Mkuu Nape, pamoja na mapungufu yanayoendelea kusababishwa na CCM, lakini mawazo kama haya ya kwako ni ya msingi kabisa. Ni vema tukubali pale tunaposhindwa ili amani ya nchi iendelee kutamalaki. Pro- CDM (baadhi yenu) mna mihemko ya hali ya juu sana, alichoongea Nape hata kama huwa natofautiana naye kwa mambo mengi lakini katika hili ametumia lugha nzuri ya kistaarabu na ninaamini hivi ndivyo inavyotakiwa na wanasiasia wote, hongera Nape kwa kukubali kushindwa.
Angalizo:
Mwigulu, Mwampamba na Shonza kama ndio mnaowategemea sijui CCM mnaipeleka wapi, lakini adui yako muombee njaa, bora muendelee kuwatumia ili CCM ing'oke bila kuendelea kumwaga damu za watu, zilizomwagika zinatosha .