mangikule
JF-Expert Member
- Jun 11, 2012
- 6,464
- 6,011
Sasa wewe ndugu nini unachopinga au kuunga mkono!! Je unaunga mkono kila DINI itangaze malalamiko yake kupitia Vyombo vyake vya habari? Ndugu yangu umetoa mifano yote hiyo kwamba kulikuwa hakuna "upanga"Usipotoshe ukweli kwa dai lako la uongo kuwa Uislamu ulienezwa kwa upanga! haya nakuuliza, Uislamu ulipoingia huku kwetu miaka 1000 kabla ya ukristo kuja ni upanga gani huo uliotumika mpaka babu zetu wakasilimu?
Maeneo ya Machame, Usangi, Ugweno, Moshi mjini, Bukoba, Musoma nk, kuna Waislamu pia sasa upanga uliotumika kuwasilimisha umeuhifadhi ktk MUSEUM yako?
2) Indonesia ni nchi yenye idadi kubwa sana ya Waislamu duniani kote, sasa uislamu ulipoingia huko ni upanga upi huo uliotumika?
India, Pakistani, Afganistani, Kosovo, Bosnia, mackedonia, Uzbekistan, Urusi, Chechenia, USA na nchi nyingi duniani wanakoishi waislamu ni upanga gani huo uliotumika?
Labda Ukristo ndio ulioenezwa kwa mtutu wa bunduki ndio maana Wazee wetu akina KINJEKITILE walikataa kudanganywa na Wazungu waliokuja kama Wamisionari kumbe lengo lau ni kuwabatiza na kuwatala!
Usituletee propaganda chafu zilizopitwa na wakati tafuta lingine la kuongea lakini sio *****!
je tuelewe hawa kila kukicha waliopo kwenye mihadhara wakati mwingine wakitumia vitabu vitakatifu hata Biblia kutoa tafsiri wanazotaka wao(Yesu kristo si mungu wala mwana wa mungu) je hii ni haki? Sasa wewe unataka na wengine watumie vitabu Quran kuvichambua na kutoa tafsiri inayowafaa? Je tutafika? Je ni jamii gani tunayotaka kutengeneza kwa kueneza chuki za aina hii?
Wamisionari walijenga hayo mahospitali, mashule yanayohudumia jamii yote ya kitanzania je si haki hata serikali kupeleka wataalamu kutoa huduma? Kipi chema kwako na wanaredio Imani kuwanyang'anya makanisa hizo taasisi za huduma na kuziendesha wenyewe yaani serikali? Mbona walitaifisha wakashindwa kuziendesha?
Wewe na wanaredio imani ni nini hasa mnataka!?
Ndugu zangu kuidai serikali kutimiza wajibu wake wa kutoa haki kwa wanajamii wa usawa huanzii kwa kushambulia unaodai wamekupunja haki utapoteza pointi! Anzia na kuidai Serikali yako na ikiwezekana unganisha nguvu na wanaharakati wengine ili ushinde. Unawaowashambulia unatengeneza wapinzani watakaokuangusha katika madai yako!
Mifano: Serikali iliponyang'anya taasisi za huduma za makanisa yaliungana yote TEC, CCT etc na kuunda muungano wao uliowawezesha kurejesha baadhi ya Taasisi zao. Na hawakupiga kelele na kusema Rais Mwinyi wakati ule aliwapendelea waislamu.!! walikaa pamoja wakaweka mikakati ya nguvu ya hoja hadi hiyo MOU mnayoipinga ikawekwa!! na niwaeleze vipengele vya hiyo MOU ni kwa "serikali haitatafisha tena hizo taasisi, kwamba serikali itachangia uendeshaji wa taasisi hizo kwa manufaa ya kutoa huduma kwa watu wote mf waganga wa Bugando/KCMC wapo wengi wanaolipwa na Serikali!! "seminari" viwanda vya kufyatua mapadre/wachungaji hayapati hata senti tano ya serikali. TEC, CCT, etc havina hata senti tano ya serikali!! lakini wenzetu BAKWATA iliundwa na serikali na inaendeshwa na serikali na sasa mahakama ya kadhi yaja!!
Kuna shida gani hapa?