Tundu Lissu na Kiinimacho cha Muungano

Sehemu ya Kwanza: Utangulizi

Mjadala wowote juu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwa kawaida unahitaji maandalizi makubwa na pia umakini wa hali ya juu, hasa iwapo unalenga hoja zenye kuuboresha kwa njia ya kuondokana na kero mbalimbali zilizopo, badala ya kuuvunja. Iwapo kuna masuala ambayo baadhi yenu mtadhania nimeyasahau au kuyaacha, ni kwa sababu ni vigumu sana kuja na mada kuhusu muungano ambayo inajitosheleza. Pamoja na hayo yote, kuna mengi nimeyaacha kwa makusudi lakini kwa lengo la kuyajadili zaidi baadae; Vinginevyo naomba mniwie radhi kwa mapungufu yoyote ambayo yatajitokeza.

Kupitia nafasi yake kama Msemaji Mkuu wa Upinzani Bungeni (Ofisi Ya Makamu Wa Rais – MUUNGANO), katika kikao cha Bajeti cha Mwaka wa Fedha, 2012-2013, Tundu Lissu (MB), aliwasilisha maoni kuhusu mtazamo na msimamo wa kambi hiyo juu ya Muungano Wetu. Kwa wale waliopata fursa ya kuisikiliza hotuba ya Lissu kwa makini, wengi watakubaliana na mimi kwamba hotuba yake ilijaa YALIO MEMA kuliko YASIYO MEMA, sio tu kwa Muungano wetu, bali pia kwa taifa letu. Vile vile, hotuba ya Lissu ina dhamira njema na yenye manufaa, sio tu kwa kizazi cha sasa, bali pia kizazi cha baadae. Lakini kama kawaida yetu, nchini Tanzania, "POLITICS HAS BECOME SURPEME TO EVERYTHING", kwani hoja ya Lissu imepotoshwa;

Kwanza: JE, Madhumuni ya Muungano Baina ya Tanganyika na Zanzibar, kwa Mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964, Yalikuwa Ni Yepi na ni Mfumo wa Serikali ngapi ndio uliokusudiwa chini ya Mkataba huu wa Mwaka 1964?

Pili: JE, Viongozi Wetu na Wananchi Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Leo hii, Wana Nia ile ile Adhimu na Malengo Yale Yale Yaliyowekwa katika Utangulizi wa Mkataba wa Muungano, 1964?

Tatu: Ifikapo Mwaka 2014, Muungano Wetu Utakuwa Umetimiza Miaka 50; By Coincidence, Kipindi hicho hicho pia Tunategemea Kupata Katiba Yetu Mpya; Swali linalofuata ni, JE: Katika Kipindi Hiki Cha Miaka 50 Ya Muungano, tutakuwa tumefikia wapi katika Kufanikisha Madhumuni Kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964?

Nne: Je, makosa ambayo yanapelekea muungano wetu kuyumba yalijitokeza wapi, na tuchukue hatua gani kurekebisha makosa haya, na kurudisha matakwa na dhamira iliyowekwa wazi kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964?


BILA TANGANYIKA, TANZANIA HAIWEZEKANI. MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE.

Nilipo RED

Waarabu tuna usemi unaonena. ''NI RAHISI SANA KUWADANGANYA WATU. LAKIN NI VIGUMU SANA KUWAAMBIA WATU KUWA WAMEDANGANYWA''

Na vile vile Mwimbaji mashuhuri wa Reggae Robbert Nesta Marley (mmarufu kama Bob Marley) kwenye wimbo wake wa "Redemption song" alisema YOU CAN FOOL SOME PEOPLE SOMETIMES BUT YOU CAN'T FOOL ALL THE PEOPLE ALL THE TIME"

Nikiwaambia waTanganyika Nyerere aliwadanganya sana na alisimamia kidete kuhakikisha HAMUWEZI KABISA KUUNDA Serikali ya TANGANYIKA pamoja na Znz kuwasaidia sana kuwaombea Serikali Hiyo katika mjadala wa kwanza kuhusu Muungano wenu.

tumeamua kuiga tabia ya "ujanja" wa mbuni wa kuzika kichwa mchangani, eti kukwepa janga. Labda tujikumbushe kidogo kwa hili.
Mdahalo wa kwanza juu ya mfumo na muundo wa Muungano ulianza kwa njia ya maoni juu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano mwaka 1983/84. Hapo, kwa mara ya kwanza ilibainika kuwa viongozi wa juu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, wakiongozwa na Rais Aboud Jumbe, na wale wa Serikali ya Tanzania, wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mwalimu Julius Nyerere, walikuwa na mitazamo tofauti inayokinzana juu ya Muungano.
Jumbe na timu yake walitaka Muungano uwe na Serikali tatu kwa maana ya Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar (iliyopo sasa) na Serikali ya Muungano yenye kushughulikia mambo ya Muungano tu, ambayo yameainishwa katika Ibara ya 6(a) ya Katiba ya Muungano (Articles of Union) na kifungu cha 8 cha Sheria ya Muungano (Acts of Union) Namba 22 ya 1964, na hatimaye ibara ya 4 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977.
Jumbe alikwenda mbali zaidi kwa kuandaa Hati ya Maombi ya kuhoji na kutaka ufafanuzi kwenye Mahakama Maalum ya Kikatiba juu ya muundo sahihi wa Muungano kwa kutumia ibara ya 125 ya Katiba.
Tofauti hizi kati yake na Mwalimu hazikwisha salama kwa Jumbe kuthubutu kukanyaga mahali "patakatifu" bila kuvua viatu. Jumbe alilazimishwa kuachia ngazi zote za uongozi wa nchi kuanzia Urais wa Zanzibar, Umakamu wa Rais wa Muungano, na nafasi zote za kichama Januari, 1984.

Utata mwingine huu uliibuka tena kwa nguvu mpya zaidi wakati Wabunge 55 (maarufu kama G55) wa Bunge la Muungano, walipowasilisha bungeni mwaka 1993, hoja ya kutaka kuundwa/kurejeshwa kwa Serikali ya Tanganyika kwa kukasirishwa na hatua ya Zanzibar kujiunga na OIC kama nchi huru nje ya Muungano, Desemba 1, 1992.
Ukweli, Bunge lilikuwa limekwisha kupitisha kwa kauli moja, Azimio la kuanzishwa kwa Serikali ya Tanganyika Agosti 24, 1993 kwa maana ya kuwa na Serikali ya Muungano inayoundwa na Serikali hai zenye Mamlaka huru, za Tanganyika na Zanzibar, kama vile tu alivyotaka Rais Jumbe mwaka 1983.
Hata hivyo, Azimio hilo lilipigwa rungu zito na Mwalimu Nyerere na likavunjika.. Na kama ilivyokuwa kwa Jumbe, hapa napo mambo hayakuisha salama; safari hii Waziri Mkuu wa wakati ule, John Malecela (hongera kwa kutimiza miaka 75) na Katibu Mkuu wa CCM, Horace Kolimba, walipoteza nyadhifa zao kwa sababu ya ama kunyamazia au kuunga mkono hoja / Azimio la G 55.


Kifupi naweza kusema mumeamua kuiga tabia ya "ujanja" wa mbuni wa kuzika kichwa mchangani, eti kukwepa janga.

Hongera sana Tundu Lissu kwani wewe ni miongoni mwa wale aliosema Bob Marley 'you can't fool all the people all the time"
 
EMT,

nashukuru kwa Hotuba hii ya Tundu Lissa, sasa nadhani tuna nyenzo zote muhimu za kutusaidia kubaini zaidi kiini macho hiki, lengo likiwa ni kuboresha muungano wetu, sio kuuvunja;

cc: jmushi1


Mkuu Salaam

1. Muungano wa Nyerere na Karume na serikali zao ni batili kwa wananchi kwa saa; ni sawa na mwaharamu aliyefanikishwa sana na kudhani hakuzaliwa nje ya ndoa halali.

2. Hotuba ya TAL kutokuwepo kwenye Hansard ni balaa lingine la kuvunja taratibu na katiba ya nchi. Kuna haja ya wahusika kuwajibishwa au kutueleza uma kilichojiri kinyume chake hansard si taarifa sahihi za Bunge.

3. Shida iko wapi ya kutafuta muungano wa udugu kwa matakwa ya ndugu si kwa kwa matakwa ya wachache? Kuna kitu kinafichwa kinachofanya baadhi yetu tuwe na kichefu chefu na muungano huu sawia na hoja za TAL bungeni

Nina mengi ya kujibu maswali yako manne, ila msingi wake sikubaliane nao unapotaka kudumumisha muungano usiotuhusu wananchi.

Msimamo wangu

1. Muungano wa viongozi na serikali uvunjwe kupitia taratibu za kibunge ili wananchi tupate fursa ya kuujadili kama tiunauhitaji na wa aina gani. Kwa kiwango cha kero cha sasa siuhitaji.

2. Ili mradi CCM ipo madarakani na wana maslahi kwenye muungano huu uliochakachuliwa, wajue kitendo hicho hakitadumisha muungano bali kinazaa maswali na mijadala kama unayoileta hapa. Ni matumaini yangu wananchi wataamua mustakabali wa CCM ili mambo mengi yarekebeki.

3. Kuna jitihada za kusuppress maoni/fikra za watu kuhusu suala la muungano, linakera kwa muda wa sasa tu lakini halitakera muda wote lina dalili ya kuisha vibaya; vyo vyote vile litaisha kwa maslahi ya Tanganyika na wananchi wa Zanzibar.
 
CUF wangekuwa na akili wangeiunga mkono CHADEMA maana ina msimamo sawa na wao kutaka zanzibar IWE HURU kwa kuwa na mfumo wa serikali tatu, lakini wanachokifanya sasa hivi kuipa nguvu CCM wakati wanajua CCM haina mpango wa kuiachia zanzibar huru wala wa kuiachia zanzibar kwa CUF kwa namna yoyote ile! Akina Jusa na Hamad ni wanafiki wa kutupwa. CUF Bara hawana sauti Lipumba ni Mwenyekiti wa CUF kivuli tu hana sauti juu CUF mpaka Hamadi Aseme.
 
Halafu mkuu mapinduzi ya Zanzibar si yalikuwa january 12 1964?I stand to be corrected.

Hata mimi nilidhania hivyo, ila nazidi kuaminishwa kwamba ni december 10th 1963,lakini nadhani hili lisitupotezee sana muda au unaonaje? suala la msingi ni kwamba znz ilikuwa nchi huru kwa miezi michache sana, since then imekuwa ni nchi inayopambana na Tanganyika kutafuta autonomy ambapo kidogo kidogo imekuwa inamegewa hilo;
 
Joka Kuu,

..Lakini ZNZ ina some autonomy at the fiscal level kwa maana ya kutoza kodi mbalimbali. kipo chombo kinaitwa Zanzibar Revenue board naomba uchunguze kina mamlaka gani huko ZNZ.

Ni kweli Zanzibar ina some sort of Fiscal autonomy lakini tukumbuke kwamba, suala hili limezidi kuwa hivyo baada ya mapambano ya muda mrefu ya watu wa Zanzibar kutaka kufanikisha hilo; Lakini nikuulize – pamoja na hayo yote, je huoni kwamba hata ule mjadala wako wa awali kuhusu uanzishwaji wa BOT na mchango wa Zanzibar katika hilo umejaa kiini macho kuliko kitu kinacho eleweka?

Mpaka leo hii, kuna mambo mengi sana ambayo Zanzibar cant finance mpaka Serikali ya Jamhuri ifanikishe. Kwa mtazamo wako, uhusiano baina ya uhalisia huu na fiscal autonomy ni nini?

..kuhusu mfumo wa serikali 3 baadhi yetu tulishaona tangu zamani kwamba mfumo huo hauwezi kukidhi matamanio waliyonayo kizazi cha sasa cha Wazanzibari.
..Mimi nadhani tuwasikilize wa-ZNZ wanataka nini sasa hivi. Kwa mtizamo wangu hawataki muungano. Hizi lugha za "muungano wa mkataba" may be they r just trying to be diplomatic.

Pamoja na kwamba sielewi kama unaongelea maoni ya Viongozi Wazanzibari au Wananchi, kama mtazamo huo upo basi nadhani ni kutokana na ukiukwaji wa Mkataba wa Muungano, 1964, ambapo mfumo wa serikali tatu wa envisaged, na Zanzibar waliutaka sana mfumo huu, lakini Katiba ya Muda ya 1965, na baadae katika ya kudumu ya JMT, 1977, ikawavunja moyo wazanzibari katika hilo; Lakini nina amini tukiamua kurejea kwenye mkataba wa muungano, 1964, tunaweza kutatua mgogoro huu na kurudi katika yale tuliyoamua yawe masuala ya muungano;

Lakini tunapozungumzia kizazi cha sasa Zanzibar, huoni kidogo huu ni ubinafsi? Kizazi cha baadae je, wao wangependelea nini? Assuming kwamba in the long term, Muungano is desirable ili mradi kila upande unaridhika na manufaa ya muungano – kisiasa na kiuchumi?

..zaidi, nadhani Tanganyika is too big kuwa na muungano na nchi ndogo kama Zanzibar bila kuwa na migogoro isiyokwisha.

Naomba nipingane na wewe katika hili. Ukubwa wa Tanganyika na udogo wa Zanzibar unapimwa na nini, land mass? Population? GDP? Ni vyema tupime ukubwa wa Zanzibar by Potential GDP, hasa iwapo watakuwa na full autonomy; Kwa mfano, Kuwait ni nchi ndogo sana hata kwa Tanganyika kwa vigezo vya land size na population, lakini kiuchumi, hawa sio wenzetu kabisa, na ningependa tutazame ukubwa wa Zanzibar kwa vigezo hivyo. Kwa mfano:

  • Total Land ya Tangnayika ni almost 50 times of Kuwait;
  • Population ya Tanganyika ni 10 times of Kuwait;
  • Lakini kiuchumi au GDP, Uchumi wa Kuwait ni over 7 times ya Tanganyika;

Naamini kwamba, given rasilimali walizonazo Zanzibar – utalii, mafuta na gesi, more autonomy to Zanzibar itapelekea taifa hili kuwa kubwa sana kiuchumi, pengine kufanana na Tanganyika kama sio kukaribiana na Tanganyika;
 
Mkuu Kobello,

Nachokizungumza mimi ni kile ambacho kiliafikiwa chini ya mkataba wa muungano, lakini kwa bahati mbaya, maafikiano yake yakakiukwa, na ndio maana leo hii tupo kwenye mgogoro;

Muungano ulilenga SHIRIKISHO – a federal republic, not a unitary system of government, kama mengine yalikuwa muhimu, ilikuwa ni suala la mazungumzo ya mbeleni, pengine hata vizazi vitakavyo ishi mwaka 3000; Lakini kwa sababu zisizo eleweka, mara baada tu ya Mkataba ule wa 1964 kusainiwa, mambo yalianza kuchukua sura tofauti kabisa.

wa mujibu wa mkataba wa muungano, 1964, iliwekwa bayana kwamba – kutakuwepo na mfumo wa serikali kuu na serikali shirikishi mbili – Tanganyika na Zanzibar, ndani ya muungano huu na serikali shirikishi hizi zitakuwa na nguvu sawa/zinazoendana kwa maana ya kwamba – mfumo wa shirikisho utakuwa na mgawanyo wa:


  • Mahakama;
  • Baraza la kutunga sheria; na
  • Urais baina na serikali kuu na serikali mbili, huku kila serikali ikiwa na nguvu kamili ndani ya mamlaka yake;
 
Nadhani umegundua kwamba hoja hii ni ngumu kuigeuza iendane na maslahi ya wanaowatuma kuja kufanya kazi humu JF;

Kuna hoja ipi hapo?

Ungeuliza kwanini Nyerere aliweka muungano usioeleweka, ningekuelewa.

Tanganyika iko wapi?
 
Hata mimi nilidhania hivyo, ila nazidi kuaminishwa kwamba ni december 10th 1963,lakini nadhani hili lisitupotezee sana muda au unaonaje? suala la msingi ni kwamba znz ilikuwa nchi huru kwa miezi michache sana, since then imekuwa ni nchi inayopambana na Tanganyika kutafuta autonomy ambapo kidogo kidogo imekuwa inamegewa hilo;
Ok mkuu,tuliache hili kwasasa,lakini kwa kuongezea tu hapo,ni kwamba uhuru haukuwa wa watu wa Zanzibar.Mwingereza alichofanya ni kuikabidhi Zanzibar mikononi mwa utawala wa Sultan hapo december 1963,na ndiyo maana kukafanyika mapinduzi hapo january 12 1964.
 
Kuna hoja ipi hapo?

Ungeuliza kwanini Nyerere aliweka muungano usioeleweka, ningekuelewa.

Tanganyika iko wapi?
Issue ya muungano ilikuwa ya Karume na Nyerere,kwahiyo unapojaribu kumbambikizia Nyerere lawama zinazokuwa derived from hatred,ndo hapo tunajiuliza uelewa wako kwenye issue hii.Matatizo hayakuwepo Tanganyika,matatizo yalikuwepo huko Zanzibar.Na bila kuungana na Tanganyika,basi mgeendelea kuchinjana vibaya sana na sidhani kama Zanzibar ingekuwa inatawalika hadi leo.Na wananchi wengi sana wangekuwa wamepoteza maisha yao bila sababu za msingi.Kwa jinsi situation ilivyokuwa,there was no way that Zanzibar ingekuwa taifa stable.Fuatilia vurugu zote za ZZP,ZNP,ASP na baadaye UMMA.Na uongozi aliokuwa akiusapoti mwingireza ni wa Sultan.Tanganyika was your rescue.Sasa hapa hata kama muungano haukuwa mzuri,haina maana kuwa matatizo yalikuwa ni ya Nyerere,matatizo yalikuwa ni ya wazanzibari wenyewe.Na sasa hivi binafsi ninaamini kuwa mmeshafikia hatua ya kuweza kuyatatua matatizo yenu nyie wenyewe.Ila kwamba mtafanikiwa,hilo bado ni debatable.Ninaamini muungano huu unahitaji marekebisho ama hata kuuvunjilia mbali ikiwezekana.
 
Kobello,

Unaweza kuwa na nchi mbili zilzoungana na zote zikawa na complete autonomy, mfano mzuri ni Inner Mongolia na China. Mfano ulioutumia wa US ni tofauti kidogo kwa sababu autonomy ya states za USA zipo highly debatable.Na Zanbzibar wana madaraka yote iliyonayo state yeyote ya Marekani. Zanzibar is a state within a State.
Ni kweli, autonomy marekani ipo highly debatable lakini mengi yanapotezewa na states husika kutokana na ukweli kwamba, kuwa a member state in the US kuna faida nyingi kuliko hasara; Ni faida za namna hii, iwapo ndugu zetu wanzazibari wangekuwa na wao wanazipata , mgogoro huu usingefikia hali ya leo;

Kuhusu serikali tatu, labda ungetuelezea kivipi? Yaani bunge gani litaamua hilo? Kama ni bunge la JMT, huoni kuwa huo ni ukiukwaji wa katiba? kuruhusu kuongezwa au kupunguzwa vipengele kama mh. Lissu alivyodai.
Kuhusu katiba ya sasa, tufahamu yafuatayo:

Kwanza, Kamati Maalum ya CCM ilichukua nafasi ya tume ya katiba; Pili, Kamati Maalum ya CCM ilichukua nafasi ya Baraza la kutunga Katiba, na hii ni kama ilivyotajwa ndani ya mkataba wa muungano, 1964, lakini kwa sababu zisizoeleweka, masharti haya yakachakachuliwa na sheria mpya iliyoitwa Sheria ya baraza la kutunga Katiba, 1965; kwa kifupi, misingi iliyowekwa ndani ya Mkataba wa Muungano 1964, mkataba ambao haukutaja neno "shughulii/maamuzi ya kisiasa", haikutaja "chama cha siasa", haikutaja "TANU", "ASP", wala "CCM", lakini bado CCM hijacked Mkataba wa Muungano, 1964 pamoja na yaliyomo, na badala ya baraza la kutunga katiba kupitisha katiba per Articles of the Union, 1964, Bunge la CCM likaipitisha katiba mpya ya 1977; Kabla sijajibu swali lako kuhusu bunge kukiuka katiba ya 1977, nikuulize kwanza, je:

Katiba unayoizungumzia hii ina uhalali gani iwapo tutakubaliana kwamba Mkataba wa Muungano, 1964, ulikuwa ndio sheria mama? Lipi ni tatizo kubwa hapa linalopelekea hali ya nchi yetu kuchafuka kutokana na mgogoro wa muungano – Ukiukwaji wa Katiba ya 1977 au Ukiukwaji wa Mkataba wa Muungano, 1964?

Umesisitiza sana suala la serikali tatu, lakini hebu tupe maelezo zaidi ni kivipi zitausaidia muungano kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Naomba nirekebisha kidogo sentensi yako; Ninacho sisitiza mimi ni kwamba, ili tuokoe muungano wetu, ni muhimu tukajerea kwenye Mkataba wa Muungano, 1964, na kuanza kushughulikia matatizo yote ya ukiukwaji wa Mkataba huu, na njia pekee ya kutatua hili ni kutumia mchakato wa sasa wa katiba mpya kwani ni ukweli ulio dhahiri kwamba mgogoro wa katiba ya 1977, is mainly The Zanzibar Question;

Baada ya kusema hayo, naomba sasa niingie katika majibu ya swali lako kuhusu faida za shirikisho la serikali tatu – kisiasa, kiuchumi na kijamii:

Kwanza tuangalie faida na hasara chini ya mfumo wa sasa wa muungano:

Faida ya kwanza ni mfanano/uniformity na vile vile consistency - kisera, na pia in terms of sheria, mfumo wa Utawala, mfumo wa siasa, enforcement ya masuala mbalimbali, throughout the country; hii inasaidia sana kupunguza duplications (na hapa ile hoja yako kwamba serikali tatu ni upotevu wa revenues inaingia…), na inasaidia kupunguza pia mikwaruzo inayoweza kujitokea baina ya serikali ya muungano na serikali shirikishi; Faida nyingine muhimu ni Umoja, Amani na Utulivu; Lakini tukumbuke kwamba the overriding reason to why kunakuwa na AMANI, UMOJA na UTULIVU ndani ya mfumo kama wetu wa sasa, ni pale tu iwapo pande zote mbili za muungano zitaridhika kwamba - kuna faida kuliko hasara za kuwa chini ya mfumo wa sasa;

Sasa tugeukie kwenye Hasara za Mfumo Wa Sasa:

Mfumo wa sasa una matatizo, ndio maana umetawaliwa na migogoro. Nitajaribu kujadili badhi ya hasara chini ya mfumo huu; Tatizo la kwanza, aidha kwa wananchi wa Tanzania kujua au kutokujua, kinachochangia tatizo la sasa la Serikali ya muungano kuwa ‘out of touch with locals concerns' – both za Zanzibar na Tanganyika, hata katika masuala yaliyokubaliwa yawe ya muungano, ni kutokana na mfumo wenyewe; Mfumo huu since its inception, umetawaliwa na Siasa kuliko matendo yanayolenga kubadilisha maisha ya wananchi; Kwa mfano, tunazidi kushuhudia jinsi gani serikali ya JMT ilivyokuwa ‘too slow' kutatua local problems – yani matatizo ya wananchi wa Tanganyika na yale ya wazanzibari;
In other words, chini ya mfumo wa sasa, Serikali ya Muungano wajibu wake ni kutatua matatizo ya wananchi wa Tanganyika [kwani Rais wa Tanganyika na serikali yake hayupo ili kutatua matatizo yasioyo kuwa ya muungano], na pia ni wajibu wa serikali ya JMT kutatua masuala ya muungano; Lakini pia tumeona kupitia historia ya muungano huu kwamba serikali hii ya JMT pai imekuwa mara nyingi inajihusisha na masuala yasio kuwa ya muungano bali ya Zanzibar kwa njia ya kunyakua nyakua masuala mbalimbali ya Zanzibar na kuyaongezea katika orodha ya masuala ya muungano;Kwa kweli mfumo huu una stretch sana serikali yetu na kwa mtazmo wangu, fedha za walipa kodi zinapotea zaidi chini ya mfumo huu ndugu Kobello contrary to your argument kwamba serikali tatu zitakuwa mzigo kifedha; naomba counter argument yako katika hili;

Hasara nyingine chini ya mfumo wa sasa ni kwamba - ni vigumu kutatua tatizo la umaskini kwa ufanisi; Serikali ya JMT, kama tulivyo ona, is too stretched, na ule usemi wa wahenga kwamba :Mshika Mengi, Moja humponyoka, ndio unaingia hapa; nadhani sijaweka usemi huu kama unavyotakiwa lakini muhimu zaidi ni kwamba, ujumbe umefika; Mfumo wa sasa unapelekea serikali ya JMT kuponyokwa na mengi muhimu in the context of kushughulikia kero za wananchi – Maendeleo ya jamii in particular; Na ndio maana pamoja na juhudi kubwa za Serikali ya JMT kujaribu kutatua local problems za Tanganyika na za Zanzibar, Serikali always imekuwa behind katika ku - meet needs za wananchi;

in my humble view, solution ni shirikisho, na ndio maana hata federation in the United States, na hata Russia kwa kiasi fulani, mambo yao yanakwenda vizuri, na member states na wananchi wao wanaona faida nyingi za kuwepo kwenye mfumo wa shirikisho kuliko hasara; hii inachangiwa sana na kila state kuwa na wigo mkubwa wa ‘autonomy', hasa katika suala muhimu linalogusa maisha ya watu – Fiscal Autonom au Fiscal Decentralization; Miaka ya nyuma, Marekani kidogo isambaratike kutokana na kukosekana kwa autonomy hii;

Sasa niingine katika faida za shirikisho chini ya mfumo wa serikali tatu katika nchi yetu:

Kwanza, serikali shirikishi zinapata nafasi nzuri zaidi to handle local problems, tofauti na mfumo wa sasa ambapo mahitaji ya wananchi wa Tanganyika na yale yaliyopo chini ya Muungano, yote yanasimamiwa na serikali moja; In the process, hakuna lolote la maana linalofanyika katika kuwaletea wananchi Maendeleo ya maana kwani kuna so much leakages than injections in the fiscal system, na hii ni kutokana na fedha nyingi kwenda kufanya shughuli za kisiasa ili kulinda maslahi yatokanayo na muungano;

Faida ya pili, serikali shirikishi na maafisa wake wanakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ku- respond to the people who elect them, kuliko katika mazingira ya sasa ambapo kuna mkanganyiko baina ya bunge la JMT na baraza la wawakilishi, huku wajumbe wa Baraza la wawakilishi majukumu yao yakiwa wazi kwamba ni kwa ajili ya wananchi wa Zanzibar, huku wabunge wa JMT, wao wakitegemewa wawakilishe maslahi yote, ya Tanganyika na ya Muungano;

Faida nyingine pia ni kwamba – serikali kuu au serikali ya muungano inakuwa na muda mzuri zaidi kujikita katika masuala ya kitaifa /muungano na pia masuala ya kimataifa tofauti na sasa ambapo kwa mfano Rais Kikwete huyo huyo analaumiwa kwa matatizo ya Tanganyika ambayo inaitwa Tanzania Bara, huyo huyo analaumiwa kwa matatizo kuhusu masuala yaliyopo kwenye orodha ya muungano; Kwa mtazamo wako, unaona ni sahihi kweli kwa Rais wa Tanganyika kuwa pia Rais wa JMT? Inawezekana, lakini maelezo yake yatakuwa yamejaa kiini macho kuliko uelewa;

Vinginevyo, huu ni mzigo mkubwa sana kwa Rais, lakini anaweza kupunguziwa lawama hizi chini ya mfumo wa serikali tatu – shirikisho;
 
Kuna hoja ipi hapo?

Ungeuliza kwanini Nyerere aliweka muungano usioeleweka, ningekuelewa.

Tanganyika iko wapi?

Basi kwanini usijenge hoja - kwamba Nyerere aliweka muungano usioeleweka ili kwa pamoja tujenge, hoping mwisho wa siku tutaboresha muungano wetu na sio kuuangamiza?; Inaonyesha kwamba haukusoma post yangu yote, vinginevyo hili la Nyerere nimelizungumzia, hivyo ni sehemu ya mjadala huu; karibu katika mjadala;
 
CUF wangekuwa na akili wangeiunga mkono CHADEMA maana ina msimamo sawa na wao kutaka zanzibar IWE HURU kwa kuwa na mfumo wa serikali tatu, lakini wanachokifanya sasa hivi kuipa nguvu CCM wakati wanajua CCM haina mpango wa kuiachia zanzibar huru wala wa kuiachia zanzibar kwa CUF kwa namna yoyote ile! Akina Jusa na Hamad ni wanafiki wa kutupwa. CUF Bara hawana sauti Lipumba ni Mwenyekiti wa CUF kivuli tu hana sauti juu CUF mpaka Hamadi Aseme.

Usisahau kwamba Chadema ni Chama Cha Tanganyika, na kina shughulika na zanzibar only because ya matakwa ya Tendwa chini ya sheria ya vyama vya siasa; Hata CCM kule zanzibar ujue ipo kimkataba kupitia ndoa yake na ASP, vinginevyo TANU, kama ilivyokuwa Chadema, ni vyama vya Tanganyika; Kwa mtazamo wangu, the only way forward for Chadema kuwa na mashiko zanzibar ni kutafuta ndoa kama ya TANU na ASP kupitia chama kinginekule; Vinginevyo usisahau pia kwamba kama inavyobakia kuwa ukweli kwamba TANU ilikufa lakini elements zake baar bado zipo, basi vile vile ASP ilikufa lakini elements zake pia bado zipo Zanzibar;
 
Mkuu barubaru,

Umezungumza hoja za msingi sana, natumaini wenye uwezo wa kuelewa wataelewa; suala la serikali tatu limekuwa linapendekezwa na wazanzibari throughout, na hii ni kutokana na uwezo na umahiri wa viongozi wao katika kipindi chote, kuwaelimisha juu ya Muungano, hasa dhamira yake ilikuwa ni kitu gani per articles of the union za 1964. Kwa bahati mbaya sana, sisi ndugu zao upande wa bara tumekuwa tunaishi katika kiza kikubwa sana, na tunaanza kuamka sasa hivi; Lakini wananchi wengi sana wa Tanzania bara, kutokana na tatizo la illiterary, watatumika vizuri sana kisiasa kuzima hoja hii, bila ya kujua kwamba wanajenga volcano aidha ya kuua muungano au kusambaratisha taifa vizazi vijavyo, kutokana nauwepo wa muungano unaoweka siasa mbele ya vitu vingine vyote muhimu;

G-55 na pia suala la Malecela na Kolimba, uamuzi wao kuhusu Tanganyika ulikuwa ni uamuzi sahihi; inawezekana isionekane hivyo kwa miaka 100 ijayo, lakini mwaka wa 101, ukweli huu utakuja kubainika, na pengine mzee wetu malecela na kolimba kuja kujengewa sanamu kama kumbukumbu;

Mwalimu alikuwa na hofu ambayo ni justified - kwamba serikali tatu itavunja muungano, lakini alijisahahu kwamba muungano huu ulikimbizwa sana kwa kuanza na muungano wa kisiasa - TANU + ASP = CCM, huku CCM sasa ikichukua hatamu katika kila kitu, na pia kuwa juu hata ya Katiba ya nchi ya 1977; Nyerere aliamini kwamba muungano wa kisiasa unge trickle down to Social and Economic issues, lakini kumbe anything Siasa huwa ni TOP - DOWN, not BOTTOM - UP;
 
Jmushi1,

Muungano wetu ni utata mtupu,nakubaliana na dhana ya kwamba wkomunisti kina Babu na Hanga walikuwa wakihofiwa na ndiyo maana mwingireza alimsaidia mwalimu kwenye hilo.Lakini pia ni mwingereza huyo huyo alimsaidia Sultan kwa kumkabidhi uhuru wa watu wa Zanzibar.Na mapinduzi yalipofanyika.Ilikuwa ni for the better of British kwa ku-fear communism ya kina Babu, pamoja na Karume aliyekuwa akiogopa influence ya kina Babu,na yeye pia akajificha chini ya mwavuli huo wa komunisti.Mwalimu yeye nia yake kiukwe inaonekana ilikuwa ni muungano kwasababu pan africanism "spirit" yake inaprove hilo.Tatizo ni means za muungano huo pamoja na hidden agendas za waingereza.Na ndiyo maana muungano ni kama ulilipuliwa lipuliwa tu.

Kwa mujibu wa rekodi zilizopo, msukomo, hamasa na mwelekeo wa KIITIKADI, nyuma ya Mapinduzi haya ilikuwa ni UMMA Party chini ya uongozi wa Abdurahaman Babu, ambae ideological orientation yake ilikuwa ni UKOMUNISTI;

Orientation hii ya Babu iliyopelekea Mapinduzi ya Zanzibar, haikuwa acceptable kwa majirani zake wote – Kenya, Uganda na Tanganyika, kwani it would have set a bad example kwa nchi hizi ambazo ndio kwanza zilikuwa zimejipatia uhuru ambao essentially ilikuwa ni uhuru wa kisiasa tu huku uchumi ukiendelea kuwa ni ule ule wa kikoloni – free market; Tukumbuke kwamba hii ilikuwa ni kabla ya ujio wa Ujamaa Tanzania, 1967; Baada ya Mapinduzi ya Zanzibar 1964, Mataifa ya Magharibi yaliingiwa na wasiwasi mkubwa kwamba pengine Zanzibar inaweza kuwa Cuba nyingine; Na kitendo cha Zanzibar kukaa kimya juu ya kuingia mikataba na pia makubaliano mbalimbali ya kimataifa baada ya kupata uhuru kiliwatia sana hofu wakubwa wa magharibi kwani hawakuwa wanaelewa Zanzibar ingefuata mkondo gani; na hapa hoja yako kuhusu suala la Ukomunisti pamoja na hoja juu ya kwanini Muungano uliarakishwa, ndipo inapoingia;

Karume na ASP waliona chama cha UMMA pamoja na Babu kama a big political threat; na kama ulivyojadili, muungano ukaharakishwa sana kuokoa tatizo hili, na ndio maana, the first important move ya Karume kama Rais, mara tu baada ya muungano ilikuwa ni makubaliano na Nyerere kuhusu Political Exile ya Babu na Makomredi wenzake, ambapo walienda bara kupewa nyadhifa mbalimbali katika serikali mpya ya JMT;

Baadae akiwa Waziri wa mambo ya nje, tunamuona Babu katika historia, akidhamiria kuiondoa Zanzibar kutoka kwenye Western block, na kuiingiza kwenye block ya nchi zisizofungamana na siasa za upande wowote; nchi hizi pamoja na kutofungamana na upande wowote, marafiki zake wakubwa walikuwa ni nchi za Kijamaa; Muda mfupi baadae, tunaona katika historia ya nchi hii Mwalimu anaibadilisha Tanzania kuwa nchi ya kijamaa; Je tunajifunza nini katika hili? Moja, significance ya Mzee Babu katika mapinduzi ya Zanzibar inafunikwa; Pili, Babu lazima alikuwa na influence kubwa sana katika uamuzi wa Tanzania kugeuka kuwa nchi ya Kijamaa, lakini hili nalo linafunikwa;

Sheria ya mkataba wa muungano ya 1964 haikuwa na madhumuni mengine zaidi ya kuestablish ama kuthibitisha hati za muungano,pamoja na kubainisha mgawanyo wa madaraka chini ya muungano ie Rais na makamu wa rais,pamoja na muundo wa muungano na katiba ya muungano. Bunge la Tanganyika ndilo lilipitisha sheria hizo za muungano,na baraza la wawakilishi lilifanya kuthibitisha tu.

Kwa kiasi fulani upo sahihi lakini kuna suala la msingi sana ambalo haujalitazama sawa. Naomba ukipata muda upitie Kipengele cha TATU hadi cha SITA, cha mkataba wa muungano, 1964, ili tuwe kwenye ukurasa mmoja kabla ya kujadiliana zaidi juu ya suala hili.

Pia ni ukweli kuwa Zanzibar hawakuwa na katiba,bali walikuwa na presidential decrees,na ndiyo maana wakai adopt katiba ya Tanganyika(adopted from colonial era) na kuitumia kama katiba ya muda kwenye kipindi cha mpito.

Hii ni sahihi, ila ningependa utazame kipengele cha tatu hadi cha sita kilisema nini hasa juu ya kipindi hiki cha mpito.
Katiba hiyo ni ya Tanganyika ya mwaka 1962,ambapo walifanya marekebisho kadhaa na kuweka cheo cha makamu wa kwanza wa rais ambaye ndiye rais wa Zanzibar na pia msaidizi wa rais katika maswala yote ya kiutawala kwa upande wa Zanzibar,na makamu wa pili wa rais akiwa ni waziri mkuu na msaidizi wa rais wa masuala yote ya utawala upande wa Tanganyika na pia kiongozi wa shughuli za serikali bungeni.Na ni katiba hiyo ya muda ya mwaka 1965 ambayo iliainisha maazimio 11 ambayo yalikubalika kuwa ni ya muungano na kwamba yatakuwa chini ya muungano kama alivyoelezea mh Lissu.

Hapa nakubaliana na wewe, ila kuna jambo lingine muhimu hapa: palikuwepo na ukiukwaji mkubwa wa Mkataba wa Muungano, 1964, na pia uchakachuaji ambao ulipelekea sheria mpya namba 24 ya mwaka 1967 iliyompa Rais wa JMT mamlaka ya kubadilisha neno TANZANIA pale ilipokuwa TANGANYIKA katika sheria za nchi; Tukumbuke kwamba – kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, Serikali ya Muungano na Bunge la Jamhuri ya Muungano halikuwa na mamlaka ya kushughulikia mambo yasiyo ya muungano, ikiwa ni pamoja na kucheza na majina ya ZANZIBAR na TANGANYIKA;

Utata mwingine ni kwamba,mkataba huo ulianisha uongozi chini ya utawala wa chama kimoja,lakini maajabu ni kwamba kulikuwepo vyama viwili,yaani TANU na ASP huko Zanzibar.

Nakubaliana na wewe pia juu ya hili i.e. suala hili kuwa ni utata mkubwa; Tuelewe pia kwamba Muungano wa TANU na ASP kuzaa CCM mwaka 1977, na mwaka huo huo wa 1977 katiba mpya ya JMT kuzaliwa, is not a coincidence, bali mkakati maalum wa CCM kujichukulia mamlaka yote juu ya muungano; ili kufanikisha hilo, ilikuwa ni muhimu kwa TANU kupata ridhaa ya ASP kwa kupitia kiini macho ya muungano wa vyama hivi wakati ukweli ni kwamba, maamuzi yote sasa juu ya muungano yalikuwa chini ya CCM na yalihamia DODOMA;

Utata mwingine ni pia hapo kwenye hizo nyongeza.Ni ukweli kwamba hayo makubaliano yaliyoongezwa kwenye katiba ya 1965 yalikiuka sheria ya muungano ya 1964?Kwasababu kiukweli,sheria za muungano zilitungwa na bunge la Tanganyika na baraza la wawakilishi hawakuwa na any say zaidi ya kuithibitisha tu pengine kwa shinikizo.

Ibara ya ‘7’ ya Mkataba wa Muungano inatoa nguvu za kuchaguliwa Tume ambayo nayo ingetoa mapendekezo ya Katiba ya JMT. Muhimu pia ni kwamba – Mkataba wa Muungano, 1964, unaamrisha kuwa Rais wa JMT kwa makubaliano na Makamu wa Rais ambaye ni Kiongozi wa Zanzibar, wataitisha BARAZA LA KUTUNGA SHERIA, ambalo kwao litakuwa na wajumbe kutoka Tanganyika na Zanzibar, kwa idadi itakayokubaliwa NDANI YA KIPINDI CHA MWAKA MMOJA wa Muungano kwa ajili ya kujadili na kutoa mapendekezo kwa Tume itakayoteuliwa na kuipitisha katiba hiyo mpya ua JMT;
Je hili lilitekelezwa?


  • Jibu ni HAPANA. Tume hiyo haikuchaguliwa kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano kutengeneza mapendekezo ya katiba mpya; lakini bado Katiba ya Muda ilianzishwa mwaka 1965;

Kitu kingine cha ajabu pia ni kwamba mwaka huo huo, Bunge la JMT lilipitisha sheria iliyolenga kuahirisha ibara ya saba ya Mkataba wa Muungano “INDEFINATELY” kama nilivyojadili kidogo hapo juu. Basically, ibara hii inasema hivi:

(vii) Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kukubaliana na Makamo wa Rais ambaye ni kiongozi wa serikali ya Zanzibar

a) Atateua tume kwa ajili ya kutoa mapendekezo kwa ajili ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.
b) Ataitisha Baraza la kutunga katiba ikiwa na wawakilishi kutoka Tanganyika na Zanzibar katika idadi itakayoamuliwa likutane katika kipindi cha mwaka mmoja tokea kuanza kwa muungano kwa madhumuni ya kutafakari mapendekezo ya tume iliyotajwa juu na kupitisha katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Badala ya mambo kwenda kama ilivyokubaliwa chini ya Mkataba wa Muungano, 1964, bunge la JMT likapitisha katiba ya muda i.e. Sheria No. 43 ya 1965, ambayo literally ilijenga madaraka kwa serikali ya JMT na pia nchi shirikishi yani Tanganyika na Zanzibar; Lakini pengine kwa sababu wahusika walijua kufanya hivyo ni kuzidi kuumiza Muungano, pengine ndio maana Tanzania ikaishi kwa miaka 12 bila ya kuwa na Katiba ya Kudumu;
 
Mchambuzi,

Asante sana kwa kuanzisha thread ambayo ya kuelemisha na kufikirisha. Nimesoma post zote na za wachangiaji wengine, mchango wako na wa wengine binafsi umenifungua sana. Sasa naona si sawa kuwaambia ndugu zetu wa Zanzibar kuwa tuwaache wajitenge kama baadhi ya michango ya thread nyingine tunavyopendekeza, nafikiri uelewa wa masuala ya muungano ni mkubwa kwa wenzetu wa Tanzania visiwani.
 
Mimibaba,
Shukrani kwa mchango wako mzuri;

Muungano wa Nyerere na Karume na serikali zao ni batili kwa wananchi kwa saa; ni sawa na mwaharamu aliyefanikishwa sana na kudhani hakuzaliwa nje ya ndoa halali.

Hata wataalam wa masuala ya katiba kama vile Issa Shivji huwa anajenga hoja juu ya ulakini juu ya uhalali wa muungano huu; Mkataba wetu una hadhi zote za kimataifa, lakini hadhi kitaifa ipo katika mashaka makubwa;

Hotuba ya TAL kutokuwepo kwenye Hansard ni balaa lingine la kuvunja taratibu na katiba ya nchi. Kuna haja ya wahusika kuwajibishwa au kutueleza uma kilichojiri kinyume chake hansard si taarifa sahihi za Bunge.

Suala la mambo kadhaa kutokwenda kwenye Hansard kwa mujibu wa utaratibu ulioweka limewahi pia kuzungumziwa nadhani na aidha Mnyika au Lissu katika vikao vya Bunge vya hivi karibuni;

Shida iko wapi ya kutafuta muungano wa udugu kwa matakwa ya ndugu si kwa kwa matakwa ya wachache? Kuna kitu kinafichwa kinachofanya baadhi yetu tuwe na kichefu chefu na muungano huu sawia na hoja za TAL bungeni

Mimi nadhani kati ya masuala yanayopelekea kung'ang'ania mfumo uliopo uendelee ni suala la kupenda UKUBWA/VYEO; Katika wanasiasa wa sasa, ni yupo ambae anapendelea zaidi kuwa Rais wa Tanganyika badala ya kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hata kama kufanya hivyo kunaleta maslahi makubwa zaidi kwa wananchi wa Tanganyika kuliko ilivyo sasa? Jibu ni HAKUNA!

Nina mengi ya kujibu maswali yako manne, ila msingi wake sikubaliane nao unapotaka kudumumisha muungano usiotuhusu wananchi.
Msimamo wangu
1. Muungano wa viongozi na serikali uvunjwe kupitia taratibu za kibunge ili wananchi tupate fursa ya kuujadili kama tiunauhitaji na wa aina gani. Kwa kiwango cha kero cha sasa siuhitaji.

Naelewa hoja yako ya msingi hapa, ni kwamba tu tunapishana mawazo au kama asemavyo nguruvi3, hili ni suala la "Mgongani wa Mawazo" tu; kwa upande wangu, njia iliyo na uhakika zaidi kubaini hatima ya muungano wetu ianze kwa kuangalia wapi tulijikwaa, na that would involve kurudia tena Mkataba wa Muungano, 1964; Suala la kuufutilia mbali lifuatie zoezi hilo kwani Mkataba ule ulikuwa ni mzuri and straight forward kwani uliweka provision ya viongozi kuujadili na kama hawataridhika nao, basi kuutupilia mbali;

2. Ili mradi CCM ipo madarakani na wana maslahi kwenye muungano huu uliochakachuliwa, wajue kitendo hicho hakitadumisha muungano bali kinazaa maswali na mijadala kama unayoileta hapa. Ni matumaini yangu wananchi wataamua mustakabali wa CCM ili mambo mengi yarekebeki.


KUZALIWA KWA TANGANYIKA LAKINI PIA KUVUNJIKA KWA MUUNGANO NI KIFO CHA CCM

Kuvunjika kwa muungano au kuzaliwa kwa serikali ya Tanganyika itakuwa ni Umauti wa CCM tena kwa kasi ya concord; Sheria maalim ya bunge mwaka 1967 ililenga kwa makusudi kabisa kulifuta jina la TANGANYIKA na kulibadilisha liwe TANZANIA; leo hii wakirudia yale waliyoyafuta, watajenga hoja gani ya kisiasa katika mazingira ya sasa ya ONE MISTAKE, ONE GOAL?

Ikumbukwe kwamba Muungano wetu ulianzia na ngazi ya Kisiasa, pale ASP na TANU walipoamua kuungana ili kufanikisha muundo wa katiba mpya mwaka 1977, baada ya nchi kuwa chini ya katiba ya muda kwa miaka 12 i.e. 1965 – 1967; Kwahiyo, muungano wa Tanzania was essentially muungano wa TANU + ASP = CCM, pengine kwa imani kwamba Tanzania ingebakia chini ya CCM milele; Ndio maana suala la vyama vingi liliwavuruga sana watawala kwani sasa kulikuwa na uwezekano kwamba ukiukaji wa Mkataba wa Muungano, ungezaa sentiments Zanzibar na kupelekea chama kimoja cha Siasa kushinda bara, huku kingine kikishinda Zanzibar; Ni Jaji Bomani ndie aliyeokoa jahazi hili kwa kupendekeza mfumo wa mgombea mwenza; Lakini kwa vile Sheria Mama – yani Mkataba wa Muungano, ilishatendewa dhambi, zimwi hili halikuisha, na ndio maana ikabidi uje ujanja ujanja mwingine wa serikali ya Umoja baina ya CUF na CCM kama njia ya kulinda muungano;

The bottom line hapa katika kujibu hoja yako hii ni kwamba, muungano wetu ulianza na a POLITICAL UNION, kwa matumaini kwamba hii inge trickle down to ECONOMICS and SOCIAL; obviously, hilo halikutokea, hence migogoro ya autonomy inayozidi kujijenga kila kukicha;

3. Kuna jitihada za kusuppress maoni/fikra za watu kuhusu suala la muungano, linakera kwa muda wa sasa tu lakini halitakera muda wote lina dalili ya kuisha vibaya; vyo vyote vile litaisha kwa maslahi ya Tanganyika na wananchi wa Zanzibar.

Matumaini yetu yapo katika katiba mpya ya 2014 kwani ifikapo mwaka huo, muungano wetu utakuwa umefikisha miaka 50; muhimu zaidi ni kwamba Katiba yetu ya sasa imejengwa kwa misingi ya muungano wetu ambao ni mbovu kwa kila namna, and until we resolve this, Mgogoro wa Katiba yetu will remain to be dominated by the ZANZIBAR QUESTION;
 
Nimeipitia kwa umakini mkubwa hotuba ya Mheshimiwa Tundu Lissu nikashindwa kuelewa ni kwanini CUF haikuiunga mkono CDM.Wanasiasa ni watu wanafki sana hasa ukimsikiliza Maalimu na Jussa ndiyo unashindwa kuelewa wanataka nini haswaa.

Tusisahau kwamba CHADEMA ni chama cha Tanganyika, sio Tanzania, ingawa katiba ya 1977 inajaribu kufanya hili liwe vice versa; Vinginevyo umuhimu wa Chadema zanzibar utaendelea tu kuwa ule unaofuata tu matakwa ya sheria ya msajili wa vyama vya siasa; Nje ya hapo, ili Chadema iwe na mashiko na pia sauti Zanzibar, ni muhimu nayo itafute a political partner kama ilivyofanya TANU kwa ASP; Vinginevyo, hata muungano ukivunjika leo, which means kwamba pia ni KIFO CHA CCM, mabaki ya CCM [Sijui yatakuwa ni TANU], yatakuwa na wakati mgumu kama wa chadema leo hii kukubalika Zanzibar, hata kama pande zote mbili zitakuwa zinasimamia hoja inayofanana;
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom