Tanzania inafuata misingi yote ya Demokrasia ya vyama vingi

Tlaatlaah

JF-Expert Member
May 18, 2023
8,154
11,561
Mapungufu madogo madogo na kasoro chache zilizopo, vipo pia kila mahali inapotekelezwa demokrasia ya aina ya Tanzania, mathalani Marekani na kwingineko.

Na kwasababu hiyo uchaguzi huru na wa haki Tz upo, Tume huru ya uchaguzi Tz ipo, Utawala wa Sheria na utawala bora Tz upo, heshima kwa haki za binadamu na makundi maalumu Tz vipo, uhuru wa maoni, habari, vyombo vya habari na mawasilino Tz vipo, uwazi na uwajibikaji Tz upo, bunge na mahakama huru Tz vipo, usawa na haki ya kupata huduma za msingi Tz vipo, ulinzi na usalama wa watu, mali na makazi yao Tz vipo, uhuru wa kuabudu na kuabudiwa Tz upo, uhuru wa kutoa na kupokea sadaka na misaada Tz upo, nakadhalika nakadhali, nakadhalika, nakadhalika.....

Tunaweza kutofautiana kwa kiwango cha kuridhika cha utekelezaji wa Demokrasia hii ya vyama vingi Tanzania na ufanisi wake. Na hiyo ni haki na ni Demokrasia ya maoni, kutofautiana na kukubaliana kutofautiana.
Mathalani, wingine anaweza kusema hakuna kabisa demokrasia, mwingine akasepa ipo kidogo, mwingine akasema ipo sana, na mwingine akasema hana maoni kabisa juu ya Demokrasia Tanzania, nakadhalika, nakadhalika, nakadhalika...

Lakini, ukweli usemwe,
Amani, Utulivu na utangamano miongoni mwa waTanzania ni matokeo na matunda matamu ya utekelezaji wa Demokrasia nchini. Ni muhimu sana hali hii ya ustahimilivu na kuvumiliana kuimarishwa zaidi ndani ya mioyo ya wanasiasa na watanzani wote ile umaja wetu usitetereke.

Maendeleo ya watu na makazi yao, maendeleo ya biashara, utalii, miundombinu ya barabara, anga, maji, reli, afya elimu, michezo na vyote vinavyoonekana na visivyo onekana kisiasa, kiuchumi na kijamii ni zao la Demokrasia ya vyama vingi nchini.

Kwa kiwango kikubwa sana maendeleo yanayonekana hivi sasa yamechochewa pakubwa sana na utekelezaji wa demokrasia ya vyama vingi. Mathalani uwazi, uwajibikaji, ulinzi na usalama serikalini.

Changamoto ndogo ndogo na kasoro chache zilizopo na mara nyingi huonekana nyakati za uchaguzi, zinarekebishika na kutatulika ikiwa tu utashi wa kisiasa na dhamira ya kweli miongoni mwa wanasiasa utawekwa kwenye mizania sawa kwa maneno na matendo, kwa maslahi mapana ya umoja na mshikamano wa Tanzania.

Njia zinazotumiwa na wanasiasa kujaribu kushinikiza marekebisho ya mapungufu na kasoro za kidemokrasia nchini, zinarefusha zaidi kupata majawabu. Ushari wa maneno ya wanasiasa dhidi ya serikali, amri na matakwa ya lazima ya wanasiasa dhidi ya serikali, ubabe na utoto wa wanasiasa dhidi ya serikali, nakadhalika nakadhalika nakadhalika.....

Hakuna ungwana, ustaarbu wala utashi katika kauli na matendo miongoni mwa wanasiasa dhidi ya serikali. Ni kutunishiana misiuli kusiko koma, kutwa kucha ni kiburi na majivuno cha eti chama hiki au kile kina wafuasi wengi kuliko kingine na kwahivyo kina haki zaidi na kinaweza kufanya chochote itakacho.

Hii si sawa.
Huu ni mwanzo wa kuharibu na kumomonyoa demokrasia ambayo tayari imekomaa, imeimarika, inashamiri na kunawiri vizuri sana nchini.

Kama raia wa Tanzania navisihi vyama vya siasa na wanasiasa, vyama vya kiraia, taasisi za dini na makundi mbalimbali ya kutetea haki nchini,
fanyieni vyovyote mfanyavyo kwa mujibu wa sheria.

Lakini chondechonde, matokeo ya hayo yote muyafanyayo iwe ni Amani, Amani, Amani, ya huyu Mama Yetu Tanzania.

wasaalam.....
 
Breafly'democracy' means rule of people (minority) over/rule majority, but typically who are the people?women,childs or men?then here we seen the word 'democracy' itself doesn't totally reflect the reality becoz it exclude childs from decesion making/vote kwahy tunakuja kutambua demokrasia ina mipaka,tamaduni na exclude baadh ya mambo.
 
Mapungufu madogo madogo na kasoro chache zilizopo, vipo pia kila mahali inapotekelezwa demokrasia ya aina ya Tanzania, mathalani Marekani na kwingineko.

Na kwasababu hiyo uchaguzi huru na wa haki Tz upo, Tume huru ya uchaguzi Tz ipo, Utawala wa Sheria na utawala bora Tz upo, heshima kwa haki za binadamu na makundi maalumu Tz vipo, uhuru wa maoni, habari, vyombo vya habari na mawasilino Tz vipo, uwazi na uwajibikaji Tz upo, bunge na mahakama huru Tz vipo, usawa na haki ya kupata huduma za msingi Tz vipo, ulinzi na usalama wa watu, mali na makazi yao Tz vipo, uhuru wa kuabudu na kuabudiwa Tz upo, uhuru wa kutoa na kupokea sadaka na misaada Tz upo, nakadhalika nakadhali, nakadhalika, nakadhalika.....

Tunaweza kutofautiana kwa kiwango cha kuridhika cha utekelezaji wa Demokrasia hii ya vyama vingi Tanzania na ufanisi wake. Na hiyo ni haki na ni Demokrasia ya maoni, kutofautiana na kukubaliana kutofautiana.
Mathalani, wingine anaweza kusema hakuna kabisa demokrasia, mwingine akasepa ipo kidogo, mwingine akasema ipo sana, na mwingine akasema hana maoni kabisa juu ya Demokrasia Tanzania, nakadhalika, nakadhalika, nakadhalika...

Lakini, ukweli usemwe,
Amani, Utulivu na utangamano miongoni mwa waTanzania ni matokeo na matunda matamu ya utekelezaji wa Demokrasia nchini. Ni muhimu sana hali hii ya ustahimilivu na kuvumiliana kuimarishwa zaidi ndani ya mioyo ya wanasiasa na watanzani wote ile umaja wetu usitetereke.

Maendeleo ya watu na makazi yao, maendeleo ya biashara, utalii, miundombinu ya barabara, anga, maji, reli, afya elimu, michezo na vyote vinavyoonekana na visivyo onekana kisiasa, kiuchumi na kijamii ni zao la Demokrasia ya vyama vingi nchini.

Kwa kiwango kikubwa sana maendeleo yanayonekana hivi sasa yamechochewa pakubwa sana na utekelezaji wa demokrasia ya vyama vingi. Mathalani uwazi, uwajibikaji, ulinzi na usalama serikalini.

Changamoto ndogo ndogo na kasoro chache zilizopo na mara nyingi huonekana nyakati za uchaguzi, zinarekebishika na kutatulika ikiwa tu utashi wa kisiasa na dhamira ya kweli miongoni mwa wanasiasa utawekwa kwenye mizania sawa kwa maneno na matendo, kwa maslahi mapana ya umoja na mshikamano wa Tanzania.

Njia zinazotumiwa na wanasiasa kujaribu kushinikiza marekebisho ya mapungufu na kasoro za kidemokrasia nchini, zinarefusha zaidi kupata majawabu. Ushari wa maneno ya wanasiasa dhidi ya serikali, amri na matakwa ya lazima ya wanasiasa dhidi ya serikali, ubabe na utoto wa wanasiasa dhidi ya serikali, nakadhalika nakadhalika nakadhalika.....

Hakuna ungwana, ustaarbu wala utashi katika kauli na matendo miongoni mwa wanasiasa dhidi ya serikali. Ni kutunishiana misiuli kusiko koma, kutwa kucha ni kiburi na majivuno cha eti chama hiki au kile kina wafuasi wengi kuliko kingine na kwahivyo kina haki zaidi na kinaweza kufanya chochote itakacho.

Hii si sawa.
Huu ni mwanzo wa kuharibu na kumomonyoa demokrasia ambayo tayari imekomaa, imeimarika, inashamiri na kunawiri vizuri sana nchini.

Kama raia wa Tanzania navisihi vyama vya siasa na wanasiasa, vyama vya kiraia, taasisi za dini na makundi mbalimbali ya kutetea haki nchini,
fanyieni vyovyote mfanyavyo kwa mujibu wa sheria.

Lakini chondechonde, matokeo ya hayo yote muyafanyayo iwe ni Amani, Amani, Amani, ya huyu Mama Yetu Tanzania.

wasaalam.....
Kwahiyo unaona ni demokrasia kwa Raisi mgombea, kujiteulia tume ya uchaguzi na wasimamizi!
 
Breafly'democracy' means rule of people (minority) over/rule majority, but typically who are the people?women,childs or men?then here we seen the word 'democracy' itself doesn't totally reflect the reality becoz it exclude childs from decesion making/vote kwahy tunakuja kutambua demokrasia ina mipaka,tamaduni na exclude baadh ya mambo.
yes, uko sahihi mkuu.
hayao ni mapungufu na dosara za demokrasia.
zinarekebishika, ikiwa utayari wa maneno na matendo ya washika hatamu na washika dau wakiwa waungwana miongoni mwao.
 
yes, uko sahihi mkuu.
hayao ni mapungufu na dosara za demokrasia.
zinarekebishika, ikiwa utayari wa maneno na matendo ya washika hatamu na washika dau wakiwa waungwana miongoni mwao.
kweli ,ujue kuna jambo moja weng hatulitak kuwaza ujue changes its abt uncertanity nd replacement kuna mambo tukiyaondoa na tukataka pure democracy basi mtaani hatutotosha mfano mdogo angalia CHADEMA njia yao ya kudai haki ni demostration unajua how will happens after const changes?
 
Kwahiyo unaona ni demokrasia kwa Raisi mgombea, kujiteulia tume ya uchaguzi na wasimamizi!
nimebainisha kwa mifano kabisa, demokrasia ipo, lakini pia zipo changamoto kwenye hiyo demokrasia, na nikaenda mbali zaidi kubainisha kua kuna utofauti katika kuridhika na utekelezaji wa hiyo demokrasia humu, zaid sana nikapendekeza nini kinaweza fanyika kuzitatua dosari na mapungufu ya hiyo demokrasia, ikiwa ni pamoja na hiyo changamoto uliyoibainisha wewe ingawa na hisi unazo changamoto zaid ya hiyo.

kusema tu kua Raisi anajiteulia tume ya uchaguzi au anachagua wasimamizi wa uchaguzi, bado haitasaidia na sio suluhisho.
 
Demokrasia ya kupitishana bila kupingwa inapatikana Tanzania tu tume huru ya kuengua wapinzani peke yake ipo Tanzania tu,tume huru ya kujaza kura fake kuibeba CCM ipo Tanzania tu,tume huru inayofanyia kazi maelekezo ya kuibeba CCM ipo Tanzania tu,tume huru ambayo wapinzani pekee ndio hawajui kujaza form za uchaguzi inapatikana Tanzania tu,demokrasia ambayo intelejensia yao inaonyesha uvunjifu wa amani ya nchi ni kwa wapinzani peke yao inapatikana Tanzania tu,tume huru ambayo wapinzani ndio wanaotekwa na kuporwa form za uchaguzi na haikemei matukio hayo inapatikana Tanzania tu.
 
Machafuko tu ama mapinduzi ya kijeshi ndio njia za kweli za kuleta mabadiliko ya kweli hapa nchini.
HAMNA HAJA YA HAYO. NCHI INATAKIWE IWE NA AMANI.
TATIZO NI KATIBA::
MMOJA ANAMTEUA MSIMAMIZI KUAMUA JAMBO AMBALO NAE ANALITAKA
 
Back
Top Bottom