Ufaulu wa darasa la nne, kidato cha pili na nne umepaishwa ili kuwafurahisha wapiga kura; ushahidi huu hapa

Watanzania tumerogwa; yaani tunafurahia matokeo feki huku elimu yetu ikizidi kushuka kila mwaka. Aliyeturoga kafa. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya matokeo ya darasa la nne (SFNA), kidato cha pili (FTNA) na kidato cha nne (CSEE) kutolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) hivi karibuni na kuonyesha kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia mbili (2%) ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2020.

Baada ya kufuatilia namna mitihani inavyotungwa na kusahihishwa kwa muda mrefu nimegundua kadri miaka inavyokwenda mbele mitihani inazidi kurahisishwa ili wanafunzi wengi zaidi wafaulu. Hii ni sera ya serikali kuongeza ufaulu kwa wanafunzi kila mwaka ili wapate cha kusema mbele za wazazi (wapiga kura) kila baada ya miaka 5 ya uchaguzi.

Nikianzia kwenye suala la utunzi wa mitihani, siku hizi mitihani inatungwa kwa urahisi sana na kwa njia ya ajabu. Tangu serikali ilipoanzisha mitihani ya kubashiri (kubet) wanafunzi wengi wasiojua kusoma wala kuandika hufaulu kujiunga na shule za sekondari na wanaendelea hivyo hivyo hadi kidato cha nne.

View attachment 2085385
Wanafunzi hawa wakifika kidato cha nne, serikali tena hutunga mitihani rahisi ili wengi wao wafaulu kujiunga kiadato cha tano kwa ubwete. Utafiti wangu umeonesha kwamba kadri miaka inayoenda mbele mitihani ya kitaifa kwa ngazi zote imekuwa ikirahisishwa kwa makusudi ili kuwafaulisha wanafunzi kisiasa. Tazama mtihani wa Biology wa NECTA 1996 ulinganishe na mtihani wa NECTA 2017 utapata jibu mwenyewe. Zamani kupata divisheni wani halikuwa jambo la mchezo. Lakini kwa maswali mchekea kama haya (2017) hata mkulima ambaye hakwenda shule hakosi kupata divisheni wani!

NECTA 1996
View attachment 2095342

NECTA 2017
View attachment 2085333
Hali ni hiyo hiyo hadi kwenye mitihani ya kidato cha sita (ACSSE) ambapo wanafunzi vilaza hupenya hadi kuingia vyuo vikuu. Na huko vyuo vikuu, mchezo ni uleule…..kazi inaendelea. Tazama mtihani wa uliotungwa kwa wanafunzi wa mwaka wa pili kutoka chuo kikuu kimoja hapa nchini Tanzania. Hali inatisha kwa kweli.
View attachment 2085338
View attachment 2085340
Mtihani gani wa kijinga kama huu? Unampima nini mwanafunzi wa chuo kikuu kwa mtihani wa kizembe kama huu? Tuache masikhara jamani; huu mtihani hata ukimtungia mwanafunzi wa darasa la nne atapasua pasi na shaka. Sasa iweje wanafunzi wa chuo kikuu tunaowategemea kuja kulitumikia taifa baada ya kuhitimu watungiwe mtihani wa ovyo kama huu? Inasikitisha sana, ten asana.

Jambo jengine ambalo serikali imeamua kulifanya kwa makusudi ni kuondoa penalty kwa wanafunzi wanaofeli hesabu (Mathematics) tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma. Pia somo la Bible Knowledge siku hizi linajumlishwa kwenye ufaulu ili kuwaboost wanafunzi wengi zaidi wapate divisheni wani za magumashi kisiasa. Tazama kielelezo kifuatacho:

View attachment 2085344

Ndugu wadau wa elimu, sio mimi tu ninayelalamikia uchakachuaji wa elimu hapa nchini. Kila mtu ni shahidi juu ya uhuni unaoendelea katika kudidimiza kiwango cha elimu na kuwafanya watanzania wavivu wa kufikiri ili watawalike kirahisi. WanaJF wengine pia wamewahi kuguswa na jambo hili na kuliongelea kwenye nyuzi zifuatazo:

Wahadhiri vilaza huzalisha wasomi vilaza

Kwanini wahadhiri hawapelekwi tena kusoma 'postgraduate degrees' kwenye vyuo vyenye hadhi kubwa duniani kama ilivyokuwa zamani?


Nini kifanyike?
Nchi hii imefika mahali pabaya sana kielimu na endapo mchezo huu utaendelea, elimu ya nchi hii itaingia kaburini. Kumbuka kama tutakaa kimya, sisi na kizazi chetu chote tutaangamia pamwe! Je, nini kifanyike kurejesha elimu yetu kwenye reli? Karibu tujadiliane.​

Wazee mna tabu Sana! Kwani Hakuna aliyefeli?
 
Ulishawahi kusikia mbunge mwenye degree anashindwa kuapa kwa kuwa hajui KUSOMA VIZURI, only in Bongo, mpe mtoto wa Form two kipande Cha gazeti asome, hawa waliosoma Saint Kayumba, utapata hofu moyoni
 
Kuna mengi yamebadilishwa, Nakumbuka wakati fulani, kusoma diploma ya Clinical officer ilihitajika angalau c c c lakini sasa d d d unaenda bila shida
 
Tanzania ni nchi ya kipumbavu sana. Wakati nchi nyingine za dunia zinapiga hatua mbele kielimu, sisi tunarudishwa nyuma na wanasiasa uchwara wenye matumbo mkubwa kama mapakacha yasiyojaa. Nchi hii imelaaniwa milele! :oops:
 
Kumbe hata zamani mitihani ilikuwa ni myepesi muno, sema zama hizo hapakuwepo na sources of referencing materials kama leo, huo mtihani ulioweka wa 1997 ni mwepesi sana pia. Kwahiyo acheni kuwananga watoto waliofaulu nyinyi wenyewe itakuwa mlikuwa vilaza
Mimi naona huo wa 1997 ni rahisi kuliko 2017
 
Mimi naona huo wa 1997 ni rahisi kuliko 2017
Kivipi mkuu? Hebu fafanua kauli yako hii tata.

Huo mtihani wa 2017 hata ikiondolewa LIST B unaweza kujaza majibu na ukapata yote. Mtihani huu hata ukimpa mtoto wa darasa la 4 ukamuondolea LIST B ata score 100% bila shida.
 
Huu ufaulu wa kimchingo unaosababishwa na serikali sikivu ya CCM ndio unaopelekea baadhi ya shule kuiba mitihani. Ipo siku CCM wataipeleka kaburini elimu ya nchi hii kama tutaendelea kuwachekea.
 
Mfumo wa Elimu usiomwangalia mwalimu kama Focal person na Hurb ya kukufikisha unapotakea unadhani nini kitatokea?
Walimu wana hali mbaya madeni kama yote stahiki zao hawawezi usitegemee cha ziada kutokea
Hivi hujafuatilia vizur nchi zote zenye mifumo mizuri ya Elimu wanafanya nini kwa Walimu wao???
Sisi ngoja tukomae na siasa
 
Watanzania tumerogwa; yaani tunafurahia matokeo feki huku elimu yetu ikizidi kushuka kila mwaka. Aliyeturoga kafa. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya matokeo ya darasa la nne (SFNA), kidato cha pili (FTNA) na kidato cha nne (CSEE) kutolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) hivi karibuni na kuonyesha kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia mbili (2%) ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2020.

Baada ya kufuatilia namna mitihani inavyotungwa na kusahihishwa kwa muda mrefu nimegundua kadri miaka inavyokwenda mbele mitihani inazidi kurahisishwa ili wanafunzi wengi zaidi wafaulu. Hii ni sera ya serikali kuongeza ufaulu kwa wanafunzi kila mwaka ili wapate cha kusema mbele za wazazi (wapiga kura) kila baada ya miaka 5 ya uchaguzi.

Nikianzia kwenye suala la utunzi wa mitihani, siku hizi mitihani inatungwa kwa urahisi sana na kwa njia ya ajabu. Tangu serikali ilipoanzisha mitihani ya kubashiri (kubet) wanafunzi wengi wasiojua kusoma wala kuandika hufaulu kujiunga na shule za sekondari na wanaendelea hivyo hivyo hadi kidato cha nne.

View attachment 2085385
Wanafunzi hawa wakifika kidato cha nne, serikali tena hutunga mitihani rahisi ili wengi wao wafaulu kujiunga kiadato cha tano kwa ubwete. Utafiti wangu umeonesha kwamba kadri miaka inayoenda mbele mitihani ya kitaifa kwa ngazi zote imekuwa ikirahisishwa kwa makusudi ili kuwafaulisha wanafunzi kisiasa. Tazama mtihani wa Biology wa NECTA 1996 ulinganishe na mtihani wa NECTA 2017 utapata jibu mwenyewe. Zamani kupata divisheni wani halikuwa jambo la mchezo. Lakini kwa maswali mchekea kama haya (2017) hata mkulima ambaye hakwenda shule hakosi kupata divisheni wani!

NECTA 1996
View attachment 2095342

NECTA 2017
View attachment 2085333
Hali ni hiyo hiyo hadi kwenye mitihani ya kidato cha sita (ACSSE) ambapo wanafunzi vilaza hupenya hadi kuingia vyuo vikuu. Na huko vyuo vikuu, mchezo ni uleule…..kazi inaendelea. Tazama mtihani wa uliotungwa kwa wanafunzi wa mwaka wa pili kutoka chuo kikuu kimoja hapa nchini Tanzania. Hali inatisha kwa kweli.
View attachment 2085338
View attachment 2085340
Mtihani gani wa kijinga kama huu? Unampima nini mwanafunzi wa chuo kikuu kwa mtihani wa kizembe kama huu? Tuache masikhara jamani; huu mtihani hata ukimtungia mwanafunzi wa darasa la nne atapasua pasi na shaka. Sasa iweje wanafunzi wa chuo kikuu tunaowategemea kuja kulitumikia taifa baada ya kuhitimu watungiwe mtihani wa ovyo kama huu? Inasikitisha sana, ten asana.

Jambo jengine ambalo serikali imeamua kulifanya kwa makusudi ni kuondoa penalty kwa wanafunzi wanaofeli hesabu (Mathematics) tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma. Pia somo la Bible Knowledge siku hizi linajumlishwa kwenye ufaulu ili kuwaboost wanafunzi wengi zaidi wapate divisheni wani za magumashi kisiasa. Tazama kielelezo kifuatacho:

View attachment 2085344

Ndugu wadau wa elimu, sio mimi tu ninayelalamikia uchakachuaji wa elimu hapa nchini. Kila mtu ni shahidi juu ya uhuni unaoendelea katika kudidimiza kiwango cha elimu na kuwafanya watanzania wavivu wa kufikiri ili watawalike kirahisi. WanaJF wengine pia wamewahi kuguswa na jambo hili na kuliongelea kwenye nyuzi zifuatazo:

Wahadhiri vilaza huzalisha wasomi vilaza

Kwanini wahadhiri hawapelekwi tena kusoma 'postgraduate degrees' kwenye vyuo vyenye hadhi kubwa duniani kama ilivyokuwa zamani?


Nini kifanyike?
Nchi hii imefika mahali pabaya sana kielimu na endapo mchezo huu utaendelea, elimu ya nchi hii itaingia kaburini. Kumbuka kama tutakaa kimya, sisi na kizazi chetu chote tutaangamia pamwe! Je, nini kifanyike kurejesha elimu yetu kwenye reli? Karibu tujadiliane.​
Ukisema mitihani ni mirahisi kwa kisa tuu cha kuchagua majibu hapana.
Kwa sasa hutakuta swali la koja kwa moja...yaan 4654+946944=
Yote ni maelezo so kama hajui kusoma hata kusolve na hizo namba hataziona.
Tuweka majungu pembeni hakuna sababu ya kuongeza ufahulu ili uwafurahishe wananzengo....HAPANA
 
Sisiyemu tu hao.. hakuna mchawi mwingine...
Kataa ccm ndo mabadiliko yatakuja..
 
Ukisema mitihani ni mirahisi kwa kisa tuu cha kuchagua majibu hapana.
Kwa sasa hutakuta swali la koja kwa moja...yaan 4654+946944=
Yote ni maelezo so kama hajui kusoma hata kusolve na hizo namba hataziona.
Tuweka majungu pembeni hakuna sababu ya kuongeza ufahulu ili uwafurahishe wananzengo....HAPANA
Lete mifano halisi mkuu
 
Tatizo ni Siasa kuingilia Wizara ya Elimu

Wanafunzi wengi 80% uwezo wao ni mdogo sana.
Hawa hawakutakiwa hata soma, ila serikali imewalazimisha kusoma na matokeo yake ndo haya tuyaonayo.

Wizara imekuja na Mkakati kuwa kila Rais aliyepo madarakani, mkoa wake au anapotokea usifeli.

Kushindanisha wanafunzi kunasababisha wanafunzi na waalimu kuiba mitihani.

Ukitaka jua wanafunzi ni vilaza, kaulize walimu wa vyuo vikuu
 
Tatizo ni Siasa kuingilia Wizara ya Elimu

Wanafunzi wengi 80% uwezo wao ni mdogo sana.
Hawa hawakutakiwa hata soma, ila serikali imewalazimisha kusoma na matokeo yake ndo haya tuyaonayo.

Wizara imekuja na Mkakati kuwa kila Rais aliyepo madarakani, mkoa wake au anapotokea usifeli.

Kushindanisha wanafunzi kunasababisha wanafunzi na waalimu kuiba mitihani.

Ukitaka jua wanafunzi ni vilaza, kaulize walimu wa vyuo vikuu
Umeongea ukweli kabisa. Asiyeamini akamatafute mhitimu wa darasa la saba amlinganishe na yule aliyemaliza fomu foo.......wa darasa la saba ana nafuu.

Nchi hi imefika hapa kwa sababu ya usikivu wa serikali makini ya CCM.
 
Wa nn hapo kuna vitu viwili
Toa mfano wa kitu komoja kimoja mkuu; wadau watakuelewa. Ndio maana hata mimi nimetoa mifano tofautitofauti kuepuka kuwachanganya watu.
 
Umeongea ukweli kabisa. Asiyeamini akamatafute mhitimu wa darasa la saba amlinganishe na yule aliyemaliza fomu foo.......wa darasa la saba ana nafuu.

Nchi hi imefika hapa kwa sababu ya usikivu wa serikali makini ya CCM.
Shule zinashindana kufaulisha, watoto wanakaririshwa mno. Wakifika chuoni inakuwa changamoto.

Mwisho wanakuja lalamika Tutors wanawaonea
 
Shule zinashindana kufaulisha, watoto wanakaririshwa mno. Wakifika chuoni inakuwa changamoto.

Mwisho wanakuja lalamika Tutors wanawaonea
Hili nalo neno mkuu. Lakini na tutors nao wanakaririsha pia; ni mwendo wa kukaririshana mwanzo, mwisho!
 
Hili nalo neno mkuu. Lakini na tutors nao wanakaririsha pia; ni mwendo wa kukaririshana mwanzo, mwisho!
Nao wamekaririshwa tokea shule za msingi.
Tukikosea shule za msingi tu basi

Elimu ya Tz ni biashara
Kuanzia Chekechea hadi Masters
 
Back
Top Bottom