Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
Mi nawambiaje...Kama kweli Masaka ni Makamba...Basi anamjuwa Jmushi...Kwani yeye ndiye aliyenirudisha hapa jf!
Na kuna waliopiga ndogo ndogo sana tuu ili nifungiwe moja kwa moja!
Madhali jf ni HURU...BASI TUTAPAMBANA!
MI MZALENDO SINA CHAMA! SIPIGANIIMASLAHI YA MTU WAL CHAMA...BALI HAKI YA MTANZANIA!
GOD WILLING....WE..."WE THE PEOPLE" WE WILL BE VICTORIOUS!
 
Umefumbwa fumbo.

Mwanakijiji anatumia lugha ya tasnifa.

Anataka kujenga hoja-kejeli kwamba kama Chadema kuna ukabila kwa sababu Chacha Wangwe kasema kuna Wachaga/Wapare watano kati ya sita basi hata CCM kuna udini kwa sababu wajumbe 25 kati ya 38 ni wa dini moja.

Tatizo la hoja-kejeli yake ni kwamba ame distort hoja ya Wangwe, kaitengeneza upya, halafu akaipa jina, Wangwe's Doctrine.

Wangwe hakusema anataka wajumbe waganywe sawa kwa sawa. 6 gawanya kwa 26 haigawanyiki. Wangwe kauliza utakuwaje Watu 5 kati ya 6 watoke eneo moja.

Wangwe na wenzake hawakuwa na mikoa miwili tu ya kugawanya nafasi kama dini zilivyo, bali 26. Walikuwa na uwezo mkubwa wa kuzigawa.

Wangwe hakutumia kigezo hicho kimoja tu cha 5 baina ya 6, ila ni shutuma ambayo haikuanza na uchaguzi wa Wabunge wa 2005, na pia amedai hata madereva na wafagiaji CHADEMA ni wa eneo moja.

Mwanakijiji ame distort alichosema Wangwe.


Sorry bro! my calculation says it's 0.23076923076923076923076923076923
 
Kwa ndogo ndogo nilizopata ni kwamba Masaka ni user name ya babu yetu Makamba! Kwa angalia sana Mama, usijetumiwa "vijiunga" online! Na wao wanafanya research na kuadvance science yao, be careful.

Mwanakijiji/mgaya/mkandara
Naomba mwongozo wa JF

Hizo ID ni halali kutaja watu wa ccm na marufuku kutaja watu wa CHADEMA.??
huu sasa uhuni
namimi nitaanza kuwataja ID zenu mkinifungia na UNBLOCK ama na ninyi na wafungia vilevile.
 
Mimi nafikiri mwanakijiji ameweka swali ambalo ni tata.

Unauliza kwamba NEC imejaa udini.

Udini ni neno zito na pana, kwa maana kwamba inamaannisha kwamba pale penye kikao cha NEC panajumuisha mambo mengi ya kidini zikiwemo swala na mengine.

Lakini hapo hapo inaonekana kwamba NEC imejaa waislamu ambao wanaonekana ndio wenye kutoa maamuzi mazito ya kuiendesha nchi kupitia CCM.

Sasa kuhusu Wangwe's Doctrine naona kwamba pana suala la ukabila kwamba kamati kuu ya CHADEMA imejaa kabila fulani tu na sio mchanganyiko.

Mimi naona msajili wa vyama apitie tena katiba za vyama vyote vya siasa kikiwemo CCM aangalie kama kuna UDINI au UKABILA.
 
Kwa ndogo ndogo nilizopata ni kwamba Masaka ni user name ya babu yetu Makamba! Kwa angalia sana Mama, usijetumiwa "vijiunga" online! Na wao wanafanya research na kuadvance science yao, be careful.

....hivi ndugu, kuna haja gani ya ku-reveal kuwa Masaka ndiye Makamba (uwe ukweli au siyo ukweli)?!

....akina Zitto wamekuja hapa na majina yao kamili kamili, wanasababu zao, nasi wengi wetu tuna majina ya ki-jf-jf, nasi tuna sababu zetu.
 
he he he he heeeeeeeeeeee, hahahahhahahahhaaaaaaaa, kwi kwi kwi kwiiiii, Peasant, kwa kweli nimechaka sana ee.

na msee namwacha aende tu huko chadema, ila krismas lasima aniletee kitenge na gauni ya dukani eeh.

Chadema ikipata urais eeh, cha kwansa ni kuchuak pesa palle benki, Mushi si ndio meneja pallllee eeh, na kununua stout ya kubeba majani ya ng'ombe mbe. Ikulu itahamia pale shanti town eeeh, yaani kiboriloni kutajengwa mall wa wausa mitumba wote, wausa kiti moto, kisusio na mbusi choma wote watajifinjari huko, hakuna mambo ya fioski tena.

Hili ni waso suri sana mamangu! Ni fizuri wasee wakawa wanapata mtori wao na mbusi kidogo kwa nafasi ati. Na utawapata wale wapenda mtula wote wa pale Polisi me, polisi mesi kweli.
Itabidi pia tuweke Metro ya kwenda kule Marangu kwansa, hao Wapalestina (Wamachame) itabidi wasubiri kwanza.
 
Mbona Hollo amekubali yeye CHENGE?
Leo kweli naye naona Kikwete.
 
Mafisadi Yamevamia Jf Na Ukabila Na Udini!
Karibuni Sana Jf...eti Peasant?!
UNAJUWA MAANA YA PEASANT WEWE?
 
....hivi ndugu, kuna haja gani ya ku-reveal kuwa Masaka ndiye Makamba (uwe ukweli au siyo ukweli)?!

....akina Zitto wamekuja hapa na majina yao kamili kamili, wanasababu zao, nasi wengi wetu tuna majina ya ki-jf-jf, nasi tuna sababu zetu.


Mwongozo wa JF haya mambo ndiyo ufisadi wenyewe

Mimi kule nimetaja ID ya mtu nikakemewa vikali nakupewa vitisho vya kufungiwa kwa vile tu nilitaja mtu wa CHADEMA.
Hapa watu wanatajwa ID za watu wala hawakemewi kwa vile wanatoka CCM ,wakemeeni hawa watu tafadhari.

Lasivyo ule msamaha nilioumba kule ni batili na mimi nitaanza kutaja ID za watu kila nitapotaka.
 
Mwanakijiji,
Niliposoma post yako mara ya kwanza nikaona sasa umeanza kuchanganyikiwa ila baadaye nimegundua unataka kuonyesha kuwa pamoja na kuwa CHADEMA ina wakurugenzi wengi kutoka Kilimanjaro lakini haimaanishi kuwa ni chama chenye ukabila.
Kwanza lazima uelewe wajumbe wengi wa Kamati kuu wanapigiwa kura na wagurugenzi wa CHADEMA wanateuliwa. Kwa hiyo kidogo hapo kunakuwa kuna ulakini. Pili, kuwa na udini ni kutumia misingi ya dini fulani kuendesha mambo yako. Labda tu utueleze ni misingi gani ya kidini ambayo kamati kuu ya CCM imetumia kuendesha CCM. Na watu hawaishutumu kamati kuu kuwa na udini pengine unaweza kuwa mtu wa kwanza kwa propaganda zako binafsi lakini watu wanaishutumu CHADEMA kwa ukabila. Pia labda tu unieleze kwa nini watu hawaishutumu CUF kwa udini lakini wanaishutumu kwa upemba pamoja na kuwa na wanachama wengi wa dini moja?
Labda tu kwa kumalizia, siyo watu wote wenye majina ya kikristo ni wakristo. Pengine kwenye kamati kuu ya CCM hakuna mkristo, who knows!
Halafu ukimaliza hii topic jaribu kuonyesha kuwa kwa kuwa ndani ya CCM kuna watu wanaoshutumiwa kwa ufisadi na hiyo haimaanishi kuwa CCM ni chama cha mafisadi. Pia usisahau kuonyesha kwa kuwa Zakayo alikuwa tajiri basi haimaanishi alikuwa fisadi kama ulivyoandika kwenye lile gazeti lenu.
 
Hili ni waso suri sana mamangu! Ni fizuri wasee wakawa wanapata mtori wao na mbusi kidogo kwa nafasi ati. Na utawapata wale wapenda mtula wote wa pale Polisi me, polisi mesi kweli.
Itabidi pia tuweke Metro ya kwenda kule Marangu kwansa, hao Wapalestina (Wamachame) itabidi wasubiri kwanza.

na ile sanamu pale kipleft tutaiondoa isiendelee kuwarusha mbio wau..wauru kweli. Tutajenga njia sa tireni sa chini kwa chini kwenda rombo mkuu, kibosho, uru kishumundu, hadi kule masama, marangu mamba, vunjo na kilema.ushindi kwa chadema mbeee mbele kabisa kweli.
 
Ndugu yangu, Hoja yako itabeba uzito zaidi endapo utatupa stats zote za CCM, km total members, and their distribution by religion, gender, education and other attributes ambazo zinaweza kusababisha jambo liitwalo confounding katika ku-test hypothesis. Kutupatia selective stats ni mbinu ambayo inatumiwa na watu wengi wanaotaka kuonyesha nusu tu ya ukweli!
 
Mwongozo wa JF haya mambo ndiyo ufisadi wenyewe

Mimi kule nimetaja ID ya mtu nikakemewa vikali nakupewa vitisho vya kufungiwa kwa vile tu nilitaja mtu wa CHADEMA.
Hapa watu wanatajwa ID za watu wala hawakemewi kwa vile wanatoka CCM ,wakemeeni hawa watu tafadhari.

Lasivyo ule msamaha nilioumba kule ni batili na mimi nitaanza kutaja ID za watu kila nitapotaka.


Sound like I,ve hit the jackpot!
 
KATIKA kauli ambazo zitawashitua watawala, Waziri Mkuu wa zamani, Jaji Joseph Warioba, amesema nchi ina viongozi dhaifu, umma unanyonywa, rushwa imeongezeka, wezi wa fedha za EPA waanikwe na Rais Msitaafu, Benjamin Mkapa akajibu tuhuma zake mahakamani.
Katika mahojiano maalumu na Raia Mwema, Warioba amesema kuna dalili ya kuwapo watu wakubwa nyuma ya kashfa ya fedha zilizopotea katika sakata la EPA na kwamba yaliyotokea ni wizi wa hali ya juu na baadhi wameghushi na kwamba hatua za kisheria ni lazima zichukue mkondo wake.


26.jpg

JAJI Warioba

"Niliyosoma hasa kutokana na taarifa ile ya Serikali, ukiisoma kwa makini unaona kuwa haukuwa ununuzi wa madeni, huo ulikuwa ni wizi wa fedha za umma," anasema Jaji Warioba.
Anasema kwa mujibu wa taarifa ya Serikali, baadhi ya madeni si madeni bali kuna watu wametumia ulaghai kuchukua madeni ambayo yamekwisha kulipwa na wao kufanya udanganyifu kuyadai.
"Wapo ambao wamefanya hivyo kwa kughushi. Sasa kuna makosa mawili hapo. Wizi na kughushi, ni makosa mazito, na kama nilivyosema wakati ule ilipotoka mara ya kwanza, ukiona makampuni ambayo yametajwa si makampuni makubwa na mengi yake yaliundwa kwa kazi hii tu," alisema katika mahojiano ambayo sehemu yake ya kwanza imechapishwa katika kurasa za 12 na 13 za toleo hili.
Akionyesha kuwapo kwa watu wakubwa nyuma ya wizi wa fedha za EPA, Warioba anasema biashara ya kununua madeni inataka mtu mwenye fedha na mwenye ujuzi wa biashara hiyo lakini makampuni yaliyoorodheshwa na serikali mengi yanamilikiwa na watu wa kawaida kabisa wasio na uwezo huo.
"Kampuni hizi ni ndogo, watu wenye kampuni hizi wameandikwa watu wenye majina ya kawaida. Kwa mtu yeyote mwenye busara atajua hii ni hadaa tu. Wanaoshughulika hawakujiandika kwenye kampuni hizi, wamechukua watu wengine tu. Kwa hiyo, kuna kazi, kuna kazi ya kuwatafuta hawa wazito waliokuwa wanahusika. Na kama ni wazito na wameingia katika wizi wa mali ya Taifa na kughushi, suala hili ni zito kuliko tunavyoliona," anasema na kuongeza;
"Mimi naamini kama kweli tunaishughulikia kwa nguvu zote, EPA ni kubwa kuliko Richmond, kuliko haya yaliyotokea. Kwa hiyo tutangojea matokeo. Na hapa kwa kuwa walau ushahidi wa kawaida upo, taarifa zinasema zile nyaraka zilizowezesha madeni hayo kununuliwa ni za kughushi, basi unaanzia hapo. Ukihakikisha kwamba ni za kughushi, kwamba haya madeni hayakuwapo, ukithibitisha kwamba hili deni halikuwapo sasa huyo aliyechukua fedha hizo alitumia wapi?"
Alisema akiwa kama raia mwema wa Tanzania anasubiri kwa makini kuona matokeo ya EPA, na kuongeza kwamba kama kweli nia ya kusafisha ipo, ni lazima waliofanya makosa wapatikane na kushughulikiwa na si wale waliotangulizwa.
"Mimi sijui utaratibu wanaotumia. Lakini kwa utaratibu wa kawaida, mimi nilikuwa Mwanasheria Mkuu wa nchi, kwa suala hili la jinai unalishughulikia linakwenda mahakamani. Adhabu inatolewa pamoja na kurudisha hizo fedha, hilo ndilo nalitarajia," anasema.
Anasema kwa kawaida hatua za kisheria ni lazima zichukuliwe na kwamba unapokwenda mahakamani unaweza kutumia sheria kurudisha fedha zilizoibwa hata ikibidi kufilisi wahusika.
Hivi karibuni timu iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kushughulikia waliochukua fedha za EPA ilieleza wazi kwamba imekua ikipokea fedha kutoka kwa watuhumiwa kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kuepuka kupoteza fedha hizo huku wanaozirejesha wakiendelea kuwa siri.
Timu hiyo ya Rais inaongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, akisaidiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Saidi Mwema, na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Edward Hosea, wote wakisaidiwa na maofisa kutoka ofisi zao na kutoka asasi nyingine za umma.
Akizungumzia kitendo cha viongozi hao wa juu wa dola kufanya mazungumzo na watuhumiwa, Jaji Warioba anasema; "Kwamba hawa ndio kweli viongozi wa ngazi ya juu wa vyombo vya dola vinavyoshughulika na uhalifu wanafanya kazi hiyo. Imani yangu ni kwamba hawatapinda sheria. Wakipinda sheria tutakuwa tumeleta madhara makubwa sana kwa nchi hii. Kwa sababu wananchi lazima kwa upande wa sheria waamini ofisi ya Mwanasheria Mkuu, ni lazima waamini ofisi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, lazima waamini ofisi ya TAKUKURU."
Warioba anasema watendaji hao wa dola wakipinda sheria, imani ya wananchi itapungua na hivyo ni jukumu lao ni kubwa, na kwamba yeye ana imani kwamba hawatapinda sheria.
Akizungumzia hali ya kisiasa ya nchi kutokana na kukwama kwa mambo mengi ikiwamo muafaka wa kisiasa Zanzibar na kuibuka kwa wimbi kubwa la tuhuma za ufisadi, Jaji Warioba anaonekana kutokua na imani na hali hiyo na anakiri kuwapo kwa udhaifu katika uongozi wa juu wa kitaifa.
"Kama nilivyosema, kila mtu ni kuzungumzia ufisadi, hata mafisadi wenyewe, maana ukiona wote hawa wanaozungumzia, huwezi kusema ni watu safi, pamoja na vyombo vya habari, navyo haviwezi kujisifu. Wengine wanaoandika juu ya ufisadi ndio hao hao waliokuwa wakichukua fedha za hawa, wanawaandika kuwa ni wazuri wakati wa uchaguzi. Walikuwa wakiwapamba. Kwa hiyo kuna wengine ni unafiki tu, ama ni ufisadi na wenyewe," anasema.
Warioba anapongeza juhudi zinazofanywa na vyombo vya habari na wabunge katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi lakini anaonya vita hiyo isitumike kufunika madhambi yaw engine ama kuwaumiza baadhi yao.
"Sina hakika kama wote wamezinduka hivi. Jana walikuwa wanasema hakuna rushwa, hakuna ufisadi. Leo ndiyo wako msitari wa mbele wanatafuta mafisadi na ukiangalia zaidi ni viongozi. Na hasa wabunge ndio wanaongoza vita hii. Ni vizuri Bunge liongoze lakini je, tunawaamini wote? Kwamba nia yao hasa ni kumaliza ufisadi au kuna sababu nyingine?
"Ikifika mahali tuwaulize hawa ambao sasa wanaonekana wana uchungu sana na ufisadi. Mwaka 2005 tuliona yaliyotokea. Hivi ni wangapi ambao wako safi? Mwananchi akimwuliza mbunge wake, na hii inawezekana kwa zaidi ya nusu ya wabunge, kwamba mbona wewe ulikuja na fedha nyingi sana kwenye uchaguzi na wewe si tajiri, ulizipata wapi?" anahoji Jaji Warioba.
Anasema wamo wengi ambao ni sehemu ya uongozi, na hivyo isije tokea mapambano ndani ya uongozi yakageuzwa kuwa ni vita ya kweli kumaliza ufisadi.
"Mimi nataka niwe na uhakika tukifika mwaka 2010 tuweze kuchagua viongozi safi, tusipate viongozi ambao katika mchakato wa uchaguzi watakwenda na takrima kwa sababu kama wanakwenda na takrima wamezipata fedha hizo kwa ufisadi," anasema.
Akizungumzia muafaka kati ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF), Jaji Wariona anasema tatizo kubwa ni mgawanyiko katika uongozi. Anasema wapo ambao hawataki muafaka wanaona njia ni kusema tupate maoni ya wananchi wakitarajia kwamba wananchi watakataa.

Kuhusu wanaotishia kurejea kwenye Afro Shirazi Party (ASP) kuliko kuingia katika Muafaka na CUF, Warioba anasema hivyo ni vitisho visivyo na maana katika mazingira ya sasa kwani hata wakiachwa hawana uwezo huo na kwamba tatizo kubwa ni udhaifu wa viongozi.
"Zaidi wanaosema warudi ASP ni watu wa Zanzibar, lakini nadhani pia kuna udhaifu katika viongozi Bara. Wakiisha kusikia madai hayo ya ASP, wanasema jamani waachieni mambo yao! Lakini haya si mambo yao, ni mambo ya nchi. Zanzibar ni sehemu ya Tanzania, likitokea tatizo Zanzibar ni tatizo la Tanzania. Hawa wanaosema waachieni haya ni mambo yao ni viongozi dhaifu," anasema na kuongeza;
"Hilo ni suala muhimu, hapo ndipo uongozi unapohitajika. Huwezi kukwepa. Uongozi kazi yake ni kuamua mambo mazito, na wakati wote unaweza kuwa na wasiwasi, lakini unaamua kwa maslahi ya taifa. Hata kama katika kuamua huko unahisi kuwa kuna baadhi watakulaumu. Usiogope lawama, dira yako iwe kuwa hii ni kwa manufaa taifa ama hapana. Manufaa ya Taifa sasa hivi ni kumaliza mpasuko wa Zanzibar. Lolote linalohitajika kumaliza mpasuko huo ni vizuri viongozi wakachukua uamuzi, utakuwa ni mgumu lakini ni wajibu wao kuchukua uamuzi."
Pamoja na kuonekana kukwepa kumshutumu Rais Mstaafu Mkapa, Jaji Warioba anasema kinga waliyonayo viongozi akiwamo rais ni ya kisiasa tu, na hivyo kwake yeye suala la kinga ya kisheria si tatizo bali ukweli na uhakika wa tuhuma zinazomgusa kiongozi husika na kwamba ni mahakama inayoweza kutoa uamuzi wa haki.
"Nimeona wanaandika na nimeona mjadala mkubwa tu unaolenga kwenye immunity. Mimi nafikiri suala hilo si la msingi kwa sasa hivi. Na mjadala unalenga kwamba aseme, naona si la msingi. Kwa sababu hatutaki kwamba huyu awe tried na vyombo vya habari. Maana hapa naona kama ni trial kwenye vyombo vya habari.
"Waseme ni kosa gani, amefanya kwa msingi wa sheria gani, sasa waendelee. Sasa mengi wanayosema ni ya kisiasa. Yakisemwa ya kisiasa unataka mtu awajibike kisiasa. Kama ni kosa la jinai, waseme amevunja wapi sheria, lakini kusema kweli mimi sioni kwa vyombo vya habari kusema yote haya na wanachotaka ni kwamba ajitetee, ajitetee wao ndio wamekuwa Mahakama?" anahoji Jaji Warioba ambaye amewahi kufanya kazi kwa karibu na Mkapa.
Warioba anasema vyombo vya habari vinataka kuwa Mahakama na akashauri kwamba kama kuna kosa alilofanya Mkapa ni vyema wakasubiri afikishwe mahakamani ambako atakuwa na nafasi ya kujitetea na kueleza upande wake.
"Immunity nasema sasa hivi siyo issue. Sema kosa lililotendeka. Anashitakiwa lakini wanasema hatuwezi kuendelea kwa sababu kuna immunity. Bila kusema kosa huwezi kufika kwenye immunity. Huwezi kuanza na immunity bila kuwa na kosa, kwa hiyo mimi sitaki kujiingiza katika mjadala wa immunity. Hii ni ya kisiasa tu," anasema

Nashangaa ni kwanini mmeshindwa kuuzingatia huo ujumbe hapo juu!
Narudia..MOJA..HAKUNA HAJA YA UKABILA WALA UDINI
MBILI..Hayo maneno yote mnayoleta hapa ya MWAKYEMBE SIJUI NA LOWASSA...HAYANA DILI KABISA KWANI SHERIA INASEMA KAMATA MAFISADI BILA HATA YA KUJALI KAMA NI RAIS! IE MKAPA!
 
Mwanakijiji,
Niliposoma post yako mara ya kwanza nikaona sasa umeanza kuchanganyikiwa ila baadaye nimegundua unataka kuonyesha kuwa pamoja na kuwa CHADEMA ina wakurugenzi wengi kutoka Kilimanjaro lakini haimaanishi kuwa ni chama chenye ukabila.
Kwanza lazima uelewe wajumbe wengi wa Kamati kuu wanapigiwa kura na wagurugenzi wa CHADEMA wanateuliwa. Kwa hiyo kidogo hapo kunakuwa kuna ulakini. Pili, kuwa na udini ni kutumia misingi ya dini fulani kuendesha mambo yako. Labda tu utueleze ni misingi gani ya kidini ambayo kamati kuu ya CCM imetumia kuendesha CCM. Na watu hawaishutumu kamati kuu kuwa na udini pengine unaweza kuwa mtu wa kwanza kwa propaganda zako binafsi lakini watu wanaishutumu CHADEMA kwa ukabila. Pia labda tu unieleze kwa nini watu hawaishutumu CUF kwa udini lakini wanaishutumu kwa upemba pamoja na kuwa na wanachama wengi wa dini moja?
Labda tu kwa kumalizia, siyo watu wote wenye majina ya kikristo ni wakristo. Pengine kwenye kamati kuu ya CCM hakuna mkristo, who knows!
Halafu ukimaliza hii topic jaribu kuonyesha kuwa kwa kuwa ndani ya CCM kuna watu wanaoshutumiwa kwa ufisadi na hiyo haimaanishi kuwa CCM ni chama cha mafisadi. Pia usisahau kuonyesha kwa kuwa Zakayo alikuwa tajiri basi haimaanishi alikuwa fisadi kama ulivyoandika kwenye lile gazeti lenu.

Haya sasa si mlisema Mbowe anajitolea
kumbe alikodi makusudi helkopita ili matumizi yawe juu ajiripe mafao makubwa angalia hizo namba za sh anazojiripa.Yesu na MAria

Imetolewa mara ya mwisho: 04.07.2008 0037 EAT
•
Baada ya CHADEMA kumwaga ugali...Wangwe amwaga mboga

Habari Zinazoshabihiana
• CCM yagaragaza tena CHADEMA, NCCR 29.02.2008 [Soma]
• Wangwe kuadabishwa na kamati iliyojadili akina Mengi na Malima 10.02.2007 [Soma]
• Mbunge amkomalia Spika 09.02.2007 [Soma]

*Alalamikia kuchafuliwa, ubaguzi wa kikabila ndani ya chama
*Awapa viongozi siku 14 kumsafisha, vinginevyo mahakamani
*Akana kutoa siri CCM, adai Mbowe ndiye hukutana nao faragha

Na Mwandishi Wetu

MGOGORO wa uongozi unaorindima ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umeingia katika sura mpya baada ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho aliyesimamishwa hivi karibuni, Bw. Chacha Wangwe, kuwapa siku 14 viongozi wa chama hicho kuthibitisha madai yao kwamba anashirikiana na CCM kukihujumu, vinginevyo atawafikisha mahakamani.

Bw. Wangwe ambaye pia ni Mbunge wa Tarime kwa tiketi ya chama hicho, aliliambia gazeti hili jana kuwa madai ya viongozi hao yamemchafulia jina na heshima kiasiasa aliyoijenga ndani ya chama hicho kwa gharama kubwa.

Wiki iliyopita katika kikao chake, mjini Dodoma, Kamati Kuu ya CHADEMA chini ya Mwenyekiti wake, Bw. Freeman Mbowe, ilimsimamisha uongozi Bw. Wangwe kwa tuhuma mbalimbali ikiwamo kutoa siri za chama hicho kwa viongozi wa CCM.

Bw. Wangwe alituhumiwa pia kukashifu chama hicho, viongozi na watendaji wake, bila kutofautisha kashfa na ukosoaji wa kisiasa na kiutendaji, kwa kutumia wanachama waliochukuliwa hatua za kinidhamu na vikao halali vya chama hicho.

Tuhuma zingine ni pamoja na kuwatuhumu viongozi wenzake wa juu na watendaji wake kwa kuwahusisha na ukabila na kuvujisha siri za vikao halali vya chama kwa watu wenye lengo la kukihujumu chama hicho.

Akizungumza katika ofisi za gazeti hili Dar es Salaam jana, Bw. Wangwe alipinga madai hayo na kueleza kuwa hayana msingi na kwamba katika kipindi chote, ameipigania CHADEMA kwa nguvu zake zote na gharama kubwa, bila kuogopa mazingira magumu kwenye harakati hizo.

Alisema akiwa kiongozi wa chama hicho wilayani Tarime, alinyakua jimbo hilo na halmashauri ya wilaya hiyo huku 'wapiganaji' wenzake wakijeruhiwa kwa vipigo, kupata vilema vya maisha, kupoteza ajira na hata maisha.

Kutokana na harakati hizo, waliwezesha kupatikana asilimia 64 ya kura za jimbo hilo ambazo zilichangia ushindi wa CHADEMA na kuiwezesha kupata ruzuku ya sh. milioni 66 kila mwezi na viti maalumu sita bungeni vya chama hicho.

Alisema jitihada zake zilimfanya mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, Bw. Mbowe kuibuka na kura nyingi kumzidi mgombea wa CCM, Rais Jakaya Kikwete wilayani humo, kwenye uchaguzi mkuu uliopita mwaka 2005.

Akizungumzia uhusiano wake na Dkt. Amani Kabourou ambaye alikihama chama hicho na kwenda CCM, alisema ni wa siku nyingi hata kabla ya kujiunga na CCM na uhusiano huo haufungamani kwa namna yoyote ile na masuala ya kisiasa kama inavyodaiwa na viongozi wa CHADEMA.

"Dkt. Kabourou nashirikiana naye siku nyingi tangu aliporudi kutoka Marekani, naheshimu uamuzi wake wa kwenda CCM na huo ni uamuzi wake mwenyewe, tangu aende CCM sijakutana naye bali Juni 7 mwaka huu, nilikwenda kwake kuhani msiba wa mama yake mzazi tukiwa na Bibi Maulida Anna Komu," alisema Bw. Wangwe.

Bw. Wangwe alishangaa suala hilo kuhusishwa na hujuma dhidi ya chama hicho na kuzidi kufafanua Katiba ya CHADEMA haina kipengele kinachozuia mwanachama kuwa na uhusiano na wanachama wa vyama vingine, bali tofauti iliyopo ni hoja.

Alimshambulia Mwenyekiti wa Chama hicho, Bw. Mbowe kwa maelezo kuwa amekuwa karibu zaidi na viongozi wengi wa CCM na wakati mwingine wanakutana faragha, lakini kama mwanachama ana uhuru wa kufanya hivyo na hakuna anayempinga kwa hilo.

"Dkt. Slaa (Wilbroad), mkewe ni kada wa CCM aliyekubuhu ni Diwani wa kuchaguliwa wanakaa pamoja, simu, nyaraka zote, wageni wote wanaokuja mama anasikiliza, hawanitendei haki mimi kwa hili," alisema Bw. Wangwe.

Alisema kuengulia kwake ni mkakati ulioandaliwa muda mrefu kumng'oa kwenye nafasi hiyo, kutokana na dhamira yake ya kutaka kufanyika mageuzi ya kweli ndani ya chama hicho.

"Nilisema uongozi uliopo tutaupumzisha, kwani umeshindwa kupeleka chama mbele," alisema Mbunge huyo machachari na kusisitiza kuwa ajenda ya kumsimamisha uongozi haikuwa kwenye mkutano wa Dodoma ila kilichokuwapo ni kuwasilishwa Ripoti ya Tume ya Mzirai, iliyoundwa kuchunguza tuhuma mbalimbali ndani ya chama hicho, lakini suala hilo likaibuliwa.

Alibainisha kuwa tofauti iliyojitokeza kati yake na Bw. Mbowe, ni suala la mgawanyo wa ruzuku kati ya makao makuu kwa upande mmoja na wilaya kwa upande mwingine, jambo alilosema kwa muda mrefu amekuwa akipigia debe chama hicho kujijenga kuanzia chini kwenda juu, jambo linalokinzana na msimamo wa mwenyekiti wake.

"Ninachopigania ni mfumo wa 'bottom up' (kuanzia chini kwenda juu) fedha zipelekwe kwenye vitovu vya mapambano zikajenge chama kwenye maeneo ambayo hakipo, lakini wenzangu wanataka mfumo wa 'up bottom' (juu kwenda chini).

Alisema gharama za kuendesha chama wilayani ni ndogo, kwani endapo kila mwezi zitapelekwa sh. 100,000 zitatosha kulipa pango la ofisi linaloweza kugharimu kati ya sh. 25,000 hadi 30,000 na sh. 70,000 zikabaki kwa matumizi mengine ya ofisi. Mbali na fedha hizo, alishauri pia kutolewa sh. 100,000 nyingine kwa ajili ya kulipa wasimamizi wa ofisi hizo.

"Yeye (Bw. Mbowe) anataka fedha zitumike kwa helikopta, sisemi kwamba helikopta ni kitu kibaya, lakini tuangalie katika mruko tulipata watu wangapi? Lazima tuwe na majimbo, wanachama na matawi ya kutosha, hata kama CCM itatuzidi nguvu, basi angalau tupate majimbo 150, hata ruzuku itapanda.

Alipinga kile alichokiita madeni hewa wanayojilipa viongozi wakuu wa chama hicho kwa madai ya kukikopesha chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, ambapo alisema Bw. Mbowe alidai kuikopesha CHADEMA sh. milioni 500, Bw. Philemon Ndesamburo sh. milioni 100 na Bibi Grace Kiwelu sh. milioni 100

"Nilipochaguliwa umakamu niligundua udhaifu huu, mfano kuhitilafiana wakati Baraza Kuu linatoa ratiba ya uchaguzi wa ndani ngazi zote...baadhi uchaguzi hautafanyika kwa sababu hakuna fedha zilizotolewa.

"Tutapataje chama chenye uhai kama hakuna fredha za kuwaewezesha wanachama kugombea? Sheria ya vyama inasema wazi, kuwa Msajili wa Vyama atafuta chama kisipochaguana kwa kuzingatia taratibu zilizopo. Kwa mwendo huu tutazamie mamluki bila uchaguzi," alisema.

Alidai kuwa hadi sasa, Bw. Mbowe ameshajilipa sh. 218,330,543.

Kuhusu ubaguzi wa kikabila, alikariri taarifa ya Tume ya Mzirai iliyobaini kuwa ubaguzi huo upo ikisema katika uongozi wa juu wa chama hicho, wakurugenzi, wenye watu wanane, wanne ni kutoka Kaskazini (Wachagga).


Alisisitiza nia yake ya kupinga kusimamishwa kwa kutumia vikao vya juu vya chama hicho ikiwa ni pamoja na Baraza Kuu, Mkutano Mkuu na hata kulifikisha suala hilo kwa wanachama kama vikao hivyo vitashindwa.
 
Mambo yanakua mambo ndio kumekucha,Helkopita ilikodiwa ili matumizi yaende juu .mama yangu.

Imetolewa mara ya mwisho: 04.07.2008 0037 EAT
•
Baada ya CHADEMA kumwaga ugali...Wangwe amwaga mboga

Habari Zinazoshabihiana
• CCM yagaragaza tena CHADEMA, NCCR 29.02.2008 [Soma]
• Wangwe kuadabishwa na kamati iliyojadili akina Mengi na Malima 10.02.2007 [Soma]
• Mbunge amkomalia Spika 09.02.2007 [Soma]

*Alalamikia kuchafuliwa, ubaguzi wa kikabila ndani ya chama
*Awapa viongozi siku 14 kumsafisha, vinginevyo mahakamani
*Akana kutoa siri CCM, adai Mbowe ndiye hukutana nao faragha

Na Mwandishi Wetu

MGOGORO wa uongozi unaorindima ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umeingia katika sura mpya baada ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho aliyesimamishwa hivi karibuni, Bw. Chacha Wangwe, kuwapa siku 14 viongozi wa chama hicho kuthibitisha madai yao kwamba anashirikiana na CCM kukihujumu, vinginevyo atawafikisha mahakamani.

Bw. Wangwe ambaye pia ni Mbunge wa Tarime kwa tiketi ya chama hicho, aliliambia gazeti hili jana kuwa madai ya viongozi hao yamemchafulia jina na heshima kiasiasa aliyoijenga ndani ya chama hicho kwa gharama kubwa.

Wiki iliyopita katika kikao chake, mjini Dodoma, Kamati Kuu ya CHADEMA chini ya Mwenyekiti wake, Bw. Freeman Mbowe, ilimsimamisha uongozi Bw. Wangwe kwa tuhuma mbalimbali ikiwamo kutoa siri za chama hicho kwa viongozi wa CCM.

Bw. Wangwe alituhumiwa pia kukashifu chama hicho, viongozi na watendaji wake, bila kutofautisha kashfa na ukosoaji wa kisiasa na kiutendaji, kwa kutumia wanachama waliochukuliwa hatua za kinidhamu na vikao halali vya chama hicho.

Tuhuma zingine ni pamoja na kuwatuhumu viongozi wenzake wa juu na watendaji wake kwa kuwahusisha na ukabila na kuvujisha siri za vikao halali vya chama kwa watu wenye lengo la kukihujumu chama hicho.

Akizungumza katika ofisi za gazeti hili Dar es Salaam jana, Bw. Wangwe alipinga madai hayo na kueleza kuwa hayana msingi na kwamba katika kipindi chote, ameipigania CHADEMA kwa nguvu zake zote na gharama kubwa, bila kuogopa mazingira magumu kwenye harakati hizo.

Alisema akiwa kiongozi wa chama hicho wilayani Tarime, alinyakua jimbo hilo na halmashauri ya wilaya hiyo huku 'wapiganaji' wenzake wakijeruhiwa kwa vipigo, kupata vilema vya maisha, kupoteza ajira na hata maisha.

Kutokana na harakati hizo, waliwezesha kupatikana asilimia 64 ya kura za jimbo hilo ambazo zilichangia ushindi wa CHADEMA na kuiwezesha kupata ruzuku ya sh. milioni 66 kila mwezi na viti maalumu sita bungeni vya chama hicho.

Alisema jitihada zake zilimfanya mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, Bw. Mbowe kuibuka na kura nyingi kumzidi mgombea wa CCM, Rais Jakaya Kikwete wilayani humo, kwenye uchaguzi mkuu uliopita mwaka 2005.

Akizungumzia uhusiano wake na Dkt. Amani Kabourou ambaye alikihama chama hicho na kwenda CCM, alisema ni wa siku nyingi hata kabla ya kujiunga na CCM na uhusiano huo haufungamani kwa namna yoyote ile na masuala ya kisiasa kama inavyodaiwa na viongozi wa CHADEMA.

"Dkt. Kabourou nashirikiana naye siku nyingi tangu aliporudi kutoka Marekani, naheshimu uamuzi wake wa kwenda CCM na huo ni uamuzi wake mwenyewe, tangu aende CCM sijakutana naye bali Juni 7 mwaka huu, nilikwenda kwake kuhani msiba wa mama yake mzazi tukiwa na Bibi Maulida Anna Komu," alisema Bw. Wangwe.

Bw. Wangwe alishangaa suala hilo kuhusishwa na hujuma dhidi ya chama hicho na kuzidi kufafanua Katiba ya CHADEMA haina kipengele kinachozuia mwanachama kuwa na uhusiano na wanachama wa vyama vingine, bali tofauti iliyopo ni hoja.

Alimshambulia Mwenyekiti wa Chama hicho, Bw. Mbowe kwa maelezo kuwa amekuwa karibu zaidi na viongozi wengi wa CCM na wakati mwingine wanakutana faragha, lakini kama mwanachama ana uhuru wa kufanya hivyo na hakuna anayempinga kwa hilo.

"Dkt. Slaa (Wilbroad), mkewe ni kada wa CCM aliyekubuhu ni Diwani wa kuchaguliwa wanakaa pamoja, simu, nyaraka zote, wageni wote wanaokuja mama anasikiliza, hawanitendei haki mimi kwa hili," alisema Bw. Wangwe.

Alisema kuengulia kwake ni mkakati ulioandaliwa muda mrefu kumng'oa kwenye nafasi hiyo, kutokana na dhamira yake ya kutaka kufanyika mageuzi ya kweli ndani ya chama hicho.

"Nilisema uongozi uliopo tutaupumzisha, kwani umeshindwa kupeleka chama mbele," alisema Mbunge huyo machachari na kusisitiza kuwa ajenda ya kumsimamisha uongozi haikuwa kwenye mkutano wa Dodoma ila kilichokuwapo ni kuwasilishwa Ripoti ya Tume ya Mzirai, iliyoundwa kuchunguza tuhuma mbalimbali ndani ya chama hicho, lakini suala hilo likaibuliwa.

Alibainisha kuwa tofauti iliyojitokeza kati yake na Bw. Mbowe, ni suala la mgawanyo wa ruzuku kati ya makao makuu kwa upande mmoja na wilaya kwa upande mwingine, jambo alilosema kwa muda mrefu amekuwa akipigia debe chama hicho kujijenga kuanzia chini kwenda juu, jambo linalokinzana na msimamo wa mwenyekiti wake.

"Ninachopigania ni mfumo wa 'bottom up' (kuanzia chini kwenda juu) fedha zipelekwe kwenye vitovu vya mapambano zikajenge chama kwenye maeneo ambayo hakipo, lakini wenzangu wanataka mfumo wa 'up bottom' (juu kwenda chini).

Alisema gharama za kuendesha chama wilayani ni ndogo, kwani endapo kila mwezi zitapelekwa sh. 100,000 zitatosha kulipa pango la ofisi linaloweza kugharimu kati ya sh. 25,000 hadi 30,000 na sh. 70,000 zikabaki kwa matumizi mengine ya ofisi. Mbali na fedha hizo, alishauri pia kutolewa sh. 100,000 nyingine kwa ajili ya kulipa wasimamizi wa ofisi hizo.

"Yeye (Bw. Mbowe) anataka fedha zitumike kwa helikopta, sisemi kwamba helikopta ni kitu kibaya, lakini tuangalie katika mruko tulipata watu wangapi? Lazima tuwe na majimbo, wanachama na matawi ya kutosha, hata kama CCM itatuzidi nguvu, basi angalau tupate majimbo 150, hata ruzuku itapanda.

Alipinga kile alichokiita madeni hewa wanayojilipa viongozi wakuu wa chama hicho kwa madai ya kukikopesha chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, ambapo alisema Bw. Mbowe alidai kuikopesha CHADEMA sh. milioni 500, Bw. Philemon Ndesamburo sh. milioni 100 na Bibi Grace Kiwelu sh. milioni 100

"Nilipochaguliwa umakamu niligundua udhaifu huu, mfano kuhitilafiana wakati Baraza Kuu linatoa ratiba ya uchaguzi wa ndani ngazi zote...baadhi uchaguzi hautafanyika kwa sababu hakuna fedha zilizotolewa.

"Tutapataje chama chenye uhai kama hakuna fredha za kuwaewezesha wanachama kugombea? Sheria ya vyama inasema wazi, kuwa Msajili wa Vyama atafuta chama kisipochaguana kwa kuzingatia taratibu zilizopo. Kwa mwendo huu tutazamie mamluki bila uchaguzi," alisema.

Alidai kuwa hadi sasa, Bw. Mbowe ameshajilipa sh. 218,330,543.

Kuhusu ubaguzi wa kikabila, alikariri taarifa ya Tume ya Mzirai iliyobaini kuwa ubaguzi huo upo ikisema katika uongozi wa juu wa chama hicho, wakurugenzi, wenye watu wanane, wanne ni kutoka Kaskazini (Wachagga).


Alisisitiza nia yake ya kupinga kusimamishwa kwa kutumia vikao vya juu vya chama hicho ikiwa ni pamoja na Baraza Kuu, Mkutano Mkuu na hata kulifikisha suala hilo kwa wanachama kama vikao hivyo vitashindwa.
 
Haya sasa si mlisema Mbowe anajitolea
kumbe alikodi makusudi helkopita ili matumizi yawe juu ajiripe mafao makubwa angalia hizo namba za sh anazojiripa.Yesu na MAria

Imetolewa mara ya mwisho: 04.07.2008 0037 EAT
•
Baada ya CHADEMA kumwaga ugali...Wangwe amwaga mboga

Habari Zinazoshabihiana
• CCM yagaragaza tena CHADEMA, NCCR 29.02.2008 [Soma]
• Wangwe kuadabishwa na kamati iliyojadili akina Mengi na Malima 10.02.2007 [Soma]
• Mbunge amkomalia Spika 09.02.2007 [Soma]

*Alalamikia kuchafuliwa, ubaguzi wa kikabila ndani ya chama
*Awapa viongozi siku 14 kumsafisha, vinginevyo mahakamani
*Akana kutoa siri CCM, adai Mbowe ndiye hukutana nao faragha

Na Mwandishi Wetu

MGOGORO wa uongozi unaorindima ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umeingia katika sura mpya baada ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho aliyesimamishwa hivi karibuni, Bw. Chacha Wangwe, kuwapa siku 14 viongozi wa chama hicho kuthibitisha madai yao kwamba anashirikiana na CCM kukihujumu, vinginevyo atawafikisha mahakamani.

Bw. Wangwe ambaye pia ni Mbunge wa Tarime kwa tiketi ya chama hicho, aliliambia gazeti hili jana kuwa madai ya viongozi hao yamemchafulia jina na heshima kiasiasa aliyoijenga ndani ya chama hicho kwa gharama kubwa.

Wiki iliyopita katika kikao chake, mjini Dodoma, Kamati Kuu ya CHADEMA chini ya Mwenyekiti wake, Bw. Freeman Mbowe, ilimsimamisha uongozi Bw. Wangwe kwa tuhuma mbalimbali ikiwamo kutoa siri za chama hicho kwa viongozi wa CCM.

Bw. Wangwe alituhumiwa pia kukashifu chama hicho, viongozi na watendaji wake, bila kutofautisha kashfa na ukosoaji wa kisiasa na kiutendaji, kwa kutumia wanachama waliochukuliwa hatua za kinidhamu na vikao halali vya chama hicho.

Tuhuma zingine ni pamoja na kuwatuhumu viongozi wenzake wa juu na watendaji wake kwa kuwahusisha na ukabila na kuvujisha siri za vikao halali vya chama kwa watu wenye lengo la kukihujumu chama hicho.

Akizungumza katika ofisi za gazeti hili Dar es Salaam jana, Bw. Wangwe alipinga madai hayo na kueleza kuwa hayana msingi na kwamba katika kipindi chote, ameipigania CHADEMA kwa nguvu zake zote na gharama kubwa, bila kuogopa mazingira magumu kwenye harakati hizo.

Alisema akiwa kiongozi wa chama hicho wilayani Tarime, alinyakua jimbo hilo na halmashauri ya wilaya hiyo huku 'wapiganaji' wenzake wakijeruhiwa kwa vipigo, kupata vilema vya maisha, kupoteza ajira na hata maisha.

Kutokana na harakati hizo, waliwezesha kupatikana asilimia 64 ya kura za jimbo hilo ambazo zilichangia ushindi wa CHADEMA na kuiwezesha kupata ruzuku ya sh. milioni 66 kila mwezi na viti maalumu sita bungeni vya chama hicho.

Alisema jitihada zake zilimfanya mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, Bw. Mbowe kuibuka na kura nyingi kumzidi mgombea wa CCM, Rais Jakaya Kikwete wilayani humo, kwenye uchaguzi mkuu uliopita mwaka 2005.

Akizungumzia uhusiano wake na Dkt. Amani Kabourou ambaye alikihama chama hicho na kwenda CCM, alisema ni wa siku nyingi hata kabla ya kujiunga na CCM na uhusiano huo haufungamani kwa namna yoyote ile na masuala ya kisiasa kama inavyodaiwa na viongozi wa CHADEMA.

"Dkt. Kabourou nashirikiana naye siku nyingi tangu aliporudi kutoka Marekani, naheshimu uamuzi wake wa kwenda CCM na huo ni uamuzi wake mwenyewe, tangu aende CCM sijakutana naye bali Juni 7 mwaka huu, nilikwenda kwake kuhani msiba wa mama yake mzazi tukiwa na Bibi Maulida Anna Komu," alisema Bw. Wangwe.

Bw. Wangwe alishangaa suala hilo kuhusishwa na hujuma dhidi ya chama hicho na kuzidi kufafanua Katiba ya CHADEMA haina kipengele kinachozuia mwanachama kuwa na uhusiano na wanachama wa vyama vingine, bali tofauti iliyopo ni hoja.

Alimshambulia Mwenyekiti wa Chama hicho, Bw. Mbowe kwa maelezo kuwa amekuwa karibu zaidi na viongozi wengi wa CCM na wakati mwingine wanakutana faragha, lakini kama mwanachama ana uhuru wa kufanya hivyo na hakuna anayempinga kwa hilo.

"Dkt. Slaa (Wilbroad), mkewe ni kada wa CCM aliyekubuhu ni Diwani wa kuchaguliwa wanakaa pamoja, simu, nyaraka zote, wageni wote wanaokuja mama anasikiliza, hawanitendei haki mimi kwa hili," alisema Bw. Wangwe.

Alisema kuengulia kwake ni mkakati ulioandaliwa muda mrefu kumng'oa kwenye nafasi hiyo, kutokana na dhamira yake ya kutaka kufanyika mageuzi ya kweli ndani ya chama hicho.

"Nilisema uongozi uliopo tutaupumzisha, kwani umeshindwa kupeleka chama mbele," alisema Mbunge huyo machachari na kusisitiza kuwa ajenda ya kumsimamisha uongozi haikuwa kwenye mkutano wa Dodoma ila kilichokuwapo ni kuwasilishwa Ripoti ya Tume ya Mzirai, iliyoundwa kuchunguza tuhuma mbalimbali ndani ya chama hicho, lakini suala hilo likaibuliwa.

Alibainisha kuwa tofauti iliyojitokeza kati yake na Bw. Mbowe, ni suala la mgawanyo wa ruzuku kati ya makao makuu kwa upande mmoja na wilaya kwa upande mwingine, jambo alilosema kwa muda mrefu amekuwa akipigia debe chama hicho kujijenga kuanzia chini kwenda juu, jambo linalokinzana na msimamo wa mwenyekiti wake.

"Ninachopigania ni mfumo wa 'bottom up' (kuanzia chini kwenda juu) fedha zipelekwe kwenye vitovu vya mapambano zikajenge chama kwenye maeneo ambayo hakipo, lakini wenzangu wanataka mfumo wa 'up bottom' (juu kwenda chini).

Alisema gharama za kuendesha chama wilayani ni ndogo, kwani endapo kila mwezi zitapelekwa sh. 100,000 zitatosha kulipa pango la ofisi linaloweza kugharimu kati ya sh. 25,000 hadi 30,000 na sh. 70,000 zikabaki kwa matumizi mengine ya ofisi. Mbali na fedha hizo, alishauri pia kutolewa sh. 100,000 nyingine kwa ajili ya kulipa wasimamizi wa ofisi hizo.

"Yeye (Bw. Mbowe) anataka fedha zitumike kwa helikopta, sisemi kwamba helikopta ni kitu kibaya, lakini tuangalie katika mruko tulipata watu wangapi? Lazima tuwe na majimbo, wanachama na matawi ya kutosha, hata kama CCM itatuzidi nguvu, basi angalau tupate majimbo 150, hata ruzuku itapanda.

Alipinga kile alichokiita madeni hewa wanayojilipa viongozi wakuu wa chama hicho kwa madai ya kukikopesha chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, ambapo alisema Bw. Mbowe alidai kuikopesha CHADEMA sh. milioni 500, Bw. Philemon Ndesamburo sh. milioni 100 na Bibi Grace Kiwelu sh. milioni 100

"Nilipochaguliwa umakamu niligundua udhaifu huu, mfano kuhitilafiana wakati Baraza Kuu linatoa ratiba ya uchaguzi wa ndani ngazi zote...baadhi uchaguzi hautafanyika kwa sababu hakuna fedha zilizotolewa.

"Tutapataje chama chenye uhai kama hakuna fredha za kuwaewezesha wanachama kugombea? Sheria ya vyama inasema wazi, kuwa Msajili wa Vyama atafuta chama kisipochaguana kwa kuzingatia taratibu zilizopo. Kwa mwendo huu tutazamie mamluki bila uchaguzi," alisema.

Alidai kuwa hadi sasa, Bw. Mbowe ameshajilipa sh. 218,330,543.

Kuhusu ubaguzi wa kikabila, alikariri taarifa ya Tume ya Mzirai iliyobaini kuwa ubaguzi huo upo ikisema katika uongozi wa juu wa chama hicho, wakurugenzi, wenye watu wanane, wanne ni kutoka Kaskazini (Wachagga).


Alisisitiza nia yake ya kupinga kusimamishwa kwa kutumia vikao vya juu vya chama hicho ikiwa ni pamoja na Baraza Kuu, Mkutano Mkuu na hata kulifikisha suala hilo kwa wanachama kama vikao hivyo vitashindwa.

Kama kweli hiyo wilaya ya WANGWE ilimpa kura MBOWE ZAIDI YA KIKWETE..BASI WALIHITAJI PESA ZA KUTOSHA!
 
Kama kweli hiyo wilaya ya WANGWE ilimpa kura MBOWE ZAIDI YA KIKWETE..BASI WALIHITAJI PESA ZA KUTOSHA!

sasa wewe unafikiri anaweza daganya mbele ya CCM thubutu.Wao wamejifanya kumtimua ili waendelee kulipana hizo milion 700,Harafu watu wana tu SPIN anajitolea. SASA kama ni kweli anakihujumu CHAMA basi wakutane huko Mahakamani
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom