Mkuu hilo swali ni gumu sana. Kwa kifupi tu kuna mambo mengi ya kuangalia. Makubwa haswa ni kwamba wewe mnunua TV unahitaji nini kwenye TV yako,viewing angle,je kwa TV ndogo kama nchi 40 (Samahani kwa huku nilipo hizo ni ndogo) je kuna faida ya kununua 1080P ?Kama hakuna faida je nikinunua 720P nikaokoa hela kuna madhara yoyote ? Najua sasa hivi kuna 4K ambayo ni 2160P je ukinunua hiyo kuna content za kuangalia kwa hiyo resolution ? Fikiria tu ukiangalia TV kwa jumla sidhani kama kuna station inayorusha matangazo kwa 1080P,zinazojitahidi sana ni 720P kwa hiyo mara nyingi utaangalia 1080P contents ukutumia blu ray,mfuko wako una urefu gani etc etc. Pia fanya research yako mwenyewe kuhusu hiyo TV,yaani kuanzia brand na model number. Model number,tafiti kwa nini kwa mfano Samsung LCD 50 inches zenye model number tofauti,zinauzwa bei tofauti.Usiulize muuzaji kwa kuwa mara nyingi atataka kuuzia ambayo ina profit margin kubwa.
Karibu