Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,772
- 218,394
Jeshi la Wananchi wa Tanzania ni Taasisi kubwa sana, si Taasisi inayoweza kutumika Kisiasa kama anavyotaka kufanya RC wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ama Chalamila hajui mipaka ya Cheo Chake au analeta Usanii wake uliozoeleka, Bali ninachokijua ni Kwamba Chalamila ameropoka bila ku consult kiongozi yeyote wa juu.
Jeshi la Wananchi haliwezI kutii maagiizo ya kijinga kutoka kwa kiongozi wa chini kama Mkuu wa Mkoa, linaweza kutii maagizo ya Rais, Waziri wa Ulinzi au Mkuu wa Majeshi, Tuliwahi kumkataza Mkuu mmoja wa Wilaya Humu kuacha kuvaa sare za Jeshi kwenye shughuli zake (Tunashukuru kwamba alituelewa )
Kwahiyo nachukua nafasi hii kumkumbusha ndugu Chalamila kwamba hana mamlaka yoyote yale ya kuliamrisha Jeshi la Wananchi katika jambo lolote lile, kwanza anapaswa kuwajibika kwa kujiuzulu kutokana na dharau kwa JW kwa kulipa kazi ya kusafisha mitaro, hii si kazi ya JW, vinginevyo atueleze hawa Wakandarasi wazoa taka wanaolipwa hela nyingi na Wananchi wapo kwa ajili ya nini.
Natoa wito kwa viongozi wa chini kama hawa Wakuu wa Mikoa kuacha kukwepa hoja za kisiasa na kujificha kwenye majeshi yetu, Huo ni Udhalilishaji, Sisi wananchi hatutakubali .
Jeshi la Wananchi haliwezI kutii maagiizo ya kijinga kutoka kwa kiongozi wa chini kama Mkuu wa Mkoa, linaweza kutii maagizo ya Rais, Waziri wa Ulinzi au Mkuu wa Majeshi, Tuliwahi kumkataza Mkuu mmoja wa Wilaya Humu kuacha kuvaa sare za Jeshi kwenye shughuli zake (Tunashukuru kwamba alituelewa )
Kwahiyo nachukua nafasi hii kumkumbusha ndugu Chalamila kwamba hana mamlaka yoyote yale ya kuliamrisha Jeshi la Wananchi katika jambo lolote lile, kwanza anapaswa kuwajibika kwa kujiuzulu kutokana na dharau kwa JW kwa kulipa kazi ya kusafisha mitaro, hii si kazi ya JW, vinginevyo atueleze hawa Wakandarasi wazoa taka wanaolipwa hela nyingi na Wananchi wapo kwa ajili ya nini.
Natoa wito kwa viongozi wa chini kama hawa Wakuu wa Mikoa kuacha kukwepa hoja za kisiasa na kujificha kwenye majeshi yetu, Huo ni Udhalilishaji, Sisi wananchi hatutakubali .