UCHAWI: Upo au haupo?

UCHAWI: Upo au haupo?

Naomba ufafanuzi kuhusu Bundi,Watu husema bundi anapolia usiku karibu na nyumban au nyumban kwako ni ishara ya jambo baya kutokea na kama kuna mtoto basi inakupasa umfinye sikio.Je,ni kweli ni ishara ya jambo baya na vp kuhusu kumfinya sikio mtoto
Mojawapo ya dhana zinazotikisa katika jamii yetu ni hii dhana ya uchawi KWAMBA UPO AMA HAUPO!...Na Kwakweli unapoongelea kuhusu uchawi unaonekana mtu usiyeelimika kabisa ama mtu fulani wa kuogopwa
Ndani ya dunia kuna;

1. Ulimwengu unaoonekana
Huu ni ulimwengu wa ithibati za kisayansi, ulimwengu wa formula, ulimwengu wa halisi (sio uhalisia) ulimwengu wa mwili wa nyama.,ulimwengu wa vinavyoonekana kwa macho na kugusika kwa mikono.

2. Ulimwengu usioonekana, ulimwengu usio na ithibati za kisayansi, ulimwengu wa roho, ulimwengu wa nafsi. Ulimwengu wa kiza... Ulimwengu huu ndio injini ya ulimwengu unaoonekana yaani ndio unaoendesha dunia ya sayansi na ithibati

4f80492adf3f0e6df2d1f5659f18f894.jpg


Sina tatizo hata kidogo na watu wasioamini uchawi kama hawamwamini Mungu mmoja (wapagani), lakini nina tatizo na mashaka makubwa na wale wenye imani kamili juu ya Mungu mmoja, muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyomo (ukiwemo uchawi)! Shida yao hii hapa! Aidha wanasoma misahafu yao kwa kukakiriri bila kuelewa, ama wanapotoshwa na wengine.....

Vile vile inawezekana kabisa wengi wanajichanganya kwenye kuamini uchawi kama dhana ya msingi na kuamini waganga wa kienyeji. ...iko hivi unaweza uamini katika uchawi lakini usiamini katika wachawi na waganga wa kienyeji
Maranyingi tumeona wale wasiomini wakitoa changamoto ya kurogwa kama kweli uchawi upo! Huku ni kupotoka kabisa na kukosa uelewa wa mambo..

Kuwepo kwa uchawi ni kitu cha kwanza lakini kuwepo na mtu akaweza kuutumia huo uchawi kwa muktadha fulani ni kitu kingine kabisa
Malumbano mengi pia yametokea kwenye kutaka ithibati za kuwepo kwa uchawi! Hizi ni fikra tengefu..

Ulimwengu wa roho ni software huwezi kuuona kwa macho ya mwili wala kuushika kwa mikono yako...tusichanganye vinavyoonekana na visivyoonekana, tukafanya hiki ndio kile na kile ndio kile
-simu unayo na unafanya mawasiliano yote ninini kinafanyika mpaka umudu kufanya hayo yote?

-Akili unayo na ukiulizwa hutabisha je ukiambiwa ionyeshe utaweza?
-Usingizi unao je kufumba macho ndio kulala usingizi?
Ni vema kuelewa kwama uchawi ni sehemu ya ulimwengu usioonekana, upo lakini hauna ithibati za kisayansi kwakuwa huwezi kuushika nk ....

Kama ilivyo nguvu iliyopo kwenye mashine yoyote ana mwanga kwenye taa yoyote ama software kwenye kifaa chochote cha kielectronic...kama ulivyo uhai ndani ya mwili
Tafakari....!

Jr
 
Naomba ufafanuzi kuhusu Bundi,Watu husema bundi anapolia usiku karibu na nyumban au nyumban kwako ni ishara ya jambo baya kutokea na kama kuna mtoto basi inakupasa umfinye sikio.Je,ni kweli ni ishara ya jambo baya na vp kuhusu kumfinya sikio mtoto
Haya ni mambo ya kiimani na kimila zaidi, kwa mfano China kumuona bundi asubuhi nje ya Nyumba ni kismati na kunguru ni nuksi
 
Nimefukuzwa kwenye mada za forex nimeambiwa sio size yangu... Mchawi na forex wapi na wapi.. Rudi kwenye mada zako za kichawi huko ndio size yako... Nimetii agizo
 
Something you can't see becomes very hard to prove & trust.

Mungu pia aliliona hilo ndiyo maana akaweka uungu wake ndani ya Yesu (mwanadamu wa kawaida) ili tuamini - it worked out.
 
Something you can't see becomes very hard to prove & trust.

Mungu pia aliliona hilo ndiyo maana akaweka uungu wake ndani ya Yesu (mwanadamu wa kawaida) ili tuamini - it worked out.
Aaamen barikiwa zaidi
 
Ntakuwa wa mwisho kuamini uchawi upo hadi unikute ndo ntaamini...
Lkn nyingine ni fix tu za kutufanya tuishi kwa uoga na kuogopa baadhi ya wazee uswahilini
 
Ntakuwa wa mwisho kuamini uchawi upo hadi unikute ndo ntaamini...
Lkn nyingine ni fix tu za kutufanya tuishi kwa uoga na kuogopa baadhi ya wazee uswahilini
Unaamini Mungu yupo lakini
 
Mimi binafsi natambua kuwepo uchawi kwa mujibu wa vitabu vitakatifu, swali langu lipo hivi mimi siamini uchawi kabisa na siamini kuwa kuna mtu anaweza kuniloga kwa lolote, hivi Kama uchawi upo na unafanya kazi kwanini wasitengeneze ndege zikasafirisha watu tukaachana na bombadia za magu? Kwanini alisilimia kubwa ya watu wanaoamini uchawi ni maskini? Kuna uhusiano gani kati ya umaskini na uchawi? Nawakilisha mkuu.
 
Mimi binafsi natambua kuwepo uchawi kwa mujibu wa vitabu vitakatifu, swali langu lipo hivi mimi siamini uchawi kabisa na siamini kuwa kuna mtu anaweza kuniloga kwa lolote, hivi Kama uchawi upo na unafanya kazi kwanini wasitengeneze ndege zikasafirisha watu tukaachana na bombadia za magu? Kwanini alisilimia kubwa ya watu wanaoamini uchawi ni maskini? Kuna uhusiano gani kati ya umaskini na uchawi? Nawakilisha mkuu.
Uchawi ni jambo la kiroho zaidi na mabombadia ni vitu vya kimwili.... Mchawi hahitaji fedha wala mali kwakuwa hana matumizi navyo akitaka kula anakula akitaka kusafiri ni kufumba na kufumbua keshafika... Uchawi ni kitu cha kibinafsi sana
 
Kwa maana hiyo uchawi hauna maana yoyote brother,
Inategemea unasimamia upande gani wa giza ama wa nuru... Kwangu mimi uchawi una maana moja tuu... Kunikumbusha kuwa kila kitu kina upande wa pili
 
Ukiwa na tabia zifwatazo wewe ni MCHAWI tu.

1-Ukiwa unachukia maeendeleo ya mtu mwingine jua wewe ni mchawi kama wachawi wengine.
2-Ukiona hupendi jambo lolote zuri lifanywalo na mtu mwingine huo pia ni uchawi tu.
3-Jirani yako kanunua kitu kizuri badala ya kumpongeza wewe unachukia huo ni uchawi tu.
4-Ukiona unapenda vitu vizuri ufanye wewe tu na sio mtu mwingine huo ni uchawi 100%
5-Tena ukiona unakelwa na masikini kutaka kujikomboa huo sasa ndio uchawi wa kiwango cha SGR.
6-Ukiona unapoteza muda mwingi kukaa vijiweni huku ukisengenya watu jua wewe ni mchawi mwenye PhD.
7-Ukipenda mke/dem au mume wa mtu wewe ni mchawi kama wachawi wengine tu.
8-Ukiona unafurahiya matatizo yaliomkumba mtu mwingine dah! ujue sasa umekubuhu kwa uchawi.
Nasema hivi,,,uchawi sio lazima uwe mganga wa kienyeji. Uchawi ni matendo ya yako dhidi ya watu waliokuzunguka.
 
Ukijiona
Unawachukia sana Mabeberu,

Jua wee ni Mchawi wa kiwango cha jiwe
2018-12-14-17-17-22.jpg
 
Nimekua nikisikia simulizi nyingi za vibwengu......na mambo mengi chungu nzima ila.... kila nikiuliza mtu anae simulia hiyo stori anasema alisimuliwa....je kuna ukweli wowote kuhusu dhana ya kuepo kwa uchawi ??


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom