Tatizo ni Zenji Factor. Nadhani Zenji wanachangia 50% ya members wanaoingia kwenye CC. Hapo sijaweka wale ambao wanaingia huko kwa heshima ama kwa nyadhifa zao (viongozi wakuu wa Chama wa pande zote mbili, marais wastaafu na wazee wa chama kama akina Kawawa).
Ukishaweka hiyo Zenji factor automatically lazima utaishia kwenye conclusion ya Mwanakijiji.
Labda swali la kujiuliza ni kwanini Zenji inapewa nafasi sawa na Bara?
Kwa kweli kwa MAONI yangu hili ndilo JIBU linalojitosheleza sana kwenye MADA hii na MSINGI wake ni KATIBA yenyewe ya CCM. Na CC ya CCM imekuwa hivi nadhani tangu 1977 pale TANU yetu na ASP yao vilipoungana. Bara (Kwa maana ya TANGANYIKA) tuli- sacrifice mambo mengi sana kwa ajili ya MUUNGANO wetu. Si unajua hata TANGANYIKA haipo ingawa ZANZIBAR ipo?