Tusio na kazi tukutane hapa

Tusio na kazi tukutane hapa

Hakuna kazi ngumu kukaa bila kazi aisee!! Hatari sana.

Kukipambazuka unaona afadhali ya jana!

Ukisikia kuku wanawika unaanza kuwaza utaanzia wapi na kuishia wapi?

Maswali yanakuwa mengi kuliko majibu

Yaani mtu hauna kazi haujaoa, kula kwako bado ni shida.

Katika hali kama hii kuoa kutakuwepo kweli!! uoe binti wa watu utakuja kumlisha nini!!!!

Tuko pamoja mkuu!
 
Nimejikuta nawaza tu, kwanini tusiwe na jukwaa la watu tusiokuwa na kazi rasmi za kufanya.

Wengine tumetumbuliwa hivi karibuni, wengine wamemaliza vyuo bado wanatafuta na wengine wana kazi lakini siyo ya maana ili mladi tuu siku ziende.

Hata mwenye job vacancies anaweza akatupata humu tukasaidiana maana hali hii siyo kabisa.

Vyuma vimekaza kila kona. Tujipigishe zetu story humu tujuzane ilikuwaje ukajikuta huna kazi.

Karibuni wadau.
Njoo PM nikupe dili la kupiga hela halali bila jasho jingi.
 
Back
Top Bottom