Uchaguzi Busanda: Majigambo, Uteuzi na Kampeni kuelekea uchaguzi

Hii sheria ndio inaliza watu wengi. Labda kwenye thread hii badala ya kuhangaika na RA tungetumia muda huu kuwaelemisha Watanzania wengine kwa faida yao ya baadaye. Nina uhakika RA ni safi kwenye hili maana watu wangeshamvaa zamani.

this is flawed reasoning.. kwa vile hawajamvaa ina maana ni safi?

Kama mtu alizaliwa na mzazi mmoja ambaye hakuwa mtanzania wakati anazaliwa na kule kwao wanatambua mtoto kama huyo kuwa raia basi wewe una uraia wa nchi mbili na unaruhusiwa mpaka miaka 18. Baada ya hapo lazima uukane uraia wa hiyo nchi nyingine. Kwa mfano baba mwingereza na mama Mtanzania, kwa miaka mpaka 18 unakuwa na uraia wa nchi mbili, baada ya hapo kwasababu Tanzania haitambui uraia wa nchi mbili, inabidi uukane uraia wa UK ili ubaki kuwa Mtanzania.

Kundi lingine la kuangalia ni lile la Watanzania wanaoishi nje ya nchi kihalali ambako mtoto akizaliwa anakuwa raia pia. Hata kama hamjaomba huo uraia, kwasababu huyo mtoto anakuwa atomatically ni raia basi baada ya miaka 18 lazima aukane uraia wa nchi nyingine, vinginevyo siku anaingia siasa, wajanja watakuwa wanamsubiri.

Hiyo sheria wala hata sio lazima uchukue gamba, inatosha tu kwamba kwa sheria za nchi husika mtu kama huyo anakuwa raia.

Huko mbele tusipobadilisha sheria kuna Watanzania wengi waliozaliwa na wazazi wote Watanzania watakumbwa na sheria hii na kuleta matatizo hasa pale watakapojihusisha na siasa.

Wanasheria tuelemisheni ili watu wajifunze na wasifanye makosa hayo hayo hata siku za mbele.

Kuna watanzania wengi sio wafuatiliaji wa sheria na wanajikuta hata hawajui nini kinaendelea. Kwa mfano kuna Watanzania wengi ambao walikuwa wanasoma UK na kupata watoto kabla ya mwaka 1983, baada ya muda kurudi nyumbani. watoto wao wamehangaika kutafuta visa za kuja Ulaya bila kujua wao automatically ni raia wa UK hata kama wazazi wao wahakuwa raia. Baadhi yao mpaka wanashutuliwa na ubalozi ndio wanajua kumbe ni raia. Kwa wale ambao wamepoteza hata vyeti ndio imetoka tena.

naomba wengine mnaojua ongezeeni.

sidhani kama hapa kuna gumu.. sheria yetu ya awali ya uraia ilikuwa inasemaje? Na mabadiliko ya sheria hiyo baadaye yaliondoa tatizo gani? Tukielewa hiyo sheria tutaona kuwa hakuna ugumu mno kwani ni sheria hiyo hiyo ilitumika kumvua Jenerali uraia wake na wenzake wengine...

Na bado inaweza kutumika kuwavua wengine pia uraia huo kama ikiamuliwa kufuatwa (kama hii kesi inavyoeleza na kama ina ukweli).

Tatizo ni serikali ya CCM inaitumia sheria hii selectively..
 
sheria inambana huyo bwana, kama mama na baba ni watu wa kutoka nchi tofauti basi ukufika 18 lazima uchague uraia wa baba, mama au wa kuzaliwa, hapa namaanisha kama baba na mama wanatoka nchi tofauti na ulizaliwa kwenye nchi ambayo sio ya baba wala mama yako
Sheria hiyo inambana tuu kama amezaliwa on a third country ambayo siyo ya baba wala mama.
kama amezaliwa nchi yoyote ambayo mmoja wa wazaziwake ni raia wa alipozaliwa. anakuwa na birthright ya uraia wa alipozaliwa na akifikisha umri wa miaka 18, anauhuru ama wa kuendelea na uraia wake wa mahali alipozaliwa bila kuomba upya uraia, ama kuukana uraia wake wa birthright, na kuomba uraia wa mzazi wake.
kama jamaa alizaliwa TZ na mama MTZ, hana haja ya kuomba uraia at 18, ni MTZ straight forward.
 
Pasco,

Hapo juu ni kama hauko sahihi, refer case ya Premji kule Kigoma.
Bahati mbaya sijaifuatilia kesi ya premji, tatizo linawezekana japo anahaki zote za Utanzania, hawa wenzetu wamekuwa na passport mbilimbli.
narudi tena kwa Mtikila na uraia wa RA, jamaa kasema anapasport mbili. ya tanzania huitumia mpaka Nairobi tuu, baada ya hapo, ni passport ya Persia. RA hakumshitaki wala ina maana kuna ka uwezekano wa kwa ukweli, unless RA aliamua kumpuuza Mtikila na sensitive issue ya urais lakini ametoa statement alipoitwa 'fisadi papa' labda kwa vile yule ni Mtikila na huyu ni Mengi.
 
Simba wa nyika amekwisha kufika huko mtasikia habari zake lazima waTanganyika watajua kama embe ntunda. :D
 
Bahati mbaya sijaifuatilia kesi ya premji, tatizo linawezekana japo anahaki zote za Utanzania, hawa wenzetu wamekuwa na passport mbilimbli.
narudi tena kwa Mtikila na uraia wa RA, jamaa kasema anapasport mbili. ya tanzania huitumia mpaka Nairobi tuu, baada ya hapo, ni passport ya Persia. RA hakumshitaki wala ina maana kuna ka uwezekano wa kwa ukweli, unless RA aliamua kumpuuza Mtikila na sensitive issue ya urais lakini ametoa statement alipoitwa 'fisadi papa' labda kwa vile yule ni Mtikila na huyu ni Mengi.
Pasco,

Wewe ni RA, una mabilioni bank uliyopata kwasababu ya Utanzania, unapata visa kirahisi kokote unakotaka kwenda, ni mbunge, kweli uta risk kuwa na passport mbili?

Arguments zingine ni vichekesho, passport mbili zinatufaa sisi walalahoi ambao ukiomba visa ya kwenda nchi nyingine ni matatizo tupu.

Kuna reseach ilifanywa hapa UK, katika wale ambao wana haki ya kupata passport na hawajaitumia kwa asilimia 100 walikuwa ni middle class. Wale wabeba box kama mimi, wanaisubiri tarehe utafikiri ni tarehe ya ndoa, ikifika wanaamkia home office.
 
Pasco,

Wewe ni RA, una mabilioni bank uliyopata kwasababu ya Utanzania, unapata visa kirahisi kokote unakotaka kwenda, ni mbunge, kweli uta risk kuwa na passport mbili?

Arguments zingine ni vichekesho, passport mbili zinatufaa sisi walalahoi ambao ukiomba visa ya kwenda nchi nyingine ni matatizo tupu.
huyo ni Mtikila, anaonekanaga kichekesho,punguani, kichaa, hamzazo bud sometimes there is some truths in between the lines. kwanini RA hakukanusha sensetive issue kama hii, leo katoa statement kukanusha 'fisadi papa'.
kwake passport 2 sio risk, its a deal.
 
this is flawed reasoning.. kwa vile hawajamvaa ina maana ni safi?
Kama ni flawed reasoning ina maana kuna strong reasoning, unaonaje mwenzetu ungetuambia hiyo ni ipi?

Kama kuna mtu ambaye uraia wake una utata angekuwa wa kwanza kufikishwa mahakamani ni RA. Ila mwenzetu kwasabau unaangalia in terms of black and white, hiyo reasoning utaitoa wapi?

Wewe mwenzetu kila kitu ni kuimba tu RA, si mpeleke mahakamani basi kama una matatizo naye kiasi hicho?

Umefungua threads 20 za RA unaona hazitoshi mpaka hata zingine zote uzibadili ziende kwa RA? Pathetic!
 
Mtanzania,
Hii ya RA kuwa na passport mbili usibishe. Inawezekana kabisa. Najua kuna waziri katika serikali ya sasa ya JK ambaye ana pasipoti mbili. Usiniulize ni nani.
 
Bahati mbaya sijaifuatilia kesi ya premji, tatizo linawezekana japo anahaki zote za Utanzania, hawa wenzetu wamekuwa na passport mbilimbli.
narudi tena kwa Mtikila na uraia wa RA, jamaa kasema anapasport mbili. ya tanzania huitumia mpaka Nairobi tuu, baada ya hapo, ni passport ya Persia. RA hakumshitaki wala ina maana kuna ka uwezekano wa kwa ukweli, unless RA aliamua kumpuuza Mtikila na sensitive issue ya urais lakini ametoa statement alipoitwa 'fisadi papa' labda kwa vile yule ni Mtikila na huyu ni Mengi.

Premji ilikuwa hivyo hivyo, alikuwa raia wa Tanzania na India kupitia wazazi wake na ilipofika miaka 18 ilitakiwa aukane uraia wa India.

Hata kama hakuwahi kuchukua passport ya India, mahakama iliona ulikuwa wajibu wake kuukana uraia mmoja. Kutokujua kwamba una uraia huo sio sababu kwenye sheria.
 
Mtanzania,
Hii ya RA kuwa na passport mbili usibishe. Inawezekana kabisa. Najua kuna waziri katika serikali ya sasa ya JK ambaye ana pasipoti mbili. Usiniulize ni nani.
Jasusi,

Kama unajua sasa unaogopa nini kumtaja na kutoa ushahidi ili tumchukulie hatua? Kuwa na passport mbili kwenye siasa ndio case rahisi kweli kushinda kuliko hata za ufisadi.

Tatizo la watanzania tunaweza kusikia ya vijiweni na kuamini ni kweli kumbe huyo mtu alishaweka mambo yake sawa siku nyingi.

Ukiweza kuonyesha mtu ana passport mbili kwa TZ atapoteza ubunge na uwaziri hapo hapo. Kama tunapigana na ufisadi kwanini tunashindwa mambo hata rahisi kama haya kama tuna ushahidi?
 
Mtanzania,
Hii ya RA kuwa na passport mbili usibishe. Inawezekana kabisa. Najua kuna waziri katika serikali ya sasa ya JK ambaye ana pasipoti mbili. Usiniulize ni nani.

Mzee Jasusi, si useme tu mwenye pasi mbili ni waziri kijana!
 
Mzee Jasusi, si useme tu mwenye pasi mbili ni waziri kijana!
Mkuu Kipunguni,

Unafikiri Masha ni mjinga kiasi hicho? Atakuwa alishaitupa hiyo passport siku nyingi?

Kuwafunga kamba watu kama hawa lazima Watanzania tuanze kufikiri mbali zaidi ya maneno ya kijuweni ambayo hayawapi shida hawa mafisadi.

Unajua ukimwambia mtu ana hili wakati hana unakuwa umemwondolea matatizo kibao.
 
Mtoto anapatika kwa mbegu (shahawa) za mwanamke na mwanaume. Ndio maana imewekwa sheria kwamba iwapo mbegu hizo zina uraia tofauti, mtoto (tunda la mbegu hizo) anatakiwa atangaze rasmi kuchagua kwa dominated na mbegu za mama au baba hasa pale kishafikisha umri wa akili timamu wa miaka 18.

Hivyo haijalishi kama umeishi nchini miaka 30 au mingapi..as long as uchakana mbegu za mazazi mmojawapo wewe utakuwa upoupo tu.....
 
Ujinga mtupu...
Kama mtoto amezaliwa Tanzania huwa moja kwa moja ni raia wa Tanzania kwa uzawa unless wazazi wake wachague kitu tofauti.. na kama kachukua passport ya Tanzania akiwa chini ya umri wa miaka 18 hana haja wala sababu ya kula kiapo akisha fikisha umri wa miaka 18 - Ni Mtanzania kwa uzawa...
 
Mkuu Kipunguni,

Unafikiri Masha ni mjinga kiasi hicho? Atakuwa alishaitupa hiyo passport siku nyingi?

Kuwafunga kamba watu kama hawa lazima Watanzania tuanze kufikiri mbali zaidi ya maneno ya kijuweni ambayo hayawapi shida hawa mafisadi.

Unajua ukimwambia mtu ana hili wakati hana unakuwa umemwondolea matatizo kibao.


Mkuu punguza jazba kidogo, kisha angalia historia ya hawa mafisadi na namna wanavyofanya ufisadi wao...kisha njoo hapa utuambie kama sio wajinga wa kupindukia.

Nakubaliana na wewe kuwa kuthibitisha kuwa fisadi ana pasipoti ya nchi nyingine ni kesi nyepesi na tena ya moja kwa moja...ila unasahau kuwa kwa sababu ni issue nyepesi kuthibitisha na kumtoa mtu madarakani basi haiondoi uwezekano wa kuwa kweli. Wewe umekaa chini ukafikiria hilo la uraia wenzio hawa mafisadi usiku na mchana wanafikiria namna ya kupeleka fedha zetu ulaya na america hawana muda wa kufikiria suala kama la pasipoti na uraia.

Angalia jinsi ufisadi wote unaojulikana jinsi ulivyokuwa rahisi kugundua kuwa hawa jamaa ni wezi, kuanzia Richmond, Kagoda, NSSF, EPA n.k ufisadi wote hakuna hata mmoja ambao umeenda shule...kote wameacha paper trail, namba za simu, address zinazofanana, majina yale yale, matumizi yale yale ya pesa...mpaka wengine wakafungua kampuni wakiwa ikulu na kuweka mke na watoto kama share holders...bado unaona hawa watu ma-genious mkuu...it's just a matter of time.
 
Ukiweza kuonyesha mtu ana passport mbili kwa TZ atapoteza ubunge na uwaziri hapo hapo. Kama tunapigana na ufisadi kwanini tunashindwa mambo hata rahisi kama haya kama tuna ushahidi?

Kweli yanaweza kuwa rahisi na mtu ukiangalia kwa juu juu unaweza kuona ni kitu cha kuchukuliwa hatua mara moja.

Nikukumbushe kesi ya Mh. Chitalilo. Watu walilalamika kwamba amegushi elimu yake ya sekondari. Swala likaenda Polisi, Polisi wakafanya kazi na wakathibitisha kwamba tuhuma ni za kweli, na report ikaenda kwa DPP. DPP akasema Chitalilo hana kesi ya kujibu.

Kabla ya hapo JK alishaenda jimboni kwa Chitalilo akasema kelele za mlango hazimnyimi usingizi mwenye nyumba. Na Chitalilo mwenyewe alisema hata watu wapige kelele kiasi gani, hakuna chochote atakachofanywa.

Sasa jiulize DPP alitumia vigezo gani kusema kwamba Chitalilo hana kesi? DPP alisema kwamba kuwadanganya wananchi siyo kosa kwa kuwa kuna wagombea wengi huwa wanatoa ahadi hewa. Hivi kweli unaweza kulinganisha ahadi hewa na udanganyifu uliofanywa kwenye fomu iliyosainiwa mbele ya Hakimu kwa kiapo? Je, mtu akila kiapo cha uongo hana kesi ya kujibu? Nilitarajia kwamba condition ya kusaini fomu mbele ya Hakimu ni kuongeza uzito kwamba ameidanganya mahakama na hivyo anakuwa na kesi ya kujibu. (Mimi siyo mwana sheria, japo hayo ni mawazo yangu)

Tatizo ni kwamba sheria za Tanzania zinaangalia sura za watu. Kama huyo mtu hatakiwi na system (serikali na CCM) basi ni kesi rahisi sana. Lakini kama system inamhitaji, siyo kitu rahisi. Maana hao unaowapelekea ushahidi ndiyo watakuwa wa kwanza kwenda kuharibu ushahidi kwenye source. Angalia kwenye hii link uone vichekesho Parliament of Tanzania

Kama mtu hakumaliza sekondari kwanini hiyo taarifa iwekwe huko? Ina maana mtu aki-disco pale UD atasema nilisoma mpaka Mlimani na sikumaliza? Something is wrong somewhere na nina uhakika maelezo yanayosema NOT COMPLETED yaliwekwa baada ya kuona Polisi wametoa report ambayo ilikuwa inaonyesha wazi kijana aligushi elimu. Jamaa mpaka leo bado anadunda na yuko mstari wa mbele kutetea mafisadi.
 
Mkuu punguza jazba kidogo, kisha angalia historia ya hawa mafisadi na namna wanavyofanya ufisadi wao...kisha njoo hapa utuambie kama sio wajinga wa kupindukia.

Nakubaliana na wewe kuwa kuthibitisha kuwa fisadi ana pasipoti ya nchi nyingine ni kesi nyepesi na tena ya moja kwa moja...ila unasahau kuwa kwa sababu ni issue nyepesi kuthibitisha na kumtoa mtu madarakani basi haiondoi uwezekano wa kuwa kweli. Wewe umekaa chini ukafikiria hilo la uraia wenzio hawa mafisadi usiku na mchana wanafikiria namna ya kupeleka fedha zetu ulaya na america hawana muda wa kufikiria suala kama la pasipoti na uraia.

Angalia jinsi ufisadi wote unaojulikana jinsi ulivyokuwa rahisi kugundua kuwa hawa jamaa ni wezi, kuanzia Richmond, Kagoda, NSSF, EPA n.k ufisadi wote hakuna hata mmoja ambao umeenda shule...kote wameacha paper trail, namba za simu, address zinazofanana, majina yale yale, matumizi yale yale ya pesa...mpaka wengine wakafungua kampuni wakiwa ikulu na kuweka mke na watoto kama share holders...bado unaona hawa watu ma-genious mkuu...it's just a matter of time.

Mkuu yebo yebo,

Unajua kabla ya kumwambia mtu ana passport mbili, angalia kwanza kwanini watu wanalazimika kuwa na passport mbili hata pale wanaona ni makosa?

Tatizo ni kurahisisha ugumu wa maisha. Mtu mwenye mabilioni yake unafikiri hata kuna haja ya kuvunja sheria na kuchukua risks zote kwa ajili ya passports mbili wakati akitaka hiyo visa anapata kirahisi tu?

Ukiwajua hawa mabepari, ukiwa na mapesa yako wanakuachia tu ili uje usaidie credit crunch huku kwao.

Tuwabane hawa jamaa pale ambapo kweli tuna sababu za kutosha vinginevyo ndio maana wengi wanadharau na kuona JF ni kijiwe cha majungu tu.
 
Kweli yanaweza kuwa rahisi na mtu ukiangalia kwa juu juu unaweza kuona ni kitu cha kuchukuliwa hatua mara moja.

Nikukumbushe kesi ya Mh. Chitalilo. Watu walilalamika kwamba amegushi elimu yake ya sekondari. Swala likaenda Polisi, Polisi wakafanya kazi na wakathibitisha kwamba tuhuma ni za kweli, na report ikaenda kwa DPP. DPP akasema Chitalilo hana kesi ya kujibu.

Kabla ya hapo JK alishaenda jimboni kwa Chitalilo akasema kelele za mlango hazimnyimi usingizi mwenye nyumba. Na Chitalilo mwenyewe alisema hata watu wapige kelele kiasi gani, hakuna chochote atakachofanywa.

Sasa jiulize DPP alitumia vigezo gani kusema kwamba Chitalilo hana kesi? DPP alisema kwamba kuwadanganya wananchi siyo kosa kwa kuwa kuna wagombea wengi huwa wanatoa ahadi hewa. Hivi kweli unaweza kulinganisha ahadi hewa na udanganyifu uliofanywa kwenye fomu iliyosainiwa mbele ya Hakimu kwa kiapo? Je, mtu akila kiapo cha uongo hana kesi ya kujibu? Nilitarajia kwamba condition ya kusaini fomu mbele ya Hakimu ni kuongeza uzito kwamba ameidanganya mahakama na hivyo anakuwa na kesi ya kujibu. (Mimi siyo mwana sheria, japo hayo ni mawazo yangu)

Tatizo ni kwamba sheria za Tanzania zinaangalia sura za watu. Kama huyo mtu hatakiwi na system (serikali na CCM) basi ni kesi rahisi sana. Lakini kama system inamhitaji, siyo kitu rahisi. Maana hao unaowapelekea ushahidi ndiyo watakuwa wa kwanza kwenda kuharibu ushahidi kwenye source. Angalia kwenye hii link uone vichekesho Parliament of Tanzania

Kama mtu hakumaliza sekondari kwanini hiyo taarifa iwekwe huko? Ina maana mtu aki-disco pale UD atasema nilisoma mpaka Mlimani na sikumaliza? Something is wrong somewhere na nina uhakika maelezo yanayosema NOT COMPLETED yaliwekwa baada ya kuona Polisi wametoa report ambayo ilikuwa inaonyesha wazi kijana aligushi elimu. Jamaa mpaka leo bado anadunda na yuko mstari wa mbele kutetea mafisadi.

Keil,

Katika vyombo ninavyoviamini Tanzania ni pamoja na mahakama kuu. Sasa kama mtu ana passport mbili kwanini tushindwe kumfungulia mashitaka?

Ku forge vyeti na kuwa na passport mbili ni makosa mawili tofauti. Hata kama yote ni makosa makubwa lakini urahisi wa hizi case una tofauti kubwa.

Naelewa CCM iko selective kwenye kuamua nani achukuliwe hatua na hilo ndilo mwanzo wa matatizo mengi ya TZ. Lakini je na sisi Watanzania wengine mbona tunakaa kimya hata pale penye makosa ya wazi kama passports mbili?

Sheria nzima ya uraia ni ujinga mtupu kama livyosema Mkandara. Mtu aliyezaliwa Tanzania na kuishi miaka yote hiyo utasemaje sio Mtanzania? mambo mengine ni kufanya formalities, waliyomfanyia Ulimwengu na wenzake ni uharamia na inatakiwa Mkapa na genge lake wawajibike kwa hilo.
 
Back
Top Bottom