Kuna binti mmoja nilikuwa naye coy moja,kasoma NGANZA Sec, binti kapewa uzuri wa umbo na tabia. Tulipo fungua mafunzo alisumbuliwa saana,ilifika wakati coy nzima tulijua,wakumpa ushauri aende kuripoti kwa Sir Major tulikuwa wengi. Lakini kilichomtokea huyo binti kila alipokuwa anaenda kutoa taarifa ni majuto hata wenye umri wa baba yake walimtaka pia. Alisumbuliwa vibaya,tukiwa tumekusanyika usawa wa coy walimfanyia dhihaka za aina mbalimbali.
Siku ngumu kwake zilianza tulipoenda Endurance training Binti alifanyiwa jambo la ajabu sana,hakuna asiye choka wengine tulipochoka tulihimizwa kwa maneno lakini kwa Mwenzetu viliongea Viboko,ni kama walimkalili kila afande alikuwa adui yake.
Mwisho wa siku aliingia kumi nane za C.I, akawa kipozeo na usumbufu toka kwa Privates wa jeshi,koplo,na wengineo.
NB:
Wengine tuna kumbukumbu mbaya zaidi juu ya jeshi kuliko hata yale mazuri tuliyopata,Mathalani kamwe sitakuja mruhusu binti yangu akajiunge na JKT,na sio tu Jkt maana wachafuzi wengi ni jw basi secta yoyote ya ulinzi na usalama wa raia.
Mkuu kuna matukio mengi jeshini yakianikwa yanaweza jaza server za JF.
Hizi habari ni bora zingeandikwa kama makala kwenye magazeti yanayowafikia waTanzania waliowengi,Akina Zitto waliyaona haya,na tuliwasimulia pia mambo tunayofanyiwa ( Wao walikuwa na say kubwa wakati wa mafunzo) Lakini wapi.
Hivyo mengi yanayoletwa hapa yanaukweli ndani yake.