Mkuu
Lucas Mobutu sina nia ya kukosoa bandiko lako but hapo kwenye wimbo Candidat Na Biso Mobutu naomba niongeze nyama kidogo kuhusu huu wimbo.
Baada ya kutoa wimbo wa kumtuhumu rais Mobutu kwa uongozi wake wa mkono wa chuma iliamriwa Frànco akamatwe atiwe jela,kisha Mobutu akampa options mbili either atumie kipaji chake kutunga wimbo mzuri utakaomfanya azidi kupendwa na wananchi wake au aendelee kukaa jela{tukumbuke huu wimbo wa kum-dis Mobutu ulipokelewa vizuri sana na masahabiki wa Frànco so nikama aliambiwa atafute kitu cha kuyafuta yale mawazo mabaya kwa wananchi kisha apandikize mazuri yanayomuhusu yeye}.
Ndipo alipotunga huu wimbo canditad na biso Mobutu na inasemekana Mobutu alipousikiliza kwa mara ya kwanza tu aliamuru Frànco atolewe jela upesi sana na apelekwe ikulu ambako ilifanyika sherehe ya kukata na shoka kwa muda wa siku tatu kisha Mobutu akataka ampe Frànco madaraka ya kisiasa ambapo aliyakataa akaomba apewe ruhusa ya kufanya shughuli zake za kimuziki kwa uhuru tu.
Copied.......