Uchawi niliowahi kuushuhudia!

Uchawi niliowahi kuushuhudia!

Kuna **** mmoja hapa jirani anapiga muziki utadhani ameazima radio,anakera mpaka basi.
"
Nikija kwenye mada,kiukweli uliposema uchawi wa Zongo umenikumbusha wakati nasoma kitabu cha Uchawi namna unavyokupata na kujikinga,kilichoandikwa na marehemu Munga Tehenan,najua Mtambuzi anakijua hiki kitabu.
"
Kwa mujibu wa marehemu Munga huo ulioutaja sio uchawi hasa bali ni nguvu ambazo mtu anazaliwa nazo na kuna wengine wanajua namna ya kuepuka kuwadhuru watu na nguvu hiyo kwa kuwa wanajua wanazo.Japokuwa wapo wanaozitumia kudhuru kwa kujua au kutokujua.
"
Lakini kumbuka kuwa ili ulogwe ni lazima uwe na wewe ni mchawi.Usishangae kwani wengi wetu ni wachawi either kwa kujua au kutokujua!
 
Last edited by a moderator:
Hakuna uchawi. Ni imani za watu zimejenga hofu kuwa kuna kitu kinaitwa uchawi. Siamini uchawi.
 
Hata HIV-AIDS inasababisha ugonjwa uitwao AIDS dementia complex. Hii nayo ni mental illness.

Ndugu zangu wa karibu, wawili, nadhani walikuwa na huu ugonjwa. Lakini kuna baadhi ya ndugu walidai eti wamerogwa.

Yaani si Waafrika tuna matatizo sana. Nikifikiria ya akina Zitto na Saanane kwenda kula yamini kwa mganga ndiyo naishiwa na matumaini kabisa.

Piga picha eti Obama na Hilary nao wanaenda kwa waganga ili wapate kura zaidi :becky:
 
Hakuna uchawi. Ni imani za watu zimejenga hofu kuwa kuna kitu kinaitwa uchawi. Siamini uchawi.

Uchawi na dini kimsingi havina tofauti maana vyote msingi wake mkuu ni imani. Labda tofauti iliyopo ni kwenye application tu ingawa hii nayo yaweza kuwa debatable.

Uchawi mtu unaweza kusema lengo lake ni ubaya wakati dini/imani kwa mungu lengo lake ni wema/ uzuri.
 
Uchawi na dini kimsingi havina tofauti maana vyote msingi wake mkuu ni imani. Labda tofauti iliyopo ni kwenye application tu ingawa hii nayo yaweza kuwa debatable.

Uchawi mtu unaweza kusema lengo lake ni ubaya wakati dini/imani kwa mungu lengo lake ni mema/ mazuri.
Nakubaliana na wewe 100%
 
Nyani Ngabu kimsingi mambo ya uchawi hayawezi kuthibitishwa,lakini hii haimaanishi kuwa uchawi haupo.
"
Wazungu ni wachawi kuliko sisi,tena uchawi wao ni kiboko zaidi.Obama na Hillary ni wachawi sana.Uchawi wao ni black Magic ambao una asili ya Kabalah.Usidhani huko haupo.
"
Hata kuipata nafasi ya kuwa mgombea uraisi wa Marekani achilia mbali kuwa raisi,ni lazima uwe mchawi na unashiriki uchawi.
"
Tatizo tumeaminishwa Ulaya na Marekani hakuna uchawi na uchawi upo Africa tu,kuamini hivi ni jambo la ajabu sana.Hakuna jamii isiyokua na uchawi.Na uchawi ukifanyika kokote ni uchawi tu!
 
Last edited by a moderator:
Hahahahahahahahahaha
Zinduna hapo kwenye kula alaf ana shiba mwingine umeniacha hoi sana!
 
Last edited by a moderator:
Kwa hiyo Pacha Zinduna na Shostito gfsonwin mnakiri kbs kuwa Tanga ndo kumejaa Uchawi???????????????

Hawadanganyi maana hata mie nimekaa na kushuhudia sana ndumba na mambo kama hayo.
Nakumbuka shule ya msingi niliyokua nasoma(jina nalihifadhi) ipo karibu kabisa na baharini, pembezoni mwa barabara ya kwenda Mombasa. Wakati wa usiku ilikua inageuka kuwa treni...sasa ole wako upande,unaenda okotwa huko Lamu umechizika.
 
Last edited by a moderator:
Uchawi na dini kimsingi havina tofauti maana vyote msingi wake mkuu ni imani. Labda tofauti iliyopo ni kwenye application tu ingawa hii nayo yaweza kuwa debatable.

Uchawi mtu unaweza kusema lengo lake ni ubaya wakati dini/imani kwa mungu lengo lake ni wema/ uzuri.

Hapo kwenye Red nakubaliana na wewe, japo ipo Dini ambayo inaongoza kwa hayo Mambo ya Ulozi.
Hapo kwenye Green si imani pekee, Bali pia na Tamaduni au Kurithishana pia huchangia.
 
vipi na wale wazee wanaocheza bao kuanzia asubuhi mpaka jioni lakini huwaoni wakienda kujisaidia, ila sasa mtazamaji anayeangalia bao utaona kila baada ya muda anaenda haja kubwa au ndogo lakini wale wazee hawanyanyuki wanaendelea kucheza tu kumbe wanakupasia mizigo yao! Mimi ishanipata miaka ya nyuma pande za mwananyamala nilikuwa nazuga kwenye bao wakati namlia mingo dem flani, wewee si mchezo kila wakati wazee wananisakizia kupeleka mizigo yao, bahati kulikuwa na bar jirani nikawa najisevia kwenye toilet yao nilipokuja kushtukia mchezo washantesa sanaa! nikawa sikai tena nikawaacha wasakiziane mizigo yao wenyewe kwa wenyewe!

dah! nimecheka ile mbaya. pole sana mkuu. hii dunia we wacha tu-
 
Hawadanganyi maana hata mie nimekaa na kushuhudia sana ndumba na mambo kama hayo.
Nakumbuka shule ya msingi niliyokua nasoma(jina nalihifadhi) ipo karibu kabisa na baharini, pembezoni mwa barabara ya kwenda Mombasa. Wakati wa usiku ilikua inageuka kuwa treni...sasa ole wako upande,unaenda okotwa huko Lamu umechizika.

Santeeeeeeee.............
 
Mwalimu gfsonwin sasa kwenye mpira enzi zile za African Sports na Coastal Union,ilikuwa balaa,kuna mechi moja mwaka 89,Yasini Napili alipiga shuti mpira umempita kipa halafu ukapasuka vipande viwili na vile vipande havikuvuka goal line kuamanisha kwamba sio goli,na mechi hiyo hiyo kulikuwa kuna babu alikuwa amepelekwa ufukweni mwa bahari wakati maji yamekupwa, wakawa kama wamemzika kwa kusimama isipokuwa kichwa na shingo ,baada ya mpira kwisha matokeo yalikuwa nunge, basi watu wakasahau kwenda kumfukua kule ufukweni mpaka maji yakawa yanajaa bahati nzuri wavuvi wakasikaa kelele alizokuwa anapiga ndio wakaenda eneo la tukio ndio wakamfukua.Nilikuwa kambini usiku kabla ya mechi hii basi vitu vingine siwezi simulia kwani huwezi amini mambo yaliyokuwa yanafanyika.Mungu alinisaidia niliacha mpira msimu uliofuata kwani nilikuwa nimechaguliwa kwenda form five toka Usagara Secondary,oops isije id ika.........Sarikoki sikjui kama ulikuwa kishazaliwa..... ha ha ha

sijui wachezaji wa mpira wa miguu wa sasa. lakini wale wa miaka 1975 - 1985 cha moto walikiona.
masuala ya kulala makaburini, kuogeshwa maji ya ajabu ajabu tulikuwa tukisema "maji ya maiti" n.k ndio ilikuwa mpango mzima. ukikataa na mechi hupangwi!
 
sijui wachezaji wa mpira wa miguu wa sasa. lakini wale wa miaka 1975 - 1985 cha moto walikiona.
masuala ya kulala makaburini, kuogeshwa maji ya ajabu ajabu tulikuwa tukisema "maji ya maiti" n.k ndio ilikuwa mpango mzima. ukikataa na mechi hupangwi!

yaani miaka ile, Acha tu
 
Back
Top Bottom