Tundu Lissu: CHADEMA haina mamlaka kisheria kufungua kesi ICC kuhusiana na Uchaguzi 2020

Safi sana Mh. Tundu Lissu umefafanua vyema kuwa taarifa zipo katika dawati la Mwendesha Mashitaka Mkuu wa ktk Mahakama ya Kimataifa ya Jinai mjini The Hague Uholanzi yaani ICC- The Hague na zinafanyiwa kazi .

Hiyo ni hatua muhimu ya mwanzo ya ICC The Hague kuchunguza matendo na nyendo za waliopo madarakani (serikalini) kwa mujibu wa Makubaliano ya Mkataba wa Rome wa mwaka 1999 Rome Statute of the International Criminal Court . Mkataba wa Rome unashugulikia manne Mauaji ya kimbari, Makosa dhidi ya binadamu, Makosa ya Kivita, Nchi kuvamia nchi nyingine.

Makosa dhidi ya binadamu yakifanyika mara nyingi dhidi ya wananchi na mara nyingi nayo ni mauaji,kutaka kuangamiza, kuwatia utumwani, kuwahamisha watu , kuwanyima watu huru wao mfano kuwekwa kizuizini kwa namna inayoonesha unawalega kundi fulani, mashambulizi ya ngono, uonevu dhidi ya kikundi kwa sababu ya kisiasa au kidini au rangi au ukabila au ukanda.

Malalamiko dhidi ya Tanzania ni yale ambayo serikali iliyopo madarakani inaonekana kwa makusudi na mbinyo mkubwa inalenga kuumiza kikundi cha watu kwa mindhali ya kisiasa mfano kuwakamata, kuwafunga, kutochunguza kesi, kunyima haki ya dhamana, kukomoa ,kuharibu mali au mashambulizi ya kuumiza mfano viongozi, wagombea, wafuasi wa chama fulani kimekuwa kikishambuliwa n.k


Kwa miaka 5 na mfumo mzima wa serikali ya Tanzania chini ya hatamu za CCM Mpya ikiwemo mihimili yake na taasisi zake za Serikali kuu kutoka Dodoma, Dar es Salaam hadi Zanzibar na serikali za mikoa / wilaya /DEDs kuelekeza nguvu zake zote kukandamiza kikundi fulani na kukiumiza kwa makusudi.
100% Tanzania hakuna kesi kama hizo. Inakuwa kesi kama waliodhulika moja kwa moja kama Lissu ni wengi kwa mamia otherwise nchi zenye migogora muda mrefu viongoz wake wangekuwa walishafungwa siku nyingi i.e Ivory cost, DRC, Sudan, Ethiopia kwa sasa n.k
 
Kweli ana maradhi ya akili?
Wakati wa kampeni alizungumza maneno mengi mengi sana yakuonyesha yupo radhi afe.
Ata alipozuiliwa kupita kwenye geti la serengeti pale alizungumza maneno ya polisi wawapige risasi kama awatomruhusu kupita.

Cha ajabu baada ya kampeni tu kuisha akakimbia,anadai katishiwa kuuwawa.ilhali wakati wakampeni alikua yupo radhi afe.
Jiulize,Lisu jasiri wa kipindi cha kampeni ni yupi,na Lisu wa baada ya kampeni ni yupi.
Hapo utagundua huyu jamaa anamatatizo kwenye kichwa.
 
Aliyekuwa mgombea uchaguzi kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHDEMA Tundu antipas Lissu amejitokeza na kutolea ufafanuzi kadha kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwa kesi huko mahakama ya uhalifu ICC dhidi ya Serikali ya Tanzania baada ya uchaguzi mkuu 2020.

Msikilizie kwa undani


Sehemu ya pili ya ufafanuzi


Lissu na wanangonjera wenzake watanyooka tu. Tuliwaambia tangu mwanzo kuwa ICC sio baraza la wananzengo la kusikiliza kesi za walevi wa Faru John. Watu wengine wanajiita wanasheria nguli sijui ni nguli kwa umbumbumbu! Mwaka jana walitupigia kelekele sana, wakitishia viongozi mbalimbali kuwapeleka ICC. Utter nonsense!

Na chizi mwenzao Trump ameisaidia dunia kufahamu dangers za uchochezi. Hapo dili la uchochezi limeshaharibika; wachochezi sasa watakula kibano kitakatifu!
 
Haya ameeleza ndugu Tundu Lissu kuwa chama chake hakina mamlaka ya kufungua kesi ICC.

Ni nchi wanachama wa mkataba wa Rome ndio wana mamlaka hayo ya kufungua kesi.

Hivyo mpaka sasa CHADEMA hawajafungua kesi ICC.

Japokuwa wametoa ushahidi wa ukiukwaji wa haki za binadamu uvunjifu wa haki za kuishi,hasa kwa wapinzani. Hivyo wanasubiri mwendesha mashitaka mkuu wa ICC kama akiridhika aje aanze uchunguzi.

My take:
CHADEMA ni waongo sana, baada ya uchaguzi kuisha walidanganya umma kuwa wamefungua kesi ICC. Hawa watu sio hata kiduchu.
 

Attachments

  • Tundu Lissu_HD.mp4
    25.8 MB
Mbona lumumba hamuishi kumfuatilia Lissu?

Kama mnamkumbuka sana muhakikishieni usalama wake arudi muwe mnamfanyia interview kila siku.

Chadema kufungua kesi au kutofungua sioni tatizo provided Chadema watatoa ushirikiano kwa Lissu kwa kumpa ushahidi wa yale yaliyofanyika, sasa hiki kicheko chenu hapa kinaonesha msivyojiamini, waoga, mnaotetemeka, ndio maana kutwa kumfuatilia Lissu.
 
Mbona lumumba hamuishi kumfuatilia Lissu?

Kama mna mkumbuka sana muhakikishieni usalama wake arudi muwe mnamfanyia interview kila siku.
Kamanda tunajidili namna mlivyodanganya kuhusu kufungua kesi ICC,leo Lissu amewaumbua kwa uongo wenu. Chadema haina mamlaka ya kufungua kesi ICC.
 
Alivyokuja hapa akakusanya bukubuku za wapuuzi alikuwa hana usalama
Mbona lumumba hamuishi kumfuatilia Lissu?

Kama mna mkumbuka sana muhakikishieni usalama wake arudi muwe mnamfanyia interview kila siku.
 
Alivyokuja hapa akakusanya bukubuku za wapuuzi alikuwa hana usalama
Wewe mbumbumbu akiwa kwenye kampeni alipewa ulinzi na serikali, baada ya kampeni kwisha serikali ikamuondolea ulinzi.
 
Back
Top Bottom