Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
UPDATES
Ni miaka karibia miwili sasa (2012), tangia tuanzishe mjadala huu humu JamiiForums juu ya umuhimu wa kuizindua Tanganyika kama njia ya kuboresha na kudumisha muungano. Miaka miwili iliyopita (2012), wengi walibeza na kukebehi hoja yetu juu ya umuhimu wa kuizindua Tanganyika humu JamiiForums. Lakini kebehi hizi hazikuwa katika mitandao ya kijamii peke yake bali hata kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa mfano, Mbunge wa Singida Mashariki (Tundu Lissu) alipoibua hoja hii bungeni mwaka 2012, mbunge huyu alibezwa na wabunge walio wengi, na hoja ya Tanganyika ikaendelea kufichwa chini ya zulia. Lakini ndani ya miaka miwili tu, uelewa na mwamko wa wananchi juu ya "maana na umuhimu" wa kuizindua Tanganyika ndani ya muungano (serikali tatu) unazidi kukua siku hadi siku, huku mwamko na uelewa huo pia ukizidi kukua miongoni mwa wajumbe wa bunge la katiba, ikiwa ni pamoja na miongoni mwa baadhi ya wabunge wa chama tawala (CCM).
Tujikumbushe mwaka 2012 tulijadili nini katika bandiko #1 la uzi huu:
Tangia tuje na mjadala huu (rejea nukuu hapo juu), mengi ya tuliyojadili wakati ule yameanza kujitokeza taratibu, huku pia wananchi wengi wakizidi kupata ufahamu juu ya umuhimu wa kuizindua Tanganyika, kama njia ya kuboresha na kudumisha muungano. Wakati bunge maalum la katiba likiwa linaendelea, yapo mambo mawili muhimu ya kuyafuatilia kwa karibu:
1. Jambo la Kwanza, CCM imeamua kuendeleza kosa lake la kufanya suala la muungano kuwa ni suala la "Chama Cha Siasa" badala ya kulifanya liwe ni suala la "kitaifa" ili kuendana na mazingira ya sasa ya kisiasa na kidemokrasia nchini. CCM imeshafanya uamuzi rasmi kuhakikisha kwamba Katiba ijayo haikidhi maoni ya wananchi walio wengi bila ya kujalisha imani na itikadi zao za vyama (Tanzania bara na Zanzibar) pamoja na taasisi zote muhimu za umma, ambazo kwa pamoja, walipendekeza mfumo wa serikali tatu kama njia ya kuboresha na kudumisha muungano.
2. Jambo la Pili - wakati kamati za bunge maalum la Katiba zikiwa zimeshaanza rasmi kujadili rarimu ya katiba, hati za muungano zimeibua utata. Yapo madai kutoka kwa baadhi ya wajumbe bado hawajapatiwa nakala za hati hizi kama walivyoomba. Kanuni zinaruhusu wajumbe hawa kupatiwa nyaraka zozote ambazo zimejadiliwa ndani ya rasimu ya katiba. Pia yapo baadhi ya wajumbe wanaodai kwamba saini ya Nyerere (Rais wa kwanza wa Tanganyika huru na Tanzania) na saini ya Katibu wa Bunge wa wakati ule (Pius Msekwa) zinazofautiana na saini halisi zilizopo kwenye nyaraka. Kwa maana nyingine, nakala za hati walizopewa wajumbe wa bunge hili maalum, zimechakachuliwa.
Maswali yanayofuatia ni je:
Tuendelee kusemezana...
Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.
Ni miaka karibia miwili sasa (2012), tangia tuanzishe mjadala huu humu JamiiForums juu ya umuhimu wa kuizindua Tanganyika kama njia ya kuboresha na kudumisha muungano. Miaka miwili iliyopita (2012), wengi walibeza na kukebehi hoja yetu juu ya umuhimu wa kuizindua Tanganyika humu JamiiForums. Lakini kebehi hizi hazikuwa katika mitandao ya kijamii peke yake bali hata kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa mfano, Mbunge wa Singida Mashariki (Tundu Lissu) alipoibua hoja hii bungeni mwaka 2012, mbunge huyu alibezwa na wabunge walio wengi, na hoja ya Tanganyika ikaendelea kufichwa chini ya zulia. Lakini ndani ya miaka miwili tu, uelewa na mwamko wa wananchi juu ya "maana na umuhimu" wa kuizindua Tanganyika ndani ya muungano (serikali tatu) unazidi kukua siku hadi siku, huku mwamko na uelewa huo pia ukizidi kukua miongoni mwa wajumbe wa bunge la katiba, ikiwa ni pamoja na miongoni mwa baadhi ya wabunge wa chama tawala (CCM).
Tujikumbushe mwaka 2012 tulijadili nini katika bandiko #1 la uzi huu:
Sehemu ya Kwanza: Utangulizi
Mjadala wowote juu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwa kawaida unahitaji maandalizi makubwa na pia umakini wa hali ya juu, hasa iwapo unalenga hoja zenye kuuboresha kwa njia ya kuondokana na kero mbalimbali zilizopo, badala ya kuuvunja. Iwapo kuna masuala ambayo baadhi yenu mtadhania nimeyasahau au kuyaacha, ni kwa sababu ni vigumu sana kuja na mada kuhusu muungano ambayo inajitosheleza. Pamoja na hayo yote, kuna mengi nimeyaacha kwa makusudi lakini kwa lengo la kuyajadili zaidi baadae; Vinginevyo naomba mniwie radhi kwa mapungufu yoyote ambayo yatajitokeza.
Kupitia nafasi yake kama Msemaji Mkuu wa Upinzani Bungeni (Ofisi Ya Makamu Wa Rais – MUUNGANO), katika kikao cha Bajeti cha Mwaka wa Fedha, 2012-2013, Tundu Lissu (MB), aliwasilisha maoni kuhusu mtazamo na msimamo wa kambi hiyo juu ya Muungano Wetu. Kwa wale waliopata fursa ya kuisikiliza hotuba ya Lissu kwa makini, wengi watakubaliana na mimi kwamba hotuba yake ilijaa YALIO MEMA kuliko YASIYO MEMA, sio tu kwa Muungano wetu, bali pia kwa taifa letu. Vile vile, hotuba ya Lissu ina dhamira njema na yenye manufaa, sio tu kwa kizazi cha sasa, bali pia kizazi cha baadae. Lakini kama kawaida yetu, nchini Tanzania, "POLITICS HAVE BECOME SURPEME TO EVERYTHING, INCLUDING EVEN RATIONALITY AND COMMON SENSE", kwani hoja ya Lissu imepotoshwa;
Tanzania tuna desturi mbaya sana ya ku ‘politicize' kila kwa maslahi binafsi; mfano ni suala zima la mjadala wa Tanganyika ambapo wale wanaopinga hoja hii ni hodari wa kutumia SIASA kupotosha mengi, na pia kuwatia HOFU watanzania, kwa mfano hoja kwamba – kujadili mfumo wa muungano wetu ni tishio kwa Amani na Utulivu wa Nchi yetu; Wanaojenga hoja hizi wakitakiwa watoe ufafanuzi juu ya hoja zao, ni kawaida sana kwa wao kuuacha Maswali mengi kuliko Majibu;
Kuna jambo moja linanishangaza. Pamoja na umuhimu wa hotuba ya Lissu aliyoitoa Bungeni, hotuba hii haipo kwenye Hansard ya Bunge. Kwa kweli this is both - Very Unusual and Very Wrong; Lakini kukosekana kwa hotuba hii kwenye Hansard haiwezi kutuwekea kikwazo sisi wananchi kuendeleza mjadala ule huku uraiani kwa nia ya kujenga, na sio kubomoa, na kwa maslahi ya taifa letu, hasa vizazi vya baadae; Sidhani kama kuna yoyote miongoni mwetu ambaye ana nia ya kuachia watoto na wajukuu zake taifa lililojaa migogoro; Kuzuia mjadala huu au kuhofia kujadili hoja hii, ni mwanzo wa maandalizi ya kuachia vizazi vyetu vya baadae MGOGORO mkubwa sana;
Nilibahatika kunukuu baadhi ya maeneo muhimu kutoka katika hotuba ya Tundu Lissu kupitia TBC1. Kwa kifupi, Lissu alikuwa ana ‘challenge' hoja ya Serikali iliyotolewa na Waziri husika wa muungano kuhusu ya hali ya muungano wetu, miaka 48 baadae [1964-2012]. Waziri huyo alizungumza mengi ikiwa ni pamoja na haya yafuatayo:
["…Katika Kipindi hicho muungano wetu umekuwa na mafanikio katika maeneo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa…muungano wetu ndio nguzo kuu ya umoja na amani…"]
Katika sehemu ya majibu yake juu ya hoja hii ya Serikali, pamoja na mambo mengine, TUNDU LISSU alitamka yafuatayo:
["…hata hivyo mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri aliliambia bunge lako tukufu kwamba, licha ya mafanikio hayo, zipo changamoto katika kumaliza vikwazo vinavyokwamisha shughuli za muungano. Mheshimiwa Spika, Waziri hakuzitaja Changamoto hizo."]
"…Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inataka Serikali itoe kauli mbele ya Bunge hili tukufu ni namna gani maoni ya wale wanaotaka kiini macho hiki cha Muungano kiishe yatashughulikiwa na Tume ambayo imepewa jukumu kisheria la kukihifadhi na kukidumisha kiini macho hicho? Ni kipi kitakachoizuia Tume ya Warioba kupuuza maoni ya watu hao kwa hoja kwamba Sheria inaielekeza Tume kuratibu na kukusanya maoni na kutoa mapendekezo ya kuhifadhi na kudumisha Muungano?"]
Kiini macho anachozungumzia Tundu Lissu ni Serikali Ya Tanganyika kupotea KIMAZINGAOMBWE, kinyume na makubaliano yaliyomo ndani ya Mkataba wa Muungano, 1964, pamoja na athari zake kwa taifa kwa ujumla. Kwa kiasi kikubwa, Mazingaombwe haya ndio chanzo cha mgogoro wa muungano wetu huku hisia tofauti zikizidi kujengeka miongoni mwa wananchi wa pande zote mbili za muungano, kila upande ukiamini kwamba mfumo wa sasa wa Muungano hauwatendei haki. Tutaliona hili kwa undani baadae katika mjadala.
Nia ya mada yangu ni kuendeleza mjadala wa Lissu, hasa kwa kuzingatia kwamba hoja yake haikupewa nafasi ya kutosha kujadiliwa bungeni; Naomba nirudie tena kusema kwamba - tofauti na UMMA unavyoaminishwa, nina amini kwamba Hotuba ya Lissu inabeba Mema kuliko Mabaya. Mjadala juu ya Muungano wetu umetawaliwa na WOGA mkubwa sana, lakini sisi kama raia wa Tanzania, nina amini kwamba ni haki yetu sote ‘kikatiba kutoa maoni yetu juu ya suala hili;
Nimekuwa napokea maneno kadhaa ya vitisho na ya kunikatisha tamaa kutokana na misimamo na maoni yangu mbalimbali humu Jamiiforums, hasa kutokana na ukweli kwamba najulikana kutokana na kuweka picha yangu ya kweli humu; Pamoja na hayo, ni muhimu wajue kwamba vitisho vyao ni motisha zaidi kwangu ya kuendelea kutumia uhuru wangu wa mawazo, hivyo sitaacha kusema ukweli mpaka pale mauti itakaponikuta; Isitoshe, TO GOD, ONE IS MAJORITY.
Sehemu ya Pili: Ujenzi Wa Muktadha wa Mjadala pamoja na yaliyomo.
Katika sehemu hii ya pili, nitajadili masuala makuu matano kama ifuatavyo:
Suala la kwanza. Ni jadi kwa viongozi wengi wa CCM (sio wote), kuwa na misimamo inayo unga mkono mfumo wa sasa wa muungano wetu – yani mfumo wa Serikali Mbili, huku wengine wakiwa na mtazamo wa serikali moja; Wengi ya viongozi hawa huwa na mtazamo kwamba, madai ya Serikali ya Tanganyika hayana nia Njema kwa muungano wetu na taifa letu kwa ujumla; Kuna sehemu kubwa sana ya UMMA ambayo inanunua kauli hizi. Ni muhimu UMMA ukaelewa kwanini viongozi wengi huwa na mtazamo huo. Sababu kuu ni Viapo wanavyokuwa baada ya kuteuliwa KUSHIKA DHAMANA ZA UMMA. Viongozi wetu huapa hivi:
"Mimi ...................bin........ ..........naapa kwamba nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwamba nitaahifadhi, kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Ewe mwenyenzi mungu nisaidie."
Ni muhimu kwa kiongozi yoyote anayeteuliwa kushika cheo kama DHAMANA, kwani kinyume chake ni kujiweka hatarini kupoteza madaraka; Lakini viongozi wengi hujisahau kwamba vyeo hivi sio lolote zaidi ya Dhamana, na wenye mamlaka ya juu kabisa na nchi yetu ni UMMA wa Tanzania, Sio VIONGOZI. Tukirejea kwenye hoja ya msingi katika hili, viongozi hawa hawana jinsi bali kuunga mkono muungano wetu kama ulivyo, vinginevyo kufanya kinyume ‘is to contravene with the cocountry's Constitution, 1977', hivyo kujiweka pabaya na madaraka/vyeo walivyonavyo.
Sehemu ya Kwanza ya Katiba yetu (1977) inazungumzia: Jamhuri ya Muungano na Watu, na inatamka hivi:
1. Tanzania ni nchi Moja na Ni Jamhuri ya Muungano.
2. Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.
Kwa maana hii, tusitegemee kiongozi yoyote aliyekula kiapo cha "kuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano, na kuhifadhi, kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania", aje na msimamo tofauti au aunge mkono hoja ya kudai Tanganyika.
Ukitizama kwa makini maneno haya yaliyomo ndani ya Katiba Ya JMT (1977), licha ya Tanzania kuwa mtoto wa Tanganyika na Zanzibar, nchi ya ‘Tanganyika' haipo, na badala yake, mzazi huyu wa Tanzania amepewa jina la ‘Tanzania Bara'; Hiki ni kiini macho cha hali ya juu; Tangia lini mzazi anapewa jina tofauti baada ya kuzaa mtoto? Suala lingine muhimu zaidi hapa ni kwamba, HUU NI UCHAKACHUAJI na ni KINYUME NA MKATABA WA MUUNGANO, 1964.
Tukirejea kwenye suala la viapo vya viongozi wetu, cha kustaajabisha ni kwamba, imekuwa ni jadi kwa viongozi wetu wengi, katika nyakati tofauti kufanya maamuzi au matendo ambayo yanakiuka Katiba ya JMT, 1977, tena kwa makusudi, and still get away with it; mifano hai ipo mingi, na tunazidi kushuhudia jinsi gani wapo tayari kuvunja Katiba ya Nchi ilikufanikisha masuala mbalimbali ya KISIASA, hata kama hayana maslahi kwa UMMA; Lakini linapokuja suala la kujadili Muungano, hasa TANGANYIKA, suala ambalo lina maslahi kwa umma, viongozi hawa hawapo tayari kufanya hivyo. Cha ajabu zaidi ni kwamba, Mkataba wa Muungano, 1964, unatoa fursa ya wazi kabisa kwa viongozi wa pande zote mbili kuujadili na kuurekebisha muungano, kila inapobidi, na hata ikibidi, KUUFUTA KABISA;
Suala la Pili. Tofauti na viongozi hawa, raia wengine wanapozaliwa, hawali kiapo cha kulinda katiba, muungano….; Vile vile kabla ya kupewa pasi zeti za kusafiria kama watanzania, hakuna kiapo tunachokula; tunapoajiriwa katika sekta sekta binafsi n.k, vile vile hakuna kiapo tunachokula; tunapoamua kuwa wajasiriamali na kupokea usajili wa makampuni yetu kule BRELA au kupokea mbalimbali zinazo turuhusu leseni kuendesha biashara zetu n.k, hatuli kiapo kama cha hawa wakubwa. Sasa iwaje tuogope kujadili muungano kama nia yetu ni kuuboresha? So Let the People Speak. Isitoshe, hatima ya nchi yetu ya Tanzania pamoja na Muungano wetu, ipo mikononi mwa UMMA, sio Viongozi hawa wanaokula viapo, kwani UMMA ndio wenye mamlaka ya mwisho katika taifa letu. Na haki ya raia kutoa mawazo yao ni kwa mujibu wa Katiba (1977);
Suala la Tatu. Kwa Mtazamo wangu, Mtanzania yeyote mwenye nia njema na muungano wetu ni lazima kwanza awe Mwaminifu Kwa Mkataba wa Muungano, 1964, badala ya kuwa Mwaminifu kwa Katiba ya JMT, 1977; Hii ni kwa sababu, Katiba ya JMT, 1997, haina mema na muungano wetu, kwani Katiba hii mbovu ndio chanzo kikubwa cha mgogoro ulipo sasa; Tutalijadili hili kwa kina baadae, hasa jinsi gani Katiba ya JMT, 1977, ilivyouchakachua Mkataba wa Muungano, 1964.
Kama tutakavyoona, Mkataba wa Muungano, 1964, ulikuwa na nia ni njema kabisa – ya kuunganisha watu wa Tanganyika na Zanzibar, huku kila taifa likiwa huru na kujiamulia mambo yake yasiyo ya muungano; Badala yake, kilichokuja kutokea baadae ni mazingaombwe na uchakachuaji ambayo ulifanya tupoteze nchi ya Tanganyika, ambae ni Mmoja ya Wazazi wa Tanzania, na mzazi huyu kupewa jina jipya la "Tanzania Bara", mara tu alipojifungua mtoto wake "Tanzania", huku mzazi mwenza "Zanzibar", nae akipewa jina jipya "Tanzania Visiwani", lakini kwa kuogopa kumchakachua zaidi, akaachiwa awe na majina mawili – yani Zanzibar na Tanzania Visiwani (kabla ya wazanzibari kulikataa jina hili), huku uchakachuaji juu yake ukiendelea kwa njia ya kuongeza orodha ya masuala ya muungano, Kinyume na Mkataba wa Muungano, 1964;
Suala la nne, ni kuhusu arrangement ya Katiba ya Tanzania, 1977. Shivji (2006) analiweka hili kwa lugha rahisi zaidi kueleweka pale anaposema kwamba: "The underbelly of Tanzania's constitutional arrangement is and has been the union or Zanzibar."
Kwa bahati mbaya sana, msimamo wa ndugu zetu wazanzibari juu ya muungano umekuwa unapotoshwa, na kuwekwa completely out of context. Je ni kwa madhumuni gani? Ni vigumu kuelewa; Lakini ukweli ulio wazi ni kwamba throughout, ndugu zetu wazanzibari wamekuwa na tatizo moja tu kuhusu muungano, na hili sio jingine bali "Loss of Their Autonomy". Kwa sababu tusizozijua, hoja yao hii ambayo ni LEGIT kabisa, hasa kwa kufuatana na Makubaliano chini ya Mkataba wa Muungano, 1964, msimamo wao umekuwa ‘politicized', na kupelekea ujenzi wa chuki kubwa baina ya ndugu hawa wawili – wazanzibari na watanganyika; Imekuwa jadi kwa baadhi ya watu kuwashutumu ndugu zetu wazanzibari kwamba misimamo yao juu ya Muungano wetu una msukumo wa kidini; huu ni upotoshwaji wa hali ya juu; Ukweli ni kwamba - throughout, Wazanzibari wamekuwa na nia njema kabisa na Muungano, lakini kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964, ambapo Serikali Tatu was envisaged;
Ningependa kusema kitu kimoja at this juncture:
Kwa sababu kadhaa, ndugu zetu wazanzibari wamekuwa ni waelewa zaidi juu ya kiini macho cha muungano kuliko wengi wetu wa upande wa bara; Mbaya zaidi ni kwamba, badala ya sisi kujikita katika kuelewa tatizo la msingi lipo wapi, hasa jinsi gani Katiba ya JMT 1977 ilivyofanya mazingaombwe na kuchakachua Mkataba wa Muungano, 1964, na badala ya na sisi kuwaiga na kudai Tanganyika yetu, kitu ambacho wao throughout wamependelea kiwepo, badala yake tunaelezeka juhudi zetu kubwa sana to fight the wrong enemy i.e. kuwakosoa ndugu zetu wa Zanzibar juu ya madai yao, badala ya kuwaelewa na kuwaiga;
Wengi wetu tunajenga hoja potofu kwamba wazanzibari wanafaidika zaidi na muungano, au wanatunyonya; hii hoja sio sahihi kwa sababu – kama ni kweli Bara tunanyonywa na muungano huu, basi ni kwa sababu ya makosa yetu wenyewe ya Kukiuka Mkataba wa muungano, 1964, kupitia katiba ya JMT, 1977; Isitoshe – iwapo mtoto wako haumpi ‘autonomy' au haumfundishi maisha ya kujitegemea, kwanini sasa uanze kumgeuka na kumuona kwamba ni mzigo kwako? Ni dhahiri kwamba, iwapo wangepewa Autonomy kwa Mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964, Zanzibar ingeweza kabisa kujitegemea; Kinyume chake, baada ya Muungano, serikali ya Muungano ikaanza taratibu kunyakua mambo mbalimbali na kuyatumbukiza kama nyongeza ya masuala ya muungano, kinyume kabisa na Mkataba wa Muungano, 1964; Leo hii tunaposema ndugu zetu wazanzibari ni mzigo, hii ni dhambi kubwa sana kwetu watu wabara;
Pia wengi tunasahau kwamba, Zanzibar ilijiunga na Tanganyika miezi minne na nusu tu baada ya kufanikisha Mapinduzi yake mwaka 1964 yaliyotokomeza Utawala wa Kisultani; Ikumbukwe pia kwamba, katika kipindi hiki cha miezi minne na nusu Ya UHURU Wao [DECEMBER 10[SUP]th[/SUP] 1963 – APRIL 26[SUP]th [/SUP]1964], Zanzibar waliamua kukaa kimya kabisa na kutokimbilia kujiingiza katika Mikataba yoyote au makubaliano yoyote ngazi ya Kimataifa; kwa maana nyingine, hawakutaka kuwa signatories wa suala lolote ngazi ya kimataifa mpaka pale watakapojipanga; Mkataba wao wa kwanza ukawa ni ule wa Muungano na Tanganyika na hatimaye kujikuta kwamba, mengi ambayo Tanganyika walikuwa wamesha establish position yake kimataifa, yakageuka kuwa binding kwa Zanzibar pia; Lakini kwa ajabu, wengi wetu suala hili tunalipuuza;
Ni muhimu tukaelewa pia kwamba - tofauti na nchi zilizokuwa jirani yake (Zanzibar), yani Tanganyika, Kenya na Uganda ambazo uhuru wao ulipatikana kwenye Board Rooms za Lancaster Hall huko London, huku wahusika wakiwa wamevaa suti na kunywa wine na kahawa katika mijadala, ndugu zetu wa Zanzibar hali ilikuwa ni tofauti; Wao uhuru wao ulipatikana "in the streets", kupitia mtutu wa bunduki; The bottom line hapa ni kwamba, mtazamo wa baadhi ya watu wa "Tanzania bara" kwamba eti Wazanzibari wanatulalia, umejaa upotoshwaji mkubwa sana.
Suala la Tano na la mwisho kujadili katika sehemu hii, ni kwamba – Kama wapo watanzania wenye ujasiri wa kumkosoa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, basi ni wachache sana; Wale wenye uoga juu ya hilo wanasahau kwamba Nyerere alikuwa ni binadamu kama wao; Mimi ni muumini mkubwa sana wa Falsafa ya Mwalimu, including suala la Muungano wetu, lakini nina amini kwamba kuna baadhi ya maeneo ambayo Mwalimu kama binadamu, aliyakosea, licha ya yeye kuwa na nia njema kwa taifa letu, hasa ikizingatiwa kwamba "Nyerere Did Not PROFIT From Politics"; Makosa ya Mwalimu juu ya muungano yalikuwa na yanaendelea kuwepo kwenye "MFUMO", sio kwenye NIA; Nyerere alikuwa was a ‘True Panafrianist', na kuna wakati alikuwa yupo tayari hata kuifanya Afrika ya Mashariki iwe ni nchi moja baada ya uhuru na kabla ya muungano na Zanzibar, kwa nia nzuri kabisa; Kwahiyo when it comes to suala la Muungano na Mwalimu, "The END" Was Justified, But Not The "MEANS"; Wasiwasi wa Mwalimu juu ya hatima ya Muungano iwapo Tanganyika itarudi, upo LEGIT; lakini tutaendelea kukaa na hofu hii mpaka lini, hasa ikizingatiwa kwamba Mgogoro wa muungano wetu unatokana na Ukiukwaji wa Mkataba wa Muungano, 1964?
Machafuko yote yaliyojitokeza Zanzibar miaka ya nyuma, na ambayo yanaendelea leo chini kwa chini, chanzo chake ni mgogoro wa Kikatiba unaotokana na Katiba ya JMT, 1977, kuchakachua Mkataba wa Muungano, 1964. Kwa mtazamo wangu, mgogoro huu wa kikatiba Poses More Threat to our Peace and Tranquility kuliko ujio wa Tanganyika; Isitoshe, hata Tanganyika ikizaliwa, nchi yetu ya Tanzania itabakia kuwa ile ile, hasa mipaka na mahusiano ya watu wake; Kitachobadilika kitakuwa ni Mfumo tu wa Serikali; Hivyo mimi sioni busara kwa Watanzania kufanya maamuzi KIHOFU HOFU na kuacha mgogoro huu ubakie kama ulivyo; Tutakuwa ni wabinafsi sana iwapo tutarithisha vizazi vyetu vyaa baadae hali hii hii ya HOFU hii lakini pia MGOGORO huu huu, ambao kiini chake ni Ukiukwaji wa Mkataba wa Muungano, 1964. Hivi kweli, Vizazi Vya Baadae Vitafikiria Sisi Tulikuwa ni Watu wa Namna Gani?
Baada ya kujadili haya, sasa nifungue mjadala kwa msisitizo kwamba, naunga mkono hoja ya Tundu Lissu kuhusu kiini macho cha muungano wetu kwa sababu nilizojadili; Nina imani kwamba mjadala utakaouzaliwa kutokana na maswali yafuatayo utatuaidia kupata mwanga zaidi juu ya kiini macho cha muungano wetu, lakini muhimu zaidi, mawazo ya kutusaidia kuboresha muungano wetu kwa faida ya kizazi cha sasa na baadae:
Kwanza: JE, Madhumuni ya Muungano Baina ya Tanganyika na Zanzibar, kwa Mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964, Yalikuwa Ni Yepi na ni Mfumo wa Serikali ngapi ndio uliokusudiwa chini ya Mkataba huu wa Mwaka 1964?
Pili: JE, Viongozi Wetu na Wananchi Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Leo hii, Wana Nia ile ile Adhimu na Malengo Yale Yale Yaliyowekwa katika Utangulizi wa Mkataba wa Muungano, 1964?
Tatu: Ifikapo Mwaka 2014, Muungano Wetu Utakuwa Umetimiza Miaka 50; By Coincidence, Kipindi hicho hicho pia Tunategemea Kupata Katiba Yetu Mpya; Swali linalofuata ni, JE: Katika Kipindi Hiki Cha Miaka 50 Ya Muungano, tutakuwa tumefikia wapi katika Kufanikisha Madhumuni Kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964?
Nne: Je, makosa ambayo yanapelekea muungano wetu kuyumba yalijitokeza wapi, na tuchukue hatua gani kurekebisha makosa haya, na kurudisha matakwa na dhamira iliyowekwa wazi kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964?
BILA TANGANYIKA, TANZANIA HAIWEZEKANI. MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE.
===========
Soma kuhusu Mkataba wa Muungano wa 1964 katika POST #6
Soma alichosema Lissu Bungeni hapa na VIDEO hapa
===========
Soma kuhusu Mkataba wa Muungano wa 1964 katika POST #6
Soma alichosema Lissu Bungeni hapa na VIDEO hapa
===========
Tangia tuje na mjadala huu (rejea nukuu hapo juu), mengi ya tuliyojadili wakati ule yameanza kujitokeza taratibu, huku pia wananchi wengi wakizidi kupata ufahamu juu ya umuhimu wa kuizindua Tanganyika, kama njia ya kuboresha na kudumisha muungano. Wakati bunge maalum la katiba likiwa linaendelea, yapo mambo mawili muhimu ya kuyafuatilia kwa karibu:
1. Jambo la Kwanza, CCM imeamua kuendeleza kosa lake la kufanya suala la muungano kuwa ni suala la "Chama Cha Siasa" badala ya kulifanya liwe ni suala la "kitaifa" ili kuendana na mazingira ya sasa ya kisiasa na kidemokrasia nchini. CCM imeshafanya uamuzi rasmi kuhakikisha kwamba Katiba ijayo haikidhi maoni ya wananchi walio wengi bila ya kujalisha imani na itikadi zao za vyama (Tanzania bara na Zanzibar) pamoja na taasisi zote muhimu za umma, ambazo kwa pamoja, walipendekeza mfumo wa serikali tatu kama njia ya kuboresha na kudumisha muungano.
2. Jambo la Pili - wakati kamati za bunge maalum la Katiba zikiwa zimeshaanza rasmi kujadili rarimu ya katiba, hati za muungano zimeibua utata. Yapo madai kutoka kwa baadhi ya wajumbe bado hawajapatiwa nakala za hati hizi kama walivyoomba. Kanuni zinaruhusu wajumbe hawa kupatiwa nyaraka zozote ambazo zimejadiliwa ndani ya rasimu ya katiba. Pia yapo baadhi ya wajumbe wanaodai kwamba saini ya Nyerere (Rais wa kwanza wa Tanganyika huru na Tanzania) na saini ya Katibu wa Bunge wa wakati ule (Pius Msekwa) zinazofautiana na saini halisi zilizopo kwenye nyaraka. Kwa maana nyingine, nakala za hati walizopewa wajumbe wa bunge hili maalum, zimechakachuliwa.
Maswali yanayofuatia ni je:
- Kuibuka kwa suala la hati za muungano kunabadili vipi upepo wa Serikali tatu (Tanganyika) katika bunge hili maalum la katiba?
- Nini itakuwa hatima ya CCM?
Tuendelee kusemezana...
Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.