Uchambuzi wa Tamko la RC - DSM Ndugu A. Chalamila: Watawala kutumia majeshi kizembe na kiholela ni jaribio la kujipindua!

Uzima Tele

JF-Expert Member
Jan 20, 2023
1,101
2,344

Maswali muhimu kujiuliza na utakayoyatumia kama msingi wa majadiliano katika mada hii:

1. Kikatiba Mkuu wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na usalama anaweza kukasimu mamlaka yake ya kutoa amri au maelekezo kwa majeshi yetu ya Ulinzi na usalama kwa mtu mwingine ili kufanya operation yoyote ya kijeshi?

2. Mkuu wa mkoa wa DSM Ndugu Albert Chalamila, alipata wapi mamlaka ya kuliagiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kufanya usafi mitaani siku ya tarehe 23 na 24/01/2024?

3. Kama aliagizwa na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na usalama Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan, Je huyu Rais hajakiuka na kuvunja katiba?

4. Na kama ni maamuzi ya RC Albert Chalamila mwenyewe bila ridhaa ya mkuu wa nchi, huyu mkuu wa mkoa bado anafanya nini ofisini mpaka sasa maana katika hili ni wazi kuwa huyu kiongozi ni "mjinga" hajui majukumu yake na katika hili amevuka mipaka ya mamlaka yake?

=====================

All in all, unaweza kutazama na kusikiliza uchambuzi maridadi kabisa wa kukujengea ufahamu juu ya jambo hili ktk video hiyo hapo☝️☝️☝️juu.

Katika video hiyo kwanza utaona upogo wa tamko la RC Chalamila na pia utajifunza kitu kuwa, hawa watawala wetu wako ktk hatua za mwisho za anguko lao kwa sababu wako desperate kulinda madaraka yao kwa gharama yoyote hata kama ni kuuza akili na ufahamu wao!
 
Kitu ambacho hajui, hao wanajeshi wanaweza toka kambini kuja kufagia kisha wakaungana na waandamanaji wanaoenda ofisi za UN na kupindisha msafara huo kuelekea Magogoni ili kusafisha hadi ndani maofisini na kuweka makazi kwa ulaini kabisa.

Wasiwachukulie poa hawa mabakamabaka, hata wao bei za sukari, mchele , matibabu yao na wazazi wao na maumivu yote wanaumia kama wengine tuu.

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Kitu ambacho hajui, hao wanajeshi wanaweza toka kambini kuja kufagia kisha wakaungana na waandamanaji wanaoenda ofisi za UN na kupindisha msafara huo kuelekea Magogoni ili kusafisha hadi ndani maofisini na kuweka makazi kwa ulaini kabisa.
Wasiwachukulie poa hawa mabakamabaka, hata wao bei za sukari, mchele , matibabu yao na wazazi wao na maumivu yote wanaumia kama wengine tuu.

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Hapo ndipo serikali ya chama cha mambizi walipofeli kutumia majeshi na waalimu ila hawawapi stahiki za kutosha umeongea vizuri sana kwamba wasichukuliwe poa wao nao wana magumu mengi tu yanayowakwaza kwenye uongozi kambini watapata vitu ila mtaani bei ni zile zile na haina cha jeshi au raia.....

Naomba Mungu wapindue nchi japo nahofia utashi wa wanajeshi wetu ila bora wao wachukue nchi kuliko hawa mambuzi
 

Maswali muhimu kujiuliza na utakayoyatumia kama msingi wa majadiliano katika mada hii:
Mkuu Ansbert Ngulumo


Ulichokisema ni kweli tupu, mkuu wa mkoa kuagiza jeshi kufanya usafi mahali pote jijini Dar Es Salaam ina maana huwa hawana kazi za msingi za kufanya kuhusu jamii? Je usafi ni janga kiasi ambacho inahitaji ushiriki wa jeshi la wananchi?

MAJUKUMU YA MSINGI YA JWTZ
  • Kulinda Katiba na Uhuru wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
  • Ulinzi wa mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
  • Kufanya mafunzo na mazoezi, ili kujiweka tayari kivita wakati wote;
  • Kufundisha Umma shughuli za ulinzi wa Taifa;
  • Kushirikiana na Mamlaka za Kiraia katika kutoa misaada ya kibinadamu na uokoaji wakati wa maafa;
  • Kukuza elimu ya kujitegemea na uzalishaji kupitia Jeshi la Kujenga Tiafa (JKT); na
  • Kushiriki katika shughuli za Ulinzi wa Amani Kimataifa.
Aidha wakati wa Amani, Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu ina wajibu mkubwa wa kuzisaidia mamlaka za kiraia katika kukabiliana na maafa pindi yanapotokea bila kusahau kutoa elimu kwa umma juu ya umuhimu wa Ulinzi na Usalama wa nchi na mipaka yetu dhidi ya adui yeyote awe kutoka ndani au nje ya mipaka ya Tanzania.
<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<
9.5.2 Mapendekezo ya Watazamaji

Kimsingi, baadhi ya mapendekezo yaliyotolewa na watazamaji wa uchaguzi ni kamaifuatavyo: -(i) elimu ya mpiga kura iendelee kutolewa kwa vyama vya siasa, mawakala nawatendaji wa vituo;(ii) ushirikishwaji wa watu wenye mahitaji maalum katika uchaguzi uboreshwe;(iii) juhudi zifanyike kuboresha mazingira ya kufanya siasa;(iv) utaratibu wa kuwatambulisha mawakala wa vyama vya siasa upitiwe upya; na(v) sheria za uchaguzi zifanyiwe marekebisho katika maeneo yafuatayo: -(a) matokeo ya uchaguzi wa Rais yaruhusiwe kupingwa mahakamani;(b) wagombea wa Ubunge na Udiwani wanaopita bila kupingwa wapigiwe kura kama ilivyo kwa mgombea wa nafasi ya kiti cha Rais;(c) utaratibu unaotumika kuwateua Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ufanyiwe marekebisho; na(d) mawakala wa vyama vya siasa wapewe vitambulisho mapema kabla ya siku ya uchaguzi.

10.4.8.2 Mapendekezo ya Kuboresha Mwitikio wa Wapiga Kura
Washiriki wa zoezi la tathmini kutoka katika makundi ya wazee, vijana, watu wenyeulemavu na wanawake walipendekeza mambo yafuatayo ili kuboresha mwitikio wa104wapiga kura katika chaguzi zijazo. Baadhi ya mambo yaliyopendekezwa ni yafuatayo: -(i) elimu ya mpiga kura iwe endelevu na itolewe kwa muda mrefu zaidi kwa maeneoyote nchini hasa vijijini;(ii) asasi za kiraia na taasisi nyingine zinazohusika na utoaji wa elimu ya mpiga kuraziruhusiwe kutoa elimu endelevu;(iii) uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura uwe endelevu;(iv) watendaji wa Tume waendelee kusimamia uchaguzi kwa kuzingatia sheria, kanunina maadili ya kazi zao bila upendeleo; na(v) Tume ianzishe utaratibu wa kupiga kura kwa njia ya mtandao (electronic voting).

SURA YA KUMI NA MBILI
HITIMISHO NA MAPENDEKEZO
12.1 Hitimisho
Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliendesha zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 kwamafanikio. Mafanikio hayo yalitokana na hali ya amani na utulivu iliyokuwepo nchini nautekelezaji wa mipango iliyojiwekea. Mipango hiyo ilitekelezwa kwa kuzingatia Katiba,sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.Katika maandalizi ya uchaguzi mkuu, Tume ilihakiki vituo vya kuandikisha wapiga kurana kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Baada ya kukamilisha zoezi la uboreshajiwa Daftari, Tume iliandaa vituo vya kupigia kura. Vilevile, Tume ilifanya ununuzi nausambazaji wa vifaa vya uchaguzi, uteuzi wa watendaji wa uchaguzi na mafunzo, uteuziwa wagombea, kushughulikia rufaa za wagombea, uratibu wa kampeni za uchaguzi,utoaji wa elimu ya mpiga kura, kusimamia zoezi la kupiga na kuhesabu kura, kujumlishana hatimae kutangaza matokeo ya uchaguzi.Kwa ujumla, zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 liliendeshwa na kuratibiwa kwamafanikio. Aidha, maoni na mapendekezo mbalimbali ya watazamaji waliowasilishataarifa zao yanabainisha kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru, wa haki na wa kuaminika.
12.2 Mapendekezo
Ili kuboresha uendeshaji wa uchaguzi, Tume inapendekeza yafuatayo: -(i) itungwe sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo itaiwezesha Tumekutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi;(ii) kuwe na watendaji wa Tume hadi ngazi ya halmashauri;(iii) mamlaka husika ziangalie uwezekano wa kuunganisha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi,Sura ya 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 ili kurahisishautekelezaji wa sheria hizo;(iv) sheria za uchaguzi zitafsiriwe kwa lugha ya Kiswahili; na(v) Serikali iangalie uwezekano wa kuziwezesha kifedha asasi na taasisi zinazotoaelimu ya mpiga kura katika hatua mbalimbali za mchakato wa uchaguzi.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
 
🤣🤣mshahara unatoka tarehe 21,watakuwa wameshiba ready kufanya usafi sweapers moopers 👁️
 
Ndio maana katiba mpya ni muhimu mno,Amiri jeshi akiamua kuliingiza jeshi mitaani ni LAZIMA BUNGE lilidhie,elewa kuwa mwanajeshi anafundishwa vita sio protest controls na mwanajeshi hana mabomu ya machozi au rubber bullets, RC ilitakiwa awe ameshawasilisha barua ya ku resign au angeomba apology kwa wote walioguswa na kauli yake
 
Kitu ambacho hajui, hao wanajeshi wanaweza toka kambini kuja kufagia kisha wakaungana na waandamanaji wanaoenda ofisi za UN na kupindisha msafara huo kuelekea Magogoni ili kusafisha hadi ndani maofisini na kuweka makazi kwa ulaini kabisa.
Wasiwachukulie poa hawa mabakamabaka, hata wao bei za sukari, mchele , matibabu yao na wazazi wao na maumivu yote wanaumia kama wengine tuu.

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
🤣
 
Back
Top Bottom