udsm iko out of 10 kitambo sana labda kama TWAWEZA wamepika data
Pole mkuu na TWAWEZA sijui ilikukosea nini.
Ubora wa chuo hutegemea mtu anazingatia nini.
Kwa taaluma, UDSM is the best kwa TZ (kulingana na world wide ranking)
Shida ni kwamba, wale wanaopenda kutafuniwa hupaona udsm pako hovyo.
Lecturers pale wanakupa skeleton tu, tena imechoka sana. Katafute mambo mengine mwenyewe.
Nakumbuka nikiwa first year, nilihudhuria lectures kwa mwezi na wk 2, sina cha maana ninachoandika. Nikajipa moyo kwamba hawaanza kufundisha. Mara tunatangaziwa test. Ikabidi nianze kuhaha kutafuta madesa na uyeboyebo wangu.
Mwendo ulikuwa huo huo hadi tunamaliza. Ttuliojituma tulitoka na kitu, waliozembea, wakavuna chao.
Hata hivyo ningeshangaa kama watu wataacha kuvisifia vyuo walivyosoma na kuvisifia vingine.
Wakati mwingine hufanya hivyo kwa sababu ndoto za kuingia kwenye hivyo vyuo (wanavyoviponda) hazikutimia. Ni kama mtu alitoswa na mwanamke halafu anaanza kumsema vibaya.
Tuuneshe ubora wa vyuo vyetu ktk jamii zetu kupitia taaluma zetu.
Kuna watu wanadai wamefanya kazi na graduates from udsm kuwa ni weupe, lkn wanasahau kuwa kuna baadhi ya graduates wa vyuo vingine pia ni majanga.
Maisha yako ya kiuanafunzi chuoni hueweza kuamua aina ya mtaalamu atakayepatikana.
NB: TWAWEZA hawajawahi kufanya ranking ya vyuo vya elimu ya juu Africa.