JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,316
- 5,479
Changamoto ya uhaba wa Petroli sio jambo geni tena kwenye masikio ya watu hapa Bongo, lakini binafsi nilikuwa sijaona changamoto hiyo kwa Dar na maeneo ya karibu na Mji huo.
Kila siku tumekuwa tunasikia mikoani tu kuwa uhaba wa mafuta na mara bei inapanda, inadaiwa kuna mgomo wa kimyakimya ambao unafanywa na Wafanyabiashara wakitaka bei ya mafuta ipande.
Serikali kupitia EWURA na Waziri Makamba naona wanakanusha kila siku kuwa hakuna changamoto hiyo lakini naona kabisa wanaanza kuzidiwa nguvu katika hiki kinachoendelea.
Usiku wa kuamkia leo nikiwa mitaa ya Kibaha Maili Moja kabla ya saa sita usiku bei ya mafuta ya Petroli Lita Moja ilikuwa shilingi 2,700, lakini ghafla ilivyofika saa sita usiku vituo vyote vikapandisha bei na Lita Moja kuwa shilingi 3,700.
Kinachosikitisha ni kuwa EWURA hawajatangaza mabadiliko hayo lakini tayari bei imepanda na kila siku tunamsikia Makamba na EWURA yake wakiishia kupiga mikwara.
Vituo vya kukuza mafuta vya Njuweni hadi Picha ya Ndege vyote bei imepanda ghafla, nimeshuhudia watu wengi walilalamika tu huku wakiwa hawana namna nyingine ya kufanya.
Kila siku tumekuwa tunasikia mikoani tu kuwa uhaba wa mafuta na mara bei inapanda, inadaiwa kuna mgomo wa kimyakimya ambao unafanywa na Wafanyabiashara wakitaka bei ya mafuta ipande.
Serikali kupitia EWURA na Waziri Makamba naona wanakanusha kila siku kuwa hakuna changamoto hiyo lakini naona kabisa wanaanza kuzidiwa nguvu katika hiki kinachoendelea.
Usiku wa kuamkia leo nikiwa mitaa ya Kibaha Maili Moja kabla ya saa sita usiku bei ya mafuta ya Petroli Lita Moja ilikuwa shilingi 2,700, lakini ghafla ilivyofika saa sita usiku vituo vyote vikapandisha bei na Lita Moja kuwa shilingi 3,700.
Kinachosikitisha ni kuwa EWURA hawajatangaza mabadiliko hayo lakini tayari bei imepanda na kila siku tunamsikia Makamba na EWURA yake wakiishia kupiga mikwara.
Vituo vya kukuza mafuta vya Njuweni hadi Picha ya Ndege vyote bei imepanda ghafla, nimeshuhudia watu wengi walilalamika tu huku wakiwa hawana namna nyingine ya kufanya.