Ni uongo Kudai 80% Walikataa Mfumo wa Vyama Vingi

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,057
Hakukuwahi kuwa na kura ya maoni ya kuwauliza wananchi kama wanataka mfumo wa vyama vingi au kuendelea na mfumo wa chama kimoja.

Hakukuwahi kuwa na tangazo lolote la kuwataka wananchi watoe maoni mahali popote kama wanataka mfumo wa vyama vingi.

Kilichofanyika ni kwamba wakati uchumi wa nchi umedorora sana, na nchi inahitaji usaidizi wa mataifa makubwa, na kunyimwa, sababu mojawapo ikiwa uminywaji wa demokrasia, Mwalimu Nyerere alitamka kwenye kikao cha Halmashauri Kuu kuwa tunalazimishwa kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi wakati wananchi hawaoni huo umuhimu. Ebu tuulizane kama kweli kuna haja hiyo?

Kama ilivyo kawaida ya CCM, hufanya mambo kwa unafiki wa kumfurahisha Mwenyekiti wao, wakijua kuwa Mwalimu hataki mfumo wa vyama vingi, wakaulizana humo ndani ya chama, wakamwendea Mwalimu na kumwambia kuwa wananchi hawataki mfumo wa vyama vingi.

Mwalimu Nyerere kwa sababu alijua taarifa ile ni ya uwongo, na wala hakujafanyika kura yoyote ya maoni, na mazingira ya kiuchumi yakiwa yameibana nchi, akayapuuza yale maoni, na kusema nchi itaingia kwenye mfumo wa vyama vingi. Viongozi wanafiki wa CCM, kama kawaida yao wakashangilia na kumpongeza Mwalimu Nyerere kwa uamuzi huo.

Kwa hiyo ni uwongo kusema kuwa wananchi waliulizwa kuwa kama wanataka mfumo wa chama kimoja au vyama vingi, halafu wananchi wakatamka kuwa wanataka mfumo wa chama kimoja. Mahojiano yalifanyika kwenye vikao vya CCM, siyo kwa umma wa wananchi wote.
 
Sidhani kama umri wa mleta uzi huu, unaweza kubadilisha ukweli aliouandika!
Hakuna kura iliyopigwa kuulizia suala hilo. Kama kuulizana, labda waliulizana makada waliokuwepo wakati huo!
Na wewe umezaliwa lini? Una uwelewa upi katika suala unalolizungumzia? Kama unalizungumzia kwa hisia basi wewe na mwenzake mko sahihi!
 
Hakukuwahi kuwa na kura ya maoni ya kuwauliza wananchi kama wanataka mfumo wa vyama vingi au kuendelea na mfumo wa chama kimoja.

Hakukuwahi kuwa na tangazo lolote la kuwataka wananchi watoe maoni mahali popote kama wanataka mfumo wa vyama vingi.

Kilichofanyika ni kwamba wakati uchumi wa nchi umedorora sana, na nchi inahitaji usaidizi wa mataifa makubwa, na kunyimwa, sababu mojawapo ikiwa uminywaji wa demokrasia, Mwalimu Nyerere alitamka kwenye kikao cha Halmashauri Kuu kuwa tunalazimishwa kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi wakati wananchi hawaoni huo umuhimu. Ebu tuulizane kama kweli kuna haja hiyo?

Kama ilivyo kawaida ya CCM, hufanya mambo kwa unafiki wa kumfurahisha Mwenyekiti wao, wakijua kuwa Mwalimu hataki mfumo wa vyama vingi, wakaulizana humo ndani ya chama, wakamwendea Mwalimu na kumwambia kuwa wananchi hawataki mfumo wa vyama vingi.

Mwalimu Nyerere kwa sababu alijua taarifa ile ni ya uwongo, na wala hakujafanyika kura yoyote ya maoni, na mazingira ya kiuchumi yakiwa yameibana nchi, akayapuuza yale maoni, na kusema nchi itaingia kwenye mfumo wa vyama vingi. Viongozi wanafiki wa CCM, kama kawaida yao wakashangilia na kumpongeza Mwalimu Nyerere kwa uamuzi huo.

Kwa hiyo ni uwongo kusema kuwa wananchi waliulizwa kuwa kama wanataka mfumo wa chama kimoja au vyama vingi, halafu wananchi wakatamka kuwa wanataka mfumo wa chama kimoja. Mahojiano yalifanyika kwenye vikao vya CCM, siyo kwa umma wa wananchi wote.
Hiyo 80% umeinukuu kutoka kwenye source ipi?
 
Mazingira ya kisiasa duniani kuna wakati yanabadilika na kulazimisha wengine kufanya jambo ambalo hawakuwa na mpango nalo, lakini kuna wakati ukifika, kwa kupenda au kutopenda, lazima mtafuata kule ulimwengu unapoelekea.

Hili la mfumo wa vyama vingi kwa mfano, niseme tu Nyerere alikuwa anaona mbali zaidi ndio maana akaliruhusu licha ya wengi chamani kulikwepa, kwa maana kwamba, hata kama Nyerere nae angelikwepa, bado lingetokea tu kwa mwingine.

Tena kwa hizi nchi zetu, zisizojiweza kwa lolote ndio balaa zaidi, utegemezi umetufanya tuwe wakuwasikiliza wazungu kwa kila wanachotaka, hatuna last say hata kwenye mambo yetu ya ndani, kama mpaka sehemu ya bajeti yako unategemea misaada toka nje, hatuna maana kabisa.
 
Kukataa vyama vingi haimaanishi kukataa Upinzani

Hata sasa Upinzani wa kweli uko ndani ya CCM yenyewe siyo hawa akina Mbowe na Zitto

Nadhani umeelewa😄
Upinzani wa ndani ya chama sio upinzani rasmi maana ni rahisi kuu-control ,si umeona Ndugai/Polepole/Kakurwa walivyonyamzishwa? SSH anaweza kumnyamazisha Mbowe/Lissu/Mwabukusi/Lema/Heche/Msigwa/Sugu wasiongeee?
 
Back
Top Bottom