Chief-Mkwawa
Platinum Member
- May 25, 2011
- 32,062
- 43,489
Mkuu nimeshaelezea sana humu ndio maana naona hata uvivu kuelezea, na kuanza kuchambua kimoja kimoja naweza andika hata page 100 u zaidi za A4, maana mambo ni mengi sana ukiingia deep zaidi ndio jinsi unavyoona. Hebu tuangalie hayo mambo matatu yaani storage, ram na camera.Usiseme si kweli, sema hakuna comparison ya hivyo vitu ulivyoorodhesha, nikuulize swali RAM sio sehemu ya specification? Storage sio sehemu ya specs? Na hivyo vyote ulivyovitaja sio specs?
Halafu kama wewe ni mtaalamu wa architecture na os za simu, unaweza kufigure out hivyo vyote unavyouliza. Halafu ukaja na findings, na baada ya kuja na findings, unaelezea hivi, kwa mfano:
1. Nimekuta processor ya Sumsung xx ni multi-core (quad, dual, octa, etc.,) processor, multi-threaded or single-threaded, RAM ni DDR4 RAM (Double data rate 4th generation synchronous dynamic random-access memory) na Tecno xx processor yake ni ..........., halafu ukaeleza jinsi hivyo vitu vinavyofanya kazi na tofauti yake, na hiyo tofauti ni kwa kiasi gani. Pia ueleze ni programs zipi na instructions gani za simu sio multi-threaded kiasi kwamba haziwezi kutake advantage ya multi-processing units , i.e, haziwezi kuwa parallelized au haziwezi kurun concurrently, toa na sababu, soma hapa:
"Although it's tempting to suppose that a quad-core processor would operate twice as fast as a dual-core processor and four times as fast as a single-core processor, things don't work out that simply. Results vary depending on the habits of the computer user, the nature of the programs being run, and the compatibility of the processor with other hardware in the system as a whole. Some programs are
just single-threaded in nature and don't speed up much from multi core CPUs" - What is quad-core processor? - Definition from WhatIs.com
2. Baada ya hapo ukaeleza aina na tofauti za storages, na kuonyesha kwa ufasaha tofauti na any significant differences, nenda mbali zaidi kuelezea cache memory.
3. Baada ya hapo ukaja tena kwenye sensor, uanze kwa kueleza sensor ni nini, inafanyaje kazi, kwa nini architecture fulani ya sensor ni nzuri kuliko nyingine? Uelezee vitu kama aperture, sensitivity, resolution, sampling rate nk., kwa kila camera (usipime resolution ya camera kwa macho), kwa nini? Kwa sababu sio kila mtu anaweza kupiga picha kwa ufasaha, upigaji picha ni utaalamu na kupiga picha nzuri sio kazi rahisi: Photography Is Difficult
Pia kuna factors nyingi zinazoathiri picha, mfano mmoja ni hali ya hewa kama vile atmosphere moisture. Isitoshe macho yanatofautiana kuona.
Kimsingi chukua kila attribute ya simu, baadhi hizi hapa: Compare Tecno i7 vs Samsung Galaxy S7 Edge Size, Specs, Camera halafu chambua kwa ufasaha, then njoo na calculated, quantitative na qualitative evidence.
Nimekupa kazi, usiikimbie. Nataka uwaeleze watu kwa kuandika kitaalamu.
Storage.
Kwenye simu kuna storage za aina nyingi sana, ila iliyo maarufu sana ni emmc, na hizi emmc zipo nyingi, yaani version tofauti tofauti, kama sijakosea emmc 5 ndio latest. Mwaka 2015 samsung akabadilisha kabisa soko la simu na kutuletea kitu kinaitwa ufs, ufs ni storage ambazo zina speed sana, mpaka leo hii simu kubwa zote aka flagship zinatumia ufs, iwe ni oneplus, HTC, samsung, huawei etc kifupi hazina mpinzani, hebu tuangalie utofauti wa speed wa emmc na ufs.
Hapo ukiangalia utaona utofauti mkubwa wa ufs ambayo imeanza 2015 kwenye s6 na simu za nyuma kama note 4 kushuka, mpaka leo hii 2017 bado flagship za Tecno zinakuja na emmc na hata hatuambiwa ni version gani,
Hivyo mtu kusema tu simu yangu ni 32GB au ni 64GB haitoshi sababu speed ya storage pia unatakiwa uijue, hii huathiri sana kufungua apps na speed ya vitu kumove toka storage ya simu hadi ram, hapa unakuta simu mbili ila moja kufungua game hadi kuanza inachukua dakika nzima na nyengine sekunde 10 tu.
tuje kwenye ram
Ram ni vile vile, zipo ddr2 za kizamani zaidi, ddr3 na ddr4 za kisasa, simu za flagship kama hio s7 inatumia ram za kisasa za ddr4 na tena ni dual chanell, yaani cpu inawasiliana na ram kwa njia mbili hivyo bandwidth inapita kwa wingi na kuongeza perfoamnce.
Cpu za mediatek zinazotumia ddr4 ni kama helio x30, lakini cpu hizi hutaziona Tecno akizitumia, anawadanganya watu na cpu xa kizamani kama helio x10 ambazo zinatumia ram za kizamani za ddr3 na pia ni single chanell, hebu tuangalie utofauti wa speed wa ram.
Na pia ikumbukwe hizi ram zina speed, zote zinaweza zikawa ni ddr4 ila moja ikawa 3200mhz na nyengine 2400mhz speed zake hazitafanana.
Na sababu simu haina dedicated gpu, ram pia hio hio hutumika kwenye matumizi ya gpu, unapoinstall launcher, unapocheza games na mambo mengine ya graphics itakusaidia.
tumalizie camera
Mkuu megapixel sio quality ya camera na hata uwe na megapixel ngapi haimaanishi camera yako itakuwa nzuri, vitu kama sensor na lens vinachangia sana quality ya picha, na camera ikiwa na megapixel nyingi huku sensor ni ndogo basi quality ya picha pia itakuwa ndogo sababu pixel zitakuwa ndogo ndogo zisizo na mwanga na noise za kutosha.
Mfano tuangalie simu kama s7 specs za Camera yake.
12 MP, f/1.7, 26mm, phase detection autofocus, OIS, LED flash, check quality
Video 2160p@30fps, 1080p@60fps, 720p@240fps, HDR, dual-video rec.,
Secondary 5 MP, 1/4.1" sensor size, 1.34 µm pixel size, f/1.7, 22mm,
Hapo kila kitu kina maana yake mkuu, kuanzia ukubwa wa sensor, ukubwa wa pixel, aperture, uwezo wa video, aina ya flash etc, tecno je?
Maisha yangu yote sijawahi ona wakitoa specs za camera zaidi ya phantom 6 plus, wakati wanaizindua wakasema wametumia sensor gani na ilikuwa ni imx 230,
Hii ni sensor ya 2014 miaka 3 iliopita na simu zote ilizotumika ni za bei ya chini kuliko hio Tecno, unaweza angalia zaidi hapa
Smartphones with IMX230 Exmor RS lens model
Then mtu huyo atakuja kujitamba hapa na tecno yake ya laki 8 kuwa ni kali balaa, wakati wenzake wananunua xiaomi za dola 100 anapata sensor hio hio.
Mkuu mambo ni mengi sana kama nilivyokuambia, kila kitu unachogusa kina maana,
Usb yenyewe kwa watu wengi ni tundu tu la kuchomekea chaja ila ina mambo mengi sana kuanzia usb otg uwezo wa kuchomeka flash, kuna usb 2 au 3 na transfer speed, kuna MHL na uwezo wa kuchomeka waya kwenye simu ukaangalia kwenye tv, etc
Kila ukiingia deep ndio unaona class za hizi simu ni tofauti na unakuta kila unapogusa Tecno wapo nyuma, kama una vyengine unataka nivielezee nitavielezea