Tiba
JF-Expert Member
- Jul 15, 2008
- 4,607
- 3,191
Ndugu yangu Tiba ; Tatizo ndani ya CCM sasa kila mtu na lwake. Ukimuambia Nape awashauri wenzake, ukumbuke ni Nape huyu huyu aliekuwa kwenye harakati za uvuaji magamba.Akatuambia magamba wamepewa siku ngapi vile? Nadhani ndani ya CCM, sasa kila mtu anafanya kinachomjia kichwani na hataki ushauri.Wangekuwa ni watu wakushaurika, basi mwigulu angekuwa ashasikia ushauri anaopewa humu.
Mkuu Betlehem, Mwigulu hawezi kusikia anachoambiwa wala kushauriwa kupitia JF kwani CCM hawataki ushauri kutoka kwa mtu yeyote anayeonekana ana muelekeo wa upinzani. Nikadhani labda mwenzake Nape anaweza kuwashauri Wazee wa chama wauone ukweli kwamba Mwigulu anaipeleka kuzimu CCM kwa speed ya ajabu. Anyway mwenye macho haambiwi ona.
Tiba