mchumia tumbo
JF-Expert Member
- Jun 19, 2012
- 1,459
- 476
Hongereni cdm.
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa).
Hivi tuliposhindwa Arumeru tulikataa kumbe?
Shikamoo chadema
hukuwahi kuleta ubabe wa kutaka kuvua watu magamba ndani ya siku 90, umeishia wapi na ubabe wako??
Hapo kwenye RED hapo,sio huyu tu,hata Juliana Shonza na Mtela Mwampamba mnawaona kama watu muhimu lakini mnawakatisha tamaa makada wenu wengine hasa vijana,lakini kumbukeni kama hawa vijana MTEla na shonza mliweza kuwarubuni wanaweza kurubunika pia,sio watu wazuri sana,jitahidini kutumia makada wenu mliokuwa nao,naamini matokeo haya yameipaisha sana CDM na kuwashusha wale wanazi wa siasa za mauaji na chuki.Wewe nape kijana mwenzangu nakuheshimu sana katika siasa ila naomba ujue kuwa kuna kitu ktk auditing kinaitwa root cause, sina shaka unajua maana yake. Siku mkikaa kutathimini matokeo haya tafuta root cause ya nyie kushindwa. CCM itaangamia kwa sababu ya kuwatumia watu wasio kuwa na matamko yenye heshima kwa raia, vilevile hao ma RC nao ni janga jingine, ifike mahala ma RC waache kutumia polisi kisiasa hasa ktk maeneo ambayo ccm inakataliwa. Pia jadili mtu huyu mwigulu, sijui kama anafaa kuwa mpiga kampaini. Ndo hayo bro. wangu.
Hongera Nape kwa busara, ila pia nikupongeze pia siasa zako ni za hoja si kama muuaji mwigulu, huyo jamaa ni janga la ccm, na bado anazidi kuchimbia kaburi chama.
Ushauri huu unamfaa MwiguluNape namna zenu za kuendesha siasa kwa mwamvuli wa CCM umekitenganisha chama na wananchi. Tafakari.
Kimkakati yuko peke yake,nafikiri ame prove failure,maana najua hata ile ishu ya kuvua gamba imeshindikana Nape Nnauye turn back hakuna atakae kucheka.Kwa mara ya kwanza kama mpinzani mkuu wa CCM kwa sera zao za kiuovu, ubabe, wizi, mauaji na ushetani wote ........ nimemuonea huruma sana Nape Nnauye ! Pole kaka ...
Mchumi wa BOT,aliepata 1st Class,leo nimegundua kwa nini watu wanaiba BOT kirahisi.Bwana Nape Nnauye,
Nawashauri mwendelee sana kumtumia Mwigulu Nchemba,
Jamaa ni "Jembe" kweli kweli na tunaona matokeo yake CCM mnapolitumia kukatia shamba la miwa
Duh! mpk mumekubali hili game kuwa mumepoteza,hakika mlitaitiwa.....