Uchaguzi Mkuu wa CCM Mwaka 2007

Uchaguzi Mkuu wa CCM Mwaka 2007

"Mzee Dar na Killtime, mnasema hii habari ina ukweli zaidi ya habari zilizoko kwenye thread yetu? Kubainika ni ukweli as a fact? Halafu hayo magazeti wamechemsha kwa sababu Mbatia hakunyimwa kugombea ujumbe, ila ameondolewa kwenye bodi ya hazina(CCM), lakini bado amepewa nafasi ya kugombea nafasi hiyo ambapo atachuana na Mama Megji! Sisi na wao magazeti tuko boti moja, ni data tu, mpaka kesho CCM watakapotangaza na tutaendelea kuzichokonyoa!

Na the latest zinasema wenyeviti wengi wa CCM wa mikoa wamepigwa chini!"


Mpaka tulisema magzeti yako wrong on Mbatia je ulikuwa udaku? Tena mpaka tukasema majina yatatangazwa kesho yaani leo, si haya yametangazwa leo sasa kama sio gele ni nini? wacheni kushusha heshima ya forum na upayukaji tu bila ukweli!

Forum oyeee! JF juuu zaidi! Where we dare to talk, na data mbele wee!
 
Komandoo aminia, kweli sasa umezaliwa upya na Komandooo haswaaaaaa.

tuendeleee baba yake
 
"Sisi na wao magazeti tuko boti moja, ni data tu, mpaka kesho CCM watakapotangaza na tutaendelea kuzichokonyoa!

Na the latest zinasema wenyeviti wengi wa CCM wa mikoa wamepigwa chini!"


Mpaka tulisema magzeti yako wrong on Mbatia je ulikuwa udaku? Tena mpaka tukasema majina yatatangazwa kesho yaani leo, si haya yametangazwa leo sasa kama sio gele ni nini? wacheni kushusha heshima ya forum na upayukaji tu bila ukweli!

Forum oyeee! JF juuu zaidi! Where we dare to talk, na data mbele wee!

Komandoo ES,

Sikupenda kuongea kwenye siasa lakini naomba niseme kuwa watu msijiangushe kiwango hicho. Huwa nasikitika pale ninapoona watu mnaamini kirahisi kuwa kosa la mwanachama au wanachama flani na imani zao kisiasa ni itikadi ya JF nzima. Basi wewe mbona una itikadi tofauti na yeye? JF kama JF haiko biased na Chama flani ama mtu flani. Mawazo yako ndiyo changamoto ya JF.

BTW: Wale wanaokuja kugundua walikuwa na wrong info au kutambua wazi kuwa walidanganya makusudi nawashauri wawe wawazi kusema 'Kumradhi nilikosea' ili kuweka bayana mambo.

Niwie radhi kwa kuingilia na mjadala mwema 🙂

Invisible
 
hata hivyo wengi wa wanachama wetu hapa wanashabikia chadema, huenda hii by accident au conspiracy kwa definition ya prof Kichuguu.

hata hivyo kama jf nnaamini ni chombo huru.

hii sawa na wanaoamini kuwa wanaume wengi kuliko wanawake sio kosa la jf.

nnatamani suku moja na viongozi wa vyama vyengine wajiunge JF, kama mie ningependekeza Komandoo salmini, Maalim Seif, Juma Duni, Feruzi ili wawakilishe siasa za zanzibar.

JF OYEEEEEEEEEEEEEEEEE, HOJA kwenda mbele
 
Wenzenu wamefanya hivi! Nanyi fanyeni the same, Hapa Mhariri ndiye aliyesema samahani na wala sio yeye aliyekusanya habari, na pia tunategemea Uongozi wa JF ufanye the same, kwa kuanzisha thread nyingine au kwa kumuandikia mpiga majungu afanye hivyo mwenyewe kwa kuweka thread dedicated for that. Ni uungwana tu, kuliko kuacha tuhuma nzito watu wengi waamini ni za kweli kumbe uongo, kwa hiyo twasema ikigundulika bila wasiwasi wowote,,, semeni samahani.

Kumradhi Mlaki, Mbatia

2007-08-03 09:20:38
Na Richard Makore


Katika gazeti la jana tulichapisha kimakosa kwamba Mhe. Rita Mlaki, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Mhe. Salome Mbatia, Naibu wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto wameenguliwa kugombea nafasi za uwakilishi katika Halmashauri Kuu ya CCM.

Tumegundua kwamba taarifa hiyo haikuwa sahihi kwani hawajaenguliwa.

Tunachukua fursa hii kuwaomba radhi, waheshimiwa hao kutokana na usumbufu walioupata kutokana na habari yetu hiyo - Mhariri

SOURCE: Nipashe
 
Kwa yeyote anayeelewa maana halisi ya Forum hawezi kuulaumu uongozi wa Forum kwa kauli za wanachama.

Hata hivyo Uongozi wa JF daima unawasisitiza wanachama kutoa taarifa za kweli na ndiyo sababu Invisible akasema: "BTW: Wale wanaokuja kugundua walikuwa na wrong info au kutambua wazi kuwa walidanganya makusudi nawashauri wawe wawazi kusema 'Kumradhi nilikosea' ili kuweka bayana mambo."

Wanachama wanatakiwa kuheshimu utu wa mtu na kuwachukulia wenzao sawa na wao japokuwa wako tofauti kiitikadi (politically), kiimani, jinsia n.k.

Ukisoma HAPA utaona haya:

Ieleweke kuwa, Yaandikwayo hapa ni mawazo ya wateja wetu na si msimamo wa JamboForums.com ama vinginevyo. Lugha za matusi hazitavumiliwa!

Tutashukuru pale ukiona jambo baya ukatufahamisha tulifanyie marekebisho haraka kabla hujakashifu au kutoa lawama. Sisi ni binadamu na tuna mapungufu yetu.
 
Uongo umekuwa ukiletwa hapa na kila mara members wenye data wamekuwa wakisahihisha na hiyo ndiyo maana ya forum hivyo Admin hapa hahusiki na maoni ya wachangiaji.

Na kwa hili la NEC baada ya ukweli kudhihiri uongo umejitenga na tunasonga mbele! Jambo la msingi ni kuwa JF members wamekuwa wakisahihisha kila pale post isiyo na ukweli inapowekwa na hilo limeimarisha credibility ya JF.

Aluta Continua ...
 
Wanajambo, kuna yoyote anayejua kuhusu Profesa Mark Mwandosya maana nasikia kuwa huyo jamaa ni sworn adversary wa JK. I wonder kama yeye ni member wa NEC au vipi!
 
Admin na Wengine,

Tutashukuru pale ukiona jambo baya ukatufahamisha tulifanyie marekebisho haraka kabla hujakashifu au kutoa lawama. Sisi ni binadamu na tuna mapungufu yetu.

Nimetimiza wajibu wangu kulingana na quote hiyo hapo juu, lakini pia mjue kuna mambo yanaathiri maisha ya mtu anayetungiwa uongo!

Jambo rahisi sana kama jambo hulijui unanyamaza tu, kuna ambalo unalijua litakuja baadaye na utachangia,,, kuliko muda wote kuongea udaku, pamoja na kwamba udaku mwingine unatenguliwa hapa hapa, lakini mwingine hautenguliwi hivyo kuwa wamjamtendea haki huyu mnayemuongelea
 
It is very dissapointing unapoona mtu ameandika mambo ambayo sio sawa na bdala ya kusimama na kusema hapa nilikosea na samahani kwa wale ambao waliumizwa namakosa yangu, wanaanza kuhalalisha hizo habari ambazo zilikuwa ni udaku mtupu.

Wengi hatuko hapa kufuata udaku, tunafuata habari na hoja zilizo imara.

Magazeti yaliyoandika uwongo yameomba msamaha, nyie mlioandika uongo hapa JF mnakaa kimya na kuja na visingizio visivyo na maana kabisa.

JF si ya CHADEMA na kama mnataka kuwaachia CHADEMA itakuwa ni makosa yetu sisi wote. JF lazima ibaki chombo huru ambacho kinakubali mawazo ya aina mbalimbali ili mradi yako sahihi.

Kama huna uhakika na habari basi eleza hivyo kwamba kuna uvumu nk. Imagine mama Mlaki au familia yake kama walikuwa wanasoma kilichoandikwa hapa, unafikiri hata lije liandikwe jambo la maana na la kwali watakuja kuamini tena?
 
Bongolander,

Kwahabari zisizothibitishwa ni kwamba Prof. Mwandosya jina lake limepitishwa kugombea na Mwang'onda kule Mbeya.
 
Yes ni kweli kulikuwa na walakini fulani hapa katika kuripoti hizi habari za mambo yanavyojiri huko ndani ya vikao.

Inaeleweka kutokea makosa hususan pale ambapo kwa baadhi ya waandishi what matters zaidi ni kuzileta hapa kwa haraka zaidi kuliko kuangalia quality ya habari.

Overall JF kama mtandao wa habari una walakini katika kusimamia uletwaji wa habari lakini hii si lawama bali ni observation kwa vile kwa wote wanaofuatilia JF huja hapa si kwa kutafuta habari bali kuangalia analysis inayotolewa.

Inaonekana wazi kabisa JF kama secondary media outlet inayoshughulika na kuchambua habari ni fantastic arena but as ''news factory'' at times we are failing.

Nilinotice jambo moja nikajaribu kusahihisha waandishi kwa PM lakini naona bado watu wamelikosea ni hili la Ridhiwani Kikwete.

Jina lake halipo katika majina yaliyorudishwa kwa vile yeye kwa mujibu wa vyombo vya habari anagombea nafasi ya kuwa mjumbe wa Bagamoyo katika mkutano mkuu na sio NEC, sijui hii ya NEC ilitolewa wapi.

Habari ya yeye kugombea Bagamoyo niliiona hapa:

http://dailynews-tsn.com/habarileo/page.php?id=2046

Nadhani overall kwa chombo kinachooperate kwa misingi ya CITIZEN JOURNALISM mchango wa hapa unasaidia ila ndio hivyo inabidi kuvumilia some lapses za facts hapa na pale.
 
Wazee ninarudia kuwa we are proud na our works on data, tulizozisema zimetokea kama tulivyosema, na hoy ya Ridhiwani wajumbe wote walioshiriki walithibitisha kuwa amepita, aliyekwenda kuliondoa jinalake na baba yake huko ndani zaidi ya uso wa wajumbe,

Froum ikoimara, mpaka leo bado media ya bongo imeshindwa kusema naything kuhusu Nchimbi, sisi tulishasema mapema kwamba he si done! Media ya bongo huwa wanakuja hapa kutafuta data, kwa hiyo tuwe na heshima, Mzee Admin, heshima mbele kwa kuweka mambo sawa,

inaonekana kuna watu wameanza kuzeeka hapa hawawezi ku-comprehend yaliyosemwa jana na leo, na kuona ukweli uko wapi na uongo uko wapi, halafu wanataka kuisingizia forum, tutaendlea na kuweka vitu hapa asiyetaka uasisome lakini usiharibu jina la forum kwa sababu ya chuki zako zisizokuwa na msingi, sisi ni watu wazima hapa, forum juu na data oyeee,

Data juu zaidi na tutaendelea kuziweka hapa, matatizo yenu ya binasfi pelekni hukooooo darhotwire!

samahani ninaweka vitu huku ninaendesha!
 
Komandoo ES,

Soma post ya Said Yakub, uelimike kidogo!!!
 
Wanafiki tu, Majina mengi hawajapublish ambayo yamepitishwa,
Kama mtu alisema hapo....Mangula, Mwandosya, yule mtoto wa Apson....etc
classic CCM
 
Mshauri wa Rais katika mambo ya siasa anaitwa Omar Luwahvi.huyu bwana kabla ya mtandao kuparaganyika alikuwa na marafiki wake wengi kwenye mtandao,mmojawapo ni mahamud Madenge!

madenge sasa hivi ana kesi ya kutoroka(?)mahabusu na kwenda kulala gesti wakati akishikiliwa na polisi wa kituo cha Chang,ombe.Mwingine ni Thomas Nyimbo.kwa wasiojua nyimbo ni mjomba wake Blandina Nyoni ambaye ni katibu mkuu wizara ya...

mwaa 2002 mwishoni Luwhavi alipelekwa Uingereza kwa masomo mafupi na CCM.akiwa huko alikutana na mwanamke wa Kikenya ambaye mpaka sasa uhusiano wake na mwanamke huyo wa kikenya hauko wazi sana.

mwanamke huyo wa kikenya alikuwa na watoto wake wawili ambao alitaka waende akaishi nao huko Uingereza.luwhavi kwa kushirikiana na watumishi wengine wa ofisi ndogo ya CCM Lumumba wakapanga dili ya kuwatorosha watoto hao kupitia Tanzania.

Mahmud Mgimwa wakati huo akiwa Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa CCM mkoa wa Iringa akapewa jukumu la kuwatorosha watoto hao.Walitolewa kenya na kuja kuishi Tanzania

wale watoto walifikia nyumbani kwa Mahmud Mgimwa Magomeni Kagera alikokuwa anaishi na wadogo zake kadhaa bila ya mke wake ambaye wakati huo alikuwa anafundisha kwenye shule moja iitwayo Mwembetogwa

Mtoto wa Luwhavi Fatuma omar Luwhavi akajifanya ni mke wa Mgimwa na wale watoto ni watoto wake wa kambo.wale watoto walipewa majina ya Rehema kwa wa kike na Baraka kwa wa Kiume

Baada ya kutoa majibu ya kujikanganya mbele ya maafisa wa ubalozi wa uingereza safari yao ikafa kifo cha kawaida ingawa Mgimwa alishapewa viza ya kwenda uingereza

wakati huo Luwhavi alikuwa anafikia kwenye guest moja iliyoko magomeni kagera iitwayo Safi Guest House. Hawa ndiyo watu wanaoongoza nchi yetu kwa sasa!

kwangu hata kama baadhi ya habari zao zitatolewa bila ya kuwa sahihi hainichanganyi kwani zilizo sahihi ni mbaya kuliko zisizo sahihi!

kama alitaka kutumia mlango wa nyuma kuwatorosha wakenya wakati hana cheo kwa sasa akiwa ni mshauri wa Rais wa mambo ya siasa atafanya mangapi maovu?
 
kigarama... asante kwa nyeti hizo... angalia watawala wetu wajue kuwa tuko karibu nao sana kuliko wanavyofikiria.
 
KadaMpinzani,

Inasikitisha kwamba unashabikia UDAKU na unaamini hatuwezi ishi au habarishana bila kusema ukweli.

Kubuni uongo just kwa sababu ya mazingira yanaruhusu hivyo, ni sawa sawa na mganga wa kienyeji ambaye siku zote anatumia mazingira ya mgonjwa wake,,, kubuni kwamba amelogwa na mwanamke mweusi jirani yake (of which lazima uwe na jirani mweusi na mwanamke kwa mazingira ya nchini kwetu) hii husabisha wagonjwa kuamini hivyo... Hivi hivi ndivyo mlivyomzuishia ZITTO kwamba ameonja tunda la mwanamke aliyeolewa just b'se walikuwa kwenye mazingira ya kuwa pamoja.

sijasema kwamba nashabikia udaku bali nimekupa hali halisi, jamani mtu yeyote ukumbini nani asiyejua udaku upo popote pale duniani ?? kama nimekosea kukwambia reality then samahani, lakini kamwe sitoshabikia udaku, hayo ni maneno yako na umeyaweka mdomoni kwangu, i deny your ideas !!
 
Back
Top Bottom