Kwa taarifa RADIO IMAAN inasikika nchi nzima kwa sasa, hivyo inawasikilizaji wengi. Pia wewe u-mtu wa ajabu, maaskofu wakisema, wakitukanä wakichochea ni sawa LAKINI MASHEHE WAKISEMA NI KOSA. Nami nasema maaskofu mnatupeleka kubaya. Msichanganye siasa na dini.
Mdau, binafsi nakupongeza kwa kuliona hilo na kuona kwamba ipo haja ya kutoa angalizo kwa kile ulichokisikia kupitia redio hiyo inayomilikiwa na taasisi ya dini ya Kiislam.
Kwangu mimi, cha msingi ninachokiona kwenye mada yako ni kuhusu uchochezi wa kidini unaofanywa na Redio hiyo na maafa yanayoweza kulikumba taifa letu kama hatua za haraka hazitachuliwa kudhibiti hali hiyo. Mimi binafsi sina tatizo na hoja yako. Kimsingi ni angalizo linalopaswa kuungwa mkono na kila mpenda amani. Hata hviyo, ninachotaka kuongeza hapa ni kwamba, hali ya mustakabali wa kidini katika Tanzania kwa sasa ni tete. Na hili halina ubishi hata kidogo, labda iwe kwa mtu mwenye hulka ya kubishia kila jambo ndiye pekee anayeweza kupingana na ukweli huu.
Hali tuliyo nayo sasa hapa nchini haishirii dalili njema hata kidogo mbele ya safari. Zinahitajika hatua za maksudi kabisa katika kukabiliana na hali hii kabla bomu halijalipuka. Ni vema watanzania tukatambua kwamba machafuko yenye sura kama hizi za kidini mahali popote yalipopata kutokea duniani, hayakuja kama mvua au kwa bahati mbaya, la hasha!. Machafuko yalianza kama masihala kwa njia kama hizi hizi za chochoko, malumbano,na uchochezi wa chini kwa chni kama tunavyoanzashudia hapa kwetu Tanzania.
Binafsi sipendi kuhukumu kwamba ni dini gani hasa ndio inayoonesha dalili za kutaka kutupeleka kwenye machafuko ya kidini ambayo ni machafuko mabaya kupita machafuko mengine yoyote katika dunia hii. Nasita kufanya hivyo kwa sababu imani yangu inanizuia kukuhukumu na kusisitiza zaidi kuchunguza boriti ndani ya jicho langu kabla ya kutoa kibanzi katika mboni ya jicho la mwenzangu. Hata hivyo, natambua dhahiri shahri kwamba mustakabli wa hali ya kidini hapa nchini imekuwa tete tangu mchakato wa uchaguzi Mkuu wa mwaka jana. Hivyo basi, ni wajibu wa kila mtanzania mwenye dini na asiye na dini kuliona hilo na kuchukua hatua kwa nafasi yake ili kuzuia dalili mbaya zinajitokeza katika taifa letu.
Na mwisho ninapendekeza kwamba, kama ilivyo hitaji la watanzania kuwa na Katiba Mpya, basi halikadhilika iwe hivyo hivyo katika jambo la kidini. Sio vibaya tukawa na mjadala wa kitaifa kuhusu hatma ya mivutano ya kidini iliyoanza kujitokeza hapa nchini. Na kwa njia hiyo pekee ndipo tutaweza kutoa fursa kwa kila upande utoe dukuduku lake na kisha kufikia muafaka wa pamoja. Lakini, tukiendelea kupuuza, kukejeliana,kutukanana na kushutumiana bila kuchukua hatua zozote haitatusaidia. Tukumbuke kwamba panapofuka moshi lazima pana moto!!
Mungu ibariki Tanzania na watu wake!!!
Kwa mwislam ambaye amesoma na kuelewa sidhaani kama anaweza kukubaliana na huo mjadala, manake ni uongo mtupu na uchochezi.
Hata ukifuatilia wanachosema si kweli maana wao ndo wachawi wa maendeleo yao, fanya tu utafiti mdogo wa shule za sekondari za kiislam kuhusu maendeleo yao utahisi kichefuchefu, manake viongozi ambao hawana elimu dunia wanang'anga'nia kuzisimamia hatimaye kuzipeleka ambako siko.
Tuwaache Mashekh na Maaskofu waendelee, sisi wafuasi wao tupambane na nchi yetu, huwa sichangii kwenye haya yanaturudisha nyuma, watanzania tuna desturi ya kupendana sana with regardless ya dini zetu na makabila yetu.Wadau, jana katika kubadilisha station ya radio yangu nilikutana na mjadala uliokuwa ukiendeshwa redio imani, hii ni redio ya kiislamu iliyoko mjini Morogoro. Ingawa si kawaida yangu kuisikiliza lakini nilishawishika kuwasikiliza kutokana na uzito wa mambo yaliyokuwa yakijadiliwa.
Mjadala ulihusu tamko walilotoa kuhusu maaskofu, walivilaumu vyombo vya habari magazeti particularly mwananchi na magazeti mengine kama nipashe, Tz Daima etc kwamba yamepotosha tamko lao pamoja na kuwa waliwapa tamko hilo kimaandishi. Nilijiuliza inakuwaje magazeti yote yanakosea kitu kilekile.
Kilichonisikitisha katika mjadala huo ni uchochezi na upotoshaji wanaoueneza hawa masheikh kwa sababu wanazojua wao. Kwa mfano walisema nchi inaendeshwa kwa mfumo wa kikiristu toka enzi za Nyerere, moja ya madai yao ni kwamba waislaumu walikuwa wakifelishwa makusudi shuleni ili wasisome, bila shaka haya ni madai makubwa sana.
Mambo mengine ni kwamba ili kudhibitisha kwamba nchi inaendeshwa kikristo ni kwa nini wakristo wana university na hospitali nyingi kuliko serikali, madai mengine ni kwamba kwa nini hospitali za kikristo zilizotaifishwa na serikali zilirudishwa, bila shaka katika hili ni kwamba serikali ilishindwa kuziendesha, lakini kwa sababu wanazojua wao waliishia kulaumu mfumo wa utawala wa kikristo. Katika hili wao walikiri kwamba hakurudishiwa kitu kwa kuwa hawakunyanganywa kitu!
Baada ya kumaliza majadiliano waliruhusu wasikilizaji kutuma sms na kupiga simu studio, wengi wa wachangiaji waliwashukuru masheikh kwa hatua yao lakini pia kuna waliosema watajichukulia sheria mkononi ili kuwaadhibu waandishi, na wengine walitaka itangazwe jihad dhidi yao.
Nilivyoona mimi hakuna shabaha nyingine zaidi ya kuleta chuki miongoni mwa dini jambo ambalo si kawaida yetu watz.
Ingawa najua kwamba redio hii haina wasikilizaji wengi lakini mijadala ya uchochezi namna ile haitakiwi kupita bila kukemewa. Katika mauaji ya Rwanda redio zilitumika sana kuchochea chuki baina ya watu, hatutakiwi kufika huko, nadhani ni wakati muafaka kwa intelijensia ya polisi kufanya kazi sasa ili kuzuia maafa yanayoweza kutokana na uchochezi wa redio imani
Wana JF naomba kuwakilisha
Wadau, jana katika kubadilisha station ya radio yangu nilikutana na mjadala uliokuwa ukiendeshwa redio imani, hii ni redio ya kiislamu iliyoko mjini Morogoro. Ingawa si kawaida yangu kuisikiliza lakini nilishawishika kuwasikiliza kutokana na uzito wa mambo yaliyokuwa yakijadiliwa.
Mjadala ulihusu tamko walilotoa kuhusu maaskofu, walivilaumu vyombo vya habari – magazeti particularly mwananchi na magazeti mengine kama nipashe, Tz Daima etc kwamba yamepotosha tamko lao pamoja na kuwa waliwapa tamko hilo kimaandishi. Nilijiuliza inakuwaje magazeti yote yanakosea kitu kilekile.
Kilichonisikitisha katika mjadala huo ni uchochezi na upotoshaji wanaoueneza hawa masheikh kwa sababu wanazojua wao. Kwa mfano walisema nchi inaendeshwa kwa mfumo wa kikiristu toka enzi za Nyerere, moja ya madai yao ni kwamba waislaumu walikuwa wakifelishwa makusudi shuleni ili wasisome, bila shaka haya ni madai makubwa sana.
Mambo mengine ni kwamba ili kudhibitisha kwamba nchi inaendeshwa kikristo ni kwa nini wakristo wana university na hospitali nyingi kuliko serikali, madai mengine ni kwamba kwa nini hospitali za kikristo zilizotaifishwa na serikali zilirudishwa, bila shaka katika hili ni kwamba serikali ilishindwa kuziendesha, lakini kwa sababu wanazojua wao waliishia kulaumu mfumo wa utawala wa kikristo. Katika hili wao walikiri kwamba hakurudishiwa kitu kwa kuwa hawakunyanganywa kitu!
Baada ya kumaliza majadiliano waliruhusu wasikilizaji kutuma sms na kupiga simu studio, wengi wa wachangiaji waliwashukuru masheikh kwa hatua yao lakini pia kuna waliosema watajichukulia sheria mkononi ili kuwaadhibu waandishi, na wengine walitaka itangazwe jihad dhidi yao.
Nilivyoona mimi hakuna shabaha nyingine zaidi ya kuleta chuki miongoni mwa dini jambo ambalo si kawaida yetu watz.
Ingawa najua kwamba redio hii haina wasikilizaji wengi lakini mijadala ya uchochezi namna ile haitakiwi kupita bila kukemewa. Katika mauaji ya Rwanda redio zilitumika sana kuchochea chuki baina ya watu, hatutakiwi kufika huko, nadhani ni wakati muafaka kwa "intelijensia" ya polisi kufanya kazi sasa ili kuzuia maafa yanayoweza kutokana na uchochezi wa redio imani
Wana JF naomba kuwakilisha
Kwa hiyo Uislam ulivyoingia Tanganyika na Zanzibar, kama sio East Africa uliingia kwa Upanga, kama unavyofikiria... Hivi unaijuwa historia ya nchi yako kweli.
Hivi Jihadi maana yake nini?
Kwanza nikushukuru kwa angalizo lako maana naona wewe ni mkereketwa wa amani ya nchi yetu, na pia unatambua mambo yatakapoharibika hakuna atakayesalimika eti kwa sababu ya dini yake. Lakini pia nikukumbushe tu sisi wakirsto huwa tunatafakali kwanza kabla ya kuanza kufanya jambo lolote, mifano ipo mingi na hata kama nitamua kuitaja hapa itakuwa ni upotoshaji wa mada. Kwa hiyo jambo la msingi ni kutafakali na kisha kuchukua hatua, ninamanisha nini kwa kusema hivyo, ni kwamba hayo yaliyosemwa katika redio imaan ni propaganda za watu ambao uelewa wao upo chini saana, na kwa sababu wameanzisha redio lakini bila kuwa na wataalam wenye uwezo wa kuwasaidia katika kuandaa mada ambazo ni za msingi na zenye kugusa maisha ya watu kama hizo basi ni jukumu lako wewe unayesikiliza kuona yote yaliyosemwa ni "off point" kisha achana nao. Katika utandawazi kama huu huwezi kufukili kuwa watu wataishia kuamini wanayoskia peke yake, lazima watajaribu kutafuta msaada na kupima waliyosikia na kisha kuchukua hatua. Tafadhali usikate tamaa kwani tayali ukweli unaujua
Maskini!!! Msiba mkubwa kabisa umeikabili nafsi yako na ubongo wako umedumaa!! (samahani lakini! nahisi unaishi dunia tofauti na hii na u mgeni kabisa!!) Sijui unaijua indonesia na malaysia ziko dunia gani au umeropokwa tu! je nako kuna mafuta kule? Hilo la Nigeria nadhani pia bado u ndotoni na si Nigeria pekee bali Afrika magharibi yote fuatilia upate majawabu halisi ili ububusa ukutoke. Wacha kutumia mdomo kufikiri tumia ubongo rafiki.
Maskini!!! Msiba mkubwa kabisa umeikabili nafsi yako na ubongo wako umedumaa!! (samahani lakini! nahisi unaishi dunia tofauti na hii na u mgeni kabisa!!) Sijui unaijua indonesia na malaysia ziko dunia gani au umeropokwa tu! je nako kuna mafuta kule? Hilo la Nigeria nadhani pia bado u ndotoni na si Nigeria pekee bali Afrika magharibi yote fuatilia upate majawabu halisi ili ububusa ukutoke. Wacha kutumia mdomo kufikiri tumia ubongo rafiki.
mimi naomba tume ya vyombo vya habari iifungie hii radio,leo nimeisikiliza ni hatari sana wanachochea chuki kwa maksudi na wanasema jihad ndo haki yao muuislam akifa akitetea uislam anaenda peponi,jamani serikali ipo wapi?