Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,836
- 12,016
Taarifa nilizozipata haraka sasa hivi ni kuwa watu wengi sana wanahisiwa kufa maji baada ya kivuko kubinuka juu chini, chini juu katika kisiwa cha UKARA wilayani Ukerewe.
Wakazi wa Ukerewe wakiwa mita chache kutoka kivuko kilipozama
====
Kivuko cha MV Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Bugorara na kisiwa cha Ukala katika ziwa Victoria kimezama huku taarifa za idadi ya watu waliokuwemo ndani ya kivuko hazijajulikana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jonathan Shana amesema kivuko hicho kimezama wakati kikielekea katika Kisiwa cha Ukara. Kiliondoka saa 6 mchana na ilipofika saa nane kamili mchana kilipinduka.
Amesema bado hawajapata idadi kamili ya waliokuwemo kwenye kivuko hicho.
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), Hassan Karonda amekiri kuzama kwa kivuko hicho na yuko njiani kulekea huko na watatoa taarifa baadaye.
Kivuko cha MV. NYERERE kilinunuliwa na kuanza kutoa huduma mwaka 2004. Kilifungwa injini mbili mpya zenye thamani ya shilingi milioni 191 JULY 2018. Kivuko cha MV. Nyerere kina uwezo wa kubeba tani 25 sawa na abiria 100 na magari 3 kwa wakati mmoja.
UPDATES: 1900HRS
=> Watu watano wamekufa na wengine 32 wameokolewa mpaka sasa ila hali zao ni mbaya kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere.
=> "Mtu Hajalipwa Mshahara Halafu Anasikia Trilion 1 Imepotea Inauma" -Joseph Mkundi
Mbunge Joseph Mkundi akitahadharisha kuhusu kivuko cha MV Nyerere Apr 24, 2018
Alikuwa akichangia hoja ya bajeti ya Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano iliyopo chini ya Waziri wake, Profesa Makame Mbarawa.
UPDATES:
AJALI YA KIVUKO CHA MV NYERERE: WATU 44 WAMEFARIKI, ZOEZI LA UOKOAJI LASITISHWA HADI KESHO
Mbali na idadi hiyo ya waliofariki, Watu 37 wameokolewa katika ajali huku hali zao zikiwa mbaya
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amesema zoezi la uokoaji limesitishwa kutokana na giza kuingia
10:40 - MIILI 86 IMESHAOPOLEWA MPAKA SASA
Idadi ya vifo katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere, Mwanza imefika watu 86 huku uokoaji ukiendelea, RC John Mongella amethibitisha
11:41 - IDADI YA WALIOOPOLEWA YAFIKA 94
Idadi ya vifo katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere, Mwanza imefika watu 94 huku uokoaji ukiendelea, RC John Mongella amethibitisha
11: 43 Chanzo cha kuzama kwa mujibu wa DC wa Ukerewe
DC Ukerewe amesema kivuko kilikuwa kimebeba zaidi ya abiria 400, kilivyokaribia kufika mwaloni(kutia nanga) nahodha akapunguza spidi hivyo abiria wakakimbilia upande wa kushukia ili wawahi kutoka, kivuko kikazidiwa uzito na kupinduka.
12:40 - MIILI ILIYOOPOLEWA YAFIKA 100
Miili ya waliokufa na kuopolewa mpaka sasa yafika 100.
12:49 - IGP SIRRO: UTAMBUZI WA MAREHEMU UNAENDELEA
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simoni Sirro amesema utambuzi wa marehemu katika ajali ya MV Nyerere mkoani Mwanza unaendelea kwa miili iliyoopolewa.
Litafunguliwa Jalada maalum la kuchunguza tukio la kuzama kwa kivuko cha MV. Nyerere
13:03 - Idadi ya miili iliyoopolewa yafika 125
Idadi ya miili iliyoopolewa kwenye kivuko cha Mv Nyerere imefikia 125 mpaka sasa
13:20 - WAZIRI ISACK KAMWELWE: ZOEZI LA KUOPOA MIILI ILIYOKWAMA LITAKAMILIKA SAA 12 JIONI LEO
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema shughuli ya uokoaji wa watu walionasa kwenye kivuko cha MV Nyerere inatarajiwa kukamilika leo saa 12 jioni
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema mazishi ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya Mv.Nyerere iliyotokea Septamba 20 huko kisiwani Ukara, Ukerewe mkoani Mwanza yatakuwa ya kitaifa ambapo viongozi wakuu wa kitaifa wanatarajia kushiriki mazishi hayo.
17:21 - MIILI ILIYOOPOLEWA YAFIKA 126
Waliofariki dunia ajali ya kivuko wafikia 126, miili 36 imeshatambuliwa na ndugu zao
17:46 - MIILI ILIYOOPOLEWA YAFIKA 131
Kwa mujibu wa Waziri wa Uchukuzi Mhandisi Isack Kamwelwe idadi rasmi ya vifo mpaka jioni hii kutokana na ajali ya MV Nyerere ni watu 131.
18:10 - IDADI YAFIKA 136
Afisa mkuu wa Polisi Tanzania, Simon Sirro anasema kuwa idadi ya watu waliofariki kutokana na mkasa huo imefikia 136
18:15 - TAMKO LA SERIKALI (Katibu Mkuu Kiongozi)
Rais Magufuli ameagiza kuwa kufuatia ajali ya MV Nyerere Bendera ya Taifa itapepea nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia kesho Septemba 22, 2018.
Rais Magufuli ameagiza viongozi wa taasisi na mamlaka zinazosimamia usafiri wa majini wahojiwe na watakaobainika kuhusika kwa uzembe wachukuliwe hatua kali.
18:30 - Waziri Mkuu Majaliwa, CDF Mabeyo wawasili Ukerewe
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na CDF Mabeyo wamewasili Ukerewe na wamepokelewa na RC Mongella na IGP Sirro.
20:00 - NAHODHA WA KIVUKO ANASHIKILIWA KWA UCHUNGUZI
Nahodha wa MV Nyerere anashikiliwa na vyombo vya ulinzi kwa kosa la kumuachia mtu asiye na uwezo(Deiwaka) kuendesha kivuko na yeye kutosafiri.
Taarifa ya Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza siku 4 za maombolezo kuanzia leo tarehe 21 Septemba, 2018 kufuatia ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere katika ziwa Victoria na kusababisha vifo vya watu 131 waliothibitika mpaka sasa.
Kivuko hicho kilipinduka na kisha kuzama majini jana mchana meta chache kabla ya kufika katika kisiwa cha Ukara kikitokea kisiwa cha Bugolora ambapo mpaka sasa watu 40 wameokolewa wakiwa hai, miili 131 imeopolewa na zoezi la uokoaji linaendelea.
Pamoja na kutangaza siku 4 za maombolezo Mhe. Rais Magufuli amewapa pole wote waliopoteza jamaa zao katika ajali hiyo, amewaombea majeruhi wapone haraka na amewapongeza viongozi wa Mkoa wa Mwanza, vyombo vya ulinzi na usalama na wananchi wote wanaoendelea kushiriki katika uokoaji.
“Kwa masikitiko makubwa nawapa pole wote waliopoteza jamaa zao katika ajali hii, huu ni msiba mkubwa uliolikumba Taifa letu, nawaomba Watanzania wote kwa wakati huu ambapo vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na wananchi wanaendelea na uokoaji tuwe watulivu na tuendelee na kushikamana kama ilivyo desturi yetu, huu sio wakati wa kulumbana na kukatishana tamaa” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewataka Watanzania kuwapuuza wanaotaka kutumia ajali hii kujipatia umaarufu wa kisiasa, na amebainisha kuwa ni vema Watanzania wote tuungane kuwaombea Marehemu wapumzike mahali pema, majeruhi wapone haraka na kuwatia moyo wote wanaoendelea na zoezi la uokoaji.
Mhe. Rais Magufuli amemtuma Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kwenda eneo la tukio, ameagiza kuundwa tume ya uchunguzi wa chanzo cha ajali hii na ameagiza wote waliohusika kusababisha ajali hii wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
“Taarifa za awali zimeonesha dhahiri kuwa kivuko cha MV Nyerere kilikuwa na idadi kubwa ya watu na mizigo kupita uwezo wake, kama kuna mtu yeyote mwenye ushahidi wa chanzo chochote cha ajali hii, tunatarajia kuwa ataupeleka mahakamani” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
21 Septemba, 2018
UPDATES: 22 SEP 2018
0845hrs: Miili 15 yaopolewa
Miili mingine 15 imeepolewa leo asubuhi na kufanya idadi ya vifo katika ajali ya MV. Nyerere kufika 151.
0820HRS: Nahodha na Mkuu wa Kivuko cha MV Nyerere ni miongoni mwa watu waliofariki
Nahodha na Mkuu wa Kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi kikiwa safarini kutoka kisiwa cha Bugorora kwenda Ukara wilayani Ukerewe, Mwanza, ni miongoni mwa watu waliofariki dunia katika ajali hiyo.
1100hrs: Idadi ya miili iliyoopolewa yaongezeka
Idadi ya watu waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi mchana Septemba 20, 2018 imefikia 157 huku uokoaji ukiendelea.
1115hrs: MHANDISI WA KIVUKO APATIKANA AKIWA HAI
Mhandishi wa kivuko #MVNyerere, Alphonce Charahani ameokolewa akiwa hai siku 2 baada ya kivuko kuzama, amekutwa akiwa amejipaka oili mwilini. Sasa majeruhi wafikia idadi ya 41.
1117hrs: Serikali kugharamia kusafirisha maiti hadi hospitali ili zitambuliwe na kutoa TSH 500,000 kwa kila familia iliyofiwa
11:26 - Mbunge wa Ukerewe: CHANGAMOTO NILIZOWASILISHA BUNGENI ZILITATULIWA
Mbunge wa ukerewe amesema changamoto za kivuko alizowasilisha bunge zilitatuliwa miezi miwili iliyopita, kilikuwa sawa na kilikuwa mbioni kubadilishiwa ratiba ikiwemo kuongeza idadi ya safari ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa eneo hilo.
12:00 - MIILI 163 IMEOPOLEWA
Idadi ya watu waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha Nyerere imefikia 163 baada ya miili mingine 27 kuopolewa leo.
12:16 - WAZIRI UMMY MWALIMU: TUACHE KUSAMBAZA PICHA ZA MAREHEMU
"Ndugu zangu Watanzania, ninawaomba sana TUACHE KUSAMBAZA NA KUPOSTI PICHA ZA MAREHEMU WA AJALI YA MV NYERERE. Tuheshimu Utu na Ubinadamu wao"
12:19 - MIILI 116 YA WALIOFARIKI YATAMBULIWA
1250hrs: Wananchiwa Ukerewe wakosa Usafiri wa kwenda Ukara
Zaidi ya wananchi 500 wamekwama katika eneo la Bugolora baada ya kukosa usafiri wa kuelekea kisiwa cha Ukara kulikotokea ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere juzi Septemba 20, 2018.
1330hrs: Idadi ya waliopoteza maisha yaongezeka.
Miili mingine 33 imeepolewa na kufanya idadi ya vifo katikia ajali ya kivuko cha MV Nyerere kufika 196. Uokoaji unaendelea.
1600hrs: Meli yenye Vifaa Maalum yaelekea kwenye tukio
Meli ya MV Nyehunge kutoka Mwanza inaelekea kisiwa cha Ukara ikiwa na vifaa maalum vitakavyotumika kukinyanyua kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi.
17:30 - Miili iliyoopolewa yafika 209
Kwa mujibu wa Msemaji wa Serikali, Idadi ya miili iliyoopolewa katika ajali ya Kivuko cha MV Nyerere mpaka sasa imefikia 209. Katika idadi hiyo miili iliyotambuliwa na ndugu na jamaa ni 172
17:45 - SERIKALI YATANGAZA KAMATA KAMATA YA WANAOTOA TAKWIMU ZA UONGO
Kupitia Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola imesema kuwa itatumia #SheriaYaTakwimu kuwakamata na kuwafikisha Mahakamani wote watakao fanya kosa hilo
20:25 - Miili iliyoopolewa yafika 218
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amesema miili 218 imeopolewa katika ajali ya MV Nyerere huku 171 kati ya hiyo ikitambuliwa. Kazi ya uopoaji itaendelea kesho
UPDATES: 23 SEP 2018
0800hrs: Siku ya tatu baada ya ajali, Miili mingine yapatikana.
Miili mingine 7 imeepolewa leo asubuhi na kufanya idadi ya vifo katikia ajali ya kivuko cha MV Nyerere kufikia 224, RC wa Mwanza
1220hrs: Ibada ya mazishi ya marehemu ambao hawajatambuliwa na wale waliombwa na ndugu kuzikwa na Serikali
Miili 9 imewasili katika makaburi ya viwanja vya shule ya sekondari Bwisya kwaajili ya maziko ya Kitaifa yatakayoongozwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, makaburi zaidi ya 80 yamechimbwa kwa sababu mpaka sasa kuna miili ambayo inaibuka kutoka majini.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Isaac Kamwele anasema; Waliofariki 223 wanawake 126, wanaume 71 watoto wa kike 17,watoto wa kiume 10.
4 Hawajatambuliwa. Wamachukuliwa DNA. Watano waliotambuliwa watazikwa na ndugu hapa. Jumla watazikwa tisa.
Wananchi wa Ukara waliokoa 40 wakiwa hai. Kivuko kilibeba watu 265,uwezo wake ni kubeba abiria 101.
Milioni 190 zimechangwa na wananchi
Serikali imeweka utaratibu mzuri wa kujenga mialo na kununua vivuko vilivyo salama
1320hrs: Waziri Mkuu Majaliwa anasema;
Rais Magufuli amepokea habari ya ajali hii kwa mshituko.
Ajali ya kivuko hiki imesababishwa na kivuko kubeba abiria wengi na mizigo mingi.
Taarifa za awali zinaonyesha abiria zaidi ya 260 walikuwa ndani ya kivuko hiki.
219 imetambuliwa na miili 214 imetambuliwa na kuchukuliwa na ndugu. Minne tutaizika hapa ikiwemo mitano iliyotambuliwa ila ndugu wameamuwa wazikwe hapa.
Serikali itachukua hatua ya kuunda tume ya wachunguzi wakiwemo wataalam ili kubaini chanzo na wote waliohusika watachukuliwa hatua.
Meli ya MV Nyahunge imeletwa kuendelea kutoa huduma.
Tayari tumewakamata maafisa wote walikuwa wanahusika na usalama wa majini.
Kuanzia tarehe 21-24 imetangazwa kama siku ya maombolezo na bendeza zitapepea nusu mlingoti.
Tumefungua account ya MV Nyerere namba 3111005726. Itakumika kujenga wigo na mnara wenye majina ya wote waliofariki.
Tutaivuta meli kuileta mwaloni. Tutaendelea na mazishi pale tutakapopata mwili mwingine, nami ntaendelea kubaki Ukara kusimamia zoezi hili.
Kwa niaba ya rais natoa pongezo kwa John Mongera Mkuu wa mkoa wa Mwanza kwa jinsi mlivyoshughulikia kazi hii. Kamwele, Muhagama nawashukuru kwa uratibu. Namshukuru Kigoma Malima, Venance Mabeyo, Vikosi vya uokoaji JWTZ na Zanzibar, Jeshi la wanamaji, Msalaba mwekundu, Jeshi la akiba la Mgambo na wananchi wa kisiwa cha Ukara. Tunashukuru Madaktari wauguzi na manesi, nashukuru Vyombo vya habari. Nawashukuru Viongozi wa dini. Tunawashukuru Wasanii kwa kutunga nyimbo za kufariji na kuwatuliza watanzania. Nawashukuru Viongozi wa Nchi mbalimbali kwa kutufikishia salamu za pole. Nawashukuru wote kwa niaba ya mheshimiwa rais.
Katika kuimalisha usafiri majini, Serikali imeendelea kuongeza vyombo. Ziwa Victoria serikali imeanza kujenga meli ya kwenda Kagera, na Vivuko vipya vya Ukara na Bugolora.
Serikali itaendelea kuimalisha usafiri mwingine sehemu nyingine.
Taifa lipata msiba mkubwa sana, wito wetu ni tushikamane. Ni majonzi makubwa sana,wafiwa wanahitaji faraja. Tujipe moyo kiwa ni mapenzi ya Mungu.
Tuendelee kumuomba mwenyezi Mungu aendelea kuwaponya majeruhi wote na awalaze marehemu wote mahali pema peponi Amina.
1344hrs: Namba ya Michango yatangazwa
Jenista Muhagama anatangaza namba ya tigo pesa ya kutoa mchango. Namba imesajiliwa kwa jina la RAS Mwanza. 0677030000
1347hrs: Inaendelea dua ya kuwaombea waliotangulia mbele ya haki
1400hrs: Majeneza yanaanza kuingizwa kwenye Makaburi. Haya ni mazishi ya pamoja ya miili 9, shughuli hii inaongozwa na Waziri Mkuu Majaliwa.
10:00 (24/09/2018) - Mwili mmoja wa mtoto umeopolewa na kufanya idadi kufikia 225
Mwili mmoja umeopolewa leo katika Ziwa Victoria na kufanya idadi ya waliokufa kwenye ajali ya MV Nyerere kufikia 225
10:54 (24/09/2018) - Miili miwili yaonekana ikiwa inaelea
Waziri wa Ujenzi Mhandisi Isack Kamwelwe amesema kuna miili mingine miwili imeonekana muda huu ikielea juu ya maji
10:40 (25/09/2018) - Mwili mmoja wa mtoto umeopolewa na kufanya idadi kufikia 227
Mwili wa mtoto mmoja umeopolewa leo katika Ziwa Victoria na idadi ya waliokufa kwenye ajali ya MV Nyerere kufikia 227
10:30 (26/09/2018) - Mwili mwingine umeopolewa eneo la ajali
Mwili mwingine umeopolewa asubuhi hii kwenye eneo palipotokea ajali na kufanya jumla ya miili 228 mpaka sasa.
1212hrs (27/092018) - Mwili wa mtoto wa kike waopolewa
Mwili wa mtoto wa kike waopolewa wakati zoezi la kukinasua kivuko cha MV.Nyerere likiendelea katika eneo la Bwisya Ukara, nakufanya idadi ya waliopoteza maisha kufikia 229.
1212hrs:
Hatimaye kivuko cha Mv Nyerere kilichopinduka Septemba 20 kimenyanyuliwa
Wakazi wa Ukerewe wakiwa mita chache kutoka kivuko kilipozama
====
Taarifa Kwa Umma Kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme-TEMESA Kuhusu Kuzama Kwa Kivuko Cha MV.Nyerere
Kivuko cha MV Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Bugorara na kisiwa cha Ukala katika ziwa Victoria kimezama huku taarifa za idadi ya watu waliokuwemo ndani ya kivuko hazijajulikana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jonathan Shana amesema kivuko hicho kimezama wakati kikielekea katika Kisiwa cha Ukara. Kiliondoka saa 6 mchana na ilipofika saa nane kamili mchana kilipinduka.
Amesema bado hawajapata idadi kamili ya waliokuwemo kwenye kivuko hicho.
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), Hassan Karonda amekiri kuzama kwa kivuko hicho na yuko njiani kulekea huko na watatoa taarifa baadaye.
Kivuko cha MV. NYERERE kilinunuliwa na kuanza kutoa huduma mwaka 2004. Kilifungwa injini mbili mpya zenye thamani ya shilingi milioni 191 JULY 2018. Kivuko cha MV. Nyerere kina uwezo wa kubeba tani 25 sawa na abiria 100 na magari 3 kwa wakati mmoja.
UPDATES: 1900HRS
=> Watu watano wamekufa na wengine 32 wameokolewa mpaka sasa ila hali zao ni mbaya kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere.
=> "Mtu Hajalipwa Mshahara Halafu Anasikia Trilion 1 Imepotea Inauma" -Joseph Mkundi
Mbunge Joseph Mkundi akitahadharisha kuhusu kivuko cha MV Nyerere Apr 24, 2018
Alikuwa akichangia hoja ya bajeti ya Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano iliyopo chini ya Waziri wake, Profesa Makame Mbarawa.
UPDATES:
Rais Magufuli atuma salamu za Rambirambi
"Nimeshtushwa na kusikitishwa sana na ajali ya MV Nyerere, nawapa pole wote waliopoteza jamaa zao na nawaombea wote walionusurika kupona haraka, kwa wakati huu nawaomba tutulie wakati juhudi za uokoaji zinaendelea"
"Nimeshtushwa na kusikitishwa sana na ajali ya MV Nyerere, nawapa pole wote waliopoteza jamaa zao na nawaombea wote walionusurika kupona haraka, kwa wakati huu nawaomba tutulie wakati juhudi za uokoaji zinaendelea"
AJALI YA KIVUKO CHA MV NYERERE: WATU 44 WAMEFARIKI, ZOEZI LA UOKOAJI LASITISHWA HADI KESHO
Mbali na idadi hiyo ya waliofariki, Watu 37 wameokolewa katika ajali huku hali zao zikiwa mbaya
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amesema zoezi la uokoaji limesitishwa kutokana na giza kuingia
10:40 - MIILI 86 IMESHAOPOLEWA MPAKA SASA
Idadi ya vifo katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere, Mwanza imefika watu 86 huku uokoaji ukiendelea, RC John Mongella amethibitisha
11:41 - IDADI YA WALIOOPOLEWA YAFIKA 94
Idadi ya vifo katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere, Mwanza imefika watu 94 huku uokoaji ukiendelea, RC John Mongella amethibitisha
11: 43 Chanzo cha kuzama kwa mujibu wa DC wa Ukerewe
DC Ukerewe amesema kivuko kilikuwa kimebeba zaidi ya abiria 400, kilivyokaribia kufika mwaloni(kutia nanga) nahodha akapunguza spidi hivyo abiria wakakimbilia upande wa kushukia ili wawahi kutoka, kivuko kikazidiwa uzito na kupinduka.
12:40 - MIILI ILIYOOPOLEWA YAFIKA 100
Miili ya waliokufa na kuopolewa mpaka sasa yafika 100.
12:49 - IGP SIRRO: UTAMBUZI WA MAREHEMU UNAENDELEA
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simoni Sirro amesema utambuzi wa marehemu katika ajali ya MV Nyerere mkoani Mwanza unaendelea kwa miili iliyoopolewa.
Litafunguliwa Jalada maalum la kuchunguza tukio la kuzama kwa kivuko cha MV. Nyerere
13:03 - Idadi ya miili iliyoopolewa yafika 125
Idadi ya miili iliyoopolewa kwenye kivuko cha Mv Nyerere imefikia 125 mpaka sasa
13:20 - WAZIRI ISACK KAMWELWE: ZOEZI LA KUOPOA MIILI ILIYOKWAMA LITAKAMILIKA SAA 12 JIONI LEO
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema shughuli ya uokoaji wa watu walionasa kwenye kivuko cha MV Nyerere inatarajiwa kukamilika leo saa 12 jioni
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema mazishi ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya Mv.Nyerere iliyotokea Septamba 20 huko kisiwani Ukara, Ukerewe mkoani Mwanza yatakuwa ya kitaifa ambapo viongozi wakuu wa kitaifa wanatarajia kushiriki mazishi hayo.
17:21 - MIILI ILIYOOPOLEWA YAFIKA 126
Waliofariki dunia ajali ya kivuko wafikia 126, miili 36 imeshatambuliwa na ndugu zao
17:46 - MIILI ILIYOOPOLEWA YAFIKA 131
Kwa mujibu wa Waziri wa Uchukuzi Mhandisi Isack Kamwelwe idadi rasmi ya vifo mpaka jioni hii kutokana na ajali ya MV Nyerere ni watu 131.
18:10 - IDADI YAFIKA 136
Afisa mkuu wa Polisi Tanzania, Simon Sirro anasema kuwa idadi ya watu waliofariki kutokana na mkasa huo imefikia 136
18:15 - TAMKO LA SERIKALI (Katibu Mkuu Kiongozi)
Rais Magufuli ameagiza kuwa kufuatia ajali ya MV Nyerere Bendera ya Taifa itapepea nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia kesho Septemba 22, 2018.
Rais Magufuli ameagiza viongozi wa taasisi na mamlaka zinazosimamia usafiri wa majini wahojiwe na watakaobainika kuhusika kwa uzembe wachukuliwe hatua kali.
18:30 - Waziri Mkuu Majaliwa, CDF Mabeyo wawasili Ukerewe
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na CDF Mabeyo wamewasili Ukerewe na wamepokelewa na RC Mongella na IGP Sirro.
20:00 - NAHODHA WA KIVUKO ANASHIKILIWA KWA UCHUNGUZI
Nahodha wa MV Nyerere anashikiliwa na vyombo vya ulinzi kwa kosa la kumuachia mtu asiye na uwezo(Deiwaka) kuendesha kivuko na yeye kutosafiri.
Taarifa ya Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza siku 4 za maombolezo kuanzia leo tarehe 21 Septemba, 2018 kufuatia ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere katika ziwa Victoria na kusababisha vifo vya watu 131 waliothibitika mpaka sasa.
Kivuko hicho kilipinduka na kisha kuzama majini jana mchana meta chache kabla ya kufika katika kisiwa cha Ukara kikitokea kisiwa cha Bugolora ambapo mpaka sasa watu 40 wameokolewa wakiwa hai, miili 131 imeopolewa na zoezi la uokoaji linaendelea.
Pamoja na kutangaza siku 4 za maombolezo Mhe. Rais Magufuli amewapa pole wote waliopoteza jamaa zao katika ajali hiyo, amewaombea majeruhi wapone haraka na amewapongeza viongozi wa Mkoa wa Mwanza, vyombo vya ulinzi na usalama na wananchi wote wanaoendelea kushiriki katika uokoaji.
“Kwa masikitiko makubwa nawapa pole wote waliopoteza jamaa zao katika ajali hii, huu ni msiba mkubwa uliolikumba Taifa letu, nawaomba Watanzania wote kwa wakati huu ambapo vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na wananchi wanaendelea na uokoaji tuwe watulivu na tuendelee na kushikamana kama ilivyo desturi yetu, huu sio wakati wa kulumbana na kukatishana tamaa” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewataka Watanzania kuwapuuza wanaotaka kutumia ajali hii kujipatia umaarufu wa kisiasa, na amebainisha kuwa ni vema Watanzania wote tuungane kuwaombea Marehemu wapumzike mahali pema, majeruhi wapone haraka na kuwatia moyo wote wanaoendelea na zoezi la uokoaji.
Mhe. Rais Magufuli amemtuma Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kwenda eneo la tukio, ameagiza kuundwa tume ya uchunguzi wa chanzo cha ajali hii na ameagiza wote waliohusika kusababisha ajali hii wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
“Taarifa za awali zimeonesha dhahiri kuwa kivuko cha MV Nyerere kilikuwa na idadi kubwa ya watu na mizigo kupita uwezo wake, kama kuna mtu yeyote mwenye ushahidi wa chanzo chochote cha ajali hii, tunatarajia kuwa ataupeleka mahakamani” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
21 Septemba, 2018
UPDATES: 22 SEP 2018
0845hrs: Miili 15 yaopolewa
Miili mingine 15 imeepolewa leo asubuhi na kufanya idadi ya vifo katika ajali ya MV. Nyerere kufika 151.
0820HRS: Nahodha na Mkuu wa Kivuko cha MV Nyerere ni miongoni mwa watu waliofariki
Nahodha na Mkuu wa Kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi kikiwa safarini kutoka kisiwa cha Bugorora kwenda Ukara wilayani Ukerewe, Mwanza, ni miongoni mwa watu waliofariki dunia katika ajali hiyo.
1100hrs: Idadi ya miili iliyoopolewa yaongezeka
Idadi ya watu waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi mchana Septemba 20, 2018 imefikia 157 huku uokoaji ukiendelea.
1115hrs: MHANDISI WA KIVUKO APATIKANA AKIWA HAI
Mhandishi wa kivuko #MVNyerere, Alphonce Charahani ameokolewa akiwa hai siku 2 baada ya kivuko kuzama, amekutwa akiwa amejipaka oili mwilini. Sasa majeruhi wafikia idadi ya 41.
1117hrs: Serikali kugharamia kusafirisha maiti hadi hospitali ili zitambuliwe na kutoa TSH 500,000 kwa kila familia iliyofiwa
11:26 - Mbunge wa Ukerewe: CHANGAMOTO NILIZOWASILISHA BUNGENI ZILITATULIWA
Mbunge wa ukerewe amesema changamoto za kivuko alizowasilisha bunge zilitatuliwa miezi miwili iliyopita, kilikuwa sawa na kilikuwa mbioni kubadilishiwa ratiba ikiwemo kuongeza idadi ya safari ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa eneo hilo.
12:00 - MIILI 163 IMEOPOLEWA
Idadi ya watu waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha Nyerere imefikia 163 baada ya miili mingine 27 kuopolewa leo.
12:16 - WAZIRI UMMY MWALIMU: TUACHE KUSAMBAZA PICHA ZA MAREHEMU
"Ndugu zangu Watanzania, ninawaomba sana TUACHE KUSAMBAZA NA KUPOSTI PICHA ZA MAREHEMU WA AJALI YA MV NYERERE. Tuheshimu Utu na Ubinadamu wao"
12:19 - MIILI 116 YA WALIOFARIKI YATAMBULIWA
1250hrs: Wananchiwa Ukerewe wakosa Usafiri wa kwenda Ukara
Zaidi ya wananchi 500 wamekwama katika eneo la Bugolora baada ya kukosa usafiri wa kuelekea kisiwa cha Ukara kulikotokea ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere juzi Septemba 20, 2018.
1330hrs: Idadi ya waliopoteza maisha yaongezeka.
Miili mingine 33 imeepolewa na kufanya idadi ya vifo katikia ajali ya kivuko cha MV Nyerere kufika 196. Uokoaji unaendelea.
1600hrs: Meli yenye Vifaa Maalum yaelekea kwenye tukio
Meli ya MV Nyehunge kutoka Mwanza inaelekea kisiwa cha Ukara ikiwa na vifaa maalum vitakavyotumika kukinyanyua kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi.
17:30 - Miili iliyoopolewa yafika 209
Kwa mujibu wa Msemaji wa Serikali, Idadi ya miili iliyoopolewa katika ajali ya Kivuko cha MV Nyerere mpaka sasa imefikia 209. Katika idadi hiyo miili iliyotambuliwa na ndugu na jamaa ni 172
17:45 - SERIKALI YATANGAZA KAMATA KAMATA YA WANAOTOA TAKWIMU ZA UONGO
Kupitia Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola imesema kuwa itatumia #SheriaYaTakwimu kuwakamata na kuwafikisha Mahakamani wote watakao fanya kosa hilo
20:25 - Miili iliyoopolewa yafika 218
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amesema miili 218 imeopolewa katika ajali ya MV Nyerere huku 171 kati ya hiyo ikitambuliwa. Kazi ya uopoaji itaendelea kesho
UPDATES: 23 SEP 2018
0800hrs: Siku ya tatu baada ya ajali, Miili mingine yapatikana.
Miili mingine 7 imeepolewa leo asubuhi na kufanya idadi ya vifo katikia ajali ya kivuko cha MV Nyerere kufikia 224, RC wa Mwanza
1220hrs: Ibada ya mazishi ya marehemu ambao hawajatambuliwa na wale waliombwa na ndugu kuzikwa na Serikali
Miili 9 imewasili katika makaburi ya viwanja vya shule ya sekondari Bwisya kwaajili ya maziko ya Kitaifa yatakayoongozwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, makaburi zaidi ya 80 yamechimbwa kwa sababu mpaka sasa kuna miili ambayo inaibuka kutoka majini.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Isaac Kamwele anasema; Waliofariki 223 wanawake 126, wanaume 71 watoto wa kike 17,watoto wa kiume 10.
4 Hawajatambuliwa. Wamachukuliwa DNA. Watano waliotambuliwa watazikwa na ndugu hapa. Jumla watazikwa tisa.
Wananchi wa Ukara waliokoa 40 wakiwa hai. Kivuko kilibeba watu 265,uwezo wake ni kubeba abiria 101.
Milioni 190 zimechangwa na wananchi
Serikali imeweka utaratibu mzuri wa kujenga mialo na kununua vivuko vilivyo salama
1320hrs: Waziri Mkuu Majaliwa anasema;
Rais Magufuli amepokea habari ya ajali hii kwa mshituko.
Ajali ya kivuko hiki imesababishwa na kivuko kubeba abiria wengi na mizigo mingi.
Taarifa za awali zinaonyesha abiria zaidi ya 260 walikuwa ndani ya kivuko hiki.
219 imetambuliwa na miili 214 imetambuliwa na kuchukuliwa na ndugu. Minne tutaizika hapa ikiwemo mitano iliyotambuliwa ila ndugu wameamuwa wazikwe hapa.
Serikali itachukua hatua ya kuunda tume ya wachunguzi wakiwemo wataalam ili kubaini chanzo na wote waliohusika watachukuliwa hatua.
Meli ya MV Nyahunge imeletwa kuendelea kutoa huduma.
Tayari tumewakamata maafisa wote walikuwa wanahusika na usalama wa majini.
Kuanzia tarehe 21-24 imetangazwa kama siku ya maombolezo na bendeza zitapepea nusu mlingoti.
Tumefungua account ya MV Nyerere namba 3111005726. Itakumika kujenga wigo na mnara wenye majina ya wote waliofariki.
Tutaivuta meli kuileta mwaloni. Tutaendelea na mazishi pale tutakapopata mwili mwingine, nami ntaendelea kubaki Ukara kusimamia zoezi hili.
Kwa niaba ya rais natoa pongezo kwa John Mongera Mkuu wa mkoa wa Mwanza kwa jinsi mlivyoshughulikia kazi hii. Kamwele, Muhagama nawashukuru kwa uratibu. Namshukuru Kigoma Malima, Venance Mabeyo, Vikosi vya uokoaji JWTZ na Zanzibar, Jeshi la wanamaji, Msalaba mwekundu, Jeshi la akiba la Mgambo na wananchi wa kisiwa cha Ukara. Tunashukuru Madaktari wauguzi na manesi, nashukuru Vyombo vya habari. Nawashukuru Viongozi wa dini. Tunawashukuru Wasanii kwa kutunga nyimbo za kufariji na kuwatuliza watanzania. Nawashukuru Viongozi wa Nchi mbalimbali kwa kutufikishia salamu za pole. Nawashukuru wote kwa niaba ya mheshimiwa rais.
Katika kuimalisha usafiri majini, Serikali imeendelea kuongeza vyombo. Ziwa Victoria serikali imeanza kujenga meli ya kwenda Kagera, na Vivuko vipya vya Ukara na Bugolora.
Serikali itaendelea kuimalisha usafiri mwingine sehemu nyingine.
Taifa lipata msiba mkubwa sana, wito wetu ni tushikamane. Ni majonzi makubwa sana,wafiwa wanahitaji faraja. Tujipe moyo kiwa ni mapenzi ya Mungu.
Tuendelee kumuomba mwenyezi Mungu aendelea kuwaponya majeruhi wote na awalaze marehemu wote mahali pema peponi Amina.
1344hrs: Namba ya Michango yatangazwa
Jenista Muhagama anatangaza namba ya tigo pesa ya kutoa mchango. Namba imesajiliwa kwa jina la RAS Mwanza. 0677030000
1347hrs: Inaendelea dua ya kuwaombea waliotangulia mbele ya haki
1400hrs: Majeneza yanaanza kuingizwa kwenye Makaburi. Haya ni mazishi ya pamoja ya miili 9, shughuli hii inaongozwa na Waziri Mkuu Majaliwa.
10:00 (24/09/2018) - Mwili mmoja wa mtoto umeopolewa na kufanya idadi kufikia 225
Mwili mmoja umeopolewa leo katika Ziwa Victoria na kufanya idadi ya waliokufa kwenye ajali ya MV Nyerere kufikia 225
10:54 (24/09/2018) - Miili miwili yaonekana ikiwa inaelea
Waziri wa Ujenzi Mhandisi Isack Kamwelwe amesema kuna miili mingine miwili imeonekana muda huu ikielea juu ya maji
10:40 (25/09/2018) - Mwili mmoja wa mtoto umeopolewa na kufanya idadi kufikia 227
Mwili wa mtoto mmoja umeopolewa leo katika Ziwa Victoria na idadi ya waliokufa kwenye ajali ya MV Nyerere kufikia 227
10:30 (26/09/2018) - Mwili mwingine umeopolewa eneo la ajali
Mwili mwingine umeopolewa asubuhi hii kwenye eneo palipotokea ajali na kufanya jumla ya miili 228 mpaka sasa.
1212hrs (27/092018) - Mwili wa mtoto wa kike waopolewa
Mwili wa mtoto wa kike waopolewa wakati zoezi la kukinasua kivuko cha MV.Nyerere likiendelea katika eneo la Bwisya Ukara, nakufanya idadi ya waliopoteza maisha kufikia 229.
1212hrs:
Hatimaye kivuko cha Mv Nyerere kilichopinduka Septemba 20 kimenyanyuliwa