Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
MWANAKIJIJI.
Jana kwenye mjadala wa Wangwe kusimamishwa na Chadema ukurasa wa 52 ulisema maneno yafuatayo, nakunukuu,

'LINAPOKUJA SUALA LA UKABILA NA UDINI UPANDE WANGU, IAM VERY STRICT AND FOCUSED KWANI HOFU YANGU NI KURUHUSU KUTENGENEZA CHUKI HATA ISIYO NA MSINGI'
mwisho wa kunukuu au rejea maneno yako nayaambatanisha hapa. chinihttps://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=14998&page=52

Swali baada ya kuweka mchango wako kule umekuja hoja kufungua mjadala wa kidini ambao kule kwenye ukabila ulijumuisha kwa kusema kuwa ni KURUHUSU KUTENGENEZA CHUKI HATA ISIYO NA MSINGI. kauli hizi mbili za kutatanisha umezitoa siku moja muda tofauti,hatukuelewi unakusudia nini au tushike lipi?

Hivi ni wapi mimi nimesema CCM kuna udini? Angalia hoja ya kwanza Mgagagigikoko don't project what you think of me na kufikiri nimesema kitu ambacho sijasema.
 
wewe sasa ndio unazidi kuharibu kabisa. Huwezi kutetea ccm kuwa chama cha kiislam sasa hivi kwa vile tu wakati wa mkapa kilikuwa cha kikristo. Hii bado haibadili hii dhambi ya kuangalia watu kwa misingi ya ukabila na udini.

Sijasema kuwa Mkapa alikuwa na CCM ukristu wala Kikwete ana CCM uislam,nimetoa data zichambuliwe kama alivyotoa Mwanakijiji ili aende zaidi unapofanya utafiti unaanzia kipindi fulani hadi fulani tuseme 1995-2010. huwezi kusema au kufanya utafiti bila data, lakini nakukumbusha dhambi za Udini Kikwete hana wasaidizi wake wa kazi kiserikali alikuwa Lowassa mkristu akaja Mizengo PINDA mkristu wa kushinda akipokea misalaba makanisani karibu wiki mbili za uwaziri mkuu alikuwa akipokea misalaba na Katibu mkuu kiongozi Luhanjo- mkristu kwenye serikali, kwenye chama yuko na Msekwa-mkristu.Umoja wa vijana kuna Emanuel Nchimbi mkristu, hadi jumuiya ya wazazi mkristu

Mkapa alikuwa na Sumaye mkristu kama waziri mkuu,Martin Lumbanga katibu mkuu Ikulu alikuwa mkristu, na MALECELA JOHN kwenye chama kama makamu mwenyekiti nae ni mkristu,Mwenyekiti wa umoja wa vijana mkristu Bwana Nchimbi.

Mwanadani wa Kikwete ni waziri Membe mkristu na Gavana Benno Ndulu mkristu,

Wakati wandani wa Mkapa walikuwa Daniel Yona Mkristu na Basil Mramba Pesa Mbili mkristu,Martin Lumbanga-mkristu,Daudi Balali Mkristu hawa ndio best wa Mkapa.

Fanyeni utafiti vizuri makatibu wakuu,mawaziri,wakurugenzi wa mashirika ya Umma,maafisa tawala wa mikoa,wilaya na wakuu wa wilaya kipindi cha Kikwete ikiwa waislam wengi basi mumtuhumu na Udini,Fuatilieni teuzi za Lowassa na pinda hasa alipokuwa TAMISEMI alirundika watu wa dini gani?
kamati kuu si KIKWETE aliowaweka hao wahusika, naomba time frame work ya utafiti wa kidini kuanzia uhuru au 1995-2008? lazima utafiti uwe na muda maalum.
 
Last edited:
Kwa maana hiyo unataka kusema kirefu cha CCM ni Chama Cha Mujahidin. Mimi simo!!!! Tehe!! tehe!! tehe!! Week end njema!!!!!
 
Sijasema kuwa Mkapa alikuwa na CCM ukristu wala Kikwete ana CCM uislam,nimetoa data zichambuliwe kama alivyotoa Mwanakijiji ili aende zaidi unapofanya utafiti unaanzia kipindi fulani hadi fulani tuseme 1995-2010. huwezi kusema au kufanya utafiti bila data, lakini nakukumbusha dhambi za Udini Kikwete hana wasaidizi wake wa kazi kiserikali alikuwa Lowassa mkristu akaja Mizengo PINDA mkristu wa kushinda akipokea misalaba makanisani karibu wiki mbili za uwaziri mkuu alikuwa akipokea misalaba na Katibu mkuu kiongozi Luhanjo- mkristu kwenye serikali, kwenye chama yuko na Msekwa-mkristu.Umoja wa vijana kuna Emanuel Nchimbi mkristu, hadi jumuiya ya wazazi mkristu

Mkapa alikuwa na Sumaye mkristu kama waziri mkuu,Martin Lumbanga katibu mkuu Ikulu alikuwa mkristu, na MALECELA JOHN kwenye chama kama makamu mwenyekiti nae ni mkristu,Mwenyekiti wa umoja wa vijana mkristu Bwana Nchimbi.

Mwanadani wa Kikwete ni waziri Membe mkristu na Gavana Benno Ndulu mkristu,

Wakati wandani wa Mkapa walikuwa Daniel Yona Mkristu na Basil Mramba Pesa Mbili mkristu,Martin Lumbanga-mkristu,Daudi Balali Mkristu hawa ndio best wa Mkapa.

Fanyeni utafiti vizuri makatibu wakuu,mawaziri,wakurugenzi wa mashirika ya Umma,maafisa tawala wa mikoa,wilaya na wakuu wa wilaya kipindi cha Kikwete ikiwa waislam wengi basi mumtuhumu na Udini,Fuatilieni teuzi za Lowassa na pinda hasa alipokuwa TAMISEMI alirundika watu wa dini gani?
kamati kuu si KIKWETE aliowaweka hao wahusika, naomba time frame work ya utafiti wa kidini kuanzia uhuru au 1995-2008? lazima utafiti uwe na muda maalum.

ni nani aliyeleta suala la Uislamu na Ukristu kwenye mada hii? Kwanini mmekimbilia Uislamu na Ukristu...
 
1) Mwanakijiji naona hapa unataka kulazimishia jambo. Ningekuona analytical zaidi kama jitihada uliyofanya kucalculate hii proportion ungefanya hivyo hivyo kujua asilimia ngapi ya wanachama wa CCM ni waislamu na ni asilimia ngapi ni wakristu. Ili hii proportionality principle yako iwe valid ni lazima ufanye hivyo. Nachojua kwa hesabu ya watu Tanzania waislamu wanazidi wakristu. Usijisingizie kuwa hujasema na kwamba umeuliza swali kwa sababu ya hii alama ya kuuliza. Maelezo yako wazi kuwa unatoa hoja na sio swali.

UFAFANUZI:

- Assume asilimia 70 ya wana CCM ni waislamu na asilimia 30 ni wakristu. Utafanya pia representation 50/50?

- Na kama asilimia 90 ni wakristu na asilimia 10 ni waislamu utafanya pia 50/50

So ili nikuamini nashauri utujulishe hili.

2) Mwanakijiji unaasume kwamba iwa CCM wanawakilisha maslahi ya dini. Hawa sio viongozi wa dini. Waislamu na wakristu si lazima wapingane kwenye sera hata kama zinahusu dini. Nakumbuka Mrema ni mkristu lakini anasaport anasupport Mahakama ya Kadhi.

3) Huwezi kujua wakristu na waislamu kwa kuangalia majina. Kuna wengine wana majina ya kiislamu lkn hawajui msikiti uko wapi, wengine majina ya kikristu lkn hawajui kanisa liko wapi. Wengine wanahudhuria matukio ya kidini km social ocassion tu na sio religious. Sasa unaweza kutuambia ni wangapi kati ya hao uliotaja ni practioners wa dini zao?
 
Mwanakijiji/mgaya/mkandara
Naomba mwongozo wa JF

Hizo ID ni halali kutaja watu wa ccm na marufuku kutaja watu wa CHADEMA.??
huu sasa uhuni
namimi nitaanza kuwataja ID zenu mkinifungia na UNBLOCK ama na ninyi na wafungia vilevile.

Kule kwenye mjadala wa Wangwe na Chadema, nilikanywa ni marufuku kumtaja mtu jina kuna watu walikuwa wakimuhisi Mpaka kielewe ni mtu wa chama fulani, mimi kuna member anayeshabikia Chadema akaniambia kuwa kuna sheria za JF ukimtaja mtu utafungiwa na sheria msumeno,

lakini katika mjadala huo huo watu wakataja kuwa HOLLO ni CHENGE na Cheyo hakuna aliesema kuwa sheria zimevunjwa na wala warning haikutolewa na mamoderators,

punde si punde nikatumiwa warning tatu na moderator kuwa nimewatukana watu wa Singida, nimetafuta tusi sijaliona na nimeuliza kwa uwazi wapi nimetukana sijapata jibu toka kwa Moderators hadi leo hii siku ya tatu,

Alianza kutishwa Mtanzania akalegea nikabaki mimi, mara naambiwa nimeongopa niombe radhi na ujumbe huo umeletwa na majina kama manne,

Ukaletwa ushahidi kukazia kauli yangu kuwa nilichosema ni sahihi na huyu mwanachama niliyesema kuwa kasema uongo, ikathibitishwa amewahi kuongopa zaidi ya mara mbili ndani ya forum hii, wenyewe walikuwa wakidai ni MwanaJF mahiri lazima aombwe radhi lakini bila ya wao kuyafanyia utafiti maneno yangu, vitu hivi zinanipa mashaka makubwa sana kama hakuna fursa sawa kwa wote, na hakuna mtu alisema kuwa nilituhumiwa kuwa muongo na sasa imedhihiri kuwa kauli yangu ilikuwa na ukweli mkubwa na nikasema nina mashahidi wengi ila namba moja awe Zitto KABWE.

hapa kuna double standard kama demokrasia ya kuandika tu tunakuwa intamidated jee kina Wangwe kwenye vikao vya siri walikuwa katika hali ngumu sana, ni rahisi kusema kunataka demokrasia au tunapropagate lakini uwazi wa kujadili hapa unafisadiwa mkipata madaraka itakuwaje?
 
ni nani aliyeleta suala la Uislamu na Ukristu kwenye mada hii? Kwanini mmekimbilia Uislamu na Ukristu...

Kwani mada yako hapa sio udini?:


...Katika pita pita yangu na kuchunguza nimegundua kuwa asilimia 65.78 ya uongozi wa Kamati Kuu ya CCM ni watu wa dini moja. Kama udini ni wingi wa watu wa dini moja kwenye ngazi fulani, tunaweza kusema kusema kuwa Kamati Kuu ya CCM ina udini? Je kuna sababu yoyote ya msingi ya kwanini watu 25 kati ya 38 wawe ni wa dini moja? Je imeshindindikana kwa CCM kutafuta njia ya kuweza kugawa nafasi hizi kwa kuangalia uwiano wa dini?

... in this case udini (yaani idadi ya watu wa dini moja mahali pamoja ambayo haina maelezo ya kuridhisha).

Na ukiongolea udini Tanzania, huongelei Ukristo na Uislamu?

Mwnkjj, utajutia hii thread, I tell you!
 
Ukweli ni kwamba, ukianza kuchunguza maeneo au majina au makabila ya watu ili kuangalia kama kuna udini au ukabila basi utajikuta unakosa kanuni kamili ya kufikia hitimisho lako.

Kwa msingi huu, mimi nilisema hapa muda mfupi baada ya uchaguzi wa ccm kuwa ccm ni chama cha kiislam kwa vile viongozi wake asilimia 75 (kwa hesabu zangu na ufahamu wangu) ni waislam.

Pitia na ufafanuzi wangu, wewe umetoa wapi asilimia 75? nijibu na takwimu nilizokupa toka MKAPA.
 
Last edited:
ni nani aliyeleta suala la Uislamu na Ukristu kwenye mada hii? Kwanini mmekimbilia Uislamu na Ukristu...

Aliyeleta Uislamu na Ukristo kwenye mada hii ni yule aliyeuliza hivi: Kamati Kuu ya CCM imejaa Udini?
Tumekimbilia Uislamu na Ukristo kwa kuwa ndizo DINI zilizotamalaki kwenye CC ya CCM tunayoiongelea hapa. Kingunge ambaye hakuwa Muislamu wala Mkristo alipigwa chini uchaguzi uliopita.
 

Kwani mada yako hapa sio udini?:




Na ukiongolea udini Tanzania, huongelei Ukristo na Uislamu?

Mwnkjj, utajutia hii thread, I tell you!

hahahah.. I have been here before my friend na karibu wengi wanaochangia have been here before. Usiwe na shauku sana. Mada yangu hapa siyo ya udini. That is where everybody miss the point while confirming it.
 
Unataka kubisha kuwa hayo majina sio ya kiislam na hivyo kuifanya ccm chama cha kidini?

Mgaya.

Utafiti wako ni finyu nakupa msaada labda upeo wako unaweza kutanuka.
1-Michael Tyson-muislam jina lake limekaa vipi?
2-Freddy Kanute mchezaji wa kimataifa ni muislam jina lake la kiislam?
3-Frank Riberry mchezaji wa Timu ya Taifa ya Ufaransa ni muislam jina lake linaweza kukusaidia kusema yuko dini gani?
4-Bondia Danny Williams ni muislam jina lake linakaa kidini gani?
5-Nicholas Anelka mchezaji wa Chelsea ni muislam jina lake linaelekea kuwa la kiislam?
6-Waziri Sophia Simba jina lake linaoekana kama muislam lakini ni mkristu,
7-DR.Batilda burian jina lake limekaa kidini ipi?

8-Ramadhan Mtoro Ongora ni mkristu muda wote kwa utafiti wako ungesema ni mtoto wa sheikh wa msikiti wa Mtoro,

9-Stephen Nemes masajage kipa wa Yanga na Taifa Stars ni muislam kwa jina utamjua?
10-Tariq Aziz aliyekuwa waziri wa karibu sana na Sadam Hussein ni mkristu wa kuzaliwa,kwa jina lake bila kuwa na utafiti utasema ni muslam(a) utasema ni mwarabu lazima awe muslam(b) jina lake utasema ni la kiislam kwa mujibu wa ubishi wako usio na hoja.

Umsimsahau Malcom X alikuwa kiongozi wa kiislam kwa jina utasemaje? nimekupa sample kidogo kama nisingekutajia watu hao dini gani katika hao 11 niliwataja ungeweza labda wawili tu.
 
Mbona Hollo amekubali yeye CHENGE?
Leo kweli naye naona Kikwete.

Nimekubali wapi?Huwezi kujua the way inavyoniumiza kubambikwa mimi ni nani wakati sivyo!Any way sijui unapata faida gani kuweka hisia fulani ni nani?
Nilisha kuambia mimi siye hao unavyosema kila mara!Sitaki unibambike majina
it hurts me a lot kwa kweli!
Asante
 
mgagagigikoko.. unathibitisha hoja kuwa ukimuona mtu anaitwa Kimaro haina maana ana ukabila! Na ukiona mama anaitwa mama Mushi haina maana ni Mchagga! Na ukimkuta mchagga aliyezaliwa na kukulia usukumani na anaitwa Massawe usije ukakimbilia na kusema anatoka Kilimanjaro! of course, kwenu mtasema anatoka Kilimanjaro kwa sababu ndicho kilichotumiwa kwa Mdee hicho siyo?
 
hahahah.. I have been here before my friend na karibu wengi wanaochangia have been here before. Usiwe na shauku sana. Mada yangu hapa siyo ya udini. That is where everybody miss the point while confirming it.

Kweli mwanakijiji tumekuwepo humu.

Mwanakijiji, Naomba ni hit target directly. Unataka kusema kuwa Anachosema Chacha Wangwe kuwa Chadema imejaa wachaga ni sawa na CCM kuwa na waislamu wengi zaidi?!!!!

Stop spinning:

1. Katiba ya CCM inatoa nafasi ya upendeleo kwa wa Zenj kujazwa zaidi ya wabara ilhali wabara ndio wengi. Katiba ya Chadema haitoi nafasi kwa wachaga kujazwa kwenye nafasi mbalimbali kuliko makabila mengine.

2. Zanzibar kutokana na point hiyo hapo juu; wengi wao ni waislamu. Kwahiyo ukiwapa nafasi ya upendeleo utakuta wengi ni waislamu. Hii ni tofauti Chadema ambao ukiwapa nafasi ya kuteuwa wabunge huteua wanaohusiana au wachaga.

3. Sio CCM tu inailea Zanzibar bali hata serikali yetu ya Muungano inailea Zenj. Swali, kwanini tusiwe na serikali ya TATU?, kwanini kamkoa kamoja kadogo kuliko hata Wilaya ya Ilala in terms of population ina representatives kibao?, Bungeni, Chama chetu na tena wana ka baraza la wawakilishi linalowakilisha mikoa miwili tu?. Think of this.

Ni sahihi wewe ku side na akina Mbowe, lakini sio sahihi wewe ku spin mambo.
 
mgagagigikoko.. unathibitisha hoja kuwa ukimuona mtu anaitwa Kimaro haina maana ana ukabila! Na ukiona mama anaitwa mama Mushi haina maana ni Mchagga! Na ukimkuta mchagga aliyezaliwa na kukulia usukumani na anaitwa Massawe usije ukakimbilia na kusema anatoka Kilimanjaro! of course, kwenu mtasema anatoka Kilimanjaro kwa sababu ndicho kilichotumiwa kwa Mdee hicho siyo?


Mwanakijiji,

You are right on the money ...
 
mgagagigikoko.. unathibitisha hoja kuwa ukimuona mtu anaitwa Kimaro haina maana ana ukabila! Na ukiona mama anaitwa mama Mushi haina maana ni Mchagga! Na ukimkuta mchagga aliyezaliwa na kukulia usukumani na anaitwa Massawe usije ukakimbilia na kusema anatoka Kilimanjaro! of course, kwenu mtasema anatoka Kilimanjaro kwa sababu ndicho kilichotumiwa kwa Mdee hicho siyo?

Acha fix. Kama atakuwa sio Mchaga atakuwa ana relate na mchaga; hence ukabila unabakia pale pale.

We huwezi kuwa msukuma na ukamuoa mhaya mtoto mkamwita KIMARO au Mushi..,........

Na ikitokea umefanya hivyo basi ujue kuwa huyu MUSHI alikuwa au ni rafiki yako mkubwa sana, bado upendeleo unakuwepo hapo.

Mzee tafuta mbinu mbadala ya kuspin. Naona unawapeleka vijana baada ya kuona wazee wenzako WAMETINGWA.

Tuendelee kutofautiana kwa amani...

Cheers
 
Nadhani tuliangalie kwa mapana zaidi, Mzee mwanakijiji hajasema ukristo na uislam, kuna dini nyingine ya ufisadi, it is possible that 65% ni waumini wa ufisadi, I admit.
 
Udini hapa nautafsiri kuwa ni wingi wa watu wa dini moja kwenye ngazi fulani ya uongozi ukilinganisha na ngazi nyingine. Katika pita pita yangu na kuchunguza nimegundua kuwa asilimia 65.78 ya uongozi wa Kamati Kuu ya CCM ni watu wa dini moja. Kama udini ni wingi wa watu wa dini moja kwenye ngazi fulani, tunaweza kusema kusema kuwa Kamati Kuu ya CCM ina udini? Je kuna sababu yoyote ya msingi ya kwanini watu 25 kati ya 38 wawe ni wa dini moja? Je imeshindindikana kwa CCM kutafuta njia ya kuweza kugawa nafasi hizi kwa kuangalia uwiano wa dini?

Nikiwa mtu mwenye maslahi ya pekee kwenye CCM naona jambo hili si zuri na litazua manung'uniko yasiyo ya lazima. Kama kikundi, taasisi, au jumuiya fulani ina watu wenye sifa moja inayolingana, sifa ambayo inawatofautisha na watu wengine hasa ya vitu kama kabila, rangi, au dini basi mahali hapo ni pa kuangaliwa kwa karibu.

Katika siasa, tukitumia "Wangwe's Doctrine" kuwa endapo asilimia 50 ya watu wenye sifa hizo wakakutwa mahali pamoja ni ukabila/ukanda basi ni wazi mahali ambapo pana asilimia 65 ya watu wenye kulingana sifazao kutofautishwa na wengine basi napo patakuwa na tatizo, in this case udini (yaani idadi ya watu wa dini moja mahali pamoja ambayo haina maelezo ya kuridhisha).

Mkuu Mwanakijiji,

Maoni yako yamenipeleka mbali sana. Umenikumbusha enzi za TANU ilipoanza.
Waasisi wa TAA na baadae TANU walikuwa na idadi kubwa sana ya Waislamu. Hili halikuwa jambo la kushangaza kwa kuwa harakati hizi zilianzia Dar-Es-Salaam ambako wengi wa wakazi wake ni Waislamu. Kwa hiyo hata idadi ya wafuasi pia walikuwa wengi ni Waislamu.

Uhuru ulipokaribia, nafasi muhimu za uongozi ghafla zikaanza kuchukuliwa na waliokuwa Wakristo. Mmoja wa wazee waasisi Sheikh Suleiman Takadiri, katika mkutano wao pale ofisi za makao makuu ya TANU mtaa wa Lumumba, akamuuliza Mwalimu Julius Nyerere, imekuaje mbona ghafla hivi tunaona idadi ya Wakristo katika viti nyeti inazidi ya Waislamu na sisi ndio tuko wengi zaidi?

Mwalimu akamgeuzia kibao kwa kumwambia, wewe mdini sana. Umejuaje kuwa idadi ya Wakristo katika viti muhimu vya uongozi iko juu zaidi kuliko ile ya Waislamu. Bila shaka huo udini wako ndio uliokuacha wewe unahesabu watu na dini zao wakati sisi tunashughulikia harakati za kupata uhuru.

Mzee Mwanakijiji, ukianza kuhesabu watu kwa makundi hutaweza kujiridhisha wala kumridhisha mwingine. Wewe unahesabu uwiano wa watu kwa dini zao. Mimi labda nitaanza kuhesabu watu kwa umri wao. Na mwingine ataanza kuhesabu watu kwa jinsia zao. Labda kuna na mwenzetu mwingine ataanza kuhesabu watu kwa rangi na nywele zao. Kweli tutafika?

Kama chama kina watu wengi wa kabila moja au wa mkoa mmoja thautawatendea haki kama tutawazuia wengine wa kabila hilo au mkoa huo kuingia chama hicho kwa kuwa kina wanachama wengi wa kabila hilo au wa mkoa huo? Hali kadhalika dini, jinsia au umri?

Kwa mtaji huo huo, huwezi kuwazuia watu wa kabila fulani, mkoa fulani, umri fulani ( wazee kwa vijana) dini fulani au rangi fulani wasigombee nafasi za uongozi katika chama chochote, kwa sababu tu kuna viongozi wengi wanaofanana nao kikabila, kimkoa, kidini. kijinsia, kiumri au kirangi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom