Binafsi yangu nimekuwa nikijiuliza maswala mengi kulingana na uchaguzi nchini toka mwaka 2000 baada ya CCM kushinda ktk uchaguzi mkuu. Yapo mengi yaliyojitokeza na mengine kujirudia haswa pale vyama vya Upinzani vilipokataa kuunganisha nguvu yao sio dhidi ya CCM bali kupinga kujiunga na uchaguzi kwa sababu mfumo mzima wa uchaguzi nchini hautoa nafasi sawa kwa vyama na kikubwa zaidi TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), sii chombo huru.
Nashindwa kuelewa hivi hawa viongozi wa vyama vya Upinzani kweli wanafikiria wataweza kushinda chaguzi na kuchukua dola kwa kutumia mfumo uliopo ama wanafuata utaratibu uliopo kwa sababu ya kujipatia ruzuku na kuachiwa baadhi ya majimbo ili kuonyesha demokrasia ili hali CCM wakijua hawaezi kukubali kushindwa kwa kupitia sanduku la Kura.
Jambo moja muhimu sana ambalo wengi tumeshindwa kulielewa ni kwamba mshindi huchukua zote (winner takes all) ni mfumo ambao unaweza kabisa kuuthibiti kwa uchakachuaji kuhakikisha rais anashinda kwa popular vote na wabunge wanaohitajika ili kuunda serikali. Rais ndiye mwajiri wa viongozi wote wa NEC, TAKUKURU na Taasisi nyinginezo simamizi ya maadili ya kitaifa tunategemea vipi hawa watu watakuwa royal na wazalendo kwa Taifa hali ni waajiriwa na rais ambaye ni mgombea ktk uchaguzi. Na kikubwa zaidi rais ndiye mwajiri wa wabunge watakaokuwa mawaziri hivyo watajipanga kwa kumtumikia bwana.
Hivi kweli kuna watu walifikiria kwamba Chadema watapewa ushindi Igunga, walifikiria kwamba CCM baada ya kupoteza imani ya wananchi wataendelea kuonyesha wanavyoporomoka baada ya kuondoka kwa Rostam, na kuwapa ushindi Upinzani wakati chama kama chama kilitaka kuonyesha wananchi kwamba kuondoka kwa Rostam sii pigo la chama na chama kitaendelea kuwatumikia wananchi na sii Magamba. Katika hali hiyo tete, hata kama ningekuwa mimi ndiye rais, nisingekubali matokeo yoyote ya kushindwa Igunga.
Sawa wapo watu wanasema vyama vya upinzani kaa Chadema wajikite vijijini ili kuwaelimisha wananchi. Wananchi wameisha elimika vya kutosha kinachotakiwa ni kufungua matawi ya vyama na kuwashirikisha wananchi wazawa na wakazi wa majimbo hayo kuwakilisha chama. hapakuwa na sababu kabisa ya Chadema, CUF vya vyama vingine 6 kupeleka nguvu kubwa Igunga wakati vyama hivi vilikuwa havina ofisi za wawakilishi ktk kata zote ambao kwa muda wote wanakuwa pamoja na wanavijiji. Zaidi ya yote CCM had to win by all means! aliyeshindwa kuliona hili basi yeye ndiye mwenye matatizo.
CCM kwa muda wote wamekuwa wakitumia vyombo vya kitaifa ambavyo wamerithi kutoka CCM ya chama kimoja toka iwajumbe wa nyumba kumi, wamekuwa wakitumia wajumbe wa Halmashauri za miji, walimu na wakuu wa wilaya na kadhalika ili kuonyesha nguvu ya chama hiki kiutawala jambo ambalo vyama vya Upinzani hawana. Kwa kila hali, utaweza vipi kushindana na chama kilichoshika mpini?.
Leo tunakubali matokeo ya Igunga kama tulivyokubali matokeo ya kitaifa na sintashangaa kama nitasoma lawama kubwa ziliel;ekezwa makao makuu ya vyama hivi kwa matumizi mabaya ama kutowekeza ktk vitu kadhaa lakini bado ukweli utasimama ya kwamba pale CCM inataka kushinda itashinda kwa hali yoyote ile. Bila mabadiliko ya Kikatiba, bila mabadiliko ya kimfumo vyama vya Upinzania vitaendelea kuambulia baadhi ya majimbo kwa manufaa ya chama tawala ili wapate kuonyesha mataifa demokrasia inafanya kazi.
Mwisho, inashangaza sana kuona kwamba bunge limekwisha na maombi ya Katiba mpya yaliwekwa kando, miaka inakwenda siku zinayoyoma na uchaguzii wa mwaka 2015 unakaribia hali hakuna mabadiliko yoyote dhidi ya kanuni mbaya zilizotumika toka mwaka 1995. Tumeshuhudia Takrima zikitolewa Igunga, tumeshuhudia vijana wakipewa ajira za muda ktk uchaguzi na sii uzalendo wa kujitolea isipokuwa njia ya kutumikia matumbo yao.
Kila naposoma mada nyingi humu JF hujiuliza hivi kweli wananchi wamejifunza lolote kutokana na uchaguzi hizi, kweli wanaweza matumaini ya kuiondoa CCM madarakani kwa kupitia sanduku la KULA...sanduku ambalo maskini wote ndipo hupatia riziki zao! Kwa mtaji huu nawahakikishieni CCM itashinda mwaka 2015 na mtarudi hapa kuzungumza kwa jazba na matusi lakini sii makosa yenu bali CCM imejiwekea mazingira ya Ushindi toka mwaka 1995 na vyama vya Upinzani vimeridhia wote wakiona usongo kushika nafasi ya pili.
Nashindwa kuelewa hivi hawa viongozi wa vyama vya Upinzani kweli wanafikiria wataweza kushinda chaguzi na kuchukua dola kwa kutumia mfumo uliopo ama wanafuata utaratibu uliopo kwa sababu ya kujipatia ruzuku na kuachiwa baadhi ya majimbo ili kuonyesha demokrasia ili hali CCM wakijua hawaezi kukubali kushindwa kwa kupitia sanduku la Kura.
Jambo moja muhimu sana ambalo wengi tumeshindwa kulielewa ni kwamba mshindi huchukua zote (winner takes all) ni mfumo ambao unaweza kabisa kuuthibiti kwa uchakachuaji kuhakikisha rais anashinda kwa popular vote na wabunge wanaohitajika ili kuunda serikali. Rais ndiye mwajiri wa viongozi wote wa NEC, TAKUKURU na Taasisi nyinginezo simamizi ya maadili ya kitaifa tunategemea vipi hawa watu watakuwa royal na wazalendo kwa Taifa hali ni waajiriwa na rais ambaye ni mgombea ktk uchaguzi. Na kikubwa zaidi rais ndiye mwajiri wa wabunge watakaokuwa mawaziri hivyo watajipanga kwa kumtumikia bwana.
Hivi kweli kuna watu walifikiria kwamba Chadema watapewa ushindi Igunga, walifikiria kwamba CCM baada ya kupoteza imani ya wananchi wataendelea kuonyesha wanavyoporomoka baada ya kuondoka kwa Rostam, na kuwapa ushindi Upinzani wakati chama kama chama kilitaka kuonyesha wananchi kwamba kuondoka kwa Rostam sii pigo la chama na chama kitaendelea kuwatumikia wananchi na sii Magamba. Katika hali hiyo tete, hata kama ningekuwa mimi ndiye rais, nisingekubali matokeo yoyote ya kushindwa Igunga.
Sawa wapo watu wanasema vyama vya upinzani kaa Chadema wajikite vijijini ili kuwaelimisha wananchi. Wananchi wameisha elimika vya kutosha kinachotakiwa ni kufungua matawi ya vyama na kuwashirikisha wananchi wazawa na wakazi wa majimbo hayo kuwakilisha chama. hapakuwa na sababu kabisa ya Chadema, CUF vya vyama vingine 6 kupeleka nguvu kubwa Igunga wakati vyama hivi vilikuwa havina ofisi za wawakilishi ktk kata zote ambao kwa muda wote wanakuwa pamoja na wanavijiji. Zaidi ya yote CCM had to win by all means! aliyeshindwa kuliona hili basi yeye ndiye mwenye matatizo.
CCM kwa muda wote wamekuwa wakitumia vyombo vya kitaifa ambavyo wamerithi kutoka CCM ya chama kimoja toka iwajumbe wa nyumba kumi, wamekuwa wakitumia wajumbe wa Halmashauri za miji, walimu na wakuu wa wilaya na kadhalika ili kuonyesha nguvu ya chama hiki kiutawala jambo ambalo vyama vya Upinzani hawana. Kwa kila hali, utaweza vipi kushindana na chama kilichoshika mpini?.
Leo tunakubali matokeo ya Igunga kama tulivyokubali matokeo ya kitaifa na sintashangaa kama nitasoma lawama kubwa ziliel;ekezwa makao makuu ya vyama hivi kwa matumizi mabaya ama kutowekeza ktk vitu kadhaa lakini bado ukweli utasimama ya kwamba pale CCM inataka kushinda itashinda kwa hali yoyote ile. Bila mabadiliko ya Kikatiba, bila mabadiliko ya kimfumo vyama vya Upinzania vitaendelea kuambulia baadhi ya majimbo kwa manufaa ya chama tawala ili wapate kuonyesha mataifa demokrasia inafanya kazi.
Mwisho, inashangaza sana kuona kwamba bunge limekwisha na maombi ya Katiba mpya yaliwekwa kando, miaka inakwenda siku zinayoyoma na uchaguzii wa mwaka 2015 unakaribia hali hakuna mabadiliko yoyote dhidi ya kanuni mbaya zilizotumika toka mwaka 1995. Tumeshuhudia Takrima zikitolewa Igunga, tumeshuhudia vijana wakipewa ajira za muda ktk uchaguzi na sii uzalendo wa kujitolea isipokuwa njia ya kutumikia matumbo yao.
Kila naposoma mada nyingi humu JF hujiuliza hivi kweli wananchi wamejifunza lolote kutokana na uchaguzi hizi, kweli wanaweza matumaini ya kuiondoa CCM madarakani kwa kupitia sanduku la KULA...sanduku ambalo maskini wote ndipo hupatia riziki zao! Kwa mtaji huu nawahakikishieni CCM itashinda mwaka 2015 na mtarudi hapa kuzungumza kwa jazba na matusi lakini sii makosa yenu bali CCM imejiwekea mazingira ya Ushindi toka mwaka 1995 na vyama vya Upinzani vimeridhia wote wakiona usongo kushika nafasi ya pili.