Mkuu wangu,
Naona unafanya siasa za kishikaji hapa. Mimi nadhani somo kubwa hapa lingekuwa kwamba JK anatakiwa kufahamu kwamba sera zake hazikuuzika na kuwa amepoteza wabunge wake (incumbents) kwa sababu wananchi hawakubaliani naye. Na hakika kura nyingi za JK zimetokana na wanachama wa CCM chenyewe ambao walikataa katakata kukiangusha chama kutokana na makosa yaliyokwisha tokea. CCM ni wale waitwao die hard wanakufa na tai shingoni hivyo JK ashukuru sana wanachama wake na hasa wanawake ambao ndio wamempa ushindi mkubwa zaidi. Siku zote wanawake ni sehemu kubwa ya wapiga kura na JK hakulala toka upande huo...
Labda nikukumbushe tu kwamba nilisema toka mwanzo kwamba uwezekano wa kumshinda JK upo na hasa kama atasimama Dr.Slaa, nadhani uchaguzi huu sote hapa tunaamini kabisa kwamba Chadema wameweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na dr. hili pia halina ubishi na kama nilivyosema toka awali CCM wanaweza kabisa kushindwa ikiwa Upinzani wangefuata na kutimiza baadhi ya maswala muhimu sana ktk uchaguzi huu.
Kwanza kabisa ikiwa ni kukosa UMOJA baina ya vyama vya Upinzani jambo ambalo tumelizungumzia sana hapa JF toka uchaguzi wa mwaka 2000 na 2005 - Haikufanyika hivyo, lakini bado hatukukata tamaa na kuendelea kuwashauri Chadema kwa mengi ya msingi. Hivyo Chadema waliingia uchaguzi huu solo na kama chama mbadala ingawa walikuwa na mapungufu mengi na yaliyokuwa wazi.
Pili, Uongozi wa Chadema wamefanya baadhi ya makosa ya wazi kabisa ambayo pia tuliyazungumzia hapa kijiweni, mojawapo nilionya toka mwanzo ni kutojiandaa kusimamisha Wagombea Udiwani na Ubunge nchi nzima. Tatizo hili linaweza kutokana na uwezo wao mdogo kuiwezesha agenda hii kwani ruzuku wanayoipata sidhani kama ingeweza kuwahudumia wagombea wote, hivyo pengine Chadema bado ni chama kichanga ambacho kinahitaji kukua zaidi, lakini nakufahamisha tu kwamba nilipoona hivyo nilijua fika Chadema hawawezi kushinda uchaguzi huu kwa kupata wabunge 100 kama walivyotarajia kwani CCM isingeweza kutoa nafasi hizo kirahisi isipokuwa pale watakapoweza kubanwa sehemu zote. Na kibaya zaidi, Chadema ilipoteza baadhi ya Wabunge ktk maeneo muhimu ambayo wagombea wake walikuwa ni mapandikizi ya CCM.
Tatu, Uongozi wa Chadema walifanya kosa jingine kubwa sana kutoingia ktk uchaguzi wa Halamashauri ambao tumeona viongozi wa CCM wakizoa majimbo mengi na ndio waliofanya ama niseme kuiwezesha CCM kushinda mwaka huu, iwe kwa uchachuaji ama lolote lile maadam kuna zaidi ya vituo 7,000 vya kupigia kura sii rahisi kabisa kwa Chadema kuweza kuweka wawakilishi wenye uchungu ktk maeneo yote.. Hivyo Chadema kutojikita ngazi za chini ambazo ni muhimu sana imekuwa pigo kubwa kwa chama na dalili zake zilijitokeza mapema wakati wa kampeni za viongozi wake..
Nne, mchezo mchafu wa CCM kuhusisha dini katika uchaguzi huu pia umechangia kwa kiasi kikubwa sana kwa Chadema kushindwa ktk baadhi ya maeleno kwani sii kila Muislaam au Mkristu anapenda chama kinachotawaliwa na Udini. Mara nyingi uongo ukizungumzwa sana hufikia watu wakaamini na haya tumeyaona hata hapa kijiweni kwani wapo watu walivutwa na udini kiasi kwamba hata mimi nilianza kujiuliza position yangu ktk siasa ikiwa swala la udini litachukua nafasi..Udini ni kuchezea akili za watu kufikia maamuzi ambayo huondoa kabisa utu na uzalendo wao, CCM walifanikiwa ktk hili.
CCM walitulisha chambo na WanaChadema kama samaki wengi wao walikula na kuuweka uchaguzi huu kama ni nguvu ya kuondoa Uislaam ktk ngazi ya Urais, haya yalikuwa makosa makubwa sana ya baadhi ya wanaChadema na hasa viongozi wa dini walipoingilia kati. Ifahamike tu kwamba CCM pamoja na kuwa wao ndio waanzilishi wa Udini walichotaka wao ni wananchi kukitazama chama Chadema kilivyoundwa kwa kufananisha na CCM.
Hivyo hata hao Masheikh walipokuwa wakimnadi JK haikuwa kosa tena pale Mapadre waliposimama nao kunadi Dr.Slaa. Na kibaya zaidi CCM waliweza kujitetea sana kwa kutokuwa na udini ndani ya chama wakieleza wazi jinsi muundo wa chama na hata nyadhifa za viongozi wake jambo ambalo sii zuri kiutawala lakini liliweza kuwapa nafasi zaidi ya Chadema. Najua fika wapo watu watapinga hili lakini ndivyo nilivyoliona mimi kuwa sababu mojawapo ya Chadema kutofanikiwa mwaka huu. Kwa hiyo ngoma ndio imekwisha tugange yajayo.
Mwisho mkuu wangu JK anatakiwa sasa kuongoza nchi kama rais, muda wa John Mtembezi umekwisha. Sasa ni juu yake yeye mwenyewe kuchagua..Kuendelea na siasa za Usanii huku akiendelea kukumbatia Ufisadi na kuwafanyia wale woote waliokuwa against yeye uchaguzi huu au kurudisha hadhi ya kiti cha IKULU na kuwawajibisha wote watakao fikwa na scandals zozote za kifisadi. Akubali mageuzi ktk sehemu nyeti ambazo ndizo zilikuwa nguzo ya Dr.Slaa hata kama zimetoka Chadema na kuacha kabisa zile hadithi za kuijenga Kigoma kama Dubai.
Ushindi wa JK ulikuwa LAZIMA, hapakuwepo na nguvu ya kutosha kumwangusha hivyo he is a survival na hasira zake tutaziona muda sii mfupi....By the way kusema kweli JK tunaweza sema ni rais mdhaifu kwa sababu nyingi sana ikiwa ni pamoja na kukumbatia Ufisadi na upande wapili wa shilingi kuwaachia Upinzani kumtia vidole vya macho in the name of Demokrasia!