Madilu System alikuwa mwanamuziki wa Afrisa International ya Tabou Ley, ilipofika safari ya kwenda ulaya akachujwa kwa mizengwe akiwa Airport. Akaona enough is enough akaomba kujiunga na OK Jazz na Franco hakuwa na hiyana. Akawa mwimbaji pamoja na waimbaji vinara wa OK Jazz- Josky, Ntessa na wengineo. Alifanya hivyo kwa miaka takribani 2/3. Ilipotokea safari ya ulaya dakika ya mwisho akapata namba. Franco wakati huo ndo amemaliza project yake ya "Lisanga ya Banganga" ambayo ilitoa santuri si chini ya 6 akiwa na Tabou Ley, Mavatiku Vissi na Josky Kiambukuta. Akiwa huko ulaya akapata idea ya wimbo wa Non au "Libala oh Libala 1982/83. Akamjaribu Madilu kama ataweza kuuimba. Baada ya kuelekezana ndo mwimbo ule ukasukwa na madilu akapiga duet na Franco na pia kuimba solo vipande vingine. Sauti ya Madilu ikapaa na OK Jazz wakaonekana wamekuja vipya-Franco akanogewa ndo akawa anatunga nyimbo za style ile (pamoja na Mamouu, Mario etc). Hapo Madilu ndipo alipopanda chati hadi kufikia 1986 Josky na Ntessa wakazira kwani waliona Franco macho yake yako kwa Madillu tu. Wakatoka OK Jazz wakatoa nyimbo kama Selengina. Ntessa alirudi kwa style ya Collaboration na OK Jazz (Album kama mbili), Josky alijiunga tena na kuongoza kikosi cha waimbaji wa OK Jazz. Baada ya kutokuelewana kati ya Familia ya Franco (Dada Yake) na Papa Simaro Lutumba 1993 Familia wakamvua Simaro uongozi, ndipo wanamuziki wote wakaiacha OK Jazz wengi wao wakianzisha Bana OK chini ya uongozi wa Simaro. Madilu akaamua kwenda solo, lakini akahakikisha mdundo wake na karibu nyimbo zake zinafuata beat ya OK Jazz na Solo ya Luambo. Alijitahidi pia akajenga bendi yake Bana Syste ambayo ukisikiliza album zake utaona role model wake ni Luambo. Si tu alitembelea nyota ya Franco bali aliishi muziki wa Odemba (style ya OK Jazz). Mwenyewe alidai kila anapoingia studio-anamuona Luambo kazini akimwongoza. Ndogo ndogo inasema mama wa Madilu ni dada wa mke wa Simaro (Maman Kelani).