Nakumbuka katika harakati za kutafuta maisha nikajikuta niko Mbeya soko matola kwenye nyumba mmoja ya bibi anaitwa binti wa kuchinja,hilo jina lina maana yake
Basi nikapata fremu ya duka,kabla ya yote nikaenda kumsimulia shangazi yangu kama nimepata fremu sehemu inatwa hilo jina,mwenyeji wangu alimind sana akaniambia yule bibi ni mchawi mkubwa watu wengi wanafilisika kwa hiyo ile fremu ya duka ilikuwa inaogopwa kupangishwa na wenyeji,wakati huo mimi nilikuwa nimetokea Iringa gangilonga uzunguni kabisa
Basi nikaingia naye mkataba kwa kupitia wajukuu zake maana yeye alikuwa mzee sana mnene,mweusi,ngozi imebabuka na midomo myekundu huwa wanasema sababu ya kula nyama za watu,
Nikasafisha duka nikatia mzigo,maana ilikuwa miaka 1995,tuko na braza wangu tumelala usiku nikaota nimetumbukizwa kwenye kaburi,halafu ndani ya kaburi kuna nyoka mkubwa mweusi,ile kuangukia ndani nikawa nimemlalia kimgongo,nilipiga kelele za nguvu sijawahi kupiga vile,hakuna aliyetoka wala kuja kuuliza kuna nini?
Cha maajabu bibi alikuja kuwa rafiki yangu mkubwa kila kitu kikitokea utasikia mkamuite Marasta,maana nilikuwa na dread miaka hiyo,nikafanikiwa nikapiga hela ndefu sana