Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
- Thread starter
- #41
Mchambuzi,
Asante sana kwa kuanzisha thread ambayo ya kuelemisha na kufikirisha. Nimesoma post zote na za wachangiaji wengine, mchango wako na wa wengine binafsi umenifungua sana. Sasa naona si sawa kuwaambia ndugu zetu wa Zanzibar kuwa tuwaache wajitenge kama baadhi ya michango ya thread nyingine tunavyopendekeza, nafikiri uelewa wa masuala ya muungano ni mkubwa kwa wenzetu wa Tanzania visiwani.
Shukrani mzawa halisi;
Naomba nikiri kwamba hata mimi kwa muda mrefu nilikuwa naishi katika hali ya kiza kingi sana huku nikiamini kwamba matatizo ni ndugu zetu wa zanzibar, kumbe ni kinyume chake; Kwa kweli ili mtu uelewe kiini macho hiki, ni lazima utumie muda mwingi sana kusoma na kutafakari mambo mbalimbali; ukitegemea wanasiasa wa bungeni ndio wakusaidia uelewe nini kinaendelea, itakula kwako;
Upo sahihi kuhusu uelewa mkubwa wa ndugu zetu wa ZnZ; Na napenda kuwapongeza viongozi wao kule visiwani ambao katika kipindi chote cha muungano, walikuwa wana waelimisha mambo mengi juu ya muungano huu, tofauti na sisi ndugu zao wabara ambao tulikuwa tunapigwa blah blah nyingi tu; Najua itachukua muda sana kwa UMMA wa watanzania kuelewa suala hili hivyo kufanya maamuzi muhimu, na kutokana na udhaifu huu, wananchi watapigwa blah blah nyingi sana wapinge hoja ya Tanganyika, na wataishia kutuona sisi wenye mwamko wa tanganyika kama ukoma, hivyo kukaa mbali kabisa na sisi; ikitokea hivyo, itakuwa rahisi sana sana kwa the state kutugeuza sisi kuwa their political enemy number one; hizo zitakuwa ni faida za the state za muda mfupi tu kwani hata ikichukua hadi mwaka elfu mbili na mia moja (2100) kwa vitukuu vyetu kuja funguka baadae na kurekebisha taifa lao, siku hiyo itakuja;
Until then, let them politicians enjoy the ride ya kupeleka nchi yetu kuzimu, kwani in the long run, we will all be dead;