Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,338
- 9,766
Ndugu zangu watanzania,
Uchaguzi ujao Ni uchaguzi ambao CCM inakwenda ikiwa na ushindi mkononi, uchaguzi ambao CCM inakwenda ikiwa na Matokeo ya ushindi wa kishindo, Hii Ni kutokana na kazi kubwa Sana iliyofanywa na serikali ya CCM chini ya uongozi shupavu na madhubuti wa Rais Samia katika utekelezaji wa ilani ya CCM.
CCM inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa na uungwaji mkono na kibali na baraka kutoka makundi yote kutokana na utendaji kazi wa serikali yake uliyogusa makundi yote pasipo kumwacha mtu nyuma au kundi lolote lile,Inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa imejibu maswali yote na kero zote kubwa kwa kuzipatia majibu ya kuridhisha.
CCM inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa imejiwekea Rekodi mpya ya maendeleo katika secta zote kuanzia Elimu ambapo Sasa Ni bure Hadi kidato Cha sita, huku ikiwa imeongeza bajeti ya mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu kufikia biliioni 654 kiasi kilichopelekea wanafunzi wote wenye sifa kupata mikopo bila shida ya aina yoyote pamoja na kuongeza fedha za kujikimu kufikia elfu kumi kwa siku Jambo lililoibua shangwe kubwa Sana hapa nchini.
CCM inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa imejihakikishia kura za Ndio kwa wakulima baada ya kuwafuta machozi na kuwaheshimisha kwa kukifanya kilimo ni biashara na hivyo kuwafanya kunufaika na jasho lao,huku mabillioni ya Ruzuku takribani billioni Mia moja hamsini yakiwa yametolewa na serikali ya CCM zilizo pelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa Elfu 70 tu.
CCM inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa inaungwa mkono na wafanyabiashara wote hapa nchini baada ya kuwa mazingira ya biashara yameboreshwa kwa kuweka Sera nzuri na kuwa na maafikiano mazuri na yenye Afya na tija katika ukadiriaji wa Kodi ,Sasa biashara zinafunguliwa kila Kona ya nchi hii badala ya kufungwa,Sasa TRA na maafisa wake wanatenda haki na kuwatendea haki wafanyabiashara na hivyo kujenga Hali ya kuaminiana katika ulipaji wa Kodi,Hali iliyopelekea kupanda kwa mapato kufikia Trioni mbili kwa Mwezi.
Ni uchaguzi utakao kuwa mwepesi Sana kwa CCM kupita na kuweza kushinda,inakwenda kuzoa Kura kwa kishindo Sana katika nafasi zote,Ni historia mpya inakwenda kuandika hapa nchini katika uchaguzi huo.
Kazi Iendeleee mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
0742-676627
Uchaguzi ujao Ni uchaguzi ambao CCM inakwenda ikiwa na ushindi mkononi, uchaguzi ambao CCM inakwenda ikiwa na Matokeo ya ushindi wa kishindo, Hii Ni kutokana na kazi kubwa Sana iliyofanywa na serikali ya CCM chini ya uongozi shupavu na madhubuti wa Rais Samia katika utekelezaji wa ilani ya CCM.
CCM inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa na uungwaji mkono na kibali na baraka kutoka makundi yote kutokana na utendaji kazi wa serikali yake uliyogusa makundi yote pasipo kumwacha mtu nyuma au kundi lolote lile,Inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa imejibu maswali yote na kero zote kubwa kwa kuzipatia majibu ya kuridhisha.
CCM inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa imejiwekea Rekodi mpya ya maendeleo katika secta zote kuanzia Elimu ambapo Sasa Ni bure Hadi kidato Cha sita, huku ikiwa imeongeza bajeti ya mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu kufikia biliioni 654 kiasi kilichopelekea wanafunzi wote wenye sifa kupata mikopo bila shida ya aina yoyote pamoja na kuongeza fedha za kujikimu kufikia elfu kumi kwa siku Jambo lililoibua shangwe kubwa Sana hapa nchini.
CCM inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa imejihakikishia kura za Ndio kwa wakulima baada ya kuwafuta machozi na kuwaheshimisha kwa kukifanya kilimo ni biashara na hivyo kuwafanya kunufaika na jasho lao,huku mabillioni ya Ruzuku takribani billioni Mia moja hamsini yakiwa yametolewa na serikali ya CCM zilizo pelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa Elfu 70 tu.
CCM inakwenda katika uchaguzi huo ikiwa inaungwa mkono na wafanyabiashara wote hapa nchini baada ya kuwa mazingira ya biashara yameboreshwa kwa kuweka Sera nzuri na kuwa na maafikiano mazuri na yenye Afya na tija katika ukadiriaji wa Kodi ,Sasa biashara zinafunguliwa kila Kona ya nchi hii badala ya kufungwa,Sasa TRA na maafisa wake wanatenda haki na kuwatendea haki wafanyabiashara na hivyo kujenga Hali ya kuaminiana katika ulipaji wa Kodi,Hali iliyopelekea kupanda kwa mapato kufikia Trioni mbili kwa Mwezi.
Ni uchaguzi utakao kuwa mwepesi Sana kwa CCM kupita na kuweza kushinda,inakwenda kuzoa Kura kwa kishindo Sana katika nafasi zote,Ni historia mpya inakwenda kuandika hapa nchini katika uchaguzi huo.
Kazi Iendeleee mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
0742-676627