Sella turcica
Senior Member
- Oct 13, 2020
- 104
- 193
Kwanza kabisa nimefurahi Messi kuchukua kombe la dunia. Isingekuwa haki kama huyu mwamba angestaafu bila kuchukua hii ndoo. Poleni timu Ronaldo, mimi nafurahi nikiona mnaumia.
Niende kwenye mada husika. Timu ya Ufaransa imejaa wachezaji wa Africa. Nimeona waafrica wengi wakiishabikia Ufaransa kwa sababu imejaza watu weusi. Mimi naona huo ni utumwa. Hawa jamaa weusi wanaochezea Ufaransa na mataifa mengine ya Ulaya hawana haki sawa na wazungu. Wana uraia sawa but they are second class citizens. Watawatumia tu kuwaburudisha lakini hawatakaa washike positions muhimu kwenye nchi kama mambo ya kibenki, mahakama, wala kumiliki nyenzo za kiuchumi. Kule jamaa wanadharauliwa. Kuna likizo moja Pogba alitembelea nchi moja ya Africa, siikumbuki jina, watu walikuwa wanamshangilia yani akajihisi kama ambavyo Messi anajihisi akiwa Argentina. Wazungu hawana shobo na watu weusi, juzi watu wamevamia nyumba ya Sterling. Aubameyang naye alivamiwa kule Barcelona.
Mahitaji ya binadamu sio pesa tu, kuna kuthaminiwa utu pamoja na heshima. Africa ingefika mbali kisoka kama wachezaji weusi wangechezea timu zao za asili. Wangepata mafanikio na kuimbwa kama mashujaa wa mataifa yao. Eti Bukayo Saka ni mwingereza😀😀😀.
Africa tuache rushwa na ukiritimba. Waafrica wengi wanakimbia matatizo huku kwao na kuzamia ulaya walau wapate ugali. Kule wanahangaika na kutupiwa mfupa wa kuchezea timu za taifa za wazungu. Ukoloni unaendelea sema kwa sura nyingine. Babu zetu walitumikishwa mashambani, viwandani na majumbani, wajukuu zao wanatumikishwa uwanjani.
Waafrika tusiposolve matatizo yetu wenyewe na kupafanya pawe mahali pazuri basi tutaendelea kutawaliwa na hao jamaa hadi tunaingia kaburini.
Niende kwenye mada husika. Timu ya Ufaransa imejaa wachezaji wa Africa. Nimeona waafrica wengi wakiishabikia Ufaransa kwa sababu imejaza watu weusi. Mimi naona huo ni utumwa. Hawa jamaa weusi wanaochezea Ufaransa na mataifa mengine ya Ulaya hawana haki sawa na wazungu. Wana uraia sawa but they are second class citizens. Watawatumia tu kuwaburudisha lakini hawatakaa washike positions muhimu kwenye nchi kama mambo ya kibenki, mahakama, wala kumiliki nyenzo za kiuchumi. Kule jamaa wanadharauliwa. Kuna likizo moja Pogba alitembelea nchi moja ya Africa, siikumbuki jina, watu walikuwa wanamshangilia yani akajihisi kama ambavyo Messi anajihisi akiwa Argentina. Wazungu hawana shobo na watu weusi, juzi watu wamevamia nyumba ya Sterling. Aubameyang naye alivamiwa kule Barcelona.
Mahitaji ya binadamu sio pesa tu, kuna kuthaminiwa utu pamoja na heshima. Africa ingefika mbali kisoka kama wachezaji weusi wangechezea timu zao za asili. Wangepata mafanikio na kuimbwa kama mashujaa wa mataifa yao. Eti Bukayo Saka ni mwingereza😀😀😀.
Africa tuache rushwa na ukiritimba. Waafrica wengi wanakimbia matatizo huku kwao na kuzamia ulaya walau wapate ugali. Kule wanahangaika na kutupiwa mfupa wa kuchezea timu za taifa za wazungu. Ukoloni unaendelea sema kwa sura nyingine. Babu zetu walitumikishwa mashambani, viwandani na majumbani, wajukuu zao wanatumikishwa uwanjani.
Waafrika tusiposolve matatizo yetu wenyewe na kupafanya pawe mahali pazuri basi tutaendelea kutawaliwa na hao jamaa hadi tunaingia kaburini.