Ubakaji JKT(mafunzoni)

Ubakaji JKT(mafunzoni)

Status
Not open for further replies.
ukienda jeshini kuendekeza uduwanzi.......utafundishwa adabu/nidhamu......ni rahisi sana kubakwa visichana vya mtaani lakini sio wasichana walio jeshini......jeshini kama ukisikia ngono ujue ni maelewano ya watu wawili....na endapo itajulikana (iwe maelewano au ubakaji) hatua za kinidhamu huchukuliwa dhidi ya wahusika, ikiwa ni pamoja kuachishwa kazi kwa afisa wa jeshi kama alihusika......

....kwa ujumla maisha ya Jeshini ni safi sana....asiwadanganye mtu na wala asiwatishe mtu yeyote.............
 
Kuna maafande wa kike mabazazi wanaweza kuwasaga watoto wa kike. Cha muhimu ni kujenga nidhamu kwa makamanda hao wapumbavu wasiokuwa na akili. Wakati wetu kulikuwepo na uchafu huo lakini sisi wanaume tulikuwa tunapambana na maafande wa namna hiyo na wale dada zetu waliokuwa wanajirahisisha kwa maafande tulikuwa tunawazomea mpaka ilifika wakati upumbavu huo uliisha pale Bulombora. Tulikuwa tayari kupigana na maafande kulinda dada zetu. Sasa hivi ni shida kwa kuwa watoto wanaoenda jeshini wengi wao bado wadogo ulilinganisha na wakati ule tulikuwa tunaingia jeshini wengi wakiwa na zaidi ya miaka ishirini. KImsingi nikuwajengea vijana wetu ujasiri kabla ya kwenda jeshinini waweze kusema no kwa hao makanda wapumbavu bila kujali adhabu yoyote na kamanda yoyote akiwasumbua waende kumripoti kwa kamanda wa nidhamu natumaini anaitwa Adjutant kama sijakosea
Daa ili balaa kubakana tena basi wazitenganishe za boys na girls na kila moja inasimamiwa na jinsia husika
 
Kuna maafande wa kike mabazazi wanaweza kuwasaga watoto wa kike. Cha muhimu ni kujenga nidhamu kwa makamanda hao wapumbavu wasiokuwa na akili. Wakati wetu kulikuwepo na uchafu huo lakini sisi wanaume tulikuwa tunapambana na maafande wa namna hiyo na wale dada zetu waliokuwa wanajirahisisha kwa maafande tulikuwa tunawazomea mpaka ilifika wakati upumbavu huo uliisha pale Bulombora. Tulikuwa tayari kupigana na maafande kulinda dada zetu. Sasa hivi ni shida kwa kuwa watoto wanaoenda jeshini wengi wao bado wadogo ulilinganisha na wakati ule tulikuwa tunaingia jeshini wengi wakiwa na zaidi ya miaka ishirini. KImsingi nikuwajengea vijana wetu ujasiri kabla ya kwenda jeshinini waweze kusema no kwa hao makanda wapumbavu bila kujali adhabu yoyote na kamanda yoyote akiwasumbua waende kumripoti kwa kamanda wa nidhamu natumaini anaitwa Adjutant kama sijakosea
Daa ili balaa kubakana tena basi wazitenganishe za boys na girls na kila moja inasimamiwa na jinsia husika
 
Jamani hii habari kama ni kweli basi hiyo JKT ipigwe marufuku. Inauma sana kwa kweli.
 
Kama kweli kuna ubakaji hiyo ni hatua mbaya imefikiwa. Sisi tuliopitia wakati huo sikuwahi kusikia msichana kabakwa jeshini isipokuwa kuna wasichana walikuwa na uhusiano wa kimapenzi na maafande kwa makubaliano yao wenyewe na walikuwa wakijitahidi sana kuficha siri maana wakidhihirika na habari ikifika ngazi za juu ni tatizo kwao. Ilikuwa pia miongoni mwa makuruta wanachukuana wenyewe kwa wenyewe, isipokuwa ilikuwa inabidi wafanye mambo yao kwa siri sana maana nidhamu ya jeshi ilikuwa hairuhusu mambo hayo. Nakumbuka sikumoja rafiki yangu alikuwa kasimama na msichana ambaye ni ndugu yake mida ya jioni wanaongea, afande akawatokea na kuwaamuru waanze kuruka kichura kwa kuwa wamesimamisha minazi, jamaa akajitetea kuwa huyo ni ndugu yake, afande hakukubali akampiga jamaa buti na jamaa akaanguka, alipoamka zikaaanza ngumi, afande alitandikwa na jamaa hadi akang'olewa jino moja na jamaa aliumia kidogo puani, afande mwenyewe alikuwa MP. habari zikafika juu na wakafikishwa kwenye 'court martial'
 
umbeya na uzandiki. Wewe ni msemaji wa jkt au familia?

KAMA unaona anadanganya lete habari za kukanusha na sio shutuma

mm nilishakutana na wanawake walioenda jeshini walilisema suala hili la ubakaji/kulazimishwa kufanya mapenzi na wakufunzi lipo, mtu akikataa atasakamwa na kupewa mazoezi mazito, usibishe tu kwa kuwa uan mdomo, tulifanyie kazi tujue ukweli wake na mazingira yake kisha tuchukue hatua stahiki. ngoja aje atendewe binti yako utakuja kutuambia hapa
 
Dada mmoja tulikuwa nae jeshini enzi hizo alikuwa na kamchezo kachafu na afande, matokeo akapata ujauzito na alijifungua mtoto kipindi tunamaliza jeshi.
 
ukienda jeshini kuendekeza uduwanzi.......utafundishwa adabu/nidhamu......ni rahisi sana kubakwa visichana vya mtaani lakini sio wasichana walio jeshini......jeshini kama ukisikia ngono ujue ni maelewano ya watu wawili....na endapo itajulikana (iwe maelewano au ubakaji) hatua za kinidhamu huchukuliwa dhidi ya wahusika, ikiwa ni pamoja kuachishwa kazi kwa afisa wa jeshi kama alihusika......

....kwa ujumla maisha ya Jeshini ni safi sana....asiwadanganye mtu na wala asiwatishe mtu yeyote.............
Hizi habari zilinishitua na ikabidi nifanye uchunguzi wangu binafsi kwa sababu kuna baadhi ya ndugu, wazazi walipigia simu kutaka kujua kinachoendelea kule. Raia wengi tunaona makambi ya Jeshi la Kujenga Taifa kama vile ni makambi ya mafunzo ya Alqaeda au Alshabaab. Lakini baada ya kufuatilia kwa kuongea na waliopita huko wale wa miezi sita ( kujitolea) pamoja na form six awamu ya kwanza pamoja pia na kuongea na maafande mbalimbali kwenye makambi tofauti kwa njia ya simu nimeridhika kwamba ubakaji ni kitu kigumu sana au haiwezekani kambini. Wengi walikiri uwezekano wa kuwepo kwa mahusiano ya hiari hasa kwa wanafunzi wavivu wasiopenda kazi za jeshi.

Wale wa form six waliniambia kuna utaratibu wa kuwaripoti wakufunzi wanapowanyanyasa na huadhibiwa kijeshi. Kwa kweli kwa huku mtaani kutokana na uvumi na kutojua kinachoendelea huko makambini tunaweza kuahamanika sana lakini siwezi kuamini kwamba viongozi wa jeshi pamoja na serikali ni wakatili kiasi cha kuacha haya mambo ya hovyo yatokee bila udhibiti ikiwemo kuwafukuza kazi na kuadhibiwa kijeshi wale wote wanaoharibu maana ya mafunzo.
 
Isitoshe watoto wa sasa hivi wanamaliza shule wakiwa wadogo sana, wanaenda kuwaumiza bure tu. I swear mtoto wangu wa kike hataenda JKT, wakimyima nafasi ya kusoma chuo au kazi ni sawa tu. Na watoto wanaokufa huko kwenye mafunzo niwengi sema hawatangazi tu



Binafsi siafiki kabisa suala la wanafunzi kupitia JKT . Hali hii ya kipuuzi/kinyama hata huko nyuma ilikuwepo sema kipindi kile magonjwa hayakua mengi. Lkn kwa nyakati hizi watoto wetu wataumia bure kisa uzalendo.
 
Labda mabadiliko ya kimazingira, ila nijuavyo mimi wakati nilipita huko jeshini wakati huo ilikuwa ni mafunzo ya mwaka mmoja, mambo ya mapenzi yalikuwa hayaruhusiwi kabisa jeshini. kulikuwa na RSM kambini kwetu alikuwa ni mlokole alikuwa safisana na ni mkalisana na alikuwa anasema hata msichana ajipendikeze kwake yeye hata taim, mke wake anatosha, kwa kweli alikuwa strict sana. RSM = regimental Sgt Major
 
Kwa hili naomba Mungu watoto wangu watakapomaliza form six jeshi liwe limeshafutwa tena. Sabab sijaona paliponipa ugumu kwa kutopita jeshini.
 
Sikubaliani na wewe hata kidogo, jeshini ubakaji uko sio kila mahali lakini ubakaji ulikuwepo mfano enzi zetu watu waliokuwa wanatembea usiku walikutwa na haya. Nakumbuka kombania yangu walichaguliwa watu kuja Dar kuhesabu sense au gwaride sina uhakika, wakiwa kambini mlalakuwa wasichana wawili marafiki mmoja akaumwa homa kali na kipindi kile dawa sindano za masaa hivyo ikabidi mgonjwa aende usiku saa 6 na rafiki akimsindikiza, wakiwa wanarudi walikutana na wanajeshi wakaanza kuwavuta kwenye giza yule mzima alipamabana wakamshindwa ikawa kazi kwa mgonjwa wanamburuta na mwenzie anapiga kelele huku anamvuta arudi barabarani kwenye mwanga mpaka wametokea watu kuwasaidia walijaa mikwaruzo na na mgonjwa akazimia na wote wakarudishwa dispensary. Hii nimeishuhudia kw amacho yangu na huyo dada alitangazwa shujaa na CO waliporudi kambini...maadili yalivyo mabaya sasa si ndio zaidi? mimi sipeleki mtoto wangu liwalo na liwe
ukienda jeshini kuendekeza uduwanzi.......utafundishwa adabu/nidhamu......ni rahisi sana kubakwa visichana vya mtaani lakini sio wasichana walio jeshini......jeshini kama ukisikia ngono ujue ni maelewano ya watu wawili....na endapo itajulikana (iwe maelewano au ubakaji) hatua za kinidhamu huchukuliwa dhidi ya wahusika, ikiwa ni pamoja kuachishwa kazi kwa afisa wa jeshi kama alihusika......

....kwa ujumla maisha ya Jeshini ni safi sana....asiwadanganye mtu na wala asiwatishe mtu yeyote.............
 
Isitoshe watoto wa sasa hivi wanamaliza shule wakiwa wadogo sana, wanaenda kuwaumiza bure tu. I swear mtoto wangu wa kike hataenda JKT, wakimyima nafasi ya kusoma chuo au kazi ni sawa tu. Na watoto wanaokufa huko kwenye mafunzo niwengi sema hawatangazi tu
bora nitafute elimu nyingine au nilipie vyuo vimejaa tele sipeleki mtu huko
 
Kama kuna mtu anasupport huu ubakaji ampeleke dadaye au mamaye abakwe aone uchungu wa kubakwa, sio kila kitu migamba inabisha tu bila kuwa na hoja ya msingi. Pambaf!
 
Sikubaliani na wewe hata kidogo, jeshini ubakaji uko sio kila mahali lakini ubakaji ulikuwepo mfano enzi zetu watu waliokuwa wanatembea usiku walikutwa na haya. Nakumbuka kombania yangu walichaguliwa watu kuja Dar kuhesabu sense au gwaride sina uhakika, wakiwa kambini mlalakuwa wasichana wawili marafiki mmoja akaumwa homa kali na kipindi kile dawa sindano za masaa hivyo ikabidi mgonjwa aende usiku saa 6 na rafiki akimsindikiza, wakiwa wanarudi walikutana na wanajeshi wakaanza kuwavuta kwenye giza yule mzima alipamabana wakamshindwa ikawa kazi kwa mgonjwa wanamburuta na mwenzie anapiga kelele huku anamvuta arudi barabarani kwenye mwanga mpaka wametokea watu kuwasaidia walijaa mikwaruzo na na mgonjwa akazimia na wote wakarudishwa dispensary. Hii nimeishuhudia kw amacho yangu na huyo dada alitangazwa shujaa na CO waliporudi kambini...maadili yalivyo mabaya sasa si ndio zaidi? mimi sipeleki mtoto wangu liwalo na liwe

....na wewe yaliwahi kukuta au uliponea chupu chupu?...... acheni kutisha na ku-disqualify JKT kwa mambo ya kusimuliwa....wewe unaijua kambi ya mlalakuwa ilivyo kweli au ndio chuki zisizo na kichwa wala miguu..........
 
umbeya na uzandiki. Wewe ni msemaji wa jkt au familia?

Naona wewe kwenu hamfi ndiyo maaan hujui uchungu wa kufiwa na hivyo, huon i hata mantiki ya kuchukua hatua za tahadhari.

Kama ndivyo, waache wanaotoka kwenye familia na koo zinazopatwa na mauti wajadili usalama wa family members wao. Wewe na wenzako msiokufa muendeleze uzandiki na udictator wa kijinga usioona hata maana ya maisha ya watu. Kuanzia hapo jipangeni mtafute msemaji wa uhai wenu udumuo kama mtampata kwa hao wabakaji ama wanaopanga mipango isiyo kuwa na umakini ama wasimamizi wasiojali, ndio mtoe tamko. Hata mkitoa tamko fake, hata mkichukua miaka, hamna tatizo maana ninyi hamfi. Na hamna haja ya kuchukua tahadhari mapema.
 
....na wewe yaliwahi kukuta au uliponea chupu chupu?...... acheni kutisha na ku-disqualify JKT kwa mambo ya kusimuliwa....wewe unaijua kambi ya mlalakuwa ilivyo kweli au ndio chuki zisizo na kichwa wala miguu..........
nimekwambia wazi ni kombania yangu na walikuwa rafiki zetu so nimeona michubuko na ikatangazwa walivyorudi, mlalakua ni nini iko mjni ila si ina bustani ina michongoma na kumbuka ni usiku zaidi ya saa 6. Hizi kambi sio safe kwa hiki kipindi cha magonjwa yasiyotibika na maadili yaliharibika. Mimi hayakunikuta na hayakuwa common kwani sie kazi tulizoea toka mashuleni itakuwa hawa wa St nini sijui. Naomba mambo ya siasa tuweke pembeni twende na wakati
 
nimekwambia wazi ni kombania yangu na walikuwa rafiki zetu so nimeona michubuko na ikatangazwa walivyorudi, mlalakua ni nini iko mjni ila si ina bustani ina michongoma na kumbuka ni usiku zaidi ya saa 6. Hizi kambi sio safe kwa hiki kipindi cha magonjwa yasiyotibika na maadili yaliharibika. Mimi hayakunikuta na hayakuwa common kwani sie kazi tulizoea toka mashuleni itakuwa hawa wa St nini sijui. Naomba mambo ya siasa tuweke pembeni twende na wakati

Wewe utakuwa unajua/unafahamu kuwa Jeshini kuna sheria na wasimamizi wa sheria hizo wapo (Matrons, Wanasheria, MPs, Kamanda wa nidhamu nk nk)......Jeshini kuna discpline ya hali ya juu.......na ili jeshi liwe Jeshi kweli NIDHAMU ni KITU NAMBA MOJA.....hayo maovu yakitokea (sio kubaka/kubakwa....hata ngono kati ya Askari na Kuruta au Kuruta na Kuruta) na yakiripotiwa wahusika hushikishwa adabu.....Askari hufungwa na kufukuzwa kazi.....Kuruta unafungwa na unalipia siku ulizokaa jela pale wenzako watakapokuwa wanaondoka baada ya kumaliza jeshi......

.....binafsi sitetei uozo wa aina yeyote ule.......haya mambo ya kubaka au kubakwa yako sehemu zote.......kuna watu wanabakwa/wanabaka maofisini (serialini na ofisi binafsi), mahospitalini! (au hujawahi kusikia Daktari kabaka mgonjwa), kuna watu wanabaka watoto wao......... na mambo kama hayo........sheria zipo sehemu zote hizo.......lakini sheria pekee hazitoshi.....

.....kinachohitajika kueleweka ni kwamba......sisi kama wazazi tuna jukumu la kuelimisha vijana wetu.....maadili yetu yameshuka sana, vijana siku hizi hawana tena heshima zile tulizukuzwa na wazazi wetu......sisi wazazi wa kile tunajifanya tunawapenda sana watoto wetu na kuwaruhusu kuiga mambo yasiyo faa kwa jamii yetu ya Kitanzania.......kama tunawafundisha tabia njema watoto wetu hata wabakaji na wabakwaji watapungua.......

....issue sio JKT,.......issue ni kuwa how effective elimu imetusaidia ili kuhakikisha mambo maovu kweny jamii zetu hayatokei.....na kuzitumia sheria zetu effective......sisi sote tuna JUKUMU HILO.....kukimbia tatizo si SULUHISHO.......

......vijana walioko boarding schools nako ni hatari tupu, vijana wengi wamejifuna kuvuta bangi na ulevi kupindukia wakiwa boarding school......na huko wanakolewa vijijini wanafanya ufuska wa kupindukia......kuna vitoto vimezaliwa huko vijijini kutokana na kadhia hii ya vijana wa boarding school.......Vijana wetu siku hizi wanabakwa kule beach na pia ngono zinaendelea sana kule baharini......wewe pita kule ukajionee......tena ningekuasa usimruhusu mtoto wako aende beach na sio JKT.....JKT ni salama......

Mimi nina watoto wa Kike na wote nimesha wapa notice kuwa watakwenda JKT.......ninajiamini wako ready kwa mazingira yeyote ya kimaisha na kama ni upuuzi basi itakuwa ni uamuzi wao wenyewe.......and they are very excited......the can't wait.......

.......Mimi (nilikuwa Kambi ya Chita....sijui kama unaifahamu.....na sijui huko ungesemaje), kaka na dada (kuna dada yangu alikuwa ngangari Nachingwea) zangu wote tumepita jeshini na hadi leo tupo safi kabisa tunapigana na maisha.......acheni hizo!......jeshini safi sana.......ni sehemu amabyo ukifuata taratibu zake uta-enjoy sana......

MSIWATISHE VIJANA.......alaah
 
Kama kuna mtu anasupport huu ubakaji ampeleke dadaye au mamaye abakwe aone uchungu wa kubakwa, sio kila kitu migamba inabisha tu bila kuwa na hoja ya msingi. Pambaf!

Sa hoja ya msingi ipo wapi kwan mbona zote tetesi tu!?
Magamba wawatu mbona mnawaandama hivyo? au wenyewe hawana wafuasi mitandaoni?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom