Infropreneur
JF-Expert Member
- Aug 15, 2022
- 14,185
- 30,687
[emoji119][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119] Heshima kwako mkuu.Hatuwezi kujua tusicho kijua, lakini, tunaweza kupunguza tusichokijua kwa kujielimisha.
Haya mambo si kwamba mtu alikaa mara moja tu akagundua, ni maelfu na maelfu ya miaka ya watu kusoma, kuvumbua, kuchambua, kuandika na kurithishana vizazi na vizazi.
Einstein alikuwa mdadisi tangu mtoto. Alipewa compass, dira, na baba yake, akawa anajiuliza kwa nini ile needle ya compass inaelekea upande mmoja tu kokote anapoenda? Alijenga udadisi huo mpaka ukubwani, akafanya thought experiments, akasoma mambo ya sayansi ya wengine, akatupa kitu alichoongeza yeye, Relativity, special na general.
Umeuliza kama Einstein alifanya thought experiments tu, au alifanya nini? Alianza kwa thought experiment, akiangalia frame of reference tofauti, mtu aliye kwenye treni na aliyesimama kituoni, jinsi muda unavyokuwa tofauti, watu walio katika elevator (lift) wanavyoweza ku simulate gravity. Ni udadisi tu. Lakini, hizo thought experiments zake ziliangaliwa kimahesabu zikakutwa sawa, zimethibitishwa, aliweza mpaka kufanya utabiri. Mfano, katika solar eclipse ya mwaka 1919, hesabu za Newton zilitabiri kwamba nyota fulani za zilizotakiwa kuwa zinaonekana pembeni ya jua zitakuwa pahali fulani, hesabu za Einstein zikatabiri kwamba, kutokana na gravity ya jua, nyota hizo zitaonekana pembeni kidogo ya zilipotabiriwa na Newton, Arthur Eddington akafanya experiment na kuona hesabu za Einstein ziko sahihi, mwaka 1919.
Kuanzia hapo, Einstein amethibitishwa mara nyingi sana katika muktadha wa Relativity. Hata GPS system inatumia kanuni za Einstein za Relativity, ukitumia Newtonian math kuendesha GPS utatengeneza ajali dunia nzima. Ukiangalaia TV inayotumia matangazo ya satellite, unatumia Relativity. Mambo mengi sana yanayotaka high accuracy in time yanatumia hesabu za Relativity.
Hiyo Big Bang Theory watu hawakugundua mara moja. Ukisoma historia za kina George Lemaitre na Edwin Hubble utaona kwamba hizi habari za ugunduzi zina safari ndefu sana ya uchunguzi, na mpaka leo watu wanachunguza na kuhakiki bado. Mimi hizi habari nazifuatilia tangu form one angalau, na ugunduzi mwingine kama wa Cosmic Microwave Background au Higgs Boson unafanyika mimi nilikuwa nausubiri kwa miaka mingi.
Ttatizo jamii yetu watu wengi hawafuatilii mambo haya kwa karibu, hivyo yanaonekana kama uchawi tu.
Hoja zako umeiva haswaa hubahatishi usemacho...
Nimejifunza mengi hapa na baadhi ya maswali yaliyokuwa yana nitatiza nimepata mwanga.
Kuna msemo mmoja wa Haile Selassie Raisi wa Ethiopia aliwahi sema kwamba
"A man who says, I have learned enough and will learn no further should be considered knowing Nothing at all"....
Na ulichosema hapa kwamba"ili kujua zaidi lazima tuendelee kujielimisha" vinapatana na msemo wa Haile Selassie.
Wengi wa watu hujifanya hawataki kwenda beyond, Ku Question uwepo wa Mungu kwa vile wame kuwa "Brainwashed" na kuwekewa Hofu zilizo wageuza waoga na kuwajengea Uoga kuhoji maswala ya imani na uwepo wa Mungu...
Nimejifunza pia, Faith prevents reasonable thinking
Kudos,Mkuu[emoji119][emoji119][emoji119][emoji122][emoji122]