Kwani matatizo yake ni matatizo ya kidunia??
Acheni uzwazwa in Zitto'z voice.
Sent using
Jamii Forums mobile app
Ukitaka kujua umuhimu wa jambo, angalia wafuatiliaji.
Kwa mwaka mzima hardtalk ya TL ndiyo iliyovunja rekodi kwa kufuatiliwa na watu wengi Duniani. Mwendeshaji wa kipindi amekiri kuwa hardtalk yake na TL inaonekana ilifuatiliwa na watazamaji wengi sana.
Baada ya hapo, ni dhahiri stations nyingi Duniani zitataka na zitamwalika kuhojiana naye.
Alipopigwa risasi, ni Tindu Lisu kwa wiki mbili mfululizo ndiye aliyeongoza kwa kuandika na vyombo vingi vya habari kuliko binadamu yeyote.
Tunaweza kumtukana, tunaweza kumdharau, tunaweza kumdhihaki lakini ukweli ni kuwa jina la huyu mtu aitwaye TINDU LISU linazidi kupaa na kujulikana Dunia nzima.
Kuukata ukweli hakutabadili ukweli kuwa uwongo.
Mungu ana namna ya kumwinua kila mtu kwa namna yake, na wale wanaoinuka kwa kupitia magumu mengi ndio hupata umaarufu wa pekee.
Hayati Nelson Mandela hakupata umaarufu kwa sababu ya kuiongoza Afrika Kusini bali ni msimamo wake wa kukubali kukaa jela kuliko kuwa huru kwa kuwainamia wazungu. Tundu Lisu inaonekana amekubali yote, amejitoa kwa namna yoyote, ikiwa ni pamoja na kuyapokea mateso, kukosa hela ya matibabu, na huenda pengine atakubali kukosa ubunge, kuliko kumwinamia JPM ambaye wengi wanaamini ana uongozi wa mkono wa chuma. Leo Tundu Lisu hata akafutiwa ubunge, watu wakaambiwa wamchangie kumtegemeza, wapo wengi watakaomchangia, tena hiari yao ya moyo bila shuruti. Atachangiwa hata na wale wasuo nacho.
Yashikeni maneno yangu, 'katika vita hii, ni JPM atakayenyong'onyea, na siyo Tundu Lisu. Nafuu ya JPM itakuwa ni kukubali kuzidiwa kuliko kuamini atamshinda Tundu Lisu. Katika kushindana na TL, JPM atapoteza zaidi kuliko kupata'.
Sent using
Jamii Forums mobile app