakayo ilikuwa hivyo hivyo , kwani baada ya kufika kibaha walianza kuulizia , lakini bahati mbaya ni kwamba hawakupata taarifa ya upande ambao damiani alikuwa ameelekea kutokana na kwamba lile duka la magodoro lilikuwa limekwisha kufungwa , lakini jambo ambalo walililolipata ni baada ya kuonyeshwa gari ya damiani upande wa kushoto .
“ huyu mshikaji alikuja mida ya asubuhi na sijui alipoelekea , lakini gari yake ile pale ile gari kali sana aliopaki “ aliongea bwana mmoja aliekuwa kwenye kibanda cha tigo pesa .
Zakayo baada ya kupata jibu kama hilo hakutaka kujisumbua sana , aliamini lazima damiani angerudi kuchukua gari yake muda mfupi ujao hivyo alilisogelea gari lake na kisha akaingia ndani akaegemeza kiti na kutulia , upande wa suzzane baada ya kumuona zakayo karudi kwenye gari yake katulia na yeye alitulia ndani ya gari akiwa mita kadhaa kwa mbele na muda huo iilikuwa yapata saa kumi na mbili inaenda na robo .
Zakayo wakati akiwa makini na eneo hilo , hapo ndipo aliposhuhudia gari ambazo zilimfanya aziangalie na gari hizo ni landcuiser na gari nyeusi aina ya range aliziangalia gari hizo mpaka zinakunja kushoto , na kuangalia namba zao na aligundua ni gari za serikali aliziangalia mpaka zinapotelea kwenye macho yake , na alitulia tu , hakutaka kuzifatilia japo kuna kasauti kalikokuwa kanamwambia azifatilie .
Upande wa suzzane na yeye alizijua fika gari hizo , kwani alikuwa ameishi sana ikulu na alikuwa akiyajua magari mengi ya ikulu na gari hizo moja kwa moja alijua ni za mke wa raisi , na jambo hilo lilimshangaza pale alipoziona , na yeye alitamani kuzifatilia , lakini alitulia ili kuona kama zakayo atazifatilia , lakini alivyoona gari hizo hazfatilii na yeye alitulia .
Mpaka giza linaanza kuingia ndipo walipoziona tena gari zile zikipita tena na muda huo zilionekana kuwa zilikuwa zikirudi na zakayo aliziona na pia alitulia tu , lakini alishangaa pia kuona gari ya noah ikitokea upande huo huo na kwa mafunzo yake ya kijasusi aliamini kwamba gari hizo zilikuwa zikifariliwa , lakini hakutaka kujihusisha na hilo pia , moyo wake ulikuwa ukimwambia kuwa gari ya damiani akiendelea kuisubiria ndio atapata majibu anayoyataka , upande wa suzzane pia aliendelea kusubiri , kwani na yeye moyo wake wote aliuweka kwa zakayo kwani alikuwa akiamini kwaba zakayo hapo kuna tego kali alikuwa akilitega na yeye kama atasubiria anaweza kupata kitoeo na ni kweli kwani ndani ya saa moja na nusu ndipo waliposhuhudia boda boda ikifika ndani ya eneo hilo na baada ya wao wote kuangalia kwa umakini japo suzzane alikuwa mbali alimtambua vyema damiani na hata kwa zakayo pia .
Upande wa damiani mara baada ya kufika eneo hilo , kuna hisia zilizokuwa zikimwambia kuwa boda boda iliokuwa nyuma yake ilikuwa ikimfatilia , ila alipanga kama ni kweli basi angeipiga chenga la macho na kupotea .baada ya kufika kibaha kwa mathias alishuka na kuliendea gari lake na kisha aliingia na kuondoka eneo hilo na mtu wa kwanza kulifatilia alikuwa ni boda aliopanda kipisi na aliyefatia alikuwa ni zakayo harafu nyuma alikuwa ni suzzane .
*****
Upande wa kina kimbona walikuwa wakifatilia kwa ukaribu operesheni ambazo vijana wao walikuwa wakifanya , kwani walikuwa wakihitaji kujua kila hatua iliokuwa ikiendelea .
Japo kimbona kazi hio alikuwa amempa zakayo , lakini hakuwa kabisa na imani nae na ndio maana na viijana wake pia alikuwa amewapa kazi ya kuendelea kufanya kazi .
Na yeye pia alikuwa kila jipya nalolipata alikuwa akiwasiliana na sam na kumpa maendeleo ya kazi .
Moja ya taarifa iliomshitua na kumchanganya bwana huyu ilikuwa ni taarifa ya vijana wake ni juu ya gari ambayo walibaini zilitoka ikulu .
“ derick unasema gari hio mwanzoni uliiona wapi “
“ ziliingia kwenye nyumba ambayo damiani na marie ndio walipoingia , sasa wakati wakusubiri ilituvamie ndio gari hizo ziliingia na baada ya muda zilitoka na ndipo tulipomuacha kipisi eneo hilo na sisi tukaendelea kuzifatilia na tumekuja kujua ni gari za ikulu “
“ kama ni gari za ikulu atakuwa ni nani alie ndani ya gari hizo”
“ hatuwezi kujua boss , lakini kipisi kapiga simu kasema kamuona damini na kwasasa anamfatilia kwa nyuma “
“ safi sasa nyie kazi yenu iishie hapo kuna mtu mwingine nimempa kazi hio “
“ sawa boss “
“ ila mwambie kipisi anendelee kuzifatilia “
“ sawa boss”.
Kimbona mara baada ya kuwasiliana na vijana wake alipiga simu kwa sam na kumpa taarifa na hapo ndipo na sam na yeye alishangaa , kwanini gari za ikulu zionekane maeneo hayo , walijadiliana na mwishowe wote wakakubaliana kwamba kama kweli damiani alifika eneo hilo basi kuna uwezekano mkubwa akawa na ushirikiano na mtu wa ikulu , na kama sio raisi henry basi ngekuwa ni mke wa raisi wema , lakini waliami kwa asiliamia kubwa kwamba anaeweza kuwa na ushirikiano mkubwa anaweza akwa ni mke wa raisi na ndio maana U-97 walileta ‘death notice’ yake .
“ kama ni hivyo kimbona , basi mpaka sasa tushajua ni nani ambaye anafanya kazi na damiani na kwanini damiani alifanikiwa kufika thailland “ aliongea sam “ hata mimi naliunga mkono jambo hilo , damiani lazima anapokea msaada kutoka kwa mke wa raisi maana kama ni mheshimiwa mwenyewe isingewezakna kwani kwa sasa yupo marekani .
“ ni kweli kabisa , na huenda pia maswala yote anashirikiana na sabi mboneche”
“nahisi hivyo pia , lakini bado kunajambo linanichanganya , unahisi ni kwasababu gani mke wa raisi anashirikiana na damiani huoni kwamba kunauwezekano pia mheshimiwa akawa anatoa maagizo kwa wema kwa sababu hao ni wanandoa “
‘ ni kweli uongeavyo , ila swala hilo hatuwezi lijua kwa sasa zaidi ya kuwa na makisio tu , muhimu ni kusubiri tumkamate damiani tumpe mateso na hapo ndipo tutajua kabisa “ aliongea sam .
*****
Upande wa damiani sasa , muda huo alikuwa ndani ya eneo la kibamba na hisia zake zilimwambia kabisa kuna gari pia ambazo zilikuwa zikimfatilia kwa nyuma na pia aligundua kuwa na kuna boda pia iliokuwa ikimfatilia na hilo aliamini atakuja kulijua akifika mbezi maana alipanga akifika eneo hilo akunje barabara ya kwenda makongo juu.
Dakika kadhaa alikuwa akipiga mbezi stendi alisonga mbele nusu kilomota kabla ya kuifikia kimara na kuunganisha na barabara iliokua ikielekea makongo juu , na hapo ndipo alipothibitisha hisia zake , kwani aliona kabisa gari mbili alizotoka nazo kibaha zikija upande wake , japo gari hizo alikuwa ameziacha umbali mrefu lakini hisia zake hazikumdanganbya kabisa , lakini pia hata yule aliekuwa kwenye boda alimjua vyema .
Aliongeaza mafuta na kukanyaka pedeli kuongeza mwendo na madakika kadhaa alikuwa akipiga nje kabisa ya nyumba yake na hautaka kuingia kwenye nyumba hio kwani alijua fika kama angeingia kwenye nyumba hio lazima wangafahamu kwamba yeye ndie stephano lamerk , na jambo hilo hakutaka litokee kabisa .
Baada ya kupita eneo hilo la nyumbani kwake dakika kadhaa alikuwa ndani ya bagamoyo road akiwa mbezi beach , aliendelea na barabara hio huku kila mara akiangalia magari yale na kwa mbali alikuwa akiyaona , alipita bondeni na kuingia lugalo na kisha hakutaka kuendelea mbele kwani alikunja kushoto na kuingia barabara iliokuwa ikilelekea kawe na ndani ya madakika kadhaa alikuwa ndani ya kawe , aliingia ndani ya barabara ya ally skyes na kisha aligeuza macho nyuma na magari yale aliyaona pia , japo pikipiki ile hakuiona tena aliendelea na kisha alikunja upande wa barabara ya mwaikibaki rd .
Upande wa zakayo alikuwa akiendesha gari yake kiumakini sana , na hakujua kuwa bwana damiani alikuwa ashamuona , lakini kuna jambo na yeye alilijua wakati wa kuendesha , ni gari aina ya brevis iliokuwa nyuma yake , alijua kuna uwezekano mkubwa na yeye alikuwa akifatiliwa kwani kumbukumbu zake zilikuwa zikimwambbia kuwa gari hio aliiona eneo la kibaha kwa mathias , alijikuta akitabasamu , na kilichomfanya atabasamu ni kiuona yeye alikuwa akimfatilia mtu na yeye pia alikuwa akifatiliwa , kwahio ilikuwa mfatano , lakini pia aliona pikipiki iliokuwa ikifatilia gari ya damiani , na hata baada ya kuipita pikipiki ile ndani ya eneo la bondeni kutokana na uwezo wake mdogo wa spidi , lakini kwa nyuma pia ilikuwepo ikionekana .
Zakayo aliendelea kuifatilia gari ya damiani kwa umbali kidogo , na alionekna alikuwa akifanya vile ili damiani asijue kama alikuwa anamfatilia .
Damiani baada ya kufika mita kadhaa kabla haujaingia kwenye jengo la E FM alikunja na kuingia upande uliokuwa ukielekea baharini na alikuja kuingiza gari ndani ya mgahawa mmoja uliokuwaukifahamika kwa jina la MAMA AFRIKA , wakati anaingiza gari yake kuna gari nyingine aina ya AUD new model ya kifahari kabisa ilikuwa ikisogelewa na mwanadada mmoja ivi mrembo , damiani baada ya kuona gari ile kama mshale alitoka na kufunga mlango na kuindea gari ila na kisha alifungua mlango wa kushoto na kuingia na wakati huo na yule mrembo alievalia jeans na tisheti yake nyeupe aliingia , yaani kilikuwa ni kitendo cha wakati mmoja kwani mwanadada yule wakati anafungua mlango wa upande wa derava na damiani alikuwa ashafungua mlango upande mwingine na wote wakaingia ndani .
“ tafadhari endesha “ ni sauti iliotoka kwa damiani pasipo kumwangalia yule mwanadada , lakini kwa upande wa yule mwanadada alitaka apige kelele lakini sura alioiona ndio ilimfanya atoe macho .
“ merina endesha gari nafatiliwa “ ilikuwa ni kauli iliomtoa kwenye mgutuo merina na aliendesha gari na kulitoa kwenye mgahawa huo .
Wakati gari ya merina inatoka ndio gari ya zakayo ilifika na kuingia ndani ya eneo hilo na kisha ilipaki na dakika chache baadae gari ya suzzane ilifika na wote walijikuta wakitoka kwenye magari yao kwa wakati mmoja na kulikimbilia gari la damiani .
“ hahha suzzane !!!” aliongea zakayo huku akimwangalia suzzane kwa tabasamu pana .
“ damiani yuko wapi “
“ too late” aliongea zakayo huku akitabasamu “

kiwa na kuongeza ishirini "a mabunda kama kumi na kumuwekea mbele zakayo .
akitoa macho kwani hela hizo zilikuINAENDELEA
SEHEMU YA 60
merina mara baada ya kutoka kazini moja kwa moja alienda mpaka nyumbani kwake kwa ajili nya kupumzika na kusubiria siku nyingine , muda wote huo mawazo yake yalikuwa kwa patrick , mwanaume ambae aliamini kwamba alikuwa akimpenda lakini yeye alikuwa akimpenda mtu mwingine jambo ambalo kwake aliliona ni gumu sana .
alikuwa na sababu mbali mbali za kumkataaa patrick sababu kubwa kwake ilikuwa ni kutokuwa na mapenzi kabisa na patrick , japo mama yake alishawahi kumwambia kuwa asiwe na uhusiano na patrick lakini alikiri kwamba hio haikuwa sababu kwake kuyasimamisha mahusianao na pat kisa mama yake kamwambia hivyo , kwake aliona kama mama yake damiani ndio angekuwa ni mama yake pat basi asingeweza kabisa kumsikiliza na angeusikiliza moyo wake .
lakini kwa sababu yeye hakuwa na mapenzi yoyote juu ya patrick kwake maneno ya madam wema yalikuwa na nguvu sana , na aliyapa nguvu yeye mwenyew kwa ajili ya kukatisha mahusiano yake na patrick .
Merina baada ya kufika nyumbani kwake muda huo ilikuwa yapata saa kumi kamili za jioni , alimpigia patrick simu kwa ajili ya kuonana nae , na walipanga wakaongee muda wa chakula , na sehemu walioichagua ilikuwa ni msasani kwenye mgahawa wa mama afrika .
Merina alijipumzisha ili kusubiria miadi yake na patrick huku akipanga siku hio akavunje uhusiano wake na patrick na kila mtu aendelee na maisha yake .
Saa moja kamili ndio muda patrick na merina walipofika ndani ya eneo hilo , merina kama kawaida yake japo alivalia simple lakini alikuwa amependeza kuliko mtu yoyote ndani ya eneo hilo.
Kwa upande wa patrick alikuwa akishine maana mwanume huyu alikuwa ni moja ya wanaume mahandsome boy mno , na ukiachana na kuwa handsome boy pia alikuwa ni kijana mwenye pesa nyingi ndani ya tanzania ukimtoa merina na baadhi ya wasanii wengine ambao walikuwa wakifatia kwa kuwa na pesa .
‘ umependeza merina “ aliongea patrick mara baada ya kukaa .
“ asante ila nimevaa kikawaida sana , wewe umependeza zaidi “ aliongea merina huku akigeuza shingo kuwangalia watu mbali mbali waliokuwa ndani ya eneo hilo ambao walikuwa wakipata chakula .
Mhudumu alifika na merina aliagiza wali na nyama ya kuku na patrick aliagiza ugali na nyama ya kuku na mvinyo wa dodoma (dodoma dry red wine ).
Chakula kililetwa huku wakati wote huo walikuwa wakipiga stori za hapa na pale , na baada ya kueletewa chakula kila mtu alikuwa bize na kula na merina hakutaka kuongea jambo lilomleta hapo mpaka wamalize kula kwani aliamini taarifa ambayo anakwenda kumpatia patrick lazima ingemuumiza mno .
Nusu saa tu walikuwa wamekula na kila mtu alikuwa na kinywaji wakishushia , merina yeye hakutaka kuagiza zaidi ya kugawana ile ile wine alioagiza patrick .
“ merina mpenzi , nimefurahi leo nimepata nafasi ya kuonana na wewe “ aliongea patrick akianzisha mazungumzo na merina alimwangalia mwanaume huyo usoni na kujikuta nafsi ikimsuta alijua taarifa ambayo anakwenda kumpa patrick muda huo ingebadilisha uso wake kabisa na kuwa na huzuni .
“ am sorry pat “
“ kwanini merina , umenikosea nini “
“ patrick , nimejifunza kukupenda kwa kipindi kirefu sana , but i cant pat siwezi kumsahau damiani hata kwa sekunde , i am crazy abaout him “ maeneno hayo japo yalitoka kwa hisia katika kinywa cha merina lakini kwa upande wa patrick yaliiingia kama vijisumari ndani ya moyo wake .
“ i know merina , but let give it time , with time kila kitu kitabadilika merina utanipenda merina usiwe na waswasi “
“ no pat , i know its hard for you , lakini naomba na kuomba sana unielewe i cant pat , isitoshe damiani anafika tanzania muda si mrefu “
“ hata kama merina , damiani hakupendi kama ninavyokupenda , kwanini usinipe nafasi hio katika moyo wako merina , kwanini unamlilia mtu ambae haoni thamani ya machozi yako don`t wait for the love you are not sure about merina , i love you merina “
“ i know pat , najua unanipenda , lakini najua pia damiani ananipenda and i can bet my heart and life on him “.
Patrick aliona kabisa ngoma ilikuwa inakwenda kupasuka na hakuwa na uwezo wa kumbadilisha kabisa mwanamke huyo kimawazo , aliona kabisa jambo hilo ni gumu kwa yeye kulifanya , akili yake ilikuwa inafanya kazi kama mashine , hasira , wivu na mengi yalikuwa yakimuandama katika maongezi hayo , aliona kabisa dalili za merina kuvunja uhusiano wake siku hio , aliona hata akiongea na kuongea asingebadilisha mawazo ya merina , maana kuna kale kamsemo kanakosemaga kwamba ni ngumu sana kumshauri mwanamke aliependa na yeye aliamini hilo .
“ kwa hio merina nipe jibu moja kama damiani hatorudi utanikubaia nikuoe”
Ilikuwa ni swali na swali ambalo kwa merina lilimshangaza na hakulitegemea lakini , kwakuwa alikuwa akiuamini moyo wake kwamba damiani lazima arudi basi hakuona shaka kukubali ahadi ya patrick .
“ndio nakubali na na ahidi lakini kwa sasa nataka kila mtiu aendelee na maisha yake “.
“ merina nimekukubalia uendelee na maisha yako kwa sasa , lakini muda ni mwaka mmoja tu damiani asipoonekana you better keep your promise “ aliongea patrick na muda huo alikuwa amesimama , na merina alitikia kwa kichwa na patrick akaondoka huku akiwmbia merina alipie bill yake .
Merina alimwangalia patrick mpaka anatokomea nje na yeye alikuwa amekaa hapo akiwaza hili na lile .
“damiani najua unanipenda na utakuja ndani ya muda nilioahidiana na patrick , i love yo uso much where ever you are “ aliongea merina , lakini alikuja kutolewa kwenye mawazo na mwanaume mmoja ambae merina alipomwangalia alimjua kuwa ni msanii mmoja maarufu hapa nchini na alikuwa akimjua sana huyo msanii maana alikuwa akimfatilia na kumtongoza kwa muda mrefu na merina kwakuwa hakuwa vizuri aliinuka na kuchukua mkoba wake na kuondoka .
Upande wa patrick baada ya kuingia kwenye gari yake mbele kidogo alikutana na gari ya damiani ikija upande wake , hakuipa kipaumbele japo gari hilo ilikuwa nzuri .
“ merina nitahakikisha kwenye maisha yako haukutani na damiani , nitamsaka dunia nzima na nitamuua kama yupo hai “ aliongea patrick kwa hasira .
Upande wa merina alijikuta akipatwa na mshangao mara baada ya kuikalia siti ya gari lake na kumuona damiani , alidhani alikuwa ndotoni mpaka pale damiani alipomwangalia machoni na kutaja jina lake na hapo ndipo alipogutuka na kuendesha gari .
*****
Zakayo ni moja ya majasusi wenye akili sana , na katika upelelezi wake alikuwa akitumia akili nyingi sana na ndio maana aliweza kumtambua suzzane tokea kibaha , na hata wakati alipomuona damiani anaingia kwenye gari lake alijua kabisa suzzane na yeye alikuwa amemuona na ndio maana alitabasamu huku akipiga mahesabu ambayo aliamini kwamba suzzane angeshindwa kumtia damiani mikononi mwake na ndio maana wakati analifatilia gari la damiani alikuwa amelipa nafasi kubwa sana , na kilichomfurahisha ni kwamba alikuwa na hisia kabisa kuwa damiani alikuwa ashajua kuwa alikuwa akifatiliwa kwa nyuma , kwani alivyoona gari ya ke inaongeza spidi alijua hilo kabisa .
Wakati anaingia ndani ya mgahawa wa mama afrika aliiona gari la merina na alimuona pia merina na damiani ndani ya gari hilo na jambo hilo lilimfanya atabasamu , na alijua hapo ni moja ya chenga kubwa mno ambayo alimpiga suzzne .
*****
Suzzane alikuwa akiliangalia gari la damiani kwa umakini mkubwa na kisha aliingia ndani ya mgahawa huo na kuangaza huku na huku lakini mtu aliekuwa akimtafuta hakumuona , alitoka mpaka nje na kumkuta zakayo kasimama ameegamia gari yake huku akionekana hakuwa na wasiwasi kabisa .
“ suzzane ushachelewa kama nilivyokuambia , damiani ashaondoka hapa “ aliongea zakayo na kumfanya suzzane afikirie kidogo na alijikuta akiachia tusi na hio ni mara baada ya kukumbuka gari aliopishana nayo .
“ fuc**k you zakayo “ aliongea suzzane na kisha alichukua namba za gari la damiani na kisha kwa hasira aliingia ndani ya gari lake na kusepa huku akipiga simu sehemu .
“ irene kuna namba za gari nataka unisaidie kufahamu mmiliki “ aliongea suzzane akiwasiliana na mtu aliekuwa akiitwa irene .
“sawa “
Alikata simu na dakika chache tu simu nyingine iliingia na alipoangalia aliona jina ni la mheshimiwa raisi .
“ suzzane kesho na kuhitaji ikulu “ ilikuwa ni sauti moja ya amri .
“ sawa muheshimiwa “
Baada ya kukata simu suzzane alipokea simu kutoka kwa irene na kisha alisikiliza .
“ gari hio inamilikiwa na stephano lamberk “ aliongea irene na kumfanya suzzane atoe tabasamu la ushindi huku akimshikuru irene .
“ damiani jihesabie siku tu nitakutia mikononi muda si mrefu “ aliongea suzzane huku akiongeza mwendo wa gari yake kuelekea nyumbani kwake .
Upande wa ikulu mara baada ya mheshimiwa raisi kufika , sabii aliaga na kuondoka kuelekea nyumbani kwake , lakini wakati akiwa njiani alipokea ujumbe na alipo angalia jina ni kutoka kwa mke wa raisi .
“DAMIANI YUPO NCHINI ANAFAHAMIKA KW AJINA LA STEPHANO LAMBERK MPANGO WETU UNATAKIWA KUANZA SASA “ ni meseji iliomshangaza lakini pia na kumfurahisha sana sabi .
“ yeesss!!!”sabi alijikuta akisema hayo maneno na kuongeza mwendo wa gari lake .
Upande wa bwana matinde mkuu wa usalama mstaafu , alikuwa muda huo ndio anaingia ndani ya nyumba yake akitoka kwenye mihangaiko yake na hapo ndipo ulipo ingia ujumbe kutoka kwa zakayo .
“ MISSION DONE DAMIANI CONFIRMED IN TANZANIA , CURRENT LOCATION HE IS AT MERINA HOUSE “
Ni ujumbr smbao ulimfurahisha mno na baada ya kupokea ujumbe huo akawatumia wenzake , huku akiwaambia kuwa wajiandae kwa mpango wao unao kwenda kuanza .
Upande wa kimbona na sam wote walikuwa wapo bar wakinywa na ndipo sam alipo onesha tabasamu lake na kimbona alimuuliza ni kipi kinachomfanya atabasamu .
“ vijana wako mjini “
“ vijana gani “
“ nilishinwa kuwapata alsh bab nikaingia makubaliano na bokoharam na sasa wametuma makomandoo wao kwa ajili ya kumaliza kazi ya kuwapoteza duniani waliowekewa alama nyekundu na U-97”.aliongea sam na kumfanya kimbona atabasamu .
Lakini wakati huo huo na simu yake kimbona ilitoa mlio na kuangalia alikuwa ni zakayo , alikuwa akipiga na alimtaarifu kwamba kazi tayari aanadae pesa yake .
MWISHO WA SEASON TWO NDIO MWANZO WA SEASON 3
ASANTENI KWA KUWA NAMI
SINGANO JR
SEASON 3 WASILIANA NAMI KUPITIA NAMBA 0687151346 KWA NJIA YA WATSAPP
 
Kitu inaenda sambamba na mishipa Kama damu shukran Sana mkuu barikiwa zaidi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom