Uchaguzi una kushinda na kushindwa...

Uchaguzi una kushinda na kushindwa...

Hayo ni matunda ya ccm kurusha mabomu huku wakilindwa na mapolis. Ccm hamfai kuendelea kuongoza taifa letu!
 
pole gamba naona umenyeshewa mvua

naona gamba linalouwa watu kichwa chini

2.jpg
Liti Mungu angetupa nafasi ya kuujua undani mioyo ya watu tuwaonao kwa macho.
 
Gharama kubwa sana hizi za chaguzi ndogo KATIBA MPYA haitatusaidia? Kuna shule za msingi nyingi tu kwenye Jiji hili la Arusha watoto wanakaa chini sakafu isiyo hata simenti lakini uliza gharama walizotumia wafuatao:
-Tume ya Taifa ya Uchaguzi;
-CCM;
-CHADEMA;
-Wagombea wenyewe.
Tutagharamia SIASA kwa mtindo huu hadi lini? Tumeanza uchaguzi huu tangu mwaka 2010 hadi leo tunaendelea kuchaguana!
 
Swali la kizushi nililokumbana nalo mtaani kwetu ni hili: Hivi Mh Mbowe na Dr Slaa wakiacha UONGOZI MKUU CHADEMA, Arusha kutabaki hivi?
 
Una vingapi umeuliza humu ndani na watu wakakujibu bila kukuona una matatizo..??? Au kunya aje kuku akija bata kaharisha..??? Hili ni weweseko la kushindwa uchaguzi..

Uchaguzi usi na tija wala hautuumizi kichwa, tumeusahau zamani, sana.
 
Fujo ndo zinawapaga kura ccm so jana hakukuwa ana fujo ndo maana Raia hawakujitokeza.police wawe wapole hakuna mtanzania yeyote aneweza kuanzisha fujo kwenye jambo la maana kama uchaguzi.Wakiendelea kuwa watulivu kama jana Arusha wataona watanzania ni watu wa rangi gani........
 
CCM unakaribia mwisho! nyerere alisema uking'ang'ania sana uongozi mwisho utaogopa kung'atuka maana makosa yazidi mno- this is what is happening to CCM, inaogopa kung'oka maana wana madhambi mengi!
:smile-big:
 
Uchaguzi usi na tija wala hautuumizi kichwa, tumeusahau zamani, sana.

Kwa nini mlishiriki uchaguzi huu "usio na tija"? Nikwambie kitu zomba, CCM haijawahi kutoambulia kiti angalau kimoja kati ya viwili vinavyogombewa katika uchaguzi wowote nchi hii. Hili ni pigo takatifu kama wewe ni mkristo!
 
kwa mara nyingine umekubali na umeliona hilo kuwa katika kila jambo (hasa uchauguzi wa arusha) kuna kushinda au kushindwa kilichobakia tuiendeleze na kujenga nchi yetu
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mambo yote yamekwenda sawa).
 
siasa za nchi hii ni ngumu sana na hasa kwa baadhi ya wanasiasa sijui wanataka kutupeleka wapi mwisho wa siku
 
Pole sana bwana Nape.Arusha hatutaki kabisa kusikia huo ujinga wenu wa CCM.
 
CCM wakubali katika hili wakae kitako wajiulize wamekosea wapi then wajirekebishe warudi wanjani 2015 kwani kuvunjika kwa koleo si mwisho wa uhunzi. by ole Rikanga.

2.jpg
[/QUOTE]
 
Jamani kama wazazi na kama wadau wa Elimu katika Tanzania nani anajua ni Ruzuku kiasi gani inatolewa na serikali katika shule yako aidha ya Msingi au Sekondari na je mtoto wako kama anasoma huko anapata kiasi gani kwa mwaka?
 
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mambo yote yamekwenda sawa).

Kauli kama hii ingekuwa ndio dhamira kwa vitendo kwa CCM na viongozi wake, nchi hii ingepiga maendeleo walau kwa kuacha haki itawale.

Nnape na wenzio kumbukeni kuwa watanzania hatutaki siasa chafu zilizojaa chuki, fitina na chokochoko ilimradi tu washenzi wachache watawale nchi wanavyotaka na kwa maslahi yao na washenzi wenzao. Tunataka HAKI SAWA ktk siasa na chaguzi huru.

Siasa za hovyo ndio zinatuletea mafisadi na viongozi wa hovyo kabisa. Nchi hii si mali yenu wanasiasa ambao kwanza ni wachache mno! Nchii hii ni ya watanzania wote. Acheni siasa chafu demokrasia ishike mkondo wake!
 
Watanzania tuamke wakati umefika wa kuwachagua wanaoaminka kuongoza kwa uadilifu bila kujali wanatoka chama gani.Hivi sasa vyama vya siasa vimegeuka klabu za mpira kila moja kutaka ushindi kwa vigezo vya uzoevu au rangi ya bendera ya vyama vyao bila kujali matakwa ya wananchi kwa wakati huu
 
Kwa nini mlishiriki uchaguzi huu "usio na tija"? Nikwambie kitu zomba, CCM haijawahi kutoambulia kiti angalau kimoja kati ya viwili vinavyogombewa katika uchaguzi wowote nchi hii. Hili ni pigo takatifu kama wewe ni mkristo!

Hivyo si marudio tu, overhaul winner ni nani?
 
Back
Top Bottom