Jatropha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2009
- 1,151
- 199
Katika kipindi cha Jahazi cha tar 31/8/2010 mtangazaji Kibonde amejifanya kuwa mtetezi wa JK na CCM kwa kuliponda pingamizi ya Dr Slaa na CHADEMA kuhusu JK kukiuka Sheria ya Gharama za Uchaguzi.
Kwa bahati mbaya sana katika kutekeleza jukumu hilo Kibonde alizidi kudhihirisha umbumbumbu wake hadharani pale alipodai kuwa "Rais anayo mamlaka ya kuagiza matumizi ya fedha za Serikali atakavyo"
Kwa maoni yangu Kibonde ana ufahamu mdogo sana wa kitu kinachoitwa Separation of Powers between the State (Serikali), Legislature (Bunge) and Judiciary (Mahakama). Hajo ya CHADEMA katika sakata hili ni mgombea wa CCM Jakaya Kikwete na Serikali yake ni kufanya matumizi ya fedha za umma kwa kukiuka Kanuni na Taratibu za Fedha za Serikali. Kwa mujibu wa Katiba Bunge ndio lenye jukumu la kuidhinisha makusanyo na matumizi ya fedha za Serikali.
Kutokea mawaka 2006 TUCTA iliwasilisha madai ya nyongeza za mishahara kwa watumishi wa Serikali kufikia kima cha chini cha Shs 315,000/=.
Kutokea mwaka 2006 JK na Serikali yake hawakuchukua hatua zozote kuongeza mishahara ya wafanyakazi kwa maana ya kupeleka ombi kwa bunge la kufanya matumizi ya ya ziada katika kulipa mishahara ya watumishi. Hivyo Bunge la 2006, 2007, 2008, 2009 na hata la 2010 Kikwete na Serikali yake walishindwa kuwasilisha ombi hilo.
Wakati Serikali ya JK ilishindwa kuwasilisha ombi la kuongeza mishahara ya watumishi wake wanyoinge. Inadaiwa katika kipindi hicho iliwaongezea mishahara na marupurupu za viongozi waandamizi wa Serikali wakiwemo Wabunge, Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi, Wakuu wa Vyombo vya Usalama, Majaji n.k na pia kulipa malimbikizo ya nyongeza hiyo. Kama tutakumbuka vizuri wabunge wenye jukumu la kupitisha matumizi ya Serikali walipoona vigogo wenzao Serikalini wamejiongezea mishahara na marupurupu; wabunge nao wakawasilisha mapendekezo ya kuongezewa mishahara na marpurupu na wakapata.
Ni kwanini CCM , Kikwete na Serikali yake waliamua kuwadharau wafanyakazi kwa miaka minnne kutoka mwaka 2006, na kuendelea kuwadharau hata pale walipotishia kugoma mwi 2010? Jibu walifanya hivyo kwa kuwa walijua TUCTA inaongea peke yake, haina asasi ingine ya kuisaidia hivyo Serikali itaweze kutumia vitisho kuzima jeuri ya TUCTA na Mgaya.
Kuteuliwa kwa Dr Slaa kuwa mgombea Urais wa CHADEMA kulikuja kama mshituko kwa CCM JK na watanzania walio wengi. Na hoja yake ya kwanza wakati anafanya mikutano ya kutafuta wadhamini katika mikoa mbali mbali ilikuwa kutamka wazi wazi kuwa anazihitaji kura za wafanyakazi zilizokataliwa na mgombea wa CCM Jakaya Kikwete katika mkutano wake na wazee wa Dar es Salam Mei 2010, na akachapisha fulana zenye ujumbe huo.
TUCTA ilipoona imepata msemaji wa kusaidiana naye katika kudai haki za wafanyakazi zilizokuwa zikipigwa danadana kutokea 2006, haikubweteka ikatoa tamko kwa wanachama wake kuwa wampatie kura mgombea anayeonyesha kuhitaji kura za wafanyakazi, kwa kuwa haiwezekani "ukampatia pilau mtu asiyeihitaji".
Ni kutokana na pressure hizi za kuanza kwa Kampeni za uchaguzi Mkuu wa 2010 CCM, Kikwete na Serikali yake wakasalimu amri na kutoa nyongeza ya mishahara kutoka Shs 135,000/= kufika Shs 235,000/= kimya kimya. TUCTA, CHADEMA na wadau wengine wakataka kufahamishwa ni nini kinaendelea ndipo Rais akajitokeza katika mikutano ya Kampeni za CCM mkoani Mwanza kudai kuwa Serikali yake inawajali sana wafanyakazi na tayari imewaongezea mishahara.
Sasa Kibonde atuambie katika mtirirko huu wa matukio, ni kweli CCM ya leo na JK wanawajali wafanyakazi? Walikuwa wapi kwa miaka minne kuwapatia wafanyakazi nyongeza hiyo?
Hoja kubwa ya Dr Slaa na CHADEMA sio wafanyakazi kuongezewa mishahara, bali wafanyakzi kutumika kama busati la kusafisha miguu na kukumbukwa baada ua upepo wa kisiasa kuwa mbaya kwa CCM na mgombea wake Jakaya Kikwete. Tujiulize kwa mtirirko uliotajwa hapo juu, iwapo vyama vya siasa vingesimamisha watu wasio makini kama Dr Slaa katika nafasi ya Urais, nyongeza ya mishahara iliyokuwa ikipigwa danadana kwa miaka minne kutoka 2006 na iliyotolewa wakati wa kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu ingepatikana?
Sambamba na hilo Dr Slaa na CHADEMA wanahaji kitendo cha Rais na Serikali yake kukikuka Kanuni na Taratibu za Fedha za Serikali. Ni ukiukwaji huu uliosababisha kuwepo kwa Kashafa ya EPA, Meremeta, Tangold, n.k.
Naomba wana JF wanaofahamu mipaka ya Rais kuagiza matumizi ya fedha za umma wakati usiokuwa wa dharura (emergency) bila ya kupata idhini ya bunge watusaidie kumhabarisha Kibonde kupitia hapa
Kwa bahati mbaya sana katika kutekeleza jukumu hilo Kibonde alizidi kudhihirisha umbumbumbu wake hadharani pale alipodai kuwa "Rais anayo mamlaka ya kuagiza matumizi ya fedha za Serikali atakavyo"
Kwa maoni yangu Kibonde ana ufahamu mdogo sana wa kitu kinachoitwa Separation of Powers between the State (Serikali), Legislature (Bunge) and Judiciary (Mahakama). Hajo ya CHADEMA katika sakata hili ni mgombea wa CCM Jakaya Kikwete na Serikali yake ni kufanya matumizi ya fedha za umma kwa kukiuka Kanuni na Taratibu za Fedha za Serikali. Kwa mujibu wa Katiba Bunge ndio lenye jukumu la kuidhinisha makusanyo na matumizi ya fedha za Serikali.
Kutokea mawaka 2006 TUCTA iliwasilisha madai ya nyongeza za mishahara kwa watumishi wa Serikali kufikia kima cha chini cha Shs 315,000/=.
Kutokea mwaka 2006 JK na Serikali yake hawakuchukua hatua zozote kuongeza mishahara ya wafanyakazi kwa maana ya kupeleka ombi kwa bunge la kufanya matumizi ya ya ziada katika kulipa mishahara ya watumishi. Hivyo Bunge la 2006, 2007, 2008, 2009 na hata la 2010 Kikwete na Serikali yake walishindwa kuwasilisha ombi hilo.
Wakati Serikali ya JK ilishindwa kuwasilisha ombi la kuongeza mishahara ya watumishi wake wanyoinge. Inadaiwa katika kipindi hicho iliwaongezea mishahara na marupurupu za viongozi waandamizi wa Serikali wakiwemo Wabunge, Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi, Wakuu wa Vyombo vya Usalama, Majaji n.k na pia kulipa malimbikizo ya nyongeza hiyo. Kama tutakumbuka vizuri wabunge wenye jukumu la kupitisha matumizi ya Serikali walipoona vigogo wenzao Serikalini wamejiongezea mishahara na marupurupu; wabunge nao wakawasilisha mapendekezo ya kuongezewa mishahara na marpurupu na wakapata.
Ni kwanini CCM , Kikwete na Serikali yake waliamua kuwadharau wafanyakazi kwa miaka minnne kutoka mwaka 2006, na kuendelea kuwadharau hata pale walipotishia kugoma mwi 2010? Jibu walifanya hivyo kwa kuwa walijua TUCTA inaongea peke yake, haina asasi ingine ya kuisaidia hivyo Serikali itaweze kutumia vitisho kuzima jeuri ya TUCTA na Mgaya.
Kuteuliwa kwa Dr Slaa kuwa mgombea Urais wa CHADEMA kulikuja kama mshituko kwa CCM JK na watanzania walio wengi. Na hoja yake ya kwanza wakati anafanya mikutano ya kutafuta wadhamini katika mikoa mbali mbali ilikuwa kutamka wazi wazi kuwa anazihitaji kura za wafanyakazi zilizokataliwa na mgombea wa CCM Jakaya Kikwete katika mkutano wake na wazee wa Dar es Salam Mei 2010, na akachapisha fulana zenye ujumbe huo.
TUCTA ilipoona imepata msemaji wa kusaidiana naye katika kudai haki za wafanyakazi zilizokuwa zikipigwa danadana kutokea 2006, haikubweteka ikatoa tamko kwa wanachama wake kuwa wampatie kura mgombea anayeonyesha kuhitaji kura za wafanyakazi, kwa kuwa haiwezekani "ukampatia pilau mtu asiyeihitaji".
Ni kutokana na pressure hizi za kuanza kwa Kampeni za uchaguzi Mkuu wa 2010 CCM, Kikwete na Serikali yake wakasalimu amri na kutoa nyongeza ya mishahara kutoka Shs 135,000/= kufika Shs 235,000/= kimya kimya. TUCTA, CHADEMA na wadau wengine wakataka kufahamishwa ni nini kinaendelea ndipo Rais akajitokeza katika mikutano ya Kampeni za CCM mkoani Mwanza kudai kuwa Serikali yake inawajali sana wafanyakazi na tayari imewaongezea mishahara.
Sasa Kibonde atuambie katika mtirirko huu wa matukio, ni kweli CCM ya leo na JK wanawajali wafanyakazi? Walikuwa wapi kwa miaka minne kuwapatia wafanyakazi nyongeza hiyo?
Hoja kubwa ya Dr Slaa na CHADEMA sio wafanyakazi kuongezewa mishahara, bali wafanyakzi kutumika kama busati la kusafisha miguu na kukumbukwa baada ua upepo wa kisiasa kuwa mbaya kwa CCM na mgombea wake Jakaya Kikwete. Tujiulize kwa mtirirko uliotajwa hapo juu, iwapo vyama vya siasa vingesimamisha watu wasio makini kama Dr Slaa katika nafasi ya Urais, nyongeza ya mishahara iliyokuwa ikipigwa danadana kwa miaka minne kutoka 2006 na iliyotolewa wakati wa kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu ingepatikana?
Sambamba na hilo Dr Slaa na CHADEMA wanahaji kitendo cha Rais na Serikali yake kukikuka Kanuni na Taratibu za Fedha za Serikali. Ni ukiukwaji huu uliosababisha kuwepo kwa Kashafa ya EPA, Meremeta, Tangold, n.k.
Naomba wana JF wanaofahamu mipaka ya Rais kuagiza matumizi ya fedha za umma wakati usiokuwa wa dharura (emergency) bila ya kupata idhini ya bunge watusaidie kumhabarisha Kibonde kupitia hapa