Komandoo ES
Kabla ya kusahihisha naomba ieleweke kwamba kukosea ni sehemu ya kujifunza, katika hili la Uchaguzi you have got pretty much lots of information right lakini nadhani comment yako ya mwisho inahitajia marekebisho kidogo:
1. Habari ambazo zimeandikwa sehemu zote na kufanyiwa uhakiki na source yake kuwekwa hapa ziliarifu kuwa Ridhiwani Kikwete anagombea nafasi ya uwakilishi wa wilaya ya Bagamoyo katika MKUTANO MKUU wa chama sio NEC [HALMASHAURI KUU], Wagombea wa Mkutano mkuu kwa lugha za kichama wanatamkwa kama wagombea uwakilishi wa wilaya X, wagombea wa Halmashauri hutajwa kama wagombea Ujumbe wa Halmashauri Kuu Taifa, hili tulikosoana awali naona mkuu kama vile umerejea kule kule, nadhani tunachanganyana kidogo hapa,
Labda kama una source nyingine lakini mimi niliona hapa:
http://dailynews-tsn.com/habarileo/page.php?id=2046
2. Nadhani maelezo yako ya hapa yamekuwa ni kama oversimplification ya kazi za Halmashauri Kuu lakini kimsingi hasa Halmashauri kuu ya CCM kazi zake ni kutoa muongozo wa kisera kwa chama na kuandaa na kupitisha Ilani ya Uchaguzi, katiba ya CCM iliyopo mtandaoni inaonesha kuna jumla ya kazi/majukumu 25! Nadhani maelezo yako yalikuwa ni kujumuisha majukumu yote hayo ingawa kauli yako kama ulivyoitoa haipo kabisa kwenye majukumu ya Halmashauri Kuu.
3. Mheshimiwa hapa kidogo idadi ya wanachama wa Kamati Kuu umeichanganya kidogo, Kamati Kuu ina wajumbe 35 na Halmashauri Kuu ina wajumbe 215 tu. Hii figure ya 100 nadhani ndio zile lapses tulizozungumzia kwenye role ya JF lakini nadhani tuwe makini katika kutoa facts as hizi errors sometimes zinaepukika...
Kwa sasa wajumbe wanaomaliza muda wao hawa hapa:
http://www.ccmtz.org/halmashaurikuu.html
Na Kamati Kuu kama nilivyoandika hapo ina wajumbe 35 ambao wanaingia kwa nafasi zao kutokana na kofia zao nyingine kichama ni hawa hapa kwa sasa:
http://www.ccmtz.org/0kamatikuu.htm
Nadhani hapo Mwawado umepata majibu ya maswali yako hapo juu.Kazi za Mkutano Mkuu Taifa nazo pia ni nyingi ila ndio kama ulivyosema ndio kikao kikubwa zaidi katika chama na kinakutana mara tatu kwa miaka mitano [at least] lakini unaweza kuzipata kazi za mkutano mkuu Taifa kikamilifu hapa:
http://www.ccmtz.org/Katiba_%20ya_ CCM.pdf
Hivyo Komandoo ES Ukifuatilia kwa karibu pia kazi na majukumu ya kamati kuu utaona kuwa ni sawa kabisa kama ulivyosema,
OMBI:
Nisaidie kidogo source ya hizi power za mwenyekiti wa CCM katika ku-overulle maamuzi ya Kamati Kuu, na hakika utaisaidia sana forum kama ukitoa mifano ya kibabe ya Mkapa kwenye Kamati Kuu. Inawezekana ikawa ni nyeti kubwa ''ya jikoni'' nitaelewa ukisema hivyo lakini kwa jinsi ulivyoieleza nadhani inawezekana tukapata chachu kidogo hapa....
Ndimi katika kujaribu kuweka mambo sawa, haya ni maoni binafsi tu katika issue hii ya NEC niliyokuwa nikiifuatilia kwa karibu kama wengine wengi humu....