Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Mkuu huyu FaizaFoxy ni mdini balaa! Yaani kamwona Pengo tu; Mufti kwake sio issue. Sometimes huyu ni wa kupuuza tu.
Hivi tafsiri ya udini ni nini uwa napata tabu kufahamu ebu tufahamishe.
 
Last edited by a moderator:
Unaweza kuwa sawa kutokana na umri wako hiyo hotuba ukaipa hiyo hadhi.

Kulikoni leo umeshindwa kumtetea Nyerere kisa aliyesema hayo maneno ni mtu unampenda Tundu Lissu.

Punguza unafiki siku ingine watu wakieleza mapungufu ya Nyerere usitokwe na povu.


Punguza udini utaeleweka. Lissu hajachambua mambo kidini bali kisiasa na ameeleweka vizuri sana. Sasa wewe na makuwadi wenzio mnapoanza kutuletea habari za Kariakoo na misikitini hamueleweki. Mnafiki mkubwa wewe.
 
Tusubiri, ukweli ukidhihiri uongo hujitenga. Kumbuka juzi, Sitta ingawa yupo busy bungeni lakini kaitwa na Pengo na kaenda mbio-mbio, jiuliize kunani?

Na wewe muongo, mzandiki mfitini na mnafiki mkubwa, Sitta aliomba kuonana na viongozi wa dini Pengo na Mufti Simba
 
Hivi tafsiri ya udini ni nini uwa napata tabu kufahamu ebu tufahamishe.

Mfuatilie FaizaFoxy na Mohamed Said role models wako utajua maana yake. Ukishafuzu kwa hao, nenda kwa Ponda upate daraja ya juu zaidi.
 
Punguza udini utaeleweka. Lissu hajachambua mambo kidini bali kisiasa na ameeleweka vizuri sana. Sasa wewe na makuwadi wenzio mnapoanza kutuletea habari za Kariakoo na misikitini hamueleweki. Mnafiki mkubwa wewe.
Wewe punguani kweli tafsiri yako ya udini mtu akiwa Muislam mambo ya Msikiti yameingiaje hapa kama siyo unafiki, kwako uwa hakuna Mkirsto mdini wadini wote ni Waislam.
 
Mimi nafurahi napoona malumbano ya namna hii na kujenga hoja kwenu,alicho kifanya lisu ni kuonyesha matendo yaliyofanywa kipindi hicho ambayo kimsingi yanaweza kuwa sahihi lakini kwa kipindi hiki yakawa ni mapungufu makubwa sana ambayo hayakuzingatia haki na uhuru wa kutoa maoni.

Sikubaliani na Muungano huu ambao kimsingi hata wazazi wetu hawaujui.
 
Hata Nyerere alishakiri kuna mambo ya kijinga serikali yake iliyafanya na akasema tuache ya kijinga tuchukue mazuri!
Kwa mtazamo wako, makosa ya Muungano kama Mh. Tundu Lissu alivyoyaanisha unayaweka wapi?.

Katika lundi la maamuzi ya kijinga au kiakili?.

Kama niya kijinga, mbona sasa wabunge wamejikita kwenye 'madudu' ya Muungano.

Kama niya kiakili, mbona wabunge wanahoji utaratibu uliotumika na nyaraka za kisheria.
 
Mkuu.
Mbona ya Shivji , Mwakyembe na ya ma Proff. Hukuyasema.
Wale wale ambao hamsomi bible nzima, mnarukia viji mistari tu ili kujenga hoja zenu mfu.
By the way Lissu kaongea uongo kwani ?
Mkataba wa Muungano ni lini Serikali ya Kuanzia Nyerere mpaka JK ulipelekwa UN ?
Kuanzia janq binafsi nimeanza kumtizama the late Julius kwa jicho la tatu.
No wonder all the Problems we have now source yake ni yeye.

Mze MUHAMED SAID Kamuelezea vizuri sana JKN lakini watu wanamuona Mze MS kama ana mchukia KJN kwa ukiristo wake.Lakini sasa nadhani waTz watamuamini MZE MS na wataamini kama Jkn mengi ktk utawala wake aliyakosea.
 
Tundu Lissu ni smart lawyer na very good mwanaharakati but he is a lousy politician....huwezi mtukana Nyerere na isi ku cost

Katika mapambano ya kudai haki, utu na usawa wachache watakubali ku risk maisha yao kwa sababu ya kutetea walio wengi, historia inazungumza hivyo na matukio mengi ya kihistoria yanadhihilisha hilo. Mimi nawewe tunapaswa tuwe sehemu ya wachache katika kutetea maslahi ya walio wengi. Vitisho havina nafasi tena katika nyakati hizi tulizonazo.

Nilipomuuliza kaka yangu Abou ambaye alikuwa Afrika ya kusini kwa takribani miaka sita kabla ya kurejea nchini mwaka 2012, yeye alienda Afrika ya kusini kwa kuzamia (Njia za panya) lakini mwaka juzi alirejea. Nilimuuliza kulikoni brother mbona umerejea ghafla ghafla kutoka Afrika ya kusini, akaniambia kuwa; Maeneo ambayo alikuwa akiishi huko Afrika ya kusini yalikuwa siyo salama hata kidogo, wazawa (Wa Afrika kusini) walikuwa wakiwawinda wageni kwa madai ya kuwa walikuwa wakiwanyima fursa mbalimbali nchini kwao. Wale wageni wa kutoka Tanzania walikuwa wakiambiwa kuwa kwasababu nchi yao wanajivunia kuwa ni ya amani basi waende hukohuko kwenye amani kwani wao waafrika ya kusini waliipigania nchi yao na hata kumwaga damu ili kutetea usawa wa watu wao hasa dhidi ya ubaguzi wa rangi na utu. Hivyo ni heri wanaojiita watu wakisiwa cha amani waende kwao. Brother Abou aliniambia kunabaadhi ya wenzake walipigwa risasi kitu ambacho kilimlazimu yeye akimbie kurudi nyumbani.

Kutokana na hilo likanikumbusha kitu fulani uhuru, utu na kujitambua hupiganiwa tena na watu wachache bila woga na wakati mwingine kuamua ku risk maisha yao. Mimi na wewe tunapaswa kuwa sehemu ya hao watu wachache bila woga tunaweza kufikia malengo tunayoyapigania.
 
Mtoa mada acha uongo na kupindisha maneno hakumsema nyerere.kuwa ndiye aliishi kwa uwongo! Alichosema ni kuwa uongoz wa sasa unaish kwa uongo na hawataki ukwel!! Kama ulikuwa unaangalia tv unakunywa viroba ndo athari zake.usijitafutie umaarufu upendwe kwa sifa za kijinga.tv kila mtu aliangalia kwenda zako ndo maana una mdomo mweus kumbe mfitin mkubwa.lete hoja zenye mashiko.pole sana kwa ubongo wa naz
Mimi huwa sina hoja zenye mashiko bali huwa nina hoja za majadiliano katika kufikia makubaliano au kukubali kutokubaliana.

Mimi sitaki hata kusikia mtu ananiambia ananipenda. Ninachotaka ni kuheshimiwa kama nilivyoyaheshimu mawazo yako ingawa hayafai hata katika jamii pevu.

viroba ndiyo nini?.

Mdomo wangu kuwa mweusi unahusiana na nini katika kuandika. Kwani wewe unaandika kwa kutumia mdomo?.
 
Hawa wanasiasa waachane na Mwalimu Nyerere,kama katiba mpya imewashinda si wauvunje huu muungano,kila kitu Nyerere!ina maana Nyerere ndo pekee aliupenda muungano?waache siasa za kinafiki,hakuna mtakatifu kuliko Nyerere.
 
Mimi huwa nadhani wanasheria ni watu wazuri sana katika uwanja wa siasa hasa ukiangalia kwa kutumia darubini katika siasa za nchi za magharibi utakuta kuwa, viongozi wengi wa nchi hizo ni wanasheria na wamefanikiwa/wanafanikiwa katika siasa zao.

Kama hoja yako ni kweli, kwa nini inakuwa tofauti kwa Mh. Tundu Lissu?.

Kwa kadri ya evidence aliyotoa Tundu wakati anatoa hoja ya wachache kwamba hati ya Muungano haijapata kuwasilishwa UN wala haipo Tanzania baada ya Zanzibar kushindwa kuwasilisha hati hiyo mahakamani baada ya kesi (ya mwaka 2005) iliyoikabili dola hiyo kuhusu uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni dhahiri kuna walakin katika utawala wa Nyerere.

Huenda ni kutokana dosari hizo za kisheria iliyosababishwa na Nyerere na Karume zilimlazimisha Nyerere kumkabili yeyote yule aliyejaribu kuhoji Muungano kwa kile kinachojulikana kama kuhoji Muungano ni uhaini. Kama Muungano ulikuwa halali ni kwa nini Nyerere aliweka mwiko wa kutouhoji? Nyerere alijua fika Muungano hauna uhalali wowote ndiyo maana aliamua kuulinda kwa mkono wa chuma ili mwl asijeadhirika ikijulikana kwamba nchi hizo mbili ziliunganishwa kihuni.

Mimi nadhani hoja alizotoa Lisu zina mashiko. Kwa nini tuishi Muungano ambao hauna baraka za Watanganyika na Wazanzibar? Kwa nini Muungano ukose legal backup huku watawala wakishinikiza kuwa Muungano ni halali? Hati ya Muungano kuwa siri nzito maana yake nini? Kwa nini Muungano uruhusu nchi moja kubaki na identity yake huku nyingine ikifutwa juu ya uso wa dunia? Kwa nini inashindikana kuwa na Muungano wa nchi moja yenye serikali moja kama kweli watawala wanaamini udugu wanaouhubiri kati ya watanganyika na wazanzibari?

Kama kweli wazanzibari na watangayika ni ndugu wa damu kama inavyodaiwa na watawala wa sasa basi tuwe na serikali moja tu ya Muungano wa Tanzania; Zanzibar ifutike katika ramani ya dunia kama ilivyofutika Tanganyika. Short of that Muungano uliopo una walakin na walakin huo ulisababishwa na Nyerere na Karume.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom