Kuna kitu kinaitwa "anthropic bias".
Anthropic bias ni tabia ya kuchukua mambo kwa upeo fulani, ambao kikawaida ni finyu na unatokana na uwezo mdogo wa watu (hence anthropic, neno anthro ni mzizi wenye kumaanisha watu, as in anthropolgy, the study of humans). So anthropic bias, ni tabia ya kukaa na ku deduce mambo tu, kutokana na upeo wetu wa kiutu.
Ukienda kwa tabia hii, ni rahisi sana kubishana na mtu kumwambia kwamba dunia ni bapa na wala si mviringo, kwa sababu, ukiangalia mambo kwa juujuu, unaona dunia ni bapa tu, inabidi ufikiri sana ili kuona dunia ni mviringo.
Kufikiri kuhusu jinsi maisha yalivyoibuka mabilioni ya miaka, au kanuni za msingi za fizikia zinavyofanya kazi, au je, kuna Mungu au hakuna Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, inabidi ujivue hii anthropic bias.
Nitakupa mfano mmoja wa bwana mmoja aliuwa mvuvi. Yule bwana aliuwa na nyavu yake ya kuvulia, ile nyavu kila tobo lina ukubwa wa sentimeta 2 ya mraba. Sasa kaenda nayo kuvua, lakini pia alikuwa anataka kujua samaki mdogo kabisa anayeweza kumkamata. Basi akavua mchana kutwa, usiku kucha, akirudia hivyo mpaka siku tatu.
Alipomaiza kuvua, akaenda kuwapima wale samaki, akitaka kujua samaki gani ni mdogo kabisa katika bahari ile.
Akaja kugundua kwamba, katika samaki wake wote aliovua, hakuna samaki aliye na mdogo kuliko sentimeta mbili za mraba.
Akajiwekea kwamba kagundua kuwa, katika bahari ile inaonekana kuwa hakuna samaki mdogo zaidi ya sentimeta mbili za mraba, kwa kuwa hajakamata samaki mdogo hivyo na kakaa kweli baharini.
Lakini, mvuvi huyu kuna kitu kimoja kidogo tu hakukifikiria. Hakufikiria kwamba, nyavu yake aliyoitumia kuvua ilikuwa na matobo ya sentimeta 2 za mraba, na hivyo, samaki yeyote mdogo kuliko sentimeta mbili za mraba, aliweza kupenya kutoka kwenye ile nyavu, na hivyo samaki huyo mdogo hakushikwa na nyavu ile.
Hapo utaona jinsi kipimo chako kinavyoweza kukufanya upate majibu yasiyo sahihi.
Wewe una "anthropic bias", una nyavu unayoitumia kuvua 9mawazo yako, utu wako, elimu yako ambayo haijui vizuri mambo mengi kama particle physics, quantum mechanics, evolution etc), nyavu hii ina ukubwa fulani, na ukubw ahuo unaathiri hata kufikiri kwako.
Kwa kutumia nyavu hii, utaweza kuvua samaki wa aina fulani tu, wadogo zaidi ya nyavu yako watakuponyoka tu, halafu ukitaka kujua samaki mdogo zaidi kwa kuangalia samaki uliovua kwa nyavu hiyo, utaweza kupata jibu lisilo sahihi kirahisi tu.
Hoja yako kwamba vitu vinaonekana kama vimeumbwa, order must come out of deliberate design, na kuhitimisha Mungu yupo, ina matatizo mengi.
Nitayaorodhesha hapa.
1. Kwanza kabisa, nakupa immanent critique. Immanent critique maana yake ni kwamba, hata nikikubaliana nawe unavyoanza, conclusion yako bado si sawa. Hata nikikubaliana nawe kwamba inaonekana vitu vina design, si lazima design hii itoke kwa Mungu muumba yote, mwenye ujuzi wote na upendo wote. This is a logoical non sequitur. Yani ni hivi, hata kama tukikubaliana kwamba wewe ni lazima uwe na mama aliyekuzaa, ukweli kwamba wewe una mama aliyekuzaa haumaanishi kwamba mama yako ni Samia Suluhu Hassan, rais wa Tanzania. Ukisema Samia Suluhu Hassan ni mama yako mzazi, inabidi utuhakikishie hilo. Hutakiwi kusema "Mimi Mama yangu mzazi ni Samia Suluhu Hassan, rais wa Tanzania" halafu watu wakikuuliza "Kwa nini unasema hivyo?", ujibu "Aaah, si lazima niwe na mama, lazima niwe na mama, unafikiri nimejizaa mwenyewe, lazima niwe na mama, na kama lazima niwe na mama, basi mama yangu ni Samia Suluhu Hassan, rais wa Tanzania".
Kwa hivyo, hoja ya kwanza, hata kama ni lazima vitu vyenye order viwe vimeumbwa kwa makusudi, hilo halimaanishi vimeumbwa na Mungu. Unatakiwa kuthibitisha kwamba vimeumbwa na Mungu.
2. Lakini pia, kwenye asili kuna uthibitisho kwamba si lazima vitu vyenye complexity/ order vitokee kwa kuumbwa kwa makusudi. Hii ni dhana ya kidini ambayo ilikuja kutaka kuelezea vitu ambavyo hatuvielewi tu. Kuna mifano mingi ya vitu vinavyotoka kuwa simple na kuwa complex, evolution inatupa mifano mingi ya natural selection by survival of the fittest. Hapa tunaongelea mabilioni ya miaka, hivyo kunaweza kutokea mabadiliko makubwa sana kuliko yanayoweza kueleweka kwa uzoefu wetu wa kawaida wa kuishi miaka michache.
3. Uiweka hoja kwamba, vilivyo complex/ vyenye order kubwa, ni lazima viwe vimeumbwa kwa design maalum, na mwenye order/ complexity kubwa zaidi, haviwezi kutokea vyenyewe vikiwa na order/ complexity kubwa au kuanzia na complexity/ order ndogo vika evolve mpaka kuja kuwa na order/ complexity kubwa, kimsingi unajenga hoja ya kukataa uwepo wa Mungu bila kujijua.
Unaweza kuona unatetea uwepo wa Mungu, kwa sababu unamuweka Mungu kama mwenye order/ complexity kubwa zaidi, akawa muumba, lakini kama tunashikilia kanuni yako ya kwamba order/ complexity haiwezi kutokea tu, ni lazima iwe designed kwa nia maalum, basi utajikuta unapata tabu kujibu swali dogo tu.
Kama kweli order/ complexity haiwezi kutokea tu, ni lazima iumbwe na order complexity kubwa zaidi, huyo Mungu katokeaje? Utajikuta inakubidi umuelezee Mungu kama kaumbwa na Mungu wake na yeye, na Mungu wake kaumbwa na Mungu wake, ad infinitum, ad nauseam. Kifupi, umemfanya Mungu kuwa ki sehemu kidogo tu cha mashine kubwa isiyo na mwisho, na kwa msingi huu, Mungu huyu aliyeumbwa, anapoteza uungu wake.
Kwa hivyo, hoja yako, ya kusema kitu chenye order/ complexity kubwa hakiwezi kutokea chenyewe, ni lazima kimeumbwa, ukiiangalia kwa juu juu, unaweza kuona inatetea uwepo wa Mungu, lakini, ukichambua kwa kina, utakuja kugundua kumbe hoja hii, ukiishikilia barabara, inatuonesha Mungu hawezi kuwapo.
Kuna mengi ya kuchambua kwa kina zaidi, lakini nisiandike gazeti, nikuachie na wewe upate nafasi ya kusoma vizuri hoja zangu, kuzichambua, na kunijibu.